.

Majibu na maelezo kuhusu “Game Carnage in Tanzania alarms Kenya”

Response and explanations regarding the article in the East African newspaper titled “Game Carnage in Tanzania alarms Kenya

Dira Jukumu

Dira ya Wizara hii ni kuhakikisha utunzaji endelevu wa  mali asili, utamaduni na Utalii na kuhakikisha ushirikishwaji wa jamii zinazohusika, mashirika yasiyo ya kiserikali na kusimamia matumizi ya mali asili kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo

Jukumu la wizara hii ni kuandaa sera na mikakati ambayo itaongoza utunzaji endelevu wa mali asili, utamaduni na mazingiza. Kuinua na kuongeza aina ya vivutio vya utalii na kuongeza mchango wa sekta hii kwa pato la taifa na uingizaji wa fedha za kigeni.

Kazi za Wizara

  • Kusimamia sera ya Utalii, Maendeleo ya Hifadhi za Taifa, Mbuga za Wanyama, Maendeleo ya fukwe  na vivutio vya utalii, urithi wa taifa, makumbusho na kumbukumbu nyingine, mali asili, misitu na upandaji miti, uvuvi na ufugaji wa nyuki.

  • Kuendeleza nguvu kazi chini ya Wizara

  • Kusimamia shighuli za Idara Kuu za Serikali, Mashirika ya Umma na miradi iliyo chini ya Wizara

  • Kusimamia shughuli za mawakala wa Serikali walio chini ya Wizara

Taasisi na Mashirika

Sekta ya Misitu 

  • Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI)
    S.L.P. 1854 Morogoro, Tanzania
    Simu:   255 023 2263725

    Taasisi hii inafanya utafiti kugundua na kusambaza  maarifa ya kisayansi kwa washikadau ambayo itachangia  usimamizi na maendeleo endelevu ya rasilimali za misitu nchini.
     

  • Mpango wa Taifa wa Mbegu za Miti (NTSP)
    S.L.P. 373 Morogoro, Tanzania
    Simu: 255 023 2563192
    Fax:   255 023 2563275

    Mpango huu unafanya kazi kama kitengo chini ya Idara ya Misitu na unawajibika kukusanya mbegu za misitu zanye ubora nzuri kwa madhumuni ya kutosheleza mahitaji ya mbegu za miti nchini na kusafirisha nchi za nje.
     

  • Chuo cha Misitu cha Olmotonyi
    S.L.P. 943, Arusha Tanzania
    Simu: 255 027 50441

    Chuo hiki kinatoa mafunzo ya vyeti na stashahada za Misitu na Ufugaji wa Nyuki.  Aidha kuna vituo vya mafunzo kwa wafanyakazi wa Misitu huko Iringa na Rongai, Moshi.
     

  • Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine
    Kitivo cha Misitu, Morogogo, Tanzania
    Simu: 255 023 2263511
    E-mail Forestry@hhettan.gn.apc.org  au Forestry@costach.gn.apc.org

    Kitivo kinatoa digrii za kwanza za Sayansi katika misitu (B.Sc. in Forestry)

 

Sekta ya Uvuvi

Taasisi ta Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI)

Shughuli za utafiti zinafanywa kwenye maji ya bahari na maji ya mengine (mito, mabwawa,na maziwa). Taasisi inashughulika na utafiti katika rasilimali za uvuvi na kusambaza matokeo ya utafiti kwa ajili ya maendeleo ya uvuvi na matumizi endelevu ya rasilimali hii nchini. Taasisi pia inatoa mafunzo na kufanya utafiti juu ya teknolojia ya uvuvi na tathmini ya idadi ya samaki.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Wizara ya Mali Asili na Utalii
Idara ya Uvuvi
S.L.P 2462, Dar es Salaam, Tanzania.
Simu: 255 022 2650043/44
 

Chuo cha Mafunzo ya Uvuvi cha Kunduchi
Chuo hiki kinatoa mafunzo ya stashahada za Uvuvi. Mafunzo haya ni pamoja na uhandisi wa vyombo vya majini, uvuvi, teknolojia ya vyakula vinavyotokana na samaki, na sayansi ya ubaharia.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Chuo cha Mafunzo ya Uvuvi cha Kunduchi
S.L.P. 60091, Dar es Salaam, Tanzania
Simu: 255 022 2650011
 

Kituo cha Maendeleo ya Uvuvi cha Mbegani

Kinatoa mafunzo ya stashahada ya uvuvi. Mafunzo hayo ni pamoja na uundaji wa mashua, usindikaji wa samaki na udhibiti wa ubora, ufundi mitambo wa vyombo vya majini, uhandisi wa vyombo vya majini na mafunzo mengine yanayotolewa kwa vikundi maalum.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Kituo cha Maendeleo ya Uvuvi cha Mbegani
S.L.P. 83, Bagamoyo, Tanzania
 

Chuo cha Mafunzo ya Uvuvi cha Nyegezi
Kinatoa mafunzo ya stashahada ya uvuvi

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Chuo cha Mafunzo ya Uvuvi cha Nyegezi
S.L.P.  1213, Mwanza, Tanzania

 

Sekta ya Wanyamapori

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA)
Hili ni shirika la umma ambalo kazi yake ni kurekebisha, kuendeleza na kusimamia hifadhi za taifa za Serengeti, Tarangire, Arusha, Kilimanjaro, Ruaha, Manyara, Katavi na Mikumi.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA)
S.L.P. 3134, Arusha, Tanzania
Simu:    255 27 2508040
Fax:      255 27 2508216
E-mail:  tanapa@habari,co,tz

 

Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro
Eneo lililo chini ya Mamlaka haya ni kilometa za mraba elfu nane na mia tatu (8,300). Eneo hili linajumuisha wanyamapori, binaadam , na maeneo ya kumbu kumbu za kihistoria barani Afrika. Pia linaongoza kwa majaribio ya matumizi ya aina mbalimbali ya ardhi.

Kazi za Mamlaka

  • Kuendeleza maisha ya pamoja ya binaadam na wanyama pori katika mfumo wa asili na utamaduni.

  • Kuhifadhi anuwai ya kibaiolojia na msimamo wa kiikolojia wa mfumo wa ikolojia wa  Serengeti na Milima ya Ngorongoro.

  • Kuhifadhi maeneo kuhimu kimataifa katika kumbukumbu ya mambo ya kale

  • Kutunza na kuendeleza  yale yote ambayo yameifanya sehemu hii ya nchi yetu kuwa sehemu muhimu ya urithi wa dunia na hifadhi ya sehemu ya dunia ambayo uhai unawezekana kuwepo.
     

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro
S.L.P. 1, Ngorongoro, Tanzania
Simu:    255 27 2504619
Fax:      255 27 2503339
E-mail:  ncaa-hq@yako.habari.co.tz

 

Taasisi Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI)
Taasisi hii inafanya utafiti wa wanyama pori na magonjwa ya wanyamapori.

  • Inakusanya, kuhifadhi na kusambaza matokeo ya utafiti kuhusu wanyamapori na kutoa ushauri juu ya maendeleo endelevu ya rasilimali za wanyamapori kwa washikadau.

  • Kuratibu shughuli za utafiti zinazofanywa na watafiti kutoka nje ya nchi kwa kushirikiana na Tume ya Sayansi na Teknolojia.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori
S.L.P. 661, Arusha Tanzania
E-mail:  harawii@online.no

 

Chuo cha Maafisa wa Wanyamapori cha Afrika
Kazi zake

Kutoa mafunzo kwa maafisa wanyamapori kwa nchi za Kiafrika zinazozungumza Kiingereza.

Kwa taarifa zaidi wasiliana na

Chuo cha Maafisa wa Wanyamapori cha Afrika
S.L.P. 32031, Moshi, Tanzania
Fax:  255 27 2551113

Sekta ya Utalii

Bodi ya Utalii Tanzania
Bodi ya Utalii inakuza maendeleo ya Utalii Tanzania

Kazi zake

  • Kuzitangaza sehemu  za utalii Tanzania ndani na nje ya nchi.

  • Kendesha kampeni za matangazo (Kutangaza, uhusiano na umma, maonyesho ya barabarani) kwa lengo la kuwavutia watalii.

  • Kuandaa na kuchapisha vipeperushi na nyaraka nyingine za matangazo

  • Kutoa taarifa za Kitalii
    Kufanya utafiti wa masoko ili kutoa taarifa mpya za kumbukumbu za utalii nchini

Kwa taarifa zaidi wasiliana na.

 

Bodi ya Utalii Tanzania
S.L.P. 2485, Dar es Salaam, Tanzania
Simu:    255 22 2110908, 2111244/5 2136105
Fax:      255 22 2116420
E-mail:  md@ttb.ud.or.tz  au Safari@ud.co.tz

Mtandao:http://www.tanzania-web.com/home2.htm

 

Chuo Cha Mafunzo ya Hoteli na Utalii
 

Kazi zake

  • Kutoa mafunzo ya uendeshaji mahoteli na utalii katika kiwango cha cheti. Mafunzo yanatolewa katika nyanja zifuatazo:

  • Vyakula na vinywaji

  • Mapokezi

  • Utengenezaji wa Vyakula

  • Utunzaji wa nyumba

Kwa taarifa zaidi wasiliana na:
Chuo Cha Mafunzo ya Hoteli na Utalii,

S.L.P  9181, Dar es Salaam, Tanzania

Simu: 255 22 2112223