MAENDELEO
YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI
WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU
KATIKA MAENDELEO | |
|||||||||
| MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI | |||||||||
Kilimo |
|||||||||
MALIASILI
NA UTALII |
|||||||||
Ukuaji
wa sekta
199. Sekta ya maliasili inajumuisha sekta ndogo za misitu na nyuki, uvuvi, na wanyamapori. Sekta ndogo ya misitu na wanyamapori ilikua kwa asilimia 4.2 ikilinganishwa na asilimia 3.0 mwaka 2002 na sekta ndogo ya uvuvi ilikua kwa asilimia 6.4 ikilinganishwa na asilimia 6.5 mwaka 2002. Kuongezeka kwa kiwango cha ukuaji katika sekta ndogo ya misitu na wanyamapori kulitokana na kukua kwa biashara ya wanyamapori pamoja na mazao yake katika soko la nje, uzuiaji wa biashara haramu ya wanyamapori hai na mazao yake na uhamasishaji wananchi katika uhifadhi wa wanyamapori na mazingira yake. Aidha, kushuka kwa kiwango cha ukuaji katika sekta ndogo ya uvuvi kulitokana na ukosefu wa mitaji kwa wavuvi wadogo, mbinu na teknolojia duni katika utunzaji na usindikaji wa mazao ya uvuvi pamoja na matumizi ya zana haramu katika uvuvi ambazo zinaharibu mazingira ya viumbe wa majini. Misitu
na Nyuki Uvunaji
na Uuzaji wa Mazao ya Misitu na Nyuki Wanyamapori 203. Katika kupambana na ujangili dhidi ya rasilimali ya wanyamapori na mazingira yao, doria ziliendelea kuwekwa ndani na nje ya hifadhi ambapo idadi ya kesi za ujangili ziliongezeka hadi 780 ikilinganishwa na kesi 520 mwaka 2002. Hadi Desemba 2003, kesi 102 zilimalizika na majangili 180 kufungwa jela. Aidha, doria za upelelezi na ukaguzi wa wafanyabiashara ya nyara ziliendeshwa ambapo nyara zenye thamani ya shilingi 188,092,536 zilikamatwa ikilinganishwa na nyara zenye thamani ya shilingi 219,785,118 zilizokamatwa mwaka 2002. Nyara zilizokamatwa ni pamoja na meno ya tembo 80 na vipande 140 vya meno ya tembo, meno ya kiboko 218, ndege hai 166, wadudu 300, wanyama 33 na kobe 44. 204. Katika mwaka 2003, waombaji 388 walipewa leseni za nyara ikilinganishwa na waombaji 278 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 28.3. Ada za leseni hizo ziliingizia Serikali mapato ya shilingi 131,398,445. Vile vile, mapato kutokana na biashara ya nyara na viumbe hai yameongezeka kwa shilingi 56,969,412 sawa na ongezeko la asilimia 77 ikilinganishwa na shilingi 74,429,033 zilizopatikana mwaka 2002. Ongezeko hili linatokana na wafanyabiashara wengi kutumia ‘quota’ zao kikamilifu. Ushirikishwaji wa sekta binafsi na wananchi katika shughuli za ufugaji wanyamapori ziliendelea kuimarika ambapo jumla ya kobe 2,816 walisafirishwa nchi za nje na kuwapatia wafugaji kiasi cha shilingi 56,320,000. 205. Katika mwaka 2003 kulikuwepo na vitalu 142, ikilinganishwa na vitalu 131 mwaka 2002, sawa na ongezeko la asilimia 7.7. Biashara ya uwindaji wa kitalii ililiingizia Taifa mapato ya dola 8.8 milioni ikilinganishwa na mapato ya dola 9.3 milioni ya mwaka 2002, mapato haya yameonyesha upungufu wa dola 0.5 milioni sawa na upungufu wa asilimia 5.04. Upungufu huu ulitokana na watalii wengi kukatisha safari zao kufuatia kuzuka kwa vita vya Iraq, mlipuko wa homa ya mapafu (SARS) na homa ya kuku (Bird flu). Uvuvi 207. Mapato ya mazao ya uvuvi katika soko la nje yalipanda kutoka karibu shilingi 99,294,249 mwaka 2002 hadi shilingi 132,502,001,939 katika mwaka 2003, ikiwa ni ongezeko la shilingi 33,207,752,036. Majedwali Na. 16, 17 na 18 yanaonyesha biashara na mapato yatokanayo na mauzo ya mazao ya uvuvi. Ili kuimarisha utekelezaji wa sera ya uvuvi, mwaka 2003 Sheria Na. 6 ya uvuvi ya mwaka 1970 ilirekebishwa na sheria na. 22 ya mwaka 2003 ilitungwa. Azma ya marekebisho haya ni kuhakikisha kuwa jamii inayojishughulisha na uvuvi inazingatia kanuni na taratibu zilizopo. 208. Katika hatua ya kudhibiti uvuvi haramu, doria 26 zilifanyika katika maeneo ya ukanda wa pwani na ukanda wa uchumi wa bahari ikilinganishwa na doria 135 mwaka 2002. Jumla ya wahalifu 9 na meli 3 zilikamatwa. Mafanikio hayo yalipatikana kwa kupitia mradi wa uthibiti na ufuatiliaji wa shughuli za uvuvi kwa kutumia meli ya chuo cha uvuvi Mbegani na kutumia ndege. Aidha, kanuni za uvuvi katika Ziwa Victoria zimeainishwa na zile za Kenya na Uganda ili kwa pamoja nchi zinazomiliki ziwa hili ziweze kukabiliana na uvuvi haramu. Utalii 210. Vivutio vipya vilivyoko sehemu mbalimbali nchini vilitathiminiwa ili kuhakikisha kwamba barabara zinazoelekea kwenye vivutio na hoteli zinapitika muda wote. Barabara kuu ya utalii kutoka Makuyuni hadi Ngorongoro yenye urefu wa km 77 ilijengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, utangazaji wa vivutio vya utalii ndani na nje ya nchi ulifanyika kwa kutumia usambazaji wa majarida, vipeperushi, mabango, Digital Video Disc (DVD) kwenye balozi zetu na sehemu mbalimbali za maonyesho mwaka 2003. Vile vile, katika kuitangaza kauli mbiu inayotumika ya “Afrika Halisi ni Tanzania”, tovuti ya utalii ilianzishwa (www.tourismtanzania.go.tz). Utalii
wa Mambo ya Kale Jedwali Na.45(UPANDAJI WA MITI (MICHE ILIYOOTESHWA)) Jedwali Na.47(MAUZO YA BIDHAA ZA MISITU NCHI ZA NJE) Jedwali Na.48(MWENENDO WA BIASHARA YA NDEGE, WANYAMAPORI NA VIPUSA NCHI ZA NJE) Jedwali Na.48A(MWENENDO WA BIASHARA YA WANYAMA HAI NA UWINDAJI WA KITALII) Jedwali Na.48B(IDADI YA WAWINDAJI (TOURIST HUNTERS)) Jedwali Na.49(MAUZO YA WANYAMA HAI NA PEMBE NCHI ZA NJE) Jedwali Na.50(UZALISHAJI KATIKA SEKTA YA UVUVI 1993-2000) Jedwali Na.51(MAUZO YA MAZAO YA UVUVI NCHI ZA NJE (2000-2002)) Jedwali Na.51A(MUHTASARI WA MAUZO YA MAZAO YA UVUVI NCHI ZA NJE - 1996-2002) Jedwali Na.51B(MWELEKEO WA MAUZO YA SANGARA NJE YA NCHI -1996-2002) Jedwali Na.52(IDADI YA WATALII, SIKU ZAO HOTELINI NA MAKADIRIO YA FEDHA ZA KIGENI ZILIZOPATIKANA) Jedwali Na.53(IDADI YA WATALII WALIOINGIA NCHINI NA KIASI CHA FEDHA ZILIZOPATIKANA (1990-2002)) Jedwali Na.54(SAFARI KATIKA HIFADHI ZA TAIFA) Jedwali
Na.55(NAFASI KATIKA HOTELI NA MATUMIZI YAKE+) |
|||||||||