MAENDELEO
YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI
WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU
KATIKA MAENDELEO | |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Kilimo |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
VIWANDA
NA BIASHARA |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Ukuaji wa Sekta
218. Sekta ya viwanda ilikua kwa asilimia 8.6 mwaka 2003 ikilinganishwa na asilimia 8.0 mwaka 2002. Mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa uliongezeka kutoka asilimia 8.4 mwaka 2002 ikilinganishwa na asilimia 8.7 mwaka 2003. Kuongezeka kwa ukuaji na mchango wa sekta katika Pato la Taifa kulitokana na kuimarika kwa viwanda na ongezeko la uzalishaji wa bidhaa hususan nguo, mabati na vyakula baada ya viwanda hivyo kufufuliwa. Viwanda hivyo vinafanyakazi vizuri kwa maana ya uzalishaji bidhaa, utoaji wa ajira na ulipaji wa kodi kwa Serikali. Aidha, mafanikio makubwa katika sekta hii yalitokana na kuongezeka kwa tija katika viwanda mbalimbali vilivyobinafsishwa. Miradi
Iliyoidhinishwa Gharama
za uzalishaji Uzalishaji
Katika Baadhi ya Viwanda Nchini 222. Kwa upande wa viwanda vya bidhaa za ujenzi, uzalishaji wa bati uliongezeka kwa asilimia 31 ikilinganishwa na asilimia 22, toka tani 31,742 mwaka 2002, kufikia tani 41,725 mwaka 2003. Uzalishaji wa saruji uliongezeka kwa asilimia 16 toka tani 1.026 milioni mwaka 2002 kufikia tani 1.186 milioni mwaka 2003. Tani 166,446 za saruji ziliagizwa kutoka nje ya nchi ikilinganishwa na tani 149,079 zilizoagizwa mwaka 2002. Vile vile, mauzo ya saruji nje ya nchi yalipungua kutoka tani 37,203 mwaka 2002 hadi tani 34,396, sawa na upungufu wa asilimia 7.5. Matumizi ya saruji yaliongezeka kwa asilimia 15.9 toka tani 1,137,958 hadi tani 1,318,484 mwaka 2003. 223. Kutokana na marekebisho ya menejimenti na kufufuliwa kwa viwanda vya nguo vya Mwatex, Mutex, Sunguratex na Mbeyatex, uzalishaji wa nguo uliongezeka kwa asilimia 1 toka mita za mraba 106,305 mwaka 2002 hadi mita za mraba 107,408 mwaka 2003. Uzalishaji wa kamba za katani uliongezeka toka tani 5,901 mwaka 2002 hadi tani 6,839 mwaka 2003. Uzalishaji wa nyavu za uvuvi uliongezeka kwa asilimia 37 mwaka 2003 toka tani 30 mwaka 2002 hadi tani 41 mwaka 2003. 224. Uzalishaji wa unga wa ngano uliongezeka kwa asilimia 62 kutoka tani 219,118 mwaka 2002 hadi tani 355,616 mwaka 2003, wakati uzalishaji wa biskuti na tambi uliongezeka kutoka tani 2,284 mwaka 2002 hadi tani 5,906 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 159. Aidha, uzalishaji wa konyagi ulipanda kwa asilimia 25 toka lita 2,937,000 mwaka 2002 hadi lita 3,670,000. Uzalishaji wa bia uliongezeka kutoka lita 175,870,000 hadi lita 194,100,000 sawa na ongezeko la asilimia 10 mwaka 2003. Uzalishaji wa Chibuku ulipungua kwa asilimia 24 mwaka 2003, kutoka lita 19,400,000 mwaka 2002 hadi lita 14,825,000 mwaka 2003. Kwa upande wa uzalishaji sigara, kulikuwa na ongezeko la asilimia 4, kutoka sigara milioni 3,778 mwaka 2002 hadi sigara milioni 3,920 mwaka 2003. Biashara
ya ndani 226. Katika kipindi cha mwaka 2002/03, sekta ya biashara ilipanuka kwa maana ya watu wengi zaidi kushiriki katika shughuli za biashara. Idadi ya leseni za biashara zilizotolewa iliongezeka kwa asilimia 3.7. Jumla ya leseni za biashara 99,767 zilitolewa na kuingiza sh.8,670 milioni mwaka 2002/03 ikilinganishwa na leseni za biashara 96,172 zilizoingiza sh.8, 127 milioni mwaka 2001/02 kama ilivyoonyeshwa katika Jedwali 14.1. Ongezeko hilo lilitokana na kuboreshwa kwa taratibu za utoaji wa leseni za biashara na kuimarika kwa mazingira ya kufanya biashara nchini. Hata hivyo, pamoja na ongezeko hilo, hali ya ukiukaji wa kanuni mbalimbali za biashara ulionekana kuongezeka. Katika mwaka 2002/03, wafanyabiashara wapatao 11,971 walitozwa kiasi cha sh. 460 milioni kama adhabu kwa kukiuka sheria na kanuni mbalimbali za uendeshaji wa biashara, ikilinganishwa na idadi ya wafanyabiashara 6,236 waliotozwa sh. 301.7 milioni kwa mwaka 2001/02, hili ni ongezeko la asilimia 89 kwa idadi ya wafanyabiashara waliotozwa adhabu na ongezeko la asilimia 52.5 kwa kiasi kilichokusanywa.
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| Jedwali 14.1:
Utoaji wa Leseni za Biashara kwa Mwaka 2003
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Chanzo: Wizara ya Viwanda na Biashara Maonyesho
ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-Salaam Jedwali 14.2:
Washiriki wa Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa wwa Kipindi
cha 2000 – 2003
Chanzo: Bodi ya Biashara ya Nje 228. Mwaka 2003, kwa mara ya kwanza, katika eneo la Afrika Mashariki, Tanzania ilikuwa mwenyeji wa maonyesho ya sita ya kimataifa ya kibiashara ya nchi za kiafrika na Kiarabu “ (6th Afro-Arab Trade Fair) yaliyofanyika Dar es Salaam kati ya tarehe 5 – 14 Desemba 2003. Maonyesho haya yalihudhuriwa na nchi 33 za Kiafrika na Kiarabu na Mashirika ya Kimataifa 5. Makampuni zaidi ya 1000 kutoka ndani yalishiriki maonyesho haya. Pia, maagizo ya kibiashara yenye thamani ya dola 171,439,429.37 yalitolewa yakihusisha asilimia 71 ya mauzo ya nje na asilimia 28 kuagiza na asilimia 1 mauzo ya ndani. Jedwali Na.58(MATUMIZI YA SARUJI NCHINI) Jedwali Na.59(UZALISHAJI WA BAADHI YA BIDHAA VIWANDANI) Jedwali Na.60(VIWANDA: IDADI YA WATU WALIOAJIRIWA*) Jedwali Na.61(VIWANDA: GHARAMA ZA KAZI*) Jedwali Na.62(VIWANDA: MUHTASARI WA MATOKEO *) Jedwali Na.63('VIWANDA - MUHTASARI WA MATOKEO KIMKOA*) Jedwali
Na.65(VIGEZO VYA UFANISI KATIKA SEKTA YA VIWANDA) |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||