.

Jamhuri ya Muungano wa Tazania ilianzishwa kutokana na muungano wa nchi huru mbili, Tanganyika na Zanzibar. 

·                    Tanganyika ilipata uhuru wake tarehe 9 Desemba 1961 na kuwa Jamhuri mwaka uliofuata (1962). 

·                    Zanzibar ilipata uhuru tarehe 10 Desemba, 1963 na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ilianzishwa baada ya mapinduzi ya tarehe 12 Januari 1964. 

Nchi mbili hizi ziliunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 26 Aprili, 1964.  

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inashughulikia masuala yasiyohusu muungano.

Habari za Kiserikali