MAENDELEO YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU KATIKA MAENDELEO |
MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI

MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI
   

Kilimo
Maliasili na Utalii
Madini
Viwanda na Biashara
Ujenzi wa Maendeleo ya Ardhi
Mawasiliano na Uchukuzi
Nishati
Maji
Elimu na Mafunzo
Afya
Maendeleo ya Jamii

         
MAJI
 
Utangulizi

261. Katika mwaka 2003, Serikali iliendelea kutekeleza Sera ya Maji kwa kupanua wigo wa ushiriki wa jamii katika uandaaji wa miradi ya maji, ujenzi wa miundombinu ya maji, uendeshaji, ukarabati na utunzaji wa miradi ya maji nchini. Aidha, Serikali, iliendelea kutekeleza mikakati mbalimbali inayolenga kuboresha na kuimarisha mfumo wa ukusanyaji wa takwimu na taarifa za maji juu na chini ya ardhi kwenye mabonde yote nchini.

Huduma ya Maji Vijijini
262. Miradi mbalimbali ya maji ilikamilika na mingine kuimarishwa. Katika mwaka 2003, miradi ya maji ya Kilimanjaro Mashariki, Moshi Vijijini na Hai, iliendelea kuimarishwa kwa kueneza huduma kwa wananchi wengi zaidi. Mradi wa maji wa Chalinze ulikamilika Desemba 2003. Pia Miradi ya Hanang’, Manyoni, Singida Vijijini na Igunga ilikamilika pia.

263. Kumekuwepo na ongezeko la usambazaji wa maji vijijini kutoka asilimia 52.8 mwaka 2002 hadi asilimia 53.5 mwaka 2003 kutokana na kukamilika kwa miradi mikubwa ya kitaifa. Baadhi ya miradi hiyo ni ya Wanging'ombe, Handeni, Kiabakari, Makondeko, Maswa, Ntomoko/ Mwisanga, Isaka, Magu na Chalinze. Katika mwaka 2003, kulifanyika ukarabati wa miundombinu katika maeneo ya Dumila, Migoli, Malya, Kiponzelo, Mwamapuli/Bulenya, Uchira, Njombe, Umbwe-Onana, Rombo, Chalinze, Igunga, Hanang', Lushoto, Mugango/Kiabakari, Magu, Iramba, Musoma Vijijini, Manyoni, Nachingwea, Same, Tunduma na Masasi.

264. Hadi kufikia mwaka 2003 bodi 30 za kusimamia mamlaka za maji zimeanzishwa katika wilaya mbalimbali nchini. Pia, kufikia Desemba 2003, jumla ya kamati za maji 8,363 zilianzishwa kukiwepo mifuko ya maji 7,226 yenye jumla ya shilingi bilioni 1.3. Jumla ya mamlaka za aina hii 46 zilizoanzishwa katika wilaya mbalimbali hapa nchini zilikuwa chini ya bodi za wilaya. Katika mwaka 2003, visima vipatavyo 7 vilifanyiwa ukarabati, pia kulifanyika utafiti wa maeneo ya kuchimba visima. Aidha, visima 190 vilichimbwa kwa gharama za watu binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali. Mradi wa Hifadhi ya Mazingira, katika Ziwa Victoria chini ya Kitengo cha Ubora wa Maji na Mfumo wa Ikolojia uliendelea.

Huduma ya Maji Mijini
265. Mapato ya mamlaka za maji mijini yaliongezeka kutoka shilingi 11.7 bilioni mwaka 2001/02 hadi shilingi 13.4 bilioni mwaka 2002/03. Pia, idadi ya wateja katika mamlaka za maji mijini iliongezeka kutoka 127,404 mwaka 2001/02 hadi 137,595 mwaka 2002/03. Aidha, ufungaji wa mita za maji uliongezeka kutoka 64,105 mwaka 2001/02 hadi 84,424 mwaka 2002/03, sawa na ongezeko la asilimia 24. Uzalishaji wa maji uliongezeka kutoka mita za ujazo 276,000 kwa siku mwaka 2001/02 hadi mita za ujazo 279,116 kwa siku mwaka 2002/03.

Jedwali Na.77(IDADI YA MAENEO YALIYOFANYIWA UTAFITI WA MAJI CHINI YA ARDHI KWA MWAKA 2002)

Jedwali Na.79(JUMLA YA VISIMA VILIVYOCHIMBWA NCHINI MWAKA 2000/2001)

Jedwali Na.79A(HALI YA KAMATI ZA MAJI NA MIFUKO YA MAJI VIJIJINI- 2002)

 
       
Back Top