|
Dira ya
ofisi ya Makamu wa Rais ni kufikia kiwango cha juu cha
maendeleo endelevu kwa binaadamu, kuondoa umasikini, matumizi
mazuri ya rasilimali kwa ajili ya kujipatia riziki kwa sasa na
vizazi vijavyo bila kuharibu mazingira au kuhatarisha afya au
usalama; na kuendeleza umoja kati ya Serikali za Jamhuri ya
Mwungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. |
Jukumu la
Ofisi ya Makamu wa Rais ni kuandaa sera na mikakati ya
kuondoa umasikini, kulinda mazingira na mashirika yasiyo ya
kiserikali pamoja na kuratibu mambo yote yanayohusu umoja
baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania na Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar. |