MAENDELEO YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU KATIKA MAENDELEO |
MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI

MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI
 

Kilimo
Maliasili na Utalii
Madini
Viwanda na Biashara
Ujenzi wa Maendeleo ya Ardhi
Mawasiliano na Uchukuzi
Nishati
Maji
Elimu na Mafunzo
Afya
Maendeleo ya Jamii

               
UJENZI NA MAENDELEO YA ARDHI
UJENZI

229. Mwaka 2003, sekta ya ujenzi ilikua kwa kiwango sawa na cha mwaka 2002 cha asilimia 11. Ukuaji huu wa wastani umeendelea kuchangiwa na kuwepo kwa shughuli za ujenzi wa majengo yasiyo ya kuishi, ujenzi wa barabara, uendelezaji wa ardhi ukijumuisha ujenzi wa nyumba za kuishi. Aidha, mchango wa sekta hii katika Pato la Taifa halisi ulikuwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 5.0 mwaka 2002.

230. Mwaka 2003, matengenezo ya kawaida ya barabara kuu kilometa 5,644 na madaraja 727 yalikamilishwa ikilinganishwa na kilometa 5,057 na madaraja 320 yaliyokamilishwa mwaka 2002. Kilometa 6,587 na madaraja 907 ya barabara za mikoa zilifanyiwa matengenezo mwaka 2003 ikilinganishwa na kilometa 3,780 na madaraja 180 mwaka 2002. Aidha, mwaka 2003 daraja kubwa la mto Rufiji (Daraja la Mkapa) linalilounganisha mikoa ya Dar es Salaam na ile ya Kusini mwa Tanzania lilikamilika.

231. Mafanikio katika sekta hii mwaka 2003 yametokana na utekelezaji wa mikakati na sera ya ujenzi, inayoweka mkazo katika ushirikishwaji wa sekta binafsi. Aidha, kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara nchini zimeendelea kutekelezwa kwa ufanisi hasa kutokana na kuwepo kwa fedha za mfuko wa barabara na taratibu nzuri za udhibiti wa makandarasi na washauri waelekezi. Kwa ujumla, sera ya ujenzi mwaka 2003 imetoa hamasa kubwa kwa wadau wa sekta hii.

Mtandao wa barabara
232. Mwaka 2003, hali ya mtandao wa barabara kuu na zile za mikoa ni kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali Na. 15.1 hapa chini. Jumla ya kilometa 3,647 za barabara kuu zimekuwa na hali nzuri mwaka 2003 ikilinganishwa na kilometa 3,300 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 10.5. Kwa upande wa barabara za mikoa, jumla ya kilometa 5,483 mwaka 2003 zilikuwa na hali nzuri ikilinganishwa na kilometa 3,725 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 47.2. Aidha, mwaka 2003, jumla ya kilometa 3,717 za barabara kuu zilikuwa na hali ya wastani ikilinganishwa na kilometa 3,900 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 4.7. Kuhusu barabara za mikoa, jumla ya kilometa 6,790 mwaka 2003 zimekuwa na hali ya wastani ikilinganishwa na kilometa 7,475 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 9.2. Kwa upande wa barabara zilizokuwa na hali mbaya, jumla ya kilometa 2,670 za barabara kuu mwaka 2003 zilionekana kuwa na hali mbaya ikilinganishwa na kilometa 2,845 mwaka 2002, sawa upungufu wa asilimia 6.2. Pia, mwaka 2003, jumla ya kilometa 6,093 za barabara za mikoa zilikuwa na hali mbaya ikilinganishwa na kilometa 7,265 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 16.1

 

 

Jedwali Na. 15.1:   Hali ya Mtandao wa Barabara Nchini Mwaka 2003

Aina ya barabara

Uzuri km (%)

Hali ya wastani km(%)

Hali mbaya km (%)

Jumla ya km za aina ya barabara

Barabara Kuu

Lami

Zisizo za Lami

 

1,874 (48%)

1,719 (28%)

 

1,444 (37%)

2,334 (37%)

 

586 (15%)

2,088 (34%)

 

3,904 (100%)

6,141(100%)

Jumla

3,647 (36%)

3,717 (37%)

2,670 (27%)

10,045 (100%)

Barabara za Mikoa

Lami

Zisizo za Lami

 

88 (36%)

5,466 (30%)

 

93 (38%)

6,924 (38%)

 

64 (26%)

5,830 (33%)

 

245 (100%)

18,220 (100%)

Jumla

5,483 (30 %)

6,790 (38%)

6,093 (33%)

18,465 (100%)

 Chanzo: Wizara ya Ujenzi

   
 
Makandarasi

233. Kwa kutambua umuhimu wa umakini katika sekta ya ujenzi mwaka 2003, Bodi inayoshughulikia usajili wa makandarasi ilisajili makandarasi 654 ikilinganishwa na makandarasi 717 mwaka 2002, sawa na upungufu wa asilimia 13. Kwa ujumla, makandarasi 2,911 mwaka 2003 walisajiliwa ikilinganishwa na makandarasi 2,565 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 13. Pamoja na usajili wa makandarasi mwaka 2003, tafiti zilizofanywa zimebainisha kwamba makandarasi wengi wazalendo wako kwenye madaraja madogo madogo. Idadi yao ni zaidi ya asilimia 70 na hawawezi kufanyakazi zenye thamani ya zaidi ya shilingi 50 milioni. Kwa upande wa ujenzi wa barabara, karibu asilimia 90 ya makandarasi wazalendo imebainika kwamba hawawezi kufanya kazi yenye thamani ya shilingi 300 milioni, kiwango ambacho ni wastani wa kujenga kilometa moja ya barabara ya lami.

Uratibu wa Kazi za Makandarasi
234. Katika kutekeleza kazi zake za udhibiti wa sekta, Bodi ya usajili wa Makandarasi ilikagua jumla ya miradi ya ujenzi 675 ikilinganishwa na miradi 308 iliyokaguliwa mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 119.2. Ongezeko kubwa hilo limetokana na kuwepo kwa miradi mingi ya ujenzi nchini. Kwa ujumla, zaidi ya asilimia 50 ya miradi ya ujenzi iliyokaguliwa imeonyesha kwamba makandarasi wengi wanafuata taratibu za ujenzi. Aidha, katika zoezi hilo la ukaguzi wa miradi mwaka 2003, Bodi ya Usajili wa Makandarasi iliwafutia usajili makandarasi 120 ikilinganishwa na makandarasi 115 mwaka 2002. Jumla ya makandarasi 1,435 walifutiwa usajili wao tangu mwaka 1998.

   
     

Jedwali Na 15.2:  Makandarasi Waliosajiliwa kwa Taaluma za Madaraja Mbalimbali 2003

 

 

Madaraja

 

Jumla

I

II

III

IV

V

VI

VII

Majengo

7

2

-

4

29

33

172

243

Majenzi

6

1

3

5

34

54

157

260

Umeme

-

-

1

2

8

6

60

77

Mitambo

-

-

-

-

3

1

8

12

Fani maalum

10

4

35

-

-

-

-

50

Wa muda

12

-

-

-

-

-

-

12

Jumla

35

7

39

11

74

94

397

654

 Chanzo : Wizara ya Ujenzi

     
   

MAENDELEO YA ARDHI

235. Katika mwaka 2003, Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 ilifanyiwa marekebisho katika vifungu vya 37,125 na 142 kwa lengo la kumwezesha mmiliki wa ardhi kuweza kuitumia kama dhamana ya kupata mikopo kutoka katika mabenki na taasisi za fedha kwa urahisi na ufanisi. Aidha, upimaji wa mashamba katika vijiji 6 vya mfano wilaya ya Mbozi mkoa wa Mbeya ulifanyika.

236. Katika kuendeleza Sera ya Taifa ya Makazi ya mwaka 2000, Mpango wa Kimkakati wa mji wa Tunduma na Rasimu za Hali ya mazingira ya miji ya Lushoto na Masasi ziliandaliwa. Pia utaratibu wa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba kwa watumishi wa Serikali na Rasimu ya Mpango wa Taifa wa Kuendeleza Nyumba (National Housing Programme) zilikamilishwa. Shirika la Nyumba la Taifa lilijenga nyumba 218 katika mikoa ya Dar es salaam, Mwanza (Isamilo) na Arusha (Kijenge). Ukaguzi na uendelezaji wa makazi katika mikoa ya Tabora, Kigoma, Rukwa, Mwanza, Mara na Ruvuma kwa lengo la kutambua maeneo yaliyokuwa tayari kuendelezwa kimji, maeneo ya wazi ya kuhifadhi na uendelezaji wa maeneo kongwe katika miji ya Iringa, Morogoro na Mtwara ulifanyika. Aidha, upimaji kwa kutumia “Global Positioning System” na utayarishaji wa ramani kwa kutumia mashine za kisasa (digital system) ulitumika katika kutayarisha ramani 205 katika uwiano mbalimbali na kupiga picha za anga kwa ajili ya kuandaa ramani katika miji 38 kanda ya Ziwa. Kama inavyoonyeshwa katika Jedwali Na. 15.3. Katika kipindi cha mwaka 2003, Mradi wa Kupima viwanja katika jiji la Dar es salaam uliendelea ambapo viwanja 26,723 vilipimwa katika sehemu za Tuangoma, Kisota, Mbweni, Buyuni, Mbweni JKT, Bunju, Mwanagati na Mivumoni kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali Na. 15.4.

237. Katika mwaka 2003, hati za kumiliki ardhi 1,037 zilisajiliwa ikilinganishwa na hati 2,976 mwaka 2002. Nyaraka 5,571 zilisajiliwa katika mwaka 2003 ikilinganishwa na nyaraka 4,856 mwaka 2002 kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali Na. 15.5. Ili kutambua viwanja vilivyopimwa na kubaini wamiliki wake, kitengo cha Mfumo wa Mtandao wa Taifa kiliwezesha kutambuliwa viwanja 51,000 katika Jiji la Dar es Salaam na jumla ya hati 86,770 za wamiliki wa viwanja kwa nchi nzima. Aidha, katika kutatua migogoro ya ardhi, jumla ya kesi 134 za ardhi zilifunguliwa katika Mabaraza ya Ardhi mikoani na Baraza la Rufaa la Ardhi ambapo kesi 61 ziliamuliwa. Pia, kesi 678 zilifunguliwa katika Mabaraza ya Nyumba ya Mikoa na katika Baraza la Rufaa la Nyumba na kesi 959 ambazo zilifunguliwa na zilizokuwa zinaendelea ziliamuliwa.

238. Katika kuongeza kasi ya uwekezaji nchini, mfumo wa Hazina ya Ardhi (Land Bank) ulianzishwa. Mfumo huu una lengo la kuainisha sehemu zinazofaa kwa uwekezaji nchini. Jumla ya vipande vya ardhi 743 vyenye ukubwa wa hekta milioni 2.6 vimebainishwa kwa ajili ya kuingizwa kwenye Hazina ya Ardhi.

Jedwali Na. 15.3:         Orodha ya Miji Iliyopigwa Picha za Anga

Mkoa

Wilaya

         Mji

Mwanza

Magu

1. Magu

2. Kisesa

3. Nyanguge/Lugeye

4. Nassa

Kwimba

1. Ngudu

2. Misasi

3. Malya

4. Sumve/Mantare

Missungwi

1. Misungwi

2. Bukumbi

3. Usagara

Shinyanga

Shinyanga

1. Shinyanga

2. Malampaka

Kahama

1. Isaka

Bukombe

1. Ushirombo/Bukombe

Meatu

1. Mwanhuzi

Maswa

2. Maswa/Nyalikungu

Kishapu

1. Kishapu/Mhunze

Mara

Bunda

1. Bunda

Musoma

1. Musoma

2. Butiama

Serengeti

1. Mugumu

Tarime

1. Tarime

2. Sirari

3. Shirati

Kagera

Bukoba

1. Kamachumu

2. Nshamba

3. Kyaka

Muleba

1. Muleba

Biharamulo

1. Biharamulo

2. Chato

Ngara

1. Ngara

2. Rusumo

Karagwe

1. Kayanga

2. Kaisho

3. Bugene

4.Rulenge

5. Murongo

Idadi ya Miji

38

Jedwali Na.15.4:  Viwanja Vilivyopimwa Katika Maeneo ya Jiji la Dar Es Salaam

Eneo

Makazi/Biashara

Huduma

Jumla

Tuangoma

3,187

147

3,334

Kisota

1,276

58

1,334

Mbweni /Mpiji

3,327

124

3,451

Buyuni

7,245

325

7,570

Mbweni JKT

1,073

45

1,118

Mtoni Kijichi

1,728

48

1,776

Bunju

4,298

240

4,538

Mwanagati

1,917

73

1,990

Mivumoni

1,532

80

1,612

Jumla

25,583

1,140

26,723

 Jedwali Na.15.5:    Nyaraka Mbalimbali Zilizosajiliwa Chini ya Sheria ya Usajili wa Hati, Sura Na. 334

Aina ya Hati

Mwaka 2002

Mwaka 2003

Tofauti (%)

Nyumba zilizouzwa

507

759

49.7

Mkataba wa Upangishaji wa nyumba

46

53

15.17

Miliki zilizowekwa rehani

374

307

-17.9

Rehani zilizomaliza deni

379

336

-11.3

Nyaraka za kuwekesha Hati

45

43

-4.4

Nyaraka za kuwekesha Hati zilizoondolewa

65

73

12.3

Surrender and Revocation

167

226

35.3

Uhamishaji wa miliki unaotokana na Bunge au sheria mbalimbali

153

296

93.5

Hati nyinginezo

411

325

-20.9

Nyaraka za tahadhari na Vizuizi

192

169

-11.9

Upekuzi wa Daftari la Hati

2517

2984

18.5

JUMLA

4,856

5,571

28.4

 

 
Back Top