HOTUBA YA BAJETI

 

UTANGULIZI

 

1.                 Mheshimiwa Spika, kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya kisekta inayohusu Wizara yangu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge sasa likubali kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2002/2003.

 

2.                 Mheshimiwa Spika, aidha niruhusu niungane na Waheshimiwa Wabunge, ndugu na marafiki katika kuwafariji na kuwapa salamu za rambi rambi familia, ndugu na wapiga kura wa marehemu Mheshimiwa Sebastian Rukiza Kinyondo aliyekuwa Mbunge wa Bukoba Vijijini, marehemu Mheshimiwa John Mangwangwa aliyekuwa Mbunge wa Mpanda Magharibi, aliyekuwa Katibu Mkuu katika Wizara yangu marehemu Alfred Edward Chale, pamoja na aliyekuwa   Mwandishi Mkuu wa Sheria Ndugu Sigfrid Lushagara, Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi, Amina.

 

3.                 Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wote wale waliotuwezesha kutekeleza majukumu ya Wizara yetu kwa kipindi cha mwaka uliopita na wale, ambao wametuwezesha kupanga mipango ya mwaka 2002/2003 na kuboresha maandalizi ya hoja zetu ambazo tunawasilisha katika hotuba hii.  Shukrani za  kwanza ziende kwa wananchi wote na  walipa kodi wa Tanzania.  Shukrani zangu za pekee zimwendee Naibu Waziri wangu, Mheshimiwa Zabein Muhaji Mhita, Mbunge na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara yangu Ndugu Raphael Peter Kabende kwa msaada na ushauri wanaonipa katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara. Shukrani za Tatu , ziende kwa watumishi wa Wizara hii pamoja na taasisi na mashirika yake kwa bidii, uvumilivu na ubunifu wao kikazi. Shukrani za Nne ziende kwa Mashirika mbalimbali ya nje na ndani ya nchi kwa misaada na ushauri wao.

 

Aidha , ninapenda kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Benedicto Mutachoka Mutungilehi, Mbunge wa Kyerwa (TLP) na Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, kwa ushirikiano wake na mchango wake katika kuboresha hoja hii. Mwisho shukrani zetu  ziwaendee waheshimiwa Wabunge wa Kamati ya Huduma za Jamii chini ya uongozi wa Mwenyekiti wao Mheshimiwa Omar Kwaang’w  Mbunge wa Babati Mashariki (CCM) kwa uchambuzi na ushauri wao.

 

4.                 Mheshimiwa Spika, Elimu katika Ulimwengu wa sasa ni mojawapo ya kigezo muhimu kwa ukuaji wa Uchumi endelevu na katika uboreshaji wa  maisha ya binadamu. Tafiti nyingi zilizokwisha fanyika zimedhihirisha kuwa mchango wa Elimu, hususan elimu ya juu una uhusiano wa moja kwa moja na ukuaji wa Uchumi endelevu. Ni katika kutambua hali hiyo, Wizara yangu inalenga katika kuhakikisha Taifa linakuwa na Jamii iliyoelimika, yenye uwiano wa kijinsia na inayoweza kujiletea maendeleo kwa kutumia Sayansi na Teknolojia.

 

5.                 Mheshimiwa Spika, katika hatua za kwanza za kuwa na mwelekeo thabiti na pia kuwa na uwezo wa kupambana na ushindani unaotokana na utandawazi ( Globalization ), Wizara yangu imekamilisha maandalizi ya Mpango Kabambe (Master plan) utakaoongoza ukuaji wa sekta za Sayansi na Teknolojia pamoja na elimu ya juu na ufundi.  Aidha, Wizara yangu imekamilisha Utafiti  (study) kuhusu gharama ya kumwelimisha mwanafunzi (student unit cost) katika vyuo vya elimu ya juu na ufundi kwa lengo la utoaji fedha katika vyuo kulingana na idadi ya wahitimu wanaotarajiwa (outputs) badala ya utaratibu wa sasa wa utoaji fedha kulingana na idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa (inputs). Aidha  mfumo huu utahakikisha matumizi bora ya rasilimali na ufanisi katika utoaji wa elimu ya juu na ufundi katika vyuo na taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi .

 

 

MAPITIO YA MWAKA 2001/2002

 

Mheshimiwa Spika, baada ya utangulizi huu, napenda sasa kutoa maelezo yafuatayo katika mapitio ya mwaka 2001/2002.

 

ELIMU YA JUU

 

6.                 Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2001/2002 Wizara yangu ilifanikiwa kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa katika vyuo vikuu vya umma toka wanafunzi 3,805  mwaka 2000/2001 hadi wanafunzi 4,755 mwaka 2001/2002.

 

v    Kufanya tathmini  ya uchangiaji gharama za elimu ya juu hususan awamu ya I na ya II, kwa lengo la kuiwezesha Serikali kuunda bodi huru ya kuratibu utoaji na urejeshwaji wa mikopo.

 

v    Kukamilisha hatua za awali za utekelezaji wa mradi wa uhuishaji wa taasisi za elimu ya juu kwa lengo la kuongeza udahili na ufanisi.

 

v    Kuandaa na kuratibu Warsha ili kubadilishana mawazo na mbinu juu ya kudhibiti udanganyifu katika udahili, kwa kuwashirikisha wadau.

 

 

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

 

7.                 Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, yafuatayo yametekelezwa:

 

v    Kuboresha njia za kufundishia na kujifunzia zikiwemo:

 

-         Matumizi ya mfumo wa “Semester” katika masomo ya shahada ya kwanza

-         Utoaji wa mafunzo kwa kutumia mtandao wa tovuti (Website)

-         Ufungaji mitambo ya “video – conferencing” katika vyumba viwili vya mihadhara,  vyenye uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 500 kwa wakati mmoja.

 

v    Kuanzisha programu 13 mpya katika Kitivo cha Uhandisi zinazoendana na mahitaji ya soko. Programu hizo ni,

-         Computer Engineering & Information Technology

-         Electro Power Engineering

-         Chemical and processing Engineering

-         Electro Mechanical Engineering

-         Mechanical Engineering

-         Mining Engineering

-         Mineral Processing Engineering

-         Civil and Structural Engineering

-         Telecommunication Engineering

-         Transportation Engineering

-         Production Engineering

-         Civil and Water Resources Engineering

-         Electrical  Engineering.

 

v    Kuboresha uwiano wa wanafunzi wa kike na kiume kupitia mafunzo maalum kwa wanafunzi wa kike (Pre-Entry Training).

 

v    Kutoa huduma za ushauri wa kitaalam ikiwa ni hatua za makusudi za kuviunganisha vyuo na wananchi.

 

v    Kuboresha na kupanua shughuli za utafiti.  Mkazo zaidi uliwekwa katika kuimarisha miundo mbinu ya utafiti ikiwemo

 

-         Kuimarishwa kwa Kurugenzi ya Utafiti na Uchapishaji.

-         Kuanzishwa kwa kitengo cha Upashanaji Habari za Taarifa za Utafiti.

 

CHUO KIKUU CHA KILIMO CHA SOKOINE

 

8.                 Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Sokoine kimetekeleza yafuatayo:

 

v    Kufanya utafiti, ambapo baadhi ya tafiti zilizofanyika na zinazoendelea ni pamoja na:-

 

-         Mradi wa kufichua mabomu kwa kutumia panya-buku unaendeshwa na SUA kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Antwerp ( Ubeligiji ).

-         Mradi wa Bustani na matunda unaoendeshwa katika maeneo ya Mgeta, Mkuyuni  na Kinole, Mkoa wa Morogoro.

-         Mradi wa kutumia Mbuzi Chotara kuzalisha maziwa.

 

v    Kuboresha na kupanua miundo mbinu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia.  Baadhi ya shughuli zilizofanyika ni:

 

-         Ukarabati wa majengo ikiwemo maktaba iliyopo kampasi ya Solomon Mahlangu, na mabweni ( 8) ya wanafunzi yaliyopo kampasi kuu.

-         Ukamilishaji wa chanzo pekee cha maji.

-         Ununuzi wa nyumba 2 za ghorofa za iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara kwa ajili ya mabweni ya  wanafunzi wa Shahada ya Uzamili.

 

v    Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa toka wanafunzi 774 mwaka 2000/2001 hadi wanafunzi 788  mwaka 2001/2002.

 

v    Kuboresha shughuli za mafunzo, mkazo zaidi uliwekwa katika:

 

-         Kuimarisha kumbukumbu za wanafunzi kwa kufunga programu maalum ijulikanayo kama CELCAT. Mfumo huu utawezesha kuzuia udanganyifu katika udahili.

-         Kupitia upya mitaala yote ili iweze kukidhi mahitaji ya “semester”.

-         Kurekebisha ratiba ya masomo ili kuongeza matumizi ya vyumba vya madarasa na maabara (capacity utilization).

 

CHUO KIKUU HURIA

 

9.                 Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Huria kimetekeleza yafuatayo:

 

v    Kufanya ukarabati katika majengo ya makazi yake mapya, ambapo jumla ya Shs. 200 milioni zimetumika.

 

v    Kuanzisha programu za Shahada ya Uzamili na Falsafa katika fani za Sayansi za Jamii, Teknolojia na Elimu ya Mazingira, Sheria na Elimu.

 

v    Kuendelea kuimarisha vituo vyake mikoani ili viweze kutimiza majukumu yake vizuri.

 

v    Kuchapisha aina ya vitabu 112 kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia.

 

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA SAYANSI NA TIBA MUHIMBILI

 

10.            Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi na Tiba cha Muhimbili kimetekeleza yafuatayo:

 

v    Kuendeleza  ukarabati katika jengo la Kitivo cha Tiba ya meno.

 

v    Kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka wanafunzi 232  mwaka 2000/2001 hadi wanafunzi  290 mwaka 2001/2002.

 

v    Kuendelea na shughuli za utafiti katika nyanja mbalimbali za Sayansi za Afya na Tiba.

 

v    Kuimarisha miundo mbinu ya mawasiliano ikiwemo mawasiliano ya mtandao wa tovuti.

 

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ARDHI NA USANIFU MAJENGO

 

11.            Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi na           Usanifu Majengo kimetekeleza yafuatayo:

 

v    Kuanzishwa kwa kitengo maalum cha uendeshaji na usimamizi wa miradi “Programme Management Unit”.

v    Kuanzishwa kwa kitengo cha kusimamia miradi ya ushauri wa kitaalam kijulikanacho kama UCLAS Consultancy Unit (UCU)

 

v    Kuendelea na ujenzi wa jengo la Utawala ambalo linatarajia kugharimu jumla ya Sh 304,057,453. Asilimia 80 ya gharama za ujenzi huu zitatokana na Fedha zitakazozalishwa na Chuo ambapo hadi sasa Chuo kimechangia jumla ya Sh. 71,166,868 katika ujenzi huu.

 

v    Kuweka uwiano mzuri baina ya idadi ya walimu na wafanyakazi wengine ili kupunguza gharama za uendeshaji na kuongeza ufanisi.  Kazi hii imekamilika kwa kupunguza  wafanyakazi 118

 

v    Kukamilika kwa maandalizi ya kuanzisha masomo ya uzamili katika Mipango na Maendeleo ya Miji.

 

v    Kuendelea kupitia mitaala kwa lengo la kuiboresha.

 

v    Kuanzisha Kitengo cha kutoa  elimu ya kukabiliana na Maafa.

 

BARAZA LA ITHIBATI LA ELIMU YA JUU

 

12.            Mheshimiwa Spika, Baraza la Ithibati la Elimu ya Juu limetekeleza yafuatayo:

 

v    Kutoa hati za usajili wa muda kwa vyuo vikuu vitatu ambavyo ni Chuo Kikuu cha Mzumbe, Chuo Kikuu Kishiriki cha Waldorf na Chuo Kikuu cha Aga Khan Kampasi ya Tanzania. Aidha, Baraza limekifuta Chuo Kikuu cha Lake – Mwanza kwa kushindwa kutimiza masharti ya uanzishwaji wa Vyuo Vikuu.

 

v    Kutoa hati za usajili kamili kwa vyuo vikuu vitatu ambavyo ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Zanzibar, Chuo Kikuu cha Tumaini na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia.

 

v    Kuratibu kazi ya udahili wa wanafunzi katika vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu.

 

ELIMU YA UFUNDI

 

13.            Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Elimu ya Ufundi Wizara yangu imetekeleza yafuatayo:

 

v    Imekarabati majengo, mitambo na vifaa mbali mbali katika karakana na maabara ya vyuo vya Ufundi Arusha na Mbeya.

 

v    Imetoa mafunzo ya muda mrefu ndani na nje ya nchi kwa walimu wa vyuo vya Ufundi  Arusha na Mbeya.  Walimu watatu (3) kwa Kiwango cha Udaktari wa Falsafa (PhD), sita (6) Shahada ya Pili (MSc), wanne (4) Diploma ya Uzamili na wawili (2) Stashahada ya Juu ya Uhandisi (ADE). Walimu ( 6 ) wamehitimu masomo yao na kurejea katika vituo vyao vya kazi. Aidha, walimu ( 9 ) bado wanaendelea na masomo.

 

v    Imeendelea na programu ya kuwahamasisha wasichana ili waweze kujiunga na elimu ya ufundi.

 

v    Imeweka mashine na mitambo yenye thamani ya Shs. Million 87 kwa Chuo cha Ufundi Mbeya katika juhudi za kukiimarisha ili kutoa mafunzo zaidi ya ngazi ya juu ya elimu ya ufundi.

 

v    Imeongeza vitabu vya kiada na rejea kwa vyuo vya Ufundi vya Arusha na Mbeya.

 

v    Imeanza na kuendelea na ujenzi wa bweni la wanafunzi kwa Chuo cha Ufundi Mbeya lenye uwezo wa nafasi 240 za malazi.

 

v    Imekamilisha mpango wa kuanzisha Stashahada ya juu ya uhandisi kwa Chuo cha Ufundi Mbeya.

 

v    Imeajiri walimu watano (5) wenye kiwango cha elimu ya Shahada ya Pili (MSc) kwa ajili ya Chuo cha Ufundi Mbeya.

 

v    Imetoa mafunzo ya uongozi kwa wakuu wa Idara za taaluma (25) katika vyuo vya Ufundi Arusha na Mbeya.

 

TAASISI YA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM

 

14.            Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaa imetekeleza yafuatayo:

 

v    Imekarabati majengo, vifaa vya karakana na maabara katika juhudi za kuboresha mazingira ya utoaji elimu.

 

v    Imewapatia mafunzo walimu kumi na moja (11) kwa kiwango cha Udaktari wa Falsafa, (PhD), sita (6) Shahada ya Uzamili (MSc), sita (6) Diploma ya Uzamili na wawili (2) Stashahada ya Juu ya Uhandisi (ADE).

 

v    Imewapatia mafunzo ya uongozi wakuu wa Idara za Taaluma.

 

v    Imeanzisha maabara mpya na ya kisasa ya kompyuta ikiwa na kompyuta hamsini (50) za kuanzia kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

 

v    Imepata mitambo na vifaa vya karakana kutoka kituo cha “High Precision Technology Centre” (HPTC) ambacho kilikuwa chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara.

 

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI

 

15.          Mheshimiwa Spika, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi           limetekeleza yafuatayo:

 

v    Limetoa usajili kamili kwa vyuo ishirini na mbili (22) vyenye uwezo wa kutoa mafunzo ya elimu ya ufundi.

 

v    Limeandaa na kukamilisha jumla ya  miongozo na taratibu tano (5) za kuwezesha kutoa ithibati, kutayarisha na kukuza mitaala ya ufundi, kudhibiti  ubora wa mafunzo, kufanya utafiti na ushauri wa kitaalamu na  kuendesha mitihani ya elimu ya ufundi.

 

v    Limepata ofisi za kudumu Katika Majengo ya kilichokuwa Kituo cha HPTC.

 

SAYANSI NA TEKNOLOJIA

 

16.          Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Sayansi na Teknolojia           imetekeleza yafuatayo:

 

v    Iliendelea na uhamasishaji wa wananchi kupitia vyombo mbali mbali vya habari kama vile redio, televisheni na magazeti juu ya umuhimu wa utumiaji wa Sayansi na Teknolojia katika maisha yao ya kila siku ambapo vipindi 56 vilitangazwa kupitia Redio Tanzania Dar Es Salaam.

 

v    Aidha, Wizara ilifanya tathmini ya usikivu wa vipindi hivyo katika mikoa ya Shinyanga, Morogoro, Dodoma, Mbeya, Mwanza na Kagera kwa lengo la uboreshwaji.

 

v    Kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Utamaduni Wizara yangu ilifanya maandalizi ya awali ya uundaji wa Kamati ya Kitaifa itakayoshughulikia uendelezaji wa Elimu ya Sayansi nchini. Aidha, iliendelea kufanya mawasiliano na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa juu ya uundaji upya wa Kamati za Sayansi na Teknolojia katika ngazi za Mikoa na Wilaya.

 

v    Imeshirikiana na taasisi ya Maendeleo ya Utafiti na Viwanda Nchini (Tanzania Industrial Research Organization – TIRDO) kufanya utafiti wa awali kuhusu  usambazaji wa matokeo ya Utafiti katika Mikoa ya Shinyanga, Tanga na Ruvuma.  Utafiti huo ni juu ya kuimarisha mfumo wa Maji na “Development and Dissemination of Biomass stove for rural Shinyanga”,  “Food preservation/processing Training Cum and Improving Water System.

 

v    Ilikukusanya takwimu mbalimbali zinazohusu hali ya Sayansi na Teknolojia katika Mikoa 10 hapa nchini.Mikoa hiyo ni pamoja na Kilimanjaro,Arusha,Mbeya,Iringa,Tanga,Dodoma,Morogoro,Shinyanga,Ruvuma, na Mwanza.

 

v    Kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, Idara ya Hisabati, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia pamoja na Shirika la Kimataifa lijulikanalo kama “ The Third World  Academy of Sciences” Wizara yangu iliendesha Warsha ya Kimataifa ya hisabati, warsha iliyofanyika tarehe 19-21 Novemba 2001, mjini Arusha kwa lengo la kuelewa ukubalikaji wa hisabati katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara.

 

v    Aidha, kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia nchini, Wizara yangu iliandaa na kuendesha warsha ya kujadili mpango wa miaka mitano wa uendelezaji wa sayansi ya msingi nchini, warsha iliyofanyika tarehe 13 – 14 Mei, 2002, jijini Dar Es Salaam.kwa kuwashirikisha wadau. 

 

v    Ilitoa Tuzo ya Sayansi kwa wasichana wanne waliofanya vizuri katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka 2001.Tuzo hiyo ilitolewa katika somo la Hisabati, Kemia, Fizikia na Baiolojia, kwa lengo la kuhamasisha wanawake na wasichana wengi kujiunga na fani ya Sayansi na Teknolojia.

 

v    Kwa kushirikiana na wataalamu katika fani ya Nishati ya Jua kutoka Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, Kitivo cha Sayansi, Wizara yangu ilifanya tathmini ya awali ya vijiji vitakavyonufaika na mradi wa matumizi ya Nishati ya Jua katika Wilaya ya Maswa, mkoani Shinyanga. Aidha, mradi huu unagharimiwa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.

 

v    Wizara imepokea maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusu kufutwa kwa Sheria Na. 5 ya mwaka 1983 iliyounda Tume ya Taifa ya Mionzi na kuanzisha kutungwa kwa Sheria mpya itakayounda Mamlaka ya nguvu za Atomiki nchini.

 

TUME YA TAIFA YA MIONZI

 

17.          Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Tume ya Taifa ya Mionzi           imetekeleza yafuatayo:

 

v    Tume iliendelea na utoaji wa huduma ya upimaji mionzi kwa wafanyakazi 943 wanaotumia mionzi katika vituo 95 kati ya vituo 125 vilivyopo nchini.

 

v    Sampuli 2,143 za vyakula, mbolea na bidhaa nyingine zilipimwa.

 

v    Ilikagua vituo 135 vya X- ray ambapo vituo 11 vilifungiwa kutoa huduma hiyo kutokana na kutokidhi viwango salama vilivyokubaliwa kimataifa katika huduma za uchunguzi wa magonjwa mahospitalini.

 

v    Ilitengeneza mashine 15 za X-ray, na vifaa 18 vya electroniki.

 

v    Ilihakiki vifaa 31 vya kupimia mionzi ambapo vifaa 9 vilitoka nchini Kenya. Aidha, ilivipatia vituo 6 vifaa vya kinga vya mionzi (Lead glass).

 

v    Iliendelea kutoa elimu ya kinga ya mionzi kwa kupitia njia za redio na televisheni

 

v    Tume iliendelea kuratibu na kusimamia utekelezaji wa miradi minne inayogharimiwa na na Shirika la Kimatifa la Nguvu za Atomiki (IAEA) ambapo taasisi husika zilipewa zaidi ya dola za Kimarekani zipatazo 500,000 kwa ajili ya mafunzo, ununuzi wa vifaa na ushauri wa kitaalamu.

 

v    Ili kuepusha athari zitokanazo na mabaki ya vyanzo vya mionzi, Tume iliweza kukusanya mabaki hayo kutoka Taasisi ya Saratani ya Hospitali ya Ocean Road, Kiwanda cha Bia Dar es Salaam, Ofisi za Ushuru wa Forodha zilizoko uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na shule ya Sekondari ya Shaaban Robert iliyoko jijini Dar Es Salaam na kuyapeleka katika hifadhi ya muda iliyoko Arusha.

 

 

 

TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA

 

18.          Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia           imetekeleza yafuatayo:

 

v    Iliendelea na ukamilishaji wa rasimu ya uanzishaji wa Masijala ya Taifa ya Takwimu za Utafiti nchini ( The National Research Registry) kwa kuzingatia maoni toka kwa wadau mbalimbali ambapo hadi hivi sasa Tume imesajili tafiti 353.

 

v    Iliendesha mafunzo ya wakufunzi kuhusu kilimo cha Uyoga katika kituo cha utafiti cha Ukiruguru, Mwanza, ambapo washiriki 20 walihudhuria mafunzo hayo.

 

v    Ilishiriki katika utafiti wa miradi miwili ya nishati mbadala ya upepo kwa ajili ya kuzalisha umeme kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini, Tanzania Technology Development Organization  (TATEDO) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

 

v    Ilishirikiana na wafadhili mbalimbali kutekeleza miradi ya Teknolojia ya mawasiliano kama:

 

(i)   Teknolojia ya mawasiliano kwa ajili ya Utawala bora katika Wilaya ya Kinondoni.

 

(ii)            Kuanzisha vituo vya mawasiliano katika kambi ya wakimbizi ya Lukole wilayani Ngara, Lugoba wilayani Bagamoyo na Dakawa mkoani Morogoro.

 

(iii)         Iliendesha mafunzo ya kompyuta kwa washiriki 308 na imeunganisha mawasiliano  ya kompyuta katika vituo 14 jijini Dar es Salaam

 

v    Ilishirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, kufanya utafiti kuhusu kupungua kwa barafu katika mlima Kilimanjaro.

 

v    Kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Tume iliendesha warsha tatu ili kupata maoni yatakayopelekea kuundwa kwa Sera ya Baioteknolojia nchini.

 

v    Ilianzisha mradi wa utafiti wa tekinolojia asilia kwa lengo la kuweka kumbu kumbu za Teknolojia hizo.

 

TUME YA TAIFA YA UNESCO

 

19.          Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya UNESCO imetekeleza           yafuatayo:

 

v    Ilishirikisha Taifa katika Kikao cha 31 cha Mkutano Mkuu wa UNESCO kilichofanyika mjini Paris, Ufaransa Oktoba/Novemba, 2001 ambacho kilipitisha mpango wa miaka 6 (2002 –2007) na programu ya kazi na bajeti ya miaka miwili (2002-2003). Katika kikao hicho Tanzania ilichaguliwa  kwa mara nyingine tena kuwa  mjumbe wa Bodi ya Utendaji wa Shirika hilo  kwa kipindi cha miaka mine ijayo ( 2002-2005).

 

v    Serikali imemteua Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania UNESCO  Prof. Mohamed Sheya kuiwakilisha  katika Bodi hiyo.

 

v    Aidha, Tanzania ilichaguliwa kushiriki katika mabaraza matano ya kitaalam ambapo wawakilishi wake wameteuliwa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni pamoja na Taasisi ya Mambo ya Bahari, Tume ya Sayansi na Teknolojia na Chuo cha Usimamizi wa Fedha.

 

v    Iliratibu utekelezaji wa miradi ya mashirikiano na UNESCO kama ifuatavyo:-

 

-     Kuipatia makazi mapya Ofisi ya Kanda ya UNESCO inayosimamia shughuli zake hapa Tanzania, Comoro, Shelisheli, Madagascar na Mauritius.

 

-          Mradi wa Mawasiliano Vijijini huko Sengerema mkoani           Mwanza.

 

-          Mradi wa kuimarisha Utawala bora kwa kutumia           Teknolojia            ya kisasa ya mawasiliano katika Manispaa ya Zanzibar.

 

-          Mradi wa kuanzisha Maktaba ya Wilaya ya Bagamoyo.

 

-         Mradi wa hifadhi ya magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo      Mnara kama sehemu ya mradi wa tamaduni za Dunia.

 

-         Mradi wa Uchunguzi/Utafiti wa kuanzisha      kumbukumbu na      makumbusho ya Msafara wa Biashara ya Utumwa.

 

v    Kwa kushirikiana na taasisi zingine Wizara yangu imetekeleza yafuatayo.

 

-         Mradi wa kuboresha utunzaji  wa Nyaraka za Taifa.

 

v    Mpango wa kuimarisha Elimu kwa Wote (Education for All Programme). Mpango huu unafuatilia utekelezaji wa maamuzi ya mkutano wa Elimu kwa wote uliofanyika Jomtien, Thailand mwaka 1990 na ule uliofanyika Dakar Senegal , mwaka 2000. Wizara ya Elimu na Utamaduni (Tanzania Bara ) na ile ya Elimu, Utamaduni na Michezo (Zanzibar) zimetekeleza maamuzi ya mikutano hiyo. Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazoshirikishwa katika Warsha za Waratibu zitakazofanyika Abijan, Nigeria na Paris, Ufaransa.

 

v    Maandalizi ya Mkutano wa Wahisani wa Kuanzishwa kwa Kituo cha Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika kitakachotoa mafunzo juu ya mwamko wa kutunza mashine, mitambo, miundo mbinu (Culture of Maintenance) katika Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam.

 

v    Iliratibu ushiriki wa watanzania katika baadhi ya  warsha, mikutano na “Scholarship” zilizoendeshwa na UNESCO kama ifuatavyo:-

 

-      Mkutano wa Kimataifa wa Walimu uliofanyika Geneva, Uswisi Septemba 2001. Mada kuu ya Mkutano ilikuwa ni Elimu kwa ajili ya kujifunza kuishi pamoja. Ujumbe wa Serikali kwenye Mkutano huo uliongozwa na Waziri wa Elimu na Utamaduni Mh. Joseph Mungai ( MB ).

 

-       Warsha za mafunzo kwa Wakufunzi wa matumizi ya Nishati ya Jua zilizofanyika Zimbabwe, Oktoba 2001 na Mjini Bagamoyo, Januari 2002. Madhumuni ya Warsha hizo yalikuwa ni kuhamasisha na kuwapatia wakufunzi wa vituo husika mbinu bora zaidi za mafunzo kuhusu ufungaji wa mitambo, utunzaji wake na matumizi ya nishati ya jua.

-       Warsha ya kuandaa mradi wa Uhifadhi wa Urithi Asilia wa Dunia nchini Tanzania iliyofanyika Mjini Moshi mwezi Januari 2002. Warsha hii iliandaliwa kwa kushirikiana na Shirika la Wanyama Pori (TANAPA) na Chuo Cha Wanyama Pori, Mweka. Madhumuni ya Warsha hiyo ilikuwa kuandaa mradi ambao utaziwezesha taasisi za Utafiti wa Wanyama Pori kupata vifaa, miundombinu na utaalam utakao zisaidia kufanya Utafiti na kutoa mafunzo bora zaidi.

 

-         Warsha ya Uendelezaji wa Sehemu Kame Kusini mwa Afrika iliyofanyika Botswana, Februari 2002. Washiriki walitoka Idara za Mazingira Tanzania Bara na Visiwani. Azimio la Mkutano huo lilitaka kila mshiriki kutafuta mbinu mwafaka za utekelezaji wa maamuzi kulingana na mazingira ya nchi husika. Tanzania imeshawasilisha msimamo wake.

 

          -          Warsha ya Elimu Endelevu iliyofanyika Kampala,                                         Uganda, Aprili 2002. Serikali iliwakilishwa kwenye                          Mkutano huo na Wizara ya Elimu na Utamaduni                                      (Tanzania Bara) na Wizara ya Elimu, Utamaduni na                       Michezo( Zanzibar ). Warsha iliandaa zana za utafiti wa                     kutathmini ubora wa uelewa wa wanafunzi katika ngazi                               ya Kidato cha Kwanza katika Masomo ya Hisabati,                     Fizikia, Kemia na Baiolojia katika nchi zinazozungumza                          Kiingereza Barani Afrika.

 

v    Mafunzo chini ya programmu ya UNESCO kuhusu uendelezaji wa fani ya mawasiliano. Katika kipindi kilichopita mfanyakazi mmoja kutoka Kituo cha Televisheni cha ITV alipatiwa mafunzo nchini Korea Kusini.

 

UTAWALA NA UTUMISHI

20.          Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Utawala na Utumishi           Wizara yangu imetekeleza yafuatayo:

 

v    Imewapandisha cheo watumishi 80 wa kada mbalimbali.

 

v    Imewapatia mafunzo ya muda mrefu watumishi 6 na muda mfupi watumishi 37 ndani na nje ya nchi.

 

v    Imeajiri watumishi 11 kwa ajili ya kupunguza uhaba wa Wafanyakazi wa Wizara na kuratibu upatikanaji wa vibali 51vya ajira za Wanataaluma Wageni kwa ajili ya Vyuo Vikuu nchini.

 

v    Imeendesha Semina moja na Warsha moja kuwaelimisha Wafanyakazi na Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu kuhusu athari ya ugonjwa wa UKIMWI.

 

v    Imekamilisha uundaji  wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara kwa lengo la kushirikisha wafanyakazi katika sehemu ya kazi. Baraza lilizinduliwa rasmi tarehe 22 Machi, 2002.

 

v    Imeendesha Semina za maadili katika utumishi wa Umma kwa Watumishi wote wa Wizara Makao Makuu kwa lengo la kuzielewa vyema Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma ili Kuboresha utoaji huduma kwa Wananchi.

 

 

MPANGO WA MWAKA 2002/2003

 

21.          Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2002/2003 Wizara yangu inatarajia kutekeleza mambo yafuatayo:

 

ELIMU YA JUU

 

v    Kuanzisha chombo cha kusimamia utoaji na urejeshwaji wa mikopo ya wanafunzi.

 

v    Kuimarisha mfuko wa elimu ili uweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

 

v    Kuendelea na utekelezaji wa mradi wa uhuishaji wa vyuo vya elimu ya juu.

 

v    kuendelea kuratibu udahili wa wanafunzi katika vyuo vya elimu ya juu.

 

v    Kuwasilisha Mswada wa Sheria ya Elimu ya Juu Bungeni.

 

 

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

 

22.          Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinatarajia           kutekeleza mambo yafuatayo:

 

v    Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodhaminiwa na Serikali kutoka wanafunzi 2,246 wa mwaka wa  kwanza hadi 2,358 na kutoka wanafunzi 600 hadi 650 wa Shahada za Uzamili.

 

v    Kuanzisha kitengo cha AUDIOVISUAL ili kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupata elimu ya juu kupitia mtandao wa kompyuta

 

v    Kuendeleza utafiti na kuimarisha kitengo cha kumbukumbu za utafiti na usambazaji wa matokeo ya utafiti.

 

v    Kujenga jengo la kupumzikia wanafunzi na kufanya ukarabati wa majengo na viwanja vya michezo.

 

v    Kuendelea kuimarisha na kuboresha uwiano kati ya wanafunzi wa kike na kiume kutoka asilimia 26 hadi asilimia 30 ifikapo mwaka 2003/2004.

 

CHUO KIKUU CHA KILIMO CHA SOKOINE

 

23.          Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine           kinatarajia kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kufanya tathmini ya mahitaji ya elimu kwa wakulima na kueneza matumizi ya stadi za uongozi bora katika jamii ya wakulima.

 

v    Kuendelea kutekeleza mpango wa chuo na kukiwezesha kuongeza mapato yake.

 

v    Kuendelea kuimarisha mafunzo ya Shahada ya kwanza kwa kuanzisha Kozi nyingi zaidi zinazokidhi mahitaji ya Soko na kuimarisha mafunzo ya vitendo.

 

v    Kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka wanafunzi 788 hadi kufikia wanafunzi 842 wa mwaka wa kwanza.

v    Kuendeleza shughuli za utafiti katika maeneo ya Kilimo, Misitu, Tiba na Sayansi ya Wanyama.

 

CHUO KIKUU HURIA

 

24.          Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Huria kinakusudia           kutekeleza           yafuatayo:

 

v    Kuendelea na shughuli za ukarabati wa majengo ya makao makuu ya chuo.

 

v    Kuimarisha mawasiliano baina ya mikoa na makao makuu., na kuendelea kuhamasisha wataalamu mbalimbali kuandaa vitabu vya kiada kwa ajili ya wanafunzi wa chuo.

 

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA AFYA NA TIBA MUHIMBILI

 

25.          Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Tiba na Afya           Muhimbili kimekusudia kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kuongeza nafasi za kulala wanafunzi kwa kununua majengo ya lililokuwa Shirika la Ukaguzi wa Mahesabu  la Taifa (TAC) huko Masaki.

 

v    Kutoa mafunzo kwa utaratibu wa ‘Semester’

 

v    Kuongeza udahili wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza kutoka wanafunzi 290 hadi wanafunzi 300.

 

v    Kupanua na kuongeza idadi ya maabara na vifaa.

 

CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ARDHI NA USANIFU MAJENGO

 

26.          Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi na           Usanifu           Majengo kinatarajia kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kuandaa upya na kuboresha mitaala na mbinu za kufundishia Shahada za Uzamili.

 

v    Kuendelaea kuweka uwiano mzuri kati ya idadi ya wanafunzi wanawake na ile ya wanaume ili kufikia kiwango cha asilimia 20 ya idadi ya wanawake kwa mwaka 2002/ 2003.

 

v    Kuendelea na shughuli za Ujenzi wa Jengo la Utawala.

 

v    Kuimarisha Kitengo cha Elimu Endelevu kwa kutoa mafunzo zaidi kuhusu kukabili majanga.

 

v    Kuimarisha kutumia mtandao wa teknolojia ya kisasa ya mawasiliano.

 

v    Kupanua jengo la Maktaba kwa msaada wa NORAD.

 

CHUO KIKUU CHA MZUMBE

 

27.                      Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Mzumbe kinatarajia kutekeleza      yafuatayo:

v    Kukamilisha muundo wa Utawala wa Chuo ambao utakuwa na,

-         Mkuu wa Chuo ( Chancellor )

-         Baraza la Chuo ambalo litakuwa na mamlaka ya mwisho juu maamuzi ya Kisera, uendeshaji na Utawala wa Chuo.

-         Seneti, ambacho ni chombo cha juu cha ushauri juu ya Sera za Kitaaluma na kitawajibika kwa Baraza.

-         Makamu Mkuu wa Chuo ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa Chuo, ambaye atawajibika kwa Baraza la Chuo kwa masuala yote ya uratibu, usimamizi na Utawala wa Chuo. Makamu Mkuu wa Chuo atasaidiwa na Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo katika masuala ya taaluma na Mrajisi katika masuala ya Utawala na fedha.

-         Bodi ya Kitivo / Taasisi / Kurugenzi ambayo itawajibika kwa Seneti katika masuala ya Programu za Kitaaluma, kuboresha, kudhibiti na kuoanisha shughuli zote za kitaaluma katika ngazi ya Kitivo/ Taasisi na Kurugenzi.

-         Kamati za Idara ambazo zitakuwa ni chombo cha msingi katika utaratibu wa kutoa maamuzi.

-         Kamati ndogo za Baraza la Chuo zitakazohusika na maendeleo ya Wafanyakazi, fedha, maendeleo na mipango.

-         Chuo kinatarajia kuwa na Vitivo, Taasisi na kurugenzi zifuatazo

 Taasisi ya Elimu Endelevu.

 Taasisi ya Taaluma za Maendeleo.

 Kitivo Cha Sayansi za Jamii.

 Kitivo cha Biashara.

 Kitivo Cha Sayansi na Teknolojia.

 Kitivo Cha Sheria.

 Kurugezi ya Utafiti, Uchapishaji na masomo ya Uzamili.

 Kurugenzi ya Maktaba na Huduma za Kiufundi.

 Kurugenzi ya Teknolojia, Habari na Mawasiliano.

v    Chuo Kikuu cha Mzumbe kitakuwa na jumla ya wanafunzi 1,154 wanaoendelea na masomo na wanafunzi 300 watakaodahiliwa kwa mwaka wa masomo 2002/2003.

v    Chuo kitaanza na jumla ya Wahadhiri 129, kati ya hao 24 ni wahadhiri wa kike na 105 ni wa kiume. Sifa za walimu hawa kitaaluma ni kama ifuatavyo.

-         Walimu wenye Shahada ya Udaktari wa Falsafa 15

-         Wanaosomea Shahada ya Udaktari wa Falsafa 19

-         Walimu wenye Shahada ya Uzamili 81

-         Wanaosomea Shahada ya Uzamili 5

-         Walimu wenye Shahada ya Kwanza 9

 

v    Kuendesha mafunzo ya muda mrefu kwa wanachuo 1,500 wa Vitivo vya Biashara, Sheria na Sayansi za Kijamii.

 

v    Kuendesha kozi fupi 48 katika Taasisi ya Uongozi.

 

v    Kuendesha ushauri kwa wateja 12.

 

v    Kufanya tafiti tisa katika nyanja mbali mbali kwenye fani za Sayansi ya Kijamii.

 

v    Kupanua Kitengo cha Kompyuta ili kiweze kuhuisha matumizi ya Teknolojia ya mawasiliano katika kufundisha na kujifunza.

 

BARAZA LA ITHIBATI LA ELIMU YA JUU

 

28.                      Mheshimiwa Spika, Baraza la Ithibati la Elimu ya Juu linatarajia      kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kutayarisha mfumo wa vyeti vitakavyotolewa baada ya kuhitimu elimu ya juu.

 

v    Kuwaendeleza wafanyakazi kwa kuinua viwango vya elimu zao.

 

ELIMU YA UFUNDI

29.                      Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2002/2003 inakusudia      kutekeleza yafuatayo:-

 

v    Kutoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa walimu na watumishi wengine ndani na nje ya nchi.

 

v    Kukarabati majengo, mitambo na vifaa mbalimbali katika vyuo vya Ufundi Arusha na Mbeya.

 

v    Kutoa mafunzo maalumu ili kuinua viwango vya taaluma ya wasichana kabla ya kujiunga na elimu ya ufundi katika vyuo vya Ufundi Arusha na Mbeya.

 

v    Kutoa mafunzo ya Stashahada ya Juu ya Uhandisi (ADE) kwa Chuo cha Ufundi Mbeya katika hatua ya kukibadili kuwa Taasisi ya Teknolojia na hatimaye baadaye kukiwezesha kutoa mafunzo ya ngazi ya Chuo Kikuu.

 

v    Kununua mashine na mitambo ya kufundishia kwa gharama ya jumla ya Shs. 150 Milioni kwa ajili ya Chuo cha Ufundi Mbeya.

 

v    Kuongeza vitabu vya kiada na rejea katika fani za mitambo, umeme, magari, usanifu majengo, ujenzi na masomo ya jumla kwa vyuo vya Ufundi Arusha na Mbeya.

 

TAASISI YA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM

 

30.                      Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2002/2003 Taasisi      inakusudia kutekeleza yafuatayo:-

 

v    Kuboresha maktaba kwa kuongeza vitabu na nyenzo za kufundishia.

 

v    Kukarabati majengo, mitambo na vifaa mbali mbali katika karakana ya Taasisi.

 

v    Kuwapa mafunzo ya muda mrefu walimu na wafanyakazi wengine ndani na nje ya nchi.

 

v    Kuandaa mpango wa kutoa mafunzo ya uzamili kwa kozi mbali mbali zitolewazo katika Taasisi.

 

v    Kuandaa mpango wa kutoa mafunzo ya Stashahada ya Juu ya Uhandisi kwa nyakati za jioni.

 

v    Kuandaa mtaala mpya wa kozi ya mafunzo ya kompyuta, kuanzisha maabara tatu za kompyuta, kuboresha mawasiliano ya mtandao katika Taasisi kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida).

 

v    Kuandaa mtaala wa mafunzo ya Ufundi Sanifu (FTC) wa migodi na madini (“Mining & Mineral Processing Engineering)”.

 

v    Kuratibu utekelezaji wa mpango wa kujenga utamaduni wa ukarabati “(Culture of Maintenance and Maintenance Network)”.

 

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI

 

31.                      Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2002/2003  Baraza      linakusudia kutekeleza yafuatayo:-

 

v    Kusajili vyuo arobaini (40) vyenye uwezo wa kutoa mafunzo ya elimu ya ufundi.

 

v    Kutayarisha mitaala ya kufundishia masomo ya ufundi kwa programu za masomo matano (5).

 

v    Kuratibu mitihani ya ufundi kwa ngazi ya Ufundi Sanifu (FTC) na Stashahada ya Juu ya Uhandisi (ADE).

 

v    Kuratibu mafunzo juu ya utayarishaji na ukuzaji wa mitaala inayozingatia umahiri (‘competence based curricula)”.

SAYANSI NA TEKNOLOJIA

 

32.                      Mheshimiwa Spika, Sayansi na Teknolojia inatarajia kutekeleza      yafuatayo:

 

v    Kuendelea na maandalizi ya kuunda upya kamati za Sayansi na Teknolojia katika ngazi za Mkoa na Wilaya na kuanza maandalizi ya kuweka Vituo vya Sayansi ( Science Parks )

 

v    Kuandaa  Sera ya Utafiti wa sayansi na Teknolojia nchini.

 

v    Kutunga Sheria Mpya itakayoipa Tume ya Taifa ya Mionzi uwezo na majukumu mapya.

 

v    Kurejea Sheria Na. 7 ya mwaka 1986 iliyounda Tume ya Sayansi na Teknolojia.

 

v    Kukamilisha uundaji wa Kamati ya Kitaifa ya Elimu ya Sayansi na Teknolojia nchini.

 

TUME YA TAIFA YA MIONZI

 

33.                      Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya Mionzi inatarajia kutekeleza      yafuatayo:

 

v    Kuendelea na uimarishaji wa huduma za kinga za mionzi kwa watumiaji mionzi pamoja na kuendelea na ukaguzi wa mionzi hiyo kwenye sampuli za vyakula na mazingira.

 

v    Kuendelea kuratibu na kusimamia matumizi ya Teknolojia za mionzi katika miradi inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki nchini.

 

v    Kuendelea na huduma za matengenezo ya vifaa vya elektroniki na mashine za X- ray

 

v    Kukamilisha mpango wa kushughulikia dharura za mionzi kitaifa (Radiological Emergency Plans and Preparedness).

 

v    Kujenga Kituo cha kudumu cha kuhifadhi mabaki ya vyanzo vya mionzi aionisha na isiyo aionisha.

 

v    Kutumia vipimo vipya maalum kwa mfumo unaokubalika Kimataifa ( Basic Safety Standards )

 

TUME YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA

 

34.          Mheshimiwa Spika, Tume ya Sayansi na Teknolojia inatarajia           kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kukamilisha Masijala ya Taifa ya Utafiti itakayojengwa COSTECH.

 

v    Kufuatilia utekelezaji wa miradi ya matumizi ya nishati mbadala kama vile makaa ya mawe, mionzi ya jua, upepo na gesi ya samadi majumbani

 

v    Kuandaa Kongamano la wanasayansi na watafiti litakalofanyika sambamba na maonyesho ya sayansi ya vijana kwa lengo la kujadili maendeleo ya sayansi nchini.

 

v    Kuendelea na upanuzi wa mtandao wa mawasiliano kwa njia ya kompyuta ili kuboresha mawasiliano  kati ya taasisi, asasi na mtandao wa watafiti wa nchi za nje

 

TUME YA TAIFA YA UNESCO

 

35.           Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya UNESCO inatarajia                     kutekeleza yafuatayo:

 

v    Kuratibu utekelezaji wa maamuzi ya Kikao cha 31 cha Mkutano Mkuu wa UNESCO kwa kushirikiana na vyombo vya Serikali na Taasisi nyingine.

 

v    Kuratibu utekelezaji wa  miradi itakayopata ushirikiano wa UNESCO.

 

v    Kuimarisha Tume kimuundo na Ofisi za UNESCO kulingana na Mkataba kati ya Serikali na Shirika hilo.

v    Kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Utamaduni ( Bara ) na Wizara ya Elimu na Michezo (Visiwani ),   Tume itaratibu maandalizi ya Mkutano wa nane wa Mawaziri wa Elimu Barani Afrika ( MINEDAF VIII ) utakaofanyika nchini tarehe 2 – 6 Desemba 2002. Mkutano huu utatanguliwa na Kikao cha Waheshimiwa Wabunge wenye taaluma ya elimu Barani Afrika tarehe 28 Novemba 2002

 

v    Kushiriki mkutano wa Wahisani kwa ajili ya kuchangisha fedha za kugharamia mradi wa kutoa mafunzo ya utamaduni wa ukarabati wa vifaa/miundo mbinu katika Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam.  Mkutano huu unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka 2002.

 

v    Kuimarisha mpango wa Klabu za UNESCO na mtandao wa shule za kushirikishwa katika mipango ya UNESCO, kwa lengo la kuimarisha utamaduni wa amani.

 

 UTAWALA NA UTUMISHI.

 

36.           Mheshimiwa Spika, Utawala na Utumishi inatarajia kutekeleza yafuatayo.

 

v    Itaendelea kushirikiana na Mamlaka husika ili kupata kibali cha kuajiri Wanataaluma, Walimu na Watumishi wengine kwa lengo la kupunguza uhaba wa wafanyakazi katikaVyuo, Taasisi za Wizara pamoja na Wizara yenyewe.

 

v    Itaendelea kuendesha Semina na Warsha za kuelimisha Wafanyakazi na Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu na Ufundi kuhusu athari za ugonjwa hatari wa Ukimwi.

 

v    Kuwapandisha cheo watumishi 60 wa kada mbalimbali ambao wametimiza masharti ya kupanda daraja.

 

v    Kudhamini watumishi 40 mafunzo ya muda mfupi na watumishi 12 kwa mafunzo ya muda mrefu.

 

v    Kuendelea kuendesha Semina za maadili Wizarani  kwa lengo la kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

MWELEKEO WA BAJETI YA MWAKA 2002/2003

37.          Mheshimiwa Spika, Wizara yangu itatoa kipaumbele katika maeneo yafuatayo:

 

v    Kuratibu uanzishwaji wa chombo cha kutoa na kurejesha mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu.

 

v    Kuimarisha Chuo cha Ufundi Mbeya ili kiweze kutoa mafunzo ya Stashahada ya Elimu ya Ufundi, kwa lengo la kufikia hadhi ya Chuo Kikuu.

 

v    Kuendelea kupitia upya mitaala ili mafunzo yatolewayo yaweze kukidhi mahitaji ya soko huria na utandawazi.Mkazo zaidi utawekwa katika kujenga uwezo wa vyuo ili viweze kutoa wataalamu watakaoweza kujiariri wenyewe badala ya kutegemea kuajiriwa.

 

v    Kuendelea kuongeza idadi ya wanafunzi katika vyuo vikuu na vya ufundi kwa kutumia njia mbalimbali.

 

v    Kuendelea kuweka uwiano mzuri kati ya idadi ya wanafunzi wa Kike na Kiume katika vyuo vya elimu ya juu na Ufundi.

 

v    Kuratibu na kuhakiki uanzishwaji wa vyuo bora vya elimu ya juu na ufundi, kuvikagua , kuvisajili na kuvipa ithibati.

 

v    Kuendelea kuhamasisha matumizi ya Sayansi na Teknolojia.

 

v    Kuendelea kuhamasisha wananchi kuhusu dhana ya uchangiaji, uendelezaji na uwekezaji katika Elimu ya Juu na Ufundi, kama vile uanzishaji mifuko ya hiari ya Skolashipu, ujenzi wa miundombinu ya Elimu ya Juu, Ufundi, Sayansi na Utafiti.

 

v    Kuboresha mazingira ya kazi ikiwa ni pamoja na uendelezaji wanataaluma, kuimarisha miundo mbinu ya vyuo.

v    Kushiriki katika shughuli za Tume ya Taifa ya UNESCO.

 

v    Kuendelea kuhamasisha wanafunzi na wafanyakazi madhara ya ugonjwa hatari wa UKIMWI.

v    Kuendeleza juhudi za kupambana na rushwa katika Wizara na Taasisi zake.

 

v    Kufuatilia utekelezaji wa miradi ya nishati mbadala

 

v    Kuendelea na upanuzi wa mtandao wa mawasiliano kwa njia ya Kompyuta ili kuboresha mawasiliano kati ya taasisi na mtandao wa watafiti wa nchi za nje.

 

v    Kuimarisha shughuli za utafiti ili ziweze kutatua kero za wananchi Mkazo zaidi utakuwa kuimarisha mbinu za usambazaji wa matokeo ya utafiti kwa sekta za viwanda na wananchi kwa ujumla.

 

v    Kuandaa Takwimu sahihi za nguvu kazi kwa lengo la kuainisha maeneo yanayopaswa kupewa kipaumbele katika mafunzo

 

v    Kusimamia utekelezaji wa mradi wa uhuishaji wa vyuo vya elimu ya juu nchini.

v    Kuimarisha utekelezaji wa Sheria ya  Mfuko wa Elimu.

 

v    Kuanza maandalizi ya kuanzisha Vituo vya Sayansi               (Science Parks) Mikoani.

 

v    Kuanzisha Sheria Mama ya Elimu ya Juu na Sheria Mpya ya kukigeuza Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi na Tiba Muhimbili kuwa Chuo Kikuu kamili.

 

v    Kuanzisha Sheria ya kuunda Mamlaka ya nguvu za Atomiki.

 

MWISHO

 

38.          Mheshimiwa Spika, mwisho ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa wahisani na washikadau mbalimbali kwa mchango wao mkubwa katika Wizara yangu.  Ni wazi kuwa msaada walioutoa na wanaoendelea kutoa hususan katika kuboresha Sayansi na Teknolojia, elimu ya juu na ya ufundi katika vyuo na taasisi umesaidia kwa kiasi kikubwa kuchangia pale ambapo Serikali imekuwa ikishindwa kutokana na ufinyu wa bajeti.  Nchi hizo ni pamoja na Sweden, Norway, Uholanzi, Japan, Ubeligiji, Korea, China, Benki ya Dunia na Umoja wa Mataifa. Aidha,Mashirika mengine ni pamoja na, Common Wealth Science Council, International Atomic Energy Agency, Third World Academy of Sciences, International Foundation for Sciences na Shirika la Kimaendeleo la Sweden. Naomba waendelee na moyo huo nasi tunaahidi kuendeleza ushirikiano huu kikamilifu.

 

39.                      Mheshimiwa Spika, ili kuiwezesha Wizara yangu kutekeleza      mipango iliyojiwekea katika mwaka wa fedha 2002/2003 sasa      naliomba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla ya      Sh.70,226,556,600.00 Kati ya fedha hizo, Sh 59,090,803,800.00. ni      kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh 11,135,752,800.00 ni kwa      matumizi ya maendeleo.

 

40.          Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.


KIAMBATISHO NA. 1:   FEDHA ZINAZOOMBWA KWA MATUMIZI YA KAWAIDA FUNGU 68 MWAKA 2002/2003

 

 

 

KIFUNGU

IDARA

FEDHA ZILIZOIDHINISHWA MWAKA 2001/2002

FEDHA ZINAOOMBWA MWAKA 2002/2003

1001

UTAWALA

881,677,900

939,971,300

1002

UHASIBU

67,162,000

71,856,900

1003

SERA NA MIPANGO

108,593,100

311,390,200

2001

TUME YA UNESCO

243,206,700

251,718,800

3001

ELIMU YA JUU

45,201,171,000

51,012,100,100

3002

ELIMU YA UFUNDI

4,877,417,700

5,027,600,600

3003

SAYANSI NA TEKNOLOJIA

1,338,657,000

1,476,165,900

JUMLA

52,717,885,400

59,090,803,800


KIAMBATISHO NA. 2

 

 

FEDHA ZINAZOOMBWA KWA MATUMIZI YA MAENDELEO FUNGU 68 MWAKA 2002/2003

 

KIFUNGU

IDARA

FEDHA ZILIZOIDHINISHWA MWAKA 2001/2002

FEDHA ZINAZOOMBWA 2002/2003

FEDHA ZA TANZANIA

FEDHA ZA NJE

FEDHA ZA TANZANIA

FEDHA ZA NJE

1003

SERA NA MIPANGO

100,000,000

1,215,000,000

122,436,300

1,200,000,000

3001

ELIMU YA JUU

1,230,000,000

1,164,000,000

1,750,000,000

7,743,316,500

3002

ELIMU YA UFUNDI

350,000,000

-

200,000,000

-

3003

SAYANSI NA TEKNOLOJIA

140,000,000

-

120,000,000

-

JUMLA

1,820,000,000

2,379,000,000

2,192,436,300

8,943,316,500

 


KIAMBATISHO NA. 3

MAOMBI YA FEDHA    FUNGU: 68

 

KIFUNGU

IDARA

FEDHA ZILIZOIDHINISHWA 2001/2002

FEDHA ZINAZOOMBWA 2002/2003

FEDHA ZA KAWAIDA

FEDHA ZA MAENDELEO

JUMLA KUU

FEDHA ZA KAWAIDA

FEDHA ZA MAENDELEO

JUMLA KUU

FEDHA ZA TZ

FEDHA ZA NJE

FEDHA ZA TZ

FEDHA ZA NJE

1001

Utawala

881,677,900

--

--

881,677,900

939,971,300

--

--

939,971,300

1002

Uhasibu

67,162,000

--

--

67,162,000

71,856,900

--

--

71,856,900

1003

Sera na Mipango

108,593,100

100,000,000

1,215,000,000

1,423,593,100

311,390,200

122,436,300

1,200,000,000

1,633,826,500

2001

Tume ya UNESCO

243,206,700

--

--

243,206,700

251,718,800

--

--

251,718,800

3001

Elimu ya Juu

45,201,171,000

1,230,000,000

1,164,000,000

47,595,171,000

51,012,100,100

1,750,000,000

7,743,316,500

60,505,416,600

3002

Elimu ya Ufundi

4,877,417,700

350,000,000

--

5,227,417,700

5,027,600,600

200,000,000

--

5,227,600,600

3003

Sayansi & Teknolojia

1,338,657,000

140,000,000

--

1,478,657,000

1,476,165,900

120,000,000

--

1,596,165,900

 

 

JUMLA YA MAOMBI FUNGU 68

 

 

 

52,717,885,400

1,820,000,000

2,379,000,000

 

 

56,916,885,400

 

 

59,090,803,800

2,192,436,300

8,943,316,500

 

 

70,226,556,600

 

4,199,000,000

 

11,135,752,800