|
Mamlaka ya Kanuni za
Usafirishaji Tanzania (TTRA)
Serikali itaanzisha
Mamlaka ya Kanuni za Usafirishaji Tanzania (TTRA) hivi karibuni. Mamlaka haya
yataanzishwa chini ya Sheria ya Kanuni za Ushafirishaji na yatakuwa na jukumu la
kusimamia uendeshaji nzuri wa barabara na usafiri wa barabara, reli, bandari,
usafiri wa majini, viwanja vya ndege na usafirishaji kwa njia ya anga.
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)
Taasisi hii iliundwa Marchi, 1999. Kazi kubwa ya
Mamlaka ni
-
Kurekebisha shughuli za Usafiri wa anga katika
Tanzania
-
Kutumia
viwango vya usafiri wa anga vya kimataifa
-
Kukagua na
kusajili ndege
-
Kutoa
ushauri kwa waendeshaji wa shughuli za usafiri wa anga na watumiaji
-
Kuhakikisha
kuwa sheria zinafuatwa
-
Kutoa
mafunzo na leseni kwa marubani na wahandisi wa ndege
-
Kutoa
leseni ya viwanja vya ndege
Mamlaka ya Leseni za
Usafiri shaji Tanzania (CTLA)
Taasisi hii kazi yake ni kusimamia
utekelezaji wa kanuni na sheria. Kazi yake kubwa ni kutoa leseni za usafiri wa
barabara. Mamlaka ya Leseni za Usafiri za mikoa zimeruhusiwa kutoa leseni kwa
wasafirishaji katika mikoa inayohusika.
Tanzania Central
Freight Bureau (TCFB)
Sheria ya mwaka 1982 iliyoanzisha
kampuni hii imerekebishwa mwaka 2000 ili kwenda na mabadiliko katika mazingira
ya soko. Wajibu wa Kampuni hii ni kuharakisha maendeleo katika sekta ya usafiri
wa majini kwa kusimamia na kuhakikisha kuwa kunakuwa na ushindani na biashara
halali kwa nia ya kuinua maendeleo ya biashara hiyo na kuhakikisha upatikanaji
wa taarifa za usafiri wa majini.
Tume ya Mawasiliano ya
Tanzania (TCC)
Tume ya Mawasiliano ilianzishwa chini
ya sheria ya Mawasiliano ya Tanzania Na 18 ya mwaka 1993 ambayo ilianza kutumika
mwaka 1994. Tume iliundwa kufuatia kuvunjwa kwa Shirika la Posta na Simu ikiwa
ni sehemu ya juhudi za serikali za kuunda upya sekta ya mawasiliano. Tume ina
jukumu la kurekebisha shughuli za watoa huduma za posta na simu. Majukumu
mengine ni kufanunua sera za kuunganisha simu na viwango vya bei, kugawa na
kusimamia njia za Redio, na kutayarisha mipango ya namba, kupanga taratibu za
kugawana mapato, na kusimamia na kuona kuwa viwango vilivyowekwa vinafuatwa.
Shirika la Utabiri wa Hali ya Hewa
Kwa habari zaidi
wasiliana na
Mkurugenzi Mkuu
S.L.P. 3056
Simu: 255 22 2110231
Dar es Salaam
E-mail:
met@meteo_tz.org |