|
Benki Kuu ya Tanzania imeanza
shughuli zake tarehe 14 Juni, 1966 chini ya sheria ya Benki Kuu ya mwaka 1965.
Sheria hii inatoa ruhusa kwa Benki Kuu kufanya kazi zote kuu zinazopaswa
kufanywa na Benki
Sheria ya Benki Kuu ta Tanzania ya mwaka 1965,
inachukuwa nafasi ya sheria ya awali na madhumuni makubwa ya sheria hii ni
kuanzisha mazingira za fedha yanayofaa kwa kuweka msimamo wa bei usioyumba.
Madhumuni ni kuanzisha na kutekeleza sera ya fedha
itakayoweza kulinda mfumko wa bei na kukuza uchumi wa Tanzania
Website:www.bot-tz.org
Shirika za Bima la Taifa
Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB)
Benki ya Posta Tanzania (TPB)
National Micro-finance Bank (NMB)
Bahati Nasibu ya Taifa
Duka la Kubadilishia Fedha za Kigeni la Taifa
Baraza la Taifa la Wahasibu na Wakaguzi wa
Mahesabu (NBAA)
Shirika la Ukaguzi wa Mahesabu la Tanzania (TAC)
Shirika la Akiba ya Wafanyakazi (PPF)
Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM)
Chuo cha Uhasibu cha Arusha
Chuo cha Uhasibu cha Dar es Salaam (DSA)
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Katika mwaka wa fedha wa 1996/97,
Serikali ilianzisha sera ya hazina ili kuongeza ukusanyaji wa mapato na
kuboresha matumizi kwa kudhibiti matumizi kwa lengo la kupunguza nakisi katika
matumizi ya serikali. Kwa upande wa mapato juhudi zilizochukuliwa ni pamoja na
kuimarisha utawala kwa kuanzisha Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania
Sheria ya Mamlaka ya Mapato ya mwaka 1995
ilianzisha mamlaka hii kama wakala wa serikali, chini ya usimamizi wa Wizara
ya Fedha.
Kazi za Mamlaka
Kazi kuu za Mamlaka ya Kodi ya Mapato
ni
-
Kukadiria, kukusanya na
kuhesabu matapo yote ya serikali
-
Kusimamia utekelezaji wa
Sheria zote za Mapato za Serikali Kuu
-
Kuishauri Serikali juu ya
mambo yanayohusu sera ya fedha
-
Kukuza ari ya wananchi ya
kulipa kodi
-
Kuinua ubora wa huduma kwa
walipa kodi
-
Kupambana na udanganyifu na
njia nyingine za kukwepa kodi
-
Kutoa takwimu za biashara na
matangazo mengine
Muundo wa Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
Bodi ya Wakurugenzi
Bodi ya Wakurugenzi ndiyo kiongozi Mkuu wa
Mamlaka na jukumu lake ni kuandaa na kutekeleza sera kwa ajili ya Mamlaka,
Bido ina wajume sita ambao ni:-
Mwenyekiti ambaye anateuliwa na Rais wa Jamhuri
ya Mwungano wa Tanzania baada ya
-
kupata mapendekezo kutoka
Wizara ya Fedha
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha
ya Serikali ya Muungano
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha
ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
-
Gavana wa Benki Kuu ya
Tanzania
-
Kamishna Mkuu wa Mamlaka
ya Mapato Tanzania
Katibu wa Tume ya Mipango
Na wajumbe wengine wanne wanaoteuliwa na Waziri
wa Fedha, ambao wana ujuzi na uzoefu katika mambo ya fedha, biashara, uchumi
au sheria kutoka Taasisi za fedha, biashara, sheria au uchumi zenye maslahi
katika Mamlaka.
Kamishna Mkuu
Kamishna Mkuu ni mtendaji mkuu katika Mamlaka.
Chini ya usimamizi na udhibiti wa Bodi, Kamishna anawajibika na kazi za kila
siku za Mamlaka, kusimamia fedha, mali na shughuli za Mamlaka na kuendesha,
kupanga na kudhibiti maafisa wengine na wafanyakazi wa Mamlaka.
Idara za Mapato
Mamlaka inaundwa na idara tatu za Mapato
zinazoshughulikia ukusanyaji wa mapato kwa kusimamia sheria za kodi
zinazohusika. Idara hizi ni:
Makamishna wa mapato ambao wanateuliwa na Bodi
wanaongoza Idara hizi. Manaibu Kamishna wa Dar es Salaam na mikoa mingine
wanamsaidia Kamishna wa Mapato. Maafisa Mapato wa Mikoa wanafanya kazi chini
ya Manaibu kamishna wa mikoa yao.
Idara Saidizi
Mamlaka ina idara saidizi saba kama zifuatavyo:
-
Ukaguzi wa Kodi na
Uchunguzi
-
Fedha na Nguvu kazi
-
Habari
-
Utafiti na Sera
-
Uenezi na Elimu kwa Walipa
Kodi
-
Ukaguzi wa Ndani wa
Mahesabu
-
Mambo ya Sheria

Kodi zinazokusanywa na Mamlaka
Kodi za Biashara za Kimataifa
Idara ya Ushuru wa Forodha inasimamia kodi zote
za biashara za kimataifa. Kodi hizi ni pamoja na kodi ya kuingiza bidhaa
nchini, ushuru wa forodha na Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa bidhaa
zinazoingizwa nchini kutoka nje ya nchi.
Kodi ya Kuingiza Bidhaa kutoka nje ya nchi.
Kodi hii inatozwa bidhaa zinazoingizwa kutoka
nje ya nchi. Kodi hii kwa kawaida inahesabiwa kama kodi ya ongezeko la thamani
ya mabadilishano katika biashara kwa kuzingatia gharama ya mali iliyoingizwa
pamoja na usafiri. Kodi hii inakusanywa kabla mali haijaondolewa sehemu
iliyoingilia iwe ni bandari, uwanja wa ndege au mpakani kwenda nchi
inayohusika au kwenye ghala au bohari inayohusika.
Kuna viwango vitano vya kodi hii
vinavyotumika:
-
0% ( au kusamehewa
kabisa) inayotumika kwa bidhaa kama mbolea,
kemikali na madawa ya mimea na wanyama
-
5% (asilimia tano) inayotumika
kwa pembejeo za kilimo
-
10% (asilimia kumi)
inayotozwa kwa kuingiza mali ghafi na mali za
mtaji
-
20% (asilimia ishirini) kwa
kuingiza bidhaa za kati ambazo zitauzwa tena
-
30% (asilimia thelathini) kwa
kuingiza nchini bidhaa zilizokwisha tengenezwa kwa matumizi makubwa na ya
muda mrefu.
Utaratibu wa Kusawazisha Ushuru unatumia kupanga
bidhaa kwa madhumuni ya kutoza kodi pamoja na kukusanya Takwimu za Biashara.
Kuhimiza biashara baina ya nchi za Umoja wa Kibiashara wa nchi za Kusini mwa
bara la Afrika, (COMESA) bidhaa zinazoingizwa kutoka nchi wanachama wa Umoja
huo zinatozwa ushuru wa chini ikilinganishwa na bidhaa kutoka nchi nyingine
ambazo si wanachama
Ushuru kwa Bidhaa zinazoingizwa kutoka Nje
Ushuru unatozwa kwa baadhi ya bidhaa
zinapoingizwa nchini. Kwa kawaida bidhaa zinazotozwa ushuru huu ni zile
ambazo zinaonekana kama hazina maadili mazuri kwa jamii kama vile sigara,
pombe na bidhaa ambazo matumizi yake yanaonekana kama ni ya anasa kama vile
mafuta ya petroli. Katika Tanzania, zaidi ya kutoza ushuru huu kwa bidhaa
kama vinywaji na magari, pia zinatozwa ushuru kwa kuongeza mapato.
Ushuru wa forodha unatozwa kwa bidhaa maalum au
kufuata na thamani ya bidhaa, na kima cha kodi ambayo inafuatana na thamani ya
bidhaa in Thamani ya bidhaa pamoja na Usafiri na kodi ya kuingia nchini.
Viwango vya kodi inayotokana na thamani ya bidhaa ni kama vifuatavyo:
Zifuatazo ni viwango maalumu na bidhaa
zinazopaswa kutozwa ushuru kwa kiwango maalum
-
Sigara
-
Divai na pombe kali
-
Bia
-
Vinywaji baridi
-
Mazao ya Petroli
-
Saruji

Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa Bidhaa
zinazoingizwa kutoka Nje
Kodi hii inatozwa kwa bidhaa zinazoingwa
Tanzania Bara kwa kiwango kimoja tu cha asilimia ishirini (20%). Thamani
inayotozwa kodi hii ni thamani ya bidhaa pamoja na usafiri pamoja na ushuru wa
forodha na kodi nyingine zinazotwa bidhaa zinazoingizwa nchini.
Wafuatao wamesamehewa kulipa kodi ya ongezeko la
thamani wanapoingiza bidhaa nchini
-
Mabalozi na maafisa wa Ubalozi
-
Bidhaa zinazoingizwa nchini
chini ya Mikataba ya Misaada ya Kiufundi
-
Mizigo ya Wasafiri
-
Serikali au Taasisi zake,
endapo bidhaa zinazoingizwa zitatumika kukisaidia chombo kinachohusika
kutelekeza majukumu yake.
-
Rais wa Jamhuri ya
Mwuungano wa Tanzania
Uingizaji wa bidhaa zifuatazo umesamehewa
kodi ya Ongezeko la Thamani
Bidhaa zote za kibishara zinazosafirishwa kuja
nchini zenye thamani ya zaidi ya dola za Kimarekani elfu tano (US $ 5,000/=)
ni lazima zikaguliwe. Kampuni iliyopewa kazi hii ni “Societe Generale de
Surveillance” ya Afrika ya Kusini (SGS) Kampuni hii inapaswa kuhakikisha ubora,
wingi, thamani na kiwango cha daraja la kodi vipo sawa kama vilivyoonyeshwa na
msafirishaji.
Bidhaa chache zilizochaguliwa, ambazo ni maarufu
kwa kukweka kodi, ni lazima zikaguliwe bila kujali ni nani anayezisafirisha.
Dhahabu, vito vya thamani na madini, kazi za
sanaa, baruti, mabomu na silaa za kivita, wanyama na bidhaa zinazooza,
magazeti mapya na majarida, vifaa vya majumbani na vifaa vya wasafiri
vimesamehewa ukaguzi. Bidhaa nyingine zilizosamehewa kukaguliwa ni zile
zinazoingiwa na mabalozi au wafanyakazi wa ofisi zao, mashirika ya dini,
mashirika ya misaada au magari mapya yanayoingizwa na wawakilishi wa
makampuni yanayotengeneza magari.

Kodi ya Matumizi:
Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa Bidhaa za hapahapa nchini
Kodi ya Ongezeko la Thamani ni kodi inayotozwa
katika bidhaa na huduma mbalimbali Kodi hii inatozwa kwa kila thamani
inayoongezwa kwa bidhaa au huduma na wazalishaji na wafanya biashara katika
kila hatua ya uzalishaji au usambazaji. Wafanyabishara wanasajiliwa kama
mawakala wa kukusanya kodi hii kwa niaba ya serikali. Kodi hii ilianzishwa
Tanzania tarehe 1 Julai mwaka 1998 na inachukuwa nafasi ya kodi za mauzo ya
bidhaa na huduma, stakabadhi na stemp ya ushuru, kodi ya hoteli, na kodi ya
viburudisho walizokuwa wanatozw3a wafanya biashara waliosajiliwa kulipa kodi
ya ongezeko la thamani.
Kodi ya Ongezeko la Thamani inatozwa kwa kiwango
kimoja tu cha asilimia ishirini (20%). Thamani inayotozwa kodi kwa bidhaa na
huduma za hapa hapa nchini ni kiasi cha fedha ambacho mteja amelipa kununua
bidhaa au huduma, au thamani ya soko huru ya bidhaa au huduma.
Hakuna kodi ya Ongezeko la Thamani kwa bidhaa
zinazouzwa nje ya nchi. Lakini Wafanya Biashara waliosajiliwa kulipa kodi hii
ambao wanasambaza bidhaa na huduma kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi
wanaweza kudai kurejeshewa kodi hii katika bidhaa wanazoingiza kutoka nje.
Utaratibu huu unawasaidia wafanyabiashara hawa kuingia katika soko la
Kimataifa na kuwafanya waweze kuhimili ushindani.
Shughuli za ugavi wa bidhaa
na huduma nyingi muhimu ambazo zinatumiwa kwa wingi na wananchi wenye kipato
cha chini hazitozwi kodi ya Ongezeko la Thamani. Na Endapo mfanyabiashara
atasamehewa kulipa kodi ya Ongezeko la Thamani, haruhusiwi kuwatoza kodi hiyo
wateja. Aidha hawana haki ya kudai kurejeshewa kodi hiyo wakati wanapolipa
kodi kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa au huduma.
Ugavi wa baadhi ya bidhaa
na huduma zimepewa msamaha maalum wa kodi ya ongezeko la thamani. Hizi ni
bidhaa au huduma zinazotolewa kwa Serikali au Taasisi zake kwa ajili ya
matumizi ya kuiwezesha serikali au Taasisi hizo kutekeleza majukumu yao ya
kikatiba. Bidhaa au huduma ambazo zimesamehewa kulipa kodi, zinatozwa kodi,
lakini kodi hiyo baadaye inarudishwa kwa muhusika. Wafanyabiashara
wanaosambaza bidhaa na kuduma kwa serikali na taasisi zake zinaruhusiwa kupata
muamana wa kodi wanaponunua bidhaa au huduma.

Ushuru wa Forodha kwa Bidhaa
Zinazotengenezwa Nchini
Ushuru wa forodha pia
unatozwa kwa bidhaa zinazozalishwa hapa nchini. Kwa kawaida ushuru huu
unatozwa kwa sigara na bia na bidhaa nyingine ambazo matumizi yake yanaonekana
kama ni ukiukaji wa maadili mema ya jamii. Ushuru huu pia unatozwa kwa
vinywaji baridi kwa ajili ya kuongeza mapato. Aidha katika utozaji wa ushuru
wa forodha kuna viwango maalum au kwa kufuata thamani ya bidhaa inayohusika.
Kiwango cha chini cha Kodi hii ni asilimia kumi na kiwango cha juu ni asilimia
thelathini.
Ushuru wa Stempu
Ushuru wa Stempu unatozwa
kwa kiwango cha asilimia mbili ya mapato ya wafanyabiashara wenye mikataba na
mamlaka ya Mapato Tanzania. Kwa wafanyabiashara ambao wanatumia mihuri
inayopigwa juu ya stakabadhi zao za malipo, wanalipa asilimia 3.6% ya mauzo.
Ushuru huu unalipwa na wafanyabiashara ambao hawakujisajili kulipa kodi ya
ongezeko la thamani.
Kodi ya Magari.
Licha ya kodi za kuingiza
magari nchini, magari yanatozwa kodi mbalimbali ambazo zinakusanywa na Idara
ya Kodi ya Ongezeko la Thamani kama zifuatazo:
Kodi ya Kusajili Gari
Kodi hii inakusanywa wakati
gari linaposajiliwa kwa mara ya kwanza nchini. Kodi ni inatozwa kwa kiwango
kimoja tu cha Sh. 95,000/= kwa kila gari inayosajiliwa na Sh. 32,000/ kwa
kusajili pikipiki.
Kodi ya Faida itokanayo
na Gari
Makampuni yote binafsi ya
biashara ambayo hayajihusishi ya biashara ya usafirishaji wanalazimika kulipa
sh. 100,000 kwa kila gari inayomiliki.
Malipo ya Kibali cha
Magari ya Kigeni na yanayoingizwa nchini kwenda nchi jirani.
Magari yote ya kigeni
yanayoingizwa nchini kwa muda yakiwa njiani kwenda nchi nyingine yanalipa ada
ya dola za Kimarekani ishirini kwa kila siku thelathini yanapokuwa hapa nchini.
Magari ya kigeni ya kibiashara yenye matela (ekseli) matatu yanatozwa dola za
Kimarekani sita zaidi kwa kila kilometa mia moja yanayotembea hapa nchini.

Kodi ya Mapato, Faida
na Utajiri kwa Ujumla.
Kodi ya Mapato ya Kampuni
Makampuni yote
yaliyosajiliwa na/au kufanya biashara zao nchini, yanatozwa kodi kutokana na
faida wanayopata kwa kiwango cha asilimia thelathini . Kwa kawaida kodi hii
inalipwa katika ngazi mbili. Katika hatua ya kwanza mlipa kodi anakadiria
mwenyewe mwanzoni mwa mwaka wa biashara., na katika hatua ya mwisho kodi
inalipwa baada ya maafisa wa kodi kufanya tathmini ya mapato yote ya kampuni
katika mwaka unaohuiska.
Katika kufikia kiwango cha
mapato ya kutozwa kodi au faida, punguzo linaruhusiwa kwa matumizi yote
yaliyotumika katika mwaka unaokusudiwa kwa ujumla au kwa kiasi cha uzalishaji
wa mapato hayo.
Aidha punguzo la matumizi
na uchakavu linaruhusiwa kwa mashine zinazomilikiwa na kampuni inayohusika na
ambazo zinatumika katika biashara. Utaratibu wa kuzingatia uchakavu
unatumiaka na kufuata viwango vifuatavyo. Asilimia 37.5 kwa mashine za daraja
la kwanza ambazo ni pamoja na matrekta, mashine za kuvunia mazao ya kilimo,
mashine za kuchimbia ardhi na nyingine kama hizo. Asilimia ishirini na tano
kwa mashine za daraja la pili kama vile ndege na asilimia 12.5 kwa mashine
nyingine kama meli.
Punguzo la Uchakavu kwa
majengo ni asilimia nne kwa majengo ya viwanda na asilimia sita majengo ya
mahoteli. Aidha kuna bonasi ya asilimia ishirini ya punguzo la kuwekeza
linaloruhusiwa kwa matumizi ya majengo ya viwanda, mahoteli na mashine
zinazowekwa humo.
Katika sekta ya kilimo,
asilimia ishirini inaruhusiwa kwa ujenzi wa karakana zote za kilimo. Asilimia
100 inaruhusiwa kwa matumizi ya mtaji katika kilimo na upandaji wa mazao ya
kudumu na asilimia 100 inaruhusiwa kwa matumizi ya mtaji katika kuzuia
mmomonyoko wa udingo katika ardhi inayotumika kwa kilimo.
Kodi ya Mapati ya Mtu Binafsi
Kodi hii inatozwa kwa
wananchi kutokana na mapato yao kwa mwaka duniani kote na kwa Tanzania
inatozwa kutokana na mapato ya wakazi wasio raia wa nchi hii. Mapato
yananyotozwa kodi ni pamoja na mapato yote au faida kutoka katika biashara zao,
ajira au huduma wanazotoa, gawio au riba wanayopata kutoka benki zinazofanya
kazi hapa nchini. Kodi hii inatozwa kufuatana na kipato cha muhusika na kuna
mafungu kumi na mbili ya vipato kuanzia sh. 20,000. Kiwango cha chini cha kodi
ni asilimia 7.5 na kiwango cha juu ni asilimia thelathini na tano kwa vipato
vinavyozidi sh. 700,000. Mafungu ya viwango vya kodi hii yanapatikana katika
jedwali na. 1.
Kodi ya mapato kwa watu
binafsi nchini Tanzania inakusanywa kwa kutumia njia mbili. Kwa waajiriwa
wenye mishahara kodi hii inaitwa PAYEE na inakusanywa na waajiri kwa kutumia
viwango vilivyotajwa hapo juu wakati wa kutayarisha mishahara. Waajiri
wanawajibika kuwasilisha kodi hii kwa Kamishna wa Kodi za Mapato. Njia ya pili
inatumika kwa wafanya biashara na wananchi waliojiajiri wenyewe ambapo makisio
ya mapato yao ya mwaka yanatokana na mapato waliyoonyesha wakati wa kuomba
leseni za biashara. Na hawa wanatakiwa kulipa kodi hii kila baada ya miezi
mitatu.

Kodi ya Mishahara
Kodi hii inalipwa na
waajiri binafsi wenye wafanyakazi wanne au zaidi. Kwa sasa kodi hii inatozwa
kwa kiwango cha asilimia nne ya mishahara ya wafanyakazi. Kodi hii haikatwi
kutoka kwenye mishahara ya wafanyakazi.
Zuio la Kodi
Zuio ni mpango wa ulipaji
kodi unaosimamiwa na Idara ya Kodi ya Mapato ambapo kodi inayotozwa inabaki
katika sehemu inayokusanywa. Kodi zinazobakizwa zinapunguzwa wakati wa malipo
ya kodi binafsi au kodi binafsi za makampuni kwa walipa kodi wazawa, na kama
kodi hiyo ni malipo ya mwisho kwa walipa kozi wageni. Kama kuna riba, gawio
na mapato ya pango, kodi hii ni ya mwisho kwa wananchi wazawa na wageni.
Riba
Mtu yeyote anayepata riba
inayozidi sh. 150,000/= anawajibika kulipa kodi ya zuio kutokana na riba
anayopata. Na kiwango kinachotumika ni asili mia 15% kwa wote wazawa na wageni.
Taasisi za fedha ni mawakala wa kukusanya kodi hii.
Gawio
Gawio linalipwa kwa raia wa
nchi hii kutoka Kampuni iliyorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam
linapaswa kulipowa kodi ya gawio kwa kiwango cha asilimia tano (5%) na
asilimia kumi na tano (15%) kwa makampuni yasiyoorodheshwa. Pato la gawio
lilolipwa kwa mkazi mgeni linatozwa asilimia ishirini bila kujali kama kampuni
inayohusika imeorodheshwa au la. Kodi ya Gawio inapaswa kubaki katika kampuni
kama kodi ya mwisho. Katika Sekta ya madini magawio yanayotolewa kwa wakazi
wageni yanatozwa kodi kwa kiwango cha asilimia kumi (10%). Makampuni
yanayotangaza magawio ndiyo wakusanyaji wa kodi hii.
Pango.
Mapato yanayotokana na
kukodisha na kupangisha yanayozidi sh. 500,000/= kwa mwaka yanapaswa kulipiwa
kodi ya zuio, ambayo pia ni kodi ya mwisho ya mapato kwa aina hii ya mapato.
Kodi hii inatozwa kwa kiwango cha asilimia 15 kwa wazawa na asilimia 20 kwa
wageni.
Ada ya Usimamizi na Utaalam
Malipo yanayofanywa kwa
mkazi mgeni, zaidi ya malipo yanayofanywa kwa mwaajiriwa na mwajiri wake,
yanayochukuliwa kama huduma yoyote ya utawala, ufundi au utaalam yanapaswa
kulipiwa kodi ya salio ya asilimia ishirini (20%). Kwa sekta ya madini kodi
ya zuio ya asilimia tatu (3%) inatozwa kwa makandarasi wadogo na ada ya
usimamizi endapo ada ya usimamizi haizidi asilimia mbili ya gharama za
uendeshaji.
Bidhaa na Huduma
Malipo ya utoaji wa bidhaa
na huduma, ukiondoa kodi ya ongezeko la thamani, yanatozwa kodi ya zuio ya
asilimia mbili kwa kila malipo kwa malipo yote ambayo ni sawa au zaidi ya sh.
100,000/=. Wazunuzi wa bidhaa na huduma kama hizo wanapaswa kuwa mawakala wa
serikali wa kukusanya kodi ya zuio. Wanaomiliki hati za machimbo ya madini
wanasamehewa kulipa kodi za zuio kwa bidhaa au huduma za hapa hapa nchini
ingawa wanapaswa kubakisha kodi hiyo kwa wanaotoa huduma au bidhaa hizo.

Kodi nyingine za
zuio
Kodi nyingine za
zuio ni
-
Kodi ya Chanzo
cha Mapato
-
Ada ya hati
miliki (asilimia 20)
-
Malipo ya
Pensheni kwa wageni (asilimia 15)
-
Ushuru wa
barabara (kwa wazawa) (asilimia 4)
-
Ushuru wa
barabara (kwa wgeni) (asilimia 15)
-
Kodi ya
Usafirishaji wa meli (asilimia 2)
-
Ukodishaji wa
ndege (asilimia 10)
-
Asilimia ya
Faida inayotokana na biashara ya Bima (asilimia 7.5)
-
Kodi za matumizi
-
Kodi ya Huduma za Kuondokea Katika Viwanja vya
Ndege
Kodi
ya Huduma za Kuondokea za Uwanja wa Ndege inatozwa kwa wasafiri wote wa
ndege wazawa na wageni katika viwanja vya ndege nchini. Wasafiri wa ndani
wanalipa sh 2,000/= kwa kila safari na wasafiri wanaokwenda nje ya nchi
wanalipa dola za Kimarekani ishirini (US $ 20) kwa kila safari. Kodi hii
inajumushwa katika bei ya tiketi na mawakala wa mashirika ya usafiri
wanapaswa kuwa mawakala wa serikali katika kukusanya kodi hii. Abiria
wanaopita na watoto chini ya miaka miwili wamesamehewa kulipa kodi hii.
-
Kodi ya Huduma za Kuondokea Bandarini
Kodi hii inatozwa kwa abiria wanaosafiri
kwenda humu humu nchini na nchi za nje kwa kutumia meli za abiria. Wananchi
wazawa wanalipa sh 500/- na wageni wanaosafiri kwa kutumia bandari za
Jamhuri ya Mwuungano ya Tanzania wanalipa dola za Kimarekani tano kwa kila
safari. Kodi hii pia imejumuishwa katika bei ya tiketi.
Idara ya Kusimamia Bima
Idara hii ni wakala wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ilianzishwa chini ya kifungu Na. 5
cha sheria ya Bima Na 18 ya mwaka 1996 ili kutoa leseni na kurekebisha mifumo
yote ya biashara ya bima nchini. Idara hii inaongozwa na Kamishna wa Bima
Kwa
maelezo zaidi wasiliana na
IDS@Africa-online.co.tz
|