UTANGULIZI
Mheshimiwa
Spika,
1. Kutokana na taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni na Mwenyekiti wa
Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maliasili na Mazingira, naomba kutoa hoja kwamba
sasa Bunge lako tukufu likubali kupitisha makadirio ya matumizi ya Wizara ya
Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2004/2005.
Napenda kuishukuru kwa dhati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili na
Mazingira kwa kujadili makadirio ya matumizi ya fedha ya Wizara ya Maliasili na
Utalii kwa mwaka 2004/2005. Wizara yangu itazingatia na kutekeleza mapendekezo
ya Kamati hiyo.
MAPITIO YA
UTEKELEZAJI WA MPANGO WA WIZARA MWAKA 2003/2004 NA MALENGO YA MWAKA 2004/2005
Mheshimiwa
Spika,
2. Katika mwaka 2003/2004, Sekta ya Maliasili na Utalii iliendelea kuongeza
mchango wake katika Pato la Taifa. Kwa
kutumia vigezo vya kawaida vya mafanikio, wananchi wengi wameendelea kupata
ajira ya moja kwa moja katika shughuli za maliasili na utalii na vile vile
wengine kujiajiri wenyewe katika biashara mbalimbali kutokana na mazao ya
maliasili hasa uvuvi, misitu na shughuli zinazoimarisha utalii.
Mheshimiwa
Spika,
3. Kwa kutumia kigezo cha mapato ya fedha za kigeni, katika mwaka
2003, ukiachia mbali mapato kutokana na utalii, uuzaji wa mazao ya samaki pekee
nchi za nje uliingizia Taifa Dola 129.6 milioni ikilinganishwa na Dola 121
milioni mwaka 2002 na Dola 95.4 milioni mwaka 2001.
Mheshimiwa
Spika,
4. Eneo lingine lililoonyesha mafanikio mazuri ni katika ukusanyaji
wa maduhuli katika maeneo yanayosimamiwa na Wizara. Lengo la mwaka 2003/2004
lilikuwa kukusanya Sh.21.3 bilioni. Hadi mwezi Mei, 2004 Wizara
ilikwishakusanya Sh.22.9 bilioni. Makusanyo ya maduhuli yamekuwa yakiongezeka
mwaka hadi mwaka kwani katika mwaka 2002/2003 lengo lilikuwa Sh. 17.7 bilioni
lakini makusanyo halisi yalikuwa Sh. 22.4 bilioni. Maongezeko haya, bila
kubadilisha viwango vya ushuru pia ni ishara ya kuboresha utoaji huduma na
kusimamia uhifadhi.
Mheshimiwa
Spika,
5. Baada ya kusema hayo ni lazima nikiri kuwa pamoja na mafanikio
hayo, pametokea pia changamoto ambazo Wizara yangu inalazimika kuzishughulikia.
Kwa mfano, tumefanikiwa katika kuboresha uhifadhi wa wanyamapori na hivyo idadi
ya wanyama imeongezeka
Mheshimiwa
Spika,
6. Baada ya kutoa maelezo hayo ya utangulizi, napenda kulihakikishia
Bunge lako Tukufu kwamba pamoja na mafanikio na matatizo niliyoyaeleza, katika
kusimamia uhifadhi endelevu, Wizara iliendelea kufanya mapitio katika Sera,
Sheria na Kanuni za sekta zake ndogo na kutekeleza programu mbalimbali za
kuimarisha sekta hizo. Vile vile,
utangazaji wa utalii uliimarishwa kwa kutafuta masoko mapya na kuongeza
ushirikiano na sekta binafsi.
Mheshimiwa
Spika,
7. Naomba sasa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji ya mwaka 2003/2004
na malengo ya Wizara kwa mwaka 2004/2005
Mheshimiwa Spika,
8. Sekta hii ni msingi wa biashara
ya utalii nchini na inachangia maendeleo ya wananchi kwa kutoa asilimia ya
mapato kugharamia miradi ya kijamii.
Sekta imetekeleza majukumu yake kwa kuzingatia ushirikishaji wa wananchi
katika kuhifadhi na kunufaika na uhifadhi huo.
Kuandaa na Kusimamia Sera
Mheshimiwa Spika,
9. Katika mwaka 2003/2004 moja ya kazi za sekta
hii ilikuwa kufanya mapitio ya Sera ya Wanyamapori pamoja na kufanya
marekebisho ya Sheria ya Wanyamapori ili iendane na marekebisho yaliyoko kwenye
sera.
Katika kipindi cha 2004/2005 sekta hii
itakamilisha mapitio ya sera na sheria husika.
Kuanzisha Maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi ya
Wanyamapori
Mheshimiwa Spika,
10. Katika mwaka 2003/2004, Wizara yangu kwa
kutumia wataalamu wake ilitoa elimu juu ya Kanuni za Maeneo ya Jumuiya ya
Hifadhi ya Wanyamapori (Wildlife Management Areas Regulations – WMAs) za mwaka
2002 kwa baadhi ya viongozi Watendaji wa vijiji na Halmashauri za Wilaya 13
kati ya 16 ambazo zimo kwenye majaribio ya matumizi ya Kanuni hizo. Wilaya hizo
ni Monduli, Kiteto, Ngorongoro, Kilolo, Morogoro, Rufiji, Tunduru, Songea,
Tarime, Urambo, Sikonge, Namtumbo na Babati ambazo zimehusisha jumla ya vijiji
73. Katika wilaya ya Serengeti elimu
ilitolewa pia kwa wananchi kwenye mikutano ya hadhara katika vijiji vitano
vinavyounda eneo la Majaribio la Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori la Ikona.
Mheshimiwa Spika,
11. Maeneo ya Majaribio ya Wilaya za Rufiji na
Morogoro tayari yameshawasilisha maombi rasmi ya kutangazwa na Jumuiya za Jamii
kutambuliwa kisheria kuwa zitasimamia wanyamapori katika ardhi za vijiji vya
Tapika na Ngarambe kwa Wilaya ya Rufiji na eneo la Ukutu linalohusisha vijiji
23 kwa Wilaya ya Morogoro. Wilaya
zilizobaki zenye vijiji vilivyomo kwenye mpango wa Majaribio ya WMA, zimo
katika hatua za kuandikisha Jumuiya za Jamii (Community - based Organisation - CBO)
kwa mamlaka husika. Aidha, Wilaya 10 kati ya 17 zimeunda Bodi za Wilaya za Ushauri
wa Masuala ya Maliasili.
Wizara imeandaa viashiria
na mpango wa utekelezaji wa viashiria hivyo kwa ajili ya ufuatiliaji wa
utekelezaji wa Kanuni za Maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori, ili
kuwezesha tathmini ya utekelezaji wa Kanuni ifikapo miaka mitatu tangu zianze
kutumika.
Katika kuendeleza
uhamasishaji na elimu kwa umma vipindi vya radio 20 vilirushwa hewani na Redio
Tanzania, picha za video 14 zilioneshwa katika Mikoa 7 na kipindi kimoja
kilirushwa kupitia Televisheni ya Taifa.
Mheshimiwa Spika,
12. Katika mwaka 2004/2005 Wizara itatoa mafunzo
kwa watumiaji viashiria kuhusu ufuatiliaji wa mabadiliko kwenye WMA na
utekelezaji wa mpango wa viashiria. Wizara itaendelea kutoa mafunzo kuhusu
Kanuni za WMA katika vijiji na Jumuiya za Jamii na itaendelea kufuatilia kwa
karibu uendeshaji na usimamizi wa Maeneo 16 ya Majaribio ya kanuni za Hifadhi
ya Wanyamapori.
Mheshimiwa Spika,
13. Ulinzi wa Wanyamapori
uliimarishwa kwa kuwapatia watumishi mafunzo maalum pamoja na kuwapatia
vitendea kazi. Hadi Aprili 2004, Doria zilizofanyika zilinasa watuhumiwa 1,700
na nyara mbalimbali za Serikali ikiwemo kilo 587.8 za meno ya tembo, kilo 79 za
meno ya kiboko na ngozi 64 za wanyama. Vile vile, bunduki 349 za aina
mbalimbali zilikamatwa.
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itaendelea kuimarisha ulinzi kwa
kuimarisha doria, kuwapatia watumishi 160 mafunzo kuhusu kupambana na ujangili
pamoja na kuongeza vitendea kazi.
Ulinzi wa Maisha na
Mheshimiwa Spika,
14. Katika
mwaka 2003/2004, siku 1,122 za doria zilitumika kusaka wanyamapori waharibifu
katika Wilaya 24. Risasi 23,350 za aina mbalimbali zilinunuliwa kwa ajili ya
kudhibiti wanyama waharibifu na kati ya hizo 3,080 zilitolewa kwa Halmashauri
za wilaya 24.
Mheshimiwa Spika,
15. Katika kipindi cha 2004/2005,
Wizara itaendeleza ulinzi wa maisha na
Usimamizi na Uendelezaji wa Mapori ya Akiba
Mheshimiwa Spika,
16. Mwaka 2003/2004, Wizara
ilikamilisha mipango ya Uendeshaji wa Mapori ya Akiba ya Burigi/Biharamulo, na
Ibanda/Rumanyika. Kazi ya kupitia mipango ya uendeshaji wa mapori ya akiba ya
Ugalla na Mkomazi/Umba inaendelea. Barabara mpya zenye urefu wa kilometa 1,753
zilitengenezwa na nyingine zenye urefu wa kilometa 2,756 zilifanyiwa ukarabati.
Viwanja vipya vya ndege vitano vilijengwa katika mapori ya akiba ya Selous,
Moyowosi/Kigosi, Mpanga/Kipengere, Lukwika/Lumesule na Ugalla. Vile vile,
viwanja 17 vilifanyiwa matengenezo ya kawaida. Mipaka ya mapori ya
Lukwika/Lumesule, Rungwa/Kizigo, Ugalla, Mpanga/Kipengere, Moyowosi/Kigosi na
Liparamba imepitiwa na kuchorwa upya. Kilometa 1,033 za mipaka ya mapori
zimefanyiwa ukarabati. Katika mapori ya Usangu na Mpanga/Kipengere mipaka
iliwekwa alama za kudumu. Aidha, nyumba 10 za watumishi zimejengwa na 42
kukarabatiwa katika vituo mbali mbali.
Vile vile, Wizara iliwahamisha wafugaji waliokuwa wanaishi ndani ya
Mheshimiwa Spika,
17. Katika kipindi cha 2004/2005,
Wizara itaendelea kupanua mtandao wa barabara katika mapori ya akiba kwa kulima
barabara mpya zenye urefu wa kilomita 350 na kukarabati barabara zenye urefu wa
kilomita 1,000. Aidha, Wizara itakamilisha kupitia mpango wa uendeshaji kwa
mapori ya Akiba ya Ugalla na Mkomazi na itaandaa mipango ya Uendeshaji mapori
ya Rukwa/Lukwika na Mpanga/Kipengele. Mpango wa uwekezaji wa
Usimamizi wa Ardhioevu
Mheshimiwa Spika,
18. Katika mwaka wa 2003/2004, Wizara
ilikamilisha kuorodhesha eneo la Bahari la Rufiji–Kilwa-Mafia kuwa eneo la
ardhioevu yenye umuhimu wa kimataifa (Ramsar site). Hivyo tangu nchi yetu
iliporidhia mkataba wa Ramsar mwaka 2002 ilishatenga maeneo manne muhimu yenye
hadhi
Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori
Mheshimiwa Spika,
19. Utafiti wa Wanyamapori umelenga
kutathmini wingi wa rasilimali pamoja na kubaini magonjwa kwa lengo la kuwa na
rasilimali endelevu ya wanyamapori.
20. Katika kipindi cha 2003/2004,
Taasisi ilifanya sensa za wanyamapori katika maeneo ya Hifadhi ya Taifa
Serengeti na Mapori ya Akiba ya Moyowosi/Kigosi na Ugalla. Aidha, Taasisi iliendelea
na utekelezaji wa miradi ya utafiti wa ufugaji nyuki katika mikoa ya
Kilimanjaro, Arusha, Tanga,
Katika kipindi cha 2004/2005, Taasisi itaendelea kufanya sensa ya
wanyamapori na ndege wa majini (water birds) pamoja na kuendeleza miradi ya
utafiti. Taasisi pia itakarabati majengo ya kituo cha Tabora pamoja na kujenga
ofisi ya makao makuu.
Mheshimiwa Spika,
21. Mfuko umekuwa ukitegemea mapato
toka kwa wahisani na wakereketwa wa uhifadhi wa wanyamapori. Fedha
zinazopatikana zinatumika kuimarisha ulinzi na uhifadhi wa wanyamapori.
Mheshimiwa Spika,
22. Katika mwaka 2003/2004, Mfuko
ulitarajia kukusanya shilingi bilioni 3.9.
Hadi kufikia Aprili 2004, Mfuko ulikuwa umekusanya shilingi bilioni
3.7. Fedha hizo zilitumika kuimarisha
doria za uzuiaji ujangili, miradi ya maendeleo, kugharimia utafiti na mafunzo
ya uhifadhi.
Katika mwaka 2004/2005, Mfuko umekadiria kukusanya shilingi bilioni 3.8.
Fedha hizo zitatumika kuimarisha na kuboresha usimamizi wa uhifadhi wa
wanyamapori na mazingira pamoja na ushirikishaji wananchi katika uhifadhi wa
wanyamapori.
Mheshimiwa Spika,
23. Hifadhi za Taifa zimekuwa
zikisimamia mbuga za wanyama zilizotengwa maalum kwa ajili ya utalii wa kuona
na kupiga picha.
Katika kipindi cha 2003/2004 hadi Februari 2004, Shirika liliendesha
doria za kuzuia ujangili na kufanikiwa kukamata majangili 1,799 na silaha
mbalimbali 36 na mbao 2,104. Aidha, wanyama 326 wa aina mbalimbali waliuawa na
majangili.
Mheshimiwa Spika,
24. Hadi kufikia Februari 2004,
Watalii 304,105 walitembelea hifadhi za taifa. Idadi hii ni pungufu kwa
asilimia 11.2 ikilinganishwa na kipindi
Chini ya Mpango wake wa Ujirani Mwema, Shirika lilitumia Shilingi
milioni 102.5 kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mheshimiwa Spika,
25. Katika mwaka 2003/2004, Shirika
liliendesha warsha tatu kwa ajili ya kupata maoni ya wadau ili kuandaa mipango
ya uendeshaji ya Hifadhi za Serengeti na Mahale. Aidha, Wizara itawasilisha
muswada kwa ajili ya kuanzisha hifadhi za Saadani na Kitulo pamoja na
kupandisha hadhi ya Misitu ya Meru/Ngrudoto, Kilimanjaro/Marang na mashamba
namba 1 – 3 ya Manyara kuwa sehemu za hifadhi.
Mheshimiwa Spika,
26. Mipango na matarajio ya Shirika
kwa mwaka 2004/2005, itaelekezwa katika kuboresha miundo mbinu kwa ajili ya
utalii, kupanua wigo wa shughuli za utalii na kukamilisha mipango ya uendeshaji
wa hifadhi za Mahale, Serengeti na Gombe.
Mheshimiwa Spika,
27. Mamlaka inasimamia uhifadhi wa
bonde la Ngorongoro ambalo ni kivutio maarufu cha utalii duniani. Eneo
28. Hadi kufikia Aprili 2004, watalii
219,761 walitembelea eneo la Hifadhi ya Ngorongoro. Kati ya hao, 160,541 walitoka nje na 59,220
walikuwa watalii wa ndani ya nchi. Jumla ya Shilingi bilioni 8.5 zilikusanywa
kutokana na watalii hao na kuvuka lengo la shilingi bilioni 6.9 la mwaka
2003/2004.
Mheshimiwa Spika,
29. Katika mwaka wa 2003/2004,
Mamlaka ilikamilisha ujenzi wa barabara kutoka Makao makuu ya Hifadhi hadi Kata
ya Naiyobi, Olbalbal na Kakesio pamoja na barabara kutoka kata ya Endulen hadi
kijiji cha Olpiro.
Mheshimiwa Spika,
30. Katika kipindi cha 2004/2005,
Mamlaka inatazamia ongezeko la asilimia 10% ya watalii watakaotembelea Hifadhi
ambao wataingiza Shilingi bilioni 7.7.
Aidha, Mamlaka itakamilisha ujenzi wa Shule
ya Sekondari ya Embarway kwa kujenga madarasa nane na nyumba tano za watumishi.
SEKTA NDOGO YA MISITU NA
NYUKI
Mheshimiwa Spika,
31. Sekta hii katika kutekeleza
majukumu yake imetoa kipaumbele katika kutekeleza Sera na marekebisho ya
sheria, usimamizi shirikishi wa misitu pamoja na uendelezaji wa mashamba ya
miti na hifadhi za nyuki. Ili Sera ya Taifa ya Misitu ya 1998 na Sera ya Taifa
ya Ufugaji Nyuki ya 1998 ieleweke kwa wadau, Wizara iliweka sera hizi katika
tovuti ya Wizara ili wadau wengi waweze kuzipata.
Usimamizi Shirikishi wa
Misitu
Mheshimiwa Spika,
32. Katika mwaka 2003/2004, Wizara
iliendesha mafunzo ya usimamizi shirikishi wa misitu katika wilaya 15. Vile vile, vijiji 39 katika wilaya za
Mpwapwa, Same, Kondoa, Dodoma Vijijini, Lindi na Kilwa viliwezeshwa kuandaa
Mipango ya Usimamizi Shirikishi wa misitu na hifadhi za nyuki. Katika kuboresha uhifadhi wa Misitu ya
Hifadhi ya vyanzo vya maji na mikoko, uhamasishaji ulifanyika katika vijiji 72
kwenye wilaya 28.
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itatekeleza mpango wa usimamizi
shirikishi wa misitu katika wilaya 37 kwenye Mikoa ya Morogoro, Lindi, Iringa,
Mbeya, Mtwara, Ruvuma, Pwani, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Singida, Dodoma,
Tabora, Kigoma, Rukwa, Mwanza, Kagera na Shinyanga.
Uvunaji wa Mazao ya Misitu
Mheshimiwa Spika,
33. Katika mwaka 2003/2004 hadi
Aprili 2004, magogo yenye mita za ujazo 24,866 yalivunwa katika misitu ya
asili, na mita za ujazo 309,100 katika mashamba ya miti.
Mwaka 2004/2005, magogo yenye mita 25,000 za ujazo katika misitu ya
asili na mita za ujazo 350,000 katika mashamba ya miti yatavunwa.
Biashara ya Nje ya Mazao
ya Misitu na Nyuki
Mheshimiwa Spika,
34. Mwaka 2003/2004, Wizara
ilikadiria kuwa sekta binafsi itauza mazao ya misitu yenye thamani ya shilingi
bilioni 9.8. Hadi kufikia Aprili 2004,
mazao ya misitu na nyuki yenye thamani ya shilingi bilioni 11.6 yaliuzwa.
Katika mwaka 2004/2005, Wizara inatarajia sekta binafsi itauza mazao ya
misitu na nyuki yenye thamani ya shilingi bilioni 10.9. Aidha, kuanzia tarehe 1
Julai 2004, usafirishaji wa magogo nje ya nchi hautaruhusiwa. Madhumuni ni kuendeleza sekta ya viwanda,
kuongeza ajira na thamani ya bidhaa.
Usimamizi na Uendelezaji
wa Mashamba ya Miti
Mheshimiwa Spika,
35. Maandalizi ya upigaji picha za
anga katika mashamba ya Sao Hill, Kiwira, Buhindi, Meru na Kilimanjaro
Kaskazini yalikamilika ikiwa ni sehemu ya kukamilisha taratibu za
kuwashirikisha wadau katika kusimamia mashamba hayo.
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itakuza miche milioni 7.5 na kupanda miti
hekta 5,000. Vile vile, itapogoa miti
katika hekta 3,000 na kupunguza miti katika hekta 1,000.
Kuendeleza Ufugaji Nyuki
Mheshimiwa Spika,
36. Mwaka 2003/2004, Wizara
iliwezesha kutenga na kuchora ramani za Hifadhi za vijiji vya Tura na Kizengi
katika wilaya ya Uyui. Shughuli za ugani
zilifanyika katika Wilaya za Newala, Lindi, Masasi, Kahama, Songea,
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itatoa huduma za ugani katika wilaya 10
na kutangaza hifadhi 4 za nyuki za vijiji.
Mheshimiwa Spika,
37. Taasisi ililenga kuendeleza
usimamiaji na uratibu wa utafiti wa misitu kwa kushirikiana na taasisi nyingine
za kitaifa na kimataifa, pamoja na kutoa ushauri ili kuendeleza rasilimali za
misitu.
Katika mwaka 2004/2005, Taasisi itapanua na kuimarisha utafiti wa kilimo
misitu katika mikoa ya Pwani, Shinyanga, Mwanza, Tabora na Tanga, kwa lengo la
kuwafikia wakulima 1,000. Vile vile,
itafanya utafiti wa kuzalisha vyahuso (cloning) ya mikaratusi inayokua haraka
katika vitalu vya majaribio vilivyoko Arusha, Lushoto, Mombo, Korogwe, Kibaha,
Morogoro,
Wakala wa Mbegu za Miti
Mheshimiwa Spika,
38. Madhumuni ya Wakala ni kuwezesha
upatikanaji endelevu wa mazao ya misitu na utunzaji wa mazingira kwa kuzalisha
na kusambaza mbegu bora za miti pamoja na vipandikizi vingine.
39. Hadi kufikia Aprili 2004, Wakala
ulikusanya kilo 13,500 za mbegu, ambapo kilo 10,582 ziliuzwa nchini na 38 nchi
za nje. Vile vile, miche 20,000
ilikuzwa.
Katika kipindi cha 2004/2005, Wakala inalenga kupanua upatikanaji na
usambazaji wa mbegu bora za miti kwa kukusanya kilo 12,500 za mbegu za miti,
kuuza kilo 10,000 nchini na kilo 50 nchi za nje.
SEKTA NDOGO YA UVUVI
Mheshimiwa Spika,
40. Sekta
Ndogo ya Uvuvi ina mchango mkubwa katika upatikanaji chakula nchini. Katika
kuzingatia
Utekelezaji wa Mpango
Kamambe
Mheshimiwa Spika,
41. Mwaka 2003/2004, Wizara ilianza kutekeleza
Mpango Kamambe wa kuendeleza Sekta ya Uvuvi kwa kuanza ujenzi wa soko la kisasa
la Kirumba katika Manispaa ya Mwanza.
Vile vile, ilianza kutekeleza mradi wa kuhifadhi mazingira ya Ziwa
Ufugaji wa Samaki na
Ukulima wa Mwani
Mheshimiwa Spika,
42. Katika mwaka 2003/2004, Wizara
yangu iliendeleza juhudi za kuboresha ufugaji samaki pamoja na ukulima wa
mwani. Wizara ilitoa mafunzo ya
uhamasishaji juu ya ufugaji bora wa samaki kwa wananchi 1,472. Aidha, Wizara
ilitoa mafunzo kwa wasimamizi wa vituo vya kuzalisha mbegu bora ya samaki aina
ya perege katika Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga.
Jumla ya wananchi 153 walinufaika na mafunzo hayo.
Mheshimiwa Spika,
43. Katika kuendeleza kilimo cha
Mwani, katika kipindi cha 2004/2005, Wizara itatoa mafunzo kwa wakulima wa
mwani 70.
Udhibiti wa Ubora wa Mazao
na Masoko
Mheshimiwa Spika,
44. Mwaka 2003/2004, Wizara ilikagua
viwanda 26 vya kusindika mazao ya samaki na meli za uvuvi 25. Washiriki 4,838 kutoka sekta binafsi walipewa
semina kuhusu njia bora za kusindika na kusafirisha mazao ya uvuvi.
Katika mwaka 2004/2005, sampuli 2,842 za minofu zitachukuliwa kuhakiki
ubora, 562 za minofu na maji zitapimwa kuchunguza uchafuzi utokanao na dawa za
kuua wadudu wa mimea. Vile vile, sampuli 2,000 za minofu zitapimwa kudhibiti
uchafuzi utokanao na mionzi viwandani. Kaguzi 16 zitafanyika viwandani kuhakiki
kiwango cha usafi unaokubalika kimataifa.
Pia, Watumishi 40 watapatiwa elimu ya ukaguzi wa mazao ya uvuvi na wadau
1,480 watapata mafunzo ya uzalishaji bora wa mazao ya uvuvi. Vituo vitano vya ukaguzi wa mazao vya Mafia,
Kilwa, Bukoba, Musoma na Mwanza vitaimarishwa na maabara ya Nyegezi
itakamilishwa.
Mheshimiwa Spika,
45. Serikali imeamua kwa mara ya
kwanza kuanzia Juni 2004 kuruhusu kuuza nje ya nchi samaki wa mapezi wa
baharini ili kuinua kipato cha wavuvi wadogo wadogo na pato la Taifa. Uamuzi huu ulifikiwa kutokana na matakwa ya
wananchi wa Ukanda wa Pwani. Mawasiliano
ya kina yalifanywa na wadau kabla ya kufikia uamuzi huu.
Udhibiti wa Uvuvi Bora
Mheshimiwa Spika,
46. Mwaka 2003/2004, doria zilifanyika kwenye
maeneo mbalimbali ambapo watuhumiwa 31na nyavu 2,143 zenye ukubwa tofauti
zilikamatwa na kuharibiwa kwa amri ya Mahakama.
Doria 12 zilifanyika pia kwenye Bahari ya Ndani na
kwenye Ukanda wa Uchumi ambapo 6 zilikuwa ni kwa meli na 6 ni kwa ndege, na
meli tatu zilishikwa kwa tuhuma ya kukiuka masharti ya leseni na kusafirisha
mizigo kinyume na sheria.
Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara itaendesha doria ya siku 12,500 za
kazi ili kudhibiti uvuvi haramu na kuzuia biashara ya magendo. Mtambo maalum wa Kompyuta utanunuliwa kwa
madhumuni ya kuratibu mwenendo wa meli zinazovua kwenye Ukanda wa uchumi wa
Bahari.
Elimu kwa Umma
Mheshimiwa Spika,
47. Mwaka 2003/2004, Wizara ilitoa
elimu kwa umma kuhusu uvuvi bora kwa kurusha vipindi 160 vya redio na 10 vya
televisheni. Ukusanyaji wa takwimu
uliimarishwa kwa kuwapa masomo ya muda mfupi watumishi 86 na kuongeza vitendea
kazi.
Mwaka 2004/2005, Wizara itatoa elimu kuhusu uvuvi bora kwa umma kwa
kurusha hewani vipindi 138 vya redio na 10 vya televisheni. Sensa ya wavuvi na
zana itafanyika kwenye Ukanda wa Pwani na Maziwa Makubwa pamoja na kutoa
mafunzo kwa wakusanya takwimu 60 ili kuimarisha matumizi endelevu ya
rasilimali.
Taasisi ya Hifadhi za
Bahari na Maeneo Tengefu
Mheshimiwa Spika,
48. Mwaka 2003/2004, Wizara yangu kwa
kushirikiana na Benki ya Dunia ilikamilisha upembuzi yakinifu kuona jinsi gani
Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu, pamoja na rasilimali za Bahari na mwambao
zinavyoweza kuchangia katika juhudi za kuondoa umaskini. Matokeo ya upembuzi huo ni utayarishaji wa mpango
ambao utahusika na usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari na mwambao.
Mpango huu vile vile utahusisha sehemu ya Tanzania Visiwani (
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itakamilisha
utayarishaji wa Mpango wa mchakato wa muda mrefu (Long Term Strategic Plan).
Aidha, Wizara itakamilisha utayarishaji wa Mkakati wa usimamizi wa fukwe za
bahari na visiwa vidogo, Hifadhi za Bahari ya Ghuba ya Mnazi na maingilio ya
Mto Ruvuma na Maeneo Tengefu ya
Kadhalika, Wizara itakamilisha Kanuni za
kutekeleza Sheria ya Hifadhi za Bahari Na. 29 ya 1994 katika Hifadhi za Bahari
ya Mafia na Ghuba ya Mnazi.
Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi
Mheshimiwa Spika,
49. Utafiti wa Uvuvi umekuwa
ukifanyika kwa lengo la kubaini wingi wa rasilimali na kutoa ushauri kuhusu
matumizi endelevu.
Katika mwaka 2003/2004, Taasisi ilifanya utafiti wa Kamba katika maeneo
ya Pwani ya Dar es Salaam, Lindi na Mtwara ili kubaini wingi wa samaki katika
maeneo hayo. Kutokana na utafiti huo
msimu wa uvuvi wa kamba ulipangwa kuanza rasmi tarehe 01 Aprili 2004 na
utaishia Septemba 2004 badala ya Machi - Novemba ya kila mwaka.
Mheshimiwa Spika,
50. Samaki “kisukuku” anayesadikika
kuishi miaka takribani milioni 60 iliyopita alipatikana kwa mara ya kwanza
kwenye maji ya
Mheshimiwa Spika,
51. Katika mwaka 2004/2005, ujenzi wa
Makao Makuu ya Taasisi na Kituo cha Utafiti cha
Mheshimiwa Spika,
52. Utalii ni sekta ambayo inaweza
kuchangia ukuaji wa kasi wa pato la taifa.
Katika kutekeleza majukumu yake, sekta hii itakamilisha maandalizi ya
utekelezaji wa Sera ya Utalii na pia itatilia mkazo kukuza na kuimarisha utalii
wa ndani.
Mheshimiwa Spika,
53. Mwaka 2003/2004, biashara ya
utalii ulimwenguni iliathiriwa na vita vya
Watalii wa ndani waliongezeka kutoka 270,934 mwaka 2002 hadi 297,077
mwaka 2003, ikiwa ni ongezeko la asilimia 10.
Katika kipindi cha 2004/2005, lengo ni kupokea watalii 607,000 kutoka
nje ya nchi, watakaoliingizia Taifa Dola za Kimarekani milioni 750.
Uendelezaji
Utalii
Mheshimiwa
Spika,
54. Katika
mwaka 2003/2004, Wizara ilibaini na kutathmini vivutio na maeneo ya uendelezaji
utalii katika mikoa ya Singida, Mtwara, Mwanza na Mara. Aidha, taarifa na picha za vivutio mbalimbali
katika mikoa hiyo ziliandaliwa.
Katika kipindi
cha 2004/2005, Wizara itafanya semina za uhamasishaji katika mikoa ya Singida,
Lindi na Mtwara na kuandaa taarifa na picha za vivutio vya utalii katika mikoa
ya Mwanza, Kagera na Mara.
Mheshimiwa
Spika,
55. Katika mwaka 2003/2004, Wizara
ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa Amani kupitia Utalii uliohudhuriwa na washiriki
350. Vile vile, Wizara ilishiriki kwenye mikutano ya Shirika la Utalii ya nchi
za Jumuiya ya Madola na “Africa Travel Association” iliyofanyika
Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara itakuwa mwenyeji wa semina ya
Shirika la Utalii Duniani kuhusu Maendeleo ya
Utalii na Kupunguza Umaskini (Regional Seminar on Tourism Development
and Poverty Alleviation) itakayofanyika Septemba 2004.
Mheshimiwa
Spika,
56. Mwaka
2003/2004, Wizara iliteua Kampuni ya “DCDM
Consulting Group” kutoa ushauri kuhusu masuala ya uwekezaji katika sekta
ya utalii. Randama (Memorandum) ya maeneo yanayofaa kwa uwekezaji na ripoti ya
Mpango wa Kudhamini Wawekezaji wadogo vimekamilika. Vile vile, Wizara
ilitayarisha Kanzidata ya wawekezaji watarajiwa.
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itatayarisha jarida litakalotoa habari za
kina za fursa za uwekezaji katika sekta ya utalii.
Mheshimiwa Spika,
57. Mwaka 2003/2004, Wizara kwa
kushirikiana na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ilikamilisha rasimu ya vigezo
vya kupanga hoteli, migahawa na loji za kitalii katika daraja. Aidha, watumishi
wanne wamepata mafunzo kuhusu taaluma ya kusimamia zoezi
Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara itaendesha semina kwa wadau kuhusu
vigezo hivyo na kuanza kuendesha zoezi
Kuboresha
Takwimu za Utalii
Mheshimiwa
Spika,
58. Mwaka 2003/2004, Wizara ilikamilisha ripoti ya matokeo ya
utafiti wa wageni wanaotoka nje. Vile vile, iliendelea na ukusanyaji wa takwimu
mbalimbali kutoka kwa watoa huduma za kitalii kwa ajili ya kutengeneza mfumo
mpya wa ukusanyaji takwimu unaojulikana
Kwa mwaka 2004/2005, Wizara itaendelea
kukusanya takwimu za watoa huduma za utalii katika vituo vyote vya maingilio ya
watalii pamoja na kuboresha tovuti.
Bodi ya Utalii
Mheshimiwa Spika,
59. Bodi imekuwa na jukumu la
kutangaza utalii kwa kushirikiana na sekta binafsi ili kuharakisha ukuaji wa
sekta ya utalii.
Katika mwaka 2003/2004, Bodi
ilifanya ziara 22 za kutangaza vivutio vya
utalii ndani na nje ya nchi. Vile vile, ilichapisha nakala 75,000 za majarida na 150,000
za vipeperushi.
Mwaka 2004/2005, Bodi itaendelea kutafuta masoko mapya ya watalii hasa
kutoka Bara la
Mheshimiwa Spika,
60. Wakala unatoa mafunzo ya Cheti
katika fani ya utalii na hoteli.
Mwaka 2003/2004, Wizara
ilipata milki ya viwanja viwili vilivyopo Mtaa wa Shaaban Robert Jijini Dar es
Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Utalii kitakachotoa mafunzo katika ngazi
ya Stashahada. Aidha, Serikali imesaini Mkataba wa Ushirikiano na Serikali ya
Ufaransa kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho ambacho kitatoa elimu ya ngazi ya
juu zaidi.
Katika kipindi cha 2004/2005,
Wizara inatarajia kuanza ujenzi huo utakaogharimu Shilingi bilioni tano. Chuo
kitakapokamilika kitakuwa na uwezo wa kutoa wahitimu wa ngazi ya usimamizi
katika fani ya hoteli ili kupunguza waajiriwa wageni katika hoteli nyingi hapa
nchini.
SEKTA NDOGO YA
MAMBO YA KALE
Mheshimiwa Spika,
61. Sekta ya Mambo ya Kale ina jukumu
la kulinda, kutafiti na kuhifadhi urithi wa Mambo ya Kale. Utekelezaji wa jukumu hili umezingatia mwono
na wito wa Sera ya Utamaduni ya mwaka 1997, Sheria ya Mambo ya Kale ya mwaka
1964 na marekebisho yake ya 1979.
Kutokana na Sekta ya Mambo ya Kale kutokuwa na Sera yake, katika mwaka
2004/2005 Wizara yangu itaandaa Sera ya Mambo ya Kale.
Utafiti wa Mambo ya Kale
Mheshimiwa Spika,
62. Mwaka
2003/2004, Wizara iliendelea kufanya utafiti wa akiolojia huko Kinole na Kola
Hill, Mkoani Morogoro. Aidha, Wizara iliratibu na kusimamia utafiti wa
akiolojia huko Ngorongoro katika Bonde la Olduvai, eneo la Laitoli, Engaruka,
Ziwa Eyasi, Hifadhi ya Taifa Serengeti na Ziwa Natron.
Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara itafanya utafiti wa kuboresha
historia ya maeneo ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara. Aidha, Wizara itakamilisha
mpango wa uhifadhi endelevu wa mji mkongwe wa Bagamoyo na kuanza kuboresha
baadhi ya vivutio vilivyoko kwenye njia ya kati ya utumwa kutoka Ujiji hadi
Bagamoyo.
Uhifadhi na Uendelezaji wa
Vituo vya Mambo ya Kale
Mheshimiwa Spika,
63. Katika mwaka 2003/2004, Wizara
ilikamilisha ujenzi wa vituo vya kumbukumbu na habari vya Isimila Mkoani Iringa
na Kolo Mkoani
Katika mwaka 2004/2005, Wizara itaendelea na ujenzi wa vituo vya
kumbukumbu na taarifa vya Ujiji, Mkoani Kigoma na Kaole, Mkoani Pwani.
Uhifadhi wa Eneo la Kilwa
Kisiwani
Mheshimiwa Spika,
64. Katika mwaka 2003/2004, Wizara
ilikamilisha ukarabati wa nyumba ya Kijerumani, uimarishaji wa gofu la Msikiti
Mkuu na jengo la Kireno huko Kilwa Kisiwani.
Aidha, Wizara ilikamilisha ujenzi wa gati, kuweka umeme wa mionzi ya jua
na mawasiliano ya redio ya upepo.
Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara itafanya tafiti za kiakiolojia,
historia, usanifu majengo, elimu jamii na kuandaa mpango wa uendeshaji wa Kilwa
Kisiwani.
Uhifadhi wa Mji wa
Kihistoria, Bagamoyo
Mheshimiwa Spika,
65. Katika mwaka 2003/2004, Wizara iliingia
mkataba na serikali ya
SHIRIKA LA
MAKUMBUSHO YA TAIFA
Mheshimiwa Spika,
66. Shirika linatekeleza jukumu la
kukusanya, kuhifadhi na kutafiti vitu vyote vya urithi wa kihistoria,
kiutamaduni, kisayansi na kiteknolojia. Taarifa za urithi huo huhifadhiwa na
kutumika kuelimisha Umma.
Mheshimiwa Spika,
67. Katika mwaka 2003/2004, Shirika lilifanya
uhamasishaji wa jamii ili zihifadhi na kuuenzi utamaduni wao. Jamii ya Wamwera
ilihamasishwa na kufanya tamasha la Siku ya Utamaduni wa Mtanzania katika
Kijiji cha Makumbusho. Aidha, katika mwaka 2003/2004, Shirika liliendelea na
maandalizi ya ujenzi wa Jumba la Utamaduni kwa kuwashirikisha wadau ambapo
warsha mbili zilifanyika kupata maoni
Katika kipindi cha 2004/2005, Shirika litaendelea
na Mpango wa maandalizi ya ujenzi wa jumba la utamaduni na kutafuta wafadhili
wa ujenzi wa jumba
Mheshimiwa Spika,
68. Mwaka 2003/2004, Shirika lilianza
kufanya utafiti wa akiolojia wilaya ya Iringa na utafiti wa Viumbe Bahari huko
Kaole, Wilayani Bagamoyo.
Katika mwaka 2004/2005, Shirika litaendeleza utafiti wa akiolojia katika
Wilaya ya Iringa na utafiti wa viumbe bahari katika Wilayani Mafia.
UTAWALA NA
UTUMISHI
Maendeleo ya Watumishi na Mafunzo
Mheshimiwa Spika,
69. Katika
kipindi cha 2003/2004, Wizara ilikuwa na watumishi 3,484. Pamoja na idadi hiyo, bado kuna upungufu wa
watumishi. Matarajio yalikuwa ni kuajiri watumishi 166 lakini watumishi
walioajiriwa katika ajira mbadala ni 20.
Katika Mwaka 2004/2005, Wizara inatarajia
kuajiri watumishi wapya 152.
Mheshimiwa Spika,
70. Katika
mwaka wa fedha 2003/2004, Wizara ilitegemea kuwapandisha cheo watumishi 286 wa
kada mbalimbali. Hadi mwezi Aprili 2004,
watumishi 150 walikuwa wamepandishwa cheo. Mapendekezo mengine yako Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.
Katika mwaka
2004/2005, Wizara inatarajia kuwapandisha cheo watumishi 326.
Mheshimiwa Spika,
71. Jumla ya watumishi 323 walipatiwa mafunzo ya
taaluma mbalimbali ya muda mfupi na mrefu ndani na nje ya nchi katika mwaka
2003/2004. Aidha, katika kuendana na mabadiliko ya teknolojia na utandawazi
Wizara imefanya zoezi la kubaini mahitaji ya mafunzo kwa watumishi na kuandaa
Mpango wa Mafunzo.
Katika mwaka wa fedha 2004/2005, Wizara
itaanza kutekeleza Mpango wa Mafunzo.
Ustawi wa Watumishi
Mheshimiwa Spika,
72. Katika kuboresha Ustawi wa
Watumishi Wizara imeingia Mkataba na Benki mbalimbali unaowawezesha watumishi
kukopa fedha. Hata hivyo, tatizo lililojitokeza ni riba kubwa inayotozwa kwa
mikopo. Wizara pia ina mipango ya kukabiliana na janga la ukimwi.
Vyuo vya Wizara
Mheshimiwa Spika,
73. Mwaka 2003/2004, Wizara
iliendelea kuboresha vyuo kwa kukarabati majengo na kuboresha mitaala pamoja na
kuvipatia vifaa vya kufundishia ili vilingane na mahitaji ya soko.
Aidha, hatua mbalimbali zilichukuliwa na vyuo ili vipate usajili wa
kudumu kutoka Baraza la Taifa la Usajili wa Vyuo vya Elimu ya Ufundi. Chuo cha
Wanyamapori Mweka ambacho kilithibitishwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa
kituo cha mafunzo bora ‘Centre of Excellence’ katika fani ya wanyamapori,
kinatarajia kupanua soko
Chuo cha Uvuvi Mbegani kimefikia katika hatua za mwisho za kupata
usajili wa awali wa Baraza la Taifa la Usajili wa Vyuo vya Elimu ya Ufundi.
Pamoja na mafunzo ya kawaida, lengo la Wizara ni kuinua hadhi ya Chuo hiki ili
kiwe taasisi ya kuendeleza shughuli za uvuvi katika Ukanda wa Bahari (Fisheries
Development Centre)
Mkataba wa Huduma kwa
Mteja,
Mheshimiwa Spika,
74. Katika kutekeleza Mkataba wa
Huduma kwa Mteja ambao ulizinduliwa mwaka juzi, kila Idara imeandaa mkataba
wake wa jinsi ya kuwahudumia wateja kwa ufanisi. Katika mwaka 2004/2005 Wizara
itaendelea kutekeleza mkataba huo. Aidha, Taasisi na Mashirika yaliyo chini wa
Wizara yametakiwa kuandaa mikataba ya Huduma kwa wateja wao.
Utawala Bora
Mheshimiwa Spika,
75. Mwaka
2003/2004, Wizara iliandaa mafunzo ya utawala bora kwa viongozi wa vyuo,
taasisi, mashirika na wakala wa serikali.
Wakuu wa vyuo na Maafisa Maliasili wa Mikoa walipata mafunzo hayo
yaliyolenga kubaini namna na kuzuia vitendo vya rushwa na kuimarisha utendaji
unaozingatia misingi ya utawala bora. Kila Taasisi, Mashirika na Wakala
wameagizwa kuwa na mipango ya kupambana na rushwa na kuimarisha utawala bora
katika maeneo
Katika mwaka 2004/2005, Wizara
itaendelea kutoa mafunzo ya utawala bora kwa watumishi katika ngazi mbalimbali.
Kurekebisha Mashirika ya Umma
Mheshimiwa Spika,
76. Hadi
Aprili 2004, Mashirika 27 kati ya 33 yaliyokuwa chini ya Wizara yalikuwa
yamerekebishwa au kubinafsishwa. Mashirika 19 yamesaini
mikataba ya mauzo na 8 yamesaini makubaliano ya awali. Kati ya Mashirika 6
yaliyobaki, 4 yamefilisiwa, moja shughuli zake zimefungwa na moja bado
halijafanyiwa marekebisho.
Katika kipindi cha 2004/2005,
Wizara itaendeleza urekebishaji wa mashirika yaliyosalia pamoja na kufuatilia
maendeleo ya uendeshaji kwa yale yaliyorekebishwa.
MWISHO
Mheshimiwa Spika,
77. Napenda kuwashukuru
Waheshimiwa Wabunge, Wananchi na Wadau mbalimbali kwa kushirikiana na Wizara
yangu katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu yake.
Aidha, natoa shukurani kwa washirika wetu wa
maendeleo wafuatao kwa michango yao ya kifedha na kitaalamu kama ifuatavyo:
Norway, Denmark, Finland, Marekani, Sweden, Japan, Ufaransa, Ujerumani,
Ubelgiji, Uingereza, Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU), ADB, AWF, FAO, FZS, GTZ,
IUCN, KfW, Trade Aid, MIGA, AFRICARE, UNESCO, UNDP, World Bank, WWF, ICCROM na
mengineyo.
Mheshimiwa Spika,
78. Naomba kutoa shukurani
zangu za dhati kwa Katibu Mkuu, Bw. Salmon Odunga, Wakurugenzi na wafanyakazi
wote wa Wizara na Taasisi zake, kwa ushirikiano walionipa na kuiwezesha Wizara
yangu kutekeleza majukumu yake katika mwaka 2003/2004.
Mheshimiwa Spika,
79. Ili Wizara yangu iweze kutekeleza majukumu na
malengo yake katika kipindi cha 2004/2005, naomba Bunge lako Tukufu liidhinishe
makadirio ya matumizi ya Shilingi
47,123,892,100. Kati ya fedha hizo, Shilingi
18,970,499,400 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Shilingi 28,153,392,700 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida.
Mheshimiwa Spika,
80. Naomba kutoa hoja.