|
Utangulizi
157. Katika mwaka 2003, serikali iliendelea
na juhudi za kupambana na umaskini nchini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
wa ndani na nje ya nchi. Wiki ya Umaskini iliyofanyika Oktoba mwaka 2003
ilitoa fursa kwa wadau kuweza kujadili kwa kina utekelezaji wa Mkakati
wa Kupunguza Umaskini nchini na hatua zilizofikiwa. Aidha, katika Wiki
ya Umaskini ulifanyika uzinduzi wa kufanya mapitio Mkakati wa Kupunguza
Umaskini. Hii inatokana na serikali kujiwekea malengo ya kila baada ya
miaka mitatu kupitia upya Mkakati huu. Taarifa ya utekelezaji wa Mkakati
ya mwaka 2002/03 ilihitimisha awamu ya kwanza ya miaka mitatu.
Mapitio
ya Mkakati wa Kupunguza Umaskini
158. Utekelezaji wa Mkakati wa Kupunguza Umaskini nchini ulifikia katika
mwaka wa tatu na wa mwisho katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wake.
Kulikuwepo na mafanikio katika utekelezaji wa Mkakati wa kwanza nchini
hasa katika sekta zilizopewa kipaumbele, hususan elimu, afya, barabara
vijijini, na maji. Pia, kulikuwepo na mafanikio katika maeneo ya masuala
ya uchumi jumla na katika mageuzi kwenye sekta mbalimbali zikijumuisha
sekta za fedha, utumishi wa umma na serikali za mitaa. Majadiliano kuhusu
mapitio ya Mkakati wa Kupunguza Umaskini yalianza katika ngazi za wadau
mbalimbali ikijumuisha serikali, mashirika yasio ya kiserikali, vikundi
vya hiari, asasi za dini na binafsi. Madhumuni ya kufanya mapitio ya Mkakati
huu ni kubaini mafanikio katika utekelezaji; matatizo yaliyojitokeza;
na mapungufu yanayoweza kuwepo kwa lengo la kuuboresha na kuharakisha
utekelezaji wa awamu ijayo ya Mkakati. Katika kufanya mapitio ya Mkakati,
mkazo umewekwa katika kupanua zaidi ushirikishwaji na umiliki wa mchakato.
Ufuatiliaji
na Tathmini ya Umaskini
159. Mfumo wa Kufuatilia umaskini nchini uliendelea kama ulivyobainishwa
katika Mpango Kamambe wa Ufuatiliaji kupitia vikundi vya Sensa na Uchunguzi;
Utafiti na Uchambuzi; Takwimu za Kiutawala; na Usambazaji Taarifa, Uhamasishaji
na Uelimishaji. Mafanikio ya mfumo huu katika mwaka 2003 ni pamoja na
kuchapisha Taarifa ya Umaskini na Maendeleo ya Watu ya mwaka 2003, Taarifa
ya Utekelezaji wa Mkakati wa Kupunguza Umaskini ya mwaka 2002/03; Usambazaji
wa matokeo ya Tafiti ya Mapato na Matumizi ya Kaya-2000/01 na matokeo
ya jumla ya Sensa ya Watu na Makazi 2003; na kufanyika kwa Wiki ya Umaskini
nchini mwezi Oktoba 2003. Aidha, mfumo huu umewezesha kufanyika kwa utafiti
shirikishi wa kutathimini umaskini nchini uliokusanya maoni ya wananchi
katika sehemu na hali ya maisha mbalimbali ya jamii kuhusu masuala ya
umaskini. Pia, warsha mbalimbali za kikanda zilifanyika kwa ajili ya kupata
takwimu za kiutawala.
Hali
ya Utekelezaji wa Mkakati wa Kupunguza Umaskini Katika Sekta za Kipaumbele
160. Katika mwaka 2002/03, serikali iliendelea kuelekeza sehemu kubwa
ya rasilimali kwenye sekta zilizobainishwa katika kupunguza umaskini kwa
lengo la kukuza maendeleo ya rasilimali watu; utoaji wa huduma za msingi
za kijamii; kuimarisha miundombinu ya kiuchumi na kuongeza uzalishaji
katika kilimo na kuhakikisha upatikanaji wa chakula.
Maendeleo
ya Rasilimali Watu
161. Katika mwaka 2002/03, serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
iliendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi uliokuwa
na malengo ya kupanua uandikishwaji wa watoto ; kuongeza ubora wa elimu
; kujenga uwezo ; kuboresha na kuimarisha utawala na mpangilio wa kiasasi.
Mafanikio katika mwaka 2003 yanaoneshwa katika jedwali lifuatalo. Katika
mwaka 2002/03, serikali ikishirikiana na wadau wengine wa sekta hii iliandaa
awamu ya pili ya Mkakati wa Sekta ya Afya unaolenga kutekeleza malengo
muhimu ya Mkakati wa Kupunguza Umaskini. Aidha, serikali katika uendelezaji
wa sekta ilianzisha mkakati wa Kitaifa wa kupambana na UKIMWI; kufanya
marekebisho katika Sera ya Afya ya mwaka 1990; na kuongeza chanjo za surua
hadi kufikia asilimia 89. Katika mwaka 2002/03, usambazaji wa maji vijijini
uliongezeka kutoka asilimia 52.8 mwaka 2002 hadi asilimia 53.5 mwaka 2003.
Aidha, katika kipindi hicho upatikanaji maji sehemu za mijini ulibakia
asilimia 73 kama ilivyokuwa mwaka 2002 wakati ambapo huduma ya maji taka
iliongezeka kwa asilimia 10 mwaka 2002 hadi asilimia 17 Juni 2003.
Jedwali: 9.1 Baadhi ya Viashirio Katika Sekta ya Elimu
|
Viashiria
|
Kipimo
|
2002
|
2003
|
|
Utambuzi
wa shule(school mapping)
|
Wilaya
|
82
|
98
|
|
Kiwango
cha Jumla ya uandikishaji
|
Asilimia
|
100.4
|
105.3
|
|
Kiwango
halisi cha Uandikishaji - miaka (7-13)
|
Asilimia
|
80.7
|
88.5
|
|
Walimu
mafunzoni
|
Idadi
|
9728
|
15285
|
|
Uandikishwaji
shule za sekondari
|
Idadi
|
323,318
|
345,411
|
|
Uwiano
wa uandikishaji kijinsia
|
Uwiano
|
1:0.87
|
1:0.93
|
|
Waliokatisha
masomo
|
Asilimia
|
6.6
|
4.7
|
Chanzo:
Wizara ya Elimu na utamaduni
Kilimo
162. Katika mwaka 2002/03, kipaumbele kilikuwa katika kuimarisha uwezo
wa kuzalisha kwa wakulima wadogo na wafugaji pamoja na kuweka mazingira
mwafaka ya kisheria yanayolenga katika kusukuma uwekezaji wa sekta binafsi.
Mambo yaliyotekelezwa ni pamoja na marekebisho ya kodi na kufutwa kwa
kodi ambazo zinaleta kero; kuongezeka kwa kilimo cha umwagiliaji; kupatiwa
mafunzo kwa wataalam wa ughani 6,688 na mabwana na shamba wa vijiji
1,130.
Barabara
163. Katika mwaka 2002/03, serikali iliendelea kutenga kiasi cha sh.
1.84 bilioni kila mwezi kwa ajili ya kuimarisha barabara zinazounganisha
mikoa mbalimbali kwa kufanya matengenezo ya kiwango cha lami sehemu
zilizo kwenye barabara ya Ukanda wa Kusini ambazo ni Dar es Salaam-Lindi-Mingoyo
na Ukanda wa Kati ambayo ni Dar es Salaam-Dodoma-Singida. Aidha, mpango
wa ukarabati wa haraka ulianzishwa kwa ajili ya maendeleo ya barabara
za wilayani, mijini na zile za vijijini zinazoingia barabara kuu. Jumla
ya kilometa 7,049 sawa na asilimia 51.4 kati ya kilometa 13,727 za barabara
vijijini zilifanyiwa matengenezo.
Jedwali Na. 9.2:
Matumizi ya
Serikali Kuu Katika
Sekta za Kipaumbele, Mwaka 1998/99 – 2003/04
Sh.bilioni
|
|
1998/99
|
1999/00
|
2000/01
|
2001/02
|
2002/03
|
2003/04
|
|
Halisi
|
Halisi
|
Halisi
|
Halisi
|
Halisi
|
Matarajio
|
|
Jumla ya Matumizi
|
338.9
|
414.3
|
499.6
|
753.8
|
953.7.0
|
1124
|
Elimu
|
164.9
|
218.0
|
254.9
|
344.9
|
436.2
|
502.3
|
|
Afya
|
72.5
|
81.2
|
100.7
|
142.1
|
186.7
|
197.3
|
|
Maji
|
14.4
|
14.5
|
18.3
|
32.5
|
51.9
|
64.4
|
|
Kilimo
|
14.9
|
21.6
|
19.1
|
31.9
|
60.2
|
93.1
|
|
Barabara
|
66.7
|
70.8
|
92.5
|
179.6
|
190.2
|
213
|
|
Mahakama
|
5.5
|
8.3
|
9.2
|
18.8
|
23.8
|
32.7
|
|
TACAIDS
|
0.0
|
0.0
|
0.0
|
4.0
|
5.3
|
21.2
|
|
Matumizi ya Kawaida
|
233.0
|
282.0
|
347.5
|
490.2
|
720.1
|
836.8
|
Elimu
|
117.6
|
158.9
|
189.2
|
282.1
|
422.9
|
471.1
|
|
Afya
|
50.7
|
53.9
|
70.3
|
90.9
|
149.1
|
177.6
|
|
Maji
|
7.1
|
5.4
|
8.1
|
15.5
|
16.5
|
17.5
|
|
Kilimo
|
8.6
|
13.7
|
10.3
|
17.2
|
36.0
|
47.7
|
|
Barabara
|
43.9
|
42.
|
60.7
|
65.7
|
71.9
|
84.5
|
|
Mahakama
|
5.
|
7.9
|
8.8
|
14.8
|
18.9
|
24.9
|
|
TACAIDS
|
0.0
|
0.0
|
0.0
|
4.0
|
4.5
|
8.1
|
|
Matumizi ya Maendeleo
|
105.9
|
132.4
|
147.1
|
263.5
|
248.3
|
293.3
|
|
Elimu
|
47.3
|
59.1
|
65.7
|
62.8
|
13.3
|
31.3
|
|
Afya
|
21.9
|
27.3
|
30.4
|
51.2
|
37.6
|
19.6
|
|
Maji
|
7.3
|
9.1
|
10.1
|
17.0
|
35.4
|
46.9
|
|
Kilimo
|
6.3
|
7.9
|
8.7
|
14.7
|
24.2
|
45.4
|
|
Barabara
|
22.8
|
28.6
|
31.7
|
113.9
|
118.3
|
128.5
|
|
Mahakama
|
0.3
|
0.4
|
0.4
|
4.0
|
4.2
|
7.8
|
|
TACAIDS
|
0.0
|
0.0
|
0.0
|
0.0
|
0.8
|
13.2
|
Chanzo: Wizara ya Fedha
|
|