Ukuaji
wa Uchumi Duniani
23.
Katika mwaka 2003, pato la dunia lilikua kwa asilimia 3.9 ikilinganishwa
na asilimia 3.0 mwaka 2002. Hali ya wasiwasi kuhusu ugaidi na usalama
haikuathiri mwenendo wa ukuaji wa uchumi duniani. Ongezeko la pato la
dunia mwaka 2003 lilichangiwa zaidi na ukuaji uwekezaji rasilimali, kukua
kwa biashara na ongezeko la uzalishaji viwandani. Aidha, kuendelea kuimarika
kwa uchumi wa Marekani na nchi za Asia kumechangia mwenendo huo. Kwa nchi
zilizoendelea, pato lilikua kwa asilimia 2.1 mwaka 2003 ikilinganishwa
na asilimia 1.7 mwaka 2002. Pato la nchi zinazoendelea lilikua kwa asilimia
6.1 mwaka 2003 ikilinganishwa na asilimia 4.6 mwaka 2002. Ongezeko hili
kubwa mwaka 2003 lilitokana na kuongezeka kwa uwekezaji wa rasilimali
pamoja na kuimarika kwa sera za uchumi. Pato la Afrika lilikua kwa silimia
4.1 mwaka 2003 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 3.5 mwaka 2002.
Jedwali
2.1:Pato la Dunia 2001 – 2003 (Badiliko %)
| |
2001 |
2002 |
2003 |
| Pato la Dunia |
2.4 |
3.0 |
3.9 |
| Nchi Zilizoendelea |
1.1 |
1.7 |
2.1 |
| Nchi Zinazoendelea |
4.1 |
4.6 |
6.1 |
| Nchi za Asia zinazoendelea |
|
6.4 |
7.8 |
| Amerika ya Kusini |
|
-0.1 |
1.7 |
| Afrika |
3.6 |
3.4 |
4.1 |
Chanzo: Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF)
24.
Kiwango cha biashara ya bidhaa na huduma duniani kiliongezeka kwa asilimia
4.5 mwaka 2003 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 3.1 mwaka 2002.
Uagizaji bidhaa kwa nchi zilizoendelea uliongezeka kwa asilimia 3.5 mwaka
2003 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 2.3 mwaka 2002. Kwa upande
wa nchi zinazoendelea, uagizaji wa bidhaa uliongezeka kwa asilimia 8.9
mwaka 2003 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 6.2 mwaka 2002 wakati
ambapo kwa nchi zilizoendelea uliongezeka kwa asilimia 2.7 mwaka 2003
ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 1.9 mwaka 2002. Kwa nchi zinazoendelea,
uuzaji nje wa bidhaa uliongezeka kwa asilimia 8.7 mwaka 2003 ikilinganishwa
na asilimia 6.5 mwaka 2002.
25.
Fahirisi ya bei ya bidhaa za viwanda iliongezeka kwa asilimia 14.5 mwaka
2003 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 2.4 mwaka 2002. Bei ya mafuta
yasiyosafishwa iliongezeka kwa asilimia 15.8 mwaka 2003 ikilinganishwa
na asilimia 2.5 mwaka 2002. Bei ya bidhaa asilia iliongezeka kwa asilimia
7.1 mwaka 2003 ikilinganishwa na asilimia 0.5 mwaka 2002. Katika nchi
zilizoendelea, bei ziliongezeka kwa asilimia 1.2 mwaka 2003 ikilinganishwa
na asilimia 1.5 mwaka 2002. Kwa upande wa nchi zinazoendelea, bei ziliongezeka
kwa asilimia 6.1 mwaka 2003, sawa na ilivyokuwa mwaka 2002. Katika nchi
za Afrika, bei ziliongezeka kwa asilimia 10.3 mwaka 2003 ikilinganishwa
na asilimia 9.6 mwaka 2002.
Hali
ya Uchumi wa Bara la Afrika
26. Nchi nyingi za Afrika zimepata mafanikio kutokana na utekelezaji wa
sera thabiti za kukuza uchumi, ambazo zimesaidia kupunguza kasi ya upandaji
bei, na kuleta nafuu ya madeni ya nje. Pamoja na kuimarika kwa shughuli
za kiuchumi katika bara la Afrika, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la
Sahara katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, hali ya umaskini imezidi
kuongezeka na imekuwepo tofauti kubwa katika hali ya ukuaji wa uchumi
baina ya nchi kutokana na sababu mbalimbali, hususan, hali ya hewa, usalama
na fursa za uwekezaji.
27.
Pamoja na kuimarika kwa hali ya amani na usalama katika Jamuhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo, pato la nchi za Maziwa Makuu lilikua kwa asilimia 3.7 mwaka
2003 ikilinganishwa na asilimia 4.6 mwaka 2002. Ukuaji huo mdogo umetokana
na ukame uliosababishwa na hali mbaya ya hewa iliyoathiri ukuaji wa sekta
muhimu za uzalishaji, hususan, kilimo. Kwa upande wa Nchi za Pembe ya
Kaskazini Mashariki, pato lilikua kwa asilimia 1.9 mwaka 2003 ikilinganishwa
na asilimia 3.9 mwaka 2002. Ukuaji huo mdogo umesababishwa hasa na ukame
na njaa katika nchi ya Ethiopia. Pamoja na matatizo ya uchumi yanayoikabili
nchi ya Zimbabwe, pato la nchi za Kusini mwa Afrika lilikua kwa asilimia
2.4 mwaka 2003 ikilinganishwa na asilimia 2.3 mwaka 2002. Ongezeko kidogo
la pato katika eneo hili limechangiwa hasa na kuimarika kwa shughuli za
kiuchumi nchini Angola kutokana na kugundulika kwa maeneo mapya ya uzalishaji
mafuta, pamoja na kuimarika kwa hali ya amani na usalama.
28.
Nchi za Afrika ya Kati na Magharibi zilipata mafanikio makubwa kiuchumi
katika mwaka 2003. Pato la nchi hizi lilikua kwa asilimia 6.4 mwaka 2003
ikilinganishwa na asilimia 3.4 mwaka 2002. Ukuaji huo mkubwa umetokana
na ongezeko kubwa la uzalishaji wa mafuta nchini Nigeria. Kwa upande wa
nchi za Kaskazini mwa Afrika, pato lilikua kwa asilimia 6.2 mwaka 2003
ikilinganishwa na asilimia 3.4 mwaka 2002. Ongezeko hilo la pato limechangiwa
na kuongezeka kwa uzalishaji katika sekta ya kilimo kutokana na hali nzuri
ya hewa, kuongezeka kwa matumizi ya serikali ya kuijenga upya Algeria
baada ya kukumbwa na janga la tetemeko la ardhi, pamoja na kuongezeka
kwa uzalishaji wa mafuta nchini Algeria. Jedwali Na. 2.2 linaonyesha mwenendo
wa viashirio muhimu katika uchumi jumla wa baadhi ya nchi za Afrika.
Jedwali Na.2.2: Mwenendo wa Pato
la Taifa, Kasi ya Upandaji Bei
na Urari wa Malipo ya
Kawaida kwa Baadhi ya Nchi
za Afrika.
| Nchi |
Pato la Taifa
(Badiliko %) |
Bei kwa Mlaji
(Badiliko %) |
Urari wa Malipo ya Kawaida
(% ya Pato
la Taifa) |
| 2001 |
2002 |
2003 |
2001 |
2002 |
2003 |
2001 |
2002 |
2003 |
|
AFRIKA |
3.6 |
3.4 |
4.1 |
13.0 |
9.6 |
10.3 |
-0.1 |
-1.7 |
-0.7 |
| Kaskazini
Algeria
Morocco
Tunisia |
4.1 |
3.4 |
6.2 |
2.6 |
2.1 |
2.2 |
7.2 |
4.5 |
6.0 |
| 2.1 |
4.1 |
6.7 |
4.2 |
1.4 |
2.6 |
12.9 |
7.8 |
11.3 |
| 6.5 |
3.2 |
5.5 |
0.6 |
2.8 |
1.2 |
4.8 |
4.1 |
3.1 |
| 5.2 |
1.7 |
6.1 |
1.9 |
2.8 |
2.7 |
-4.3 |
-3.5 |
-2.9 |
| Kusini mwa Jangwa la Sahara |
3.8 |
3.4 |
4.4 |
21.6 |
14.0 |
17.4 |
-3.9 |
-5.6 |
-4.0 |
| Pembe ya Afrika
Ethiopia
Sudan |
6.1 |
3.9 |
1.9 |
1.8 |
1.3 |
10.5 |
-7.4 |
-8.5 |
-7.3 |
| 7.7 |
1.2 |
-3.8 |
-7.1 |
-7.2 |
15.1 |
-4.2 |
-5.7 |
-4.7 |
| 5.3 |
6.0 |
5.8 |
4.9 |
8.3 |
7.7 |
-10.3 |
-9.7 |
-8.3 |
| Nchi za Maziwa Makuu
DRC
Kenya
Tanzania
Uganda |
2.3 |
4.6 |
3.7 |
54.6 |
8.8 |
7.7 |
-3.9 |
-3.0 |
-3.3 |
| -2.1 |
3.5 |
5.0 |
356.7 |
27.7 |
9.1 |
-4.7 |
-2.7 |
-2.0 |
| 1.2 |
1.0 |
1.5 |
5.8 |
2.0 |
9.7 |
-3.5 |
- |
-2.3 |
| 5.6 |
6.3 |
5.5 |
5.2 |
4.6 |
5.0 |
-1.5 |
-4.0 |
-2.6 |
| 5.5 |
6.7 |
4.9 |
4.5 |
5.7 |
5.9 |
-6.8 |
-6.3 |
-6.0 |
| Kusini mwa Afrika
Angola
Zimbabwe |
2.9 |
2.3 |
2.4 |
35.2 |
44.3 |
54.3 |
-4.8 |
-3.5 |
-3.7 |
| 3.2 |
15.3 |
4.5 |
152.6 |
108.9 |
98.3 |
-2.0 |
-5.8 |
-6.2 |
| -8.8 |
-12.8 |
-13.2 |
76.7 |
140.0 |
431.7 |
-9.7 |
-2.2 |
-4.5 |
| Afrika ya Kati na Magharibi
Ghana
Nigeria |
4.0 |
3.4 |
6.4 |
12.0 |
8.4 |
9.7 |
-2.7 |
-7.0 |
-3.6 |
| 4.2 |
4.5 |
4.7 |
32.9 |
14.8 |
26.4 |
-6.6 |
0.5 |
-0.4 |
| 2.8 |
1.5 |
10.6 |
18.9 |
13.7 |
14.4 |
2.7 |
-10.7 |
-2.8 |
| CFA franc zone
Cameroon
Cote d’ Ivoire |
4.9 |
4.4 |
4.1 |
4.2 |
3.8 |
2.0 |
-6.7 |
-4.7 |
-4.1 |
| 5.3 |
6.5 |
4.2 |
2.8 |
6.3 |
1.2 |
-1.7 |
-7.2 |
-3.1 |
| 0.1 |
-1.6 |
-3.8 |
4.4 |
3.1 |
3.8 |
-2.0 |
6.2 |
4.9 |
|
Afrika ya Kusini |
2.8 |
3.6 |
1.9 |
5.7 |
8.9 |
6.0 |
-0.1 |
0.3 |
-1.2 |
|
Nchi zinazonunua mafuta |
3.8 |
3.1 |
3.0 |
11.9 |
8.9 |
9.6 |
-2.4 |
-1.9 |
-2.2 |
|
Nchi zinazouza mafuta |
3.0 |
4.6 |
8.0 |
16.8 |
12.3 |
12.6 |
6.2 |
-1.1 |
3.4 |
Chanzo: Shirika
la Fedha la Kimataifa,
(IMF)
|
|
|
| |
Jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC)
29.
Katika mwaka 2003, Jumuiya ya Afrika Mashariki imeendelea kutekeleza mkakati
wa maendeleo wa miaka mitano (2001-2005) kwa lengo la kuimarisha ushirikiano
baina ya nchi wanachama na kutekeleza programu zilizopewa kipaumbele kama
inavyoainishwa katika mwongozo wa utekelezaji. Juhudi zilielekezwa zaidi
katika kukamilisha itifaki ya ushuru wa pamoja wa forodha. Maeneo muhimu
yaliyokamilika katika itifaki hiyo ni pamoja na uondoaji wa ushuru wa
bidhaa kwa biashara za ndani na utaratibu wa kuhakiki uasili wa bidhaa,
uanzishaji wa mfumo mmoja wa ushuru wa forodha ambapo viwango vitakavyotumika
ni asilimia 0, 10 na 25.
30.
Mkutano wa nchi wanachama kuhusu maendeleo ya barabara za nchi za Afrika
Mashariki ulifanyika mwezi Aprili, 2003 ambapo nchi wanachama na wahisani
walikubaliana kuongeza juhudi katika kuendeleza miradi iliyoainishwa katika
mtandao wa barabara. Upembuzi yakinifu kuhusu mpango wa miaka mitano wa
kuendeleza na kuwekeza katika sekta ya hali ya hewa umeshaanza uwekezaji
kwa miaka mitano ijayo. Utekelezaji wa Mpango Kamambe wa Nishati wa Afrika
Mashariki uliendelea. Itifaki ya Maendeleo Endelevu ya Bonde la Ziwa Victoria
ilisainiwa Novemba, 2003. Nchi wanachama zilikubaliana na mkakati wa utekelezaji
na unasubiri kuridhiwa. Vilevile, mradi wa usimamizi na uendelezaji uvuvi
katika ziwa Victoria ulizinduliwa Oktoba, 2003 mjini Jinja, Uganda. Mradi
huu unalenga katika kuweka vifaa vya kuimarisha uvuvi endelevu katika
ziwa Victoria.
Jumuiya
ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
31. Katika mwaka 2003, Tanzania ilikuwa mwenyeji na mwenyekiti wa mkutano
wa Wakuu wa Nchi za SADC uliofanyika Dar es salaam Agosti, 2003. Wakuu
wa Nchi na Serikali waliidhinisha mkakati wa mpango wa maendeleo (Regional
Indicative Strategic Development Plan-RISDP) wa ushirikiano kwa kipindi
cha miaka kumi na mitano ijayo. Ili kufanikisha ufuatiliaji na utekelezaji,
mpango wa “RISDP” umeweka malengo na muda wa utekelezaji wa
malengo hayo katika sekta mbalimbali za ushirikiano.
32.
Nchi wanachama wa SADC walitia saini mkataba wa Ulinzi na Usalama ili
kudumisha mahusiano, kuunganisha nguvu za utekelezaji wa malengo yaliyowekwa,
pamoja na kuweka moja ya misingi imara katika suala zima la ulinzi na
usalama katika bara la Afrika. Hali ya Kisiasa katika umoja wa nchi za
SADC ilizidi kuimarika katika mwaka 2003 baada ya kusainiwa kwa mkataba
wa kuleta amani Angola Aprili, 2002 na kuwekwa madarakani kwa serikali
ya mpito katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Juni, 2003.
33.
Pamoja na jitihada zilizochukuliwa na Nchi wanachama wa SADC kupunguza
umaskini na kukuza maendeleo ya kijamii kikanda, bado changamoto ni kubwa.
Kasi ya kupungua kwa umaskini bado hailingani na malengo ya kimataifa
ya kupunguza umaskini kwa nusu ifikapo mwaka 2015. Ongezeko la umaskini
katika nchi za SADC limechangiwa na sababu nyingi zikiwa ni pamoja na
ukame wa mara kwa mara, mafuriko, ukosefu wa amani na usalama, pamoja
na magonjwa kama UKIMWI, malaria na magonjwa mengine ya kuambukiza.
Mpango
Mpya wa Ushirikiano wa Kusukuma Maendeleo ya Nchi za Afrika (NEPAD)
34. Katika mkutano wa pili wa Umoja wa Afrika uliofanyika Maputo, Msumbiji
Julai, 2003 viongozi wa Afrika walikubaliana kuendelea kutimiza malengo
ya NEPAD ili kuondoa umaskini na kukuza uchumi wa bara la Afrika. Tayari
nchi 15 za Afrika zimeshajiunga na utaratibu unaotoa fursa kwa nchi kufanyiwa
ukaguzi na kupimwa ufanisi wake katika kutekeleza vigezo vya uchumi na
utawala bora (NEPAD Peer Review Mechanism). Mpango huo unasisitiza uimarishaji
na uzingatiaji wa masuala ya uwazi, utawala bora, utekelezaji wa haki
za binadamu na ufanisi katika uendeshaji uchumi. Mafanikio ya NEPAD katika
mwaka 2003 yalionekana pia katika ushirikiano ulioonyeshwa na nchi zote
za Afrika na jumuiya ya kimataifa. Aidha, wakuu wa Nchi na Serikali wa
Ukanda wa Mashariki ya Afrika walikutana mjini Nairobi, Kenya Oktoba 2003
kujadili, kuchambua na kukubaliana kuhusu vigezo vya programu na miradi
ya kupewa kipaumbele chini ya mpango wa NEPAD, utaratibu wa kuratibu programu
na miradi ya kikanda, na jinsi ya kushirikisha sekta binafsi kwenye utekelezaji
wa mpango wa NEPAD. Ili kuongeza ufanisi katika kuratibu programu na miradi
ya kimaendeleo katika ukanda wa mashariki ya Afrika, Wakuu wa Nchi waliridhia
Kenya kuwa mratibu wa programu na miradi ya kimaendeleo kikanda.
Ushirikiano
wa Kiufundi baina ya Nchi Zinazoendelea (TCDC)
35. Mkutano wa 13 wa kamati ya ushirikiano wa kiufundi baina ya nchi zinazoendelea
ulifanyika New York, Marekani Mei, 2003. Mkutano huu ulifanyika sambamba
na maadhimisho ya miaka 25 ya utekelezaji wa mpango mahsusi wa “Buenos
Aires Plan of Action”. Ili kufuatilia maamuzi ya mkutano huo, kundi
la nchi zinazoendelea (Group 77) pamoja na China zilikutana Desemba, 2003
nchini Morocco na kulikubali azimio la “Marrakesh” kama moja
ya misingi ya makubaliano ya utekelezaji wa mpango wa Havana. Kuhusu ushirikiano
wa kubadilishana ufundi, Serikali ilifaidika kutokana na misaada ya serikali
ya China ambapo wataalam wa Kitanzania walihudhuria mafunzo nchini China
katika maeneo yanayohusu utumiaji na utengenezaji wa vyombo vya hali ya
hewa, utunzaji wa mazingira, utunzaji wa nafaka, ukulima wa mboga, teknolojia
ya tarakishi, nishati ya maji, usindikaji wa vyakula na bidhaa, na teknolojia
ya upimaji wa viwango.
Ushirikiano
wa kirafiki kati ya nchi za Afrika na China
36. Mkutano wa pili wa mawaziri wa nchi za Afrika na China ulifanyika
Addis Ababa, Ethiopia Desemba, 2003 kwa lengo la kuendeleza ushirikiano
kati ya Afrika na China kiuchumi, kijamii na kisiasa. Katika mkutano huo,
mpango wa utekelezaji wa Addis Ababa kwa mwaka 2004-2006 (Addis Ababa
Action Plan 2004-2006) ulipitishwa. Katika mpango huo nchi ya China imepanga
kutoa mafunzo kwa wataalamu zaidi ya 10,000 kutoka katika bara la Afrika
kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo ili kuongeza ujuzi wa wafanyakazi katika
bara la Afrika. Pamoja na hayo, China iliahidi pia kuondoa kodi kwa baadhi
ya bidhaa zinazoingia ndani ya nchi hiyo kutoka Afrika.
Mkutano
wa Kimataifa wa Tokyo kwa ajili ya Maendeleo ya Afrika (TICAD)
37. Mwaka 2003, TICAD ilitimiza miaka kumi kwa mkutano wa TICAD III kufanyika
Tokyo, nchini Japan. Maeneo yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na; usalama,
utawala bora, kilimo, maendeleo ya sekta binafsi, miundombinu, rasilimali
watu, afya, maji, ushirikiano wa kikanda na ushirikiano kati ya nchi za
Afrika na Asia. TICAD III ilitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kusaidia
juhudi za Afrika za kuleta maendeleo. Mikakati ya Tanzania ya maendeleo
kama ilivyoanishwa katika Dira ya Taifa 2025 inawiana na maeneo yaliyopewa
kipaumbele katika mpango wa TICAD. Hivyo, agenda ya Serikali katika utekelezaji
wa TICAD inawiana pia na mpango wa taifa wa kupunguza umaskini.
Mpango
wa Marekani wa Kusaidia Maendeleo ya Afrika (AGOA)
38. AGOA ni mpango ulioanzishwa na serikali ya Marekani mwaka 2000 kwa
lengo la kusaidia nchi za Kiafrika zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara
kuongeza mauzo ya bidhaa zao kwenye soko la Marekani kwa kutotozwa ushuru
au kutowekewa kiwango. Mpango huu umebuniwa ili kuziwezesha nchi hizi
kuongeza mapato yao ya fedha za kigeni na hivyo kuimarisha uwezo wao wa
kupunguza umaskini. Tanzania kwa upande wake bado haijaweza kunufaika
vizuri kutokana na fursa hii ikilinganishwa na baadhi ya nchi nyingine
zilizoko katika mpango huu. Matatizo yanayochangia hali hii ni kutokuwepo
kwa uzalishaji wa bidhaa nyingi na zenye ubora unaotakiwa na soko la Marekani,
udhaifu wa miundombinu, na ufahamu mdogo wa wadau kuhusu soko lenyewe.
Kwa kufahamu matatizo hayo, Serikali ikishirikiana na sekta binafsi imebuni
na kutekeleza mikakati ambayo italetea kufanikisha azma hii. Baadhi ya
mikakati iliyobuniwa na kutekelezwa ni pamoja na kuwaelimisha wadau juu
ya masharti na mbinu za kujipenyeza kwenye soko hilo, kutoa vivutio kwa
wawekezaji wenye nia ya kuzalisha bidhaa kwa ajili ya soko hilo, na kuanzisha
na kuendeleza maeneo huru ya uzalishaji bidhaa za kuuza nje (EPZ). Kutokana
na mikakati hii, tayari baadhi ya wadau wameshaanza kunufaika na fursa
hii. Viwanda vya Sunflag na Star Apparel vimeshaanza kuuza bidhaa za nguo
Marekani. Kwa mwaka 2003, bidhaa zenye thamani ya dola 1.5 milioni ziliuzwa
Marekani. Vile vile, kumekuwepo na mauzo ya nyuzi Mauritius kwa ajili
ya utengenezaji wa nguo za kuuza Marekani chini ya mradi wa AGOA.
Shirika
la Kimataifa la Biashara (WTO)
39. Mkutano wa tano wa Mawaziri wa Shirika la Kimataifa la Biashara (WTO)
ulifanyika Cancun Mexico Septemba 10 – 14 mwaka 2003 na lengo likiwa
ni kuendeleza na kukamilisha majadiliano ya biashara yaliyotokana na mkutano
wa nne yajulikanayo kama Agenda ya Maendeleo ya Doha. Hata hivyo, mkutano
huo ulifungwa bila kufikia makubaliano katika mambo mengi muhimu. Mambo
yaliyokwamisha mafanikio ya mkutano huo yalikuwa ni pamoja na masuala
ya ruzuku katika kilimo ambapo nchi zinazoendelea zilitaka nchi zilizoendelea
kuondoa ruzuku zinazotoa kwa wakulima wao ili bidhaa zao ziwe na ushindani
sawa katika soko. Nchi zilizoendelea hazikukubaliana na matakwa ya nchi
zinazoendelea katika suala hili. Jambo la pili na la msingi lililokwamisha
majadiliano lilikuwa ni juu ya kuendeleza majadiliano kwa masuala ya Singapore
yanayojumuisha biashara na vitega uchumi, biashara na sera ya ushindani,
uwazi katika manunuzi ya Serikali na usaidizi wa kibiashara. Katika masuala
haya, nchi zinazoendelea hazikutaka majadiliano yaanze wakati zile zilizoendelea
zilitaka kuendeleza majadiliano. Mkutano ulivunjika baada ya nchi zinazoendelea
kutokubaliana na mpango wa kuanza majadiliano katika mambo haya. Kutokana
na msimamo ulionyeshwa na nchi zinazoendelea huko Cancun Mexico, nchi
zilizoendelea zimekubali kuondoa katika meza ya majadiliano masuala matatu
ya Singapore hasa biashara na vitega uchumi, pamoja na biashara na sera
za ushindani. Hata hivyo, juhudi kubwa zinafanyika katika ngazi ya WTO
ili kuhakikisha kuwa majadiliano katika mambo muhimu yanaendelea kwa lengo
la kufikia makubaliano yatakayoboresha mazingira ya biashara duniani.
Tanzania kwa upande wake iliendelea kushirikiana na nchi nyingine zinazoendelea
katika kudai maslahi mazuri zaidi kutoka kwa nchi zilizoendelea. |
|