HOTUBA YA WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA
NA MASOKO MHE. NAZIR MUSTAFA KARAMAGI (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA
MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2006/2007
A. UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
1. Kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni
na Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji na Biashara iliyochambua bajeti ya Wizara
ya Viwanda, Biashara na Masoko, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu sasa
likubali kujadili na kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Fedha ya Wizara ya
Viwanda, Biashara na Masoko kwa mwaka 2006/07.
Mheshimiwa Spika,
2.
Awali ya yote napenda kumpongeza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa kwao kwa ushindi
mkubwa wa kishindo. Aidha, nampongeza
kwa namna ya kipekee Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuchaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Kitaifa.
Napenda pia, kumpongeza Mhe. Amani Abeid Karume kwa kuchaguliwa kwake
kwa kipindi cha pili kuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Vile vile,
nampongeza Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (Mb.), kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mbunge
na hatimaye kuteuliwa na kuthibitishwa na Bunge kwa kura nyingi kuwa Waziri
Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Nne ya Jamhuri ya Muungano wa
3.
Aidha,
napenda kukupongeza wewe mwenyewe Mheshimiwa kwa kuchaguliwa kwako kwa kura
nyingi kuwa Spika na Mhe. Anna Makinda (Mb.) kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika
katika Bunge la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Mheshimiwa Spika,
4.
Napenda
kuchukua nafasi hii kuwapa pole Waheshimiwa Wabunge waliopata mikasa ya kufiwa
na jamaa zao. Tunaomba Mungu awape
faraja na azilaze roho za marehemu mahali pema peponi – Amina.
Majukumu
Mheshimiwa Spika,
5.
Majukumu ya
Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko yamezingatia Dira ya Maendeleo ya Taifa
(National Development Vision 2025) ambayo imeweka bayana kwamba sekta za
Viwanda, Biashara na Masoko ndiyo ziwe mihimili mikuu ya kuuwezesha uchumi wa
nchi yetu kukua na kufikia kiwango cha kati cha Maendeleo ya uchumi wa Viwanda.
Majukumu ya msingi ya Wizara ni pamoja na:-
a)
Kuandaa na kusimamia
utekelezaji wa Sera za kuendeleza sekta za Viwanda, Biashara na Masoko;
b)
Kuandaa mipango na mikakati
ya kushirikisha na kuimarisha Sekta Binafsi katika kuchangia maendeleo ya
uchumi wa Taifa kupitia uendelezaji wa uwekezaji katika sekta za Viwanda,
Biashara na Masoko;
c)
Kusimamia utekelezaji
wa sheria mbalimbali chini ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko;
d)
Kusimamia utekelezaji
wa mikakati mahsusi ya uendelezaji wa mauzo ya mazao na bidhaa za
e)
Kubaini na kutekeleza
mikakati ya kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi na nchi nyingine ili kuhakikisha
kwamba Taifa linapata manufaa kwa kiwango cha juu hususan kupitia sekta ya
Viwanda, Biashara na Masoko; na
f)
Kuimarisha uwezo wa
Wizara na Asasi zilizo chini yake ili kutekeleza majukumu yake kwa kiwango cha
ufanisi wa hali ya juu.
Muundo
Mheshimiwa Spika,
6.
Kufuatia
kuundwa kwa Serikali ya Awamu ya Nne, sekta ya Masoko imeunganishwa na sekta za
Viwanda na Biashara na kuunda Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko. Kwa hiyo, muundo mpya wa Wizara sasa una
Idara nne zenye majukumu muhimu ya kisekta na Idara mbili za huduma na uratibu.
Idara za majukumu kisekta ni Idara ya Viwanda, Idara ya Biashara ya Kimataifa,
Idara ya Maendeleo ya Masoko na Idara ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo.
Idara za huduma na uratibu ni Idara ya Utawala na Utumishi na Idara ya Sera na
Mipango.
Mheshimiwa Spika,
7.
Wizara
inashirikiana kikamilifu na Sekta Binafsi kwa kuzingatia azma ya Serikali
kwamba Sekta Binafsi ndio mhimili mkuu katika kutekeleza majukumu yake
mbalimbali ya uwekezaji na biashara katika mkakati mzima wa kukuza uchumi na
kuondoa umaskini. Baadhi ya taasisi
zinazoshirikiana na Wizara yangu ni Tanzania Private Sector Foundation - TPSF,
Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture - TCCIA, Confederation
of Tanzania Industries – CTI pamoja na Asasi Zisizo za Kiserikali – AZISE.
Aidha, hushiriki katika mikutano ya kila mwaka inayoshirikisha Sekta ya Umma na
Sekta Binafsi na kupata michango
C. UTEKELEZAJI
WA ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA TAWALA KATIKA KIPINDI CHA MIEZI SITA
Mheshimiwa Spika,
8.
Wakati tukiendelea kutekeleza mpango wa MKUKUTA,
uongozi wa Serikali ya awamu ya nne ulipoingia madarakani, Wizara yangu
ilioanisha MKUKUTA na utekelezaji wa ahadi za Chama Tawala (CCM)
zilizobainishwa katika Ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2005.
Mheshimiwa Spika,
9.
Ilani ya Chama Tawala imebainisha wazi kinachotakiwa
kufanyika katika sekta zinazosimamiwa na Wizara yangu ili kuleta maendeleo
katika nchi yetu. Katika sekta ya
Viwanda, Ilani imeelekeza kuwa ifikapo mwaka 2010 kiwango cha ukuaji wa sekta
kifikie asilimia 15 kwa mwaka. Hii ni changamoto na hatua muhimu katika
mikakati ya kuwezesha kufikia kiwango cha Maendeleo ya kati ya Uchumi na
Viwanda ifikapo mwaka 2025 kama ilivyoonyeshwa kwenye Dira ya Maendeleo ya
Taifa. Aidha, katika sekta za Biashara
na Masoko, Ilani imeelekeza kuandaa mikakati itakayouwezesha uchumi wa Taifa
kuhimili ushindani na kulifanya Taifa letu liwe na uwezo madhubuti wa kushiriki
na kufaidika katika mfumo wa biashara kwenye masoko ya Kitaifa, Kikanda na
Kimataifa katika mazingira ya utandawazi.
Hii inatarajiwa kuwa kichocheo cha kuongeza uwezo wa uwekezaji na uzalishaji katika uchumi wa
ndani kwa kuzingatia fursa zilizopo za malighafi na masoko. Aidha, Ilani imesisitiza
kipaumbele kiwekwe katika shughuli za kupanua ajira kwa kuendeleza rasilimali
watu na wajasiriamali katika viwango vya viwanda vidogo na biashara ndogo.
Mheshimiwa Spika,
10.
Katika kipindi ambacho uongozi wa awamu ya nne
umekuwa madarakani, Wizara yangu imeweza kutekeleza yafuatayo kama sehemu ya
utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi:-
a) Zoezi la kumpata
mwekezaji wa Mradi wa Kuzalisha Magadi wa Ziwa Natron limekamilika. Uzalishaji wa magadi kwa ajili ya matumizi ya
mbolea, vioo, madawa na vigae unatarajiwa kuanza mwaka 2008. Aidha, Mradi unatarajiwa kutoa ajira kwa watu
wasiopungua 500;
b) Maandalizi ya
utekelezaji wa mradi wa makaa ya mawe ya Mchuchuma na mradi wa chuma wa Liganga
yamefikia hatua ya kuanza kubainisha wawekezaji;
c) Teknolojia mbalimbali
zinazofaa kutumika vijijini na mijini kwa kurahisisha kazi, kuendeleza viwanda
vidogo mijini na vijijini, kuhifadhi na kusindika mazao, pamoja na kuchangia
hifadhi ya mazingira zimeendelezwa na taasisi zilizo chini ya wizara. Teknolojia hizo zinajumuisha yafuatayo:-
·
Ukamilishaji wa maandalizi ya mradi wa wachimbaji
wadogo wa madini hadi hatua ya ufungaji wa mitambo Igunga, Tabora;
·
Majembe ya kukokotwa na ng’ombe yapatayo 5,352 katika
Mikoa tisa inayojumuisha Mwanza, Kagera, Arusha, Rukwa, Iringa, Dodoma,
Singida, Mbeya na Shinyanga yalitengenezwa;
·
Viwanda Vidogo 199 ambavyo vimeajiri watu 406
vilianzishwa;
·
Mafunzo mbali mbali ya ufundi yamefanyika katika kozi 59
kwa washiriki 2,254; kozi nane za usindikaji wa vyakula kwa wajasiriamali 160;
utengenezaji wa zana za kilimo na uchukuzi vijijini kwa wajasiriamali 23 pamoja
na utumiaji udongo-saruji katika ujenzi wa nyumba bora zenye gharama nafuu
vijijini kwa wajasiriamali 10.
·
Mashine ndogo 101 zilitengenezwa katika karakana za
Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO); na
·
Jumla ya mikopo 831 yenye thamani ya shilingi milioni 556
ilitolewa katika Mikoa 11 na kutoa
nafasi za ajira kwa watu 4,100.
d) Chama cha Hakimiliki na
Hakishiriki (Copyright Society of Tanzania - COSOTA) cha kulinda maslahi ya
wasanii kimejisajili katika taasisi ya kulinda maslahi ya wasanii duniani
(International Confederation of Authors and Composers - CISAC). Kwa
kujiandikisha huko, muziki wa Tanzania
utalindwa katika nchi mbalimbali ambazo ni wanachama wa CISAC;
e) Wakala wa Usajili wa Biashara
na Leseni (BRELA) imeanza kutumia sheria mpya (New Company Act No. 12 of 2002)
tangu tarehe 1 Machi 2006. Sheria hii inatoa fursa kwa wafanyabiashara kusajili
kampuni bila kulazimika kuorodhesha shughuli zote kwenye “Memorandum”
f) Kituo cha kutoa taarifa za
kibiashara kwa wananchi na wadau mbali mbali kuhusu haki za ubunifu
kimeanzishwa ndani ya BRELA;
g) Ujenzi wa tembe
bora 5 za ukaushaji wa tumbaku huko Mkoani Ruvuma zimekamilika na tayari zinatumiwa
na wakulima;
h) Viwango vya Ubora
vya Taifa 38 vimekamilishwa kwa bidhaa za huduma zikijumuisha nne katika nyanja
mbalimbali za uhandisi; 32 za vyakula, kemikali na nguo; na viwili vya
ufungashaji; na
i)
Leseni za ubora wa bidhaa saba zenye alama ya “tbs”
zikijumuisha
saba kwa viwanda vidogo 21 kwa viwanda vikubwa na 163 kwa bidhaa zinazoingizwa
kutoka nje.
D. UTEKELEZAJI
WA MALENGO YA BAJETI YA MWAKA 2005/06
Mheshimiwa Spika,
11.
Sehemu kubwa ya bajeti ya mwaka 2005/06 ililenga
katika kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini
Tanzania maarufu kwa jina la MKUKUTA. Wizara yangu ilielekeza nguvu katika
kuwaongezea uwezo wanaviwanda na wafanyabiashara wadogo kushiriki katika juhudi
za kukuza uchumi na kuondoa umaskini wa kipato. Msisitizo uliwekwa katika
kuendeleza wajasiriamali kwa kuwawezesha katika nyanja za kiufundi, masoko,
mawasiliano na huduma za kifedha hususan vyanzo vya mtaji. Ili kufikia malengo
hayo, Wizara yangu ilishirikiana na Taasisi zilizo chini yake na Sekta Binafsi
katika kuboresha mazingira wezeshaji katika sekta za Viwanda, Biashara na
Masoko.
D.1: Sekta ya
Viwanda
Mheshimiwa Spika,
12.
Katika kipindi cha mwaka
2005/06, sekta ya viwanda ililenga kufanya yafuatayo: -
a)
Kutekeleza sera na mikakati ya
kuendeleza sekta ya viwanda ili kukuza mchango wa sekta katika pato la Taifa;
b)
Kuendelea kuwaongezea uwezo
wanaviwanda na wafanyabiashara wadogo ushiriki wao katika shughuli za kukuza
uchumi na kupunguza umaskini wa kipato;
c)
Kutoa huduma za kiufundi na
kuendeleza ujasiriamali, masoko, mawasiliano na huduma za kifedha kwa ajili ya
mitaji;
d)
Kushirikiana na Taasisi zilizo
chini ya Wizara (SIDO, CAMARTEC, TEMDO, TIRDO, TBS na NDC) katika kuendeleza
sekta ya viwanda chini ya bajeti ya MKUKUTA; na
e)
Kushirikiana kwa karibu na
wenye viwanda ili kujua matatizo yao na kuyatafutia ufumbuzi.
Utekelezaji wa
Sera ya Maendeleo Endelevu ya Viwanda
Mheshimiwa Spika,
13.
Wizara iliendelea na utekelezaji wa Sera ya Maendeleo
Endelevu ya Viwanda (1996 – 2020) kwa kutekeleza programu mbali mbali ikiwa ni
pamoja na awamu ya pili ya Mpango wa Maendeleo ya Viwanda. Mpango huu unalenga katika kuhamasisha,
kuwezesha na kuelekeza wawekezaji binafsi katika kujenga viwanda vya usindikaji
wa mazao na bidhaa za kilimo ili kuongeza thamani, nafasi za ajira na kupunguza
uharibifu baada ya mavuno. Mradi wa majaribio wa kusindika matunda
ulioanzishwa huko Muheza, Tanga ni mmojawapo wa baadhi ya miradi katika lengo
kuu la kuongeza thamani ya mazao yanayolimwa ndani ya nchi. Kazi nyingine
iliyotekelezwa chini ya mpango huu wa awamu ya pili ni kutoa mafunzo ya
utengenezaji wa bidhaa za ngozi kwa watu wenye ulemavu ambapo vijana 10
walipatiwa mafunzo hayo yaliyoendeshwa na “Leather Association of Tanzania -
LAT”, kwa ushirikiano kati ya Wizara na UNIDO kwa lengo la kuwawezesha
kuanzisha miradi ya kujiajiri wenyewe.
Mheshimiwa Spika,
14.
Katika kipindi cha 2005/06, yamekuwepo maendeleo ya
kutia moyo katika sekta ya viwanda vya kuyeyusha chuma baada ya Serikali kuzuia
uuzaji nchi za nje chuma chakavu kinachoweza kuyeyushwa na viwanda vya hapa
nchini. Kutokana na hatua hiyo, viwanda sita vipya vimeanzishwa na kutoa nafasi
mpya za ajira kwa wananchi wasiopungua 1,000 na hivyo kuwaongezea kipato na
kupunguza umaskini. Aidha, Wizara imewakutanisha
wadau wa sekta ya chuma chakavu kwa lengo la kupata maoni
Mheshimiwa Spika,
15.
Wizara pia
iliandaa semina za kuhamasisha wamiliki wa viwanda kuhusu masuala ya kuhifadhi
na kulinda mazingira katika uzalishaji viwandani ambapo watendaji wakuu
viwandani wapatao 30 waliohudhuria semina hiyo walijifunza mengi yenye manufaa
ikiwa ni pamoja na Sera ya Mazingira, Sheria ya Mazingira, “Cleaner Production
Technology’’, ‘‘Environmental Impact Assessment’’ na ‘‘Environmental Audit”.
Aidha, walitoa maoni
Mheshimiwa Spika,
16.
Baada ya marekebisho ya Sheria ya
Maeneo Huru ya Uzalishaji wa Bidhaa za Kuuza Nje (Export Processing Zone - EPZ)
kukamilika na kupitishwa na Bunge tarehe 15 Februari 2006, Wizara imeunda
Mamlaka ya EPZ. Kuhusu upatikanaji wa
wawekezaji katika programu ya EPZ katika kipindi cha 2005/06, wawekezaji watano
walipewa leseni za uzalishaji (EPZ Operators’ Licence) ambao ni: Tsubasa Renew
Car (EA) Ltd, Dar es Salaam; Net Health Ltd, Arusha; Vector Health
International Ltd, Arusha; African Packaging International Ltd, Dar es Salaam;
na Metrec International Ltd, Dar es Salaam.
Aidha, wawekezaji watatu, Fruit Kin Concentrates Ltd, Kibaha; Net Health
Ltd, Arusha; na Vector Health Ltd, Arusha walipewa leseni ya ujenzi wa miundombinu
ya EPZ (EPZ Developers’ Licence). Jumla ya mtaji uliowekezwa katika EPZ hadi
sasa ni Dola za Kimarekani milioni 121.98.
Mheshimiwa Spika,
Ili
kubaini hali ya maendeleo ya viwanda nchini, katika kipindi cha mwaka 2005/06,
Wizara ilifanya ziara ya kutembelea viwanda katika kanda tatu ambazo ni Kanda
ya Ziwa, Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Mashariki ambayo ilisaidia katika
kudumisha ushirikiano na kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya viwanda. Aidha, ziara hizo zilisaidia kutathimini
mafanikio na changamoto zinazokabili viwanda na kuwezesha Serikali kubuni
mikakati ya kutatua matatizo na kuboresha mazingira ya uwekezaji katika sekta
ya viwanda.
Mheshimiwa Spika,
17.
Kwa ujumla uwekezaji katika viwanda
unaendelea kuongezeka na kutoa nafasi za ajira. Kati ya viwanda vipya
vilivyoanzishwa ni pamoja na
Mheshimiwa Spika,
18.
Kutokana na
hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Wizara
Mheshimiwa Spika,
19.
Katika
kipindi cha mwaka 2005, sekta ya viwanda ilikabiliwa na changamoto mbalimbali
zikiwemo upatikanaji wa umeme usio na uhakika na gharama kubwa ya nishati;
miundombinu duni hususan barabara za vijijini zinakotoka malighafi; kuporomoka
kwa thamani ya shilingi kulikochangia kuongezeka kwa gharama za malighafi na
vipuri kutoka nje pamoja na gharama kubwa za usafirishaji kutokana na kupanda
kwa bei ya mafuta na bidhaa za petroli.
Utekelezaji wa Sera ya Biashara
Mheshimiwa Spika,
20.
Sera ya
Taifa ya Biashara iliyozinduliwa rasmi mwezi Agosti 2003, ina madhumuni ya
kujenga uwezo wa Sekta Binafsi, Asasi na Taasisi za Umma katika ushindani wa
biashara. Aidha, Sera ya Taifa ya
Biashara inabainisha nyenzo zitakazotumika katika kupanua na kukuza biashara
kwa kuzingatia misingi ya kuongeza tija na ushindani katika sekta za uzalishaji
Mheshimiwa Spika,
21.
Sera ya
Taifa ya Biashara imeendelea kutekelezwa kwa kuendesha mafunzo kwa wadau
mbalimbali kutoka Wizara, Idara za Serikali, Taasisi na Sekta Binafsi katika
jitihada za kuwajengea uwezo wa kuchambua na kushiriki kwa manufaa katika
majadiliano ya Kimataifa. Aidha, Wizara
kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha, Kitengo cha Usimamizi wa Miradi (Project
Management Unit – PMU) iliendesha mafunzo maalum ya wiki sita kwa kutumia
wataalam kutoka Taasisi ya Biashara Duniani (World Trade Institute). Mafunzo hayo maalumu yalilenga kuboresha
uwezo wa kushiriki majadiliano katika Shirika la Biashara la Dunia (WTO),
kwenye maeneo ya kilimo, bidhaa za viwandani, biashara ya huduma, hakimiliki,
biashara na uwekezaji na utatuzi wa migogoro ya kibiashara. Aidha, Wizara kwa kushirikiana na Shirika la
Maendeleo la Denmark (DANIDA) kwa mwaka wa fedha 2005/06 imefadhili watumishi
24 wa Wizara, Idara za Serikali, Sekta Binafsi na Asasi nyingine kusomea
Shahada ya Uzamili ya Biashara ya Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam. Katika mwaka wa fedha 2006/07,
jumla ya wanafunzi 26 watajiunga na mafunzo hayo. Lengo la mafunzo hayo ni
kujenga uwezo wa wataalam kushiriki katika masuala ya biashara ya Kimataifa
ikiwa ni pamoja na kuwaongezea uwezo mahiri katika ujuzi wa mbinu za kushiriki
katika majadiliano ya biashara.
Mheshimiwa Spika,
22.
Dunia ya sasa ya utandawazi imeegemea sana kwenye
Biashara ya Kimataifa. Kwa kutambua
hili, Sera ya Biashara ya Taifa imeweka msukumo madhubuti katika kukuza mauzo
ya bidhaa zetu katika soko la nje.
Mauzo ya Nje
Mheshimiwa Spika,
23.
Kutokana na
utekelezaji wa msukumo huu, mauzo nje yamekuwa yakiongezeka mwaka hadi mwaka.
Mauzo ya nje yaliongezeka toka Dola za Kimarekani milioni 682.9 mwaka 1995 hadi
Dola za Kimarekani milioni 1,549.3 mwaka 2005.
Aidha,
kiwango cha ukuaji wa sekta ya biashara kiliongezeka toka asilimia 3.1 mwaka
1995 hadi asilimia 16.5 mwaka 2005, angalia Jedwali Na. 3 na Kielelezo Na. 2.
Mheshimiwa Spika,
24.
Katika
jitihada za kukuza biashara ya nje, Wizara imewezesha Halmashauri ya Biashara
ya Nje (BET) chini ya mpango wa MKUKUTA kuchangia zoezi la kuongeza msukumo wa
mauzo ya nje kwa kubuni mikakati mbalimbali. BET
ikishirikiana na Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) iliviunganisha vikundi
mbalimbali vya Sanaa za Mikono na kuunda Chama cha Kitaifa cha Sanaa za mikono
(Tanzania Handcraft Association – TanCraft). Katika mchakato huu, yaliandaliwa maonesho ya bidhaa hizo
na kuhudhuriwa na wanunuzi wa bidhaa
kutoka Marekani, Canada na Ulaya.
Wanunuzi hawa walipata fursa ya kubainisha mahitaji ya masoko yao na
kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na wajasiriamali wa Tanzania. Aidha, katika jitihada za kuendeleza na
kuongeza uzalishaji wa mazao ya viungo kwa ajili ya soko la nje, BET
ikishirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine imeanzisha mpango wa kuendeleza
zao la iliki katika Tarafa ya Turiani Wilaya ya Mvomero na mazao ya mdalasini
na pilipili manga katika Tarafa ya Mkuyuni Wilaya ya Morogoro Vijijini. Dhana ya utekelezaji ni ile ya kuwa na
“Export Production Villages” ambayo inahimiza aina moja ya zao kuzalishwa
katika eneo moja kwa lengo la kuongeza uzalishaji. Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, kinatoa
mafunzo na pia kusambaza mbegu bora kwa wakulima wa mfano bora walioteuliwa ili
hatimaye ujuzi huo uigwe na wakulima wengine.
Mheshimiwa Spika,
25.
BET
imefanikiwa kupata wakufunzi washauri 11 katika mpango wa pamoja wa Taasisi za
Afrika Mashariki zinazokuza Biashara ya Nje kwa ushirikiano na Kituo cha Kukuza
Uagizaji Bidhaa kutoka Nchi Zinazoendelea (Centre for Promotion of Imports from
Developing Countries) cha Uholanzi. Wakufunzi washauri watatumiwa na BET katika
programu zake za mafunzo kwa wajasiriamali na makundi mengine.
Mheshimiwa Spika,
26.
BET
iliratibu ushiriki wa
Mheshimiwa Spika,
27.
Katika mkakati wa kutafuta masoko
kwa bidhaa zetu, BET ilifanya utafiti wa soko la asali na nta ya
Mheshimiwa Spika,
28.
Manunuzi ya bidhaa kutoka nje yaliongezeka kutoka Dola za
Kimarekani milioni 1,340.5 mwaka 1995 hadi kufikia Dola za Kimarekani milioni 2,677.8 mwaka 2005. Kadhalika, manunuzi ya bidhaa kutoka nje
yaliongezeka toka asilimia 2.38 mwaka 1995 hadi kufikia asilimia 7.2 mwaka
2005, kama ilivyoonyeshwa katika Jedwali
Na. 3 na Kielelezo Na.2. Katika mwaka
2005, urari wa biashara ya bidhaa ulikuwa na nakisi ya Dola za Kimarekani
milioni 985.5, ikilinganishwa na nakisi za Dola za Kimarekani milioni 866.6
mwaka 2004 sawa na asilimia 13.7. Kuongezeka kwa nakisi katika urari wa
biashara ya bidhaa kulichangiwa zaidi na ongezeko la thamani ya bidhaa
zilizoagizwa kutoka nje ikilinganishwa na mauzo ya bidhaa nje. Aidha, urari wa
biashara ya huduma ulikuwa na ziada ya Dola za Kimarekani milioni 35.2 mwaka
2005 ikilinganishwa na ziada ya Dola za Kimarekani milioni 151.9 mwaka 2004.
Kupungua huko kulichangiwa na ongezeko kubwa la malipo ya huduma, hasa malipo
ya gharama za uingizaji mizigo pamoja na safari za nje ikilinganishwa na
ongezeko la mapato yaliyotokana na biashara ya huduma.
Fursa za masoko ya
masharti nafuu kwa nchi zinazoendelea
Mheshimiwa Spika,
29.
Kuwepo kwa fursa nyingine za masoko, kutawawezesha wafanyabiashara wa
Mheshimiwa Spika,
30.
Ushirikiano Kikanda; EAC na SADC
Mheshimiwa Spika,
31.
Mwenendo wa
biashara kati ya
Mheshimiwa Spika,
32.
Mabadiliko
ya kimuundo katika SADC yamewezesha kuanzishwa kwa mpango kamambe wa kimkakati
ujulikanao
Ushirikiano na nchi za
ACP na EU
Mheshimiwa Spika,
33.
Majadiliano ya utaratibu mpya wa kudumu wa ushirikiano
(Economic Partnership Agreements – EPAs) baina ya nchi za Afrika, Carribean na
Pacific (ACP) na Jumuiya ya Ulaya (EU) yanaendelea. Mpango huu ni wa kubadilishana fursa za
biashara yaani “nipe nikupe” (reciprocity) na unatarajiwa kuanza kutumika
ifikapo Januari 2008, kwa misingi ya Mkataba mama wa Cotonuo. Majadiliano ya kibiashara kati ya SADC na
Jumuiya ya Ulaya yanaendelea. Kwa upande wa SADC, katika majadiliano ya SADC/EPA na EU, Tanzania
imepewa jukumu la kuratibu majadiliano hayo katika Biashara ya Huduma na Sera
ya Uwekezaji na Ushindani. Maandalizi
haya yanaendeshwa na Serikali ikishirikiana na wadau katika kuweka misimamo ya
Kitaifa na Kikanda kuhusu maeneo yote yanayohusika katika majadiliano.
Utandawazi
Mheshimiwa Spika,
34.
Serikali
iliazimia kushiriki kikamilifu katika michakato ya Kimataifa kwa lengo la
kuboresha mazingira ya Biashara ya Kimataifa na utandawazi kwa ujumla yakiwamo
majadiliano ya
Mchango wa Taasisi za Uwezeshaji katika Sekta ya Biashara
Mheshimiwa Spika,
35.
Chuo cha
Elimu ya Biashara (CBE) kinatoa mafunzo ya taaluma za Uhasibu, Masoko, Ununuzi
na Ugavi ambayo yanawezesha watu mbalimbali kupata utaalamu wa kushiriki nyanja
mbalimbali za kuanzisha na kuendeleza biashara. Aidha, Chuo kina mpango wa
kupanua mtandao wa mafunzo ya elimu ya biashara kwa kuanzisha tawi jingine
Kanda ya Ziwa jijini Mwanza kwa lengo la kusogeza huduma zake karibu na
wananchi. Vile vile, CBE inaendesha mafunzo kwa mfumo wa masomoya jioni.
Mheshimiwa Spika,
36.
Uboreshaji
wa mitaala katika CBE kulingana na mahitaji ya soko unazingatiwa hasa katika
michepuo ya masoko, uhasibu, ununuzi na ugavi. Aidha, uenezaji wa elimu ya
biashara ya ujasiriamali, uendeshaji na usimamizi bora wa biashara ndogo na za
kati unatolewa na Chuo hiki. Pia, mafunzo ya ushauri na utafiti ya Ujasiriamali
yanatolewa kwa wafanyabiashara katika stadi za uhasibu, fedha, utunzaji
kumbukumbu za biashara na ukuzaji wa masoko na mauzo. Vile vile, Chuo kinatoa mafunzo ya ushauri wa
kitaalamu na utafiti vijijini kupitia Kitengo cha ujasiriamali.
Mheshimiwa Spika,
37.
Kituo cha
Kibiashara cha
Mheshimiwa Spika,
38.
Changamoto zinazoikabili sekta ya biashara ni pamoja na:
a)
Gharama kubwa za uzalishaji;
b)
Ufungashaji wa bidhaa usiofikia viwango vya ubora wa
Kimataifa;
c)
Ukosefu wa taarifa za masoko na taaluma ya utumiaji wa
teknolojia ya mawasiliano;
d)
Mwitikio mdogo wa
wawekezaji;
e)
Ukosefu wa teknolojia zinazoinua ufanisi wa uzalishaji wa
bidhaa nyingi na za viwango vya ubora unaokidhi mahitaji ya soko la Kimataifa;
f)
Kutokuwepo Maafisa Biashara Waambata katika Balozi zetu
nje ambao wangetafiti na kutoa taarifa
za ‘‘Market intelligence” na kuwa kiungo
kati ya Serikali na wafanyabiashara;
g)
Mfumo wa ushindani wa Biashara
ya Kimataifa usio wa haki;
h)
Kushindwa kuongeza thamani
katika bidhaa zetu;
i)
Kushindwa kupanua wigo wa
bidhaa na masoko; na
j)
Miundombinu hafifu.
Mheshimiwa Spika
39.
Hatua
zifuatazo zimechukuliwa ili kukabili changamoto hizo:
a)
Wizara inawezesha wadau kushiriki kikamilifu katika
majadiliano ya biashara ya kikanda na Kimataifa;
b)
Kupitishwa kwa sheria ya EPZ mwanzoni mwa mwaka 2002 na
marekebisho ya mwaka 2006 kutawezesha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi
kuzalisha bidhaa bora kwa ajili ya soko la nje;
c)
Katika kutatua tatizo la ukosefu wa taarifa za masoko,
tayari kituo cha taarifa za masoko (Trade Portal) kimeanzishwa BET, ikiwa ni
pamoja na vituo vya kupokea na kutoa taarifa za biashara (Reference Centres)
vilivyoko CBE, TCCIA, TBS, WVBM na Wizara ya Kilimo, ambapo wafanyabiashara
wanaweza kupata taarifa mbalimbali za masoko;
d)
Mchakato wa kuboresha maabara za Tanzania na kuzifanya
zitambulike (Accredited) na asasi za Kimataifa za viwango unaendelea;
e)
Katika kuimarisha Ofisi ya Geneva Wizara imeongeza
mtaalamu wa biashara katika ubalozi wa Tanzania Geneva, ikiwa ni pamoja na
mtaalamu mmoja kupata mafunzo kazini katika ubalozi huo; na
f)
Pamoja na kuimarisha Kituo cha Biashara cha Tanzania
kilichoko London; katika mwaka huu wa Fedha, Wizara itafungua kituo kingine
Dubai kwa ajili ya soko la Mashariki ya Kati.
D.3: Sekta ya
Masoko
Sera na Mkakati wa Maendeleo ya Masoko
Mheshimiwa Spika,
40.
Kwa kuwa maendeleo ya sekta ya kilimo hutegemea kwa kiasi
kikubwa upatikanaji wa masoko ya uhakika kwa mazao yanayozalishwa, Serikali
imekuwa ikifanya mabadiliko ya kisera na kimkakati ili kukuza masoko ya mazao
ya kilimo tangu mwanzoni mwa miaka ya tisini.
Baadhi ya matokeo ya mabadiliko haya yanajumuisha kuimarika kwa bei za
mazao; kuongezeka kwa uzalishaji na mauzo ya nje kwa baadhi ya mazao;
kuongezeka kwa vyanzo vya mikopo pamoja na kuboreshwa kwa miundombinu ya masoko
na mfumo wa upatikanaji wa taarifa za masoko. Aidha, mafanikio mengine
yanajumuisha yafuatayo:-
a)
Wizara kwa kushirikiana na Programu ya Kuendeleza Mifumo
ya Masoko ya Mazao imeviunganisha vikundi vya wakulima na masoko maalum ikiwa
ni pamoja na kuanzisha kilimo cha mkataba kwa mazao ya mboga mboga kati ya
wakulima wadogo na Kampuni zinazouza
mboga mboga katika soko la Jumuiya ya Ulaya;
b)
Kufanya utafiti wa zao la Vitunguu Wilayani Kilosa;
utafiti kuhusu biashara ya zao la Kahawa Mkoani Kagera ili kuainisha chanzo cha
kuwepo kwa biashara isiyo rasmi kati ya Mkoa huo na nchi za jirani unaoendelea
na uchunguzi wa vipimo vinavyotumika kununulia mazao kutoka kwa wakulima;
c)
Mafunzo ya ukusanyaji, uchambuzi na usambazaji wa taarifa
za masoko yalitolewa kwa wakusanyaji wa taarifa za masoko kutoka Wilaya 75. Vile vile, wakusanyaji wa taarifa hizo katika
ngazi ya Mkoa walipatiwa vitendea kazi zikiwemo kompyuta sita;
d)
Wizara imepanua wigo wa usambazaji wa taarifa za bei za
mazao kwa kupitia ujumbe mfupi wa maneno
katika simu za mikononi za Kampuni ya Vodacom Tanzania Limited; na
e)
Wizara imeboresha mfumo wa kuhifadhi na kuchambua taarifa
za masoko kwa kutumia kompyuta na programu maalumu kwa taarifa za masoko ya
mazao.
Pamoja na mafanikio hayo, bado kumekuwepo na changamoto zinazowakabili
wazalishaji, wasindikaji na wafanyabiashara wa mazao. Ili kuweka mwongozo wa kisera na kimkakati
katika kushughulikia changamoto za masoko ya mazao na bidhaa za kilimo,
Serikali iko katika hatua za mwisho za maandalizi ya Sera ya Masoko ya Mazao ya
Kilimo.
Ununuzi
wa Mazao Asilia
Mheshimiwa Spika,
41.
Mazao ambayo ununuzi wake uliongezeka katika msimu wa
mwaka 2005/06 ikilinganishwa na msimu wa mwaka 2004/05, yanajumuisha pamba
mbegu, tumbaku ya mvuke, korosho, mkonge, maua ya pareto na miwa. Jedwali Na. 8 na Kielelezo Na.7 vinatoa
takwimu za ongezeko kwa kila zao.
Kuongezeka kwa ununuzi wa mazao hayo kulitokana na kuongezeka kwa
uzalishaji. Aidha ununuzi wa mazao ya
tumbaku ya moshi, kahawa na chai ulipungua kama Jedwali Na. 8 na Kielelezo
Na.7 vinavyodhihirisha. Kushuka kwa
ununuzi wa kahawa na chai kulisababishwa na kushuka kwa uzalishaji ambao kwa
kiasi kikubwa kulisababishwa na ukame.
Bei ya Mkulima
(Producer Price)
Mheshimiwa Spika,
42.
Bei ya mkulima iliongezeka kwa mazao ya kahawa ya robusta,
kahawa ya arabica, chai pamoja na zao la miwa kwa mkataba (outgrowers)
kama Jedwali Na. 10a linavyoonyesha. Kuongezeka kwa bei ya mkulima kwa mazao ya
kahawa na chai kulisababishwa na kuimarika kwa bei ya mazao hayo katika soko la
dunia na kuongezeka kwa ubora wa mazao. Kwa mfano, bei ya kuuzia nje kahawa
aina ya arabica iliongezeka kwa asilimia 13 na bei ya chai iliongezeka
kwa asilimia 2. Aidha, bei ya mkulima
kwa zao la pamba ilishuka kutoka wastani wa Shilingi 250 kwa kilo msimu wa
2004/05 hadi Shilingi 220 kwa kilo msimu wa 2005/06 ikiwa ni anguko la asilimia
12, ona Jedwali Na. 10a.
Bei ya Kuuzia Nje (FoB
Price)
Mheshimiwa Spika,
43.
Bei ya kuuzia nje kahawa aina ya arabica iliongezeka
kwa asilimia 13, pamba asilimia 10, tumbaku ya moshi asilimia 25, chai asilimia
2 na mkonge asilimia 7. Bei ya kuuzia nje korosho ghafi na tumbaku ya mvuke
ilipungua kwa asilimia 17 na 20 sawia. Bei ya kuuzia nje korosho ghafi ilishuka
kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa zao hilo duniani. Uzalishaji wa
korosho duniani umeongezeka maradufu kutoka tani milioni 0.8 mwaka 1995 hadi
tani milioni 1.6 mwaka 2005. Zao jingine lililoonyesha kushuka kwa bei ya
kuuzia nje ni kahawa aina ya robusta ambayo ilishuka kwa asilimia moja kama
ilivyoonyeshwa kwenye Jedwali Na. 10b.
Mauzo ya Ndani
Mheshimiwa Spika,
44.
Mauzo ya korosho kwa wabanguaji wa ndani yaliongezeka
kutoka tani 7,070 msimu wa 2004/05 hadi tani 20,000 msimu wa 2005/06. Aidha,
jumla ya tani 381 za kahawa safi ziliuzwa kwa wasindikaji wa ndani msimu wa
2005/06 ikilinganishwa na tani 229 msimu
wa 2004/05. Jumla ya tani 363 za kahawa zilisindikwa katika viwanda vya ndani
msimu wa 2005/06 ikilinganishwa na tani 214 msimu wa 2004/05.
Mheshimiwa Spika,
45.
Jumla ya tani 3,000 za chai zenye thamani ya Shilingi
bilioni 3.6 zinatarajiwa kuuzwa katika
soko la ndani msimu 2005/06 ikilinganishwa na tani 4,329 zilizouzwa msimu wa
2004/05 zilizokuwa na thamani ya Shilingi
bilioni 4.3. Aidha, mauzo ya pamba kwa viwanda vya ndani msimu wa
2005/06 yamefikia tani 25,100 ikilinganishwa na tani 30,475 zilizouzwa msimu wa
2004/05. Msimu wa mauzo wa 2005/06 bado unaendelea.
Mauzo ya Nje
Mheshimiwa Spika,
46.
Katika msimu wa 2005/06 mauzo ya nje kwa mazao
makuu ya biashara yalipungua kwa mazao mengi isipokuwa zao la tumbaku na pareto
kama Jedwali Na. 9 linavyoonyesha.
Aidha, mauzo ya mkonge yalilingana na mauzo ya msimu uliotangulia ambapo
tani 11,693 ziliuzwa. Hata hivyo, thamani ya mauzo hayo iliongezeka kwa
asilimia 8 kutoka Dola za Kimarekani 8,214,505 hadi Dola za Kimarekani
8,899,694. Aidha, mauzo ya korosho ghafi
nje yalishuka kutokana na kuongezeka kwa wasindikaji wa ndani. Jumla ya tani
20,000 ziliuzwa kwa wasindikaji wa ndani msimu wa 2005/06 ikilinganishwa na
tani 7,070 msimu 2004/05.
Mheshimiwa Spika,
47.
Hadi kufikia mwezi Mei 2006, mauzo ya kahawa safi nje ya
nchi yalikuwa tani 31,356 na kuliingizia Taifa Dola za Kimarekani 59,406,628.
Msimu wa mauzo ya kahawa bado unaendelea. Jumla ya tani 42,517 za kahawa safi
zenye thamani ya Dola za Kimarekani 74,792,907 ziliuzwa nje ya nchi msimu wa
2004/05. Wanunuzi wakuu wa kahawa ya
Tanzania msimu wa 2005/06 walikuwa ni Japan (33%), Ujerumani (22%), Italia
(19%), Marekani (6%), Uswis (4%), Ubeligiji (4%), Uholanzi (4%) na nchi
nyingine (8%).
Mheshimiwa Spika,
48.
Mauzo ya nje kwa zao la pamba msimu wa 2005/06 hadi
Aprili 2006 yalifikia tani 83,362 ikilinganishwa na tani 84,021 zilizouzwa
msimu wa 2004/05. Msimu wa mauzo unaendelea na hivyo kuna uwezekano wa kuzidi
kiwango cha mauzo yaliyopatikana msimu wa 2004/05.
Mauzo ya Nje kwa Mazao ya Biashara Yasiyokuwa
Asilia
Mheshimiwa Spika,
49.
Thamani ya mauzo ya maua na
mboga nchi za nje yaliongezeka kutoka Dola za Kimarekani milioni 14.3 kipindi
cha msimu wa 2004/05 na kufikia Dola za Kimarekani milioni 18.3 msimu wa
2005/06. Ongezeko hili ni asilimia 28 na kwa kiasi kikubwa limetokana na
kuongezeka kwa wastani wa bei na matumizi katika soko la dunia pamoja na
kuongezeka kwa uzalishaji nchini.
Bei ya Mazao Makuu ya Chakula
Mheshimiwa Spika,
50.
Wastani wa bei ya mazao makuu
ya chakula hususan mahindi, mchele na maharage ulipanda mwishoni mwa mwaka 2005
na mwanzoni mwa mwaka 2006 kutokana na kupungua kwa ugavi wa mazao hayo,
kulikosababishwa na kuchelewa kwa msimu wa mvua za vuli na masika. Kwa mfano,
bei ya jumla ya gunia la mahindi la kilo 100 katika jiji la Dar es Salaam
ilipanda kutoka wastani wa Shilingi 15,438 mwezi Septemba 2005 hadi Shilingi
20,700 mwezi Desemba 2005 na kuendelea kupanda hadi kufikia wastani wa Shilingi
30,000 mwezi Machi 2006. Katika Jiji la Mbeya bei ya jumla ya mahindi
iliongezeka kutoka Shilingi 12,041 mwezi Septemba 2005 na kufikia Shilingi
29,916 mwezi Machi 2006. Bei ya mchele Jijini Dar es Salaam iliongezeka kutoka
Shilingi 52,958 mwezi Septemba 2005 na kufikia Shilingi 82,500 mwezi Machi
2006. Jijini Mbeya, bei ya jumla ya mchele iliongezeka kutoka Shilingi 44,833
mwezi Septemba 2005 na kufikia Shilingi 64,166 mwezi Machi 2006.
Mheshimiwa Spika,
51.
Tofauti kubwa ya bei ya mazao
makuu ya chakula kati ya masoko mbalimbali nchini ni kiashirio cha kuendelea
kuwepo kwa matatizo ya miundombinu duni ya masoko kama barabara za vijijini, magulio
au vituo vya kuuzia na kununulia mazao. Gharama kubwa za kusafirisha mazao
kutoka maeneo yanakozalishwa kwenda kwa walaji husabisha kushuka kwa bei
anayopata mzalishaji. Aidha, soko la mazao ya chakula bado linakabiliwa na
matatizo ya kiwango cha chini cha usindikaji wa mazao hayo, kukosekana kwa
mitaji kwa wafanyabiashara wadogo na udhaifu katika usimamizi wa uuzaji wa
mazao kulingana na madaraja, ubora na vipimo.
Mifugo na Mazao Yake
Mheshimiwa Spika,
52.
Sekta ya mifugo imeendelea
kutegemea soko la ndani kwa maendeleo yake. Sababu kubwa ya mifugo na bidhaa
zake kuendelea kutegemea soko la ndani ni pamoja na kuwepo kwa magonjwa ya
mifugo na ubora usiokidhi mahitaji na masharti katika masoko ya nchi za nje. Serikali imeendelea
kuweka mazingira mazuri yatakayowezesha bidhaa hizo ziweze kuuzwa katika masoko
ya Kimataifa. Tanzania huuza mifugo
katika nchi za Ghuba na Visiwa vya Comoro ingawaje biashara hii siyo kubwa.
Aidha, biashara ya mifugo isiyo rasmi hufanyika kati ya nchi yetu na nchi za jirani.
Mheshimiwa Spika,
53.
Ununuzi wa ngozi za ng'ombe, mbuzi na
kondoo katika msimu wa 2005/06 uliongezeka kwa asilimia 4 ikilinganishwa na
msimu wa 2004/05. Mapato ya wafugaji kutokana na mauzo hayo yaliongezeka kwa
asilimia 24 kutoka Shilingi bilioni 5.5 hadi Shilingi bilioni 6.2 msimu wa
2005/06 kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali
Na 11 na Kielelezo Na.8.
Aidha, mauzo ya ngozi nje ya nchi katika
kipindi hicho yaliongezeka kwa asilimia 8 kutoka vipande milioni 3.2 hadi
vipande milioni 3.7 na mapato kutokana na mauzo hayo yaliongezeka kwa asilimia
86 kama inavyonyeshwa kwenye Jedwali Na.
12 na Kielelezo Na.8.
Mheshimiwa Spika,
54.
Pamoja na kuwepo kwa fursa mbalimbali za masoko ndani
na nje ya nchi, Tanzania haijazitumia
fursa hizo kikamilifu kutokana na matatizo ambayo bado yanaukabili mfumo wa
masoko ya mazao ya kilimo nchini. Matatizo hayo ni pamoja na:
a)
Gharama kubwa za kufanya biashara ya mazao kutokana na
uduni wa miundombinu ya kusafirisha, kuhifadhi na kusindika mazao ya kilimo;
b)
Uduni wa ubora na uchache wa mazao yanayozalishwa na
hivyo kushindwa kushindana na bidhaa kutoka nchi nyingine hasa katika soko la
dunia;
c)
Upungufu wa
taarifa sahihi za masoko kwa wazalishaji, wasindikaji na wafanyabiashara;
d)
Uwezo mdogo wa kuyaongezea thamani mazao ambao pamoja na
sababu zingine unatokana na ukosefu wa mtaji;
e)
Udhaifu katika kusimamia sheria, kanuni na taratibu za
ununuzi wa mazao na hasa yale yasiyosimamiwa na Bodi za Mazao; na
f)
Kuongezeka kwa ushindani usiokuwa wa haki wa mazao na
bidhaa za kilimo zinazoingizwa kutoka nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika,
55.
Ili
kukabiliana na matatizo yanayoikabili sekta ya masoko ya mazao na bidhaa za
kilimo, Wizara ilichukua hatua zifuatazo: -
a) Kuandaa, kusimamia, kuratibu na
kufuatilia utekelezaji wa Sera, Sheria na kanuni zinazohusu masoko ya mazao na
bidhaa za kilimo kwa kutekeleza yafuatayo:-
·
Kukamilisha
Sera ya Masoko ya Mazao ya Kilimo;
·
Kukamilisha
Kanuni za Utekelezaji wa Sheria ya Stakabadhi za Mazao Ghalani ya mwaka 2005;
na
·
Kuhamasisha
wadau mbalimbali (wakulima, wafanyabiashara, taasisi za fedha) kuhusu matumizi
ya Mfumo huo.
b) Kuanzisha na kuendeleza mikakati ya
kukuza masoko ya mazao na bidhaa za kilimo ndani na nje ya nchi. Utekelezaji wa
jukumu hili ulihusisha yafuatayo:-
·
Kuhamasisha
wakulima na wasindikaji kuzalisha kulingana na mahitaji ya soko ili kuifanya
shughuli ya kilimo kuwa na manufaa;
·
Kuhamasisha uwekezaji katika miundombinu ya masoko na
uongezaji thamani wa mazao na bidhaa za kilimo;
·
Kuhamasisha
na kuendeleza matumizi ya mbinu mbalimbali za kukinga athari zinazojitokeza
katika masoko;
·
Kuhamasisha
na kuendeleza soko la ndani kwa mazao na bidhaa za kilimo zinazozalishwa
nchini;
·
Kuhamasisha
wakulima na wafanyabiashara kutumia fursa zilizopo za masoko ya kikanda na
Kimataifa; na
·
Kufanya tafiti mbalimbali za masoko ili kuainisha matatizo
kwa lengo la kuyatafutia ufumbuzi.
c) Kuboresha upatikanaji na usambazaji wa
taarifa za masoko ya mazao na bidhaa za kilimo. Utekelezaji wa hatua hii
ulihusisha:-
·
Kuandaa Kitabu cha Orodha ya Wanunuzi na Wasindikaji wa
Mazao ya Kilimo (Agribusiness Directory);
·
Kuimarisha
na kuendeleza mfumo wa ukusanyaji, uchambuzi, hifadhi na usambazaji wa taarifa
za masoko ikiwa ni pamoja na kuwezesha Halmashauri kutekeleza jukumu hilo.
d) Kusimamia utekelezaji wa Programu ya Kuendeleza Mifumo ya
Masoko. Utekelezaji wa jukumu hili unahusisha Wilaya 38 katika Mikoa nane kwa
kutekeleza yafuatayo:-
·
Kuwezesha maandalizi ya Sera
ya Masoko ya Mazao kwa kugharamia wataalamu, washauri waelekezi na mafunzo;
·
Programu ilitoa mafunzo kwa Wahandisi
na Mafundi kutoka Wilaya 18 na kukamilisha ujenzi wa masoko ya kisasa katika
maeneo ya Kikatiti (Arumeru), Matai (Sumbawanga) na Kwasadala (Hai). Pia ujenzi
wa ghala la kuhifadhia mazao katika mji mdogo wa Magugu (Babati) umekamilika na
ukarabati wa maghala katika vijiji vya Qash (Babati), Chimala (Mbarali) na
Iwindi (Mbeya) umefanyika. Aidha, jumla ya kilomita 210 za barabara za vijijini
zilijengwa katika Wilaya nane (Arumeru, Hai, Babati, Muheza, Mufindi, Mbeya,
Sumbawanga na Songea);
·
Mafunzo ya matumizi ya mfumo
wa stakabadhi za mazao ghalani yalitolewa kwa wanachama wa vyama vya kuweka na
kukopa (SACCOS), pamoja na kuunganisha
vyama hivyo na mabenki yanayotoa mikopo kwa ajili ya mfumo wa stakabadhi za mazao;
Benki za CRDB na Exim ndizo zilizokubali kutoa mikopo chini ya Mfumo wa
Stakabadhi za Mazao. Mfumo huu umeonyesha mafanikio makubwa kwa wakulima kupata
bei nzuri za mazao yaliyojaribiwa katika mfumo huo;
·
Kuboresha upatikanaji wa
mitaji na mbinu za kujikinga na maanguko ya bei za mazao kwa kutumia Mfumo wa
Stakabadhi za Mazao Ghalani; na
·
Kujasirisha wakulima na
wafanyabiashara wa mazao na bidhaa za kilimo na
kuwaunganisha na masoko.
e) Kusimamia Mradi wa Kuendeleza na
Kuboresha Biashara ya Pamba na Kahawa kwa kufanya kazi zifuatazo katika mwaka
2005/06: -
·
Kujadili na kupokea maoni ya wadau kuhusu Rasimu ya Kanuni za Sheria ya
Mfumo wa Stakabadhi za Mazao Ghalani;
·
Kushiriki katika mikutano ya wadau wa mazao ya pamba na kahawa kwa lengo
la kuboresha masoko ya mazao hayo na kufuatilia utekelezaji wa mradi; na
·
Kuandaa stakabadhi zitakazotumika katika Mfumo wa Stakabadhi za Mazao
Ghalani na kuendeelea kuhamasisha matumizi ya mfumo huo.
D.4: Sekta ya
Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo.
Utekelezaji wa
Sera ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo
Mheshimiwa Spika,
56.
Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo imeendelea
kutoa mchango muhimu katika ukuaji wa
uchumi. Maendeleo ya sekta hii ni muhimu hasa kwa vile pamoja na kuongeza
ajira, inasaidia kutoa msingi wa ujuzi na uzoefu kwa wanaviwanda na wafanyabiashara wadogo. Katika kuchochea maendeleo ya sekta hii, Wizara iliandaa Sera
ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo katika mwaka 2003. Sera hii
inalenga kuweka mazingira mazuri yatakayowezesha uanzishaji wa miradi mipya na
wakati huo huo kuwezesha miradi iliyopo kuimarika na kuongeza mchango wa sekta
hii katika pato la Taifa. Mikakati iliyoainishwa katika sera ni pamoja na
kuboresha mfumo wa sheria na taratibu; kuimarisha miundombinu; kuboresha huduma
za masoko, ujasiriamali, upatikanaji wa taarifa na teknolojia na pia kuboresha
upatikanaji wa huduma za kifedha.
Mheshimiwa Spika,
57.
Semina za kikanda zilifanyika ili kuendelea
kuelimisha wananchi juu ya Sera ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo na pia
kuwafahamisha juu ya fursa zilizopo. Vile vile, nakala ya sera katika lugha
rahisi inaandaliwa. Wizara imekwishaanza kuchukua hatua mbali mbali za
utekelezaji wa sera, hii ikiwa ni pamoja na maandalizi yaliyofanyika kwa
kushirikiana na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ya kuanzisha
programu ya kuendeleza viwanda vidogo na biashara ndogo vijijini. Kwa kuanzia,
programu hii itatekelezwa katika Mikoa ya Pwani, Tanga, Manyara, Mwanza, Iringa
na Ruvuma. Vile vile, Mfuko maalum wa kuchochea ukuaji wa viwanda vidogo na
biashara ndogo (SME competitiveness Facility) umeanzishwa kwa msaada wa Shirika
la Maendeleo la Denmark (DANIDA). Madhumuni ya mfuko huu ni kuwezesha
wajasiriamali wadogo kuimarisha ubora wa bidhaa zao ili kuweza kuyafikia masoko
ya nje. Vile vile, Wizara kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania imeendelea
kufuatilia utekelezaji wa mfuko wa kudhamini miradi ya viwanda vidogo na
biashara ndogo. Pia, Wizara inashirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO) kutekeleza mradi wa kuendeleza
wajasiriamali wanawake kwa kuwapatia mafunzo yanayochochea ujasiriamali,
uimarishaji wa vikundi vya uzalishaji na utafutaji wa masoko. Aidha, Wizara
imeendelea kuimarisha taasisi zinazohudumia sekta ya viwanda vidogo na biashara
ndogo, hii ikiwa ni pamoja na SIDO ili taasisi hizi ziimarishe utoaji wa huduma kwa wajasiriamali wadogo.
Mheshimiwa Spika,
58.
Katika kipindi
cha 2005/06, Wizara kupitia SIDO iliendelea kutoa huduma za kiufundi kwa
wajasiriamali wadogo ambapo, jumla ya mashine 383 zilitengenezwa na
wajasiriamali 540 walipatiwa mafunzo ya kiufundi. Pia, jumla ya
wajasiriamali 4,926 walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali na mbinu za biashara,
wajasiriamali 1,066 walipatiwa mafunzo ya usindikaji na uhifadhi wa vyakula na wajasiriamali 4,200
walipatiwa ushauri. Aidha,
wajasiriamali wadogo 968 walipata fursa ya kushiriki katika maonesho ya kikanda
yanayoendeshwa na SIDO ambapo waliweza kufanya mauzo ya shs. 120 millioni na pia kupata oda za Shilingi milioni 160.
Mheshimiwa Spika,
59.
Miradi ya kuendeleza ardhi na
miundombinu kwa ajili ya viwanda vidogo na biashara ndogo inayotekelezwa ni
pamoja na:- vituo vya biashara vya
Songea na Moshi; uimarishaji wa kituo cha mafunzo na uzalishaji cha Njombe;
ujenzi wa majengo ya wafanyabiashara wadogo katika miji ya Makambako na Babati;
ujenzi na uimarishaji wa majengo kwa ajili ya viatamizi kwa ajili ya Dar es
Salaam na Mbeya; na ujenzi wa vituo vya wajasiriamali kuoneshea bidhaa zao.
Aidha, kwa kutumia utaratibu wa kushirikisha Sekta Binafsi kuendeleza maeneo,
ujenzi wa majengo ya viwanda unaendelea katika mitaa ya viwanda iliyoko Mikoa
ya Mwanza na Ruvuma.
Mheshimiwa Spika,
60.
Serikali iliendelea kusambaza teknolojia
mbalimbali zilizobuniwa, kuzalishwa na kujaribiwa ili ziwafikie walengwa na
ziweze kuchangia katika kuongeza ufanisi wa uzalishaji mali, kuongeza ajira na
kipato na hatimaye kupunguza umaskini. Mashine za kuwasaidia wakulima katika
kilimo na usindikaji wa mazao ya kilimo zilitengenezwa na Taasisi za TEMDO,
CAMARTEC, TIRDO, ‘‘Technology
Development and Transfer Centre’’
na SIDO.
Mheshimiwa Spika,
61.
Mfuko wa Wafanyabiashara Wananchi
– NEDF ulioanzishwa mwaka 1994 hadi kufikia mwezi Machi, 2006 ulikuwa umetoa mitaji yenye
thamani ya Shilingi bilioni 8.34 kwa wajasiriamali 23,578 na kuwezesha
upatikanaji wa ajira kwa wananchi 33,404.
Mwaka 2005/06 mfuko ulitoa mikopo ya thamani ya Shilingi milioni
285. Aidha, wajasiriamali wadogo 268
walipatiwa mikopo yenye thamani ya Shilingi milioni 481 kutoka Mfuko wa Mitaji
ya Mikoa unaosimamiwa na SIDO na wengine 44 walipatiwa mikopo yenye thamani ya
Shilingi milioni 243 kutoka mfuko ulioanzishwa na SIDO kwa kutumia fedha za
Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Spika,
62.
Sekta ya viwanda vidogo na biashara
ndogo nchini bado inakabiliwa na changamoto mbali mbali. Hii ni pamoja na
mwamko mdogo wa wananchi kuzitumia fursa zilizopo, uwezo mdogo wa taasisi
zinazoihudumia sekta, ukosefu wa taarifa muhimu hususan kuhusu masoko, matumizi
ya teknolojia na miundombinu duni, pamoja na kushindwa kunufaika na mitaji
inayotolewa na taasisi za fedha, ikijumuisha kushindwa kumudu masharti ya
mikopo.
Mheshimiwa
Spika,
63.
CAMARTEC iliendelea kueneza teknolojia ya ‘‘biogas’’,
majiko sanifu na teknolojia ya udongo-saruji.
Katika kipindi hicho, mafunzo na ujenzi wa mtambo wa ‘‘biogas’’ wenye
mita za ujazo 16 vilifanyika mjini Dar es Salaam kwa mafundi waashi
watano. Pia mtambo mmoja wenye ukubwa wa
mita 50 za ujazo ulitengenezwa kituoni CAMARTEC. Mafunzo kuhusu Teknolojia ya majiko sanifu
yalitolewa kwa wajasiriamali 20 waliofundishwa katika Wilaya za Rombo na Ulanga. Katika Wilaya ya Kondoa mafunzo ya teknolojia
ya udongo–saruji yalitolewa kwa wajasiriamali sita kwa ajili ya ujenzi wa
nyumba bora vijijini.
Mheshimiwa Spika,
64.
TEMDO
katika mwaka 2005 ilibuni teknolojia ambazo zililenga katika kuboresha hali ya maisha
ya wananchi walio wengi pamoja na kuendeleza ujasiriamali na kuongeza
ajira. TEMDO katika kipindi hicho
iliendeleza teknolojia za kukamua mafuta ya alizeti, kusindika matunda na
kupukuchua mahindi. Lengo ni kueneza
teknolojia hizo vijijini ili kurahisisha kazi na kuhamasisha uanzishaji wa
viwanda vidogo vya kusindika mazao ya kilimo.
Mheshimiwa Spika,
65.
TIRDO
katika kipindi cha mwaka 2005 ilibuni teknolojia ambazo zililenga katika
kuboresha hali ya maisha ya wananchi, kuendeleza ujasiriamali na kuongeza
ajira. TIRDO katika kipindi hicho imetoa mafunzo ya uchomeleaji vyuma kwa
wazalishaji wadogo na wajasiriamali 75 huko Morogoro,
Mheshimiwa Spika,
66.
TIRDO imeendelea kutoa mafunzo ya kilimo cha uyoga kwa
wakulima 237 katika Mikoa ya Kilimanjaro, Morogoro na Dar es Salaam.
Wazalishaji wadogo 20 wamefundishwa jinsi ya kutumia mtambo wa majaribio wa
kutengeneza chumvi wenye uwezo wa kuzalisha tani nne kwa wiki katika Mkoa wa
Singida. Kuhusu utengenezaji wa chaki wajasiriamali 154 wamefundishwa katika
Wilaya za Nzega, Ulanga (Mahenge) na Songea. Mafunzo hayo yanaendelea katika
Mikoa ya Morogoro na Mtwara. Katika kuongeza thamani ya mwani, Shirika
limefundisha wakulima wa mwani 85 katika Wilaya za Muheza na Pangani. Aidha,
vikundi vinne vya wajasiriamali 82, vimefundishwa juu ya ukusanyaji, usafishaji
na kurejea taka za plastiki na karatasi kwa lengo la kutunza mazingira na
kuongeza ajira.
Mheshimiwa Spika,
67.
Katika
kutekeleza majukumu yao, taasisi hizi za utafiti zimekuwa zikikabiliwa na
matatizo kama vile uwezo mdogo kifedha kwa ajili ya kufanya tafiti, uwezo mdogo
wa wajasiriamali kuzalisha kibiashara teknolojia zilizopasishwa kwa matumizi,
uwezo mdogo wa kutangaza teknolojia zilizopasishwa, uwezo mdogo wa walengwa
kununua na kutumia teknolojia zinazobuniwa, na kupanda kwa gharama za
malighafi. Aidha, viwanda vinavyomilikiwa na Makampuni ya Kimataifa hupendelea
kutumia kampuni mama katika utafiti na hivyo kutotumia huduma za taasisi zetu.
Mheshimiwa Spika,
68.
Hatua
zilizochukuliwa ili kukwamua matatizo ya Taasisi hizo ni pamoja na serikali
kuzitengea fedha kutokana na bajeti ya MKUKUTA ili kuziwezesha kufanya tafiti
mbalimbali na kutangaza teknolojia zilizokwisha pasishwa ziweze kufikia walengwa.
Aidha, Wizara kwa kushirikiana na wadau wengine imeendelea kufanya marekebisho
ya sheria zilizoanzisha taasisi hizi ili ziendane na wakati.
D.6: Usimamiaji
wa Sheria za Udhibiti
Mheshimiwa Spika,
69.
BRELA iliendelea kutekeleza
majukumu yake ya usajili na kusimamia sheria ya makampuni, majina ya biashara,
alama za biashara, hataza, na sheria ya leseni ya viwanda. Katika mwaka
2005/06, ufanisi wa utendaji kazi wa wakala ulikuwa na matokeo na mabadiliko
mazuri ambapo uandikishaji wa shughuli zitolewazo na Wakala uliongezeka,
usajili wa kampuni ambao haukuwa na muda maalum kwa sasa usajili unapatikana
kati ya siku tatu hadi tano kuanzia siku maombi yalipopokelewa. Vivyo hivyo, kazi ya usajili wa majina ya
biashara hukamilika ndani ya siku moja hadi tatu. Muda anaotumia mteja kupata
huduma ulipungua, kiwango cha kutii sheria kwenye makampuni na kufuata taratibu
zake uliongezeka na mapato ya wakala.
Mheshimiwa Spika,
70.
BRELA imefanikiwa kupunguza
kero za wateja na washitiri wake katika kusubiri muda mrefu kuandikisha
kampuni, jina la biashara na kupata leseni ya viwanda kwa kuondoa masharti
yasiyokuwa ya lazima. Mafanikio mengine ni pamoja na Sheria mpya ya Makampuni
Na.12 ya mwaka 2002 kuanza kutekelezwa mwezi Machi 2006. Mafanikio hayo yamewezesha kuongezeka kwa
majina ya biashara zinazosajiliwa kutoka 5,890 mwaka 2004/05 hadi 7,409 mwaka
2005/06 na makampuni yaliyoandikishwa kutoka 3,347 mwaka 2004/05 hadi 3,791
mwaka 2005/06. Ongezeko
Mheshimiwa Spika,
71.
Wakala wa Vipimo (WMA) uliendelea kutekeleza wajibu
wake kwa mujibu wa Sheria na Kanuni ili kuhakikisha kuwa kuna biashara ya haki
kati ya wadau. Katika mwaka 2005/06,
Wakala ulichukua hatua madhubuti ya kuelimisha wananchi kuhusu matumizi sahihi
ya vipimo. Kwa kuanzia, mafunzo hayo yalitolewa katika Mikoa ya nyanda za juu
kusini. Vile vile, wafanyabiashara wameendelea kupewa ushauri kuhusu vipimo
wanavyostahili kuvitumia. Elimu hiyo pia
ilitolewa kupitia matangazo katika vyombo vya habari
Ubora
Mheshimiwa Spika,
72.
TBS
iliendelea na majukumu ya uwekaji viwango vya ubora wa bidhaa na usimamiaji
wake. Hadi kufikia mwezi Machi 2006,
Shirika lilikuwa limetayarisha Viwango vya Taifa 957 katika sekta mbalimbali
zikiwemo za kilimo na chakula, nguo, kemikali, uhandisi na mazingira. Aidha, Shirika liliendelea kusimamia
utekelezaji wa Viwango vya Taifa kwa kutumia mifumo iliyopo ya kuhakiki ubora
(certification scheme). Hadi kufikia
mwezi Machi 2006, Shirika lilikuwa limetoa jumla ya leseni 706 za ubora wa
bidhaa mbalimbali katika viwanda 433 vya humu nchini.
Mheshimiwa Spika,
73.
Pamoja na
mafanikio hayo, TBS inakabiliwa na uchakavu wa vifaa vya maabara na uhaba wa
nyenzo nyingine zinazotumika kupima na kudhibiti viwango vya ubora wa bidhaa
mbalimbali. Pia, uelewa mdogo wa umma na wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa
viwango vya ubora katika kulinda afya na usalama wa mlaji na kuzifanya bidhaa
zikubalike katika soko la Kimataifa.
Mheshimiwa Spika,
74.
TBS kwa kushirikiana na
taasisi mbalimbali za Kimataifa ikiwemo DANIDA, Sida, UNIDO, UNFPA na FAO,
ilifanikisha upatikanaji wa vyombo na mahitaji mbalimbali ya maabara. Aidha,
TBS kwa msaada wa Sida waliweza kutoa mafunzo kwa umma na jumuiya ya
wafanyabiashara juu ya umuhimu wa viwango vya ubora wa bidhaa.
Ushindani wa Haki
Mheshimiwa Spika,
75.
Katika kipindi
cha mwaka 2005/06, maandalizi ya utekelezaji wa Sheria mpya ya Ushindani 2003,
yalifikia hatua ya kuteua Mwenyekiti, Mkurugenzi Mkuu, Makamishna wa Tume ya
Ushindani pamoja na Mwenyekiti na Wajumbe wa Baraza la Ushindani mwezi Novemba
2005. Baada ya uteuzi huo, Makamishna wa Tume na Wajumbe wa Baraza la Ushindani
walipata mafunzo ya awali mwezi Desemba 2005 kuhusu sheria na wajibu wao. Vyombo hivi sasa vinakamilisha ajira ili
kuweza kutekeleza vyema majukumu yake. Aidha, Baraza la Taifa la Ushauri kwa
Mlaji lilianzishwa mwezi Julai 2005.
E. MWELEKEO
KATIKA SEKTA ZA VIWANDA, BIASHARA NA MASOKO KWA MWAKA 2006/07
Mheshimiwa Spika,
76.
Katika
kipindi cha mwaka 2006/07, Wizara yangu itaendelea kutekeleza MKUKUTA na Ilani
ya Uchaguzi ya Chama Tawala ya mwaka 2005.
Kama nilivyokwishasema, Ilani hiyo, imebainisha wazi mwelekeo wa Sekta
za Viwanda, Biashara na Masoko kama ifutavyo: - Sekta ya Viwanda ikue kwa
asilimia 15 ifikapo 2010; Sekta za Biashara na Masoko zijenge uwezo wa
kushiriki na kufaidika na mfumo wa Biashara ya Kikanda na Kimataifa katika mazingira
ya utandawazi. Katika hili Wizara inalenga kutekeleza
E.1: Sekta ya
Viwanda
Mheshimiwa Spika,
77.
Katika mwaka 2006/07, mkazo umewekwa katika juhudi za kuanzisha viwanda mama, kwa kutafuta wabia wa
kuwekeza katika mradi wa makaa ya mawe ya Mchuchuma, mradi wa chuma wa Liganga
na tafiti za miradi mingine iliyo katika Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara.
Kipaumbele kingine ni kuendelea na utekelezaji wa programu inayolenga katika
kuimarisha usindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo na maliasili; kuendelea
kuhamasisha uanzishaji wa maeneo ya uzalishaji kwa ajili ya uuzaji nje (EPZ)
pamoja na uwekezaji katika viwanda ndani ya maeneo hayo.
Mheshimiwa Spika,
78.
Changamoto
kubwa ambazo zinaikabili sekta ya Viwanda ni pamoja na ukosefu wa vyanzo vya
mikopo ya muda mrefu kwa ajili ya uwekezaji katika sekta ya Viwanda, Ufinyu wa
soko la ndani unaotokana na kasumba ya wananchi kuthamini na kupendelea kununua
bidhaa kutoka nje badala ya zinazotengenezwa na viwanda vya hapa nchini hata
kama vina ubora wa juu ikilinganishwa na bidhaa za aina hiyo toka nje. Vile vile, kutokana na wananchi wengi kuwa na
kipato kidogo uwezo wao wa kununua bidhaa za viwandani ni mdogo. Changamoto
nyingine ni kushindwa kufikia viwango vya ubora wa bidhaa na mbinu za utafutaji
masoko ya bidhaa ili kuweza kushindana vema katika soko la Kimataifa na la
ndani. Vile vile, upungufu wa wataalamu
hasa katika fani ya taaluma maalum kwa mfano wataalam wa nguo (textiles
technologists) na ngozi (leather technologists).
Mheshimiwa Spika,
79.
Ili
kukamilisha malengo ya mwelekeo huo na kukabili changamoto, kazi zifuatazo zimepangwa
kutekelezwa katika kipindi cha mwaka 2006/07: -
a)
Kuandaa taarifa
kuhusu fursa za uwekezaji katika miradi ya maendeleo ya viwanda (project
profiles);
b)
Kuendelea kutekeleza
mkakati wa kuimarisha sekta ya ngozi na viwanda vya ngozi;
c)
Kuwezesha na kuhamasisha
uanzishaji wa viwanda vya kusindika
mazao ya kilimo, mifugo, maliasili na viwanda vya msingi;
d)
Kuimarisha Mamlaka ya
EPZ pamoja na BET ili kuongeza juhudi za kuongeza mauzo ya nje;
e)
Kutekeleza mkakati wa kuhifadhi Mazingira ya Ardhi na
Vyanzo vya Maji na kufuatilia utekelezaji wa tamko la serikali la kupiga
marufuku utengenezaji wa mifuko laini ya plastiki;
f)
Kuweka utaratibu wa kudumu wa biashara ya chuma chakavu;
g)
Kuimarisha taasisi za utafiti na maendeleo ya
viwanda hususan, CAMARTEC, TEMDO, TIRDO; na
h)
Kushirikiana na Sekta Binafsi katika kubuni mikakati
ya kuendeleza sekta ya viwanda kwa lengo la kukuza mchango wa sekta hiyo katika
maendeleo ya uchumi wa Taifa.
Mheshimiwa Spika,
80.
Wizara
itaendelea kushirikiana na Wizara na Taasisi nyingine pamoja na Sekta Binafsi
katika kubainisha na kutafuta ufumbuzi wa matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja
na matatizo ya upatikanaji wa mikopo ya muda mrefu kwa wawekezaji. Aidha,
Serikali itaendelea kuvutia na kuhamasisha wawekezaji wa nje na wa ndani kwa
kubainisha fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali za viwanda na fursa za
mitaji. Pia, Wizara itaendelea
kuhamasisha wananchi kwa kufanya kampeni ya ‘NUNUA BIDHAA ZA TANZANIA JENGA
E.2: Sekta
ya Biashara
Mheshimiwa Spika,
81.
Katika mwaka 2006/07, Sekta ya Biashara inaandaa
mikakati itakayouwezesha uchumi wa Taifa kuhimili ushindani na kuweza kushiriki
kikamilifu na kufaidika na mfumo wa biashara katika mazingira ya utandawazi
kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani ya uchaguzi.
Vile vile, Wizara itaendelea na utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Biashara, katika
kutekeleza malengo ya MKUKUTA. Aidha, masuala muhimu ni pamoja na kukuza na
kuendeleza biashara na nchi mbalimbali, kuendeleza ushirikiano wa kibiashara na
nchi za Mashariki ya Mbali na Mashariki ya Kati kwa lengo la kupanua wigo wa
masoko badala ya kuendelea kutegemea masoko asilia ya nchi za Ulaya Magharibi. Aidha, Wizara yangu
itatoa elimu kwa wananchi juu ya kanuni za masoko na biashara nchi za nje
hususan Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Forodha wa
Afrika Mashariki (EAC Customs Union) na nchi nyingine ambazo zinatoa upendeleo
kwa bidhaa zinazozalishwa katika nchi zinazoendelea kwa lengo la kupanua soko la bidhaa zetu na
kuvutia wawekezaji.
Mheshimiwa Spika,
82.
Katika
kuendeleza biashara, changamoto zinazoikabili sekta ya biashara ni uwezo mdogo
wa uzalishaji wa bidhaa kukidhi mahitaji ya soko, kupanua wigo wa bidhaa
tunazozalisha, kuhakikisha
Mheshimiwa Spika,
83.
Katika kuitangaza Tanzania nje, Kituo cha Biashara cha
Tanzania kilichopo London kitaendelea kushirikiana na Makampuni Binafsi,
Mashirika na Mamlaka mbalimbali ili kuongeza ufanisi wa mauzo ya bidhaa na
mazao ya asili kwa lengo la kuliongezea Taifa mapato ya fedha za kigeni. Kituo hiki cha biashara kitaendeleza mkakati
wa kuitangaza Tanzania kiutalii katika vyombo vya habari nchini Uingereza.
Aidha, Wizara yangu kupitia Chama cha Hakimiliki na Hakishiriki cha Tanzania
(COSOTA) itaendelea kuboresha zoezi la ukusanyaji wa mirabaha kutoka maeneo
mbali mbali baada ya kuchapisha Kanuni za Usajili wa Wanachama na Kazi Zao ya
mwaka 2005 (The copyright Registration of Members and their works Regulations
2005).
Mheshimiwa Spika,
84.
Katika kipindi cha mwaka 2006/07, BET itaboresha Maonesho
ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam ambayo sasa yanatambulika na Chama
Kinachosimamia Maonesho Duniani (Union des Foires Internationale - UFI). Lengo ni kuendeleza viwanja vya maonesho vya
Mwalimu J.K.Nyerere kufikia kiwango cha ubora wa Kimataifa. Vile vile, BET itaendelea kutoa mafunzo kwa
wajasiriamali wapatao 100, kuhusu ubora wa bidhaa, utaalamu wa kuuza nje kwa
ujumla na jinsi ya kuzitumia fursa za upendeleo zinazopatikana katika masoko
kadhaa. Aidha, Wizara itaendeleza kampeni ya “NUNUA BIDHAA ZA TANZANIA JENGA
TANZANIA”. Vile vile, nachukua fursa hii
kuzipongeza Wizara zilizoshiriki kwenye Maonesho ya 30 ya Biashara ya Kimataifa
ya Dar es Salaam na hasa Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda, Biashara na
Masoko ambazo zimeshiriki kwa mara ya kwanza. Natoa mwito kwa Wizara nyingine
nazo kushiriki kwani hii ni fursa nzuri ya kuwaonyesha na kueleza umma wa
Watanzania kuhusu fursa mbali mbali za shughuli za serikali kwa maendeleo ya
wananchi. BET pia, itaendelea kufikisha huduma za kutoa habari za biashara
“Tele-Centres” katika Mikoa ya Morogoro na Mbeya. Kwa upande wa Zanzibar BET itaimarisha na
kuongeza wafanyakazi na vitendea kazi.
Aidha, Serikali inakusudia kuiunda upya BET kuwa Mamlaka ya Maendeleo ya
Biashara (Tanzania Trade Development Authority) yenye jukumu la kuendeleza
biashara na wafanyabiashara. Hatua hiyo
inalenga kuiwezesha Mamlaka hiyo kusimamia maendeleo ya biashara vizuri zaidi.
Mheshimiwa
Spika,
85.
Sekta ya Biashara katika kipindi cha mwaka 2006/07 itaendelea
kutekeleza yafuatayo:-
a)
Kuendelea kutekeleza Sera ya Taifa ya Biashara;
b)
Kuainisha na kuandaa mkakati wa utekelezaji wa fursa
zitokanazo na makubaliano ya WTO;
c)
Kuendelea kufanya mashauriano na wadau kuhusu programu ya
kuainisha matatizo yanayokwamisha biashara (Diagnostic Trade Integration Study
- DTIS);
d)
Wizara kwa
kushirikiana na DANIDA itafadhili watumishi 26 wa Wizara, Idara za Serikali,
Sekta Binafsi na Asasi zingine kuchukua
mafunzo ya Shahada ya Uzamili ya Biashara ya Kimataifa katika Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam;
e)
Kuendeleza
shughuli za vituo vya kupokelea na kutolea taarifa mbalimbali zilizoanzishwa na
mpango wa pamoja (UNCTAD/WTO/ITC) wa kujenga uwezo wa kitaalamu katika muasuala
ya biashara;
f)
Kuendelea na majadiliano ya EPAs baina ya nchi
zinazoendelea na Jumuiya ya Ulaya;
g)
Kuendelea kuboresha mazingira
ya biashara nchini ikiwa ni pamoja na kukamilisha utaratibu wa uandikishaji wa
biashara badala ya utaratibu wa utoaji wa leseni;
h)
Kuendeleza mkakati wa
kurasimisha biashara; na
i)
Kamati ya Kitaifa ya kusimamia utekelezaji wa mpango wa
AGOA itaimarishwa kwa madhumuni ya kutoa ushauri katika masuala ya utekelezaji
na uenezaji wa taarifa za masoko kwa Sekta Binafsi ili waweze kuuza zaidi
kupitia mpango wa AGOA;
E.3: Sekta ya Masoko
Mheshimiwa Spika,
86.
Malengo ya sekta ya Maendeleo ya Masoko ya mazao na bidhaa za kilimo kwa
mwaka 2006/07 ni kuendelea na jitihada za kuwezesha mazao ya wakulima kuuzwa
kwa bei ya kuridhisha kulingana na mahitaji ya ubora wa soko la ndani na nje.
Vile vile, mwelekeo wa sekta ya masoko ya mazao ya kilimo ni kuendeleza
usindikaji wa mazao yanayozalishwa hapa nchini ili kuongeza thamani na nafasi
za ajira. Pia, kuhakikisha upatikanaji wa masoko kwa bidhaa zisizokuwa za
kilimo.
Mheshimiwa Spika,
87.
Changamoto zinazoendelea kukabili masoko ya mazao na bidhaa za kilimo
nchini ni pamoja na kuporomoka mara kwa mara kwa bei za mazao katika masoko ya
Kimataifa; miundombinu duni ya masoko ya mazao; uzalishaji mdogo usiokidhi
wingi na viwango vya ubora unaohitajika katika masoko ya Kimataifa; kuongezeka
kwa ushindani wa Kimataifa usiokuwa wa haki; kuongezeka kwa matumizi ya mazao
na bidhaa mbadala; na kuwepo kwa magonjwa ya mifugo na mimea yanayoathiri
Biashara ya Kimataifa.
Mheshimiwa Spika,
88.
Ili kuhakikisha upatikanaji wa masoko ya uhakika, Wizara
imepanga kufanya mambo yafuatayo katika kipindi cha mwaka 2006/07:-
a)
Kukamilisha Sera na Mkakati wa Masoko ya Mazao ya Kilimo
nchini;
b)
Kuimarisha na kuendeleza mfumo wa ukusanyaji, uchambuzi
na usambazaji wa taarifa za masoko;
c)
Kuwezesha mchakato wa ujenzi wa masoko ya Kimataifa ya
mazao ya kilimo na bidhaa zake;
d)
Kufanya tathmini ya uboreshaji wa miundombinu ya masoko;
e)
Kukamilisha Kitabu cha Orodha ya Wanunuzi na wasindikaji
wa mazao;
f)
Kuelimisha wadau kuhusu maendeleo ya masoko ya mazao na
bidhaa ndani ya nchi na katika Jumuiya za Ushirikiano wa Kibiashara (EAC, SADC,
EU) na nchi nyingine;
g)
Kuimarisha uwezo wa Halmashauri na Manispaa kukusanya na
kusambaza taarifa za masoko;
h)
Wizara itaendelea kushirikiana
na Ofisi ya Waziri Mkuu na wadau wengine kuratibu na kusimamia Programu ya
Kuendeleza Mifumo ya Masoko ya Mazao ya Kilimo;
i)
Kuendelea kutekeleza Mradi wa Kuendeleza na Kuboresha
Biashara ya Pamba na Kahawa hususan utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi za Mazao
Ghalani; na
j)
Kuendeleza soko la ndani kwa kukuza matumizi ya mazao na
bidhaa mbali mbali zinazozalishwa nchini.
E.4: Sekta ya
Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo
Mheshimiwa Spika,
89.
Katika kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na
Biashara Ndogo kwa mwaka 2006/07, msukumo utawekwa katika kuhamasisha
uanzishaji na uimarishaji wa viwanda vidogo na biashara ndogo. Aidha, Serikali
itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma zinazolenga kuchochea uanzishaji na
uimarishaji wa viwanda vidogo na biashara ndogo. Huduma hizi zitatolewa katika
nyanja za ufundi, mafunzo, ushauri, masoko, habari na mitaji.
Mheshimiwa Spika,
90.
Mikakati mbalimbali italenga kutoa huduma kwa
wajasiriamali wadogo hususan wanawake na vijana kwa lengo la kuongeza nafasi za
ajira na kipato. Msukumo wa huduma za ufundi katika mwaka 2006/07 utalenga
kujenga uwezo wa wajasiriamali kuzalisha kwa tija kwa kutafuta na kusambaza
teknolojia zilizotengenezwa na kujaribiwa na taasisi mbalimbali za hapa nchini.
Aidha, SIDO itawawezesha wajasiriamali kuanzisha miradi ya usindikaji wa
vyakula na kutoa huduma za ushauri wa kiufundi kwa wajasiriamali. Kwa
kushirikiana na Serikali za Mitaa, SIDO itatafuta maeneo na kuratibu ujenzi wa
miundombinu na majengo kwa matumizi ya wajasiriamali wadogo.
Mheshimiwa Spika,
91.
Wizara
itahamasisha zaidi huduma zitakazoweka msisitizo katika kusaidia maendeleo ya
shughuli za uzalishaji na biashara vijijini hasa kujenga na kuimarisha uwezo wa
wahunzi na makundi mengine. Aidha, huduma za kiatamizi zitaendelea kutolewa
pamoja na huduma kwa wachimbaji wadogo wa madini katika maeneo mbalimbali ya
nchi. Uzalishaji wa bidhaa za ngozi utahamasishwa kwa kutoa mafunzo na huduma
kwa wazalishaji. Wizara yangu kupitia SIDO itaendesha kozi za ujasiriamali na
uongozi wa biashara na kutoa mafunzo kwa wasindikaji wa vyakula na matunda.
Pia, Shirika litatumia mbinu ya kuwaendeleza wazalishaji wadogo kwa kuwatumia
wazalishaji na wafanyabiashara waliofanikiwa (mentorship program).
Mheshimiwa Spika,
92.
Wizara yangu itaendelea kuilea mifuko ya mitaji iliyopo
na kuhakikisha kuwa mitaji inatolewa na kutumika kwa ufanisi. Aidha, Shirika
litaendelea kutoa mitaji kwa wajasiriamali wadogo na kutafuta vyanzo mbalimbali
vya fedha kwa ajili ya mitaji ya wajasiriamali.
Wizara itaendelea na juhudi zake za kuwawezesha wajasiriamali kushiriki
katika masoko ya ndani na nje ya nchi na pia litaandaliwa kongamano la Kitaifa
litakalowakutanisha wadau mbali mbali wa sekta kwa madhumuni ya kuzungumzia
maendeleo ya sekta ya viwanda vidogo na biashara ndogo, hii ikiwa ni pamoja na
fursa zilizopo nchini.
Mheshimiwa Spika,
93.
Katika kipindi cha mwaka 2006/07, taasisi za utafiti
yaani CAMARTEC, TEMDO na TIRDO, zinalenga katika kubuni teknolojia
zitakazokwamua matatizo yanayokabili sekta ya kilimo na viwanda hususan,
viwanda vidogo na vya kati ambavyo havina uwezo wa kufanya utafiti vyenyewe.
Hii ni pamoja na kuongeza uwezo wa taasisi hizi kwa kufundisha wataalamu wake.
Lengo ni kuboresha na kuinua maendeleo ya sekta hizi muhimu. Vile vile, taasisi hizi zinalenga katika
kutangaza teknolojia wanazobuni na kuzitengeneza ili ziweze kufahamika na wengi
na kupata wajasiriamali watakaozitengeneza kwa wingi na kuzisambaza kwa
wananchi, kwa matumizi katika shughuli zao hususan, kilimo vijijini na
kuanzisha viwanda vidogo huko vijijini vya kusindika mazao yanayozalishwa.
Aidha, eneo lingine jipya litakaloshughulikiwa katika utafiti wa mashirika haya
ni teknolojia ya mawasiliano.
Mheshimiwa Spika,
94.
Serikali itaendelea kuzitengea Taasisi hizi fedha za
bajeti kupitia MKUKUTA na kutafuta wafadhili kwa lengo la kuziwezesha kuendelea
na shughuli zao. Vile vile, taasisi
zenyewe zitaongeza nguvu katika kutangaza teknolojia walizobuni na kutengeneza
ili kupata soko na kujipatia fedha. Aidha,
zitazingatia kubuni teknolojia kulingana na soko (demand driven) badala ya
kuzitengeneza ndipo watafute soko.
E.6: Usimamiaji wa Sheria za Udhibiti
Ubora
Mheshimiwa Spika,
95.
Katika mwaka 2006/07, TBS
inalenga kukamilisha ununuzi wa vifaa muhimu vya Kituo cha Ufungashaji kwa
lengo la kuongeza ubora wa ufungashaji wa bidhaa zinazozalishwa hapa nchini na
kuhakiki vifungashio kwa bidhaa zinazotoka nje ya nchi. Pia, Shirika linatarajia kuanza utekelezaji
wa kiwango cha mita za teksi na kukamilisha ujenzi wa maabara ya kemikali. Pia,
Shirika litaendelea na hatua za kuthibitisha maabara za shirika na mifumo ya
utendaji wa Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO certification) pamoja na
kuhakikisha kuwa maabara zake zinaboreshwa ili kuweza kutoa huduma nzuri zaidi
kwa wananchi.
Ushindani wa Haki
Mheshimiwa Spika,
96.
Tume ya Ushindani, baada ya
zoezi la uteuzi wa wataalamu, katika kipindi cha mwaka 2006/07, itaendelea
kutoa mafunzo kwa wataalam wake, kuelimisha umma na utekelezaji wa Sheria ya
Ushindani ya mwaka 2003.
Vipimo
Mheshimiwa
Spika,
97.
Katika
mwaka 2006/07, Wakala wa Vipimo unategemea kutekeleza majukumu yake yakiwemo: -
a)
Kuhakiki vipimo
vinavyotumika kwenye biashara;
b)
Kutangaza majukumu ya Wakala ili wadau waweze kuelewa
huduma zinazotolewa;
c)
Kushirikiana na taasisi nyingine hususan Wizara ya
Kilimo, Chakula na Maendeleo ya Ushirika na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa ili kuhakikisha wauzaji wa mazao ya kilimo wanatumia
vipimo sahihi; na
d)
Kuhakikisha mianya yote ya wizi na udanganyifu wa kutumia
vipimo visivyokuwa sahihi na rasmi katika biashara vinakomeshwa.
Usajili
Mheshimiwa
Spika,
98.
Katika mwaka 2006/07, BRELA itatekeleza yafuatayo:-
a)
Kuanza kutekeleza mpango wa awamu ya tatu wa mwaka
2006/07-2008/09. Katika kutekeleza
mpango huu mambo ambayo yatazingatiwa ni kuboresha na kusimamia sheria,
kuelimisha na kuhamasisha wadau wake kwa kutangaza huduma zake kupitia redio na
luninga, kujenga uwezo wa ndani, kujenga na kutumia mbinu za kisasa za
utekelezaji na kupanua wigo ili kupeleka huduma karibu na wananchi;
b)
Kuboresha na kuzingatia mkataba wa huduma kwa wateja;
c)
Kupunguza kero za wadau kwa kuanzisha mtandao wa
kuratibu matatizo yanayojitokeza wakati wa kuwahudumia; na
d)
Kuendelea
kujijengea uwezo wa utendaji kazi na ufanisi wa utekelezaji kwa msaada wa
MKUMBITA.
E.7: Uendeshaji wa
Wizara na Taasisi Zilizo Chini Yake
Mheshimiwa
Spika,
99.
Wizara
yangu inaweka mkazo katika kuzingatia misingi ya utawala bora na uwajibikaji. Wizara imeunda Kamati
ya Uadilifu kufuatilia ukiukwaji wa maadili sehemu za kazi. Aidha, Kamati ya
Ukaguzi wa matumizi na mapato ya Serikali imeundwa ili kuhakikisha matumizi bora ya fedha za
umma.
Vita Dhidi ya Rushwa
Mheshimiwa
Spika,
100.
Katika
juhudi za kupambana na rushwa, Wizara yangu imeendesha warsha nne za utawala
bora na huduma kwa mteja kwa watumishi wake na watumishi wa wakala wa vipimo. Aidha, juhudi hizo
zitaendelezwa katika mwaka wa fedha wa 2006/07 ikiwa ni mwendelezo wa
utekelezaji wa Mkakati wa Wizara wa Vita dhidi ya Rushwa.
Mapambano Dhidi ya UKIMWI
Mheshimiwa
Spika,
101.
Wizara
yangu iliendelea kutekeleza mpango mkakati wa kudhibiti UKIMWI sehemu za kazi,
ikiwa ni pamoja na kuandaa vipeperushi na kuendesha semina sita juu ya mbinu za
kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu kwa watumishi wa Wizara na Taasisi zake.
Vile vile,
katika mwaka 2006/07, Wizara yangu kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya
Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) itaendeleza juhudi hizo kwa lengo la kupambana na
kupunguza athari zitokanazo na ugonjwa huu hatari. Wizara itapitia na kuboresha
Mkakati wake wa kupambana na UKIMWI, ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya
hali halisi ya maambukizi kwa watumishi wake.
Masuala ya Jinsia
Mheshimiwa
Spika,
102.
Katika
mwaka wa fedha 2005/06, Wizara yangu ilianzisha Dawati la Jinsia na Kuunda
Kamati ya Jinsia ya Wizara pamoja na kuandaa mkakati wa kushughulikia masuala
ya jinsia ambayo yanapaswa kuingizwa kwenye Sera, mipango, programu na katika
utendaji wa kila siku. Aidha, Kamati za Jinsia zilianzishwa kwenye Mashirika,
Taasisi na Wakala chini ya Wizara yangu, ili ziweze kuzingatia uingizaji wa
masuala ya jinsia katika mafunzo na uzalishaji. Katika mwaka 2006/07, Wizara
yangu imepanga kuendesha semina za uhamasishaji kuhusu masuala ya jinsia ili
wafanyakazi waweze kuwa na uelewa wa jinsi ya kuyahusisha katika kazi zao za
kila siku.
Mheshimiwa
Spika,
103.
Katika
kutekeleza azma ya Serikali ya kuwa na utendaji kazi bora katika Utumishi wa
Umma, Wizara yangu imeajiri jumla ya watumishi 20 kwa mwaka 2005/06. Aidha,
Wizara imewapatia watumishi 35 mafunzo ya muda mfupi na mrefu ndani na nje ya
nchi kwa nia ya kuinua viwango vyao vya utendaji kazi.
F: MAKADIRIO
YA BAJETI YA 2006/2007
Shukrani
Mheshimiwa
Spika,
104.
Napenda
kutumia nafasi hii kuzishukuru Nchi rafiki na Mashirika ya Kimataifa ambayo
yamekuwa yakitoa misaada iliyoiongezea Wizara uwezo wa kutekeleza majukumu yake
kwa ufanisi na tija zaidi. Napenda
kuzishukuru nchi za Austria, Canada, China, Denmark, Finland, Ireland, Uswis,
India, Japan, Marekani, Sweden, Uholanzi, Uingereza, Ujerumani na nchi nyingine
ambazo zimeendelea kuisaidia Wizara.
Aidha, napenda kuyashukuru Mashirika ya Sida, UNIDO, DANIDA, DFID, GTZ,
ILO, IFAD, NORAD, WTO, UNCTAD, OECD, USAID, UNDP, OPEC Fund, JICA, WIPO, ARIPO,
SECO na ITC. Nazishukuru pia Taasisi za
Kimataifa za Benki ya Dunia, Shirika la
‘‘Common Fund for Commodities – CFC’’ na African Development Bank (ADB)
kwa misaada na michango
Mheshimiwa
Spika,
105.
Hoja hii ni
matokeo ya kazi nzuri na ushirikiano wa karibu nilioupata kutoka kwa wenzangu
katika Wizara, Mashirika, Wakala, Asasi, Taasisi na Makampuni yaliyo chini ya
Wizara. Naomba kutoa shukrani zangu za
dhati kwa Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko Mhe. Dkt. David Mathayo
David, Mbunge wa Same Magharibi, Bw. Wilfred L. Nyachia, Katibu Mkuu, Bw.
Godfrey Mkocha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu na watumishi wote wa Wizara,
Mashirika, Wakala, Asasi, Taasisi na Makampuni yaliyo chini ya Wizara kwa
michango yao katika kufanikisha kazi za Wizara na kwa kuhusika na maandalizi ya
Bajeti ninayoiwasilisha leo. Nazishukuru
pia Jumuiya na Taasisi za Sekta Binafsi, ikiwemo CTI, TCCIA na TPSF. Aidha, nazishukuru taasisi za elimu ya juu na
utafiti, hasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, Chuo
Kikuu Mzumbe na ESRF kwa michango yao ya mawazo wakati wa mikutano, warsha,
semina na makongamano mbalimbali kuhusu Sekta za Viwanda, Biashara na
Masoko. Ushirikiano huu ni muhimu katika
kuendeleza na kuimarisha Sekta za Viwanda, Biashara na Masoko kwa maendeleo ya
Taifa letu. Natoa pia shukrani za dhati
kwa Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kwa huduma muhimu ya kuchapa hotuba hii.
MAOMBI YA
FEDHA
Mahitaji
ya Fedha kwa Matumizi ya Maendeleo
Mheshimiwa
Spika,
106.
Katika mwaka wa 2006/2007, Wizara inaomba Shilingi 3,002,000,000.00 kwa ajili ya
shughuli za miradi ya maendeleo ya Viwanda, Biashara na Masoko. Kati ya fedha hizi, Shilingi 326,000,000.00 ni fedha za ndani ambazo zitatumika katika
shughuli za maendeleo ya Taasisi zilizo chini ya Wizara na Shilingi 2,676,000,000.00 ni fedha za nje kutoka kwa wahisani
ambazo zitatumika kulipia tafiti za kitaalamu na vifaa kwa miradi mbalimbali
itakayotekelezwa na Wizara.
Maombi ya
Fedha kwa Matumizi ya Kawaida
Mheshimiwa
Spika,
107.
Mheshimiwa
Spika,
108.
Pamoja na
hotuba hii, nimeambatisha majedwali na vielelezo mbalimbali ambavyo kwa pamoja
vinatoa takwimu zitakazowezesha Waheshimiwa Wabunge kutafakari vizuri zaidi
maendeleo na utendaji katika sekta za Viwanda, Biashara na Masoko. Ninaomba takwimu hizi zichukuliwe
G. KUTOA HOJA
109.
Mheshimiwa Spika, Naomba kutoa hoja.