MAENDELEO YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU KATIKA MAENDELEO |
MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI

UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI

Uendelezaji wa Sekta Binafsi
Masuala Maalum Yanayohusu Sekta Zote
Maendeleo ya Juhudi za Kupambana na Umasikini

   
MASUALA MAALUM YANAYOHUSU SEKTA ZOTE
UTAWALA BORA

142. Katika mwaka 2003, serikali kwa kushirikiana na wadau wengine iliendelea kutekeleza programu mbalimbali ikiwa ni pamoja na Mkakati wa Taifa wa Kupambana na Rushwa kwa lengo la kuboresha na kuimarisha utendaji katika Serikali. Wizara, Idara zinazojitegemea na Wakala ziliendesha warsha kwa watumishi wao kwa lengo la kujenga uelewa kuhusu tatizo la rushwa katika sekta zao. Serikali ilitenga sh. 80 milioni kwa ajili ya kuziwezesha Wizara, Idara na Wakala kutekeleza shughuli za Mkakati wa Taifa wa Kupambana na Rushwa. Kitengo cha Kuratibu Masuala ya Utawala Bora kiliendelea kuandaa taarifa za utekelezaji kila robo mwaka na kuzisambaza kwa wadau wa vita dhidi ya rushwa. Aidha, Serikali iliendelea kuchukua hatua za kisheria, kiutawala na kinidhamu kwa waliobainika kuhusika na vitendo vya rushwa.

143. Juhudi za serikali zilielekezwa katika kuimarisha uwezo wa wananchi kuzidisha mapambano dhidi ya rushwa. Wananchi walielimishwa na kuhamasishwa juu ya haki zao, mbinu za kutambua na kukabiliana na vitendo vya rushwa, mbinu za kutoa taarifa za rushwa kwenye vyombo vya dola na namna ya kujikinga dhidi ya athari zinazotokana na kuwaumbua wala rushwa. Katika kutekeleza azma hiyo, Taasisi ya Kuzuia Rushwa iliandaa na kurusha hewani jumla ya vipindi 224. Vipindi vilirushwa hewani na Radio Tanzania, Radio Maria ya Songea, Radio Kuizera ya Ngara, Radio Chemichemi ya Sumbawanga, Radio Faraja ya Shinyanga na Radio Sauti ya Injili Moshi. Pia, vikundi 34 vya sanaa vilihamasishwa kuelimisha umma kuhusu madhara ya rushwa.

144. Katika kuhakikisha serikali inasimamia utekelezaji wa maadili ya Viongozi wa Umma kwa mujibu wa Sheria ya Maadili na Miiko, Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliendelea kupokea, kuchambua na kuhakiki taarifa ya mali na madeni ya viongozi zinazotolewa kwenye hati rasmi ya kutolea tamko. Aidha, Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi imeanzisha ofisi za kanda ili kusogeza huduma zinazotolewa na Sekretarieti karibu zaidi na wananchi.

Jinsia
145. Katika mwaka 2003, serikali iliendelea na uchambuzi wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2002, kwa kuzingatia kwa undani zaidi masuala ya kijinsia. Takwimu zilizochambuliwa zinaonyesha kuwa asilimia 48 ya wakuu wa kaya ni wanawake. Katika takwimu hizo uchambuzi unaonyesha kuwa kati ya watoto wanaoongoza kaya walio chini ya umri wa miaka 18, asilimia 82 ni wanawake.

146. Katika mwaka 2003, serikali ilitoa mafunzo ya awali kwa maafisa 30 walioteuliwa katika vitengo vinavyoshughulikia masuala ya jinsia katika taasisi za umma kuhusu majukumu yao na mbinu mbalimbali za kuwawezesha kushughulikia masuala ya jinsia katika maeneo yao. Vilevile, sera ya wanawake ilifanyiwa mapitio na kutafsiriwa katika lugha rahisi. Zaidi ya nakala 50,000 zilichapishwa na kusambazwa kwa wadau katika ngazi mbalimbali, kwa lengo la kuhamasisha na kuelimisha umuhimu wa kuzingatia masuala ya jinsia katika nyanja zote za uchumi na kijamii.

147. Katika kuendeleza azma ya kuleta usawa wa kijinsia nchini, serikali iliendelea kuongeza nafasi za ajira na kuwapa madaraka wanawake ambapo katika mwaka 2003 kwa upande wa utumishi wa ngazi ya kati, jumla ya watumishi 211 waliajiriwa na kati ya hao 63 sawa na asilimia 29.9 walikuwa wanawake. Kati ya watumishi 234 waliothibitishwa kazini wanawake walikuwa 71 sawa na asilimia 30.34. Jumla ya watumishi 8,060 walipandishwa vyeo, kati ya hao 2,434 walikuwa ni wanawake sawa na asilimia 30.2. Takwimu za utumishi wa ngazi ya juu zinaonyesha kuwa watumishi 105 waliteuliwa katika nyadhifa mbalimbali, kati ya hao 25 walikuwa ni wanawake, sawa na asilimia 23.81 ikilinganishwa na wanawake 17 sawa na asilimia 19.54 ya walioteuliwa mwaka 2002. Mwaka 2003 waliopandishwa vyeo walikuwa 267, kati ya hao 58 walikuwa wanawake, sawa na asilimia 21.72. Aidha, mwaka 2003, wanawake 61 walithibitishwa kazini katika nyadhifa mbalimbali; idadi hii ni sawa na asilimia 21.86 ya watumishi 218 waliothibitishwa ikilinganishwa na wanawake 36, sawa na asilimia 15.13 ya watumishi 238 waliothibitishwa kazini mwaka 2002.

 Jedwali Na. 8.1: Idadi ya Watu Walioajiriwa na Kupandishwa Vyeo Katika Ngazi ya Kati na Ngazi ya Juu, 2002 - 2003

 

 

 

Ngazi ya kati

2002

2003

Idadi

Mahusiano kijinsia Ke/Jumla

Idadi

Mahusiano kijinsia Ke/Jumla

 

Jumla

 

Wanaume

 

Wanawake

 

Jumla

 

Wanaume

 

Wanawake

Ajira

 

 

 

 

211

148

63

29.86

Walithibitishwa

 

 

 

 

234

163

71

30.34

Walipata vyeo

105

49

56

53.85

8060

5626

2434

30.20

Jumla

105

49

56

53.83

8505

5937

2568

30.19

Ngazi ya juu

 

 

 

 

 

 

 

 

Uteuzi

87

70

17

19.54

105

80

25

23.81

Waliopandishwa vyeo

370

309

61

16.49

267

209

58

21.72

Waliothibitishwa

238

202

36

15.13

279

218

61

21.86

Jumla

695

581

114

16.40

651

507

144

22.12

Chanzo: Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma

148. Katika mwaka 2003, mradi wa mafunzo wa kuongeza ujuzi na uwezo wa watumishi wanawake serikalini ulidhamini jumla ya watumishi wanawake 20 katika fani mbalimbali za shahada ya uzamili ikilinganishwa na wanawake 17 mwaka 2002, ikiwa ni ongezeko la asilimia 17.7 Vilevile, wanawake 40 walidhaminiwa katika kozi za tarakishi ikilinganishwa na wanawake 26 waliodhaminiwa mwaka 2002. Aidha, katika mwaka 2003 serikali ilitayarisha taarifa ya utekelezaji wa mikakati na mipango mbalimbali ya kuleta usawa wa jinsia nchini kulingana na maazimio ya mpango wa utekelezaji wa Beijing pamoja na Mkutano Mkuu wa Tatu wa Baraza la Umoja wa Mataifa. Katika taarifa hiyo takwimu nyingi za kisekta pamoja na kiutawala zilibainishwa kijinsia ambapo taarifa kuhusu uwakilishi wa wanawake katika ngazi za utoaji maamuzi zilionyesha kuwa kuna ongezeko la asilimia 5.6 tu la wawakilishi wa wanawake katika ngazi zote. Kwa kiasi kikubwa ongezeko hilo limetokana na ongezeko la nafasi za uwakilishi kwenye ngazi za wakurugenzi wa wilaya, makamishina, wakurugenzi, wakurugenzi wasaidizi pamoja na majaji.

 Jedwali Na. 8.2:Idadi ya Wawakilishi Katika Ngazi za Maamuzi Kuanzia Mwaka 1997 - 2003

Ngazi

1997

2003

 

Jumla

Wanaume

Wanawake

Asilimia

Jumla

Wanaume

Wanawake

Asilimia

Mawaziri

27

24

3

11.11

27

23

4

14.81

Naibu Mawaziri

16

13

3

18.75

17

12

5

29.41

Wakuu wa Mikoa

20

19

1

5

21

19

2

9.52

Makatibu wakuu

21

17

4

19.05

30

23

7

23.33

Makamishina

-

-

-

 

19

16

3

15.79

Makatibu wa Tawala wa Mikoa

17

17

-

0

20

16

4

20

Wakuu wa Wilaya

99

79

20

20.20

109

86

23

21.10

Makatibu Tawala wa Wilaya

109

89

20

18.35

99

85

14

14.14

Wakurugenzi Wilaya

-

-

-

 

114

94

20

17.54

Wakurugenzi

-

-

-

 

119

89

30

25.21

Wakurugenzi Wasaidizi

-

-

-

 

153

118

35

22.88

Mabalozi

30

29

1

3.33

35

34

1

2.86

Majaji

36

33

3

8.33

49

42

7

14.29

Mahakimu

-

-

-

 

115

82

33

28.70

JUMLA

375

320

55

14.67

927

739

188

20.28

Ongezeko la wawakilishi wanawake kutoka mwaka 1997 hadi 2003 ni asilimia 5.61

Chanzo:            Taarifa ya utekelezaji wa mazimio ya Beijing kupitia Beijing Platform of Action

 MAZINGIRA

149. Katika mwaka 2003, Serikali iliandaa mafunzo kwa ajili ya kuhamasisha serikali za mitaa kuhusu utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Mazingira kwa kuhusisha halmashauri za miji na wilaya 45. Vilevile, wananchi na viongozi walishirikishwa katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika tarehe 5 Juni 2003, ambapo wizara, asasi na mikoa mbalimbali ziliwakilisha shughuli zao.

150. Tanzania iliendelea kutekeleza mikataba ya kimataifa inayohusu mazingira, ikiwa ni pamoja na ‘Agenda ya 21’ kuhusu maendeleo endelevu. Tanzania iliridhia mikataba mbalimbali ikiwemo mkataba wa Rotterdam unaohusu uthibiti wa biashara ya kimataifa ya baadhi ya kemikali hatari na madawa ya kuulia wadudu waharibifu; Itifaki ya Montreal kuhusu kemikali zinazoharibu ukanda wa ozoni angani; Itifaki ya Kyoto inayohusu kupunguza uzalishaji wa gesi zanazosababisha mabadiliko ya tabianchi; Mkataba wa Basel unaohusu uthibiti wa taka zenye sumu baina ya nchi na nchi; Itifaki ya Cartagena inayohusu bioteknolojia salama kwa matumizi ya binadamu na mazingira; na Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Kuenea kwa Hali ya Jangwa na Ukame. Aidha, taasisi zisizo za kiserikali zipatazo 7 zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya kuenea kwa jangwa na ukame katika mikoa ya Mtwara, Morogoro, Dodoma, Shinyanga, Kagera na Rukwa zimepatiwa fedha chini ya utaratibu wa NAP-IFAD; na ushirikishwaji wa wananchi katika kuhifadhi mazingira uliimarishwa ikiwa ni pamoja na kutekeleza Kampeni ya Taifa ya Upandaji wa Miti. Miti ipatayo 47,863,257 ilipandwa ikilinganishwa na miti 82,671,132 iliyopandwa mwaka 2002

151. Programu ya Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria iliendelea kutekelezwa kwa ushirikiano na taasisi na wadau mbalimbali. Dira ya Bonde la Ziwa Victoria ya miaka 10-15 iliandaliwa na kuwasilishwa kwenye Sekretariati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Vilevile, mkataba wa ushirikiano wa hifadhi na uendelezaji wa mazingira ya ziwa Tanganyika ulikamilishwa na kuwekwa sahihi na Tanzania, Burundi, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na Zambia.

152. Katika mwaka 2003, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) liliendelea kutekeleza shughuli mbalimbali za kuhifadhi mazingira ikiwa ni pamoja na kuaandaa mikakati ya kusimamia utoaji wa elimu ya mazingira nchini. Aidha, Baraza, kwa kushirikiana na wananchi na wadau wengine, liliboresha matumizi endelevu ya maeneo ya pwani ambapo wananchi na wadau wengine walipata ujuzi, elimu na utaalamu wa kuhifadhi maeneo ya Pwani, na kuandaa mipango ya matumizi endelevu ya rasilimali zilizoko katika maeneo chepechepe katika ukanda wa ziwa Victoria na Bonde la Kihansi. Vilevile, Baraza lilifanya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) kwa zaidi ya miradi 24 ya maendeleo katika sekta za madini, ujenzi wa barabara, kilimo, uvuvi, nishati na mawasiliano; na lilishirikiana na wadau mbalimbali katika kubainisha, kutangaza na kuendeleza teknologia sahihi za hifadhi ya mazingira.

UKIMWI

153. Ugonjwa wa UKIMWI ni janga kubwa la Taifa. Idadi ya watu waliogunduliwa kuwa na UKIMWI iliongezeka katika mwaka 2002 hadi kufikia watu 157,17 kutoka watu 144,498 mwaka 2001, sawa na ongezeko la watu 12,675 au asilimia 8.8. Wengi wa walioambukizwa ni wale ambao wako katika umri wa kati ya miaka 20 na 49, wengi wao wakiwa katika umri kati ya miaka 25-34 kwa wanawake na miaka 30-39 kwa wanaume. Kundi hili ndilo ambalo ni la nguvu kazi. Vijana chini ya miaka 20 wengi wao wameambukizwa au wako katika hatari ya kuambukizwa UKIMWI. Ili kukabiliana na janga hili, katika mwaka 2003 serikali iliendelea kutoa elimu ya afya kwa jamii hususan juu ya namna ya kuepuka kuambukizwa, na pia kuhimiza malezi katika vituo vya afya na majumbani kwa wagonjwa ili kuondokana na unyanyapaa.

154. Serikali imechukua hatua mbalimbali katika harakati za kupambana na ugonjwa huu. Hatua hizo zinajumuisha kuendelea kutekelezwa kwa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI unaozishirikisha sekta zote. Mpango umekuwa ukitoa umuhimu mkubwa katika tiba na mafunzo kwa wagonjwa wa UKIMWI; ushauri na upimaji kwa hiari; usalama wa damu; kutambua na kutibu magonjwa ya zinaa; kufuatilia mwenendo wa ugonjwa wa UKIMWI; kutoa elimu ya afya kuhusu UKIMWI; kufanya utafiti kuhusu UKIMWI; kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto; ukiandaa mwongozo wa matibabu kwa watoaji wa huduma za afya kwa waishio na UKIMWI; ukihamasisha viongozi katika ngazi mbalimbali, wanafunzi na wananchi kwa jumla ili kubadili tabia na mienendo potofu; na kusambaza kondom za kike na kiume katika mikoa yote nchini kama njia mojawapo ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI na magonjwa mengine ya zinaa. Mpango huu unatekelezwa katika ngazi mbalimbali, kuanzia ngazi ya taifa, mikoa hadi wilaya.

155. Tume ya Kudhibiti UKIMWI ambayo ni chombo chenye jukumu la kuratibu shughuli za UKIMWI nchini iliandaa Sera ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI mwaka 2001. Katika kutekeleza sera hii, tume iliandaa mkakati wa kudhibiti UKIMWI kutoka mwaka 2003 hadi mwaka 2007. Mkakati unaelezea na kutoa miongozo ya namna ya kutekeleza sera ya kudhibiti UKIMWI. Aidha kamati za kiufundi za masuala ya UKIMWI katika wizara ziliundwa. Kamati hizi zinawajibika kuratibu shughuli zote za UKIMWI katika wizara husika. Utafiti kuhusiana na madhara ya UKIMWI katika wizara ni moja ya maelekezo yaliyotolewa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI. Wizara zinatakiwa kufanya utafiti na kisha kuandaa mkakati wa wizara wa kudhibiti UKIMWI kwa kuzingatia hali ya halisi ya wizara, kama utafiti ulivyoonyesha.

156. Majedwali namba 8.1 na 8.2 yanaonyesha watu walioambukizwa na kiwango cha ongezeko na wanaombukizwa katika kipindi cha miaka 20 iliyopita kuanzia 1983 had 2002. Idadi ya waathirika nchini ni kubwa kuliko ile iliyotolewa taarifa. Hii inaonyesha wazi kwamba UKIMWI bado ni tatizo sana katika Taifa letu. Kwa kuzingatia taarifa za Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI, mmoja tu kati ya waathirika watano ndiye anayetoa taarifa. Kulingana na takwimu zilitolewa na Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI, mikoa yenye kiasi kikubwa cha waathirika wa UKIMWI ni Mbeya, ikifuatiwa na Dar es Salaam. Mkoa wenye kiasi kidogo ni Mara. Jedwali Namba 8.3 linaonyesha matukio ya maambukizi kulingana na umri na jinsia.


 

Jedwali Na. 8.3: Idadi  ya Walioambukizwa Waliotolewa Taarifa 1983 - 2001

Mkoa

Miaka

 

1983

1984

1985

1986

 1987

1988

 1989

 1990

 1991

 1992

Arusha

0

0

0

10

47

217

433

647

1,117

1,637

Coast

0

0

1

4

79

224

465

938

1,676

2,215

Dar es Salaam

0

0

51

471

1,470

3,093

5,209

7,246

8,834

9,259

Dodoma

0

0

0

7

47

105

262

310

536

762

Iringa

0

0

1

3

68

305

374

728

2,281

3,334

Kagera

3

106

322

847

1,666

2,143

2,576

3,472

4,742

5,813

Kigoma

      0

0

0

3

68

305

374

728

2,281

3,334

Kilimanjaro

0

1

8

36

207

455

571

966

2,060

3,707

Lindi

0

0

0

1

10

46

113

484

842

1,211

Mara

0

0

0

3

30

99

141

280

639

980

Mbeya

0

0

0

16

208

751

1,077

3,890

6,924

9,890

Morogoro

0

0

0

11

88

254

354

637

2,398

3,598

Mtwara

0

0

1

5

26

90

199

479

1,361

1,968

Mwanza

0

0

15

54

171

448

667

1,303

3,041

4,207

Rukwa

0

0

0

1

5

98

94

140

261

496

Ruvuma

0

0

0

20

46

81

210

571

1,197

1,807

Shinyanga

0

0

0

8

31

144

238

583

1,278

496

Singida

0

0

0

6

74

197

284

456

763

1,807

Tabora

0

2

5

6

59

232

525

927

1,400

1,972

Tanga

0

0

2

13

80

210

210

838

1,914

2,636

Mahali pasipojulikana

-

-

-

-

-

-

-

1

1

1

TANZANIA

3

109

404

1,525

4,462

9,301

14,256

25,503

44,195

59,352

...........Jedwali linaendelea ukurasa unaofuata

Mkoa

 

Miaka

  1993

1994

1995

1996

1997

1998

1999

2000

2001

2002

Arusha

2,185

2,368

2,615

2,787

3,244

3,367

3,948

4,196

4,688

4785

Coast

2,740

3,023

3,268

3,559

3,796

4,266

4,375

5,348

5,580

5737

D’salaam

10,406

11,050

11,302

12,983

13,899

14,517

14,643

16,053

18,627

24501

Dodoma

1,028

1,294

1,608

1,938

2,517

2,641

2,748

2,941

3,170

3565

Iringa

4,462

4,674

4,785

4,883

5,008

5,031

5,076

5,179

5,298

5318

Kagera

6,646

7,064

7,223

7,426

7,671

7,881

8,310

8,529

8,976

9072

Kigoma

1,920

2,070

2,257

2,280

2,426

2,481

2,613

2,732

2,815

2860

Kilimanjaro

4,699

5,119

5,513

5,991

6,618

7,375

7,766

8,088

9,097

10042

Lindi

1,691

1,966

2,173

2,480

2,712

3,074

3,559

4,155

4,710

5008

Mara

1,304

1,393

1,486

1,486

1,486

1,515

1,634

2,021

2,229

2345

Mbeya

11,439

12,214

12,371

14,685

16,835

19,949

23,688

26,952

30,320

31172

Morogoro

4,328

4,575

4,903

5,189

5,438

5,534

5,863

6,388

6,820

7073

Mtwara

2,090

2,201

2,267

2,444

2,569

2,843

3,000

3,262

3,638

3886

Mwanza

5,349

5,731

5,974

6,365

7,006

7,384

7,884

8,338

8,752

9194

Rukwa

715

777

801

882

1,227

1,359

1,621

1,997

2,382

2706

Ruvuma

2,480

2,847

3,087

3,345

3,752

4,260

4,760

5,406

6,381

7080

Shinyanga

2,624

3,062

3,361

3,824

4,217

4,515

4,861

5,440

6,310

7174

Singida

1,472

1,688

1,908

2,135

2,167

2,262

2,329

2,396

2,692

2872

Tabora

2,786

3,075

3,428

3,805

4,278

4,733

5,199

5,946

6,349

6810

Tanga

3,207

3,475

3,793

4,062

4,278

4,632

4,792

4,975

5,620

5819

Manyara

 

 

 

 

 

 

 

 

 

110

Mahali pasipojulikana

 

1

 

2

 

44

 

44

 

44

 

44

 

44

 

44

 

         44

 

44

 

Jumla

73,572

79,668

84,167

92,593

101,188

109,863

118,713

130,386

144,498

157173

Chanzo: Wizara ya Afya – NACP Surveillance Report No. 17

Jedwali Na. 8.4:   Matukio na Viwango vya Maambukizo kwa Mikoa Nchini

 

Mkoa

Matukio mwaka 2000

Kiwango cha matukio mwaka  2000

Matukio mwaka 2001

Kiwango cha matukio mwaka  2001

Matukio  mwaka 2002

Kiwango cha matukio mwaka 2002

Idadi ya watu mwaka 2002

Arusha

248

12.2

492

23.6

97

7.5

1292973

Pwani

973

117.4

232

27.2

157

17.7

889154

Dar es Salaam

1,410

63.1

2,574

112.1

5874

235.2

2497940

Dodoma

193

11.7

229

13.5

395

23.3

1698996

Iringa

103

6.2

119

7.0

20

1.3

1495333

Kagera

219

11.7

447

23.3

96

4.7

2033888

Kigoma

119

10.1

83

6.8

45

2.7

1679109

Kilimanjaro

322

16.3

1,009

49.7

945

68.4

1381149

Lindi

596

71.6

555

64.9

298

37.7

791306

Mara

387

28.6

208

14.9

116

8.5

1368602

Mbeya

3264

155.6

3,368

156.1

852

41.2

2070046

Morogoro

525

30.7

432

24.6

253

14.8

1759809

Mtwara

262

24.1

376

33.7

248

21.9

1128523

Mwanza

454

17.8

414

15.8

442

15.0

2942148

Rukwa

376

34.5

385

34.4

324

28.4

1141743

Ruvuma