HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA
MHESHIMIWA ANNA MARGARETH ABDALLAH, MBUNGE,
KUHUSU MAKADIRIO YA
MATUMIZI YA FEDHA
KWA MWAKA 2005/2006
UTANGULIZI
1.
Mheshimiwa
Spika, kufuatia taarifa
iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge
ya Huduma za Jamii iliyochambua bajeti ya Wizara ya Afya, naomba kutoa hoja
kwamba sasa Bunge lako likubali kupokea na kujadili taarifa ya mafanikio ya
utekelezaji wa kazi za Wizara ya Afya kwa mwaka 2004/2005 na malengo ya bajeti
ya mwaka 2005/2006. Aidha, naliomba
Bunge lako Tukufu likubali kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Mpango wa Maendeleo kwa ajili ya Wizara ya Afya kwa
mwaka 2005/2006.
2.
Mheshimiwa
Spika, awali ya yote napenda kuchukua
nafasi hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
3. Mheshimiwa Spika, nawapongeza kwa dhati Mheshimiwa Dr. Abdallah Omari Kigoda (Mb.), Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Ubinafsishaji na Mheshimiwa Basil Pesambili
Mramba, (Mb.), Waziri wa Fedha kwa hotuba zao nzuri za Hali ya Uchumi Nchini,
Mipango ya Maendeleo na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2005/2006. Aidha, ninampongeza Mheshimiwa Frederick
Tluway Sumaye, Mbunge wa Hanang, Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa
4.
Mheshimiwa
Spika, napenda kuungana na Waheshimiwa Wabunge wote
walionitangulia kusema, kuwapongeza Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mbunge wa
Chalinze, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa kuchaguliwa na
Chama cha Mapinduzi kuwa Mgombea Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
5. Mheshimiwa Spika, tangu mwaka jana niliposimama hapa
kuwasilisha bajeti yangu baadhi ya Wabunge wenzetu wamefariki dunia. Natoa rambirambi kwa
familia za wafiwa na namwomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira kwa yote
yaliyowafika. Waheshimiwa Wabunge
waliofariki dunia ni Mheshimiwa Captain (Mstaafu) Theodorus James Kasapira,
aliyekuwa Mbunge wa Ulanga Mashariki, Mheshimiwa Frank Michael Musati aliyekuwa Mbunge wa Kasulu
Mashariki. Mheshimiwa Balozi Ahmed
Hassani Diria,
aliyekuwa Mbunge wa Raha Leo na Mheshimiwa Abu-Towegale Kiwanga,
aliyekuwa Mbunge wa Kilombero. Tukio la ghafla la kifo cha mwenzetu Mheshimiwa
Magreth Bwana, aliyekuwa Mbunge wa CCM Viti Maalum
limetutia simanzi sio tu sisi Wabunge bali hata Watanzania wote hasa wananchi
wa Sumbawanga. Kwa kuwa hakina mwenyewe
lililobaki kwetu sote ni kumwomba Mwenyezi Mungu
aziweke roho za marehemu mahali pema peoponi.
Amina.
6. Mheshimiwa Spika, napenda kuishukuru kwa
dhati Kamati ya Huduma za Jamii ya Bunge lako Tukufu, chini ya Mwenyekiti wake
Mheshimiwa Omar Shaban Kwaangw’, Mbunge wa Babati Mashariki kwa ushauri
walioutoa ambao umeendelea kuboresha huduma za Sekta ya Afya pamoja na
matayarisho ya bajeti ya Wizara yangu ambayo naiwasilisha mbele ya Bunge lako
tukufu. Kwa kuwa hiki ni
kikao cha mwisho cha Bunge la Serikali ya Awamu ya Tatu, ninawatakia wajumbe
wote wa kamati hii kila la kheri katika uchaguzi ujao na ni matumaini yangu
kuwa watachaguliwa tena kurudi Bungeni kutokana na kazi nzuri waliyoifanya.
7.
Mheshimiwa
Spika, hotuba yangu imegawanyika katika
maeneo
yafuatayo:-
·
Muhtasari wa
mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tatu kuanzia Novemba 1995 hadi 2005,
·
Muhtasari wa
utekelezaji wa Serikali kuhusu Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2000-2005,
·
Taarifa ya
utekelezaji wa majukumu pamoja na mipango ya maendeleo iliyoidhinishwa katika
bajeti ya mwaka 2004/2005,
·
Kuelezea mipango,
majukumu na malengo ya bajeti ya Wizara,
kwa mwaka 2005/2006,
·
Maombi ya fedha kwa mwaka 2005/06.
MUHTASARI
WA MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA TATU NOVEMBA 1995 HADI SASA
8.
Mheshimiwa Spika, katika
miaka 10 ya Serikali ya Awamu ya Tatu,
Wizara imefanikiwa kutekeleza Mabadiliko katika Sekta ya Afya kwa lengo la
kuinua kiwango cha ubora wa huduma za afya zinazotolewa kwa wananchi na
kuongeza kiwango cha uwajibikaji kwa wasimamizi na watoaji wa huduma hizo. Mabadiliko hayo yameleta mafanikio katika nyanja mbalimbali za utoaji huduma za afya zikiwemo kinga,
tiba, mafunzo na utawala. Aidha, katika kipindi cha miaka 10 iliyopita toka
1995/1996 hadi 2004/2005, Wizara imefanya mapitio ya Sera ya Afya na kuainisha marekebisho ya sheria, miongozo, kanuni,
taratibu na viwango vya ubora wa huduma mbalimbali.
Huduma
za Kinga
9. Mheshimiwa
Spika, Wizara iliimarisha na kuboresha huduma za kinga. Matokeo ya uimarishaji huo ni
Magonjwa
ya watoto yanayozuilika kwa chanjo ambayo ni polio,
homa ya ini, kifua kikuu/dondakoo, surua na pepopunda yamepungua. Hali hii imetokana na kuimarika kwa huduma za chanjo
kulikoongezeka kutoka asilimia 30 mwaka 1995 na kufikia wastani wa zaidi ya
asilimia 90 mwaka 2004. Aidha ugonjwa wa polio umedhibitiwa kiasi kwamba hajapatikana mgonjwa wa
polio tangu mwaka 1996. Sasa tunasubiri
cheti cha uthibitisho kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) ili
10. Mheshimiwa
Spika, kutokana na uongozi mzuri wa
Serikali ya Awamu ya Tatu uliopelekea kuimarika kwa uchumi, Serikali kuanzia
miaka 3 iliyopita inagharamia kwa asilimia 100 ununuzi wa chanjo za Homa ya
Ini, Polio na Pepopunda hivyo kuondokana na utegemezi wa wahisani uliokuwepo
kwa kipindi kirefu cha nyuma.
11. Mheshimiwa Spika, huduma za afya ya uzazi na
mtoto zimeendelea kuboreshwa na kutolewa bila malipo. Idadi ya wanawake
wanaotumia huduma za kliniki, iliongezeka kutoka asilimia 70 mwaka 1995 hadi
asilimia 90 mwaka 2005. Idadi ya kinamama wanaotumia huduma ya uzazi wa mpango nayo iliongezeka kutoka asilimia 12 mwaka 1995
hadi 22 mwaka 2005. Vile vile mafunzo ya
kuzuia ukeketaji kwa wanawake yalifanyika kwa
viongozi 1,227 wa ngazi ya Vijiji, Kata na Tarafa nchini na hivyo
kuongeza uelewa kwa viongozi wa jamii juu ya madhara ya mila hii mbaya na kuhamasisha jamii kuachana
na mila hiyo.
12. Mheshimwa
Spika, Wizara imefanikiwa kukabiliana
na magonjwa ya milipuko hasa ugonjwa wa Kipindupindu
ambao ulipungua kutoka wagonjwa 12,266 mwaka 1999 hadi wagonjwa 6,254 mwaka
2004. Ugonjwa wa Tauni ulipungua kutoka wagonjwa 831 na vifo 74 mwaka 1995 hadi kufikia wagonjwa 4 bila kifo mwaka 2004. Katika
Halmashauri ya Lushoto, vijiji vilivyoathirika na ugonjwa huu vimepungua kutoka
47 mwaka 1995 hadi kufikia vijiji 5 mwaka 2004.
Wizara
imeanzisha Kitengo cha Kukabiliana na Dharura kwa
kushirikiana na Idara ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu ili kukabiliana na matukio
ya ajali na magonjwa ya milipuko
Huduma za Tiba
13. Mheshimiwa
Spika, Wizara imeendelea kuhakikisha
kuwa dawa muhimu na vifaa tiba vinawafikia wananchi
katika ngazi zote za utoaji wa huduma za afya. Upatikanaji wa
dawa na vifaa tiba umetokana na uamuzi wa Serikali yetu kutoa kipaumbele kwa
huduma za afya na hivyo kuendelea kuiongezea Wizara yangu bajeti. Kiasi cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa
na vifaa kimeongezeka kutoka shilingi bilioni 10 kwa mwaka 2000 hadi kufikia
shilingi bilioni 30
kwa mwaka 2004/2005.
Aidha,
Wizara imeanzisha utaratibu ambapo kituo cha kutolea huduma za afya huagiza
dawa kulingana na mahitaji halisi (indent system) kwa
kuzingatia mgao wa fedha na mzigo wa magonjwa (burden of disease). Hadi sasa, zahanati 1,498 na
vituo vya afya 179 zinapatiwa dawa kwa kufuata mfumo huo. Mfumo
huu unasaidia kupunguza matumizi mabaya ya rasilimali.
14. Mheshimiwa Spika, Hospitali 98 za
Wilaya, Mikoa, Rufaa na Maalum zilipatiwa vifaa na mashine mbalimbali
zikijumuisha eksirei, Hadubini
(microscope) na mashine za
“Ultra Sound”, kulingana na mahitaji
yao. Vifaa na mashine hizi zimetolewa na
mpango wa ORET. ORET pia ilitoa magari maalum katika kanda zote kwa ajili ya
matengenezo ya vifaa hivyo. Serikali pia
ilinunua vifaa vifuatavyo “CT-Scan” kwa ajili ya hospitali za rufaa, mashine moja aina ya “Cobalt 60”,
mashine moja ya eksirei inayohamishika (Mobile X-Ray unit), “Gama cameras”, tatu na “Intracavity Radio
therapy machine” moja, kwa ajili ya
Hospitali ya
15. Mheshimiwa
Spika, kutokana na mabadiliko yanayoendelea katika
huduma za afya, hadi kufikia mwaka 2004, hospitali 184, vituo vya afya
298, zahanati 992 na nyumba za waganga
583 zimefanyiwa ukarabati. Jumla ya
zahanati 790, vituo vya afya 90, hospitali 39 na
nyumba za waganga 826 mpya zilijengwa nchini kote. Aidha, hospitali zimeongezeka kutoka 194
mwaka 1995 hadi 233 mwaka 2004, vituo vya afya kutoka 343 mwaka 1995 hadi 433
mwaka 2004 na zahanati zimeongezeka kutoka 3,832 mwaka 1995 hadi 4,622 mwaka
2004.
16. Mheshimiwa
Spika, Serikali kwa
kutambua mchango unaotolewa na Waganga wa Tiba za Jadi imetunga Sheria namba 23
ya mwaka 2002 itakayosimamia na kuratibu shughuli zote za Tiba Asili
nchini. Aidha, Baraza la kusimamia
maadili na mienendo ya Waganga wa Tiba za Jadi
limekwishaundwa.
Huduma
ya Mafunzo
17. Mheshimiwa
Spika, Wizara inaendelea kutoa
mafunzo kwa wataalam mbalimbali ili kupata wataalamu
wa kutosha. Wataalam wa tiba waliohitimu kwa mwaka waliongezeka kama
ifuatavyo:- Madaktari wa Uzamili na Shahada mwaka 1995 waliohitimu 83 na mwaka 2004 walihitimu 212, Madaktari Wasaidizi mwaka 1995 walihitimu 118
na mwaka 2004 walihitimu 134, Madaktari
wa Meno hapakuwa na mhitimu mwaka 1995 na
mwaka 2004 wahitimu 12. Wauguzi
wenye Shahada mwaka 1995 wahitimu 3 na mwaka 2004 wahitimu 40, Wauguzi waliopata Stashahada mwaka 1995
walihitimu 205 na mwaka 2004 walihitimu 457 na Wauguzi waliopata Cheti
waliongezeka kutoka 989 mwaka 1995 hadi 1,162 mwaka 2004. Hata hivyo, ongezeko hili
bado halijakidhi mahitaji halisi ya wataalamu hao nchini mwetu. Katika kuendelea kuimarisha huduma za
mafunzo vituo 43 vya mafunzo ya afya viliboreshwa kwa
kufanyiwa ukarabati, na kupatiwa vifaa vya kufundishia.
18. Mheshimiwa
Spika, idadi ya wanafunzi wanaosomea
udaktari katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi za Afya Muhimbili imeongezeka maradufu. Chuo hicho kimeanzisha shahada mpya za uuguzi
na Afya ya
Mazingira (Bsc-Nursing and Bsc-Environmental Health). Shahada ya Uzamili ya Afya ya Jamii (Masters
in Public Health) imeanzishwa katika vyuo vya Muhimbili na
Tumaini University (KCMC). Aidha, Chuo
Kikuu cha Agha Khan kimeanzisha masomo ya Shahada ya
Uuguzi. Vyuo vipya vilivyoanzishwa vina
uwezo wa kutoa shahada ya Udaktari. Vyuo hivyo ni Tumaini (KCMC), Mtakatifu Augustino
(Bugando, Mwanza), Kumbukumbu ya Hurbert Kairuki (Mikocheni,
·
Madaktari –
Muhimbili 103, KCMC 11, Kairuki 12, IMTU 5,
·
Madaktari wa Meno
– Muhimbili 13,
·
Wauguzi –
Muhimbili 19.
·
Maafisa Afya –
Muhimbili 19.
·
Wafamasia –
Muhimbili 32.
Napenda
kuliarifu Bunge
lako tukufu kuwa kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu, tumepata
daktari mmoja katika fani ya maumbile na mimba tete (Anatomy and Embryology)
kutoka Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi ya Afya Muhimbili.
Hospitali
ya KCMC imeanzisha kituo cha ushauri nasaha cha ANGAZA na hospitali hiyo inashirikiana na chuo kikuu cha Tumaini
katika kutoa mafunzo katika taaluma mbalimbali za afya katika hospitali hiyo.
Aidha, huduma za upasuaji wa moyo zimeanza kutolewa
katika hospitali hii.
Huduma za Utawala na
Utumishi
19. Mheshimiwa Spika, Wizara imefanikiwa kuwapandisha vyeo watumishi
mbalimbali wa kada za afya 32,994 ambao ni sawa na asilimia
94 ya lengo la kuwapandisha vyeo watumishi 35,100.
Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya
20. Mheshimiwa Spika, mafanikio ya Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya ni
pamoja na:-
·
Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali ulinunua mtambo wa uchunguzi wa “Deoxyribo
Nucleic Acid” (DNA) na vifaa vingine vya kisasa na kufungua maabara mpya
ya kwanza ya kanda jijini Mwanza.
·
Katika kuboresha
utendaji Serikali iliunganisha iliyokuwa Bodi ya Madawa na
Tume ya Kudhibiti Vyakula na kuunda Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) chini ya
sheria No. 1 ya mwaka 2003.
·
Aidha, Mamlaka
imejenga maabara mpya ya kisasa yenye uwezo wa kupima
ubora wa vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba na kuanzisha Mpango wa kuhakiki
ubora wa dawa, vyakula na vipodozi (Quality Assurance program).
·
Taasisi ya
Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu imefanya na inaendelea
kufanya tafiti nyingi za kuimarisha huduma za afya ikiwa ni pamoja na usugu wa
vimelea vya malaria, utokomezaji wa magonjwa ya matende, mabusha na usubi.
MUHTASARI
KUHUSU UTEKELEZAJI WA SERIKALI KUHUSU ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2000-2005
21. Mheshimiwa
Spika, Wizara yangu katika kutekeleza
Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2000 mpaka 2005 Ibara ya 57
imefanikiwa kutekeleza yafuatayo:
·
Madaraka, majukumu na rasilimali zaidi za afya
zilipelekwa kwa jamii na hivyo kufanikisha uhamasishaji wa uanzishaji wa Bodi
za Huduma za Afya za Halmashauri 113 na Kamati za Vituo vya kutolea huduma za
afya. Bodi hizi zinasimamia utoaji wa
huduma bora za afya pamoja na kusimamia matumizi ya fedha ya uchangiaji wa
huduma za afya. Hadi kufikia Aprili 2005,
Halmashauri 61 zilikwisha zindua Bodi za Huduma za Afya na 51 kati ya
hizo zilishazindua Mfuko wa Afya ya Jamii.
Halmashauri 52 zilizobaki ziko katika hatua mbalimbali za kuzindua Bodi
na Mfuko wa Afya ya Jamii. Mfuko wa Afya ya Jamii umewasaidia wananchi
kupunguza matatizo ya uhaba wa dawa na vifaa, ukarabati wa majengo na pia umeziwezesha baadhi ya Halmashauri
kama vile Mbinga kuajiri wataalamu wanaotoa huduma za Afya. Wanachama hupatiwa kadi na hupata matibabu
bila kutoa fedha taslimu wakati wa kupata matibabu na hivyo kuziba mianya ya
rushwa.
·
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ambao unatoa huduma za
matibabu kwa watumishi wa umma na wategemezi wao ulianzishwa na umeonyesha
mafanikio makubwa. Walengwa wameongezeka
kutoka 691,774 mwaka 2002 hadi 1,141,637 mwaka 2004. Vituo vyote vya
Serikali na 518 vya sekta binafsi vinatoa huduma za matibabu. Aidha,
maduka ya dawa 32 ya sekta binafsi yamesajiliwa kutoa huduma kwa
wanachama. Makusanyo ya mfuko yameongezeka kutoka shilingi milioni 12,546.1
mwaka 2001/2002 hadi shilingi milioni 22,007.7 mwaka 2003/2004. Katika kikao
hiki cha Bunge la Bajeti kinachoendelea, Bunge
lako Tukufu limefanya marekebisho
ya sheria ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya namba 8 ya mwaka 1999 ibara ya 17 na kumpa Waziri mwenye dhamana,
madaraka zaidi ya kuandaa na kuongeza orodha ya huduma ambazo zinazotolewa na
mfuko.
·
Hospitali zimeongezeka kutoka 203 mwaka 2000 hadi 233
mwezi Mei 2005, vituo vya afya vimeongezeka kutoka 367 mwaka 2000 hadi vituo
433 Mei, 2005 na zahanati zimeongezeka kutoka 4,232 mwaka 2000 hadi 4,622 Mei,
2005. Vituo hivi vya huduma vimejumuisha
vile vya Serikali, Mashirika ya dini na binafsi.
·
Kiwango cha
chanjo kimeongezeka na kufikia zaidi ya asilimia 90 ya
lengo. Kwa mlinganisho mafanikio yalikuwa
-
Chanjo za kawaida
DPT- HB ziliongezeka kutoka asilimia 90 mwaka 2000 hadi asilimia 91 mwaka 2004.
-
Chanjo ya
pepopunda TT2+ kwa wanawake wajawazito kutoka asilimia 77 mwaka 2000 hadi
kufikia asilimia 88 mwaka 2004.
-
Chanjo ya polio
kiwango kiliongezeka kutoka asilimia 64 mwaka 2000 hadi asilimia 96 mwaka 2004.
-
Chanjo ya surua
kiwango kiliongezeka kutoka asilimia 78 mwaka 2000 Hadi asilimia 94 mwaka 2004.
·
Katika kuimarisha
huduma za chanjo, majokofu 2,287 ya mafuta ya taa yalibadilishwa na majokofu mapya ya kutumia gesi kwenye vituo vya mikoa 17
na majokofu 125 ya mionzi ya jua yalifungwa katika mikoa 7.
·
Ununuzi na usambazaji wa dawa za uzazi wa mpango nchi nzima
ulifanyika. Pia huduma za mama wajawazito ziliendelea kuboreshwa kwa kutoa vifaa
vya kujifungulia. Aidha Halmashauri 9
zenye kiwango cha juu cha vifo vya akina mama vinavyotokana na uzazi walipewa
magari ya kubebea wagonjwa ili kupunguza tatizo hilo. Halmashauri hizo ni Bariadi, Maswa, Kahama,
Kasulu, Ngara, Karagwe, Manyoni, Igunga na Tarime. Ninazipongeza Halmashauri nyingine
zilizoamua kununua magari ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya kupunguza tatizo la
akina mama wajawazito na wagonjwa wengine wanaohitaji rufaa. Halmashauri hizo ni Geita, Urambo, Korogwe,
Lushoto, Manispaa za Iringa, Tanga, Ilala, Temeke na Kinondoni. Aidha, simu za upepo (redio call) 20
zimenunuliwa na kusambazwa katika Wilaya za Bariadi, Kahama na Maswa ili
kurahisisha mawasiliano.
·
Idadi ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano
waliopata matone ya vitamini A iliongezeka kutoka watoto 1,457,000 mwaka 2000
hadi watoto 5,746,299 mwaka 2005 sawa na ongezeko la asilimia 294.
·
Tatizo la upungufu wa madini joto nchini limepungua
kutoka asilimia 25 ya miaka ya tisini hadi asilimia 7 hivi sasa. Aidha, asilimia 95 ya kaya za
Tanzania sasa wanatumia chumvi yenye madini joto.
·
Katika kupunguza kasi ya maambukizi ya UKIMWI na
kuhakikisha upatikanaji wa damu salama, Serikali ilinunua na kusambaza vipimo
vya damu (HIV Test Kits) 1,100,000 katika hospitali zote zinazotoa damu kwa
wagonjwa nchini. Ushauri nasaha ulitolewa katika vituo zaidi ya 400 vya
Serikali na visivyo vya Serikali. Ununuzi wa mashine za kupimia chembe chembe
za CD4 kwa waathirika ulifanyika na kusambazwa katika hospitali za rufaa, mikoa
na hospitali za Manispaa 3 za Dar es
Salaam.
·
Mpango wa kuzuia maambukizi ya Virusi vya UKIMWI toka kwa
Mama mjamzito kwenda kwa mtoto (PMCT) umeonyesha mafanikio. Baada ya mafanikio ya majaribio ya awali, sasa
Wizara imepanua mpango huu ili uweze kufikia mikoa yote ya Tanzania Bara kwa
awamu. Mpango huu sasa unaendeshwa
sambamba na utoaji wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI (ARVs) kwa wagonjwa
wale wenye sifa za kupewa dawa hizi.
·
Mpango wa kutoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI (ARVs)
umeanza na dawa zinatolewa katika vituo 96 vya hospitali za Serikali, mashirika
ya dini na binafsi. Dawa hizi hutolewa bila malipo. Hadi kufikia Mei 2005
wagonjwa 6,000 wa jinsia zote wakiwemo watoto wananufaika na mpango huu. Aidha,
wagonjwa 44,000 wanatarajiwa kunufaika na mpango huu
ifikapo Desemba 2005.
·
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imefanikiwa kusambaza na kufunga
vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Units) katika hospitali zote za Mikoa na
Wilaya. Hii ilikuwa ni
katika mpango wa awamu ya kwanza ambao ulianza mwaka 2002/2003 na umekamilika
katika mwaka 2004/2005.
·
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kuthamini mchango
mkubwa unaotolewa na hospitali za Mashirika ya Dini na hasa mahali ambapo
hakuna kituo cha kutolea huduma cha Serikali.
Aidha, Wizara imekuwa ikiongeza ruzuku kwa
kitanda kutoka shilingi 7,500/= mwaka 2002/2003 hadi kufikia shilingi 30,000/=
mwaka 2004/2005.
·
Udhibiti wa Uwiano wa magonjwa ya watoto (Integrated
Management of Childhood Illnesses – IMCI)
Wizara
iliendeleza mafunzo kwa watumishi wa afya wa ngazi
zote jinsi ya kutoa matibabu kwa magonjwa yale yanayosababisha vifo zaidi kwa
watoto kwa pamoja. Magonjwa hayo ni Malaria, Kichomi, Kuharisha, Surua, Utapiamlo na upungufu
wa damu. Pia jamii ilihamasishwa
kuzingatia mambo yanayohusu makuzi na maendeleo ya
watoto ikijumuisha kuhamasisha akina mama wakamilishe unyonyeshaji na kuwapa
watoto virutubisho muhimu, kuzuia
maradhi yanayozuilika kwa chanjo,
kuhimiza matumizi ya vyandarua vyenye viuatilifu, kuwapeleka watoto kliniki wapate chanjo na
kuchunguzwa afya zao. Mpango huu na mpango wa Chanjo kwa pamoja umesaidia kupunguza idadi ya
vifo vya watoto wachanga. (Infant Mortality Rate).
·
Dawa za kifua
kikuu na ukoma zilinunuliwa na kusambazwa katika vituo
vya kutolea huduma za afya nchini kwa kipindi chote cha miaka 5 bila
upungufu. Kampeni kuhusu ukoma
ilifanyika katika mikoa 11 na wagonjwa wapatao 23,067
walitambuliwa na kupewa dawa, viatu na viungo bandia. Utafiti wa maambukizi ya kifua kikuu
ulifanyika katika shule za msingi 731 katika mikoa 20 na wanafunzi 110,243
walifanyiwa uchunguzi kati yao wanafunzi 4,617 sawa na asilimia 4.2 walikuwa na
maambukizi na kuanzishiwa matibabu.
·
Wizara iliendelea
kuhamasisha na kuhimiza jamii kuhusu umuhimu wa lishe
bora, usafi wa mazingira na matumizi bora ya vyoo. Aidha, Wizara imeanzisha mashindano ya
utunzaji mazingira kwa Halmashauri zote nchini.
·
Katika
kukabiliana na ugonjwa wa malaria, dawa mpya ya
Sulphadoxine Pyrimithmine (SP) ilianza kutumika kuanzia mwaka 2001 baada ya
Klorokwini kuonyesha usugu mkubwa dhidi ya vimelea vya malaria. Hata hivyo, utafiti umeonyesha kuwa vimelea
vya malaria vimekuwa sugu kwa dawa ya SP kwa asilimia
25. Kwa sasa yanafanyika maandalizi ya
kubadili matibabu ya malaria kutoka dawa ya SP kwenda dawa ya mseto iitwayo
Arthemether/Lumefantrine. Serikali pia
imeanzisha mpango wa Hati punguzo ili kuwawezesha
watoto wenye umri chini ya miaka mitano na mama wajawazito kupata vyandarua
vyenye viuatilifu kwa bei nafuu.
·
Wizara hadi
kufikia mwaka 2004/2005 ilijenga matanuru 56 ya kuteketeza taka zinazozalishwa na hospitali katika hospitali za rufaa, maalumu, mikoa na
wilaya.
·
Wizara imeanzisha
Mfuko wa Pamoja (Basket Fund) ambao umechangia katika kuimarisha huduma
za afya katika ngazi za wilaya. Mfuko umekuwa ukinunua magari mapya kwa ajili
ya kubadilisha magari machakavu kwa Halmashauri. Magari haya yanatumika katika shughuli za
chanjo na huduma nyingine za afya ili ziweze kuwafikia wananchi wote hasa
walioko vijijini.
·
Huduma za tiba ziliendelea kuimarika na yafuatayo
yamefanyika: Kununua na kusambaza
makasha ya dawa (drug kits) kwenye zahanati 2,033 na vituo vya afya 206. Zahanati na Vituo vya Afya vingine vimepewa
dawa kwa kutumia mfumo wa (Indent system) yaani
utaratibu wa kuagiza dawa kulingana na mahitaji halisi kwa kila kituo
kwa kuzingatia mgao wa fedha na mzigo wa mgonjwa (Burden of disease –
BOD). Mpango huu umewezesha Zahanati
1,498 na Vituo vya Afya 179 kununua dawa.
Jumla ya zahanati zote za Serikali pamoja na za Mashirika ya Dini
zilipatiwa makasha ya dawa na zilizonunua kwa mfumo wa ‘indent’ ni 3,531 na vituo vya afya ni 385. Serikali pia ilianzisha utaratibu
unaowawezesha wagonjwa kununua dawa kwa nusu ya bei (Capitalization of Hospital
Pharmacies).
·
Mradi wa Uimarishaji Huduma
Muhimu za Afya (MUHUMA) umekuwa ukitekelezwa katika wilaya mbili za Morogoro
vijijini na Rufiji toka Mwaka 1997 mpaka mwaka 2004 ulipofikia kikomo kama
mradi. Utafiti umeonyesha kuwa kumekuwa
na upunguaji wa kasi ya vifo katika wilaya zote mbili kwa asilimia zaidi ya 55
kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano na asilimia 18 kwa watu wazima.
Kupungua huku kumeziweka wilaya hizo mbili kwenye matumaini ya kufikia moja ya
malengo ya milenia ya Umoja wa Mataifa ya kupunguza kasi ya vifo miongoni mwa
watoto wadogo kwa theluthi mbili ifikapo mwaka 2015. Aidha, uzoefu uliopatikana
katika wilaya hizi utasaidia kupanga mbinu sahihi ya kukabiliana na kupunguza
vifo vya watoto wachanga na watu wote kwa ujumla.
UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA MIPANGO YA MAENDELEO ILIYOIDHINISHWA
KATIKA BAJETI YA MWAKA 2004/2005
22. Mheshimiwa Spika, ifuatayo ni taarifa ya
utekelezaji wa bajeti katika mwaka 2004/2005. Utekelezaji huu umegawanyika
katika sehemu kuu mbili, Miradi ya Maendeleo na Matumizi ya Fedha za Kawaida.
Miradi ya Maendeleo
23. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka
2004/05, Wizara ya Afya ilitengewa kiasi cha shilingi 91,215,753,600/=
kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Jumla ya shilingi 3,552,448,200/= zilitolewa na Serikali ya Tanzania na
shilingi 87, 663, 305,400/= zilitolewa
na wahisani mbalimbali, wakiwemo
wahisani wanaochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya (Health Basket Fund). Fedha hiyo imetumika kutekeleza miradi ifuatayo: -
Ukarabati
wa Hospitali ya Taifa Muhimbili
·
Wizara kwa
kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) inaendelea na ukarabati
mkubwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Ukarabati wa Wodi ya Sewahaji, ujenzi wa tanuru
la kuchomea taka (incinerator) na karakana umekamilika. Pia mashine 10 mpya za
kufulia, moja ya kutakasia vifaa na ya kuchomea taka
hatari zimefungwa na zinafanya kazi. Ukarabati wa jengo la wodi za Kibasila, upasuaji,
eksirei na chumba cha upasuaji wa
akinamama wenye matatizo ya kujifungua ulianza na unaendelea vizuri. Ukarabati wa majengo mengine uko katika hatua
za mwisho ikiwa ni pamoja na nyumba ya kuhifadhia maiti, vibanda vya mitambo ya
umeme na majenereta. Ukarabati wa njia za maji
·
Wizara kwa
kushirikiana na wadau wengine ambao ni Abbott/Axios wametoa msaada uliotumika
kujenga uzio kuzunguka hospitali, kufanya ukarabati mkubwa wa jengo la maabara
(Central Pathology Laboratory) na ujenzi wa jengo jipya la wagonjwa wa nje (OPD). Ujenzi wa uzio na
ukarabati wa maabara umekamilika. Ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD)
lenye vyumba 35 vya matibabu
liko kwenye hatua za mwisho na linatarajiwa kukabidhiwa mwezi
Agosti, 2005. Pia Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na
Taasisi ya Kuzuia Magonjwa ya Marekani (CDC) imekamilisha ujenzi wa jengo jipya
la ushauri nasaha katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na limeanza kutumika.
·
Ujenzi wa jengo la huduma kwa watoto (Paediatric Complex)
uliendelea vizuri. Ujenzi wa Ghorofa ya msingi (basement), Ghorofa ya chini (ground
floor) na Ghorofa ya kwanza (first floor) ulikamilika. Ghorofa ya chini inatumika kwa
wagonjwa waliohamishwa kutoka kwenye wodi zinazofanyiwa ukarabati, vyumba vya
upasuaji, chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) na Maabara ya Kifua Kikuu.
Ukarabati utakapokamilika jengo hili litaendelea kutumika kwa
ajili ya huduma za watoto
Kuimarisha
Hospitali, Taasisi na vyuo vya Afya
Kazi zifuatazo zilifanyika:
·
Ukarabati wa majengo
ya huduma ya wagonjwa wa nje, upasuaji, mfumo wa maji taka katika hospitali ya
·
Michoro kwa ajili ya ujenzi wa hosteli mpya ya madaktari wanafunzi
imekamilika na taratibu za kumpata mjenzi zinaendelea na ujenzi wa chumba cha
wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya umekamilika.
·
Taratibu za
ununuzi wa vifaa vya tiba kwa ajili ya hospitali za
rufaa na maalum zimekamilika. Vifaa
hivyo ni “Oxygen concentrator, Electroencephalograph (EEG) machine, Autoclave
(High pressure steam sterilizer),
Gynaecological beds, Automatic
film processor machine, Mammograph machine,
Electro-Cardiograph (ECG) machine, Mortuary refrigerator (12
bodies), Defibrillator, Cardiac monitor,
Orthopaedic Operating Table, Basic Neuro-Surgical instrument na Basic
Laminectomy instrument set”.
·
Serikali imetoa mchango wake wote (counterpart fund) wa kununulia vifaa vya Taasisi ya
Mifupa ya Muhimbili –MOI.
·
Ujenzi wa jengo la
ofisi za Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Tukuyu ulikamilika
na kukabidhiwa. Kwa sasa ununuzi wa vifaa unaendelea.
·
Ukarabati wa mifumo ya njia za umeme kwenye jengo la ofisi za Huduma
za Mama na Mtoto
·
Ukarabati wa ofisi,
mabweni na madarasa katika vyuo 32 vya afya vilivyo chini ya Wizara umekamilika
kwa asilimia 80. Pia ujenzi wa nyumba za watumishi, maktaba na vyumba vya mazoezi ya
vitendo umefanyika katika vyuo vyote 21 vya uuguzi vya Serikali.
Udhibiti
wa magonjwa ya kuambukiza
24. Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti magonjwa ya kuambukiza mambo
yafuatayo yalifanyika:-
·
Vituo vyote vya huduma za afya vimepata dawa na vifaa kwa ajili ya kukinga na kutibu magonjwa ya zinaa –
STIs.
·
Serikali
iliendelea kutoa mchango wake kwa ajili ya kugomboa na
kusambaza dawa za ugonjwa wa Kifua Kikuu na Ukoma.
25. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea na
juhudi za kuelimisha na kuhamasisha wananchi na jamii kuhusu mabadiliko
yanayoendelea katika Sekta ya Afya.
Katika uelimishaji huu, Halmashauri ambazo ni
kitovu cha utekelezaji wa mabadiliko haya, zimehamasishwa kukamilisha
uanzishwaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Uelimishaji na uhamasishaji huo umekwenda
pamoja na maelekezo ya kuunda Bodi za Huduma ya Afya za Wilaya na Kamati za
Afya kuanzia ngazi ya Zahanati, Kata, Kituo cha Afya na Hospitali ya
Wilaya. Kazi hii inakwenda sambamba na awamu za
mabadiliko ya Serikali za Mitaa. Hadi
Desemba 2004, Halmashauri zote 113 nchini zilikwishahamasishwa kuhusu uundaji wa Bodi za Afya za Wilaya na Kamati mbalimbali za afya
katika ngazi zote. Aidha Halmashauri 61 kati ya 113 zimeshazindua Bodi za
Huduma za Afya na zinafanya kazi.
26. Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kuwa
wafanyakazi wanatekeleza kwa ufanisi malengo na majukumu yaliyokusudiwa na
Mabadiliko katika Sekta ya Afya, Wizara yangu imeendelea kuwaelimisha na
kuwahamasisha wajumbe wa Timu za
Uendeshaji na Usimamizi wa Huduma za Afya mkoani na wilayani ili wawaeleweshe
wafanyakazi wanaowasimamia, mabadiliko
katika Sekta ya Afya na wajibu wao kwa wateja wanaowahudumia. Aidha
viongozi wafawidhi wa vituo vya Afya na Zahanati zote
katika Halmashauri 66 nao wamekwisha hamasishwa.
27. Mheshimiwa
Spika,
jamii pia imeendelea kuelimishwa na kuhamasishwa
kuhusu mabadiliko, haki na wajibu wao katika kumiliki Huduma za Afya kwa njia
mbalimbali zifuatazo:
·
Vipindi na matangazo katika redio na televisheni,
·
Mabango na vipeperushi,
·
Mabadiliko katika huduma za afya kupitia michezo ya kuigiza (TV),
·
Mikutano ya Bodi na Kamati mbalimbali za Afya.
28. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/05 Wizara ilifanikiwa kuhamasisha
na kutoa mafunzo kwa Halmashauri za wilaya 92 za Tanzania Bara na kuziwezesha
kuandaa na kupitisha Sheria ndogo ya kuanzisha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Halmashauri hizo hazijumuishi Halmashauri za
wilaya 8 mpya
kwa kuwa Wizara bado inazisubiri zipate mabaraza ya Madiwani mwezi Oktoba 2005.
Halmashauri za wilaya 51 kati ya 92 zilizohamasishwa, zimekwishazindua Mfuko wa Afya ya Jamii na zilizobaki 41 ziko katika hatua
mbalimbali za uzinduzi.
29. Mheshimiwa
Spika, Serikali hutoa kiasi cha fedha
kinacholingana na kiasi cha fedha kinachongwa na
wananchi katika mfuko wa Afya ya Jamii (Tele kwa Tele). Ili Halmashauri iliyokwisha kuanzisha Mfuko wa Afya ya Jamii iweze kupata fedha za tele kwa tele,
inatakiwa kuwekeana mkataba na Wizara ya Afya.
Mkataba huo unatoa mwongozo wa matumizi ya
fedha za CHF. Halmashauri 15 kati ya 51
zilizoanzisha CHF zimekwisha wekeana mkataba na Wizara
ya Afya. Hadi sasa jumla ya shilingi
milioni 500 za tele kwa tele zimekwishalipwa. Tunazihimiza Halmashauri zilizobaki
zikamilishe taratibu za mikataba ili nazo ziweze
kulipwa fedha za tele kwa tele.
30. Mheshimiwa
Spika, maandalizi ya Hati rasmi na miongozo ya kufundishia jinsi ya kutekeleza mpango wa
TIKA yamekamilika. Halmashauri ya
Mwanza, Iringa na Mji wa Mtwara wataanzisha mfuko huu.
Aidha, Umoja wa Matibabu katika Sekta isiyo Rasmi
(UMASIDA) ulioanzishwa katika Jiji la
Mfuko
wa Taifa wa Bima ya Afya
31. Mheshimiwa
Spika, katika kutekeleza majukumu
yake ya mwaka 2004/2005 Mfuko huu hadi kufikia tarehe 2 Aprili 2005 ulitekeleza
yafuatayo:-
·
Kusajili
wanachama wapya 6,321 na hivyo kuufanya Mfuko
kufikisha jumla ya wanachama 248,829 ikilinganishwa na wanachama 242,508
waliokuwepo kipindi
·
Jumla ya shilingi
bilioni 7.35 zimelipwa kwa watoa huduma wa Serikali na
wa asasi zisizo za Serikali tangu utaratibu huu ulipoanza kutumika miaka minne
iliyopita, ikiwa ni marejesho kwa huduma walizotoa kwa wanachama.
32. Mheshimiwa
Spika, jumla ya vituo 3,558 vya
matibabu vilisajiliwa na Mfuko ili kuhudumia wanachama, ambapo asilimia 70 ya
vituo hivyo viko vijijini. Kati ya vituo hivyo vituo 518 vinamilikiwa na madhehebu ya dini na asasi zisizo za Serikali na maduka
ya dawa 36 yanamilikiwa na wamiliki binafsi. Usajili wa
vituo zaidi vya matibabu umesaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma za
matibabu karibu zaidi na wanapoishi wanachama na hivyo kuongeza ushindani
miongoni mwa watoa huduma. Wanachama wana uhuru wa
kuchagua wapi wakapate huduma za
matibabu kati ya vituo vinavyomilikiwa na Serikali au vile vinavyomilikiwa na madhehebu ya dini
na mashirika ya kujitolea.
33. Mheshimiwa
Spika, upatikanaji wa dawa
umeendelea kuridhisha japo bado kuna tatizo katika baadhi ya maeneo ambayo yana
usimamizi hafifu. Mfuko uko katika
hatua za mwisho za kusajili baadhi ya maduka ya dawa muhimu (ADDO – “ Accredited Drug Dispensing Outlet”) yaliyoanza kutoa
huduma mkoani
34. Mheshimiwa Spika, Mfuko umetoa elimu kwa wadau 96,414 wakiwemo
Viongozi wa vyama vya wafanyakazi, watoa huduma na kwa wanahabari.
35. Mheshimiwa Spika, Mfuko uliimarisha ofisi zake saba za kanda kwa kuzipatia nyenzo na madaraka zaidi. Katika kipindi hicho jumla ya watumishi 37
waliajiriwa katika Ofisi za Kanda wengi wao wakiwa ni
wakaguzi na hivyo kufanya Mfuko kuwa na watumishi 121 nchi nzima. Uimarishaji huu umeuwezesha Mfuko kuzisogeza
huduma karibu zaidi na wadau.
36. Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu
Bunge lako tukufu kuwa katika kipindi cha mwaka wa
fedha 2004/05, Mfuko umeimarisha shughuli zake kupitia teknolojia ya habari na
mawasiliano. Hii ni pamoja na
kuziunganisha ofisi zote saba za kanda na Makao Makuu, na kurahisisha uandaaji
wa malipo kwa watoa huduma na mawasiliano ya haraka na wateja. Aidha, mfuko ulizindua tovuti yake yenye anwani ifuatayo ya www.nhiftz.com ambapo shughuli nyingi sasa
zinafanyika kupitia mfumo huo.
37. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/05 Wizara yangu imeendelea kutoa
kipaumbele kwa upatikanaji wa takwimu katika Sekta ya
Afya. Pamekuwepo na
mikakati ya makusudi ili kuhakikisha kuwa takwimu zinazohitajika zinapatikana
kwa ajili ya mipango, kutoa tathmini ya utoaji wa huduma za afya, kufuatilia
utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kisekta na kuboresha sera na miongozo
mbalimbali ili kuhakikisha kwamba huduma za afya zinatolewa katika ubora
unaostahili.
38. Mheshimiwa
Spika, katika kufanikisha mipango ya
upatikanaji wa takwimu sahihi mikakati ifuatayo
imetekelezwa:-
·
Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya (MTUHA), umezidi
kuboreshwa katika ngazi ya wilaya,
baada ya kuweka kompyuta na programu ya kuchambua takwimu hizo. Hii imesaidia kuongeza kasi ya upatikaji wa takwimu katika ngazi ya wilaya, mkoa na taifa.
·
Takwimu
zinazopatikana kupitia mfumo wa tafiti mbalimbali nazo zimeimarishwa zaidi (Operational
Research).
·
Mafunzo
yametolewa kwa wajumbe wa Kamati za Afya za Uendeshaji
wa Huduma wilayani na mikoani. Lengo la
mafunzo hayo lilikuwa kuwapa uwezo na mbinu za kufanya utafiti ili kukusanya
takwimu zilizo sahihi, kuchambua na
kutumia matokeo yake kuboresha huduma za afya ngazi ya mkoa, wilaya na jamii kwa ujumla.
·
Kutayarisha na
kusambaza vitabu vya mfumo wa taarifa za uendeshaji wa Huduma za Afya nchi
nzima.
MATUMIZI YA KAWAIDA
Udhibiti wa
Magonjwa ya Kuambukiza (Epidemiologia)
39. Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti magonjwa ya kuambukiza Wizara
iliendelea kutumia mbinu zifuatazo:-
· Wilaya zilihamasishwa na kuweza kutumia mbinu shirikishi (Participatory Hygiene
and Sanitation Transformation – PHAST) ili kuwezesha jamii kubuni, kupanga,
kutekeleza na kusimamia mipango ya afya ya mazingira ili kudhibiti magonjwa ya
kuambukiza na milipuko.
· Fremu za mabamba ya vyoo 490 zilitengenezwa na kugawanywa katika Wilaya ili ziweze kutumika kwa mafunzo
na ujenzi wa vyoo bora.
· Matanuru 4 ya kuteketekeza taka yalijengwa katika hospitali
maalum ya Kibong’oto, hospitali ya
· Mashindano ya usafi wa
mazingira katika Halmashauri za Manispaa, Miji na Halmashauri za Wilaya
yalifanyika.
Mbinu
zote hizi ziliwezesha kuboreshwa kwa usafi wa mazingira na hivyo kupunguza
idadi ya wagonjwa wa kipindupindu kutoka wagonjwa 6,254 na vifo 217 mwaka
2003/2004 hadi kufikia wagonjwa 3,462 na vifo 93 mwaka 2004/2005.
40. Mheshimiwa Spika, tatizo la watu kuumwa na
mbwa au wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa cha mbwa limekuwa likiongezeka kila
mwaka. Mwaka 2004 watu 16,750 waliumwa
na mbwa au wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa cha mbwa na kati yao watu 97
walifariki ikilinganishwa na mwaka 2003 ambapo watu 12,587 waliumwa na kati yao
77 walifariki. Kuanzia Januari hadi
Aprili, 2005, walioumwa ni 6,350 na waliofariki ni
34. Katika kupambana na
tatizo hili, Wizara yangu ina jukumu la kununua dawa za kuchanja wagonjwa
walioumwa na mbwa. Jumla ya shilingi milioni 259.35
zilitumika kununua dawa ya chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kichaa cha mbwa katika
kipindi cha Julai 2004 hadi Mei, 2005.
Gharama za kumchanja mtu aliyeumwa na mbwa ni
dola za kimarekani 24 na gharama ya kumchanja mbwa ni dola za kimarekani
0.4. Kwa kuwa kuchanja mbwa ni rahisi, Wizara yangu ikishirikiana na Wizara ya Maji na
Mifugo imeandaa taarifa yakinifu (concept paper) inayopendekeza kubadilisha
kifungu cha sera ya Kilimo ya mwaka 1997 sehemu ya 3, kifungu kidogo cha 3,
kipengele cha 1, sehemu D, kibadilishwe na jukumu la kuchanja mbwa liwe la
Serikali badala ya kuachiwa jukumu
41. Mheshimiwa Spika, ugonjwa wa malaria bado ni
tatizo kubwa nchini na linahitaji jitihada za pamoja katika kukabiliana nalo.
Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara yangu ilitekeleza majukumu mbalimbali
katika kukabiliana na ugonjwa wa malaria. Utekelezaji ni kama ifuatavyo:-
·
Kutoa mafunzo kwa wataalam mbalimbali wa afya kuhusu
tiba sahihi,
·
Kuhamasisha umma juu ya utumiaji wa vyandarua vyenye
viuatilifu hasa kwa mama wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano,
·
Kutafiti usugu wa vimelea vya malaria,
·
Kuendeleza
utafiti wa tiba ya dawa mseto,
·
Kutoa tiba ya
tahadhari kwa vipindi (Intermittent Preventive Treatment) kwa mama wajawazito,
·
Kutoa tahadhari
ya kudhibiti milipuko ya malaria katika wilaya zenye milipuko ya mara kwa mara ya malaria na kuimarisha udhibiti wa malaria ngazi
ya jamii.
42. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea na uhamasishaji wa jamii katika
kutumia vyandarua vyenye viuatilifu. Tarehe 22 Oktoba mwaka 2004, Wizara yangu
ilizindua Mpango wa Taifa wa Hati Punguzo. Mpango
ambao unawawezesha mama wajawazito na watoto walio
chini ya umri wa miaka mitano kupata vyandarua vyenye viuatilifu kwa bei
nafuu. Kwa hivi sasa, mpango wa Taifa wa Hati Punguzo unatekelezwa katika mikoa ya
Dar-es-salaam,
43. Mheshimiwa Spika, mwaka huu Wizara yangu kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali iliadhimisha Siku ya Malaria Afrika
iliyofanyika Kitaifa tarehe 25 Aprili, 2005 mkoani Singida. Kauli mbiu ya maadhimisho
hayo ilikuwa “Tushirikiane kwa pamoja tushinde malaria”. Kauli mbiu hii inatukumbusha na kusisitiza
umuhimu wa kuwashirikisha wadau wote katika Sekta ya Afya kupiga vita malaria, hii
ikiwa ni pamoja na jamii, Serikali kuu, Serikali za mitaa, wahisani mbalimbali,
mashirika ya dini na watu binafsi.
44. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Julai 2004 mpaka Juni 2005, Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na
Ukoma ulifanya ufuatiliaji wa watoto wa shule 1,048 waliobainika kuwa na
uambukizo wa ugonjwa wa Kifua Kikuu katika mikoa ya Singida, Iringa, Mbeya,
Kigoma na Kagera. Asilimia 48 ya watoto
hao walipata uambukizo ndani ya kaya zao na jumla ya watoto 75 yaani asilimia 3 walikuwa tayari na ugonjwa wa
kifua kikuu (active TB) na walipewa dawa za matibabu.
45. Mheshimiwa Spika, kampeni za kutokomeza ugonjwa wa ukoma zilifanyika
katika mikoa ya Kagera, Rukwa na Tabora ambako jumla ya wagonjwa wapya 836
waligunduliwa na kuanzishiwa tiba. Aidha katika juhudi za kurekebisha ulemavu (prevention
and rehabilitation of disabilities) unaotokana na ukoma, watu walioathirika
na ukoma wenye ulemavu 175 walifanyiwa upasuaji wa aina mbalimbali na wengine
5,811 walipewa viatu maalumu na watu 37 walipewa miguu bandia. Vile vile
madaktari bingwa wa upasuaji 5 walipewa mafunzo rejea juu ya upasuaji wa
wagonjwa waliopata ulemavu kutokana na ukoma.
Kutokana na takwimu za Shirika la Afya Duniani, ili nchi ihesabiwe kuwa
imetokomeza ukoma inatakiwa kufikia mgonjwa 1 kwa kila watu 10,000. Hadi hivi sasa Tanzania imefikia wagonjwa 1.3
kwa kila watu 10,000. Mafanikio haya ni
makubwa lakini tunatakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji ili hatimaye kutokomeza
ugonjwa huu kabisa.
46. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2004/2005, jamii iliendelea
kuelimishwa kwa kutumia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa matangazo kwa
kutumia vyombo vya habari, kusambaza vipeperushi na mabango yenye ujumbe wa
jinsi ya kutambua dalili, kujikinga na matibabu ya kifua kikuu na ukoma. Aidha
dawa za kutosha za kifua kikuu na ukoma ziliendelea kusambazwa katika mikoa,
wilaya na vituo vyote vya matibabu. Dawa hizo zilitolewa kwa wagonjwa wote bila
malipo.
Mpango wa
Taifa wa Kudhibiti UKIMWI:
47. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza
Mkakati wa Sekta ya Afya wa Kudhibiti UKIMWI 2003-2006, Wizara yangu inaendelea kutekeleza
yafuatayo:-
Huduma
ya kutoa elimu ya UKIMWI
48. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/2005 huduma ya elimu ya UKIMWI
iliendelea kutolewa kwa kutumia mbinu na njia mbalimbali,
Huduma
za Ushauri Nasaha na Upimaji wa Hiari
49. Mheshimiwa
Spika,
katika mwaka 2004/2005 huduma za Ushauri
Nasaha na upimaji wa afya kwa hiari ziliendelea kutolewa katika vituo 521
vinavyotoa huduma hiyo nchini kote. Aidha, idadi ya watu waliohudhuria katika
vituo hivyo walikuwa 227,973 ukilinganisha na mwaka
2003/2004 ambapo watu 139,972 walipata huduma hii. Ongezeko hili linatokana na kuongezeka kwa idadi ya vituo vinavyotoa ushauri huo
kutoka 332 mwaka 2003 hadi 521. Hata
hivyo pamoja na ongezeko hili idadi ya watu
wanaojitokeza kwa ajili ya upimaji bado ni ndogo
50. Mheshimiwa Spika, mafunzo kuhusu ushauri nasaha yalitolewa kwa watumishi wa afya 165 na kufanya idadi ya wataalam wa
ushauri nasaha kufikia 12,000.
Huduma ya Damu Salama
51.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005, Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI uliendelea kuhakikisha kuwa
damu inayotolewa kwa wagonjwa ni salama. Vifaa vya kupima damu
(Rapid Tests) 755,908 vilisambazwa nchini kote.
Usambazaji wa
Kondomu
52. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka
2004/2005, Wizara yangu ilipokea jumla ya kondomu millioni 52. Wizara
ilisambaza kondomu za kiume millioni 21 kati ya hizo na milioni 21 nyingine za
kiume na 10,000 za kike zilizobaki
zilisambazwa kupitia mashirika yasiyokuwa ya kiserikali chini ya
utaratibu wa ‘social
marketing’.
Huduma ya Magonjwa ya Ngono
53.
Mheshimiwa Spika, Mpango wa
Taifa wa Kudhibiti UKIMWI unaendelea kuratibu upatikanaji wa huduma za kutibu
magonjwa ya ngono nchini kote. Tiba ya magonjwa ya ngono ni
njia mojawapo ya kudhibiti kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI. Sasa hivi huduma hii inapatikana mikoa yote nchini.
Huduma za
kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama
kwenda kwa Mtoto (Prevention of Mother to Child Transmission – PMTCT)
54. Mheshimiwa
Spika, katika
mwaka 2004/2005 Wizara imesambaza huduma
ya kuzuia maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto
katika mikoa 9 zaidi ya Tanzania Bara. Mikoa hiyo ni
Lindi,
55. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea na mpango
wa kutoa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI kwa akina mama
wajawazito, wazazi wenzao na watoto wao.
Mpango huu ambao unaitwa “PMTCT – Plus” unaenda sambamba na mpango wa Taifa wa kutoa dawa za kupunguza makali ya
UKIMWI (ART programe) na hivyo umeanza kutekelezwa katika vituo 96 vilivyo
katika mpango wa ART.
Dawa za Kupunguza Makali ya Ugonjwa wa
UKIMWI (Anti- Retro
Viral – ARVs)
56.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005, shilingi bilioni 8.3 zilitumika kununua dawa za
kupunguza makali ya UKIMWI. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 3.5 zilitolewa
na Serikali, dola za
Huduma ya Tiba ya Wagonjwa wa UKIMWI Nyumbani (Home Based Care)
57. Mheshimiwa
Spika, huduma ya tiba kwa wagonjwa
wa UKIMWI nyumbani ni ya muhimu
Huduma
ya Kufuatilia Mwenendo wa maambukizi ya Virusi vya
UKIMWI katika Jamii
58. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/2005 Wizara yangu kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI ilifuatilia vidokezo vifuatavyo
katika mwenendo wa ugonjwa wa UKIMWI: Kiwango cha maambukizi ya UKIMWI na
magonjwa ya ngono, njia za maambukizi, maambukizi ya virusi vya UKIMWI miongoni
mwa wajawazito na tabia za maambukizi ya UKIMWI miongoni mwa vijana. Utafiti wa tabia nchini
Mpango wa Taifa wa Huduma za
Macho
59. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka
2004/2005 Tanzania imekuwa ni nchi
mojawapo ya kwanza kuandaa na kukamilisha Mpango Mkakati wa miaka mitano
(2004-2008) wa Huduma za Macho unaoelekeza kutokomeza upofu unaozuilika ifikapo
mwaka 2020. Mpango Mkakati huu unatoa
dira na mwelekeo wa Huduma za Macho katika jitihada za kudhibiti upofu
unaozuilika.
60. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa msaada wa shirika la
Kitamaifa la kudhibiti ugonjwa wa vikope
imeainisha Wilaya 50 zenye tatizo la ugonjwa wa vikope. Aidha, utafiti wa kina wa ugonjwa huu umekamilika
katika Wilaya thelathini (30) na kuthibitisha kwamba Wilaya 26 kati ya 30 zina
ugonjwa huu kwa zaidi ya asilimia 10 ya wakazi.
Kutokana na mwongozo wa Shirika la Afya Duniani, inapogundulika kuwa
jamii imeathirika na ugonjwa huu kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10, jamii
yote inatakiwa kupewa dawa. Kutokana na
matokeo hayo, tumeanza kutoa dawa ya Zithromax katika Wilaya 6 kati ya 26 za
Sikonge, Handeni, Dodoma Vijijini, Tunduru, Ruangwa na Magu. Utafiti katika wilaya 20 zilizobakia
unaendelea. Tanzania imekuwa nchi ya
kwanza kufanya utafiti kama huu kwa nchi zenye ugonjwa huu na kuifanya kuwa
nchi ya mfano. Dawa ya Zithromax ni
msaada kutoka Kampuni ya Pfizer kupitia Shirika la Kimataifa la Kudhibiti
Ugonjwa wa Vikope (International Trachoma Initiative – ITI). Kampuni ya Pfizer iko tayari kutoa dawa ya
kiasi chochote tunachohitaji kulingana na mahitaji yetu.
61. Mheshimiwa Spika, Mpango wa Taifa wa kudhibiti ugonjwa wa Usubi uligawa dawa ya
mectizan katika vijiji 650 vilivyoko katika wilaya 14 ambazo ni Ulanga,
Kilombero, Kilosa, Songea, Mbinga, Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela, Muheza,
Mvomero, Morogoro, Korogwe, na Lushoto. Jumla ya wananchi 2,948,862
walipatiwa dawa hii.
Huduma ya Elimu ya Afya Kwa Umma
62. Mheshimiwa
Spika, Wizara yangu imetoa mafunzo kwa Kamati za Uendeshaji
Huduma za Afya za Halmashauri 32 ili ziweze kupanga, kutekeleza, kufuatilia na
kutathmini huduma za elimu ya afya kwa umma.
Msisitizo uliwekwa katika kuongeza ubunifu wa mikakati na njia za
mawasiliano zenye uwezo wa kuhimiza na kuleta mabadiliko ya tabia na mienendo
inayolenga kuboresha afya katika jamii yetu.
Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto
63. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2004/2005 huduma maalum kwa
wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano ziliendelea kutolewa bila
malipo katika vituo vyote vya kutolea huduma vya Serikali. Huduma hizo ni
pamoja na huduma kwa wanawake wajawazito, huduma za kujifungua, chanjo,
matibabu kwa watoto wagonjwa wenye umri chini ya miaka 5 na uzazi wa mpango.
Aidha Wizara yangu ilihakikisha upatikanaji na usambazaji wa dawa mbali mbali
za uzazi wa mpango unafanyika nchini kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali.
64. Mheshimiwa Spika, tathmini ya kina ya kutambua hali halisi ya uwezo wa
vituo vyetu katika kukabiliana na dharura ya uzazi pamoja na rufaa imefanyika.
Taarifa kamili itakuwa tayari mwaka 2005/2006. Matokeo yatatumika katika
kuimarisha mikakati iliyopo ya kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi ambapo
wilaya zitakuwa ni watekelezaji wakuu. Aidha tathmini ya kitaifa kuhusu hali
halisi za Afya (Tanzania Demographic Health Survey) iliyoanisha takwimu za
Uzazi na Mtoto imefanyika kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (National
Bureau of Statistics). Matokeo ya awali yaliyopatikana mwezi Mei, 2005
yameonyesha kuwa vifo vinavyotokana na uzazi vimeongezeka kutoka 529 mwaka 1996
hadi 578 mwezi Mei 2005 kwa kila kinamama 100,000 wanaojifungua. Kutokana na matokeo haya ya awali imeonekana
kuwa tatizo hili bado linaongezeka.
Wizara yangu itaendelea kuwaelimisha watoa huduma pamoja na jamii kuhusu
mbinu za kutambua vidokezo vya hatari na kuimarisha huduma za rufaa.
65. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2004/2005 watoa huduma na wakufunzi
130 walipata mafunzo rejea kuhusu uzazi wa mpango kutoka mikoa ya Dodoma, Kilimanjaro,
Morogoro, Tanga, Lindi, Mbeya, Pwani na Mwanza. Pia watoa huduma 100 kutoka
mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Mtwara, Morogoro, Lindi, Mbeya, Mwanza na
Pwani walipata mafunzo rejea ya utoaji huduma kwa wajawazito ikijumuisha
matibabu ya tahadhari kutoa kinga kwa wajawazito dhidi ya malaria na upimaji wa
ugonjwa wa Kaswende.
Mkakati wa
Kutibu Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano (Intergrated Management of Childhood
Illness-IMCI)
66. Mheshimiwa
Spika, katika kipindi
2004/2005 Wilaya 87 zinaendelea kutekeleza mkakati wa IMCI. Jumla ya watoa
huduma za Afya 300 wamepata mafunzo
kuhusu stadi za kumtibu mtoto. Watoa huduma za afya 40 kutoka hospitali 7 za
Amana, Temeke, Mwananyamala, Morogoro, Tumbi, KCMC pamoja na Hospitali ya Taifa
ya Muhimbili wamepata mafunzo juu ya utoaji wa huduma ya dharura na kuboresha
utoaji huduma kwa mtoto aliyezidiwa. Aidha jamii imeendelea kuelimishwa juu ya
mienendo inayoboresha afya ya mtoto. Mienendo hii inakazia lishe kwa mtoto,
makuzi ya mwili na akili, pamoja na uzuiaji wa magonjwa ya watoto kwa njia ya
chanjo. Mafunzo haya yametolewa katika ngazi ya kaya katika wilaya 13 za
Mtwara, Masasi, Hai, Musoma vijijini, Magu, Ngara, Kilosa, Mbinga, Makete,
Songea Vijijini, Kisarawe, Kibaha na Mbarali.
Mpango wa Taifa wa Chanjo
67. Mheshimiwa Spika, huduma za chanjo zimeendelea kutolewa nchi nzima kwa
watoto ikiwa ni juhudi ya Serikali ya
kupunguza vifo na magonjwa ya watoto yanayozuilika kwa chanjo. Magonjwa hayo ni
kifua kikuu, dondakoo, kifaduro, pepopunda, polio, surua na homa ya ini.
Viwango vya chanjo vimeendelea kuongezeka vikilinganishwa na viwango vya mwaka
uliopita; chanjo ya DPT- Hepatitis B kutoka asilimia 89 hadi 91, Surua kutoka asilimia 90 hadi 94, Polio
kutoka asilimia 92 hadi 96, Kifua Kikuu kutoka asilimia 94 hadi 95. Mafanikio
haya yametokana na juhudi ya Serikali, jamii na wadau mbalimbali wakiwemo
Global Alliance for Vaccine and Immunisation (GAVI), ambao tunawashukuru
sana.
Huduma ya
Afya Shuleni
68. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005
Wizara yangu ilisambaza kadi za kuwekea kumbukumbu ya afya ya wanafunzi kwa
kuanzia katika manispaa za IIala, Temeke na Kinondoni. Waratibu 150 kutoka ngazi ya mkoa na wilaya
walipatiwa mafunzo juu ya udhibiti wa magonjwa ya kichocho na aina nyingine za
minyoo. Aidha utafiti kuhusu ugonjwa wa kichocho katika shule za msingi
umefanyika katika wilaya zote nchini. Matokeo ya utafiti huu yatatolewa katika
kipindi cha 2005/2006. Vile vile
Waratibu 75 wa Afya Shuleni wakiwemo wa mikoa yote, na wa Wilaya 17 za Kanda ya
Kaskazini walipata mafunzo ya Huduma ya Kwanza (First Aid).
Afya ya
Mazingira
69. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma za Afya ya Mazingira na kuinua
kiwango cha usafi, Wizara yangu ilianzisha mashindano ya usafi wa mazingira
nchini. Katika kipindi cha 2004/2005
mashindano yalifanyika katika makundi matatu ambayo ni Jiji na Manispaa,
Halmashauri za Miji na Halmashauri za Wilaya.
Washindi katika makundi yote matatu ni kama ifuatavyo:-
Washindi katika kundi la kwanza la Manispaa na
Jiji walikuwa ni Manispaa ya Moshi
ambayo imekuwa mshindi wa kwanza, Jiji la Mwanza limeshika nafasi ya Pili na
Manispaa ya Tanga imeshika nafasi ya Tatu.
Kundi la pili washindi walikuwa Halmashauri za Singida Mjini mshindi wa
kwanza, Songea Mjini mshindi wa pili na Sumbawanga Mjini mshindi wa tatu na
kundi la tatu washindi walikuwa
Halmashauri ya Arumeru mshindi wa kwanza, Lushoto mshindi wa pili na Njombe
mshindi wa tatu.
70. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha
2004/2005 Wizara iliandaa na kusambaza miongozo ya utekelezaji wa huduma za
afya ya mazingira nchini. Miongozo na mikakati iliyoandaliwa ni pamoja na:-.
·
Mwongozo wa Mafunzo ya Mbinu Shirikishi Jamii katika
kuboresha tabia za Afya na Usafi wa Mazingira,
·
Mwongozo wa
Udhibiti wa Taka (Waste Management Policy Guideline),
·
Mwongozo wa Afya
ya Mazingira (National Environmental Health Policy Guideline),
·
Na rasimu ya
Mkakati wa Kitaifa wa Afya na Usafi wa Mazingira
(National Environmental Health, Hygiene and Sanitation Strategy).
71.
Mheshimiwa
Spika,
ili kuinua kiwango cha usafi na ubora wa vyoo, kalibu (moulds) za
kutengenezea mabamba (slab) 560 zilitengenezwa na kusambazwa katika
Wilaya za Rungwe, Bagamoyo, Kisarawe, Monduli na Mufindi na Mkoa wa Kigoma ili
zitumike kujengea vyoo bora.
72. Mheshimiwa Spika,
Wizara yangu pia imeimarisha udhibiti wa taka zinazozalishwa katika hospitali
(Health Care Waste Management) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali pamoja na
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuendesha mafunzo juu ya udhibiti wa taka
hizo, na ujenzi wa matanuru katika hospitali za Wilaya za Kilosa, Mahenge,
Hospitali ya Ocean Road na Hospitali ya Rufaa ya Kibongoto.
Afya katika Sehemu ya Kazi
73.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa afya ya Wafanyakazi
hususan maeneo ya viwanda, ujenzi na mashamba, Wizara yangu imefanya
ufuatiliaji na uhamasishaji wa Bodi za Afya za Halmashauri za wilaya 48 jinsi ya kuainisha huduma za afya sehemu za kazi na huduma za
afya ya msingi. Aidha mafunzo ya Afya
kazini ya kukabiliana na athari mbalimbali za kiafya
kwa wachimbaji wadogo wadogo wa madini katika Mikoa ya Arusha na Mwanza
yametolewa kwa wachimbaji 70.
Taasisi
ya Chakula na Lishe
74. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha mwaka 2004/2005 Wizara ya Afya kupitia Taasisi ya Chakula na Lishe
iliendelea kutoa ushauri wa kitaalam kwa wilaya na kushirikiana na Taasisi na
wadau mbali mbali katika kuboresha hali ya lishe ya jamii nchini.
75. Mheshimiwa Spika, Taasisi
iliendelea kuimarisha uwekaji wa madini joto kwenye chumvi katika wilaya 25
zenye wazalishaji chumvi wadogo wadogo kwa kuhamasisha viongozi 285. Aidha
Taasisi ilitoa mafunzo kwa wakaguzi wa chumvi 451 na kuunda timu za wakufunzi
wa wazalishaji wa chumvi katika wilaya za; Mtwara, Lindi, Kilwa, Rufiji,
Mkuranga, Temeke, Kinondoni, Bagamoyo, Dodoma, Manyoni, Singida, Iramba,
Kigoma, Njombe na Mbozi. Wilaya nyingine ni Tanga, Pangani, Muheza, Korogwe, Same, Mwanga, Meatu,
Babati, Hanang na Karatu. Juhudi zilielekezwa katika wilaya hizo kwa sababu takwimu zinaonyesha kwamba kati ya wazalishaji
hao wadogo ni asilimia 30 tu ndio wamekuwa wakiweka madini joto kwenye chumvi.
Wizara iliendelea kusambaza vifaa mbalimbali vya kuwekea madini joto kwenye
chumvi kwa wazalishaji. Vifaa hivyo ni
pamoja na kilo 5,000 za madini joto na pampu 4,650 za kunyunyuzia madini joto
kwenye chumvi na jumla ya chupa 93,750 za kemikali ya kupima uwepo wa madini
joto kwenye chumvi (iodine test solution).
76. Mheshimiwa Spika, Taasisi iliendelea kuratibu utoaji wa matone ya
vitamini A kwa watoto wa umri kati ya miezi sita hadi miaka mitano na vidonge
vya kutibu minyoo ya tumboni kwa watoto wa umri kati ya mwaka mmoja hadi miaka
mitano katika mikoa yote ya Tanzania Bara; ambapo hadi Desemba, 2004 asilimia 93 ya
watoto walengwa walipata matone ya vitamini A na asilimia 90 walipata vidonge
vya kutibu minyoo.
77. Mheshimiwa Spika,
mkakati wa kitaifa unaoelekeza jinsi ya kusimamia
lishe na afya ya mtoto mwenye umri chini ya miaka mitano umeandaliwa na
kuzinduliwa. Aidha, Mwongozo wa kitaifa kuhusu lishe
bora kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI umeandaliwa. Jumla ya nakala 10,000 za
mwongozo huo zilichapishwa na kusambazwa kwenye Wizara
hospitali za rufaa, hospitali za mkoa na wilaya, vyuo vya afya na taasisi
mbalimbali zinazoshughulika na tatizo la UKIMWI hapa nchini.
78. Mheshimiwa
Spika, Mpango wa Hospitali Rafiki
kwa Mama na Mtoto unaotekelezwa nchini toka mwaka 1992 unalenga katika
kuboresha hali ya afya na lishe ya watoto wachanga. Chini ya mpango huu
hospitali zinatakiwa kutekeleza na kuboresha Huduma ya
Afya na Uzazi kwa wanawake wajawazito na waliojifungua. Hadi kufikia mwaka 2005 katika kufuatilia
Hospitali Rafiki kwa Mama na Mtoto, hospitali 68 nchini zilifanikiwa kuwa rafiki kwa
Mama na Mtoto kwa vigezo vya kimataifa.
Taasisi
ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (National Institute
for Medical Research – NIMR)
79. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka 2004/2005, Taasisi
ilishughulikia usimamizi, uratibu, udhibiti, uenezi, utangazaji wa matokeo na ukuzaji wa utafiti nchini. Magonjwa
yaliyofanyiwa utafiti ni Malaria, Matende na Mabusha,
Usubi, Kichocho, Minyoo ya Tumbo, Kuhara, Magonjwa ya Zinaa, Malale, Kifua
Kikuu na UKIMWI.
80. Mheshimiwa Spika, katika kipindi 2004/2005 tafiti mbalimbali za
malaria zimetoa matokeo ambayo yanaonyesha kuwa usugu wa
vimelea vya malaria kwa dawa ya SP unakua na umefikia asilimia 25. Hatua hii ya
usugu iliyofikiwa inahitaji mabadiliko ya tiba dhidi ya malaria itakayoweka
viwango vipya vya dawa za kutibu malaria na kuweka
bayana mabadiliko ya sera ya tiba ya malaria. Kiutafiti pendekezo linalotolewa
kukabiliana na usugu huu ni matumizi ya dawa
mchanganyiko (combination therapy). Taasisi pia inafuatilia kuona
81. Mheshimiwa Spika, Wizara pia kwa kupitia
Taasisi ya Utafiti wa magonjwa ya Binadamu imefanya utafiti ili kutathmini
kiwango cha dawa kinachopatikana katika mmea wa Artemisia annua na pia
kufanya utafiti katika ngazi ya kimaabara ya namna ya kutengeneza dawa
itokanayo na mmea huo. Kutokana na utafiti huu, Wizara
imefanikiwa kupata mtiririko wa namna ya kutengeneza “Artemisinin” na baadaye kuibadilisha “Artemisinin” kuwa “Dihydro-artemisinin”,
dawa inayofaa kwa kutibu malaria. Aidha,
watafiti wa Kituo cha Utafiti cha Ifakara kwa kutumia tabia ya maumbile ya mbu
ya kupenda kupumzika gizani baada ya kufyonza damu, wameweza kutumia njia za asili za kibaolojia
kutengeneza dawa ambayo itawaangamiza mbu bila ya kuharibu mazingira. Utafiti huu bado unaendelea na utakapokamilika tutalijulisha Bunge lako tukufu.
82. Mheshimiwa Spika, uchunguzi juu ya nguvu za viuatilifu ya kuulia
wadudu wanaosababisha usubi ulifanyika katika wilaya za Rungwe na Kyela. Matokeo yalionyesha mafanikio mazuri, kwa kuua wadudu hao
83. Mheshimiwa Spika, Utafiti wa kuangalia ukubwa wa tatizo la ugonjwa wa matende
umeonyesha
kuwa asilimia 6.6 ya watanzania wameathirika na ugonjwa huu. Tathmini pia
imegundua kwamba watu wenye vimelea vya ugonjwa wa matende wapo katika wilaya zote
za nchi yetu isipokuwa wilaya ya Babati na Chunya. Aidha, katika jitihada za
kupambana na tatizo la matende na mabusha Wizara yangu katika mwaka 2004/2005
iligawa dawa kwa watu 900,000 katika mkoa wa Tanga na hivyo kufanya jumla ya
watu 5,000,000 waliofikiwa na mradi huu tangu ulipoanza mwaka 2000 katika
wilaya 24. Huduma ya upasuaji wa mabusha inaendelea katika mkoa wa Pwani
hususan katika hospitali za wilaya za Mafia na Kibaha. Jumla ya watu 2000
walifanyiwa upasuaji katika mkoa wa Pwani.
84. Mheshimiwa Spika, taasisi ilifanya utafiti kwa wagonjwa
walioathirika na kifua kikuu pamoja na UKIMWI mkoani Mwanza. Wagonjwa hawa
walipewa virutubisho na dawa za kutibu kifua kikuu. Matokeo yalionyesha kwamba
idadi ya vifo ilipungua kwa asilimia 72 ikilinganishwa na wakati walipopewa
dawa za kifua kikuu peke yake. Aidha kwa kushirikiana na kituo cha Munufu
kilichopo Ubungo Dar es Salaam, Taasisi
imeifanyia utafiti wa awali dawa ya tiba ya asili ya Muhanse inayotumiwa na baadhi
ya wagonjwa wa UKIMWI na kuiona haina madhara ya kuhatarisha maisha ya
mtumiaji. Taasisi itaendelea kuifanyia
utafiti zaidi ili kujua uwezo wake wa
kutibu.
85. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa ushirikiano na Taasisi imefanya tathmini ya magonjwa ya kichocho na minyoo ya
tumbo katika Ukanda wa Ziwa kwa wanafunzi 8,580 wa shule 143 za msingi za mikoa
ya Shinyanga, Mwanza, Tabora na Kagera.
Matokeo ya tathmini hii yatasaidia kupata njia muafaka za kupambana na magonjwa
haya.
Kuimarisha Huduma za Afya
Wilayani
86. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2004/2005 Wizara yangu imebadilisha
magari machakavu na kutoa mapya 19 kwenye Halmshauri za Monduli, Kiteto, Mbeya,
Songea, Nkasi, Rufiji, Muleba, Singida, Mbinga, Rombo, Magu, Kibondo, Kigoma,
Urambo, Kyela, Rungwe, Manispaa ya Tabora, Jiji la Mwanza na ofisi ya Mganga
Mkuu Kagera kwa ajili ya ufuatiliaji na usambazaji wa dawa, vifaa tiba na kinga
kwenye vituo vya kutolea huduma.
HUDUMA
ZA TIBA
Huduma ya Dawa, Vifaa na
Vifaa Tiba
87. Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2004/05,
kiasi cha shilingi 30,660,128,899.37/= zilitumika kununua dawa, vifaa na vifaa
tiba kwa matumizi ya hospitali, zahanati na vituo vya afya. Aidha, hospitali za
wilaya, mikoa na rufaa ziliendelea na utekelezaji wa
uchangiaji wa gharama za dawa chini ya mfumo wa ‘Capitalization of Hospital
Pharmacies’ ambapo wananchi wanalipa nusu ya bei halisi ya dawa. Fedha kutokana
na mauzo ya dawa ziliingizwa kwenye mfuko wa dawa (Drug
Revolving Fund) kuwezesha hospitali hizo kununua dawa nyingine
zilizohitajika.
88. Mheshimiwa
Spika, Bohari ya Madawa ndicho chombo
kikuu cha Serikali cha ununuzi na usambazaji wa dawa
na vifaa tiba vikiwemo vinavyotolewa kwa kupitia misaada mbalimbali ya miradi
misonge (vertical programme). Katika kipindi hicho, Bohari ya Madawa ilisambaza
dawa za chanjo, dawa za kutibu kifua kikuu na ukoma,
usubi, uzazi wa mpango, matende, mabusha na magonjwa ya mtegesheo kwa watu
waishio na virusi vya UKIMWI.
89. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/2005, zahanati mpya 526 na vituo vya afya 36 vilivyojengwa na Halmashauri na kwa
nguvu za wananchi vilipewa masanduku ya dawa. Aidha, zahanati 716 na vituo vya afya 88 katika mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na
Shinyanga vilianza kuagiza dawa na vifaa kwa kutumia mfumo wa kuagiza dawa
kulingana na mahitaji (indent). Kutokana na
hatua hiyo, Bohari ya Mwanza sasa imeondokana na mfumo wa usambazaji wa
masanduku ya dawa.
90. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu pia ilitoa mafunzo ya utekelezaji wa mfumo wa
kuagiza dawa kulingana na mahitaji kwa wajumbe wa Kamati za Uendeshaji wa Huduma
za Afya katika mikoa ya
Huduma za Uchunguzi wa
Magonjwa
91. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/2005, Mradi wa
uimarishaji wa huduma za eksirei na ultrasound (Overseas Related Export
Trade – ORET) ulikabidhiwa kwa Serikali na kampuni ya “Philips Medical
Systems” ya Uholanzi. Makabidhiano
hayo yalifanyika Jijini Mwanza katika hospitali ya Bugando tarehe 22 Februari
2005. Katika makabidhiano hayo,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
92. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/2005 Wizara
yangu, imezipa Karakana za kanda vipuli, na nyenzo za utekelezaji wa
matengenezo ya mashine za kutolea huduma za afya. Wizara pia imetoa mafunzo kwa mafundi ili kuhakikisha kuwa mashine hizo pamoja na
vifaa na vifaa tiba vinadumu kwa muda mrefu zaidi.
93. Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha huduma
za maabara za hospitali ili ziweze kufuatilia wagonjwa wanaopatiwa dawa za
kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI, Wizara yangu imeweka mashine za kupima CD4 katika hospitali zote za rufaa,
mikoa yote pamoja na hospitali za manispaa za Dar es Salaam. Vile
vile, mashine kwa ajili ya vipimo vingine (Clinical Chemistry & Haematology)
kwa ajili ya hospitali 10 za mikoa na 13 za wilaya zimekwisha agizwa. Vipimo hivyo ni kwa
ajili ya kufuatilia athari zinazoweza kuwapata wagonjwa kutokana na kutumia
dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI.
Damu
Salama
94. Mheshimiwa Spika,
mwaka 2004/2005 Wizara yangu imeimarisha upatikanaji wa damu salama kwa
kukamilisha mwongozo wa utoaji wa huduma za damu salama na kukamilisha vituo 3
vya kanda (Zonal Blood Transfusion Centres- ZBTC) katika kanda za Ziwa,
Kaskazini na Nyanda za Juu Kusini.
Vituo hivyo vya Kanda vitahudumia hospitali zote zilizoko katika kanda
hizo.
Kwa upande wa Kanda ya
Mashariki, ujenzi wa kituo umekwisha anza Dar es Salaam eneo la Mchikichini. Hadi hivi sasa Mkandarasi amemaliza asilimia
30 ya kazi. Kituo hiki kitakapokamilika
kitahudumia hospitali zote zilizoko katika Kanda ya Mashariki.
Huduma
ya Afya ya Kinywa
95. Mheshimiwa Spika, katika
mwaka 2004/2005 Wizara ya Afya imefunga vifaa
vya Tiba ya Meno (Dental Units) katika
hospitali zilizobakia katika awamu ya kwanza katika Halmashauri za
Wilaya zifuatazo: Mbarali, Karatu,
Ngorongoro, simanjiro, Kiomboi, Morogoro Vijijini, Mbozi, Hanang, Sikonge,
Mpanda, Mvomero, Bariadi, Bukombe, Kilombero, Liwale, Njombe, Ludewa, Sengerema,
Geita, Ukerewe, Misungwi, Newala, Mwanga, Kwimba na Manispaa ya Morogoro. Aidha,
hospitali za mikoa ya Iringa,
Bombo, Mawenzi, Mt. Meru na hospitali ya rufaa ya KCMC nazo zilipata vifaa
hivyo.
Huduma ya Afya ya Akili na
Vita dhidi ya Madawa ya kulevya
96. Mheshimiwa Spika,
mwaka 2004/2005 Wizara imeendelea kusimamia uboreshaji wa huduma za afya ya
akili ngazi ya msingi. Shughuli hizo
zinaendelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Manyara, Mtwara na Mwanza. Pia
vitabu vya kiswahili vinavyobainisha na kutibu magonjwa ya akili yanayojitokeza
kwa wingi ndani ya jamii vimechapishwa
na kusambazwa.
Huduma za Hospitali za
Mashirika ya kujitolea, Makampuni na
Watu Binafsi
97. Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2004/2005 ruzuku ya kitanda ilipandishwa kutoka Tshs 15,000/= hadi
TShs 30,000/= kwa mwaka. Aidha, hospitali mbili za Mashirika ya Dini (Karatu na
Mugana) ziliombwa na Halmashauri za Wilaya ya Karatu na Bukoba Vijijini
zitumike kama Hospitali Teule. Hospitali hizo tayari zimeanza kutumika kama
hospitali Teule za wilaya hizo. Katika mwaka huo kulikuwa na ongezeko la
vitanda 174 kwa ajili ya kupewa ruzuku na kufanya jumla ya vitanda vinavyopewa
ruzuku hadi sasa kufikia 5,623. Wizara yangu pia ilisajili vituo vya kutolea
huduma za afya 53 kati ya 73 vlivyoombewa
usajili.
Huduma ya Tiba Asili
98. Mheshimiwa Spika,
katika kutekeleza Sheria namba 23 ya mwaka 2002 inayosimamia Dawa, Tiba Asili
na Tiba Mbadala, Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala tayari limekwisha teuliwa
na mamlaka husika kwa mujibu wa Sheria hiyo. Wizara ya Afya imeandaa Kanuni na
Miongozo ya usajili wa Waganga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala, usajili wa vituo
vya kutolea huduma, nidhamu na maadili,
usimamizi na usajili wa bidhaa nyinginezo za Asili zinazotumika kwa ajili ya
afya ya binadamu.
Huduma ya Matibabu Nje ya Nchi
99. Mheshimiwa Spika, kama nilivyoahidi katika hotuba ya mwaka
jana, Wizara yangu imefanya mazungumzo na shirika la TOKUSHUKAI kutoka Japan na
limeahidi kutusaidia kujenga hospitali ya ubora wa hali ya juu itakayotumika
kutibu magonjwa mbalimbali yaliyokuwa yakitibiwa nje ya nchi yakiwemo magonjwa
ya moyo. Aidha, tunaendelea na mazungumzo na Serikali ya China na India ili
tupate hospitali nyingine za kiwango kama hicho.
Hospitali
za Rufaa na Hospitali Maalumu
Hospitali
ya Taifa Muhimbili
100. Mheshimiwa Spika,
hospitali iliendelea kutoa huduma kwa wagonjwa huku
ukarabati mkubwa ukiendelea katika hospitali hiyo. Aidha, hospitali hiyo
ilianzisha matibabu kwa wagonjwa 1,211 wa UKIMWI. Hata hivyo, huduma za upasuaji na maabara ya pathologia zilipungua kutokana na ukarabati unaoendelea
katika hospitali hiyo.
101. Mheshimiwa Spika,
kufuatia kukamilika kwa kazi ya Kamati ya Mpito, wafanyakazi wa
lililokuwa Shirika la Afya Muhimbili walipangwa ama Hospitali ya Taifa
Muhimbili au chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi za Afya (Muhimbili University
College of Health Sciences – MUCHS).
Hivi sasa Hospitali ya Taifa Muhimbili imeandaa muundo mpya wa utumishi
unaolingana na hali ya sasa na mabadiliko yanayoendelea katika hospitali hiyo
ya taifa.
102. Mheshimiwa Spika, hospitali hiyo, imeweza kutoa huduma muhimu bila ya
kulimbikiza madeni ya malipo ya kazi za ziada (overtime). Hospitali hiyo pia imefanikiwa kulipa madeni ya kazi
za ziada kwa watumishi ya tangu 2001. Hayo yaliwezekana
kwa sababu hospitali hiyo kutokana na juhudi za hospitali kuongeza ufanisi. Kuhusu makusanyo
katika mwaka 2004/2005 hospitali hiyo ya taifa ilikusanya zaidi ya shilingi
bilioni moja kutokana na huduma binafsi na uchangiaji
wa huduma za afya.
Hospitali
ya Bugando
103. Mheshimiwa
Spika, utekelezaji wa maboresho ya
huduma za afya uliendelea katika hospitali ya Bugando katika mwaka
2004/2005. Maboresho hayo yalilenga
katika ukarabati, utoaji mafunzo, utoaji wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI
(ARVs) na ujenzi wa kituo cha kanda cha kuhifadhi damu salama (zonal blood
bank) pamoja na kutoa
huduma ya kutembelea hospitali za nje (outreach services).
Aidha hospitali imeanzisha chumba cha kisasa cha kuhudumia
wagonjwa mahututi (intensive care unit).
104. Mheshimiwa
Spika, hospitali hii yenye jengo kuu
la hospitali lenye ghorofa 11 imefanya ukarabati wa
ghorofa 5, kwenye maeneo yanayotumika kwa kutoa huduma kwa wagonjwa. Ukarabati huo uliojumuisha wodi na chumba cha
upasuaji wa wazazi wenye matatizo uliogharimu shilingi 142,153,250 zilizopatikana kwa
msaada wa Japan/Tanzania Food
Counterpart Fund. Napenda kuchukua nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Serikali ya Japan
kwa msaada wao.
105. Mheshimiwa Spika, mafunzo
mahali pa kazi yalitolewa kwa wafanyakazi wa hospitali
wa vitengo mbalimbali ili kuboresha huduma zinazotolewa. Aidha wafanyakazi 45
walipelekwa kwenye mafunzo ya kujiendeleza vyuoni.
106. Mheshimiwa
Spika, hospitali ya Rufaa ya Bugando ilianza kutoa dawa za
kupunguza makali ya UKIMWI mwezi Oktoba 2004.
Wananchi wengi wamejitokeza na zoezi
linaendelea vizuri. Wagonjwa
1,000 wanahudhuria kliniki kati ya hao 300 ndio wako kwenye matibabu ya dawa za
kupunguza makali ya UKIMWI. Aidha
huduma za kuzuia maambukizi ya UKIMWI toka kwa mama kwenda kwa mtoto zinaendelea kutolewa.
107. Mheshimiwa
Spika, hospitali ya Bugando
imeanzisha mpango maalum kwa kushirikiana na AMREF wa
kupeleka Madaktari Bingwa kwenye hospitali za mikoa ya Kagera, Kigoma,
Shinyanga na Mwanza kila mwezi kutoa huduma za ubingwa.
Hospitali
ya KCMC
108. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/05, hospitali ya KCMC ilikamilisha
awamu ya kwanza ya upanuzi wa jengo la Idara ya
Wagonjwa wa Dharura. Jengo
109. Mheshimiwa
Spika, napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kwamba katika
kipindi cha mwaka 2004/05 nilizindua maabara kubwa ya Bio-Technolojia kwa ajili ya utafiti wa malaria katika hospitali ya KCMC.
Aidha, hospitali hiyo ilipokea vifaa vipya kwa ajili
ya Kitengo cha “Endoscopy” vyenye thamani ya shilingi millioni 300 kupitia
Bohari Kuu ya Madawa pamoja na kununua mashine ya kufulia. Vifaa hivyo
vimefungwa na vinatumika. Katika kipindi hicho,
hospitali hiyo ilianza uzalishaji wa hewa muhimu ya “oxygen” na hivyo
kuondokana na gharama za ununuzi wa hewa hiyo na ina uwezo wa kutoa huduma hiyo
ya oxygen kwa hospitali za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga.
110. Mheshimiwa
Spika, hospitali hiyo ilifanya upasuaji wa
kwanza kwa wagonjwa wa moyo 13. Upasuaji huo ulifanywa na
madaktari wa hospitali hiyo kwa kushirikiana na madaktari kutoka Chuo Kikuu cha
111. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/05, mafunzo ya uganga yaliendelea
kuongezeka
112. Mheshimiwa
Spika, Wizara yangu ilianza kutoa fedha kwa ajili ya huduma za
akina mama wenye matatizo ya VVF mwaka 2003/2004. Hadi hivi sasa jumla ya akina mama ……………….
wamefaidika na huduma hii muhimu. Wizara yangu itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya huduma hii.
Huduma
hii inatolewa na hospitali za Serikali pamoja na
Mashirika ya Dini nay a kujitolea ambayo ni Bugando, CCBRT, Selian Arusha na
Peramiho.
Hospitali
ya Rufaa Mbeya
113. Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka 2004/05
hospitali ya Rufaa Mbeya iliendelea kutoa huduma za tiba ngazi ya rufaa kwa
mikoa ya nyanda za juu kusini inayojumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na
114. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2004/2005 hospitali ilitekeleza
miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na:
·
Ujenzi wa kitengo cha
kuhudumia wagonjwa mahututi (intensive care unit),
·
Ukarabati wa wodi za
hospitali kuu,
·
Uwekaji wa mfumo wa maji
moto unaotumia mionzi ya jua kwa ajili ya kitengo cha wazazi
·
Uanzishaji wa ukusanyaji
wa damu salama, baada ya kukamilika kwa ujenzi wa kituo cha kanda,
·
Kuongeza idadi ya
madaktari wanaofanya mafunzo ya vitendo kwa mwaka
mmoja (intern doctors) kutoka
20 mpaka 45.
Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa (MOI)
115. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/05,
Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa (MOI) iliendelea kutoa huduma za kibingwa
za Tiba kwa wagonjwa wa mifupa na upasuaji wa mishipa
ya fahamu kwa ufanisi zaidi. Taasisi hii ilihudumia jumla ya wagonjwa 1,811
ambapo wagonjwa 1,577 sawa na asilimia 86 walikuwa wa kawaida, na wagonjwa 234
sawa na asilimia 14 walikuwa wa kulipia (private). Aidha, kutokana na kuendeleza mfumo wa kutibu wagonjwa wa kawaida na wa
kulipia (Public/Private Mix) Taasisi ilikusanya jumla ya shilingi 442,615,161
ambayo ni asilimia 13 ya mapato yote ya Taasisi. Fedha hii ilitumika kutoa motisha kwa wafanyakazi, kusaidia uendeshaji wa Taasisi.
116. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005 Taasisi ilianzisha huduma za
upasuaji ambazo awali hazikuwepo na ilibidi wagonjwa
waende kutibiwa nje ya nchi na hivyo kuigharimu Serikali fedha nyingi. Upasuaji huu ni pamoja
na ubadilishaji wa mifupa ya nyonga (total hip replacement) na pia
upasuaji wa ubongo. Aidha ili
kufanikisha upasuaji huo muhimu, Serikali ilinunua na kufunga
vitendea kazi katika vyumba vitano (5) vya upasuaji, vyumba vya wagonjwa
mahututi (ICU), majeruhi (casualty) na dharura.
Huduma ya ubadilishaji wa mifupa ya nyonga (total
hip replacement), ilitolewa na hadi
hivi sasa wagonjwa 32 wamebadilishiwa mifupa ya nyonga, na viungo bandia 446
vilitengenezwa na kutolewa kwa wagonjwa. Aidha, tanuru (incinerator)
la kuchomea taka lilijengwa.
Taasisi ya Saratani ya
117. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005, Taasisi ya Saratani ya
Hospitali
ya Kibong’oto
118. Mheshimiwa
Spika, hospitali ya Kibong’oto ni hospitali maalum kwa ajili ya kutibu ugonjwa wa Kifua
Kikuu ulioshindikana kutibiwa katika hospitali nyingine. Hospitali pia hutoa
huduma kwa wananchi wenye magonjwa ya kawaida. Katika mwaka wa
2004/05 hospitali ya Kibong’oto imeendelea kutoa huduma kwa wagonjwa wa kifua
kikuu waliopewa rufaa toka hospitali za mikoa hasa ya Arusha, Kilimanjaro,
Tanga,
Hospitali
ya Mirembe na Taasisi ya Isanga
119. Mheshimiwa Spika,
katika mwaka wa 2004/2005 Hospitali ya Mirembe na
Taasisi ya Isanga ilitekeleza miradi ya maendeleo na shughuli za kawaida
·
Ukarabati wa wodi tatu
za wagonjwa,
·
Ukarabati wa mfumo wa
maji taka katika Taasisi ya Isanga,
·
Ujenzi wa ukuta wa ngome
ya wanawake katika Taasisi ya Isanga pamoja na kuweka taa za usalama/ulinzi,
·
Ukarabati wa jengo la
kutolea huduma za kinywa na meno,
·
Ujenzi wa tanuru la kuchomea taka ngumu (incinerator).
·
Utoaji wa mafunzo ya kuboresha ujuzi wa watumishi wa kuzuia
maambukizi yanayotokana na kuchomwa na vitu vyenye ncha kali
·
Ununuzi wa dawa muhimu,
vifaa tiba na vifaa vya usafi vya kutosha,
·
Wauguzi 70 walipatiwa
mafunzo ya kuzuia maambukizi, kwa wagonjwa wanapokuwa
wodini (Hospital Acquired Infecious).
·
Chuo cha uuguzi Mirembe
kilitoa stashahada kwa wataalamu 40 wenye taaluma ya
kuhudumia wagonjwa wenye magonjwa ya akili.
·
Kutoa elimu kuhusu
madhara ya dawa za kulevya kwa wanafunzi wa shule zilizofanyiwa utafiti,
·
Makusanyo ya fedha za
uchangiaji huduma za afya yaliongezeka kutoka shilingi millioni 3.6 mwaka
2003/04 hadi shilingi millioni 5.1 mwaka 2004/05. Fedha hii ilitumika kufanyia
ukarabati wa majengo pamoja na kununulia dawa muhimu za ziada.
HUDUMA
ZA UTAWALA NA UTUMISHI
120. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2004/2005, Wizara ya Afya
imeendelea kutekeleza sera ya menejimenti na ajira
katika utumishi wa umma ya mwaka 1999, kwa kuajiri jumla ya watumishi 148 wa
kada mbalimbali za afya. Aidha katika kushughulikia maslahi na
maendeleo ya watumishi ili kuimarisha utendaji kazi Wizara ya Afya
imewapandisha vyeo watumishi 6,587. Hili ni ongezeko
la asilimia 65 ya lengo lililokuwa limewekwa la kuwapandisha vyeo watumishi
4000.
121. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005 watumishi 110 wa kada na ngazi tofauti walifanyiwa upekuzi (vetting) kwa
madhumuni ya kuwawezesha kuelewa na kuzingatia misingi ya maadili mema katika
utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Msisitizo
mkubwa uliowekwa katika mafunzo hayo ulihusu suala zima la matumizi sahihi ya
taarifa za Serikali na utii kwa Serikali. Aidha Wizara
iliendelea kutoa mafunzo ya jinsia kwa watumishi ili
kuendelea kudumisha Utawala Bora. Jumla ya watumishi 744
walipatiwa mafunzo hayo.
122. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2004/2005 Wizara ya Afya ilitoa
mafunzo kwa maafisa waandamizi na wa ngazi ya kati
kuhusu misingi ya Utawala Bora na mapambano dhidi ya rushwa ili kuzuia matukio
ya rushwa na kuziba mianya ya rushwa. Mafunzo haya yaliwahusisha Wakurugenzi wa Wizara ya Afya, Waganga Wakuu wa Mikoa, Waganga Wakuu wa
Wilaya, Wakuu wa Vyuo vyote vya Afya nchini na Maafisa wengine. Jumla ya watumishi 1,169 walipatiwa mafunzo hayo.
123. Mheshimiwa Spika,
sambamba na mapambano dhidi ya rushwa, Wizara ilichapisha
vijarida vya Mkataba wa Huduma kwa Mteja na kuvisambaza kwa wadau. Lengo
lilikuwa kuwafahamisha wateja wetu mahusiano na
majukumu yetu kwao pamoja na haki na wajibu wao. Mkataba huu unaelekeza pia
namna mteja anavyoweza
kutoa malalamiko/maoni kuhusu huduma zetu.
HUDUMA
YA MAFUNZO
124. Mheshimiwa Spika, katika
kipindi 2004/2005, jumla ya wanafunzi 214 walihitimu mafunzo katika ngazi ya
Shahada wakiwemo Madaktari, Madaktari wa Meno,
Wafamasia Maafisa Afya Mazingira na Wauguzi. Mchanganuo wake ni
125. Mheshimiwa Spika, Jumla
ya wanafunzi 2,803 walihitimu fani za Sayansi ya Afya na
Uuguzi katika vyuo vyote vya mafunzo hapa nchini. Jumla ya wanafunzi 1,481 walihitimu kutoka vyuo vya
Serikali na 1,322 walihitimu kutoka vyuo vya Mashirika ya dini na Binafsi. Wanafunzi 2,820 walipata nafasi ya mafunzo
katika vyuo vya Sayansi ya Afya na Uuguzi. Wakati huo huo wanafunzi 1,490 kati ya hao
walipata nafasi katika vyuo vya Serikali na 1,330
walipata nafasi katika vyuo vya Mashirika ya Dini na Binafsi. Aidha, jumla ya Waganga Wasaidizi Vijijini 52
walihitimu mafunzo ya Maafisa Tabibu (Clinical Officer) kwa kupita mafunzo yanayotolewa kwa
njia ya posta na 253 walihitimu kupitia vyuo vya serikali na vya Mashirika ya
dini. Jumla ya wahitimu wa Maafisa Tabibu walikuwa 305.
126. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutoa mafunzo ya kujiendeleza mahali pa kazi kwa watumishi
wake ili kuinua na
kutoa huduma bora kwa
wateja. Katika kipindi 2004/2005 jumla
ya watumishi 492 wa kada mbalimbali za afya
wamepata mafunzo ya stadi ya
kuwahudumia wagonjwa wanaotumia dawa za kupunguza makali ya UKIMWI (Anti-Rentro
Viral). Aidha, Watumishi katika
hospitali 68 wakiwemo madaktari wafawidhi wa
hospitali, Wauguzi waandamizi na Wafamasia walipata mafunzo ya kujiendeleza
kuhusu matumizi sahihi ya dawa hizo.
127. Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa
ngazi ya mkoa katika usimamizi na utoaji huduma kwa Halmashauri, Wizara ya Afya
imetoa mafunzo ya kuimarisha utendaji kwa ujumla kwa watumishi 72 kutoka katika timu za afya za mikoa ((RHMT) 9 ya
Tanga,
128. Mheshimiwa Spika, katika
kuboresha mafunzo yanayotolewa katika vyuo vya Afya hapa nchini, Wizara
imevifanyia ukarabati vyuo 32 na kuanza ujenzi wa
majengo ya Chuo cha CEDHA. Sambamba na
ukarabati wa vyuo, huduma ya ukaguzi wa vyuo unaozingatia usafi wa mazingira,
ubora wa viwango vya masomo yanayotolewa, mafunzo ya vitendo ulifanyika kwa
vyuo 54. Katika kipindi 2004/2005 vyuo 7
kati ya vyuo vya mafunzo 110 vimepatiwa ithibati (accreditation) na Baraza la Elimu ya Ufundi (National Council for Technical
Education – NACTE). Aidha,
vyuo vilivyobaki 103 viko katika hatua mbalimbali za kupata ithibati.
OFISI
YA MGANGA MKUU KIONGOZI
Huduma
za Dharura na Maafa
129. Mheshimiwa
Spika, Wizara imeendelea kujiandaa kukabiliana na dharura na maafa mbalimbali yanayoweza kutokea katika
nchi yetu wakati wowote. Katika kipindi cha mwaka 2004/2005, Wizara yangu
imefanya ufuatiliaji wa huduma za dharura na maafa
katika mikoa ya Singida, Iringa, Manyara, Pwani, Mtwara na
130. Mheshimiwa Spika, mafunzo ya jinsi ya
kukabiliana na dharura na maafa yalitolewa kwa wajumbe
wa Kamati za Uendeshaji za Huduma za Afya za Mikoa (RHMT) katika mikoa ya
Kigoma, Tabora, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara na Pwani. Mafunzo haya pia
yametolewa kwa baadhi ya wafanyakazi wa afya, walioko katika hospitali za mikoa
ya Mwanza, Mara, Pwani na Singida. Aidha mafunzo maalumu ya jinsi ya kutumia
mwongozo wa kukabiliana na dharura na maafa (emergency operations plan)
yalitolewa kwa watumishi wa afya, walioko katika hospitali ya Taifa ya
Muhimbili, Singida, Iringa, Manyara, Pwani, Mtwara na Ruvuma. Mikoa mingine ni Kilimanjaro,
Arusha na Tanga. Wizara pia ilichapisha na kusambaza vitabu viwili vya miongozo ya
utoaji wa huduma za dharura na maafa (health sector guidelines and protocol
on emergency and disaster management) na mpango wa uendeshaji huduma za dharura
(emergency operations plan - EOP) nakala 1,000 kila kimoja.
Huduma
za Uuguzi
131. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005, Wizara ya Afya imetayarisha
Mwongozo wa kuzuia maambukizi kwa
watoaji wa huduma kutoka kwa wagonjwa walioathirika na virusi vya UKIMWI.
Nakala 8,000 za mwongozo huu
zimetayarishwa na zitasambazwa katika Halmashauri zote nchini. Aidha, Wizara imefanya ukaguzi wa huduma za
afya za uuguzi na ukunga katika mikoa ya
Morogoro, Ruvuma, Tabora, Mtwara, Lindi, Mbeya, Shinyanga na Singida.
Taarifa ya usimamizi huo ilionyesha kuwa kuna upungufu wa vifaa na watumishi
katika hospitali zote. Wizara inaitumia
taarifa hii kuwasiliana na Halmashauri husika kuhusiana na upungufu huu.
Mabaraza ya Kitaaluma
132. Mheshimiwa Spika, mwaka 2004/2005 Baraza la Madaktari na Baraza la
Wauguzi na Wakunga yalifanya uchunguzi (inquiries) wa makosa ya ukiukwaji wa
maadili na miiko katika utendaji kazi kwenye hospitali nne (4) za Morogoro, Mt
Meru Arusha, Temeke na hospitali ya Ligula Mtwara. Watumishi 5 waliobainika na
makosa walichukuliwa hatua za kinidhamu, wawili walipewa onyo, wawili
walisimamishwa na mmoja alifutiwa usajili.
Aidha Baraza la Famasia liliandaa mwongozo wa kusajili wafamasia wa
ndani na nje ya nchi), na mwongozo wa
mafunzo kwa Wafamasia wanaofanya mazoezi ya vitendo baada ya kuhitimu mafunzo
ya shahada ya Ufamasia. Mabaraza mengine
yakiwemo Hospitali Binafsi, Mafundi Sanifu Maabara na Waganga wa Tiba Asili
yaliendelea kufanya kazi za kitaaluma na kuisaidia Wizara katika kuboresha
huduma za afya.
WAKALA ZILIZO CHINI YA WIZARA YA AFYA
Mamlaka ya
Chakula na Dawa (TFDA)
133. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2004/2005 jumla ya aina 279 za dawa za binadamu aina 12 za dawa za mifugo
na aina 22 ya bidhaa za vyakula zilisajiliwa.
Katika jitihada ya kuhakikisha kuwa vyakula, vipodozi na
vyakula dawa vimesajiliwa kwa kuhakiki usalama wake kwa watumiaji. Mamlaka imebaini aina 5066 za vyakula, aina
26 za dawa na aina 921 za vipodozi
havijasajiliwa. Jumla ya maombi
17 ya kusajili dawa zitokanazo na mimea yalipokelewa
na yanaendelea kufanyiwa tathmini.
Sampuli 767 zilizofanyiwa uchunguzi wa
kimaabara, sampuli 608 zilikidhi viwango na 159 hazikukidhi viwango. Bidhaa ambazo hazikukidhi viwango ziliondolewa
katika soko na kwa zile ambazo zilikuwa zinaombewa
usajili, cheti cha usajili hakikutolewa na hivyo kutokuruhusiwa kuingizwa
katika soko la
Aidha,
Mamlaka imeendelea kuhakikisha kuwa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kwa wagonjwa wa UKIMWI, zinazoingizwa nchini ni bora, salama
na zina ufanisi unaofikia viwango vinavyotambulika kimataifa. Aidha matukio 42
ya madhara yaliyoshukiwa kutokana na matumizi ya dawa
yametolewa taarifa kwa usahihi na kufanyiwa tathmini ili kutambua madhara
yaliyotokea
134. Mheshimiwa Spika, Mamlaka imefanya ukaguzi katika jumla ya maduka 630
ya dawa, 70 ya vipodozi, maduka 39 ya vyakula, viwanda 183 vya chakula na 72 vya dawa (66
vya nje, na 6 vya ndani). Jumla ya maombi 3,474 ya vibali vya
kuingiza bidhaa nchini yalipokelewa. Vibali 3117 kwa
ajili ya kuingiza vyakula na dawa vilitolewa.
Maombi 357
yalikataliwa.
135. Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na
tatizo la ukiukwaji wa sheria unaofanywa katika maduka ya dawa baridi, Mamlaka
imeanzisha maduka 41 ya dawa muhimu (Accredited Drug Dispensing Outlets –
ADDO) mkoani
136. Mheshimiwa
Spika, katika kuelimisha wadau na
kuboresha upashanaji habari mwaka 2004 Mamlaka ilizindua tovuti www.tfda.or.tz. Pia mafunzo ya wadau 515 yanayofafanua sheria
na majukumu ya TFDA yalifanyika katika kanda za Kusini
na Kaskazini.
137. Mheshimiwa
Spika, ili kusogeza huduma karibu
na wananchi Mamlaka imefungua ofisi za kanda katika mikoa ya Mwanza na Arusha.
Mamlaka pia imeimarisha maabara kwa kununua vifaa vya kisasa vya maabara na
kusomesha baadhi ya wafanyakazi wake ili
kuongeza ufanisi na uwezo wao wa kuchunguza na kupima vipimo mbalimbali vya
vyakula, dawa na vipodozi kwa viwango vya kitaifa na kimataifa.
Huduma
za Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali
138. Mheshimiwa Spika, Wakala ulichunguza jumla ya sampuli 8,147 na kutoa matokeo katika wastani wa siku 14
kama ilivyoainishwa katika Mkataba wa Huduma kwa Mteja na kupata jumla ya
shillingi 193,344,842. Kati ya sampuli zilizochunguzwa sampuli 3,934 zilikuwa ni
za vyakula, dawa, maji, maji taka, kemikali na mazao yake. Sampuli 4,213
zilikuwa ni za madawa ya kulevya na
makosa mengine ya jinai. Idadi ya sampuli za madawa ya kulevya na makosa
mengine ya jinai zilizochunguzwa iliongezeka kutoka sampuli 3,718 mwaka 2003,
hadi 4,213 mwaka 2004 ambazo ni ongezeko
la asilimia 13. Matokeo ya uchunguzi huo
yamesaidia mamlaka zinazohusika kuchukua hatua zinazostahili na kuharakisha usikilizaji wa kesi na utoaji
haki.
139. Mheshimiwa Spika, katika kusimamia na kudhibiti kemikali zinazotumika
Viwandani na Majumbani, Wakala umepokea
na kushughulikia maombi 150 ya usajili wa kemikali kutoka kwa wadau mbalimbali
wa Tanzania Bara. Vibali 365 kwa ajili ya uagizaji na uingizaji wa
kemikali kutoka nje ya nchi vilivyotolewa.
Mafunzo kwa wakaguzi 92 wa kemikali nchini yalifanyika.
140. Mheshimiwa Spika, ili kusogeza huduma karibu na wananchi, Wakala wa
Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali
tarehe 7/01/2005 ilizindua rasmi maabara ya kwanza ya kanda jijini Mwanza. Kuanzishwa kwa Maabara
hii kumesaidia kuondoa kero ya
kusafirisha sampuli na gharama kubwa inayohitajika kwa mteja kufika Dar es
Salaam ili kufuatilia matokeo ya uchunguzi.
MIPANGO, MAJUKUMU NA MALENGO YA
BAJETI YA MWAKA 2005/2006
MIRADI YA MAENDELEO
141. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2005/2006,
Wizara yangu inaomba kiasi cha shilingi 90,862,748,400
kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hiyo shilingi 5,000,000,000 ni fedha
za ndani na shilingi 85,862,748,400
ni kutoka Taasisi za Kimataifa na Wahisani wanaochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya (Basket Fund – BF) na
wale walioko nje ya mfuko.
142. Mheshimiwa Spika, fedha zilizoainishwa hapo juu
zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo ifuatavyo:-
·
Kuendeleza
ukarabati na upanuzi wa Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili na hospitali za Jiji la Dar es Salaam (
·
Ukarabati wa wodi, maabara, chumba cha upasuaji na kuendeleza ujenzi
wa hosteli ya madaktari wanafunzi (intern’s doctors) katika hospitali ya
Rufaa Mbeya.
·
Kuendeleza
ukarabati wa wodi, nyumba za watumishi na jiko katika
hospitali maalum ya Mirembe na Taasisi ya Isanga.
·
Kukarabati wodi
6, nyumba za watumishi 3, mfumo wa maji taka, kuanza kujenga nyumba 3 za
watumishi na kuendeleza ujenzi wa maabara ya kuchunguza vimelea sugu vya ugonjwa
wa Kifua Kikuu, kuandaa eneo kwa ajili ya kusimika mashine za kutakasia vikombe
vya makohozi ili kuzuia uambukizo wa magonjwa ndani ya hospitali na ununuzi wa
vifaa kwa ajili ya hospitali maalum ya Kifua Kikuu ya Kibong’oto.
·
Kuendeleza ujenzi
wa wodi ya watoto katika hospitali ya Taifa ya
Muhimbili.
·
Kukarabati wodi
za wagonjwa hospitali ya
·
Kutoa mchango wa
Serikali (counterpart funds) kwa ajili ya kuendeleza ukarabati wa
majengo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, ujenzi wa hospitali mpya maalum Dar es
Salaam itakayojengwa kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania na Shirika la
TOKUSHUKAI la Japani na maandalizi ya ujenzi wa hospitali ya rufaa Kanda ya
Kusini – Mtwara.
·
Kukamilisha
ujenzi wa maabara ya kudhibiti ubora (quality control
laboratory) Makao Makuu ya Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali pamoja na
ununuzi wa vifaa na kemikali kwa ajili ya maabara mpya ya Mwanza.
·
Ukarabati wa
vituo vya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Amani, Gonja, Mwanza, Tukuyu na ofisi za
Makao Makuu –
·
Ukarabati wa jengo la Ofisi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
·
Kuendeleza
ukarabati wa vyuo vya afya 35.
·
Kununua vifaa
tiba kwa hospitali za Rufaa na hospitali maalum.
SERA NA MIPANGO
Mabadiliko katika Sekta ya Afya
143. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
itaendelea kuelimisha na kuhamasisha Halmashauri na jamii kuhusu haki na wajibu
wao katika mabadiliko yanayoendelea kwa njia
zifuatazo:
·
Vipindi na matangazo katika
redio na televisheni, mkazo utawekwa
zaidi katika kutumia redio za kanda zilizoko mikoani.
·
Kuziwezesha Halmashauri kujenga
uwezo wa vyombo vya uwakilishi wa jamii (Bodi
na Kamati za Vituo vya huduma za Afya) wa kuelimisha na kuhamasisha
wananchi, ili jamii iendelee kuunga mkono mabadiliko, kuelekeza juhudi zao
katika Mfuko wa Afya ya Jamii – CHF, umiliki, usimamizi na ufuatiliaji wa
utoaji huduma za Afya katika maeneo yao.
·
Kutengeneza na kusambaza nyenzo
na vielelezo mbalimbali (vipeperushi,
vijitabu, mabango, na majarida) vyenye ujumbe wa kuelimisha na kuhamasisha
mabadiliko katika Sekta ya Afya kwa Halmashauri, vituo vya kutoa huduma za afya
na Watendaji wa Kata, Mitaa na Serikali za Vijiji.
144. Mheshimiwa Spika, Mabadiliko
katika Sekta ya Afya, yanahitaji mabadiliko ya tabia, mwenendo, mwelekeo,
mazoea, desturi na masuala yote yanayohusu mwenendo mzima wa mfanyakazi. Kwa
kuwa utaratibu wa mabadiliko ya kitabia huchukua muda mrefu, Wizara yangu
itaendelea kuwaelimisha na kuwahamasisha
wafanyakazi wa afya watambue umuhimu wa mabadiliko, wajibu na majukumu yao
katika ngazi zote za utekelezaji kwa njia za: mafunzo, mikutano na majadiliano,
mapitio ya utekelezaji wa mabadiliko, vijitabu, majarida na vipeperushi.
Mfuko wa Afya ya Jamii
145. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2005/06 Wizara,
itatekeleza yafuatayo:
·
Kutoa mafunzo ya
njia bora za kufanya makisio ya makusanyo,
·
Kuendelea kuhamasisha jamii kuhusu CHF,
·
Kutoa mafunzo
yanayohusu utunzaji na matumizi bora ya fedha za CHF kwa kufuata miongozo,
·
Kushirikiana na
mikoa kuteua waratibu wa CHF wa mikoa na Halmashauri chini ya Kamati za
uendeshaji huduma za afya za mikoa
- (RHMT) na za Halmashauri (CHMT) ili wawe kiungo kati ya
Wizara, Mikoa na Halmashauri.
146. Mheshimiwa
Spika, kwa mwaka 2005/06 Wizara
imepanga kuhamasisha na kuziwezesha Halmashauri zote za Miji/Manispaa/Jiji
kuanzisha mpango wa Tiba kwa Kadi – TIKA.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya
147. Mheshimiwa Spika, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba katika
mwaka wa 2005/06, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya utatekeleza yafuatayo:
·
Kuanza kutekeleza mpango mkakati wa miaka mitano ambao
umetoa kipaumbele katika upatikanaji wa huduma za matibabu hususani vijijini
ambako zaidi ya asilimia 70 ya wanachama wa Mfuko huu wanaishi.
·
Kuongeza idadi ya wanufaika wa
Mpango huu hadi kufikia asilimia 5 ya Watanzania wote.
·
Kuboresha kitita cha mafao
pamoja na kurahisisha upatikanaji wa mafao hayo.
·
Kushughulikia suala zima la
upatikanaji wa dawa hasa vijijini kwa ushirikiano na wadau na mamlaka husika.
·
Kuanzisha mashindano na kutoa
tuzo kwa vituo vya matibabu vitakavyotoa huduma bora kwa wanachama.
Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa
Huduma za Afya (MTUHA) na Utafiti
148. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006,
Wizara yangu itaunganisha mfumo wa kompyuta uliopo makao makuu ya Wizara na
mifumo iliyopo mikoani na katika hospitali za mikoa na za rufaa. Lengo kuu ni kurahisisha ubadilishanaji wa
taarifa mbalimbali zikiwemo takwimu za afya.
149. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu itaboresha mfumo wa
kukusanya takwimu za afya katika ngazi ya Wilaya. Mfumo huu unalenga kuhakikisha kuwa takwimu
zinazokusanywa kutoka vituo vya kutolea tiba zinaingizwa kwenye kompyuta Wilayani na kupelekwa moja kwa moja Makao
Makuu. Aidha, kukusanya takwimu kutoka
vituo vya afya peke yake hakutupatii taswira halisi ya hali ya afya nchini. Kutokana na umuhimu wa ukusanyaji wa takwimu
kutoka katika Jamii, Wizara yangu itaboresha mfumo huu ili matokeo ya mifumo hii miwili ya ukusanyaji
takwimu iweze kutoa taswira ya hali halisi ya nchi nzima.
MATUMIZI YA KAWAIDA
IDARA YA
KINGA
150. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2005/2006 Wizara yangu inaomba kiasi cha
shilingi 180,305,853,900. Kiasi cha shilingi 6,406,945,600
ni kwa ajili ya mishahara na kiasi cha shilingi 173,898,908,200 kwa ajili ya
matumizi ya kawaida. Fedha hii itatumika
kutekeleza kazi zifuatazo:
Udhibiti wa Magonjwa ya Kuambukiza (Epidemiologia)
151. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/06 Wizara itaendeleza udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza magonjwa ya
milipuko na kutoa mfunzo ya ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa kwa wataalamu
wa afya.
Mpango wa
Taifa wa Kudhibiti Malaria
152. Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada kubwa
zinazofanyika ili kudhibiti ugonjwa wa malaria nchini, kuna wilaya 24 ziko
katika hatari ya kupata milipuko ya ugonjwa wa malaria. Wilaya hizo ni Mufindi,
Makete, Njombe, Rungwe, Mbozi, Ileje, Mbinga, Ilolo, Ludewa, Same, Hai, Dodoma,
Mpwapwa, Kongwa, Lushoto, Korogwe, Hanag, Babati, Karatu, Ngorongoro, Nkasi,
Sumbawanga, Karagwe na Muleba. Wizara yangu katika mwaka wa fedha 2005/06
imeandaa mikakati ya kuziweka wilaya hizo zenye uwezekano wa kupata milipuko ya
malaria katika hali ya tahadhari ya kutabiri milipuko
na kudhibiti milipuko hiyo kwa kuwafundisha watendaji wa Wilaya jinsi ya
kutumia takwimu za wagonjwa, kuangalia kuzaliana kwa mbu na kiasi cha mvua na
hali ya joto.
153. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha 2005/06 Wizara yangu itaendelea na
maandalizi ya kubadilisha matibabu ya malaria kutoka dawa ya SP kwenda
dawa mseto ya Artemether/Lumefantrine (ALU/Coartem). Shughuli zitakazofanyika
katika maandalizi hayo ni kubadili mwongozo wa matibabu pamoja na kuendesha
mafunzo kwa watoa huduma za afya kuhusu tiba mpya na kuelimisha jamii. Baada ya
maandalizi hayo kukamilika, tutaanza kutumia dawa mseto mara moja.
Mpango wa
Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma
154. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha 2005/06 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma utaendeleza
kampeni za kutokomeza ukoma katika mikoa ya Ruvuma, Morogoro na Tanga. Aidha
shughuli za kuhuisha rejesta za wagonjwa wa ukoma zitaendelea sambamba na kampeni ya kutokomeza ukoma ili
kufikia lengo la kimataifa la mgonjwa
mmoja kwa kila watu 10,000 ili kufikia lengo hilo ifikapo Desemba mwaka 2005.
Mpango utaendelea kuimarisha huduma za pamoja za kudhibiti Kifua Kikuu na
UKIMWI na zile za kudhibiti Kifua Kikuu sugu ili kisienee nchini.
155. Mheshimiwa Spika, Wizara
itaendelea kuagiza na kusambaza dawa za kutosha za Kifua Kikuu na Ukoma katika
vituo vyote vya matibabu nchini. Aidha Mpango utaendelea kuelimisha jamii kwa
kutumia njia zote za upashanaji habari.
Aidha, mpango utaendelea kuelimisha jamii jinsi ya kujikinga na
maambukizi, kutambua mapema dalili za ugonjwa
na taratibu za kufuata wakati wa matibabu ya magonjwa ya kifua kikuu na ukoma.
156. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
itaanzisha huduma kwa wagonjwa wenye Kifua Kikuu sugu (Multi Drug Resistant
- TB) katika hospitali ya Kibong’oto iliyoko wilayani Hai. Aidha, Wizara
yangu itaanzisha mpango wa kutumia dawa za mseto (four Fixed Dose
Combinations) kutibu Kifua Kikuu.
Mpango huu utaanzishwa katika
wilaya 6 za mwanzo kwa majaribio. Mabadiliko haya yana lengo la kupunguza wingi
wa dawa anazotumia mgonjwa na kupunguza usugu wa vimelea vya Kifua Kikuu. Aidha
tutaendelea na utekelezaji wa mpango wa pamoja wa kudhibiti uambukizo wa kifua
kikuu na UKIMWI katika wilaya za Temeke, Korogwe na Manispaa ya Iringa.
Mpango wa Taifa wa Kudhibiti
UKIMWI
157. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
katika mwaka wa fedha 2005/2006
itaendelea kufuatilia mwenendo wa maambukizi ya virusi vya UKIMWI katika jamii kwa
kuwafuatilia wajawazito katika kliniki 93 zilizopo kwenye mikoa 15 ya Tanzania
Bara. Matokeo ya ufuatiliaji huu yatatoa taswira ya kuenea kwa virusi vya
UKIMWI katika jamii na kusaidia kuimarisha
mikakati ya udhibiti.
158. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha 2005/06 Wizara yangu itakamilisha mwongozo wa ufuatiliaji wa usugu wa
virusi vinavyosababisha ugonjwa wa UKIMWI kwa dawa zinazotumika hivi sasa
kupunguza makali ya UKIMWI, na kuanzisha ufuatiliaji wa wagonjwa katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo dawa za
kupunguza makali ya UKIMWI zilianza kutumika kabla ya Serikali kuanza mpango wa
kutoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kwa wagonjwa wa UKIMWI. Matokeo yake
yatasaidia katika kujua aina ya dawa
ambazo tayari virusi vya UKIMWI
vinaonyesha kuwa sugu kwa dawa hizo na hivyo kutopunguza tena makali ya
ugonjwa wa UKIMWI kwa watumiaji na hivyo kusaidia wataalamu kutoa maelekezo ya
dawa zinazofaa.
159. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu itanunua na kusambaza dawa za kupunguza makali ya UKIMWI
katika vituo 198 vilivyoteuliwa kutoa huduma hiyo vikijumuisha vituo 96 vya
mwaka jana na 102 vipya ili kuwafikia wagonjwa wapya 56,000 kwa nia ya kufikia
lengo jipya lililowekwa na mpango la kuwafikia wagonjwa 100,000 nchini kote
ifikapo Desemba 2006. Vituo vipya vitakavyohusishwa katika mpango huu ni pamoja
na hospitali zote za wilaya na hospitali zisizo za Serikali zilizoko kwenye
mikoa ya pembezoni na mikoa iliyo na viwango vya maambukizi ya UKIMWI zaidi ya
asilimia saba. Mikoa hiyo ni Tabora,
Mwanza, Kilimanjaro, Pwani, Mtwara, Dar es Salaam, Iringa na Mbeya. Aidha
Serikali kwa mwaka 2004/2005 imetenga shilingi 20,000,000,000/=
kwa ajili ya ununuzi na usambazaji wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na
shilingi 4,291,856,000 kwa ajili ya ununuzi, usambazaji wa vifaa tiba pamoja na
kazi zote za kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI.
160. Mheshimiwa Spika, Wizara
itaendelea kutoa huduma za ushauri nasaha na upimaji wa hiari katika vituo 521
vinavyotoa huduma hii ili kutoa ushauri nasaha kwa wagonjwa wote 100,000
watakaokuwa kwenye tiba ya dawa za UKIMWI ifikapo Desemba, 2006. Aidha mafunzo kwa wataalam wa kutoa huduma ya
dawa za kupunguza makali ya UKIMWI katika kila kituo yanatolewa kwa wataalam
wanne ambao wanatakiwa kuwa katika kila kituo cha kutolea huduma hii.
161. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
itaendelea kutoa huduma kwa magonjwa ya zinaa katika mikoa yote 21. Pia itaendelea kuelimisha jamii kuhusu
ugonjwa wa UKIMWI, kupiga vita
unyanyapaa na kuzingatia matumizi sahihi ya dawa za kupunguza makali ya ugonjwa
wa UKIMWI.
Mpango wa Taifa wa Huduma za
Macho
162. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha 2005/2006, Wizara yangu inatarajia kuongeza wilaya 10 zaidi katika mpango
wa kudhibiti ugonjwa wa vikope nchini kwa kutumia mtindo mpya wa “District
Wide-Approach”. Wilaya 8 kati ya hizo zinatarajiwa kutoa dawa ya Zithromax kwa
wananchi. Wilaya zitakazojumuishwa katika mpango huo ni Kongwa, Kilosa, Meatu,
Iramba, Singida vijijini, Igunga, Simanjiro, na Mkuranga. Wananchi wapatao 2,300,000 wanatarajiwa kupata matibabu na kinga ya ugonjwa wa
vikope.
163. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha 2005/2006, Wizara yangu inatarajia kugawa dawa ya “Mectizan” kwa ajili ya
tiba ya ugonjwa wa usubi (mass treatment) kwa wananchi wapatao 3,000,000 katika vijiji 690 vilivyopo katika wilaya 15 za
Ulanga, Kilombero, Kilosa, Songea, Mbinga, Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela,
Muheza, Mvomero, Morogoro vijijini, Korogwe, Lushoto, na Ileje.
Huduma ya Afya ya Uzazi na Mtoto
164. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006, Wizara yangu itaendelea kuboresha huduma za afya
ya uzazi na mtoto bila malipo katika vituo vya Serikali vya kutolea huduma na
zitatolewa bila malipo. Huduma hizi ni
pamoja na matibabu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, chanjo, uzazi
wa mpango, huduma kwa wanawake wajawazito watakaohudhuria kliniki na
kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma.
Aidha, Wizara yangu itaendelea kununua na kusambaza dawa za uzazi wa
mpango nchi nzima. Wizara imetenga fedha kiasi cha shilingi billioni 6.8 kwa
ajili ya kununulia dawa za uzazi wa
mpango na kuzisambaza.
165. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006, Wizara yangu imepanga kutoa mafunzo mbalimbali katika maeneo ya
uzazi wa mpango, uzazi salama na afya ya
uzazi kwa vijana katika mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Mtwara, Morogoro,
Lindi, Mbeya, Mwanza na Pwani.
Udhibiti wa Magonjwa ya Watoto
kwa Uwiano (IMCI)
166. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006 Wizara yangu itatekeleza
mkakati wa IMCI ili kupunguza vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka
mitano. Wizara inatarajia kutoa mafunzo
ya stadi za kutibu watoto kwa watoa huduma za afya katika ngazi ya zahanati na
vituo vya afya. Pia mafunzo maalum yatatolewa kwa watoa huduma za afya kwa
wakufunzi 60 na watoa huduma za afya 220.
Aidha, wakufunzi 60 watakaofundishwa wataendelea kutoa mafunzo katika
Halmashauri zao. Mkakati huu pia unalenga kuendeleza mienendo inayoboresha afya
ya mtoto katika ngazi ya jamii na kaya.
Mpango wa Taifa wa Chanjo
167. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006, Wizara yangu kwa kushirikiana na mikoa itaendelea kusimamia huduma
ya chanjo katika ngazi ya wilaya. Wizara
yangu itaendelea kutoa vitendea kazi na chanjo ili kuhakikisha watoto wote
wanaostahili chanjo wanapata chanjo.
Aidha juhudi zaidi zitaelekezwa katika kutokomeza polio, kupunguza
ugonjwa wa surua, kufuta pepopunda kwa watoto wachanga na hivyo kupunguza vifo.
Wizara yangu pia itaendelea kufanya tathmini ya magonjwa mengine yanayozuilika
kwa chanjo ambayo chanjo zake hazijaanza kutumika hapa nchini.
Huduma za Afya Shuleni
168. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006 Wizara itatoa mafunzo ya huduma ya kwanza kwa waratibu 80 wa afya
shuleni wa ngazi ya wilaya na mikoa kwa mikoa ya Rukwa, Mbeya na Iringa. Aidha
kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na
Wizara ya Elimu na Utamaduni tutachapisha na kusambaza kadi za kupima afya za
wanafunzi wa shule za awali na sekondari.
Mpango wa utoaji dawa za kichocho /minyoo kwa wanafunzi utatekelezwa katika mikoa 7 iliyoathirika
zaidi ya Mwanza, Mara, Tabora, Kagera, Shinyanga, Kigoma na Tanga.
Afya ya
Mazingira
169. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006, Wizara inakusudia kuanzisha mashindano ya kupata vijiji bora katika
wilaya 5, kila wilaya itatoa kijiji bora kimoja kitakachokidhi mahitaji yote ya kiafya. Vijiji vyote katika wilaya moja vitashindanishwa ili kupata kijiji bora
kimoja kwa kila wilaya. Aidha Wizara itaendelea kushirikiana na Wizara mbali
mbali, jumuia za kimataifa, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) na jamii
katika kupanga mipango shirikishi jamii ili kuboresha hali ya afya na usafi wa
mazingira katika mikoa yote.
170. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
itaendeleza mashindano ya afya na usafi wa mazingira nchini, ambayo yataendelea
kujumuisha Halmashauri zote nchini (Jiji, Manispaa, Miji na Wilaya). Lengo kuu
la mashindano haya ni kushirikisha wananchi, sekta binafsi katika kuboresha
hali ya usafi wa mazingira katika maeneo yao.
171. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
katika kipindi cha 2005/2006 itaanza kutekeleza Mpango Maalum wa muda wa miaka
mitano 2005/2006 – 2009/2010. Mpango
maalum wa kudhibiti taka zinazozalishwa
hospitalini utaanzishwa ili kudhibiti hali ya uambukizo wa magonjwa
kwa watoa huduma, wateja na jamii kwa jumla.
Mpango huu utazihusisha hospitali
zote nchini.
Afya Bandarini na Mipakani
172. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
itaendelea kuimarisha utendaji wa vituo vya mipakani ili kuhakikisha kuwa
magonjwa ya kuambukiza yanadhibitiwa kwa kufuata sheria za afya. Vituo hiyo vya
mipakani vitapatiwa usafiri. Vituo hivyo
ni Kabanga, Kasumulo, Holili, Kigoma, Kyaka na Tunduma. Pia udhibiti wa uingizwaji wa vyakula, dawa
na vipodozi visivyokidhi viwango vya afya utaimarishwa kwa kushirikiana na
wadau mbalimbali.
Afya Kazini
173. Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana
na vyama vya wafanyakazi, Wizara yangu itashirikiana na wadau wote kikamilifu
kuendeleza mpango wa kuzuia maambukizi ya UKIMWI mahali pa kazi. Ili kufikia
azma hii watumishi wa afya 118 wa Halmashauri za wilaya watapatiwa mafunzo juu
ya uboreshaji wa afya ya wafanyakazi sehemu za kazi. Wizara pia itahakikisha
kuwa watumishi wote wanashiriki kwenye michezo ili kuboresha afya zao. Katika
bajeti ya mwaka 2005/06 Wizara imetenga fedha kwa ajili ya kujenga chumba cha
mazoezi cha kisasa ili kuwawezesha watumishi wote wa Wizara kufanya mazoezi
kila siku.
Taasisi ya
Chakula na Lishe
174. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006, Wizara yangu kupitia Taasisi ya Chakula na Lishe itaendelea kuratibu
shughuli za kitaifa za utoaji matone ya vitamini A na vidonge vya kutibu minyoo
kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano katika mikoa yote ya Tanzania
Bara. Wizara itaendelea kufuatilia na kutoa mafunzo na mkazo juu ya uwekaji wa
madini joto kwenye chumvi, kufikia asilimia 90 kiwango kinachopendekezwa na
Shirika la Afya Duniani, Tanzania kwa sasa imefikia asilimia 84.
175. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006 Taasisi pia itafanya utafiti kuhusu tatizo la upungufu wa damu kwa
nchi nzima ili kuwa na takwimu sahihi za hali halisi ya tatizo hilo. Kupatikana
kwa takwimu hizo kutasaidia katika kupanga mikakati na programu za kupunguza
tatizo hili. Aidha, Taasisi itaandaa na kuchapisha vitabu nakala 10,000 zaidi
vya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu lishe bora kwa wenye UKIMWI. Pia Wizara
itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu lishe bora ili kuepukana na magonjwa
sugu yenye uhusiano na ulaji usiozingatia lishe bora kama vile
kiriba tumbo (obesity), magonjwa ya mfumo wa mishipa ya damu, moyo, na mengineyo.
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa
Magonjwa ya Binadamu
176. Mheshimiwa Spika,
Taasisi hii inashughulikia utafiti wa magonjwa ya binadamu yakiwemo malaria,
usubi, matende na mabusha, malale, kichocho/minyoo na kifua kikuu. Utafiti
utaofanyika utalenga maeneo yafuatayo;
177. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006, Taasisi itaendelea kufanya utafiti zaidi wa aina
za dawa mchanganyiko dhidi ya malaria ili kutoa ushauri sahihi juu ya dawa zitakazoweza kuhimili usugu wa vimelea vya
malaria. Aidha Taasisi itaendeleza
utafiti wa dawa zinazotokana na mimea
zinazoweza kuua na kufukuza mbu wa aina mbalimbali.
178. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
2005/06, Taasisi itafanya utafiti wa kupima kiwango cha usubi katika jamii
inayoishi kando kando ya mito inayonyunyiziwa dawa ya kuuwa wadudu wanaoeneza
ugonjwa wa usubi. Aidha, utafiti
wa uelewa wa ugonjwa wa UKIMWI utaendelezwa katika Wilaya za Korogwe, Kibaha na
Iringa. Pia utafiti wa kutathmini maendeleo ya wagonjwa wanaopewa dawa za
kupunguza makali ya UKIMWI (ARVs)
utaendelea katika wilaya ya Muheza.
179. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti
Matende na Mabusha unatarajia kuwafikia walengwa 2,800,000
katika Manispaa tatu za mkoa wa
Dar-es-Salaam.
Huduma za Afya Wilayani (District
Health Services)
180. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/06 tutakamilisha uzinduzi wa Bodi za Afya katika Halmashauri 52 zilizobaki
kati ya 113 mara Hati Rasmi (instrument) za Bodi hizo zitakapotangazwa
kwenye Gazeti la Serikali. Kwa kuwa uanzishwaji wa Mfuko wa Afya ya Jamii
unatanguliwa na uzinduzi wa Bodi za Afya
za Halmashauri, mwaka 2005/06 tutazisaidia Halmashauri za Wilaya 41 zilizobakia
nazo zizindue Mfuko huu. Halmashauri
mpya za Wilaya zitakazoundwa baada ya
Uchaguzi Mkuu zitahamasishwa ili ziunde Bodi na kuanzisha Mfuko wa Afya ya
Jamii.
181. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/06 Wizara itaendelea kutoa usimamizi wa kitaalamu kwa Halmashauri juu ya
uendeshaji wa huduma za afya katika ngazi ya wilaya ili kuboresha huduma. Pia
itapeleka gari mpya 15 kwenye Halmashauri kwa ajili ya kazi ya ufuatiliaji na
usambazaji wa dawa na vifaa muhimu vya afya.
182. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
itatoa mafunzo ya kuainisha Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini
Tanzania (MKUKUTA), unavyohusiana na Kitita cha Huduma Muhimu za Afya (National
Essential Package of Health Interventions), Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya
wa miaka mitano (Health Sector Strategic Plan) 2003 - 2008 na Mipango
Kabambe ya afya ya Halmashauri (Comprehensive Council Health Plans). Aidha mafunzo yatatolewa kwa Maafisa Mipango wa Wilaya jinsi ya kutayarisha
bajeti na mipango ya Afya ya Halmashauri
(comprehensive council health plans) inayozingatia mzigo.
Huduma ya Elimu ya Afya kwa Umma
183. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006 Wizara yangu itaendelea kuelimisha na kuhamasisha jamii ishiriki
katika kutambua na kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya ki-afya yanayoisibu. Wizara yangu itashirikiana na wadau mbali
mbali kuelimisha wananchi mbinu za kubadili tabia na mitindo ya maisha
inayohatarisha afya zao. Aidha Wizara yangu itaimarisha uratibu na kupanua wigo
wa shughuli za utoaji elimu ya afya kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya
habari vilivyopo katika jamii yetu na kuimarisha matumizi ya sanaa kwa
maendeleo, ili kuweza kufikisha ujumbe wa afya kwa wananchi wengi.
HUDUMA ZA TIBA
184. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2005/06, Wizara ya Afya imetengewa jumla ya shilingi 47,394,729,600 kwa
ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba kwa matumizi ya zahanati, vituo
vya afya, hospitali za wilaya, hospitali teule, hospitali za mikoa, rufaa,
maalum na hospitali ya taifa ya
Muhimbili. Wizara pia imetenga shilingi 6,000,000,000/=
zitakazotumika kulipa sehemu ya deni la MSD.
185. Mheshimiwa Spika, Wizara ya Afya
kupitia Bohari ya Madawa (MSD), itasambaza dawa na vifaa katika zahanati 3,706
na vituo vya afya 410. Kati ya hivyo, zahanati 175 na vituo vya afya 25
vitakuwa vipya vilivyojengwa na Halmashauri na nguvu za wananchi na kuthibitika kuwa vina ubora
unaofaa. Aidha, katika kuboresha usambazaji wa dawa, vifaa na vifaa tiba,
Wizara ya Afya itaendesha majaribio ya mfumo wa ‘Integrated Logistics System’
katika mikoa ya Dodoma na Iringa. Mfumo huu utawezesha zahanati, vituo vya afya
na hospitali kuagiza dawa na vifaa vya kawaida, na vya miradi ya misaada kwa
mfumo mmoja. Mfumo utaiwezesha Wizara ya
Afya kukusanya takwimu za mahitaji na matumizi halisi ya dawa, vifaa na vifaa
tiba.
186. Mheshimiwa Spika, Wizara itaingia
mkataba wa miaka mitano (5) na kampuni ya Philips Medical Systems katika
kuhakikisha kuwa, mashine za eksirei, Ultrasound na vifaa vingine chini ya
mradi wa kuimarisha huduma za uchunguzi wa magonjwa nchini zinadumu kwa miaka
mingi ili ziendelee kutoa huduma kwa wananchi.
Katika mkataba huo mafunzo maalum hasa yale ya mashine zenye teknolojia
ya hali ya juu yatatolewa kwa watumiaji, Wahandisi na mafundi waliopo katika
karakana za kanda. Wizara pia itaendelea
kutoa utaaalam wa matengenezo ya mara
kwa mara ya vifaa tiba kupitia karakana za kanda kwa maeneo yote yanayotoa
huduma ya afya kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa.
187. Mheshimiwa Spika, Wizara
itaendelea kuimarisha huduma za maabara kwa kuagiza mashine nyingine, na vifaa
vya maabara kwa ajili ya kufuatilia wagonjwa wanaopatiwa dawa za kusaidia
kupunguza makali ya UKIMWI. Wizara
itakamilisha ujenzi wa kituo cha Kanda ya Mashariki cha damu salama pamoja na kuanza mipango ya
ujenzi wa Kanda za Kusini (Mtwara) na Kati (Dodoma). Wakati huo huo Kanda za Ziwa, Nyanda za Juu
Kusini na Kaskazini zitaendelea na kazi ya kukusanya damu salama, kwa kushirikiana
na Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania.
Aidha, maabara 13 za mikoa na 8 za Wilaya zitaboreshwa kwa kufanyiwa ukarabati
ili kukidhi mahitaji ya utoaji wa huduma bora.
Huduma za kuzuia Maambukizi ya
Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto
188. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/06 Wizara imepanga kupanua huduma za
kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT)
katika hospitali zote za Wilaya zilizokuwa bado hazijaanza kutoa huduma hiyo na
kufanya Hospitali zote za Wilaya kuwa na huduma hii. Vile vile Wizara itaendelea kuimarisha huduma
ya PMTCT – Plus. Kwa lengo la
kuhakikisha akina mama wajawazito walioathirika na Virusi vya UKIMWI – VVU na
wenye vigezo vya kupata “ART” wanapata huduma hiyo na wale ambao hawana vigezo
wakishajifungua waendelee kufuatiliwa.
Huduma za
Hospitali za Mashirika ya kujitolea, Makampuni na Watu Binafsi
189. Mheshimiwa Spika, ili kupeleka madaraka zaidi kwa wananchi, Halmashauri
zimepewa mamlaka ya kuingia makubaliano ya kutoa huduma za afya (Service
Agreement) na Hospitali za Mashirika
badala ya mfumo wa zamani ambapo mikataba ya huduma ilikuwa kati ya hospitali
hizo na Wizara ya Afya. Halmashauri zitaingia mkataba na hospitali hizo baada ya
kupata ridhaa ya Wizara ya Afya. Wizara
pia itaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya sekta binafsi na ile ya umma
katika utoaji wa huduma za afya. Aidha,
kwa kuthamini mchango unaotolewa na Mashirika ya Dini katika kuboresha huduma
za afya, Serikali imeongeza ruzuku ya
kitanda kutoka shilingi 30,000 mwaka 2004/05 hadi shilingi 50,000 kwa mwaka
2005/06.
Huduma za
Afya ya Kinywa
190. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2005/2006 itaanza awamu ya pili ya ufungaji vifaa vifuatavyo vya meno katika
kliniki za meno za Hospitali za Wilaya, Mkoa, rufaa na za mashirika. Vifaa hivyo ni:- viti (dental chairs),
taa maalum (operating lights) na viti vya kukalia. Hospitali
zitakazopatiwa vifaa hivyo ni; Muheza, Korogwe, Chunya, Ileje, Mbeya Vijijini,
Mbarali, Rungwe, Kyela, Karatu, Ngorongoro, Simanjiro, Iramba, Morogoro
Vijijini, Mbozi, Hanang, Sikonge, Mpanda, Musoma, Kilombero, Mvomero, Bariadi,
Bukombe, Kishapu, Liwale, Njombe, Ludewa, Karagwe, Sengerema, Geita, Ukerewe,
Misungwi, Newala, Mwanga, Kwimba, Tarime, Bunda, Biharamulo, Mbinga, Morogoro,
Dodoma na Tabora. Pia hospitali nyingine
zitakazopatiwa vifaa hivyo ni; Kibosho,
Mbeya Rufaa, Mawenzi, Mount Meru, Bombo, Iringa, Mbeya Mkoa, Mirembe, Kilema,
Bugando, Dareda, Ligula, Maweni, Singida na Bukoba.
Huduma
za Afya ya Akili na Madawa ya Kulevya
191. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006 shughuli za kueneza stadi za
kutoa huduma za magonjwa ya akili katika mikoa ya Mwanza, Kagera, Mara na Shinyanga zitaendelea. Pia vijitabu vya mwongozo wa
utambuzi na matibabu ya
magonjwa ya akili ngazi ya msingi vitasambazwa mikoa yote.
Hospitali za Rufaa
Hospitali
ya Taifa ya Muhimbili
192. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/06 huduma za tiba kwa wananchi zitaimarishwa ikiwa ni pamoja na waathirika wa
UKIMWI. Jengo jipya la kutoa huduma kwa wagonjwa wa
nje lenye vyumba 35 litaanza kutumika na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa
msongamano na pia litawezesha kuchujwa kwa wagonjwa wanaohitaji huduma maalum
za rufaa. Wagonjwa
wote watalazimika kupitia katika jengo hili kwanza kabla ya kupata huduma za
afya.
Hospitali ya Bugando
193. Mheshimiwa Spika, katika
mwaka 2005/06 hospitali ya Bugando itaendelea na ukarabati wa wodi za wagonjwa,
kuimarisha utoaji huduma na kuendelea kutafuta Madaktari Bingwa na wa
kawaida, ili kutosheleza mahitaji ya hospitali.
Hospitali
ya KCMC
194. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006,
hospitali ya KCMC inatarajia kuwapeleka madaktari wa upasuaji, nusu kaputi na
wauguzi kwenye mafunzo ya muda mfupi ili kupata taaluma zaidi ya upasuaji wa
moyo. Aidha, hospitali hiyo kwa kushirikiana na mashirika ya nje na hapa
nchini, itaendelea kuimarisha utafiti wa magonjwa ya malaria na UKIMWI.
195. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/06, hospitali
itaimarisha huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Bima ya Afya kwa kuteua mratibu
ambaye ataratibu shughuli zote za mfuko. Aidha, itapanua huduma kwa wagonjwa wa
UKIMWI kufuatia kukamilika kwa majengo ya wagonjwa wa nje.
196. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/06, hospitali
ya KCMC itatoa nafasi ya masomo kwa madaktari katika Chuo Kikuu cha Tumaini
(KCMC) ili kuongeza idadi ya madaktari
bingwa katika fani mbali mbali. Aidha, Chuo hiki kitaongeza
nafasi za masomo ya udaktari ili kuongeza idadi yao hapa nchini.
Taasisi
ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (Muhimbili Orthopaedic Institute (MOI)
197. Mheshimiwa
Spika, baada ya ununuzi wa
vifaa muhimu, katika kipindi cha
2005/06 Taasisi itapanua huduma za upasuaji katika fani ya mifupa, ubongo na
mishipa ya fahamu ambazo awali zilikuwa hazipatikani nchini.
198. Mheshimiwa
Spika, Taasisi ya MOI, itaendelea kutoa tiba ya mazoezi ya viungo kwa wagonjwa wa nje na wa
ndani, huduma ya viungo bandia, huduma kwa wagonjwa
mahututi, huduma za maabara na mionzi (X-ray).
Hospitali
ya Rufaa Mbeya
199. Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2005/2006 hospitali ya Rufaa Mbeya itaendelea kutoa huduma kwa ajili ya wagonjwa wa nje na ndani wanaopata rufaa kutoka
mikoa yote ya Kanda za Nyanda ya Juu Kusini.
Aidha hospitali itaendelea na utafiti wa
chanjo ya ugonjwa wa UKIMWI (Vaccine
Trial Centre) kwa msaada wa Serikali ya Ujerumani. Hospitali itaendelea kuboresha sehemu ya
kuhifadhi kumbukumbu za wagonjwa na kuanza kutumia
huduma kutoka sekta binafsi katika maeneo ya ulinzi, usafi wa nje na ufuaji
nguo.
Taasisi
ya Saratani ya Ocean Road
200. Mheshimiwa Spika, mwaka 2005/2006 Taasisi itaendelea kutoa huduma za
uchunguzi na matibabu kwa wagonjwa wa saratani wa
ndani na nje. Aidha,
Taasisi itafunga mashine mpya 2 za mionzi. Mashine hizo 2 zikifungwa
zitafanya Taasisi kuwa na mashine 5 na hivyo kutoa uwezo
zaidi wa kumudu kuhudumia ongezeko la asilimia 10 ya wagonjwa. Taasisi kwa kushirikiana na shirika la Mionzi
Duniani (International Atomic Energy Agency – IAEA) litakamilisha
maandalizi ya uanzishaji wa mafunzo ya
kufundishia mafundi wa kuendesha mashine za mionzi yaani “Radiotherapy
Technologists”
Hospitali
ya Mirembe na Taasisi ya Isanga
201. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006 hospitali ya Mirembe
itaendelea kutoa huduma kwa wagonjwa wenye matatizo ya
afya ya akili wa ndani na nje. Kwa kushirikiana
na Tume ya Taifa ya Kudhibiti madawa ya kulevya,
itaendelea kutoa huduma kwa waathirika wa pombe na madawa ya kulevya. Wizara ya Afya kwa
kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Taasisi ya Isanga itaendelea
kutoa huduma kwa watuhumiwa wa makosa ya jinai yaliyotendeka kutokana na
matatizo ya afya ya akili.
Hospitali ya Kibong’oto
202. Mheshimiwa
Spika, katika mwaka 2005/2006
hospitali itaendelea kutoa huduma za tiba kwa wagonjwa
wa Kifua Kikuu na wagonjwa wengine.
Aidha, hospitali itaendelea na uchunguzi wa
vimelea sugu vya kifua kikuu.
HUDUMA ZA UTAWALA NA UTUMISHI
203. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2005/2006
Wizara ya Afya itaendelea kutoa kipaumbele katika kuimarisha na kuboresha uwezo
wa utendaji kazi kwa watumishi wake ili kuimarisha na kuongeza tija. Aidha, Wizara itaendelea kuajiri watumishi
wapya kwa mujibu wa ikama iliyoidhinishwa.
Wizara pia itawapandisha vyeo watumishi
waliopo kwa kuzingatia sifa, vigezo na ikama. Ili kwenda sambamba na mabadiliko
yanayoendelea kufanyika katika Sekta ya Afya, Wizara imejiwekea mpango wa kutoa
mafunzo ya Huduma kwa Mteja kwa watumishi wake wote (Client Service Charter).
Mafunzo haya yatawahusisha watumishi wapatao 3,336 kutoka Makao Makuu ya
Wizara, Hospitali za Rufaa maalum, na Vyuo vya Afya 110.
HUDUMA YA MAFUNZO
204. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu
imedhamiria kuboresha na kupanua huduma ya mafunzo ili kuongeza idadi ya watoa
huduma za afya nchini. Hivyo chuo
kipya cha madaktari wasaidizi (Assistant Medical Officers) kitaanzishwa
huko Ifakara. Chuo hiki awali
kilikuwa kinatoa mafunzo ya Maafisa Tabibu. Aidha, Mapitio ya mitaala ya vyuo vya Sayansi ya Afya na Uuguzi yatafanyika ili kuboresha mafunzo yanayotolewa
vyuoni. Mafunzo ya Matibabu ya Watoto kwa uwiano (Integrated
Management of Chilhood Illness – IMCI) kwa waalimu 40 wa vyuo vya Mafunzo
yatatolewa.
205. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kutoa mafunzo ya kujiendeleza ili kutoa huduma bora. Mafunzo yatatolewa kwa
timu 12 za mikoa ikiwa ni watumishi 96 watakaopatiwa mafunzo hayo. Lengo ni kuzipatia timu za afya za mikoa uwezo wa kusimamia na
kuziekeleza timu za Wilaya ili zitoe huduma sahihi. Aidha wahitimu 136 wa ngazi ya Shahada wakiwemo Madaktari, Madaktari wa meno,
Wauguzi na Wafamasia watapatiwa mafunzo ya kuwaandaa kuanza kazi katika vituo
vya kazi watakavyopangiwa yaani “Induction Course”. Jumla ya Waganga Wasaidizi
Vijijini 21 wanatarajia kuhitimu mafunzo ya Maafisa Tabibu kupitia mafunzo kwa njia ya Posta na 253 wanatarajia kuhitimu katika vyuo
vya mafunzo. Aidha, Waganga Wasaidizi
vijijini 190 wako katika hatua mbalimbali za masomo kwa
njia ya posta.
OFISI YA MGANGA MKUU KIONGOZI
Huduma za Kupambana na Maafa
206. Mheshimiwa
Spika, katika kipindi cha mwaka 2005/06, Wizara inakusudia kufanya kazi
zifuatazo:
·
Usimamizi wa huduma za dharura na maafa katika mikoa 9
kila mkoa wilaya 2, kwa lengo la kutathmini utoaji wa huduma za afya na kutoa
ushauri wa kitaalam na maelekezo ili kuboresha huduma.
·
Kutoa mafunzo ya namna ya kukabiliana na dharura na
maafa kwa wajumbe 40 wa Timu za Uendeshaji wa Huduma za Afya za Mikoa na
mafunzo maalum kwa watumishi 36 wa hospitali za Mikoa na Rufaa. Mafunzo haya
yatawawezesha watumishi kuongeza ufanisi katika kusimamia utendaji wa kazi
wakati itokeapo dharura kwenye hospitali zao.
Ukaguzi wa Huduma za Afya
207. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu katika mwaka 2005/2006 itaendelea
kufanya ukaguzi kwa ajili ya kuhakikisha ubora wa huduma za afya zinazotolewa
kwa ngazi zote.
Huduma
za Uuguzi
208. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2005/06
Wizara itasambaza nakala 8,000 za
mwongozo wa jinsi ya kutoa huduma kwa wagonjwa walioathirika na UKIMWI katika Halmashauri zote nchini.
Wizara itafanya ufuatiliaji na usimamizi
wa huduma za uuguzi na ukunga katika mikoa ya Mwanza, Pwani, Kilimanjaro,
Kigoma, Kagera, Dodoma, Arusha, na
Rukwa. Aidha, Wizara yangu itaandaa Mpango Mkakati wa utoaji huduma za uuguzi na ukunga wa miaka
mitatu.
Mabaraza ya Kitaaluma
209. Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa mabaraza ya kitaaluma,
katika kusimamia maadili, Wizara yangu kwa mwaka 2005/2006 itatekeleza
yafuatayo: -
·
Kutayarisha na kukamilisha mwongozo wa Maadili na
Kanuni kwa taaluma za Madaktari na Madaktari wa Meno, Wafamasia, Mafundi Sanifu
wa Maabara, Wataalam wa Macho na Wauguzi/Wakunga.
·
Kuandaa Mpango
Mkakati (strategic plan) kwa mabaraza ya
Famasia, Fundi Sanifu wa Maabara na Wauguzi/Wakunga.
WAKALA ZILIZO CHINI YA WIZARA YA AFYA
Mamlaka ya Chakula na
Dawa (TFDA)
210. Mheshimiwa Spika, mwaka 2005/06 Mamlaka ya
Chakula na Dawa inatarajia kutekeleza yafuatayo:-
·
Kusimamia ubora na usalama wa vyakula, dawa, vipodozi,
vifaa tiba na kuimarisha mfumo wa usajili.
Aidha, ukaguzi wa maduka, viwanda vya nje na ndani na vituo vya mipakani
utaendelea.
·
Kuimarisha maabara kuu na ndogo zinazohamishika zilizoko
katika vituo vya mipakani na mikoani ili ziwe na uwezo wa kupima vipimo mbali
mbali kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika.
·
Kuandaa miongozo na kanuni ili kuwezesha utekelezaji bora wa Sheria.
·
Kutoa mafunzo kwa watumishi ili waweze kufanya kazi kwa
ufanisi zaidi.
·
Kutoa elimu kwa wadau na wananchi kwa njia za vyombo vya habari na tovuti.
·
Kufungua Ofisi ya Kanda
Mbeya ili kusogeza huduma karibu na wananchi.
Wakala
wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali
211. Mheshimiwa Spika, mwaka 2005/2006
Wizara yangu itaendelea kuimarisha uwezo wa Wakala wa
Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ili utoe huduma za uchunguzi wa kimaabara
kwa ufanisi zaidi. Wizara itanunua
kemikali na vitendea kazi. Wizara itatoa mafunzo kwa wataalamu 19 wa Wakala
katika nyanja mbalimbali zitakazosaidia kuimarisha utoaji huduma.
212. Mheshimiwa Spika, ili kusogeza huduma za Wakala wa Mkemia Mkuu wa
Serikali karibu na wananchi, Wizara itakamilisha taratibu za kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa Maabara ya Kanda ya Kaskazini.
213. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza usimamizi wa sheria ya Kemikali za
Majumbani na Viwandani, Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali utaendelea
kuimarisha na kusimamia usajili, ukaguzi na utoaji wa habari kuhusu kemikali
mbalimbali. Kutayarisha miongozo
mbalimbali ya utekelezaji wa sheria na kutangaza kazi zake kwa njia ya vyombo
vya habari na vipeperushi ili kuelimisha umma juu ya sheria yenyewe, madhara na
faida zinazoletwa na kemikali.
USHIRIKIANO WA NDANI NA NJE YA
NCHI
214. Mheshimiwa Spika, Serikali
imeendelea kuwa na ushirikiano mzuri na wa karibu na nchi rafiki na mashirika
ya kimataifa yanayosaidia sekta ya afya. Wizara ya Afya, pia imepata
ushirikiano mzuri kutoka sekta nyingine ambazo zinasaidia kuboresha huduma za
afya.
215. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imeendelea kuadhimisha siku mbali mbali za
Afya zinazodhimishwa Kitaifa na
Kimataifa. Naomba kuchukua nafasi hii
kuwashukuru viongozi mbalimbali wa kitaifa, mikoa, wilaya na wananchi wote kwa
ujumla kwa kufanikisha maadhimisho ya siku hizo.
216. Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi
hii kipekee kuzishukuru nchi za Denmark, Uswisi, Uholanzi, na Ujerumani na
mashirika ya Benki ya Dunia, UNFPA, Development Cooperation of Ireland (DCI)
kwa kutoa misaada yao katika Mfuko wa Pamoja wa Sekta ya Afya (Basket Fund)
ambao umesaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za afya. Pia napenda
kuzishukuru nchi nyingine za China, Cuba, Canada, Hispania, India, Ireland,
Italia, Japan, Korea Kusini, Marekani, Misri, Sweden, Ufaransa, Norway na
Uingereza,ambazo zimeendelea kuisaidia sekta ya Afya kwa njia mbali mbali.
217. Mheshimiwa Spika, Mashirika ya Kimataifa pia yanastahili shukrani kwa
ushirikiano wao mzuri na Wizara yangu.
Naomba kuchukua tena nafasi hii kutoa shukrani kwa Jumuiya ya Nchi za
Ulaya (EU), Shirika la Umoja wa Kimataifa la Maendeleo (UNDP), Shirika la Afya
Duniani (WHO), Shirika la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Shirika la Umoja wa
Mataifa la Uzazi wa Mpango (UNFPA), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kudhibiti
UKIMWI (UNAIDS), Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR),
Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), Benki ya Nchi za Kiarabu
kwa ajili ya Maendeleo ya Uchumi ya Nchi za Afrika (BADEA), Umoja wa Nchi
zinazotoa Mafuta kwa wingi Duniani (OPEC), na Madaktari Wasio na Mipaka
(Medicine Sans Frontieres – MSF). Wengine ni CIDA (CANADA), CUAMM, DANIDA, DFID, GTZ,
IDRC, JICA, KFW, MISERIOR, SAREC, SDC,
CDC, SIDA (SWEDEN), Engender Health (USA), CORDAID (Netherlands) BASIC NEED
(UK) na USAID. Tunawashukuru pia
Wafadhili wa mradi wa kudhibiti magonjwa ya usubi na vikope ambao ni African
Programme for Orchorcerciasis Control, International Eye Foundation, Merk,
Pfizer, Hellen Keller Foundation na International Trachoma Initiative. Taasisi nyingine za Kimataifa ni Axios
International, US President’s Initiative, Bill Clinton Foundation, Bill and
Melinda Gates Foundation, Abbot Laboratories, London School of Hygiene and
Tropical Medicine, John Hopkins University, Global Fund for HIV/AIDS, TB and
Malaria, University of Columbia, CMB, Germany Leprosy Relief Association,
Gabriel Project ya Marekani, Citi Bank, General Electric (GE – USA), Havard
University na Duke University za Marekani, Community of Saint Egidio (DREAM) na
Glasgow Smith Kline (GSK).
218. Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii kwa
niaba ya Serikali kuwashukuru watu binafsi, vyama vya hiari, na mashirika
yasiyo ya kiserikali ya ndani ya nchi kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia
uimarishaji wa huduma za afya. Mashirika
hayo ni pamoja na Aga Khan Foundation, AMREF, Lions Club, Rotary Club
International, BAKWATA, CCBRT, Christian Social Services Commission (CCT),
ELCT, TEC, Msalaba Mwekundu, Shree Hindu Mandal, Hubert Kairuki Memorial
Hospital, Regency Hospital, TPHA, USADEFU, NSSF, PASADA, PSI, Women Dignity
Project, Tanzania Diabetic Association, MEHATA, TANESA na vyama vyote vya
kitaaluma vya Sekta ya afya. Napenda pia kuwapongeza Tanzania Heart Institute kwa hatua waliyofikia katika kuanzisha huduma za upasuaji wa
moyo hapa nchini.
MWISHO
219. Mheshimiwa Spika, katika kipindi chote cha mwaka wa fedha 2004/2005
nimefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na viongozi wenzangu wa Wizara ya
Afya. Nachukua fursa hii ya pekee
kuwashukuru wafuatao Mheshimiwa Dr. Hussein Ali Mwinyi (Mb.) Naibu Waziri wa
Afya, Ndugu Mariam Joy Mwaffisi, Katibu Mkuu, Dr. Gabriel Upunda, Mganga Mkuu
Kiongozi, Wakurugenzi wa Idara zote katika Wizara ya Afya, Wakurugenzi wa
Hospitali za Rufaa na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya, Waganga Wakuu wa
Mikoa na Wilaya, Wakuu wa Hospitali, Vituo vya Afya, Zahanati na Wakuu wa Vyuo
vya Mafunzo ya Afya na wafanyakazi wote wa sekta ya afya. Nawaomba waendelee kufanya kazi kwa nguvu
zote na kwa moyo wa kujitolea kwa manufaa ya wananchi na taifa letu kwa ujumla.
220. Mheshimiwa Spika, sitaweza kumaliza hotuba yangu bila kuwashukuru
wafuatao, mume wangu Mheshimiwa Pius Msekwa na watoto wetu, pamoja na wananchi
wa Jimbo la Lulindi ambao mimi ninawawakilisha katika Bunge hili tukufu. Nawashukuru sana kwa uvumilivu wao. Mara
nyingi sipo pamoja nao kwa ajili ya majukumu yangu ya kitaifa. Wamenisaidia na wamenipa imani na ushirikiano
mkubwa. Kwa wananchi wa Jimbo la
Lulindi, nawashukuru kwa heshima mliyonipa kwa kunichagua mara mbili niwe
Mbunge wenu. Kwa kuwa sitagombea tena Ubunge wa Jimbo katika uchaguzi ujao,
naahidi kushirikiana na Mbunge ajaye na wananchi wa Lulindi kwa ujumla katika
kulijenga jimbo letu na Wilaya yetu.
MAOMBI YA FEDHA MWAKA 2005/06
221. Mheshimiwa Spika, ili kuiwezesha Wizara ya Afya kutekeleza kazi
zilizopangwa mwaka 2005/06 naliomba Bunge lako tukufu litafakari, lijadili, na
kuidhinisha makadirio ya Wizara ya Afya
na Asasi zake yenye jumla ya Shilingi 271,168,602,300 kati ya
fedha hiyo, Shilingi 180,305,853,900 ni kwa ajili ya mishahara na
matumizi ya kawaida, shilingi 90,862,748,400 ni kwa ajili ya kugharamia
utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha za maendeleo shilingi 5,000,000,000
ni fedha ya ndani na shilingi 85,862,748,400 ni
fedha ya nje.
222. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
VIAMBATANISHO
KIREFU CHA MAJINA YA MASHIRIKA YA KITAIFA NA KIMATAIFA
YANAYOSAIDIA HUDUMA ZA AFYA
ADB - African Development Bank
AMREF - African Medical and Research Foundation
BADEA - Bangue Arabe pour Development Economique
en Afrique
BAKWATA - Baraza Kuu la Waislamu
CBM - Christoffel Brinden Mission
CCBRT - Comprehensive
Community Based Rehabilitation in
CCT - Christian Council of
CDC - Centre for Disease Control and
Prevention
CIDA - Canadian International Development
Agency
CSSC - Christian Social Services Commission
CUAMM -
DANIDA - Danish International Development Agency
DFID -
DSE - Deusche
stiftung fur Internationale Entwicklung
ELCT -
EU - European Union
FINNIDA - Finnish International Development Agency
GSF - Good
Samaritan Foundation
GTZ - Gesellschaft
fuer Technische Zusammenarbeit
IDRC - International Development Research
Centre of
IMA - International Missionary Association
JICA - Japan International Cooperation Agency
MDP - Mectizan Donation Programme
NBC - National Bank of Commerce
NIMR - National Institute for Medical Research
NORAD - Norwegian Agency for Development
NSSF - National Social Security Fund
OPEC - Organisation of Petroleum-Producing
Countries
SADC -
SAREC - Swedish Agency for Research Cooperation
in Development Countries
SDC - Swiss Agency for Development and
Cooperation
SIDA - Swedish International Development
Authority
TAC-AIDS -
TAMWA -
TANESA -
TANESCO - Tanzania Electric Supply Company
TBL - Tanzania Breweries Limited
TEC -
TPDC - Tanzania Petroleum Development Corporation
TRA -
TTCL - Tanzania Telecommunication Company
Limited
UNDP - United Nations Development Programme
UNFPA - United Nations Fund for Population
Activities
UNHCR - United Nations High Commission for
Refugees
UNICEF - United Nations Children Fund
USADEFU - Usambara Development Fund
USAID - United States Agency for International
Development
WHO - World
Health Organisation
PSI - Population
Service International
VIREFU VYA
VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA NDANI:
ADB - African Development Bank
ARV - Anti Retro Viral
BOD - Burden of Diseases
CDC - Centre for Disease Control
CHF - Community Health Fund
DNA - Deoxyribo NucleicAcid
DPT-HB - Diptheria,
Pertussis Tetanus, Hepatitis B
GAVI - Global
HIV - Human Immuno Deficiency Virus
ICU - Intensive Care Unit
ILO - International Labour Organisation
IMCI - Integrated Management of Childhood
Illness
KCMC - Kilimanjaro Christian Medical Centre
MOI - Muhimbili Orthopaedic Institute
MTUHA - Mfumo wa
Taarifa za Uendeshaji Huduma za Afya
MUCHS -
NHIF - National Health Insurance Fund
NIMR - National Institute for Medical Research
ORCI - Ocean Road Cancer Institute
ORET - Overseas Related External Trade
PMTCT - Prevention of Mother To
Child HIV Transmission
SP - Sulphadioxine Pyrimithmine
STI - Sexual Transmitted Infections
TAMISEMI - Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa
TIKA - Tiba
kwa Kadi
TPRI - Tanzania Pesticides Research Institute
TT - Tetanus Toxoid
TV - Television
UKIMWI - Upungufu wa
Kinga Mwilini
ORODHA
YA HALMASHAURI 61 ZILIZOKWISHAZINDUA BODI ZA HUDUMA ZA AFYA
1.
Wilaya ya Hai
2.
Manispaa ya Tanga
3.
Wilaya ya Shinyanga
4.
Mji wa Singida
5.
Wilaya ya Mbulu
6.
Wilaya ya Mpwapwa
7.
Manispaa ya Kinondoni
8.
Wilaya ya Mufindi
9.
Wilaya ya Monduli
10.
Wilaya ya Kiteto
11.
Wilaya ya Hanang
12.
Wilaya ya Lushoto
13.
Wilaya ya Kigoma
14.
Manispaa ya Temeke
15.
Manispaa ya Arusha
16.
Manispaa ya Tabora
17.
Mji wa Songea
18.
Wilaya ya Ngara
19.
Wilaya ya Igunga
20.
Wilaya ya Mwanga
21.
Wilaya ya Ulanga
22.
Wilaya ya Masasi
23.
Wilaya ya Sumbawanga
24.
Wilaya ya Babati
25.
Wilaya ya Geita
26.
Wilaya ya Sengerema
27.
Wilaya ya Iringa
28.
Manispaa ya Iringa
29.
Wilaya ya Njombe
30.
Wilaya ya Makete
31.
Wilaya ya Handeni
32.
Wilaya ya Arumeru
33.
Wilaya ya Mbozi
34.
Wilaya ya Rombo
35.
Wilaya ya Kasulu
36.
Manispaa ya Moshi
37.
Manispaa ya Mbeya
38.
Wilaya ya Newala
39.
Wilaya ya Mtwara
40.
Wilaya ya Kilwa
41.
Wilaya ya Lindi
42.
Wilaya ya Liwale
43.
Manispaa ya Morogoro
44.
Jiji la Mwanza
45.
Wilaya ya Kondoa
46.
Wilaya ya Singida
47.
Wilaya ya Morogoro
48.
Wilaya ya Serengeti
49.
Wilaya ya Muheza
50.
Wilaya ya Biharamulo
51.
Wilaya ya Karagwe
52.
Wilaya ya Bukoba
53.
Mji wa Bukoba
54.
Wilaya ya Ngara
55.
Wilaya ya Muleba
56.
Wilaya ya Kibondo
57.
Wilaya ya Magu
58.
Mji wa Musoma
59.
Wilaya ya Bunda
60.
Manispaa ya Shinyanga
61.
Wilaya ya Korogwe.
Kiambatanisho
Na.4
ORODHA YA HALMASHAURI 51 AMBAZO ZIMEANZISHA MFUKO WA AFYA YA JAMII
Kiambatanisho Na.5
MIKOA
17 ILIYOBADILISHIWA MAJOKOFU YA MAFUTA YA TAA KWA MAJOKOFU MAPYA YA KUTUMIA
GESI
1. Tanga 11. Arusha
2. Pwani
12. Manyara
3.
4. Morogoro 14. Mara
5. Lindi 15. Kagera
6. Mtwara 16. Shinyanga
7. Iringa 17. Tabora
8. Mbeya
9.
10. Singida
HALMASHAURI 15 ZILIZOWEKEANA MKATABA NA WIZARA NA KUPEWA FEDHA ZA TELE KWA TELE KUANZIA MWAKA 2000 - 2005
|
|
JINA LA HALMASHAURI |
KIASI
KILICHOKWISHALIPWA (TSHS.) |
|
|
Singida Vijijini |
46,747,500.00 |
|
|
Iringa Vijijini |
66,665,000.00 |
|
|
Kilosa |
14,055,000.00 |
|
|
Igunga |
87,630,000.00 |
|
|
Hanang |
28,640,000.00 |
|
|
Karatu |
11,130,000.00 |
|
|
Iramba |
20,677,262.60 |
|
|
Nzega |
16,190,000.00 |
|
|
Sumbawanga |
19,255,000.00 |
|
|
Masasi |
80,000,000.00 |
|
|
Mufindi |
7,910,000.00 |
|
|
Kigoma Vijijini |
13,390,000.00 |
|
|
Songea Mjini |
56,772,000.00 |
|
|
Mbulu |
16,782,000.00 |
|
|
Mwanga |
16,205,000.00 |
|
|
JUMLA |
502,048,762.60 |
Mpango wa Taifa wa
Kudhibiti Vikope (Trachoma)
A. Wilaya 30 zilizokwisha fanyiwa utafiti wa awali wa kujua kiwango cha ugonjwa wa vikope mwaka 2004:
1. Tunduru 9. Monduli 17.Kiteto 24. Lindi vijijini
2. Iramba 10. Igunga 18.Singida vijijini 25. Simanjiro
3.
4. Kondoa 12.
Manyoni 20.Kilosa 27. Meatu
5. Ruangwa 13.
Mpwapwa 21.Sikonge 28. Kongwa
6. Mkuranga 14.Rufiji 22.Magu 29. Shinyanga
7. Kishapu 15.Nzega 23.Rombo 30.Singida mjini
8. Hai 16.
Iringa vijijini
B. Wilaya 26 zilizogundulika kuwa na
ugonjwa wa vikope kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10
1. Monduli 8.
Tunduru 15.
Kiteto 21.
Lindi vijijini
2. Iramba 9.
Igunga 16.
Singida vijijini 22.
Simanjiro
3.
4. Kondoa 11.
Manyoni 18.
Kilosa 24.
Meatu
5. Ruangwa 12.
Mpwapwa 19.
Sikonge 25.
Kongwa
6. Mkuranga 13.
Rufiji 20.Magu 26.Shinyanga
7. Kishapu 14.
Nzega
C. Wilaya 4 zilizogundulika kuwa na
ugonjwa wa vikope kwa kiwango cha
chini ya asilimia 10
1. Rombo 2.
Singida mjini 3.
Hai 4.
Iringa vijijini
D. Wilaya 10 ambazo zitafanyiwa utafiti wa awali wa kujua kiwango cha
ugonjwa wa vikope mwaka huu 2005.
1.
Songea vijijini 4. Karagwe 7. Newala
9. Mtwara Vijijini
2. Liwale 5.
Bagamoyo 8.Kilwa 10.Mbarali
3. Kilindi 6.
Tandahimba
Halmashauri 32 Zilizopata Mafunzo Ili ziweze kupanga,
kutekeleza, kufuatilia na kutathmini huduma za Elimu ya Afya Kwa Umma kwa
Kamati za Uendeshaji
Morogoro
1. Kilosa 3.
Kilombero 5.
Morogoro Vijijini
2. Ulanga 4.
Morogoro Manispaa 6.
Mvomero.
Kilimanjaro
7. Same 9.
Rombo 11.
Mwanga
8. Moshi Manispaa 10. Moshi
Vijijini 12. Hai
Mbeya
13. Kyela 16.
Mbarali 18.
Mbeya Vijijini
14. Ileje 17.Rungwe 19. Mbozi
15. Mbeya Manispaa
Iringa
20. Iringa Manispaa 22. Mufindi 24. Ludewa
21. Njombe 23.
Iringa Vijijini 25.
Makete
Arusha
26. Arumeru 27.
Arusha Manispaa 28.
Monduli
29.
Manyara
32. Babati
1. ARUMERU 137 87.2%
2. LUSHOTO 134 85.4%
3. NJOMBE 132 84.0%
4. MBINGA 129 82.1%
5. KAHAMA 120 76.4%
6. MOSHI VIJIJINI 117 74.5%
7. MPANDA 115 73.8%
8. MPWAPWA 114 72.6%
9. KYELA 112 71.3%
10. NZEGA 109 69.4%
11. GEITA 107 68.1%
12. MANYONI 102 64.2%
13. HANANG 96 61.1%
14. NGARA 92 58.5%
15. KILOSA 87 55.0%
16. RUANGWA 82 52.2%
17. BAGAMOYO 66 42.0%
18. KIGOMA VIJIJINI 50 31.8%
19. NEWALA 46 29.2%
20. MUSOMA VIJIJINI 44 28.0%
1. SONGEA 95 84.6%
2. SINGIDA 92 83.6%
3. SUMBAWANGA 90 81.8%
4. BUKOBA 83 75.5%
5. MTWARA 69 62.7%
6. LINDI 68 61.8%
7. KIGOMA 61 55.5%
8. MUSOMA 54 49.1%
9. KIBAHA 51 46.0%
10. BABATI 44 40.0%
ALAMA ASILIMIA
1. MOSHI 90 82.0%
2. MWANZA 83 75.0%
3. TANGA 80 73.0%
4. IRINGA 78 71.2%
5. MBEYA 77 70.0%
6.
7. ARUSHA 73 66.4%
8. ILALA 72 65.5%
9. TABORA 71 64.6%
10. KINONDONI 69 62.7%
11. TEMEKE 68 62%
12. MOROGORO 56 51%
13. SHINYANGA 45 41%
Wilaya 48 ambapo Ufuatiliaji wa
Afya Kazini katika Maeneo ya Viwanda, Ujenzi na Mashamba Ulifanyika
1. Hanang 15.
Kibaha 27.
Kisarawe
2. Tanga 16.
Muheza 28.
Korogwe
3. Rombo 17.
Arumeru 29.
Mwanga
4. Sumbawanga 18.
Mbeya Manispaa 30.
Mbarali
5. Kondoa 19.
Mpwapwa 31.
Kongwa
6. Morogoro Vijijini 20.Morogoro Manispaa 32. Kilosa
7. Kilombero
8. Lushoto 21.
Moshi Manispaa 33.MoshiVijijini
9. Babati 22.
Monduli 34.Same
10. Mufindi 23.
Iringa Vijijini 35.IringaManispaa
11. Rungwe 24.
Mbeya Vijijini 36.
Ilala
12. Kinondoni
13. Temeke 25.
Shinyanga 37.
Kahama
14. Nzega 26.Igunga 38. Pangani
39.
Hai
40. Arusha
41.
42. Mvomero
43.
44. Mbozi
45. Tukuyu
46. Tabora
47. Nzega
48. Manispaa ya Tabora
Kiambatanisho Na.11
HOSPITALI 68 ZILIZOPITISHWA KUWA RAFIKI KWA MAMA NA MTOTO KUANZIA 1992 HADI 2005
MKOA |
NA. |
JINA LA HOSPITALI |
|
Arusha |
1. 2. |
Babati |
|
|
||
|
|
3. 4. 5. 6. 7. 8. |
Hindu Mandal |
|
Dr. Khan |
||
|
Ilala (Amana) |
||
|
Mwananyamala |
||
|
Temeke |
||
|
Muhimbili |
||
|
|
9. 10. 11. |
|
|
Kondoa |
||
|
Mpwapwa |
||
|
Iringa |
12. 13. 14. 15. 16. 17. |
Iringa |
|
Ilembula |
||
|
Tosamaganga |
||
|
Mafinga |
||
|
Makete |
||
|
Njombe |
||
|
Kilimanjaro |
18. 19. 20. 21. 22. 23. 24. |
Huruma |
|
KCMC |
||
|
Hai |
||
|
Machame |
||
|
Mawenzi |
||
|
Same |
||
|
Usangi |
||
|
Mbeya |
25. 26 27. 28. 29. 30. |
Chimala |
|
Igongwe |
||
|
Kyela |
||
|
Mbeya Rufaa |
||
|
Mbozi Vwawa |
||
|
Tukuyu |
||
|
Kagera |
31. 32. 33. 34. 35. |
Ndolage |
|
Biharamulo |
||
|
Nyakahanga |
||
|
Mugana |
||
|
Rubya |
||
|
Mwanza |
36. 37. 38. 39. 40. 41. 42. |
Bugando |
|
Geita |
||
|
Mugumu |
||
|
Ngudu |
||
|
Sekou Toure |
||
|
Sengerema |
||
|
Magu |
||
|
Mara |
43. |
Bunda |
|
|
44. 45. |
Musoma |
|
Tarime |
||
|
Pwani |
46. 47. 48. |
Bagamoyo |
|
Kibaha |
||
|
Kisarawe |
||
|
Singida |
49. 50. 51. 52. |
Kilimatinde |
|
Makiungu |
||
|
Manyoni |
||
|
Singida |
||
|
Tanga |
53. 54. 55. 56. 57. 58. |
Bombo |
|
Handeni |
||
|
Korogwe |
||
|
Lushoto |
||
|
Muheza |
||
|
Pangani |
||
|
|
59. 60. 61. 62. |
Songea |
|
Mbinga |
||
|
Litembo |
||
|
Peramiho |
||
|
Mtwara |
63. 64. |
Ligula |
|
Ndanda |
||
|
Shinyanga |
65. 66. 67. |
Mwadui |
|
Meatu |
||
|
Shinyanga |
||
|
Kigoma |
68. |
Kasulu |
|
S/N |
JINA LA
CHUO |
KAZI /
MRADI |
|
1 |
Tanga AMO |
Rehabilitation of administration block and domitories |
|
2 |
Sumbawanga COTC |
Rehabilitation of domitories, 3 staff houses, class rooms,
laboratory and office, kitchen and dinning |
|
3 |
Kiomboi NTC |
Finalization of rehabilitation of buildings |
|
4 |
Newala NTC |
Rehabilitation of administration block, domitories and
dinning hall |
|
5 |
Mpwapwa HO |
Construction of staff quarters, laboratory and kitchen |
|
6 |
Same PHN |
Rehabilitation of administration block, class rooms and
fence |
|
7 |
Kahama PHN |
Extention of 2 staff quarters,recreation room,
construction of laundry and library |
|
8 |
Mtwara PHN |
Rehabilitation of domitory, dinning room and kitchen |
|
9 |
Mbozi NTC |
Rehabilitation of school buildings |
|
10 |
Geita PHN |
Construction of toilets, laundry, library,demonstration
room, corridor, wardens house and rehabilitation of staff quarters and deep
well |
|
11 |
Tanga NTC |
Rehabilitation of school buildings |
|
12 |
Kagemu HT |
Rehabilitation of 5 domitories |
|
13 |
Maswa COTC |
Rehabilitation of administration block, 2 class rooms,
laboratory, kitchen and dinning hall and semidetached wardens house |
|
14 |
Ngudu HT |
Construction of library |
|
15 |
Mkomaindo NTC |
Rehabilitation of 2 class rooms, demonstration rooms, 4
offices, dinning hall, 4 domitories, 2 staff houses, library, recreation hall
and kitchen |
|
16 |
Tukuyu NTC |
Rehabilitation of domitory, principals,quarter and
finalization of construction of fencing wall |
|
17 |
Mtwara COTC |
Finalization of construction of fencing |
|
18 |
Musoma COTC |
Rehabilitation of drainage, water systems and school
buildings |
|
19 |
Mafinga COTC |
Rehabilitation of domitories |
|
21 |
Njombe PHN |
Completion of security fence and rehabilitation of toilets |
|
22 |
Tarime PHN |
Rehabilitation of school buildings |
|
23 |
Songea COTC |
Completion of rehabilitation of domitories |
|
24 |
Kilosa COTC |
Rehabilitation of school buildings |
|
25 |
Bagamoyo PHN |
Rehabilitation of students domitory and construction of
shallow wells |
|
26 |
Kibaha COTC |
Rehabilitation of school buildings |
|
27 |
CEDHA |
Constuction of multipurpose bilding ( office, laboratory,
theatre rooms) |
|
28 |
Mirembe NTC |
Construction of class rooms, dorminories and staff quarter |
|
29 |
Tanga HO |
Construction of sttudents hostel |
|
30 |
Vector Control |
Rehabilitation of school buildings |
|
31 |
Kondoa PHN |
Construction of library and demonstration room |
|
32 |
Kigoma COTC |
Rehabilitation of class rooms domitories |
Kiambatanisho Na.13
ORODHA YA AINA
ZA DAWA ZILIZOLETA MADHARA KWA WATUMIAJI
1. SP - 16
2. Contrimoxazole - 6
4. Amodiaquine -
2
5. Seprin -
2
6. Annate -
2
7. 6 Norplant Implant - 1
8. Ampclox -
1
10. Thiabendazole - 1
11. Diclofenac - 1
12. Quinine - 1
13. Amolin - 1
14. Tramadol - 1
15. Depoprovera - 1
16. Asprin - 1
17. Methyldopa - 1
18. PPF - 1
42
Kiambatanisho Na.14
|
Mkoa |
Halmashauri |
Zahanati |
Vituo vya
Afya |
|
Arusha |
Arumeru |
Olkeriani |
|
|
Ngyani |
|
||
|
Terrati |
|
||
|
Kipandenkoavele |
|
||
|
|
|
|
|
|
Arusha
Manispaa |
|
Themi |
|
|
|
|
|
|
|
Monduli |
Matale |
Engarenaibor |
|
|
Lendikinya |
|
||
|
Meserani |
|
||
|
Ilorionito |
|
||
|
Oldonyondoroboni |
|
||
|
|
|
|
|
|
Karatu |
Oldeani |
Aya - |
|
|
|
Gyekrum -
Lambo |
||
|
|
|
|
|
|
Ngorongoro |
Irkeekpusi |
|
|
|
Oloipiri |
|
||
|
Oloirien/Magaiduru |
|
||
|
Esere |
|
||
|
|
|
|
|
|
DSM |
Ilala
Manispaa |
Ukonga Ogombolwa |
|
|
|
|
|
|
|
Kinondoni
Manispaa |
Msewe |
|
|
|
Mlalakuwa |
|
||
|
Makongo
Juu |
|
||
|
|
|
|
|
|
Temeke
Manispaa |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Ntuba |
|
|
Zuzu |
|
||
|
Chahwa |
|
||
|
Michese |
|
||
|
Ntyuka |
|
||
|
Gawaye |
|
||
|
|
|
|
|
|
|
Ndembwe |
|
|
|
|
Mpamantwa |
|
|
|
|
|
|
|
|
Mpwapwa |
Chinyanguku |
|
|
|
Tambi |
|
||
|
Matonya |
|
||
|
Chitemo |
|
||
|
Nghambi |
|
||
|
Ikuyu |
|
||
|
Kiboriani |
|
||
|
Kimagai |
|
||
|
Mtamba |
|
||
|
Kidenge |
|
||
|
|
|
|
|
|
|
Kondoa |
|
|
|
|
|
|
|
|
Kongwa |
Ihanda |
|
|
|
Nghumbi |
|
||
|
Chiwe |
|
||
|
Lenjulu |
|
||
|
Chamkoroma |
|
||
|
Mbagilwa |
|
||
|
Pingalane |
|
||
|
Ndurugumi |
|
||
|
|
|
|
|
|
Iringa |
Iringa
Manispaa |
|
|
|
|
|
|
|
|
Iringa
Vijijini+Kilolo |
Masisiswe |
Kimande |
|
|
|
Idegenda |
|
|
|
Ngongwa |
|
||
|
|
|
|
|
|
Ludewa |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Makete |
Ibanga |
|
|
|
Ilungu |
|
||
|
Ivirikinge |
|
||
|
Ukange |
|
||
|
Kipagalo |
|
||
|
Kinyika |
|
||
|
|
|
|
|
|
Mufindi |
Bumilainga |
Mgololo |
|
|
Igombavanu |
Sadani |
||
|
Ilogombe |
|
||
|
Mninga |
|
||
|
Mtambula |
|
||
|
Mtula |
|
||
|
Mkonge |
|
||
|
Ihanzikwa |
|
||
|
Kilolo |
|
||
|
|
|
|
|
|
Njombe |
|
Makoka |
|
|
|
|
|
|
|
Kagera |
Biharamulo |
|
|
|
|
|
|
|
|
Bukoba
Mjini |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Bukoba
Vijijini |
Bulembo |
|
|
|
Kibirizi |
|
||
|
Kashenye |
|
||
|
Buzi |
|
||
|
Nyakato |
|
||
|
|
|
|
|
|
Karagwe |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Muleba |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Ngara |
|
|
|
|
|
|
|
|
Kigoma |
Kasulu |
Nyanchenda |
Janga |
|
Kanazi |
|
||
|
Muhunga |
|
||
|
Songambele |
|
||
|
Mugera |
|
||
|
Kajana |
|
||
|
Nyamugali |
|
||
|
Rusaba |
|
||
|
|
|
||
|
|
|
|
|
|
Kibondo |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Kigoma -
Ujiji |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Kigoma
Vijijini |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Kilimanjaro |
Hai |
|
|
|
|
|
|
|
|
Moshi
Manispaa |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Moshi
Vijijini |
Mdawi |
|
|
|
Mahoma |
|
||
|
Leghomulo |
|
||
|
Kindi |
|
||
|
Kimangara |
|
||
|
Marangu Kiraracha |
|
||
|
|
|
|
|
|
Mwanga |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Rombo |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Same |
Karamba |
|
|
|
Bwambo |
|
||
|
Mhezi |
|
||
|
|
|
|
|
|
Lindi |
Kilwa |
|
|
|
|
|
|
|
|
Lindi
Mjini |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Lindi
Vijijini |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Liwale |
|
|
|
|
|
|
||
|
|
|
||
|
|
|
|
|
|
Nachingwea |
Namalongo |
Marando |
|
|
|
Kihuwe |
|
|
|
|
Nakaloji |
|
|
|
|
|
|
|
|
Ruangwa |
|
|
|
|
|
|
|
|
Manyara |
Hanang |
Endasaki |
|
|
Waranga |
|
||
|
Genuwasi |
|
||
|
Simbai |
|
||
|
|
|
|
|
|
Mbulu |
Bargish |
|
|
|
Gehandu |
|
||
|
Ngorat |
|
||
|
Hasama |
|
||
|
Tsawa |
|
||
|
Endaharghadat |
|
||
|
Diyomat |
|
||
|
|
|
|
|
|
Kiteto |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Babati |
Minjingu |
Gallapo |
|
|
|
Dohom |
|
|
|
|
Qash |
|
|
|
|
Gendamar |
|
|
|
|
Arri |
|
|
|
|
Dabir |
|
|
|
|
Mayoka |
|
|
|
|
|
|
|
|
Simanjiro |
Kwitai B |
Mererani |
|
|
Lemukuna |
|
||
|
Loibor
Soit A |
|
||
|
Nomeuti(Kambi
ya Chokaa) |
|
||
|
Narakau |
|
||
|
Mara |
Bunda |
Kunzugu |
|
|
Wariku |
|
||
|
|
|
|
|
|
Musoma
Mjini |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Musoma
Vijijini |
Mirwa |
|
|
|
|
|
|
|
|
Serengeti |
Bwitegi |
Nata |
|
|
|
|
|
|
|
Tarime |
Ochuna |
Sirari |
|
|
|