MAENDELEO YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU KATIKA MAENDELEO |
MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI

MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI
 

Kilimo
Maliasili na Utalii
Madini
Viwanda na Biashara
Ujenzi wa Maendeleo ya Ardhi
Mawasiliano na Uchukuzi
Nishati
Maji
Elimu na Mafunzo
Afya
Maendeleo ya Jamii

         
MAWASILIANO NA UCHUKUZI
Ukuaji wa Sekta

239. Katika mwaka 2003, sekta ya mawasiliano na uchukuzi ilikua kwa asilimia 5.1 ikilinganishwa na asilimia 6.4 mwaka 2002. Sababu za kushuka kwa ukuaji wa sekta hii kulitokana na kushuka kwa mchango wa sekta ndogo ya mawasiliano ambako kulitokana na kupungua kwa njia za simu kulikosababishwa na ubadilishaji wa mitambo na kupungua kwa simu zilizounganishwa katika zoezi la kuhakiki na kuweka takwimu sawa za ankara za wateja. Aidha, mchango wa sekta hii katika Pato la Taifa halisi ulikuwa asilimia 5.4 ikilinganishwa na asilimia 5.5 mwaka 2002.

UCHUKUZI

Usafiri wa Barabara

240. Katika mwaka 2003, usafirishaji wa abiria mijini uliendelea kuboreshwa hasa kutokana na kuwepo mazingira ya ushindani. Idadi ya mabasi ya abiria katika jiji la Dar es Salaam iliongezeka hadi mabasi 9,872 mwaka 2003 ikilinganishwa na 5,801 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 70.2. Ongezeko hili kubwa limetokana na mahitaji makubwa ya mabasi katika Jiji la Dar es Salaam. Kwa upande wa miji ya Arusha, Mbeya, Mwanza, Musoma na Morogoro, idadi ya mabasi ilipungua hasa kutokana na ushindani uliokuwepo. Katika miji mingine ya mikoa, mabasi ya abiria yaliendelea kuongezeka. Mchanganuo wa idadi ya mabasi ya abiria mijini ni kama unavyoonyeshwa katika Jedwali Na. 16.1.

Jedwali Na. 16.1:         Idadi ya Mabasi ya Abiria Mijini

Miji

Idadi ya Mabasi

2002

2003

Dodoma

150

153

Arusha

1118

960

Moshi

220

225

Lindi

3

5

Tanga

120

134

Morogoro

312

250

Kibaha (Pwani)

-

-

Dar es salaam

5801

9872

Sumbawanga

-

-

Mtwara

35

49

Songea

52

84

Iringa

97

112

Shinyanga

-

-

Mbeya

355

250

Singida

-

7

Tabora

15

17

Kigoma

66

70

Bukoba

19

25

Mwanza

660

546

Musoma

49

32

Manyara (Babati)

-

-

Jumla -Tanzania Bara

9,072

12,791

 
Usafiri wa Reli

Shirika la Reli Tanzania

241. Shirika la Reli Tanzania lilisafirisha mizigo yenye uzito wa tani 1,442,713 mwaka 2003 ikilinganishwa na tani 1,445,757 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 0.2. Kwa upande wa abiria, Shirika lilisafirisha abiria 683,481 mwaka 2003 ikilinganishwa na abiria 684,796 mwaka 2002 sawa na upungufu wa asilimia 0.2. Aidha, kutokana na huduma zilizotolewa, Shirika limeweza kupata mapato ya shilingi 61.5 bilioni mwaka 2003 ikilinganishwa na shilingi 58.3 bilioni zilizopatikana mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 5.5. Pamoja na kupungua kwa uchukuzi wa mizigo na abiria, mapato ya shirika yaliongezeka kutokana na kupanda kwa bei za usafirishaji. Aidha, katika mwaka 2003, Shirika la Reli Tanzania lilikabiliwa na matatizo ya uchakavu na uhaba wa mabehewa na injini, uchakavu wa njia za mawasiliano, na ajali.
Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA)
242. Katika mwaka 2003, mizigo iliyosafirishwa kupitia Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) ilipungua hadi kufikia tani 613,693 toka tani 677,000 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 9.4. Idadi ya abiria waliosafirishwa katika mwaka 2003 ilishuka kwa asilimia 4.4 kutoka abiria 1,068,287 mwaka 2002 hadi abiria 1,021,384 mwaka 2003. Mamlaka ilipata jumla ya shilingi 26,266 milioni mwaka 2003, ikilinganishwa na shilingi 24,335 milioni mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 7.9. Pamoja na ongezeko la mapato katika mwaka 2003, yalikuwepo matatizo ya uhaba wa fedha za uendeshaji wa shughuli za Mamlaka, uchakavu na uhaba wa vitendea kazi ikiwa ni pamoja na injini na mabehewa.

Usafiri wa Anga
243. Katika mwaka 2003, huduma za usafiri wa anga nchini ziliendelea kutolewa na mashirika kadhaa ya ndege ambayo idadi kubwa humilikiwa na sekta binafsi. Baadhi ya makampuni ya ndege ya ndani ya nchi ambayo yaliendelea kutoa huduma hizo ni pamoja na Air Tanzania Company Limited (ATCL), Precision Air, Wakala wa Ndege za Serikali, Coastal Travel, Regional Air Services, Eagle Air, Air Excel, Flight Link, na Zan Air. Katika mwaka 2003, safari za anga ziliongezeka toka 123,136 mwaka 2002 hadi 153,465 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 24.6. Idadi ya abiria wa ndani na kutoka nje iliongezeka kufikia 1,521,191 mwaka 2003 ikilinganishwa na abiria 1,356,525 mwaka 2002. Kulikuwepo ushindani mkubwa katika usafiri wa anga kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL)
244. ATCL ilitimiza mwaka mmoja tangu ilipoanza shughuli zake mwaka 2002. Jumla ya abiria 149,540 walisafiri kwa ndege za Kampuni mwaka 2003, ikilinganishwa na abiria 134,370 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 11.2. Aidha, kati ya wasafiri hao, 70,342 walikuwa wa safari za nje ya nchi, na 79,198 wa safari za ndani. Kwa upande wa mizigo, jumla ya tani 1,488 za mizigo zilisafirishwa mwaka 2003 ikilinganishwa na tani 2,232.6 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asimilia 33.4. Pamoja na upungufu huo, kulikuwepo na mafanikio katika ukusanyaji wa mapato kwa zaidi ya mara mbili kutoka dola 1.2 milioni mwezi Desemba, 2002 hadi dola 2.8 milioni mwaka 2003. Aidha, mafanikio mengine yaliyopatikana ni pamoja na ongezeko la vituo vya safari kutoka 7 mwaka 2002 hadi 15 mwaka 2003; ongezeko la safari kutoka 28 mwaka 2002 hadi 97 mwaka 2003; ongezeko la kiwango cha ndege kutoka asilimia 5 mwaka 2002 hadi asilimia 90 mwaka 2003; na ongezeko la ndege kutoka moja mwaka 2002 hadi tano mwaka 2003.

Makampuni mengine ya Ndege
245. Katika mwaka 2003, makampuni mengine binafsi ya ndege yalisafirisha nchini abiria 579,107 ikilinganishwa na abiria 475,734 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 21.7. Jedwali 16.2 linaonyesha idadi ya abiria waliosafirishwa na ndege nchini.

Jedwali na. 16.2:         Idadi ya Abiria Waliosafirishwa na Ndege Nchini

Kampuni za Ndege

Idadi ya Abiria Waliosafirishwa

Mwaka 2002

Mwaka 2003

Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL)

134,370

149,540

Precision Air

174,926

248,375

Coastal Travel

64,762

76,856

Regional Air Services

30,241

23,179

Eagle Air,

4,799

Imesimamisha huduma

Air Excel

14,220

Imesimamisha huduma

Flight Link

1,357

413

 Zan Air

30,044

35,372

Makampuni Mengineyo

31,015

45,372

Jumla

475,734

579,107

Chanzo: Wakala wa Usalama wa Anga (TCAA)

Usafiri wa Majini

Uchukuzi wa Baharini
246. Katika mwaka 2003, bandari ya Dar-es-Salaam ilihudumia jumla ya tani 4,861 milioni ikilinganishwa na tani 4,557 milioni katika mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 6.3. Kati ya shehena yote iliyohudumiwa katika bandari ya Dar-es-salaam, tani 1,868 milioni, sawa na asilimia 38.4 ilihudumiwa na Kitengo cha Kontena chini ya mwendeshaji binafsi. Aidha, mwaka 2003, jumla ya meli 4,034 zilihudumiwa ikilinganishwa na meli 3,894 zilizohudumiwa mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 3.6. Kwa upande wa tija mwaka 2003, makontena 22.6 yalihudumiwa kwa saa ikilinganishwa na makontena 20 kwa saa katika mwaka 2002. Pia, muda wa makontena kukaa bandarini uliendelea kushuka toka wastani wa siku 11.6 mwaka 2002 hadi siku 11.3 mwaka 2003.

SINOTASHIP
247. Katika mwaka 2003, meli za kampuni ya SINOTASHIP inayomilikiwa na Serikali za China na Tanzania zilifanya safari 25 ikilinganishwa na safari 41 mwaka 2002. Kupungua kwa safari za meli kumetokana na ukosefu wa mizigo, ushindani mkali uliopo katika biashara ya uchukuzi na hali mbaya ya uzalishaji wa mazao ya biashara iliyosababishwa na ukame. Aidha, kampuni ilisafirisha jumla ya tani 253,241 za shehena mwaka 2003 ikilinganishwa na tani 497,979 mwaka 2002, sawa na pungufu ya asilimia 49.1. Mapato ya kampuni yalipungua toka dola 9.3 milioni mwaka 2002 hadi dola 6.5 milioni mwaka 2003, sawa na pungufu ya asilimia 30.

Usafiri katika Maziwa
248. Huduma za uchukuzi na usafiri katika maziwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa hutolewa na Kampuni inayomilikiwa na Serikali iitwayo Kampuni ya Huduma za Meli pamoja na makampuni binafsi. Kampuni ya Huduma za Meli ina jumla ya meli 15, kumi ziko katika Ziwa Victoria, tatu katika Ziwa Tanganyika na mbili katika Ziwa Nyasa. Meli hizi hutoa huduma za ndani ya nchi na jirani zilizoko katika mwambao wa maziwa hayo. Nchi hizo ni pamoja na Kenya na Uganda katika Ziwa Victoria; Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Zambia katika Ziwa Tanganyika; na Malawi katika Ziwa Nyasa. Mwaka 2003, Kampuni ilisafirisha jumla ya abiria 347,564 ikilinganishwa na abiria 370,588 mwaka 2002, sawa na pungufu ya asimilia 6.2. Kwa upande wa mizigo, Kampuni ilisafirisha jumla ya tani 143,751 mwaka 2003 ikilinganishwa na tani 144,473 mwaka 2002, sawa na pungufu ya asimilia 0.5.

HUDUMA ZA MAWASILIANO

Shirika la Posta
249. Katika mwaka 2003, barua zilipungua kwa asilimia 2.7 kutoka barua 18.7 milioni mwaka 2002 hadi barua 18.2 milioni. Hata hivyo, barua ziendazo nchi za nje ziliongezeka kwa asilimia 4.8 kutoka barua 6.2 milioni mwaka 2002 hadi kufikia barua 6.5 milioni mwaka 2003. Barua za rejesta ziliongezeka kwa asilimia 32.5 kutoka barua 324,204 mwaka 2002 hadi kufikia barua 429,688 mwaka 2003. Pia, barua za rejesta ziendazo nje ya nchi ziliongezeka kwa asilimia 45 kutoka 31,204 mwaka 2002 hadi kufikia 46,218 mwaka 2003. Mwaka 2003, vifurushi vilivyotumwa ndani ya nchi vilipungua kwa asilimia 7.9 kutoka vifurushi 31,969 mwaka 2002 hadi vifurushi 29,422 mwaka 2003. Aidha, vifurushi vilivyotumwa nje ya nchi viliongezeka kwa asilimia 17.5 kutoka vifurushi 5,700 mwaka 2002 hadi kufikia vifurushi 6,699 mwaka 2003.

250. Huduma ya kutuma barua, fedha na ujumbe kwa njia ya EMS, zimeonyesha mafanikio makubwa mwaka 2003. Vitu vilivyotumwa ndani ya nchi kwa njia ya EMS viliongezeka kwa asilimia 18.9 kutoka vitu 260,486 mwaka 2002 hadi vitu 309,736 mwaka 2003. Kwa vilivyotumwa nje ya nchi kwa EMS, kulikuwa na ongezeko la asilimia 49.5 kutoka vitu 19,675 mwaka 2002 hadi kufikia vitu 29,418 mwaka 2003. Utumaji wa fedha kwa njia ya EMS uliongezeka kwa asilimia 14.7 kutoka utumaji 188,790 mwaka 2002 hadi kufikia utumaji 216,700 mwaka 2003. Kwa upande wa ujumbe, kulikuwa na ongezeko la asilimia 41.8 kutoka mara 13,515 mwaka 2002 hadi kufikia 19,164 mwaka 2003. Katika mwaka 2003, Kampuni ya Posta ilipata faida ya jumla ya sh. 14.9 bilioni.

Huduma za Simu
251. Katika mwaka 2003, uwezo wa mitambo ya simu za msingi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) ulipungua kutoa njia 244,381 hadi kufikia 233,352, sawa na punguzo la asilimia 4.7. Hii ilitokana na kuondoa mitambo ya zamani na kuweka mitambo mipya ya kisasa kulingana na mahitaji ya wateja. Pia, idadi ya simu zilizounganishwa zilipungua kutokana na zoezi la kuhakiki na kuweka takwimu sahihi za wateja halali ambalo lilisababisha wateja wasiolipa ankara zao kwa muda mrefu kuondolewa. Zoezi lilikumba wateja wengi na hivyo kusababisha idadi ya simu zilizounganishwa kupungua sana.

252. Idadi ya watumiaji wa simu za mkononi iliongezeka kwa asilimia 61 kutoka simu za mkononi 805,000 mwaka 2002 hadi simu 1,298,000 mwaka 2003. Ongezeko hili limetokana na mahitaji makubwa ya simu za mkononi kwa wateja. Katika mwaka 2003, kampuni za simu za mkononi ziliendelea kuwa ni Celtel, Vodacom, Zantel na Mobitel. Mchanganuo wa ongezeko la wateja wa simu za mkononi ni kama ilivyoainishwa katika jedwali Na. 16.3 hapa chini.

Jedwali Na. 16.3:  Ongezeko la Simu za Mkononi kwa Kampuni

Jina la Kampuni

Idadi ya Wateja

2002

2003

MOBITEL

190,000

210,000

VODACOM

430,000

700,000

ZANTEL

35,000

68,000

CELTEL

150,000

320,000

JUMLA

805,000

1,298,000

Chanzo: Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania

Udhibiti wa shughuli za Mawasiliano
253. Mwaka 2003, Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mawasiliano ilianzishwa kufuatia kuunganishwa kwa Tume ya Mawasiliano Tanzania na Tume ya Utangazaji Tanzania na kupata Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania. Kazi za Mamlaka mpya ni pamoja na kudhibiti makampuni yanayotoa huduma za kusafirisha vifurushi na vipeto na kuboresha, kupanga na kusimamia matumizi ya masafa ya mawasiliano. Mchanganuo wa watoa huduma za aina mbalimbali za mawasiliano ni kama inavyoonyeshwa katika Jedwali No. 16.4.

Jedwali Na.16.4:  Mchanganuo wa Watoa Huduma za Mawasiliano

Watoa Huduma

Idadi ya Watoa Huduma

2002

2003

Simu za Mkononi

4

4

Watoa huduma za kusafiririsha takwimu kwa mtandao wa Tarakishi

14

18

Watoa huduma za mtandao wa Tarakishi

19

21

Posta

15

16

Chanzo: Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania

 

Jedwali Na.67(SHIRIKA LA RELI TANZANIA)

Jedwali Na.68(RELI YA UHURU - TAZARA )

Jedwali Na.69(USAFIRISHAJI KWA MELI: DAR ES SALAAM)

Jedwali Na.70(HUDUMA ZA POSTA)

Jedwali Na.71(HUDUMA ZA SIMU)

Jedwali Na.72(HUDUMA ZA SIMU)

Jedwali Na.73(SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA (ATC)+)

Back Top