MAENDELEO
YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI
WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU
KATIKA MAENDELEO | |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Kilimo |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
KILIMO
NA MIFUGO |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
KILIMO
Ukuaji wa Sekta 189. Sekta ya kilimo katika mwaka 2003 ilikua kwa asilimia 4.0 ikilinganishwa na asilimia 5 mwaka 2002. Kupungua kwa kiwango cha ukuaji kulitokana na ukame uliojitokeza sehemu nyingi za nchi hasa mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga Pwani, Arusha, Manyara na Tabora ambayo iliathiriwa sana na ukame. Mikoa ya Mbeya, Iringa, Lindi, Mara, Mwanza, Tanga, Kilimanjaro na Mtwara pia iliathirika na ukame lakini kwa kiasi tu. Mchango wa sekta ya kilimo katika Pato la Taifa ulikuwa asilimia 46.8. Mazao
ya Chakula |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| Jedwali Na. 11.1:
Uzalishaji wa Mazao ya Chakula Mwaka
2002 Na 2003
Chanzo: Ofisi ya Taifa ya
Takwimu
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Mazao ya Biashara
191. Uzalishaji wa mazao mengi makuu ya biashara katika mwaka 2003 uliongezeka kama ifuatavyo: uzalishaji wa pamba uliongezeka kutoka tani 149,000 mwaka 2002 hadi tani 188,000 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 26. Uzalishaji wa chai uliongezeka kutoka tani 25,000 mwaka 2002 hadi tani 30,000 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 20. Uzalishaji wa korosho uliongezeka kutoka tani 78,000 mwaka 2002 hadi tani 92,000 mwaka wa 2003, sawa na ongezeko la asilimia 18. Uzalishaji wa mkonge ulibakia tani 24,000 mwaka 2003 kama ilivyokuwa mwaka 2002 kutokana na wawekezaji kuwa na mitaji midogo na wengine kushindwa kupata hati za mashamba husika. Uzalishaji wa tumbaku ulipungua kutoka tani 59,000 mwaka 2002 hadi tani 20,000 mwaka 2003, sawa na upungufu wa asilimia 66 kutokana na kuwepo kwa ukame na kupatikana kiwango kisichoridhisha cha mbolea za kupandia na kukuzia. Uzalishaji wa pareto ulipungua kutoka tani 2,000 mwaka 2002 hadi tani 1,000 mwaka 2003, sawa na upungufu wa asilimia 50. Uzalishaji wa kahawa ulipungua kutoka tani 67,000 mwaka 2002 hadi tani 53,000 mwaka 2003, sawa na upungufu wa asilimia 21 kutokana na upungufu wa mvua za vuli ambazo ni muhimu katika kukomaza na kusaidia kuchanua kwa maua. Uzalishaji wa mazao ya biashara mwaka 2003 unaonyeshwa kwenye Jedwali Na. 11.2. Jedwali Na. 11.2:
Uzalishaji wa
Mazao Mbalimbali
ya Biashara 2001 –2003
Chanzo: Ofisi ya Taifa ya
Takwimu MIFUGO 192. Tanzania inakadiriwa kuwa na kiasi cha ng'ombe wapatao 17.7 milioni, mbuzi 12.5 milioni, kondoo 3.5 milioni, kuku 47.0 milioni na nguruwe 880,000. Hatua zilizochukuliwa ili kuboresha mifugo na mazao yake yaweze kukubalika katika masoko ya ndani na ya nje (kikanda na kimataifa) mwaka 2003 zilikuwa ni pamoja na kuzalisha dozi 65,995 za mbegu bora za ng'ombe, kuhamilisha ng'ombe 51,398, kusambaza mitamba 3,937 kwa ajili ya wafugaji wadogo wadogo wa ng'ombe wa maziwa nchini, kuchimba malambo 171 katika mikoa 16 kwa kushirikisha wilaya 49, ujenzi wa minada 52, vituo 15 vya kukagulia afya ya mifugo, vituo 78 vya kupumzikia mifugo, vituo 12 vikubwa vya kupakilia ng'ombe, vituo vya reli vya kupakilia na kupakulia mifugo kwenye mabehewa, kukarabati mabehewa 50 ya kubebea mifugo na kuendesha kampeni za kitaifa za kuhamasisha ulaji mazao ya mifugo ili kuinua matumizi ya mazao ya mifugo. 193. Uzalishaji wa mazao ya mifugo ulikuwa kama ifuatavyo:- Nyama kutoka tani 332,000 mwaka 2002 hadi tani 341,500 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 2.78; maziwa kutoka lita 900 milioni mwaka 2002 hadi lita 980,500 milioni mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 8.21; na mayai ya kuku kutoka 650 milioni mwaka 2002 hadi 790 milioni mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 17.72. Ongezeko katika uzalishaji lilitokana na upatikanaji wa kuridhisha wa malisho, maji na juhudi za ukusanyaji na usindikaji na kupanuka kwa wigo wa soko la ndani la bidhaa. Hali ya uzalishaji wa mazao na bidhaa za mifugo inaonyeshwa kwenye Jedwali 3. Jedwali
Na. 11.3:Uzalishaji wa Mazao ya Mifugo Msimu 2000/01 Hadi 2002/03
Chanzo: Wizara
ya Maji na Maendeleo ya Mifugo 194. Katika mwaka 2003, wakulima 932 walipatiwa mafunzo ya aina mbalimbali yanayohusu kilimo cha umwagiliaji wa zao la mpunga. Aidha, jumla ya wataalamu wa kilimo wapatao 250 wenye astashahada katika fani mbalimbali za kilimo walifadhiliwa kwa masomo ya stashahada. Mabwana shamba 22 kutoka wilaya 10 za Serengeti, Babati, Bunda, Mbinga, Ngara, Mbeya Vijijini, Arumeru, Muheza, Magu na Musoma walipatiwa mafunzo ya Mbinu Shirikishi na Shamba Darasa ili kueneza matumizi ya mbinu hizo. Kazi ya kuboresha mitaala ya uzalishaji mazao na lishe ilikamilika. Mitaala ya mafunzo ya mboga, maua na matunda, matumizi bora ya ardhi na hifadhi ya udongo imefanyiwa marekebisho. Mbinu mbalimbali zilibuniwa na kutumiwa na wataalamu wa ughani katika kufikisha ujumbe sahihi kwa wakulima zikiwa ni pamoja na mbinu shirikishi jamii kwa timu za kata na wilaya husika, vipindi 13 vya ukulima wa kisasa viliandaliwa na kurushwa na Redio Tanzania Dar Es Salaam. Aidha, Gazeti la Mkulima wa Kisasa limechapishwa mara mbili na kusambazwa. Maendeleo
ya utafiti Vyama
vya Ushirika na Masoko Upatikanaji
wa Mikopo kwa Ajili ya Ununuzi wa Mazao na Pembejeo Masoko
na Mazao Jedwali Na.35(UZALISHAJI WA MIWA NA SUKARI NCHINI) Jedwali Na.36( PAMBA ILIYONUNULIWA NA MAUZO NCHINI) Jedwali Na.38(KAHAWA ILIYONUNULIWA NA MAUZO NCHINI) Jedwali Na.39(ENEO LILILOPANDWA MKONGE NA KATANI ILIYOPATIKANA ) Jedwali Na.40(TUMBAKU ILIYONUNULIWA NA MAUZO NCHINI) Jedwali Na.41(MAUA YA PARETO YALIYONUNULIWA NA MAUZO YA BIDHAA ZA PARETO NCHINI) Jedwali Na.42(KOROSHO ZILIZONUNULIWA NA MAUZO NCHINI) Jedwali
Na.43(MUHTASARI WA KIASI CHA MAZAO MUHIMU YA BIASHARA YALIYONUNULIWA) |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||