Hotuba
ya Waziri wa Elimu na Utamaduni
Mhe. Joseph J. Mungai (MB) Kuhusu Makadirio
ya Matumizi ya
Fedha kwa Mwaka 2004/05
I.
UTANGULIZI
1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja
kwamba Bunge lako tukufu baada ya kuzingatia taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii lijadili na
kupitisha makadirio ya matumizi ya kawaida na ya maendeleo ya Wizara ya Elimu
na Utamaduni kwa mwaka wa fedha 2004/05.
2 Mheshimiwa Spika,
awali ya yote napenda niungane na Waheshimiwa Wabunge
wenzangu kuwapongeza Mhe. Getrude Mongella, Mbunge wa
Ukerewe, kuwa Rais wa Bunge la Afrika, Mhe. Dkt. William Shija, Mbunge wa Sengerema, Mhe. Dkt. Amani W.A. Kabourou, Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Dkt. Remigius Edington Kissassi,
Mbunge wa Dimani Zanzibar na Mhe. Athumani Janguo,
Mbunge wa Kisarawe kwa kuchaguliwa kuwa Wabunge wa
Bunge la Umoja wa Afrika. Aidha, nawapongeza Mhe. Sophia Simba, Mbunge wa Viti Maalum na pia Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Kudumu ya Maendeleo ya Jamii kwa kuteuliwa kuiwakilisha
Mheshimiwa Spika,
naomba kutumia nafasi hii ya mwanzo kuwapongeza na kuwashukuru; (a) Mheshimiwa
Dkt. Abdallah Kigoda (MB), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na
Ubinafsishaji kwa hotuba yake ambayo imetoa tathmini, mwenendo na mwelekeo wa
uchumi wa Taifa kwa jumla; na (b) Mheshimiwa Basil Pesambili Mramba (MB),
Waziri wa Fedha, kwa hotuba yake iliyofafanua kwa ufasaha Bajeti ya Serikali ya
mwaka 2004/05 ambayo imetoa kipaumbele kwa sekta muhimu katika kukuza uchumi
ikiwemo Sekta ya Elimu ambayo inao
wajibu mkubwa katika Mkakati wa Kupunguza Umaskini (MKU) na kuboresha ufanisi
wa nguvu kazi ya taifa kwa njia ya elimu.
Aidha, namshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu katika Hotuba yake ya bajeti kwa kufafanua mambo muhimu ya elimu yaliyoamuliwa na
Serikali, na kwa uamuzi na maagizo yake kuhusu madai ya walimu.
3. Mheshimiwa Spika, natoa shukrani zangu kwa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Huduma za Jamii, inayoongozwa na mwenyekiti wake Mheshimiwa Omar S.
Kwaangw’ Mbunge wa Babati Mashariki kwa kutoa ushauri na maelekezo ya
kuboresha Bajeti na utekelezaji wa Wizara ya Elimu na Utamaduni baada ya
uchambuzi wa kina.
4.
Mheshimiwa
Spika, Wizara ya Elimu na
Utamaduni imeendelea kuwa na majukumu yake
(a) Elimu ya Msingi na Elimu ya Awali
(b) Elimu ya Sekondari ya Kawaida (Ordinary Level): Kidato cha 1 hadi 4; na
Elimu ya Sekondari ya Juu (Advanced Level):
Kidato cha 5 hadi 6
(c) Elimu Maalumu (Special Education) itolewayo kwa wenye
ulemavu
(d) Elimu ya Watu Wazima (Adult Education) ikiwa ni pamoja na utoaji wa Elimu ya Msingi na Sekondari kwa mfumo
usio rasmi kwa watoto na watu wazima walioikosa.
(e) Utamaduni wa
Taifa ikiwemo Lugha, Sanaa, Mila na Desturi na Ukaguzi wa Filamu.
(f)
Mafunzo
ya Ualimu Daraja A na Stashahada (Diploma).
(g) Ukaguzi wa Shule
katika ngazi zote (Elimu ya Awali hadi Kidato cha 6) na Vyuo vya Ualimu.
(h) Kupanga na
kuratibu mipango yote ya elimu kuanzia Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu.
(i)
Taasisi
na Mabaraza yaliyo chini ya Wizara ambayo ni:
(i)
Taasisi
ya Elimu Tanzania (TET);
(ii)
Taasisi
ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW);
(iii)
Baraza la Mitihani Tanzania (BAMITA);
(iv)
Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA);
(v)
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA);
(vi)
Bodi
ya Huduma za Maktaba Tanzania (BOHUMATA) na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa
Elimu (ADEM).
Katika kutekeleza majukumu hayo
Wizara inaongozwa na (a) Sheria ya Elimu Na. 25 ya 1978; (b) Sera ya Elimu na Mafunzo; (c)
Sera ya Utamaduni; (d) Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2025; (e) Mkakati wa
Kupunguza Umaskini (MKU); na (f) Ilani ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2000 ya Chama
Tawala cha CCM.
II.
UTEKELEZAJI WA MIPANGO
YA MWAKA 2003/04
NA
MALENGO YA MWAKA 2004/05
5.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mipango ya Wizara
yangu kwa Mwaka 2003/04 na malengo ya mwaka 2004/05 kwa kila Idara, Taasisi na
ngazi ya elimu ni
Malengo
Maalumu ya Elimu ya Msingi
6. Mheshimiwa
Spika, Idara ya Elimu ya Msingi inayo Malengo Maalum yafuatayo:
(a)
Kurejesha Elimu ya Msingi kwa Wote (Universal Primary Education - UPE) yaani kwa kuwaingiza Darasa
la
(b)
Kuongeza asilimia ya rika la Elimu ya
Msingi (miaka 7-13) waliomo shuleni kutoka 57% mwaka 2001 hadi 95% mwaka 2005.
(c)
Kupunguza kasi ya kuacha shule (Drop Out Rate) kutoka 6.6% kwa mwaka hadi 3.0 % kwa
mwaka ifikapo 2005 katika kila shule.
(d)
Kuboresha Elimu ya Msingi kutoka waliofaulu 22 % mwaka 2000
hadi zaidi ya 50% mwaka 2005.
(e)
Kuongeza wahitimu wa Darasa la VII
wanaoingia Sekondari kutoka
19.5% mwaka 2000 hadi 50% mwaka 2010.
6. Mheshimiwa
Spika, mwaka 2003/04 shughuli za Elimu
ya Msingi zimeongezeka ifuatavyo:
6.1 Shule za Awali zimeongezaka 2,753 kutoka
6,948 hadi 9,701 ambalo ni ongezeko la 39.6%.
6.2 Shule
za Msingi zimeongezeka 884 kutoka 12,649 mwaka 2003 hadi 13,533 mwaka 2004 sawa na
ongezeko la 7%; na Wanafunzi wameongezeka
kwa 8% kutoka 6,562,772 mwaka 2003 hadi
7,083,063 mwaka 2004 ambayo vilevile ni 61.6% ukilinganisha na wanafunzi
4,382,410 mwaka 2000 Bunge hili lilipochaguliwa.
6.3 Walimu 14,261 wameajiriwa.
6.4 Wanafunzi
196,273 sawa na 40.1% waliofaulu Mtihani wa Darasa la VII mwaka 2003 wameongezeka
kwa 62,599 sawa na 46.8% kutoka 133,674 mwaka 2002.
Kielelezo Na. 6: Matokeo ya
Mtihani ya DVII 1998 – 2003

TANBIHI: Alama ya kufaulu mwaka 2003 ilikuwa 85/200, badala ya 65/150
baada ya kuongezwa somo la nne.
Nawapongeza
sana Maafisa Elimu,Walimu Wakuu na Walimu wote wa
Shule za Msingi kwa mafanikio hayo.
7. Mheshimiwa Spika, mafanikio
ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya
Msingi (MMEM) 2002-2006 ni
7.1 Mwaka 2004 watoto 1,368,315
waliandikishwa Darasa la I sawa na 83.4% ya
kulinganisha na lengo la 1,640,969 wakiwemo wavulana 697,594 na wasichana
670,721. Kati
7.2 Jumla ya wanafunzi
katika shule za msingi mwaka 2004 ni 7,083,063. ikilinganishwa na 6,562,772 mwaka 2003 ambalo ni ongezeko la
wanafunzi 520,291 sawa na 8.0%.
Kielelezo 7.1: Wanafunzi
wa DI na DI-VII Kulinganisha na
Idadi ya Watoto wa Miaka 7-13 [2000-2004]

7.3
Kwa mujibu wa
takwimu zilizooneshwa katika Kielelezo 7.1
(a)
Wanafunzi wa rika
la elimu ya msingi (miaka 7-13) walioko shuleni (Net Enrolment Ratio – NER) imeongezeka kutoka 58.8% mwaka 2000 hadi
90.5% mwaka 2004. Kwa hiyo malengo
yaliyokuwa yamepangwa ya kufikia NER ya 77% na GER ya
85% yaliyomo katika Mkakati wa Kupunguza
Umaskini (MKU) kwa mwaka 2003 yamevukwa.
(b)
Wanafunzi wote
shuleni kama asilimia ya idadi ya watoto wa rika lengwa (Gross Enrolment Ratio – GER) imeongezeka kutoka 77.6% mwaka 2000 hadi
106.3% mwaka 2004.
(c)
Mikoa ya Lindi,
Morogoro, Kigoma,
Kielelezo 7.2: Mikoa kwa
(GER) Katika Shule za Msingi
ya Watoto wa Rika la Elimu ya Msingi: Miaka 7-13 [2004]
|
Mkoa |
Idadi ya Watoto Miaka 7- 13 |
Wanafunzi Darasa 1-V11 |
GER |
NER |
|
1.
Mara |
289,901 |
366,307 |
126.2 |
100.0 |
|
2.
Ruvuma |
216,082 |
257,950 |
119.4 |
99.3 |
|
3.
Mbeya |
411,670 |
488,131 |
118.6 |
99.3 |
|
4.
Kilimanjaro |
298,704 |
345,885 |
115.8 |
100.0 |
|
5.
Mwanza |
596,045 |
689,735 |
115.7 |
99.5 |
|
6.
Tanga |
341,054 |
387,514 |
113.6 |
97.9 |
|
7.
Iringa |
318,046 |
359,418 |
113.0 |
99.1 |
|
8.
Pwani |
165,323 |
184,687 |
111.7 |
94.5 |
|
9.
Mtwara |
190,773 |
209,622 |
109.9 |
94.2 |
|
10.
|
386,121 |
419,590 |
108.7 |
93.1 |
|
11. Manyara |
209,724 |
224,673 |
107.1 |
89.5 |
|
12. Singida |
228,952 |
242,586 |
106.0 |
85.0 |
|
13.
Kagera |
417,192 |
431,729 |
103.5 |
86.8 |
|
14.
Arusha |
256,240 |
264,930 |
103.4 |
91.9 |
|
15.
Rukwa |
234,903 |
242,313 |
103.2 |
87.9 |
|
16. Shinyanga |
588,946 |
594,253 |
100.9 |
86.3 |
|
17. Lindi |
140,446 |
139,401 |
99.3 |
84.1 |
|
18.
Morogoro |
336,658 |
329,528 |
97.9 |
81.9 |
|
19.
Kigoma |
355,092 |
328,440 |
92.5 |
77.2 |
|
20.
|
335,920 |
301,770 |
89.8 |
76.3 |
|
21. Tabora |
347,549 |
274,601 |
79.0 |
68.2 |
|
Jumla |
6,665,341 |
7,083,063 |
106.3 |
90.5 |
7.4 Walimu
14,261 wameajiriwa hadi 30 Juni, 2004 sawa na asilimia 91.8% ya lengo la walimu
15,533 waliotarajiwa kuwa wameripoti na kuanza kazi.
7.5 Walimu
Tarajali wanaochukua mafunzo ya Ualimu Daraja A ni 10,788, ikilinganishwa na lengo
la mwaka 2004 la wanachuo 10,000.
7.6 Ruzuku
ya Maendeleo ya shilingi 1,185,000,000 imetolewa na Serikali Kuu kwa
Halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na ununuzi
wa madawati. Albaki ya Shilingi
65,742,120,600 ya Ruzuku ya Maendeleo itatolewa wakati wowote kutokana na mchango
wa Wahisani ili kukamilisha malengo ya mwaka 2003/04.
7.7 Ruzuku
ya Uendeshaji ya shilingi 56,172,632,210 ilitolewa kwa Halmashauri kwa ajili ya
ununuzi wa vitabu vya kiada na ziada, penseli, kalamu, chaki na madaftari, vivunge
vya sayansi (Science kits), matengenezo na mitihani ya ndani ya shule na
shughuli za utawala ngazi ya shule. Kiwango hiki ni sawa na shilingi 7,930.55
kwa kila mwanafunzi. Albaki ya shilingi 14,762,862,790 sawa na shilingi 2,069.45
kwa mwanafunzi zitatumwa kwa Halmashauri wakati wowote baada ya kuzipokea kutoka
kwa wahisani.
Utekelezaji wa Miradi
ya Elimu ya Msingi
8. Mheshimiwa Spika, katika
mwaka 2003/04 utekelezaji wa miradi mingine ya Elimu
ya Msingi uliendelea
8.1 Mradi wa Lishe Shuleni
Mradi huu unaendeshwa kwa ushirikiano na
Shirika la Mpango wa Chakula Duniani yaani “World Food Programme (WFP)” na
utaendelea hadi mwaka 2006 katika mikoa ya Arusha,
Wilaya za Mradi wa Lishe Shuleni (1) Monduli; (2)
Ngorongoro; (3) Simanjiro; (4) Kiteto; (5) Dodoma [V]; (6) Kondoa; (7) Mpwapwa; (8) Singida [V];
(9) Iramba; (10) Manyoni, (11) Karatu. Jumla ya shule 230 zinanufaika na
mpango huu zikiwemo 10 za bweni na 220 za kutwa. Aidha, jumla ya wanafunzi
99,511 wananufaika na mpango huu. Kati ya hao wavulana ni 52,697 na wasichana ni 46,814. |
8.2 Mradi wa Shule
Zenye Mazingira Yanayomjali Mtoto “
|
Shule Zenye Mazingira Yanayomjali Mtoto (1)
Kisarawe; (2) Masasi;(3) Songea [V]; (4) Musoma [V]; (5) Ngara; (6) Magu; (7)
Mufindi; (8) Hai; (9) Ilala; (10) Kinondoni na (11) Temeke. Utafiti wa awali
[Baseline Survey] na majadiliano na Jamii [Community Dialogue] ulifanyika na
kukamilika katika Wilaya 5 (1) Kisarawe; (2) Masasi; (3) Songea [V]; (4) Musoma [V]; na (5) Ngara. Aidha,
uchapishaji wa zana ya upimaji wa utekelezaji wa shule zinazomjali mtoto umekamilika, semina
kwa walimu 60 toka wilaya za Kisarawe
na Masasi zimefanyika. |
8.3
Mradi wa Uboreshaji wa Elimu Ngazi ya Kata (UBEKA) au WABEM [Ward Based Education Management]
unatekelezwa katika wilaya sita.
|
Wilaya za Mradi wa uboreshaji Elimu Ngazi ya Kata (1) Kisarawe; (2) Masasi; (3)
Hai; (4) Musoma [V]; (5) Mufindi; na (6) Songea [V]. Semina za awali katika ngazi ya Kata
zilikwishafanyika. Katika gharama za
awali mradi ulikadiriwa kutumia Dola za Kimarekani 1,189,553 ambazo
zimetolewa kwa uhisani wa UNICEF. Kwa
makubaliano ya UNICEF na Wizara shughuli hizi zitakwenda kwa pamoja na Mradi
wa Shule zenye mazingira yanayomjali mtoto.
|
8.4 Mradi
wa Utafiti wa Hali Halisi na Mipango ya Elimu ya Shule [School Mapping and Micro-Planning]. Vilevile, hadi kufikia Juni 2004 Halmashauri 76 ambayo ni asilimia 64 ya Halmashauri zote nchini zimeshafanyiwa
‘School Mapping na Microplaning’. Aidha, Halmashauri
16 zimeshaanza kufanyiwa “School Mapping na Microplanning” kuanzia Juni 2004.
|
Kuanzia Juni 2004 (1) Monduli; .(2)
Hanang; (3) Kondoa, (V); (4) Dodoma (V); (5) Mpwapwa; (6) Ludewa; (7) Same;
(8) Kiteto; (9) Ngorogoro; (10) Mbozi; (11) Kwimba; (12) Sengerema; (13)
Iramba; (14) Singida(V); (15) Igunga na (16) Urambo. |
8.5 Mheshimiwa Spika,
Mwaka 2003/04 Kutokana na uhisani wa Serikali ya
Japan yamejengwa Madarasa 107, Ofisi za Walimu 9, na Matangi ya Maji 24 na
maliwato matundu 107 pamoja na samani yakiwemo madawati, mbao za kuandikia na
za matangazo katika shule 15 za Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni. Aidha, ujenzi wa
madarasa 250 kwa uhisani wa
|
Shule Zilizojengewa Vyumba vya Madarasa Mkoa wa (1) Boma; (2)
Mchikichini; (3) Gongo la Mboto (B); (4)Msongola; (5) Mvuti; (6) Kimara (B); (7) Uzuri; (8) Mbezi; (9) Mabibo; (10) Mwananyamala B; (11) Azimio; (12) Sokoine; (13) Madenge; (14) Rangi Tatu; na (15) Temeke. |
8.6
Mradi wa Kuzuia Ajira Mbaya ya Watoto
kupitia MEMKWA. Mradi huu unaendeshwa kwa
ushirikiano na Shirika la Kazi la Dunia, Halmashauri husika na Wizara yangu. Madhumuni ya Mradi huu ni
kupunguza ajira mbaya ya watoto kwa kuwapatia Elimu kwa utaratibu wa MEMKWA. Mradi huu unatekelezwa katika Wilaya 11.
(1) Ilala, (2)
Kinondoni, (3) Temeke, (B); (4) Mufindi; (5) Iringa (V); (6) Simanjiro, (B);
(7) Arumeru; (8) Arusha; (9) Kondoa; (10) Iramba; na (11) Urambo.
(ii) Malengo ya Elimu ya Msingi 2004/05
9. Mheshimiwa Spika, 2004/05 ni Mwaka wa Nne wa utekelezaji wa MMEM ambao una malengo yafuatayo
ya kutoa Elimu bora ya Msingi kwa wote:
9.1
Kujenga jumla ya madarasa 7,794 na nyumba za Walimu 6,000
yakiwemo madarasa ya MMEM 6,794 na nyumba za walimu 2,186;
9.2
Kuajiri walimu 7,286 na Walimu tarajali 10,000;
9.3
Kuandikisha Darasa la I watoto wote 1,041,880 wa
miaka 7
9.4
Kutoa Ruzuku za Maendeleo na Uendeshaji; na
9.5
Kutekeleza MEMKWA kwa
ukamilifu zaidi katika Wilaya zote.
10. Mheshimiwa Spika, katika
Bajeti ya mwaka 2004/05 ili kutekeleza malengo hayo
zimetengwa Shilingi 271,222,783,504. Kati
ya hizo shilingi 230,394,438,504 zimeombwa kupitia katika Mafungu
yanayosimamiwa na mwenzangu mwenye dhamana ya
TAMISEMI. Aidha, shilingi 40,829,345,000
zinaombwa kwa ajili ya kazi za MMEM zinazosimamiwa na
Wizara yangu.
Malengo Maalumu ya Elimu ya Sekondari
(a) Kuongeza nafasi ya utoaji Elimu ya
Sekondari kwa rika la Elimu ya Sekondari (miaka 14 -
17) kutoka 7% ya mwaka 2003 hadi kufikia 50% ifikapo 2010.
(b) Kupanua Elimu ya Sekondari katika kutekeleza Mpango wa Elimu ya Sekondari (MMES) kwa
kuongeza nafasi ya kidato cha 1 kutoka 21% mwaka 2003 hadi 45% ifikapo mwaka
2009.
(c) Kuboresha Elimu ya Sekondari kwa kuongeza asilimia ya wanaofaulu
mitihani ya kitaifa ya Kidato cha 4 katika madaraja I, II na III kutoka 39.1%
mwaka 2003 hadi zaidi ya 50% ifikapo mwaka 2005.
(d) Kutoa Elimu ya Sekondari kwa usawa kwa jinsi zote, Wilaya zote kwa kuzingatia maelekezo
ya kifungu 11 (3) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
“Serikali itafanya jitihada kuhakikisha kwamba watu wote
wanapata fursa sawa za kutosha kuwawezesha kupata elimu na
mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za shule na vyuo vingine vya mafunzo”.
(i) Mafanikio ya
Mwaka 2003/04
11. Mheshimiwa Spika, mwaka 2003/04 Idara ya Elimu
ya Sekondari imekuwa na mafanikio yafuatayo:
(a)
Ongezeko la shule 208 za
sekondari na la wanafunzi 47,746 wa Kidato cha Kwanza na 82,111 wa Kidato cha 1
hadi 4.
(b)
Shule za Sekondari za Serikali
zimeongezeka kutoka 649 mwaka 2003 hadi 828 mwaka 2004. Hili ni ongezeko la shule 179 (27.6%). Aidha, shule za Sekondari zisizo za Serikali
zimeongezeka kutoka 434 mwaka 2003 hadi 463 mwaka 2004. Hili ni ongezeko la shule 29 (6.7%).
Kielelezo Na. 11.1: Ongezeko la Sekondari na Wanafunzi 2004
|
Aina
ya Sekondari |
Mwaka |
Ongezeko |
|
|
2003 |
2004 |
||
|
Sekondari za
Serikali |
649 |
828 |
179 (27.6%) |
|
Sekondari Zisizo za
Serikali |
434 |
463 |
29 (6.7%) |
|
Jumla Sekondari
zote |
1083 |
1,291 |
208 (19.2%) |
|
Wanafunzi wa Kidato cha 1 |
99,744 |
147,490 |
47,746 (47.9%) |
|
Wanafunzi wa K.1 - 4 |
319,487 |
401,598 |
82,111 (25.7%) |
(c)
Jumla Shule za Sekondari zimeongezeka
kutoka 1,083 mwaka 2003 hadi 1,291 mwaka 2004. Hili ni ongezeko la shule 208 sawa na 19.2%.
(d)
Wanafunzi wa Kidato cha 1 wameongezeka
kutoka 99,744 mwaka 2003 hadi 147,490 mwaka 2004. Hili ni ongezeko la wanafunzi 47,746 au 47.9%.
Kielelezo Na.11.2: Idadi ya Wanafunzi K1 kwa Jinsi, 2000-2004
(e)
Wanafunzi wote wa Kidato cha 1 hadi cha 4
wameongezeka kutoka 319,487 mwaka 2003 hadi 401,598 mwaka 2004 ikiwa ni
ongezeko la 25.7%. Ongezeko hili ni
kubwa kuliko mwaka wowote uliopita.
Kielelezo Na.11.3: Wanafunzi Shule za Sekondari K.1-K.4, [2000-2004]
11.2 Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia
na kufundishia kwa:
(a) Kukarabati
kwa uhisani wa Serikali ya Japan shule za Serikali 14 ambazo ni: (1) Utete; (2) Korogwe; (3) Nyang’wale; (4) Itengule; (5) Iringa Wasichana; (6) Kibiti; (7) Zunzuli; (8) Tabora Wavulana; (9) Bwabuki; (10) Maneromango; (11) Makambako; (12) Kilwa; (13) Manyara na (14) Itandula.
(b) Kuzipa
magari Shule 5 katika mikoa 5 ambayo ilikuwa haijapewa magari mapya kwa ajili
ya huduma za shule hizo na pia kuhudumia shule nyingine zilizomo katika mikoa
hiyo. Shule zilizopewa magari ni:
Loleza, Kantalamba, Mwenge, Wotta na
Musoma Kutwa.
(c) Kununua Kompyuta 80 kwa ajili ya Shule za Sekondari.
11.3
Idadi ya Shule za Sekondari za
Serikali zinazotoa elimu ya Kidato cha 5 na Kidato cha 6 imeongezeka kutoka 81 mwaka 2003 hadi 84 mwaka 2004. Shule zilizoongezwa ni Kahororo, Mara na
Longido. Shule zisizo za Serikali
zinazotoa elimu ya Kidato cha 5 na Kidato cha 6 ni 127. Kwa hiyo jumla ya sekondari zenye Kidato cha 5
na ni 211.
11.4
Mikondo mipya ya Kidato cha
5 imeongezwa katika Shule za Sekondari za Kilakala, Tabora Wavulana, Msalato,
Tanga Ufundi, Musoma Ufundi, Minaki, Lindi, Songea Wasichana, Mawenzi, Ifunda,
Bwiru Wasichana na Mwakaleli.
11.5
Wanafunzi waliochaguliwa
kuingia Kidato cha 5 waliongezeka kutoka 10,158 mwaka 2003 hadi 12,253 mwaka 2004.
Hili ni ongezeko la wanafunzi 2,075 sawa
na 9.5%. Wanafunzi wengine 1,130
watachaguliwa kujaza nafasi katika shule za Serikali zitakazopanuliwa mwezi
Julai/Agosti, 2004, na kufanya jumla kuwa wanafunzi 13,383 wa Kidato cha 5.
Kielelezo Na.11.4: Jumla ya Wanafunzi
na % Wasichana K5

11.6
Jumla ya Wanafunzi wa Kidato
cha 5 na 6 imeongezeka kutoka 25,954 mwaka 2003 hadi 31,001 mwaka 2004.
Kielelezo Na.11.5: Jumla Wanafunzi Shule za Sekondari K5-K62000-2004
11.7.
Jumla ya wanafunzi wa Sekondari
Kidato cha 1 hadi 6 imeongezeka kutoka 261,896 mwaka 2000 hadi kufikia 432,599 mwaka
2004.
Kielelezo Na.11.6:
Wanafunzi Shule za Sekondari K1-K6, 2000-2004
11.8. Katika
kutoa Elimu ya Sekondari kwa usawa, Serikali imeendelea:
(a)
Kuhakikisha kuwa idadi sawa
ya wasichana na wavulana wanachaguliwa kuingia Kidato cha 1 kila mwaka.
(b)
Kulipia gharama za elimu kwa
wanafunzi kutoka familia zisizo na uwezo kiuchumi. Jumla ya wanafunzi 12,000 wanagharimiwa mpaka
sasa.
(c)
Kulipia Elimu ya Sekondari
kwa Wasichana 2,361 wa Kidato cha 3 hadi 6 ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwalipia.
(d)
Kuhamasisha ufunguzi wa
shule za sekondari za kutwa hususan kwenye maeneo ambayo hayakuwa na shule za
kutosha. Shule mpya 179 zimefunguliwa. Napenda kuipongeza Mikoa, Wilaya/Halmashauri zilizofungua
shule nyingi mpya mwaka huu.
Wilaya/ Halmashauri hizo ni: (1) Moshi Vijijini 9, (2) Rungwe 8, (3) Mbozi 7, (4) Geita 7, (5) Magu 5, (6) Masasi 5, na (7) Mbinga 5.
Mikoa iliyofungua shule nyingi zaidi ni : (1) Mbeya 27; (2) Kilimanjaro 18; (3) Mtwara 16; (4) Iringa 15; (5) Mwanza 14; (6) Kigoma 9; (7) Ruvuma 8; (8) Pwani 6 na (9) Rukwa 5.
Nawapongeza hao wote kwa juhudi zao.
11.9 Mheshimiwa Spika, katika kuboresha Elimu ya
Sekondari yafuatayo yalifanyika:
(a)
Shule za sekondari za Serikali
51 zilipewa jumla ya Shilingi 330,432,530 kwa ajili ya ukarabati wa
majengo. Utekelezaji ulivuka lengo kwa
70%.
(b)
Shule za Sekondari za Serikali
644 zilipewa kiasi cha shilingi 490,152,400 kwa ajili ya ununuzi wa vitabu vya
Sayansi na Hisabati.
(c)
Walimu 461 walipatiwa
mafunzo kazini: 327 mafunzo ya mbinu bora za ufundishaji wa masomo ya Sayansi
na Hisabati; 87 Programu maalumu ya Shahada ya Hisabati katika Chuo Kikuu cha
Tumaini; 39 mafunzo ya Stashahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam; 5 mafunzo ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; na
3 mafunzo ya kompyuta katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha;
(d)
Walimu 102 wa Shahada na
1,000 wa Stashahada waliajiriwa. Aidha,
walimu 615 wasiokuwa na ualimu kwa kusomea wameajiriwa kufundisha kwa liseni
baada ya mafunzo mafupi ya pedagogia.
(e)
Ujenzi wa maabara za masomo
ya Sayansi uliendelea katika shule 11 za:
Mbekenyera, Makiba, Mwaya, Mitole, Matekwe, Zingibari, Kongwa, Mangaka,
Meatu, Mahiwa na Runzewe. Ukamilikaji wa
ujenzi uko kati ya 60% na 88% katika shule mbalimbali.
(f)
Ufaulu katika mitihani ya Kidato
cha 4 Daraja la I hadi III umeongezeka kutoka 36.2% mwaka 2002 hadi 39.1% mwaka
2003.
11.10 Katika kuimarisha na kuboresha
uongozi na usimamizi wa kutoa Elimu, Wizara ilipata mafanikio katika:
(a)
Kuwapatia mafunzo ya Uongozi
ya mwezi mmoja Wakuu wa Shule 132 na Makamu Wakuu wa shule 126 wa shule za
Serikali.
(b)
Jumla ya Wakuu wa shule 360
walishiriki katika mkutano mkuu wa Elimu uliofanyika Arusha tarehe 8-12/12/2003
na kuweka mikakati ya kuboresha huduma za Elimu katika ngazi mbalimbali.
12. Mheshimiwa Spika, miradi mbalimbali
ilitekelezwa na Wizara yangu kwa lengo la kuboresha Elimu
ya Sekondari.
12.1 Mradi wa Uboreshaji wa Elimu ya Sayansi (Science Education for Secondary
Schools (SESS): Mradi huu una
sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inalenga kuboresha
ufundishaji wa masomo ya Sayansi na Hisabati (Science Education for Secondary Schools
- SESS) na sehemu ya pili ni Elimu
dhidi ya UKIMWI, “Prevention and
Awareness in Schools of HIV and AIDS” (PASHA) ambao ulianza rasmi Julai,
2003. Mradi wa
SESS ulitoa mafunzo ya mbinu bora za kufundisha masomo ya Sayansi na Hisabati
kwa walimu. Kazi mahsusi zilizofanywa na mradi huo katika kipindi hiki ni:
(a) Kutoa mafunzo kwa
wawezeshaji (trainers) 60 kutoka
mikoa ya Tabora, Kigoma na Shinyanga.
(b) Kuwalipatia mafunzo mahali pa kazi (cluster workshop) walimu 243 katika mikoa ya Iringa,
(c) Kuwalipatia mafunzo ya kufundisha
mada za HIV/AIDS walimu 24 kutoka mikoa ya
(d) Kuwalishirikisha katika kambi ya
Sayansi wanafunzi wasichana 187 kutoka Mikoa ya Tanga, Pwani na
Morogoro.
12.2 Mradi wa Pili wa Elimu (Education II Project)
(a) Uliendelea na
ujenzi wa maabara za masomo ya Sayansi katika Shule za Sekondari 36 za Serikali zilizojengwa na wananchi. Hadi kufikia Machi 2004 maendeleo ya ujenzi wa
maabara katika shule 36 za awamu zote tatu ulikuwa
|
Awamu |
% Wastani wa
Matarajio |
% Kiwango
Kilichojengwa |
|
1 |
100 |
88.05 |
|
2 |
100 |
63.37 |
|
3 |
87.39 |
42.96 |
(b) Kwa wastani ujenzi wa
maabara zote umekamilika kwa 71.6%.
(c) Shule 18 zimepatiwa samani za
maabara. Aidha, samani kwa ajili ya shule 8 zimenunuliwa na zinasubiri
ukamilishwaji wa maabara husika.
(ii) Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES) 2004-2009
13. Mheshimiwa
Spika, katika hotuba yangu ya bajeti ya mwaka 2003/04 niliahidi kuwa
Serikali ingekamilisha Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES). Ninafurahi kulitaarifu Bunge lako tukufu
kwamba utayarishaji wa Mpango huo umekamilika na
utagharimu jumla ya Shilingi bilioni 1,433.084
kwa miaka mitano ya 2004-2009.
Katika bajeti ya mwaka 2004/05 zimetengwa jumla ya Shilingi 91,481,468,500 zikiwemo Shilingi 59,413,581,900 za Maendeleo na Shilingi 32,067,586,900 za matumizi ya kawaida. Hii mara ya kwanza kuwa na
bajeti kubwa kiasi hiki kwa Elimu ya Sekondari.
Namshukuru Rais wetu Mheshimiwa Benjamini William Mkapa kwa jitihada zake anazofanya kuhusu Elimu.
14. Mheshimiwa
Spika, lengo kuu la Mpango 2004/05 ni kuongeza
vijana wa
14.1 Kuongeza wanaojiunga na sekondari (improvement of access) kufikia 50 % ya rika
lengwa (miaka 14-17) na 50% ua wahitimu wa Darasa la VII; pia 50% ya wahitimu
wa Kidato cha 4 kujiunga Kidato cha 5 kila mwaka. Lengo hili litafikiwa kwa kufanya yafuatayo:
(a) Upanuaji wa shule zilizopo na ujenzi wa
shule mpya hususan kule ambako haziko.
Inatarajiwa kujenga shule mpya
1500 katika kipindi cha mpango.
(b) Kuongeza nafasi za Kidato cha 5 na 6 zaidi ya mara tano za
mwaka 2003.
(c) Utumiaji mzuri wa walimu waliopo, na
upanuaji wa mafunzo na ajira ya walimu. Chuo cha
Ualimu Dar es Salaam na Shule ya Sekondari Mkwawa vitabadilishwa
kuwa Vyuo Vikuu Vishiriki vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ili pamoja na
Stashahada za Elimu vitoe pia Shahada ya Ualimu katika miaka 3. Aidha, mafunzo ya Stashahada na Shahada yataoanishwa ili mafunzo ya Stashadada yatosheleze
sehemu ya Shahada ya Ualimu ya mwaka wa kwanza. Kwa hiyo, mwenye Stashahada ya Ualimu ataweza kujiunga
na Chuo Kikuu kukamilisha miaka 2 iliyobakia ili apate
Shahada yake ya Ualimu.
(d) Kuisaidia Sekta binafsi inayotoa Elimu ili iboreshe shule zake kwa sababu inasaidia Serikali kutoa
elimu.
(e) Kupanua elimu ya
sekondari kwa njia ya posta
(f) Kupunguza viwango vya
kuacha shule, kurudia na kufeli katika ngazi zote.
(g) Kupunguza mzigo wa elimu ya
sekondari kwa familia kwa kupunguza ada na michango.
Kielelezo 14: Malengo ya MMES 2004-2009
|
Na. |
MALENGO |
MWAKA |
||||||
|
2004 |
2005 |
2006 |
2007 |
2008 |
2009 |
2010 |
||
|
1.. |
Wanafunzi K1 |
132,146 |
171,793 |
225,317 |
297,971 |
397.097 |
532,786 |
719,328 |
|
2. |
Wanafunzi K1-K4 |
379,534 |
461,384 |
585,298 |
768,749 |
1,030,256 |
1,386,043 |
1,869,903 |
|
3. |
Kidato cha 5 |
18,229 |
23,558 |
31,687 |
42,912 |
58,454 |
80,017 |
109,987 |
|
4. |
Jumla Wanafunzi
K1-K6 |
411,973 |
503,170 |
640,543 |
843,348 |
1,131,622 |
1,524,513 |
2,059,907 |
|
5. |
Walimu wapya |
1,124 |
2,740 |
4,593 |
7,023 |
9,481 |
13,269 |
16,194 |
|
6. |
Madarasa mapya
|
885 |
1,678 |
2,788 |
3,442 |
5,633 |
6,596 |
|
|
7. |
Nyumba za Walimu |
1,633 |
2,414 |
3,890 |
6,337 |
5,910 |
3,298 |
|
|
8. |
Maabara |
682 |
596 |
1,039 |
1,773 |
3,470 |
3,298 |
|
|
9. |
Maktaba |
335 |
199 |
346 |
591 |
1,157 |
1,649 |
|
14.2
Kuongeza usawa (improvement of equity) kwa jinsi zote, wilaya
zote, wenye ulemavu na makundi tofauti ya mapato kwa:
(a) Kuelekeza uwekezaji
kule kwenye uhaba wa shule pamoja na kukamilisha shule
zilizopo.
(b) Kuwalipia ada watoto wa familia maskini.
(c) Kuongeza kujiunga,
kubakia shuleni na kufaulu kwa wasichana.
(d) Kuboresha majengo na vifaa katika shule zenye wanafunzi wenye ulemavu.
(e) Kuboresha utoaji wa elimu kwa jamii zilizo nyuma kielimu na zisizofikika kwa
urahisi.
(f) Kupunguza ada katika
Sekondari za Serikali za kutwa.
14.3
Kuongeza ubora (quality improvement) wa elimu ili wanaofaulu
Kidato cha 4 katika Madaraja I-III waongezeke kutoka 36% mwaka 2003 hadi 70% mwaka
2009; kwa kuchukua hatua zifuatazo;
(a) Kuongeza na kuimarisha Mafunzo ya Ualimu Kazini.
(b) Kuboresha sifa za
kujiunga na mafunzo ya ualimu wa Stashahada na Shahada.
(c) Kuboresha mitaala kwa kuzingatia masomo sahihi ya Elimu ya Sekondari na
kuingiza ndani yake Elimu ya Kujitegemea na kuacha kufundisha masomo ya
michepuo hususan ya Ufundi Kilimo na Biashara.
(d) Kuboresha maktaba za
shule.
(e) Kutoa Ruzuku ya
Uendeshaji wa Shule kwa kwa ajili ya mahitaji ya vifaa
vya kufundishia na kujifunzia.
(f) Kuboresha muundo na ubora wa mitihani.
(g) Kupanua mafunzo ya
Elimu ya Ualimu ya Stashahada na Shahada.
(h) Kuingiza katika
mitaala masuala mtambuka
14.4Kufanya mageuzi ya kutoa madaraka
(Devolution of powers) kwa
Mikoa, Wilaya na Shule ili kuboresha usimamiaji na uendeshaji wa shule za
sekondari. Madaraka ya uamuzi, utendaji,
usimamiaji wa fedha yatahamishwa kutoka Wizara kwenda
ngazi za Mkoa, Wilaya na Bodi za Shule.
14.5
Kuboresha Mfumo wa Usimamiaji wa Elimu kwa lengo la kuhakikisha kuwa Wizara
inatekeleza majukumu yake ya msingi (core functions) wa kubuni sera,
kufuatilia na kutathmini, kutunga kanuni, kuainisha, na kuhakiki utumiaji wa
raslimali. Lengo hili litafikiwa kwa;
(a) Kuimarisha Ukaguzi wa Shule na kuimarisha Uongozi
wa Shule.
(b) Kuboresha upatikanaji
na utumiaji wa mfumo wa taarifa na mawasiliano ya
Kielimu (Education Management Information
System - EMIS).
(c) Kujenga uwezo (capacity building) katika ngazi zote.
(d) Kuimarisha
mawasiliano na ufahamikaji wa mpango
(e) Kuimarisha
ufuatiliaji na tathmini (monitoring and evaluation).
(iii) Mkakati wa
Kibajeti wa Utekelezaji wa MMES 2004-2009
15. Mheshimiwa Spika, mkakati wa utekelezaji
wa mpango huu utakua kwa kuongeza uwekezaji katika elimu kwa njia ya bajeti ya Serikali
inayokwenda moja kwa moja kwa walengwa.
Hatua na njia muhimu zitakazotumika kuanzia
Bajeti ya mwaka 2004/05 zitakuwa:
15.1 Kutoa
Ruzuku ya Maendeleo kwa ajili ya shule za Serikali
zinazojengwa na wananchi
(a) Shilingi 7.0 milioni kwa ajili ya ujenzi wa darasa
ili kununulia vifaa vya ujenzi kutoka viwandani (mabati, saruji, nondo,
misumari, rangi na vioo) pamoja na madawati, kabati, mbao za kuandikia, meza na
viti.
(b) Shilingi 9.0 milioni kwa ajili ya ujenzi wa
nyumba ya mwalimu ili kununulia vifaa vya ujenzi vinavyotengenezwa
viwandani (mabati, saruji, nondo, misumari, rangi na vioo).
(c) Ujenzi wa maabara na maktaba kwa zabuni ya
serikali ngazi ya Wilaya
(d) Kusaidia ujenzi wa hosteli pale
inapohitajika kwa kulipia vifaa vya ujenzi vinavyotengenezwa viwandani (mabati,
saruji, nondo, misumari, rangi, na vioo vya madirisha).
15.2 Kutoa
Ruzuku ya Uendeshaji wa
Shule (capitation grant) kwa ajili ya vifaa vya kufundishia na
kujifunzia ya:
(a) Shilingi 30,000 kwa
kila mwanafunzi kwa Sekondari za Serikali;
(b) Shilingi 15,000 kwa mwanafunzi kwa Sekondari zisizo za Serikali
ambazo haziendeshwi kibiashara na siyo seminari.
15.3 Kutoa Ruzuku ya Maendeleo kwa
mwenye shule asiye Serikali aliyeidhinishwa na Afisa Elimu Kiongozi kwa
ajili ya ujenzi wa shule za wanafunzi wenye ulemavu kwa viwango sawa na ile
inayotolewa kwa ajili ya Sekondari za Serikali zinazojengwa na wananchi.
15.4 Kupunguza ada ya Sekondari za
Kutwa za Serikali kutoka Shilingi 40,000 kuwa Shilingi 20,000 kuanzia
Januari 2005. Hatua hii imechukuliwa ili watoto wengi wa familia zenye mapato ya chini waweze
kujiunga na sekondari kwa kulipia angalau shilingi 10,000 kwa muhula.
15.5 Kuongeza maradufu Ruzuku ya Elimu ya Sekondari kwa
watoto wa familia maskini ili
watakaonufaika waongezeke kutoka 6,000 kwa mwaka kuwa 12,000 kwa mwaka kuanzia mwaka
2005.
16. Mheshimiwa
Spika, Mpango huu umeongeza uwezekano wa watoto wa
familia maskini kujiunga na Sekondari za Bweni kwa Serikali kufanya yafuatayo:
(a)
Kubakiza shuleni ada yote ya shilingi 70,000;
(b)
Kutoa pia shilingi 30,000 za Ruzuku ya Uendeshaji na kufanya jumla
iwe shilingi 100,000 kwa mwanafunzi kwa mwaka; na pia
(c)
Zimepangwa shilingi 862.47 za chakula kwa
mwanafunzi kwa siku.
17. Mheshimiwa
Spika, kutokana na hatua hizo za kibajeti
Sekondari zote za Serikali zitapewa fedha ya kutosha ya uendeshaji wa
shule. Kwa hiyo Bodi za shule haziruhusiwi kutoza michango yoyote kwa ajili ya uendeshaji wa sekondari zote za Serikali. Serikali
inataka watoto wote wanaochaguliwa kwenda sekondari, wawe wanajiunga na kuendelea bila kuacha shule mpaka wahitimu ili tuweze
kuyafikia malengo ya Mpango huu ya kuwa na wanafunzi wa Sekondari 2,000,000
ifikapo mwaka 2010, na wahitimu wa Sekondari wasiopungua 500,000 kila mwaka.
(iv) Mwaka wa
18. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mwaka wa kwanza wa Mpango huu utakuwa
ifuatavyo:
18.1
Kutoa Ruzuku ya Maendeleo ya
Shilingi 7.0 milioni kwa darasa kukamilisha ujenzi
wa madarasa 1,456 katika shule zilizopo
za mikondo 2 na 3 ili ziwe za mikondo minne. Jumla ya Shilingi
10,192,000,000 zimetengwa kwa ajili hiyo.
18.2
Kutoa Ruzuku ya Maendeleo
ya Shilingi 7.0 milioni kwa ujenzi wa darasa kukamilisha ujenzi wa madarasa 458 katika sekondari mpya
katika maeneo yasiyo na sekondari za kutosha (underserved areas). Jumla zimetengwa Shilingi 3,206,000,000.
18.3
Kutoa Ruzuku ya Maendeleo
ya Shilingi 9.0 milioni kwa ujenzi wa kila nyumba ili kukamilishia ujenzi wa Nyumba za Walimu 957. Jumla ya Shilingi 8,613,000,000 zimetengwa kwa ajili hiyo.
18.4
Kukarabati shule 40 za
Serikali zilizopo kwa Shilingi 2,734,000,000.
18.5
Kukarabati shule 8 za
sekondari zenye wanafunzi wenye ulemavu na kuchangia
ujenzi wa shule mpya 2 za wenye ulemavu Shilingi 1,231,400,000.
18.6
Kukamilisha ujenzi wa maabara 90 katika shule 36 kwa Shilingi 1,109,273,900.
18.7
Kujenga majengo yanayohitajika katika sekondari 14 za Serikali ili kuzibadilisha
mwaka unaofuata zitoe elimu ya Kidato
cha 5 na 6 tu na kupanua nyingine 64 za “A
- level” kwa Shilingi 3,132,000,000.
18.8
Kugharimia Elimu ya Sekondari kwa watoto 12,000 wa familia maskini kwa Shilingi 2,160,000,000 kwa Kidato cha 1
mwaka 2005.
18.9
Kutoa Elimu ya Sekondari kwa mfumo usio rasmi (Open and distance learning) kwa Shilingi 1,878,000,000.
18.10
Kutoa Ruzuku ya Shilingi
20,000 kwa kila mwanafunzi wa Sekondari ya Serikali ya
Kutwa kufidia punguzo la karo. Jumla
Shilingi 4,939,000,000 zimetengwa.
18.11
Kutoa Ruzuku ya
Uendeshaji ya Shilingi 20,000 kwa mwanafunzi kwa sekondari
za Serikali na sh. 10,000 kwa
Sekondari zisizo za Serikali ambazo sio za kibiashara na sio Seminari. Jumla Shilingi
7,074,219,000 zimetengwa.
18.12
Kupunguza masomo ya Sekondari kutoka
13 kuwa 8 yakiwemo Mathematics, Lugha
(Kiswahili na English),
masomo ya Sayansi (Biology, Physics na Chemistry)
na Sayansi ya Jamii (History, Geography na
Civics); na kuacha kufundisha
michepuo (Technical Studies, Agriculture na
Commerce) ambayo ina vyuo vyake chini
ya Wizara husika.
18.13
Kuongeza nafasi za Mafunzo ya Ualimu
wa sekondari, kwa kukibadilisha Chuo cha Ualimu Dar es
Salaam na Shule ya Sekondari Mkwawa kuwa Vyuo Vikuu Vishiriki vya Elimu ya Ualimu
ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
18.14
Kutoa chakula sekondari za bweni: Shilingi. 9,417,173,200 sawa na sh 862.47 kwa mwanafunzi kwa siku;
18.15
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na mazungumzo na Wabia na Wahisani ili kupata fedha za kutosha
kutekeleza malengo yote ya Mpango. Naishukuru
Kielelezo: 18
Shughuli Kuu Zitakazofanyika Katika MMES Mwaka wa
|
No |
Shughuli |
Kiasi cha Kazi/Idadi |
Jumla (Sh.’000) |
|
1 |
Ujenzi madarasa katika
shule 728 zilizoko |
Madarasa 1,456 |
10,192,000 |
|
2 |
Ujenzi wa madarasa katika
shule mpya |
Madarasa 458 |
3,206,000 |
|
3 |
Ujenzi wa nyumba za walimu
katika shule zilizoko na mpya |
Nyumba za walimu
957 |
8,613,000 |
|
4 |
Matengenezo shule za zamani |
Shule 40 |
2,734,000 |
|
5 |
Upanuzi wa "A -
level" tupu |
Shule
14 |
1,000,000 |
|
6 |
Upanuzi wa "A - level" katika shule nyingine
64 |
Shule 64 |
2,132,000 |
|
7 |
Ujenzi wa madarasa na
miundombinu shule zenye walemavu |
Shule
10 |
1,231,400 |
|
8 |
Upanuzi wa Elimu ya
Ualimu-Stashahada |
Vyuo
12 |
1,396,200 |
|
9 |
Upanuzi wa Elimu ya
Ualimu-Shahada |
Vyuo
2 |
390,000 |
|
10 |
Upanuzi na uimarishaji wa
Open and Distance learning |
Kazi
mbalimbali |
1,878,000 |
|
11 |
Kutayarisha Curriculum and
Examination Framework |
Kazi
mbalimbali |
88,000 |
|
12 |
Ruzuku ya vifaa vya
kufundishia na kujifunzia shule za Serikali na zisizo za Serikali |
Aina
mbalibali |
6,054,219 |
|
13 |
Ruzuku ya uendeshaji
kufidia ada |
Wanafunzi 246,950 |
4,939,000 |
|
14 |
Kulipia ada wanafunzi kutoka familia masikini |
Wanafunzi
12,000 |
2,160,000 |
|
15 |
Chakula cha wanafunzi |
Wanafunzi
40,440 |
9,417,173 |
|
16 |
Ujenzi wa Uwezo ( |
Makundi
mbali mbali |
788,175.9 |
|
JUMLA |
56,219,167.9 |
||
Malengo Maalumu ya Elimu
ya Ualimu
(a)
Kuandaa walimu wa ngazi ya cheti Daraja A na Stashahada ili kukidhi
mahitaji kwa shule za Awali, Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu.
(b) Kuboresha mazingira ya kutolea
mafunzo katika Vyuo vya Ualimu kwa kutoa vifaa bora na
vya kutosha vya kufundishia na kujifunzia.
(c) Kuimarisha Vituo vya Walimu (“Teachers’
Resource Centres – TRCs”) katika ngazi ya Wilaya, Kanda na Taifa.
(d)
Kuboresha taaluma na utaalamu wa ufundishaji wa masomo ya shule za msingi
hususan kwa kuwapatia mafunzo maalumu kazini ya Daraja A (“In-Service Grade A”) walimu wote wa Daraja B/C na kuwatahini.
(e)
Kupanua
mafunzo ya Ualimu sambamba na upanuaji wa Elimu ya Msingi
na Sekondari.
19. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2003/04, Idara ya
Elimu ya Ualimu ilitoa mafunzo kwa:
(a)
Walimu tarajali wa Daraja A ambapo
walimu 6,578 walihitimu kwa kufaulu baada ya mazoezi kwa vitendo.
(b)
Mwaka 2003, wanachuo 15,283
waliandikishwa kufanya mitihani; na kati yao 14,836 walifaulu na kuendelea
mwaka wa pili wa mafunzo kwa vitendo shuleni.
(c)
Walimu wa
Stashahada 2,390 wamehitimu. Wizara ilifanya ukarabati Vyuo vya Elimu ya
Ualimu 10 kwa gharama ya Shilingi 130,300,000. Vyuo vilivyofanyiwa ukarabati ni:
Marangu, Dar es Salaam, Kleruu, Ilonga, Nachingwea, Tandala, Sumbawanga,
Morogoro, Tarime na Mpuguso.
(d)
Mwaka 2004, wanachuo 10,037 wamejiunga
na Mafunzo ya Ualimu Daraja A tarajali katika Vyuo vya Ualimu vya Serikali na 751
katika vyuo visivyo vya Serikali.
|
AWAMU |
MAELEZO |
IDADI |
|
2002 |
Wanachuo walioandikishwa Daraja A Tarajali Wanachuo Waliofanya
mtihani (na kufaulu mwaka wa kwanza) |
7,284 7,070 |
|
2003 |
Wanachuo waliofanya mazoezi shuleni (mwaka wa pili) Wanachuo waliohitimu mwaka wa pili Wanachuo walioshindwa mwaka wa pili Wanachuo ambao hawakutahiniwa mwaka wa pili |
6,607 6,578 4 25 |
|
Pili 2003 |
Wanachuo Daraja A Tarajali walioandikishwa Wanachuo waliofanya mtihani na kufaulu mwaka wa kwanza |
15,283 14,836 |
|
Tatu (2004) |
Wanachuo Daraja A Tarajali walioandikishwa Wanachuo Stashahada walioandikishwa Wanachuo Stashahada waliohitimu |
10.037 3,105 2,390 |
19.5 Wawezeshaji 763 walipatiwa
mafunzo kwa ajili ya kuwaendeleza walimu wa C/B kufikia Daraja la A (Inservice Grade A). Walimu 25,000 wa Daraja C/B, wameandikishwa
kwa ajili ya mafunzo hayo.
Mafunzo
Kwa Wawezeshaji
|
Maelezo |
Idadi |
|
Wawezeshaji
Ngazi ya Taifa |
35 |
|
Wawezeshaji
Ngazi ya Kanda |
300 |
|
Wawezeshaji
Ngazi ya Wilaya |
428 |
|
Jumla |
763 |
19.6 Walimu 16 ambao hawajasomea
taaluma ya Ualimu wanalipiwa gharama ya mafunzo ya Stashahada ya Uzamili katika
Elimu («Post Graduate Diploma in
Education»). Aidha, wakufunzi 250
wanasoma Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa kugharamiwa na Serikali.
20. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/05, wanachuo tarajali 10,000 wa Daraja A na 3,624
wa Stashahada watajiunga na mafunzo ya Ualimu. Walimu 25,000 wa Daraja C/B watajiunga na
mafunzo ya kujiendeleza. Walimu 49,000
watajiunga na mafunzo kazini ya ufundishaji kwa kutumia njia na mbinu
shirikishi kupitia Vituo vya Ualimu (TRCs).
Aidha, walimu wa shule za msingi wa Daraja
A watapewa mafunzo kazini ya aina mbalimbali kwa kutumia njia na mbinu
shirikishi.
Wanachuo Wapya,Mafunzo ya Ualimu 2004/05
|
Maelezo |
Idadi |
|
Wanachuo Daraja A
tarajali |
10,000 |
|
Wanachuo tarajali
Stashahada |
3,624 |
|
Jumla ya Walimu wapya |
13,624 |
|
Mafunzo kazini |
|
|
Mafunzo kazini kwa
walimu wa Daraja la A (Elimu ya Awali 200, fani za Sanaa na Ufundi 70, Elimu
Maalumu 60, Sayansi Kimu Cheti 140, Stashahada Elimu Maalumu 30 na Sayansi Kimu 50) |
550 |
|
Mafunzo Kazini kwa walimu ya ufundishaji kutumia
njia na mbinu shirikishi kupitia Vituo vya Walimu (TRCs) |
49,000 |
|
Mafunzo Kazini kwa Walimu wa Daraja C/B |
25,000 |
|
Jumla mafunzo Kazini |
74,550 |
21. Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka 2003/04, Idara ya Ukaguzi wa Shule ilikagua
jumla ya asasi za elimu 15,733 sawa na 82% ya lengo la mwaka. Katika kuboresha kazi ya ukaguzi wa shule, Wizara imenunua magari mawili, kwa ajili ya
ukaguzi wa shule na imeendesha mafunzo ya awali ya ukaguzi wa shule kwa
wakaguzi wa shule wapya 127.
Malengo na Utekelezaji wa Ukaguzi wa
Shule 2003/04
|
Aina ya Asasi |
Lengo |
Utekelezaji
wa Lengo |
%
Lengo |
|
Shule za Awali Shule za Msingi Vituo vya Ufundi Stadi Shule za Elimu Maalumu Vituo vya Elimu ya Watu Wazima Shule za Sekondari Vyuo vya Elimu ya Ualimu |
2,812 7,747 182 113 7,747 617 41 |
2,810 6,552 160 74 5,557 539 41 |
99.9 84.5 88 65 72 87 100 |
|
Jumla
|
19,259 |
15,733 |
82 |
Shughuli nyingine
zilizofanyika ni pamoja na:
(a)
Kutoa Jarida la FAHAMU ELIMU Na. 6 kuhusu somo la Kiswahili kwa lengo la kubaini maendeleo ya somo
(b)
Kufanya ukaguzi maalumu wa shule za Sekondari 179 kwa ajili ya upanuzi wa Elimu ya
Sekondari.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/05,
Wizara imepanga kufanya ukaguzi wa asasi mbalimbali za
Elimu 19,332. Aidha, Idara itanunua
magari 13 na kutoa mafunzo ya awali ya Ukaguzi wa Shule
kwa wakaguzi wa shule wapya 127.
Malengo ya Ukaguzi wa Shule 2004/05
|
Shule za Awali |
2,812 |
|
Vituo vya Ufundi Stadi |
|
Shughuli
nyingine zitakazofanyika ni pamoja na:
21.3
Utafiti kuhusu maendeleo ya
ufundishaji wa somo la Stadi za Kazi katika Shule za Msingi na Vyuo vya Ualimu Daraja
la A.
21.4
Kuandika Jarida la FAHAMU ELIMU Na. 7 kuhusu somo la Civics.
Malengo Maalumu ya Maendeleo ya
Utamaduni
(a) Kupanua kiwango cha Ushiriki wa wananchi katika shughuli za Utamaduni.
(d) Kuboresha Usimamizi na Uendeshaji wa shughuli za Utamaduni.
(e) Kuimarisha Elimu na
Mafunzo ya Fani za Utamaduni.
(f) Kuimarisha na
kukuza Tasnia na Miundo Mbinu ya Utamaduni.
(g) Kulinda na
kuimarisha Maadili na Utambulisho wa Taifa.
(h) Kuimarisha Ushirikiano wa Kimataifa katika Utamaduni.
22. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Idara ya Maendeleo ya Utamaduni kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ilitekeleza mambo yafuatayo:
(a) Iliandaa mashindano ya kupata Vazi la Taifa
kwa wanaume na wanawake.
(b) Ilitoa misaada kwa miradi mbalimbali ya
Utamaduni kupitia Mfuko wa Utamaduni.
(c) Iliendesha mradi wa Sanaa kwa wanafunzi wa
shule za Msingi katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Pwani. Aidha, Wizara iliendesha Mradi wa TUSEME
katika shule 16 za Sekondari za Wasichana na za mchanganyiko 7.
(d) Iliendesha tamasha la Sanaa la Ishirini na
mbili la Bagamoyo lililoshirikisha wasanii wa Vikundi 64 vya ndani na nje ya
nchi.
(e) Ilitoa Mafunzo ya Stashahada kwa wanafunzi 87
na mafunzo ya muda mfupi kwa washiriki 60 katika Chuo cha Sanaa, Bagamoyo.
(f)
Ilitoa mafunzo kwa Maafisa Utamaduni wa Wilaya 96 juu ya jinsi ya kubadili
mila na desturi zinazoongeza kasi ya maambukizi ya UKIMWI.
(g) Iliendesha Mkutano Mkuu wa Sekta ya
Utamaduni.
Katika mwaka
2004/05, Idara ya Utamaduni itatekeleza mambo kumi
kuhusu utafiti wa mila na desturi, maonesho ya utamaduni na mafunzo ya
utamaduni yafuatayo:
(a)
Itafuatilia matokeo ya
mchakato wa mashindano ya Vazi la Taifa kwa wanaume na wanawake.
(b)
Itaendesha mafunzo ya
ukusanyaji, uhifadhi na usambazaji wa takwimu za Utamaduni kwa Maafisa
Utamaduni 113 wa Halmashauri .
(c)
Itaendesha mkutano wa Sekta
ya Utamaduni utakaowashirikisha wajumbe 300 kutoka Serikali Kuu, Serikali za
Mitaa, Mashirika, Vyama vya Hiari na Asasi zisizo za Serikali.
(d)
Itaendesha programu za Sanaa
kwa wanafunzi wa shule za msingi 70 katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani,
Morogoro na Jiji la Mwanza pamoja na programu ya TUSEME kwa shule za sekondari
23 za mikoa 19 ya Tanzania Bara.
(e)
Itaendesha mafunzo ya
Stashahada kwa wanafunzi 90 na mafunzo ya muda mfupi kwa washiriki 60.
(f)
Itaendesha Tamasha la
ishirini na tatu la Sanaa Bagamoyo.
(g)
Itaendelea kusaidia miradi
ya utamaduni kupitia Mfuko wa Utamaduni.
(h)
Itaendesha tamasha la
Utamaduni la Taifa litakaloshirikisha Mikoa yote.
(i)
Itaendesha warsha ya
mapambano dhidi ya UKIMWI.
(j)
Itatengeneza filamu moja juu
ya UKIMWI itakayooneshwa nchini kote.
23. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2003/04, Idara ya Utawala na Utumishi ilishughulikia ajira ya walimu wapya 2,904 wa shule za Sekondari, Vyuo vya Elimu
ya Ualimu na watumishi wasio walimu 28.
Ajira ya Walimu na Watumishi Wasio Walimu
|
Walimu 1.
Walimu wa
Sekondari wapya |
2,839 |
|
2.
Walimu
mbadala wa sekondari |
65 |
|
Jumla ya Walimu wa Sekondari |
2,904 |
|
Watumishi Wasio Walimu |
|
|
1. Karani
Masijala |
1 |
|
2.
Maafisa Maghala Wasaidizi |
1 |
|
3. Mkutubi |
1 |
|
4. Wasaidizi
wa Hesabu na Wahasibu |
9 |
|
5. Fundi
Sanifu |
2 |
|
6. Madereva |
9 |
|
7. Katibu
Mahususi |
4 |
|
8. Wahudumu |
1 |
|
Jumla ya Watumishi Wasio Walimu |
28 |
|
Mambo Mengine ya Ajira |
|
|
1. Watumishi waliopandishwa vyeo |
173 |
|
2. Waliothibitishwa kazini |
168 |
|
3. Waliopewa barua za ajira ya kudumu |
156 |
|
Jumla |
497 |
Aidha, jumla
ya watumishi 275 walipata mafunzo mbalimbali ya muda mfupi na
mrefu ndani na nje ya nchi.
|
Mafunzo kwa Wafanyakazi |
|
|
1. Mafunzo ya Shahada ya kwanza 2. Mafunzo ya Shahada ya pili 3. Mafunzo ya Muda Mfupi Fani Mchanganyiko 4. Mafunzo ya Stashahada 5. Mafunzo ya Cheti 6. Stashahada za Uzamili |
75 25 72 46 15 42 |
|
Jumla Kuu |
275 |
Katika mwaka 2004/05, Wizara
inatarajia kuomba kibali cha ajira mpya ya watumishi 2,780 wa
kada mbalimbali. Katika jitihada za
kujenga uwezo wa watumishi, Wizara itapeleka Watumishi
100 kwenye mafunzo ya muda mrefu na 50 ya muda mfupi ndani na nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/05, Idara itahakikisha
Programu ya kuboresha Utumishi wa Umma inatekelezwa
kwa kushirikisha Sekta binafsi katika kutoa huduma za usafi, ulinzi na mapokezi
katika jengo la Wizara Makao Makuu. Aidha, kuanzia Julai 2004 Wizara itaanza
utekelezaji wa mpango wa mwaka wa tathmini ya utendaji kazi wa watumishi kwa
utaratibu mpya unaolenga kuweka malengo na matokeo katika utendaji kazi (“Performance Management System”) kwa watumishi
wa Makao Makuu ya Wizara na kwenye Shule na Vyuo.
24. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Wakala wa Maendeleo
ya Uongozi wa Elimu (Agency for the Development of Education
Management – ADEM), walitoa mafunzo ya menejimenti na utawala kwa
viongozi watendaji wa elimu wa ngazi mbalimbali 518.
Mafunzo ya Menejimenti ADEM 2003/04
|
Mdau na
Aina ya Mafunzo |
Walengwa |
|
1.Stashahada ya
Uongozi wa Elimu kwa Viongozi wa Idara mbalimbali za Elimu |
147 |
|
2.
Mafunzo Mafupi ya wakuu wa shule za Sekondari za
Serikali na zisizo za Serikali. |
113 |
|
3. Maafisaelimu wa Wilaya (Wiki 1-2) |
4 |
|
4. Waratibu wa Elimu Kata |
69 |
|
5. Walimu Wakuu wa Shule za Msingi |
185 |
|
Jumla Kuu |
518 |
Katika mwaka 2004/05, ADEM itatoa mafunzo
mbalimbali kwa viongozi watendaji wa elimu 6,108 wakiwemo Stashahada ya Uongozi
wa Elimu kwa wanachuo 90.
Mafunzo
ya Wafanyakazi
|
Aina
ya Mafunzo |
Wingi |
|
1. Stashahada
ya Uongozi wa Elimu Wanachuo 2. Mafunzo
ya miezi 3 kwa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi 3. Mafunzo
mafupi kwa Waratibu wa Elimu wa Kata 4. Maafisa
Elimu wa Wilaya 5. Wakuu
wa Shule za Sekondari |
90 3,200 2,500 118 200 |
|
Jumla
Kuu |
6,108 |
25.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2003/04,
Idara ya Sera na Mipango ilishirikiana na Idara nyingine:
(a)
Kupanga, kuratibu na kutekeleza mipango
ya elimu kulingana na Sera ya Elimu na Mafunzo na Utamaduni.
(b)
Imesimamia ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa mipango ya
kazi
(c)
Imesimamia na kuratibu ukarabati wa shule
za Sekondari na Vyuo vya Elimu ya Ualimu.
(d)
Imetekeleza wajibu wake wa kuwa kiungo kati ya Wizara yangu, Wizara
ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ofisi ya Rais Mipango na
Ubinafisishaji, Wizara ya Fedha, Wahisani na Wadau mbalimbali
(e)
Shughuli nyingine zilizofanyika ni pamoja
na kutayarisha programu na mipango ya muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu ya
sab-sekta ya elimu ya awali, msingi, sekondari, ualimu, elimu ya watu wazima na
utamaduni, pamoja na kuandaa na kuratibu rasimu za maandiko mbalimbali zikiwemo
hotuba za bajeti.
Katika mwaka 2004/05, Idara ya Sera na
Mipango itashughulikia masuala mbalimbali pamoja na:
(a)
Kufanya utafiti na tathmini kwa matumizi
ya baadaye, kufuatilia mwenendo na utoaji wa huduma za elimu na utamaduni na
kutoa ushauri wa kitaalamu.
(b)
taendelea kuandaa na kuratibu rasimu na maandiko
mbalimbali ya kitaalamu yanayohusu miradi na mipango, sera, takwimu, hotuba na
makala mbalimbali.
(c)
Itaendelea kuandaa mapitio ya matumizi ya fedha za umma (“Public Expenditure Review”) kuandaa “Medium Term Expenditure Framework - MTEF)”
za Wizara na Sekta ya Elimu kwa ujumla kwa
kushirikiana na sab sekta nyingine za elimu.
(d)
Itaendelea kusimamia na kuratibu
ukarabati wa shule za Sekondari na Vyuo vya Elimu ya Ualimu.
(e)
Itatoa mafunzo kwa jumuiya za shule na
vyuo kuhusu matengenezo madogo madogo na dhana ya utunzaji wa majengo na
mazingira yake.
(f)
Kuratibu
misaada ya wahisani pamoja na kusimamia uimarishaji wa
EMIS.
(g)
Itasimamia
uthibiti wa ubora wa vitabu na zana za kufundishia
zinazotumika shuleni na vyuoni.
H: Ofisi
ya Afisa Elimu Kiongozi
26. Mheshimiwa
Spika, Afisa Elimu Kiongozi pamoja na kuratibu
utekelezaji wa Sera za Elimu na Mafunzo, na Utamaduni na kutoa miongozo ya
kuboresha Elimu na Utamaduni, huongoza vitengo maalumu vilivyo katika ofisi
yake. Aidha, Afisa Elimu Kiongozi
husimamia shughuli za uhusiano wa Kimataifa ikiwa ni
pamoja na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC.
Kitengo cha Elimu ya Watu Wazima
26.1.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2003/04
Kitengo cha Elimu ya Watu Wazima kilihamasisha Viongozi 759 wa
Mikoa na Halmashauri kuhusu utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa Elimu ya Watu
Wazima na MEMKWA. Aidha, Kitengo kilitoa
mafunzo ya wiki tatu kwa wawezeshaji wa MEMKWA 496 wa
ngazi ya Halmashauri, watendaji wa ngazi ya Mikoa, watendaji wa Kanda na
washiriki kutoka
Wawezeshaji Waliopewa
Mafunzo ya MEMKWA
|
Na. |
Ngazi ya Washiriki |
Idadi |
|
1. |
Halmashauri |
456 |
|
2. |
Mikoa |
21 |
|
3. |
Kanda |
14 |
|
4. |
|
5 |
|
|
Jumla |
496 |
Mheshimiwa Spika, katika kuboresha elimu itolewayo katika madarasa
ya EWW na MEMKWA, Kitengo kiliendesha mafunzo ya
wawezeshaji 73 wa Elimu ya Watu Wazima na 96 wa MEMKWA katika Manispaa za
Ilala, Kinondoni na Temeke.
Mheshimiwa Spika, idadi ya wanafunzi wanaosoma kupitia MEMKWA na wanakisomo kupitia MUKEJA ni 340,060:
Wanafunzi/Wanakisomo wa MEMKWA na
MUKEJA
|
1.
|
Mpango |
WV/ME |
WS/KE |
Jumla |
|
2.
|
MEMKWA |
35,850 |
44,210 |
80,060 |
|
3.
|
MUKEJA |
158,706 |
101,294 |
260,000 |
|
|
JUMLA |
194,556 |
145,504 |
340,060 |
Katika mwaka 2004/05, Kitengo cha Elimu ya Watu Wazima kitatekeleza
yafuatayo:
(a)
Kutoa mafunzo kwa wawezeshaji wa MEMKWA
1,475 na MUKEJA 2,706.
(b) Kununua na kusambaza moduli za MEMKWA 81,132 na nakala 570 za
Miongozo ya Elimu ya Watu Wazima katika Halmashauri.
(c)
Kufuatilia maendeleo ya madarasa ya MEMKWA
(d) Kuratibu masomo ya Elimu
ya Sekondari kwa njia ya Posta utakaotekelezwa chini
ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES) 2004-2009.
(e)
Kutoa miongozo ya uendeshaji wa MEMKWA na MUKEJA
26.2 Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Wizara ilitoa mafunzo ya muda mfupi kwa walimu 164 wasio wataalamu wa Elimu Maalumu kuhusu Elimu
Ujumuisho. Pia, ilichapisha na kusambaza jumla ya nakala 1,500 za vitabu vya masomo
mbalimbali ya shule za msingi kwa wanafunzi wasioona.
Vitabu vya Wanafunzi Wasioona Vilivyochapishwa
|
|
Aina |
Idadi ya Nakala |
|
1. |
Hisabati Darasa la VII |
500 |
|
2. |
Stadi za Kazi Darasa la
V |
600 |
|
3. |
Stadi za Kazi Darasa VI |
400 |
|
|
Jumla |
1,500 |
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/05, Wizara itanunua mtambo
mpya kwa ajili ya kuchapa vitabu na makala mbalimbali
za “Braille” na itatoa mafunzo ya
muda mfupi kwa walimu wataalamu 36 wa wanafunzi Viziwi kuhusu Lugha ya Alama,
matengenezo ya Shime Sikio (“Hearing Aids”)
na utunzaji wake. Pia, itatoa mafunzo ya
muda mfupi kwa walimu 128 wasio wataalamu wa Elimu
Maalumu kuhusu Elimu Ujumuisho. Vilevile,
Wizara itatengeneza na kusambaza michoro mguso 100,
ramani mguso 500 na Shime Sikio 500.
26.3. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04,
Kitengo cha Usajili wa Shule, kilisajili shule zisizo
za serikali 90. Aidha,
shule103 zimethibitishwa Mwenye Shule na Meneja.
Shule Zilizosajiliwa
|
Na. |
Aina ya Asasi |
Idadi |
|
1. |
Shule za awali |
5 |
|
2. |
Shule za msingi |
6 |
|
3. |
Shule za awali na
msingi |
43 |
|
4. |
Shule za Sekondari |
35 |
|
5. |
Chuo cha Elimu ya Ualimu |
1 |
|
|
Jumla |
90 |
Shule Zilizothibitishwa Mwenye Shule na
Meneja
|
Na. |
Aina ya Asasi |
Idadi |
|
1. |
Shule za Awali |
24 |
|
2. |
Shule za Msingi |
37 |
|
3. |
Shule za Sekondari |
42 |
|
Jumla |
103 |
|
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2003/04 shule 179 zilizojengwa kwa nguvu za wananchi zilipewa
kibali cha kuanzishwa. Aidha, katika mwaka 2003/04 waombaji 326 walipewa leseni
za kufundisha baada ya kuwa na sifa zinazostahili.
Waombaji Waliopewa Leseni
za Kufundisha
|
Na. |
Aina ya Asasi |
Idadi |
|
1. |
Shahada ya Uzamili |
48 |
|
2. |
Shahada ya |
180 |
|
3. |
Stashahada |
42 |
|
4. |
Cheti cha Ualimu |
38 |
|
5. |
Kidato cha 6 |
18 |
|
Jumla |
326 |
|
Mwaka 2004/05 Kitengo cha Usajili wa
Shule kimepanga:
(a) Kushughulikia maombi 130
ya kuanzisha na kuthibitishwa Meneja, Mwenye Shule
zisizo za serikali.
(b) Kushughulikia maombi 229
ya vibali vya kuanzisha shule za sekondari.
(c) Kushughulikia maombi 400
ya leseni za kufundisha.
(d) Kuchapisha nakala 200,000
za vyeti vya usajili wa walimu.
(e) Kukusanya takwimu za
walimu walio kazini na kuendelea kuwasajili.
(f) Kuratibu masuala ya
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na Jumuiya ya Kusini
mwa Afrika.
(g) Kuratibu Utafiti Na. 3 wa Ubora wa Elimu Katika Nchi 15 za Kusini mwa Afrika.
Kitengo cha Elimu kwa
Redio
(a) Sehemu ya Redio
26.4 Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Wizara yangu kwa kushirikiana na Redio
Tanzania Dar es Salaam (RTD) iliandaa na kutangaza vipindi 104
Mheshimiwa Spika, mwaka 2004/05 vipindi 248 vitatangazwa
(a)
Itaandaa na kutangaza vipindi 52 vya
‘Boresha Elimu’ ili kuendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu MMEM 2002-2006 na
MMES 2004-2009.
(b)
Itaandaa na kutangaza vipindi 52 vya
Ufundishaji mitaala mipya kwa walimu.
(c)
Itatangaza vipindi 96 vya Kiingereza
na Maarifa ya
Jamii darasa la VI na VII.
(d)
Itaandaa na kutangaza vipindi 48 vya
Kiingereza na Maarifa ya Jamii la DV.
(b) Sehemu ya Elimu Dhidi ya UKIMWI
26.5. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Wizara iliendesha semina za wadau wanaohusika na utekelezaji wa Mpango wa Elimu Dhidi ya UKIMWI kwa
waelimishaji wenza katika Asasi na Idara mbalimbali. Aidha, mafunzo ya elimu hiyo yalitolewa kwa walimu 48 wasioona, walimu wa shule za msingi 800,
walimu wa shule za sekondari 1,620, pamoja na wafanyakazi wa Baraza la Mitihani
la
Katika mwaka 2004/05, Wizara itatekeleza mambo yafuatayo kuhusu Elimu
Dhidi ya UKIMWI
(a) Kukamilisha mada za Elimu
ya Kujikinga na UKIMWI kwa ajili ya kuingizwa kwenye
mihtasari ya masomo chukuzi katika shule za Sekondari na vyuo vya Elimu ya
Ualimu.
(b) Itaendelea kuchapisha na kusambaza maandiko ya mafunzo ya Elimu ya Kujikinga na
UKIMWI shuleni na vyuo vya Elimu ya Ualimu.
(c) Itaendesha mafunzo kwa walimu wa shule za sekondari.
(d) Itafanya ufuatiliaji na tathmini ya programu ya UKIMWI shuleni.
(e) Itaendelea kutekeleza
programu ya UKIMWI shuleni.
I: Taasisi
na Mabaraza yaliyo chini ya Wizara
Taasisi ya Elimu
27. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04,
27.1
Taasisi ya Elimu
(a)
Ilikamilisha Mfumo wa Taifa wa Ukuzaji
Mitaala. (“National Curriculum
Development Framework”).
(b) Ilitoa mafunzo ya MEMKWA kwa wawezeshaji 371 toka kanda zote 7 za elimu.
(c)
Ilitoa mafunzo mbalimbali kwa wakuza
mitaala 33 na wafanyakazi waendeshaji 42.
(d) Iliandaa miongozo miwili
ya kufundishia na kujifunzia Hisabati na Sayansi kwa
shule za msingi.
(e)
Ilifanya tathmini ya Mtaala wa Elimu ya
Msingi.
(f)
Ilirekebisha Mihtasari ya Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti kwa masomo yote na kuandikia moduli .za masomo hayo.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/05, TET itatekeleza mambo
makuu yafuatayo:
(a)
Kuchapisha na kusambaza Mfumo wa Taifa wa
Ukuzaji Mitaala (“National Curriculum
Development Framework”).
(b)
Kuendesha mafunzo kwa wawezeshaji wa
MEMKWA mwaka wa pili na wa tatu na kufanya tathmini ya ufundishaji wa masomo
sita ya MEMKWA.
(c)
Kufaragua visanduku viwili vya Sayansi na
Maarifa ya Jamii kwa shule za msingi.
(d)
Kuboresha mtaala wa elimu ya msingi.
(e)
Kugharimia mafunzo ya Wakuzaji Mitaala 3 na
waendeshaji 3.
(f)
Kuandika “Instructional Manual” ya masomo ya Arts, Crafts, Muziki na Michezo.
(g)
Kuitisha mikutano 12 ya majopo ya masomo.
(h)
Kuandika “Instructional
Manual” 2 kwa ajili ya shule za msingi na shule za
awali.
(i)
Kurekebisha mihtasari ya sekondari na
ualimu ngazi ya Stashahada.
(j)
Kuandika “Methods Manuals”
kwa ajili ya walimu.
(k)
Kutayarisha Moduli tatu za chati za masomo ya Sayansi, Hisabati,
Maarifa Jamii na Stadi za Kazi kwa shule za msingi.
(l)
Kuandaa na kurekodi vipindi vinne vya
masomo sita ya shule za msingi katika redio na televisheni.
(m)
Kuandika miongozo miwili ya kufaragua zana zinazotumika
kufundishia na kujifunzia.
(n)
Kufanya semina tatu za taaluma kwa wakuza
mitaala.
(o)
Kununua gari moja kwa ajili ya usimamizi,
utafiti na ufuatiliaji.
(p)
Kuendesha semina sita za wakuu wa shule
za msingi na sekondari.
(q)
Kuandika na kuchapisha maandiko kuhusu
ugonjwa wa UKIMWI na madhara yake pamoja na kujumuisha mada za UKIMWI katika
baadhi ya masomo ya shule za msingi na sekondari.
(r)
Kununua vifaa mbalimbali kwa ajili ya
Kituo cha Maarifa Kielimu, Vyumba vya majaribio ya Sayansi na kuboresha
mandhari katika maeneo ya TET.
(s)
Kuchapisha na kusambaza kijarida cha TET (TIE Newsletter) na jarida la
‘Tanzania Educational Journal’ (TEJ).
(t)
Kununua vitabu vya Dewey “Decimal
Classification” kwa ajili ya maktaba ya TET.
(u)
Kuendesha semina za
kuwahisisha (sensitize) wafanyakazi
kuhusu ugonjwa wa UKIMWI na athari zake.
(v)
Kujaribisha, kurekebisha na kusambaza
maandiko kuhusu ugonjwa wa UKIMWI na madhara yake katika Shule za Msingi, Sekondari
na Vyuo Elimu ya Ualimu.
Taasisi ya Elimu
ya Watu Wazima (TEWW)
27.2 Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Taasisi
ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) imetekeleza mambo yafuatayo:
(a)
Imekarabati majengo ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima katika Mkoa
wa Morogoro (WAMO).
(b) Imetoa mafunzo ya muda
mfupi kwa watumishi 12 kuinua viwango vya elimu.
(c)
Imetoa nakala 1,000 za majarida ya “Studies in Adult Education No.
60” na Journal of “Adult Education No. 12”.
(d) Imeboresha masomo ya
Elimu kwa Njia ya Posta kwa kuhariri na kuchapa makala
za Historia na Kiswahili.
(e)
Imeendesha mafunzo ya cheti cha sheria kwa
wanafunzi 166, stashahada ya Elimu ya watu Wazima 159 na mafunzo ya ushonaji
12.
(f)
Imenunua kiwanja mkoa wa
(g)
Imerekebisha mihtasari ya mafunzo ya Cheti na
Stashahada ya juu ya EWW.
Katika mwaka 2004/05, Taasisi ya Elimu ya
Watu Wazima itatekeleza mpango wenye mambo yafuatayo kwa
lengo la kuimarisha utoaji wa Elimu ya Watu Wazima na Elimu ya Kujiendeleza nje
ya mfumo rasmi kwa walioikosa walipokuwa katika umri sahihi wa kuwa shuleni;
(a)
Kuendesha mafunzo
ya Stashahada ya EWW kwa watendaji 150.
(b) Kuimarisha, kurekebisha na kuchapa masomo kwa Njia ya Posta.
(c)
Kutoa mafunzo kwa wakufunzi na walimu wa
muda 200.
(d) Kuongeza wanafunzi wa Elimu ya Sekondari kwa Njia ya Posta kutoka 4,000 hadi
10,000.
(e)
Kutoa majarida ya “Studies in Adult Education No. 61” na “Journal
of Adult Education 13,” (nakala 1000).
(f)
Kuongeza wanafunzi wa mafunzo ya Cheti
cha Sheria kutoka 166 hadi 250.
(g)
Kutoa mafunzo ya muda mfupi kulingana na
mahitaji kwa washiriki 200.
(h)
Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa TEWW 60.
(i)
Kukarabati vituo vya Iringa na Tabora.
(j)
Kujenga/kununua majengo kwa ajili ya
vituo vya TEWW.
(k) Kuajiri wakufunzi 20 ili kuimarisha utendaji mikoani na Makao Makuu.
(l)
Kuimarisha kitengo cha Utafiti na kununua
magari matatu kwa ajili ya ufuatiliaji wa shughuli za Taasisi mikoani.
(m) Itaendelea kutoa elimu ya
UKIMWI kwa jamii kwa kuendesha kampeni ya kitaifa
ambayo inawalenga wananchi vijijini ambao hawapati taarifa sahihi juu ya mbinu
za kupambana na janga la UKIMWI.
Bodi ya Huduma za Maktaba
27.3 Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Bodi ya
Huduma za Maktaba
(a)
Iliongeza vitabu
37,759 katika maktaba.
(b)
Ilitembelea shule na taasisi mbalimbali 227 kwa ajili ya kuhamasisha.
(c)
Iliendesha kambi za
kujisomea katika vituo 5 vya Korogwe, Singida, Tukuyu, Kilosa na Songea.
(d)
Iliendesha Tamasha
la Wiki ya Vitabu katika vituo 10 vya maktaba za mikoa.
(e)
Ilitoa matangazo ya
zabuni kwa ajili ya ukarabati maktaba za Kagera na
Tabora pamoja na kuboresha maktaba ya Mwl. J.K. Nyerere ya Butiama.
(f)
Iliendelea na ujenzi wa Maktaba ya Mkoa wa
(g)
Ilitoa mafunzo ya
muda mrefu na mfupi kwa watumishi 57.
Mheshimiwa Spika, mwaka 2004/05, BOHUMATA
itatekeleza mambo yafuatayo katika mpango wake wa
kuendeleza maktaba nchini;
(a)
Kuimarisha na kuboresha huduma kwa
kuongeza machapisho 40,000.
(b)
Kuendeleza ujenzi wa maktaba ya mkoa wa
(c)
Kujenga majengo mahsusi ya Chuo cha Ukutubi na
Uhifadhi Nyaraka, Bagamoyo.
(d)
Kuendesha Tamasha la Wiki ya Vitabu katika mikoa ya Kilimanjaro,
Arusha, Iringa, Mbeya, Songea, Tabora, Singida, Musoma, Mwanza na Morogoro.
(e)
Kuendesha warsha na semina 4 za kuongeza
uelewa na athari za UKIMWI.
Baraza la Mitihani la Tanzania (BAMITA)
27.4
Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2003/04, Baraza la Mitihani liliendesha
mitihani ya Kitaifa ya kumaliza: (a)
Elimu ya Msingi ya Darasa la VII Tanzania Bara, (b) Elimu ya Sekondari ya Kidato cha 4; (c) ya Kidato cha 6 na (d) Mitihani ya Ualimu Tanzania Bara na
Tanzania Visiwani.
Mheshimiwa Spika, kuhusu
Mtihani wa Kitaifa wa kumaliza Elimu ya Msingi, yaani Darasa la VII mwaka 2003
kati ya watahiniwa 490,018 waliofanya mtihani waliofaulu walikuwa 196,273 sawa
na 40.1% ikilinganishwa na 133,674 sawa na 27.1% waliofaulu mwaka 2002.
Kielelezo Na.
27.1 Matokeo ya Mtihani ya D.VII 1998 – 2003

TANBIHI: Alama ya kufaulu mwaka 2003 ilikuwa 85/200, badala ya 65/150 baada
ya kuongezwa somo la nne
Mheshimiwa Spika, kuhusu
mtihani wa kitaifa wa kidato cha 4 mwaka 2003, kati ya watahiniwa 54,904 wa
shule, waliofaulu katika Daraja I, II, na III walikuwa 23,751 sawa na 38.1% ikilinganishwa
na 17,939 sawa na 36.2% waliofaulu mwaka 2002.
Nawapongeza wakuu
wa shule na walimu wote waliohusika na ongezeko la
waliofaulu 5,812 pamoja na wanafunzi husika wote 23,751.
Kielelezo Na.27.2: Matokeo ya Mtihani wa K. 4 kwa
Wanafunzi wa
Shule 1998-2003
|
Mwaka |
Idadi ya Watahiniwa |
Waliofaulu |
|
|
Daraja
I-III |
Daraja
I-IV |
||
|
1998 |
42,887 |
12,404 (28.9%) |
32,468 (75.7%) |
|
1999 |
44,172 |
12,774 (28.9%) |
35,468 (80.0%) |
|
2000 |
47,397 |
12,237 (25.8%) |
37,140 (78.4%) |
|
2001 |
50,820 |
14,397 (28.3%) |
39,326 (77.4%) |
|
2002 |
49,512 |
17,939 (36.1%) |
42,746 (86.3%) |
|
2003 |
62,359 |
23,751 [38.1%] |
54,904 [88.1%] |
Kielelezo Na27.3: Waliofaulu K.4 D. I-III na
D. 0 Shule za Serikali
[Pamoja na Zilizojengwa na
Wananchi] 1999 – 2003

Kielelezo
Na.27.4: Matokeo ya Mtihani wa
Kitaifa wa Kidato cha 4 Daraja I-III Shule zote (za Serikali na zisizo za
Serikali) 1998 - 2003

Kielelezo Na. 27.5: Asilimia
ya Kufaulu Kidato cha 4 katika kila Daraja

Mheshimiwa Spika, uchambuzi wa matokeo ya Mtihani wa Taifa wa
Kidato cha 4 mwaka 2003 unaonesha kuwa juhudi za kuboresha Elimu ya Sekondari
zinazaa matunda mema
Kielelezo Na.27.6: Matokeo
ya Mtihani wa K. 4 Sekondari za Serikali na
Zisizo za Serikali kwa
Pamoja,
D.I+D.II+D.III = 39.1%

Kielelezo Na.
27.7: Matokeo ya Mtihani wa
K. 4 Sekondari za
D.I+D.II+D.III = 45.9%

Kielelezo Na. 27.8: Matokeo
ya Mtihani wa K. 4 Sekondari
Zisizo za
Serikali
D.I+D.II+D.III = 40.4%

Kielelezo Na27.9: Matokeo ya Mtihani wa K.
4 Sekondari
D.I+D.II+D.III = 19.5%

Mheshimiwa Spika, kuhusu
mtihani wa Kitaifa Kidato cha 6 mwaka 2002/03 kati ya watahiniwa 12,003,
waliofaulu katika Daraja I, II na III walikuwa 10,584 sawa na 88.2%
ikilinganishwa na 9,992 sawa na 86.3% waliofaulu mwaka 2001/02.
Kielelezo Na. 27.10: Matokeo ya
Mtihani wa K. 6, Watahiniwa Shuleni : 1998-2002/03
Kielelezo Na.27.11:
Matokeo ya Mtihani wa K. 6,
Watahiniwa Binafsi: 1997/98-2002/03
Mheshimiwa
Spika, katika mitihani ya Ualimu ya
mwaka 2003 waliofaulu walikuwa 18,522 sawa na 94.7% ya watahiniwa wote 19,569. Katika mitihani ya Elimu ya Ufundi
ya mwaka 2003 waliofaulu walikuwa 514 sawa na 54.6% ya
watahiniwa 942 wa mitihani hiyo.
Kielelezo Na. 27.12: Matokeo ya
Mtihani wa Ualimu , 2000-2003
Kielelezo Na. 27.13: Matokeo ya
Mitihani wa Ufundi , 2000-2003
Mheshimiwa Spika, mwaka 2003/04, BAMITA imetekeleza
mambo muhimu yafuatayo yaliyopendekezwa na Tume Maalumu ya Serikali
iliyochunguza mianya ya uvujaji wa mitihani miaka iliopita;
(a)
Ujenzi wa Jengo la Usajili wanapofikia wageni bila kuingia ofisi
zingine za Baraza la Mitihani Tanzania.
(b)
Ukarabati wa jengo la Kitengo cha Chapa na Uchapishaji.
(c)
Ununuzi wa baadhi ya mashine za uchapaji mitihani.
(d)
Ununuzi wa baadhi ya kompyuta na vifaa vyake kwa ajili ya kuandaa na
kutoa matokeo ya mitihani.
(e)
Kuweka
mtandao wa Kompyuta (Local Area Network-LAN) kwa madhumuni ya kutoa huduma bora.
(f)
Kufanya maandalizi
ya awali ya ujenzi wa kituo cha Usahihishaji Mitihani Mbezi Wani
Mheshimiwa Spika, kutokana na utekelezaji huo ninayo furaha
kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa kuanzia mwaka jana mitihani ya Kitaifa ya
Darasa la VII, Kidato cha 4 na Kidato cha 6 imeanza kuchapwa hapa nchini kwa
usalama.
Katika mwaka 2004/05, Baraza la Mitihani la
(a) Litafanya utafiti, tathmini, usanifu na ukuzaji mitihani mbalimbali ya kitaifa.
(b) Litaendesha mitihani ya: kumaliza elimu ya msingi; Maarifa (Qualifying
Test); Kidato cha 4 na 6; kuhitimu Elimu ya Ualimu
daraja la A na Stashahada (Diploma) ya Ualimu.
(c) Litaendesha mitihani ya: Cheti cha
Ufundi Sanifu (Full Technician
Certificate - FTC); na Stashahada ya juu ya
Uhandisi kwa niaba ya Baraza la Taifa la elimu
ya Ufundi.
(d) Litasimamia mitihani ya nje
inayofanywa na watahiniwa hapa nchini.
(e) Litaendeleza ujenzi wa kituo cha kusahihishia mitihani.
(f) Litatengeneza programu ya kompyuta
itakayowezesha utoaji wa matokeo ya kufaulu mtihani wa Kidato cha 4 na uchaguzi
wa wanafunzi wa kuingia Kidato cha 5 kwa pamoja ili kuongeza ufanisi wa utoaji
wa elimu.
27.5 Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2003/04 Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)
lilitekeleza mambo yafuatayo:
(a)
Lilitoa elimu ya sanaa na
uongozi kwa wasanii 104 katika taaluma zifuatazo: Uongozi wa vikundi, sarakasi,
majukwaa, uingizaji, utengenezaji ala za muziki wa kiasili, ubunifu wa ngoma na
miondoko, utawala bora na utunzi wa nyimbo za kuhamasisha maendeleo ya jamii
(b)
Lilihamasisha Umma kutambua
na kuthamini sanaa kwa kupitia
mashindano ya kuchora, nyimbo za halaiki, matamasha ya sanaa kwa watoto
na watu wazima
(c)
Liliendesha kwa kushirikiana
na Baraka Women Group, mafunzo ya kuimarisha miradi kwa kazi za ufundi wa
mikono kwa akina mama katika mikoa ya Dodoma, Morogoro na Tanga.
(d)
Liliendesha warsha na semina juu ya elimu ya Hakimiliki na
Hakishiriki kwa wasanii 304 mikoa ya Dar es Salaam ,
(e)
Lilikamilisha michoro ya
ujenzi wa ukumbi wa wazi (Open Air
Theatre) na kuiwasilisha kwa Mhandishi wa Halmashauri ya Jiji kwa uhakiki.
(f)
Liliendelea na ujenzi wa ukuta kuzunguka eneo la BASATA ambapo asilimia
75 imekamilika.
(g)
Lilitoa elimu ya UKIMWI kwa mikoa 4 kwa kuendesha mashindano ya kuchora,
maonyesho, matamasha na mashindano ya sanaa.
Katika
mwaka 2004/05, BASATA litatekeleza mpango wenye mambo yafuatyo
ya kukuza sanaa;
(a) Litakuza ujuzi, elimu ya kisanii kwa wasanii
wa ufundi, maonyesho na muziki kwa kuendesha kozi fupi fupi 27.
(b) Litaendelea kutoa elimu ya Hakimiliki na
Hakishiriki kwa wasanii 600, wakuzaji sanaa 90 na viongozi 13 wa vyama vya
sanaa.
(c) Litahimiza jamii kuthamini na kuboresha
muziki, kuanzisha/kuimarisha matamasha, halaiki na mashindano ya sanaa
mbalimbali vijijini.
(d) Litaendesha Elimu ya Uongozi na Bajeti kwa
watendaji 10.
(e) Litaanzisha ujenzi wa ukumbi wa wazi (“Open Air Theatre”).
(f) Litakamilisha ujenzi wa uzio.
Baraza la Kiswahili la Taifa
(BAKITA)
27.6 Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2003/04,
Baraza la Kiswahili la Taifa limetekeleza mambo yafuatayo;
(a) Lilisanifu Istilahi mpya za mchanganyiko kwa
ajili ya kuziba pengo la msamiati katika mawasiliano ya kila siku serikalini,
mashirika na sekta binafsi na kuzisambaza kwa watumiaji kupitia vyombo vya
habari.
(b) Lilikusanya na kusahihisha makosa kutoka
vyombo mbalimbali vya habari na kuyawasilisha katika sehemu husika ili
wayazingatie.
(c) Liliendesha semina kwa wafasiri, wakalimani,
waandishi wa habari na watayarishaji wa vipindi vya Redio na Televisheni.
Katika mwaka wa 2004/05, Baraza la Kiswahili la Taifa litatekeleza mambo yafuatayo katika kukuza
Kiswahili:
(a)
Litafanya maadhimisho ya
Nane ya Siku ya Kiswahili kwa kushirikiana na asasi mbalimbali za Kiswahili,
kuwatunukia na kuwaenzi waliochangia maendeleo ya Kiswahili kwa kuzingatia
kauli mbiu ya «Kiswahili na Janga la UKIMWI, 2004/05».
(b)
Litaendeleza vuguvugu la
kuhamasisha matumizi ya Kiswahili kwenye sekta ya biashara na viwanda kwa
kufanya utafiti kupitia Shirika la Viwango Tanzania .
(c)
Litaratibu matumizi fasaha
ya Kiswahili kwa vyombo vya habari kwa kuendesha Semina kwa Wahariri wa Vyombo vya
Habari.
(d)
Litaendesha Warsha ya
Kusanifu Istilahi 250 mchanganyiko ili kuziba pengo la msamiati na kuleta
uwiano wa matumizi.
III.
MATATIZO
KATIKA UTEKELEZAJI
28. Mheshimiwa
Spika, Wizara yangu imebaini matatizo yafuatayo:
28.1 Baadhi ya
Halmashauri zimeonesha udhaifu katika kutoa taarifa za utekelezaji na
kutokufunga hesabu za mwaka za fedha za Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi
(MMEM) kwa wakati, jambo ambalo ni kinyume na sheria, kanuni na taratibu za
usimamizi bora wa fedha za umma. Kasoro
hii sharti irekebishwe mara moja kwa kuimarisha mfumo wa ukaguzi wa ndani. Udhaifu huu umesababisha kuchelewa kwa fedha za
mwaka wa tatu kutoka kwa wahisani. Kila
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri na Maafisaelimu (Wilaya) warekebishe kasoro
hii.
28.2
Bado baadhi ya wakurugenzi wa HALMASHAURI
hawataarifu Walimu Wakuu na Kamati za Shule kiwango
kilichotolewa kwa kila mwanafunzi cha Ruzuku ya Uendeshaji iliyopokelewa
kutoka Serikali Kuu. Narudia maagizo yangu ya mwaka jana kuwa lazima Walimu
Wakuu na Kamati za Shule wapewe taarifa hiyo ili wafuatilie fedha
zao kulingana na jumla ya wanafunzi walionao ili wazipangie matumizi.
28.3
Baadhi ya Halmashauri kuendelea
kutokuzingatia vigezo sahihi katika ujenzi na uendeshaji wa Shule za Msingi, hivyo
naagiza tena:
(a)
Ujenzi wa
majengo ya madarasa na nyumba za walimu uzingatie vipimo sahihi vilivyoelekezwa
na Wizara.
(b)
Ukubwa wa
Shule ya Msingi kwa wingi wa wanafunzi vijijini usizidi mikondo miwili
yaani wanafunzi 40 wa mkondo mmoja x mikondo 2 x 7 (D I-VII)= wanafunzi 560;
na MIJINI usizidi mikondo mitatu yaani 40 x 3 x 7= wanafunzi 840.
(c)
Wingi wa
Wanafunzi Darasani (Class Size) wasiwe zaidi ya wanafunzi 40; wa umri sawa
au karibu sawa ili wafundishike vizuri kwa kasi moja.
IV.
MAAMUZI
MUHIMU
29. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/05,
Wizara yangu itatekeleza maamuzi yafuatayo:
(a)
Kupunguza ada ya wanafunzi wa kutwa wa Elimu
ya Sekondari kutoka Shilingi.
40,000/- na kuwa Shilingi 20,000/- kwa mwaka, na kuendelea kutoa elimu ya
msingi ya bure na ya lazima kwa kila mtoto.
(b)
Kutoa Ruzuku ya Uendeshaji ya Shilingi 20,000 kwa mwanafunzi kwa Sekondari za kutwa za Serikali kufidia punguzo la ada.
(c)
Kujenga Maabara na Maktaba katika Shule za Sekondari
za Serikali zinazojengwa
na wananchi kwa tenda ya Serikali.
(d)
Kuimarisha Mitaala ya Elimu ya Sekondari kwa kuingiza Elimu ya Kujitegemea; na Stadi
za Kazi; na Masuala Mtambuka (Cross-cutting
Issues) katika kila somo na kupunguza idadi ya masomo yatolewayo kutoka 13
kuwa 8 ili kubakia na masomo ya msingi (Core
subjects) Civics, Kiswahili, English,
Mathematics, Biology, History, Geography, Physics na Chemistry. Masomo ya hiari (options) yaani Home Economics, Computing & Information Science, Music, Fine Art,
French, Arabic, Bible Knowledge, Islamic Studies, Pysical Education na Additional Maths yatafundishwa katika
shule zitakazoteuliwa kwa ajili hiyo.
(e)
Kupeleka fedha na madaraka ya ununuzi
wa vitabu vya kiada na ziada kwa Kamati za Shule, badala ya Halmashauri ili
kuboresha uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi kufikia kitabu kimoja kwa mwanafunzi
katika shule zote za msingi za Serikali
(f)
Kutoa Ruzuku ya uendeshaji ya Shilingi 10,000 kwa mwanafunzi kwa Shule za
Sekondari zisizo za Serikali ambazo sio za kibiashara na siyo seminari.
(g)
Kutoa Ruzuku ya maendeleo kwa wananchi wanaojenga sekondari ya Shilingi
milioni 7.0 kwa darasa na Shilingi milioni 9.0 kwa nyumba ya mwalimu na
kusaidia ujenzi wa Hosteli. Aidha, aliyeidhinishwa kuendesha Sekondari kwa
ajili ya walemavu atapewa Ruzuku viwango hivyo hivyo vya Ruzuku ya maendeleo.
(h)
Kusambaza nakala
za kutosha za miongozo yote muhimu ya MMEM na MMES kwa kila Halmashauri na
shule zote za msingi na sekondari nchini.
V.
SHUKRANI
NA PONGEZI
30. Mheshimiwa
Spika, mafanikio ya mwaka 2003/04, yametokana na ushirikiano mkubwa
uliotolewa na wananchi kwa mchango wao wa hali na mali katika kushiriki na
kuchangia mipango ya elimu na utamaduni. Waheshimiwa Wabunge, kama mnavyofahamu
sehemu kubwa ya maendeleo katika Sekta
ya elimu hutokana na moyo wa
kujitolea katika kujenga majengo ya shule hususan madarasa na Nyumba za Walimu.
Nachukua fursa hii kuwapongeza wananchi pamoja na viongozi wote wa Mikoa,
Wilaya, Vijiji pamoja na Waheshimiwa
Wabunge na Waheshimiwa Madiwani kwa mchango wao walioutoa katika
kufanikisha ujenzi wa shule na utoaji na uendeshaji wa elimu na utamaduni.
31. Mheshimiwa
Spika, nazishukuru nchi rafiki na mashirika ya kimataifa kwa michango yao
katika kuandaa na kufanikisha utekelezaji wa mipango ya elimu na utamaduni
katika mwaka 2003/04. Nchi hizo rafiki na wahisani ni: Sweden, Japan, Norway,
Uingereza, Ufaransa, Ireland, Uholanzi, Finland, Canada, Ujerumani, Ubelgiji,
China na Korea ya
Kusini. Mashirika yaliyochangia elimu na
utamaduni ni Benki ya Dunia, ADB, Sida, NORAD, ,GTZ, DFID, WFP, UNICEF, UNESCO, UNFPA , UNDP, CIDA, ILO,
EU, JICA, USAID, JOVC, VSO,Celtel, CBP, Peace Corps, Book Aid International, Aga
Khan Education Foundation, Plan International, World Vision, Ireland Aid, Care
International na Mashirika mbalimbali yasiyokuwa ya kiserikali.
32. Mheshimiwa Spika, pamoja na misaada utekelezaji wa mipango ya elimu na utamaduni kwa
mwaka 2003/04 haungefanikiwa na kukamilika katika kiwango nilichoelezea bila
jitihada, ushirikiano na uongozi wa pamoja katika Wizara yangu. Natoa shukrani zangu za pekee kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu na Utamaduni,
Mheshimiwa Bujiku K. P. Sakila,
Mbunge wa Jimbo la Kwimba, kwa ushirikiano, uaminifu na uadilifu wake
aliouonesha kwangu na kwa viongozi wetu Wakuu na kwa ushirikiano wake na
wenzetu wote Wizarani. Ninapenda pia
kutoa shukrani zangu kwa Katibu Mkuu wa
Wizara ya Elimu na Utamaduni Bibi Mwatumu J. Malale, pamoja na wasaidizi
wake akiwemo Afisaelimu Kiongozi, Wakurugenzi wa Idara wote, Viongozi wa Elimu
katika ngazi mbalimbali, Waalimu na Wafanyakazi wengine wote wa Wizara yangu
kwa ushirikiano walionipa katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara
hususan jukumu mama la utoaji elimu na ukuzaji wa utamaduni kwa mwaka
2003/04; na katika maandalizi ya Bajeti hii.
33. Mheshimiwa Spika, natoa shukrani zangu
pia kwa Wenyeviti, Wakurugenzi Watendaji, Makatibu
Watendaji na Wajumbe wa Mabaraza na Taasisi zote zilizo chini ya Wizara yangu
na wafanyakazi wengine wote katika ngazi mbalimbali kwa kazi nzuri waliyoifanya
ya kuimarisha na kuendeleza elimu na utamaduni. Pia, natoa shukurani na pongezi za pekee kwa uongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT)
kwa ushirikiano wao mzuri na ari yao ya kutatua matatizo ya walimu kwa
kushirikiana na Wizara yangu na Serikali kwa ujumla. Napenda kuwashukuru viongozi wa tawi la TUGHE la Makao Makuu ya Wizara kwa ushirikiano na
ushauri wao katika kushughulikia masuala ya wafanyakazi.
VI MAKADIRIO YA BAJETI YA WIZARA
34. Mheshimiwa Spika, baada ya kueleza yote hayo, ninaomba sasa Bunge lako Tukufu baada ya kuijadili hoja yangu pamoja na kuzingatia Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii, lipitishe makadirio ya matumizi ya