.

Dira Jukumu

Kuunda Sekta ya viwanda iliyo yenye nguvu, anuwai, imara, na yenye kuhimili ushindani itayoongeza mchango wa sekta hii katika pato la Taifa na kuwa ba  mfumo wa biashara wenye uwezo wa kuchochea uzalishaji wa bidhaa na huduma na uchumi wa hali ya juu wa fedha

Kuharakisha maendeleo ya viwanda na kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya kuongeza uzalishaji  wa viwanda vilivyopo na kuvutia wawekezaji wapya katika biashara,  kuleta ushindani katika masoko ya ndani na ya nje.

Kazi  za  Wizara

  • Kuandaa sera za Viwanda na Bishara

  • Kusimamia na kurekebisha Biashara za Nje na Ndani

  • Kulinda hatimiliki na haki za Ujirani

  • Kufuatilia masuala ya Haki za Kitaaluma

  • Kuandaa maazimio ya utendaji wa kibiashara

  • Kuweka viwango na kuanzisha vipimo vya uzito na urefu

  • Kuwasiliana na kuratibu Mashirika ya Kimataifa (WIPO, ARIPO, GATI, UNCTAD, UNIDO, SADCC, Group 77 n.k)

  • Kusimamia shughuli za Idara za Serikali, Mashirika ya Umma na Miradi iliyo chini ya Wizara

  • Kusimamia shughuli za Taasisi zilizo chini ya Wizara hii

Taasisi/Mashirika

  • Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC)
    Shirika hili ni kiongozi wa mashirika ya maendeleo nchini, ambalo lilianzisha kama kampuni ya kisheria na sharia ya Bunge mwaka 1962 kusaidia na kukuza maendeleo ya Taifa kiuchumi.  Shirika hili linamilikiwa na Serikali ya Jamhuri ya  Muungano  ya  Tanzania

  • Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO)

  • Shirika la Viwango Tanzania (TBS)

  • Chama cha Maendeleo ya Uhandisi na Ufundi Mitambo Tanzania

  • Shirika la Vipimo

  • Shirika la Utafiti wa Viwanda na Maendeleo

  • BRELA

  • Kituo cha  matumizi ya mashine katika kilimo na technolojia ya vijijini (CAMARTEC)