|
Matokeo
ya Uchaguzi ya Kuingia Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi
Muundo
wa mfumo rasmi wa Elimu na Mafunzo nchini Tanzania unajumuisha
miaka miwili ya mwanzo ya (elimu ya chekechea) kumtayarisha mtoto
kabla ya kuanza darasa la kwanza, ikifuatiwa na miaka 7 ya elimu
ya msingi, miaka 4 ya elimu ya awali ya Sekondari (ordinary
level), miaka 2 ya mwisho ya Sekondari (high level) na kumalizikia
na miaka 3 au zaidi vyuo vikuu (tertiary levels).
Wizara
ya Elimu na Utamaduni na Wizara ya Sayansi, teknolojia na Elimu ya
Juu ndizo zinazosimamia na kuratibu shughuli zote za sekta ya
Elimu hapa nchini. Kadhalika,
Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa nayo pia inasimamia
Elimu ya Msingi.
Idadi
ya vyuo na vyuo vikuu hapa nchini ilifikia 28 mwaka 2000.
Kati ya vyuo hivyo, 9 vinatambuliwa kama vyuo vikuu vya
Serikali na vya binafsi, 7 kama vyuo vikuu vishiriki na 12 vyuo
vya kawaida vya mafunzo. Idadi ya shule za msingi na Sekondari za Serikali na za
binafsi inaweza kupatikana katika mtandao wa kompyuta kwa kutumia
anuani: www.tzonline.org
·
Lugha
ya kufundishia
Kiswahili
na Kingereza ndizo lugha kuu mbili za masomo nchini Tanzania.
Kingereza ni muhimu kwa vile kinasaidia kuiunganisha
Tanzania na nchi nyingine za dunia katika masuala ya teknologia,
biashara na utawala. Kiswahili
nacho kinawasaidia wanafunzi katika kuendeleza mila na utamaduni
wao wa Kitanzania. Kingereza
kinatumika kama somo mojawapo la lazima katika elimu ya msingi
wakati ambapo katika ngazi za elimu zinazofuata (post-primary
education) kinatumika kama lugha mahsusi ya kufundishia.
Kiswahili nacho kinatumika kama lugha mahsusi ya
kufundishia katika elimu ya msingi na kutumika kama somo mojawapo
la lazima katika elimu ya Sekondari.
Katika vyuo siyo somo la lazima.
·
Washika
Dau/Taasisi za Elimu
-
Taasisi ya Elimu Tanzania:
Ilianzishwa mwaka 1964 kama sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam (Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki).
Mwaka 1975 iligeuzwa rasmi kuwa taasisi ya kujitegemea
chini ya Sheria ya Bunge Na. 13 ya 1975, na kuitwa Taasisi ya
Elimu Tanzania. Mawasiliano yote yanafanywa kwa kupitia kwa
Mkurugenzi, Taasisi ya Elimu Tanzania, S.L.P. 35094, Dar es
Salaam, TANZANIA. Simu:
255-22-73005/74420. Fax:
255-22-74420. Waraka umeme: educate@intafrica.com
- Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima: Ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 12 ya 1975.
Kazi yake kubwa ni kufanya utafiti, kushauri na
kushughulikia maendeleo ya elimu ya watu wazima nchini, ikiwa
ni pamoja na kuendesha kampeni za
kushawishi wananchi wajiunge na mpango wa elimu ya watu
wazima. Anuani: S.L.P. 20679, Dar es Salaam, TANZANIA.
-
Baraza la Mitihani Tanzania:
Hili ni Baraza lililoanzishwa chini ya Sheria ya Bunge Na.
23 ya 1973. Kazi yake
mahsusi ni kusimamia na kuratibu shughuli zote za mitihani hapa
nchini. Pia linatoa
stashahada rasmi za elimu ya msingi, sekondari na elimu ya juu
isipokuwa ya Chuo Kikuu. Anuani:
S.L.P. 2624, Dar es Salaam, TANZANIA.
Simu: 255-22-700493/4.
-
Baraza la Sanaa la Taifa:
Lilianzishwa chini ya Sheria ya Bunge Na. 23 ya 1984.
Kazi yake maalum ni kuhimiza maendeleo ya sanaa, msukumo
mkubwa ukiwa kwenye muziki, sanaa za maigizo na kazi za sanaa.
Shughuli za sanaa zinafanywa na watu wasiopungua milioni 4
nchi nzima, waliojitayarisha katika makundi, vyama, Kampuni na
watu binafsi. Anuani:
Kituo cha Sanaa Ilala, S.L.P. 4779, Dar es Salaam,
TANZaNIA. SIMU:
255-22-2863749.
-
Baraza la Kiswahili Tanzania:
Baraza hili limepewa jukumu la kutekeleza sera ya Kukuza
lugha ya Kiswahili hapa nchini.
Vilevile imetayarisha mipango ya utekelezaji wa Sera ya
Utamaduni ya 1997. Anuani:
Coronation Building, Mtaa wa Azikiwe/Samora, S.L.P. 4766,
Dar es Salaam, TANZANIA, Simu: 255-22-23452/24139.
-
Tume ya Sayansi na teknologia (COSTECH).
Anuani: SOSTECH,
S.L.P. 4302, Dar es Salaam. TANZNAIA.
Simu: 255-22-2227515.
Waraka Umeme: costech@costech.opc.org
-
Baraza la Usajili wa Elimu ya Juu (HEAC).
Anuani: HEAC,
S.L.P. 6562, Dar es Salaam, TANZANIA.
Simu: 255-22-2137585.
-
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).
Anuani: NACTE,
S.L.P. 7109, Dar es Salaam, TANZANIA.
Simu: 255-22-2137585.
|