MAENDELEO
YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI
WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU
KATIKA MAENDELEO | |
|||||||
| MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI | |||||||
Kilimo |
|||||||
MAENDELEO
YA JAMII |
|||||||
Elimu na Mafunzo 285. Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi ambavyo madhumuni yake ni kujenga uwezo wa wanavijiji wa kutambua, kuamua kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo, vilitoa mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi. Mafunzo ya muda mrefu yalitolewa kwa wanakijiji 7,489 ambapo wanaume walikuwa 4,738 na wanawake 2,751. Mafunzo ya muda mfupi yalitolewa kwa wanavijiji 10,007 na kati ya hawa wanawake walikuwa 5,144 na wanaume walikuwa 4,863. Aidha, Mafunzo yalitolewa nje ya vyuo kwa wananchi 4,872 wakiwemo wanaume 2,331 na wanawake 2,541. Jumla ya wananchi 13,263 walipewa mafunzo kuhusu kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa UKIMWI. Kati ya hao wanawake walikuwa 6,215 na wanaume walikuwa 7,048. 286. Vyuo vya Maendeleo ya Jamii hutoa mafunzo katika ngazi ya cheti na stashahada. Wanafunzi 163 kati ya hao 92 wanawake na 71 wanaume walihitimu ngazi ya cheti. Aidha, wanafunzi 60 kati ya hayo 23 wanawake na 37 wanaume walihitimu ngazi ya stashahada. Pia, mitaala minne, mitatu ya stashahada ya juu na mmoja wa ngazi ya Cheti ilichapishwa na kukubalika na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE). Maendeleo
ya Wanawake 288. Mafunzo ya muda mfupi kwa wanawake wa kada mbalimbali yaliendelea kutolewa kwa lengo la kuongeza uwezo wao wa kiutendaji. Baada ya Serikali kukubali kuanzishwa kwa madawati ya jinsia katika wizara na taasisi mbalimbali za umma, mafunzo ya watendaji wapatao 34 yalifanyika, ambapo wizara 20 na Idara 4 zinazojitegemea zilishiriki. Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wapatao 40 walipewa mafunzo kuhusu jinsia. Aidha, watumishi 40 wa Wizara ya Maliasili na Utalii, na Tume ya Ualimu walipewa mafunzo ya namna ya kuingiza maswala ya jinsia katika shughuli mbalimbali. Maendeleo
ya Watoto |
|||||||