MAENDELEO YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU KATIKA MAENDELEO |
MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI

MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI
   

Kilimo
Maliasili na Utalii
Madini
Viwanda na Biashara
Ujenzi wa Maendeleo ya Ardhi
Mawasiliano na Uchukuzi
Nishati
Maji
Elimu na Mafunzo
Afya
Maendeleo ya Jamii

         
MADINI
Ukuaji wa Sekta

212. Katika mwaka 2003, sekta ya madini ilikua kwa asilimia 17.0 ikilinganishwa na asilimia 15 mwaka 2002. Ukuaji huo ulitokana na kuongezeka kwa uzalishaji hasa wa dhahabu. Mwaka 2003, mchango wa sekta ya madini katika Pato la Taifa ulikuwa asilimia 2.9 ikilinganishwa na asilimia 2.7 mwaka 2002. Katika mwaka 2003, jumla ya mauzo ya madini nchi za nje yalikuwa ni dola 553.1 milioni ikilinganishwa na dola 471.0 milioni mwaka 2002. Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 17.4

Utafutaji Madini
213. Katika mwaka 2003, jumla ya leseni 299 za utafutaji madini zilitolewa ikilinganishwa na leseni 264 zilizotolewa katika mwaka 2002.

Uchimbaji na Uuzaji wa Madini:

Almasi

214. Thamani ya almasi iliyozalishwa katika mwaka 2003 ilikuwa dola 31.9 milioni ikilinganishwa na dola 28.1 milioni mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 13.5. Sababu ya ongezeko hilo ni kuongezeka kwa kiasi cha almasi kilichouzwa katika soko la nchi za nje. Jumla ya karati 236,382 zilizalishwa katika mwaka 2003 ikilinganishwa na karati 213,491 za almasi zilizozalishwa mwaka 2002.

Dhahabu
215. Kiasi cha dhahabu kilichozalishwa katika mwaka 2003 kilifikia kilo 45,299 ikilinganishwa na kilo 34,065 zilizozalishwa mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 33. Mwaka 2003, thamani ya dhahabu iliyouzwa nchi za nje ilikuwa dola 491.9 milioni ikilinganishwa na dola 396.1 milioni mwaka 2002. Ongezeko hilo la mauzo ya dhahabu nchi za nje ni sawa na asilimia 24. Sababu kubwa ya ongezeko hilo ni kuimarika kwa uchimbaji unaofanywa na makampuni makubwa.

Vito vya Thamani
216. Katika mwaka 2003, jumla ya kilo 1,531,547.1 zilipatikana ikilinganishwa na kilo 113,142 zilizopatikana mwaka 2002. Thamani ya mauzo ya vito vya thamani katika soko la nchi za nje kwa mwaka 2003 ilikuwa dola 19.05 milioni ikilinganishwa na dola 19.8 milioni kwa mwaka 2002. Sababu kubwa ya ongezeko la vito vya thamani lisiloendana na thamani ya mauzo ni kutokana na ukweli kuwa vito vilivyouzwa mwaka 2003 vilikuwa na ubora duni ikilinganishwa na vito vya mwaka 2002. Baadhi ya vito vyenye bei duni vilivyouzwa ni pamoja na quartz, moonstone na feldspar. Madini haya yana uzito mkubwa lakini thamani yake ni ndogo.

Makaa ya Mawe
217. Mwaka 2003, makaa ya mawe yaliyozalishwa na Kampuni ya Makaa ya Mawe Kiwira ilifikia kiasi cha tani 54,610 ikilinganishwa na kiasi cha tani 78,980 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 30.9. Kushuka kwa uzalishaji wa makaa ya mawe kulitokana na uchakavu wa mitambo inayotumika kuchimba makaa hayo.

Jedwali Na.56(UCHIMBAJI WA MADINI: KIASI KILICHOPATIKANA)

Jedwali Na.57(MADINI YALIYOUZWA NCHI ZA NJE 1993 - 2002)

 
Back Top