MAENDELEO
YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI
WA SEKTA BINAFSI | SUALA MAALUMU KATIKA MAENDELEO | |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| SUALA MAALUM KATIKA MAENDELEO | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
MFUMO
WA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO
2025 NA MKAKATI WA KUPUNGUZA UMASKINI |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
UTANGULIZI
164. Serikali ya Tanzania imeweka sera, mipango na programu mbalimbali zinazolenga kuimarisha ukuaji wa uchumi na kuinua hali ya maisha ya Watanzania. Mifumo mbalimbali ya ufuatiliaji iliwekwa kwa ajili ya kufuatilia mabadiliko, na kutathmini mafanikio na mambo yanayokwamisha utekelezaji. Hata hivyo, imebainika kuwa mfumo wa ufuatiliaji nchini hautoshelezi matarajio kwa vile bado haujazingatia ushiriki wa sekta zote. Kila sekta ina mfumo wake wa ufuatiliaji bila kuwa na uhusiano na sekta nyingine. Hivyo, panahitajika utaratibu utakaowezesha kuratibu mifumo mbalimbali ya ufuatiliaji iliyopo. Lengo kuu la mada hii ni kubainisha mwelekeo wa mfumo thabiti wa ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa mipango na programu za maendeleo inayozingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na Mkakati wa Kupunguza Umaskini. Maana
ya Ufuatiliaji na Tathmini Katika Muktadha wa Maendeleo 166. Tathmini ya utekelezaji wa mipango/programu inajaribu kueleza mabadiliko katika maisha na ustawi wa walengwa. Tathmini inalinganisha hali iliyokuwepo kabla ya mpango/programu na baada ya utekelezaji, na inachambua matokeo mazuri na mabaya ya mabadiliko. Mara kwa mara, tathmini inachangia katika kufanya maamuzi ya kusimamisha shughuli fulani za mpango/programu au kuongeza shughuli nyingine. Katika mchakato wa kutathmini, hali zilizo nje ya mipango/programu ambazo zinaweza kuathiri shughuli za kuleta matokeo fulani katika hali za walengwa, pia zinaangaliwa. MUHTASARI WA MAPITIO YA MCHAKATO WA UFUATILIAJI NA TATHMINI NCHINI Mfumo
wa Ufuatiliaji na Tathmini Kabla ya Mwaka 1995 168. Mpango wa kwanza wa maendeleo wa miaka mitano ambao ulizinduliwa mwaka 1964 ulikuwa ni awamu ya kwanza katika utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa muda mrefu wa miaka kumi na tano. Ili kufikia madhumuni na malengo yaliyokuwa katika mpango wa muda mrefu ililazimika kukusanya nguvu za sekta zote kwa njia ya taratibu zilizohitajika na kwa makusudi kabisa ili kuendeleza viwango vikubwa vya ukuaji wa uchumi. Mchakato huu ulitumia mapitio ya katikati ya kipindi cha mpango ambayo yalibaini masuala ya kisera na kiutekelezaji yaliyohitaji kuangaliwa kwa makini zaidi katika kipindi cha mpango kilichosalia. 169. Mpangilio wa kiasasi kwa ajili ya utekelezaji na ufuatiliaji wa mpango wa miaka mitano uligawanywa katika utaratibu ufuatao; Wizara ya Uchumi na Mipango ya Maendeleo (sasa Ofisi ya Rais, Mipango na Ubinafsishaji) ilikuwa ndiyo yenye jukumu la jumla la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa mipango. Ili kusaidia juhudi za kuleta maendeleo katika ngazi za mikoa, wilaya na vijiji, kamati za maendeleo ziliundwa ili kusaidia kazi na kutoa urahisi wa mawasiliano kati ya ngazi mbalimbali za utawala. Mchoro ufuatao unaonyesha mfumo uliokuwepo.
Mfumo wa
Ufuatiliaji wa Mipango na Utekelezaji:
Mpangilio wa Kiasasi katika Miaka ya Sitini na Sabini
170. Pamoja na kuwepo kwa mfumo bayana wa ufuatiliaji wa mipango na programu, kulikuwepo na vikwazo vifuatavyo: kwanza, majukumu ya kila mtendaji hayakueleweka vizuri; pili, kulikuwepo na tatizo la uhaba wa wafanyakazi katika mazingira ya kazi nyingi, tatu, kutokana na kutokuwa na vitengo vya mipango katika baadhi ya wizara, Wizara ya Uchumi na Mipango ya Maendeleo haikuwa inapokea taarifa za miradi katika wakati unaotabirika, matokeo yake ilikuwa kwa kiasi kikubwa si rahisi kuchukua hatua za kuondoa vikwazo vya utekelezaji. Mapitio ya Mchakato wa Ufuatiliaji na Tathmini Baada ya Mwaka 1995 Muhtasari
wa Utekelezaji wa Sera za Uchumi Jumla na Uhusiano Wake na Mchakato wa
Ufuatiliaji na Tathmini tangu mwaka 1995 Mwenendo wa
Baadhi ya Viashirio vya Uchumi Jumla Mwaka 1996 - 2003
Chanzo; Ofisi ya Rais, Mipango na Ubinafsishaji
MCHAKATO WA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA MKAKATI WA KUPUNGUZA UMASKINI NA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2025 172. Mchakato wa ufuatiliaji na tathmini nchini una ngazi tatu ambazo ni wizara kuu, wizara za kisekta, na mikoa na serikali za mitaa. Katika kila ngazi, kuna viashirio muhimu vya ufuatiliaji na tathmini ambavyo vinaendana na vigezo na maana zilizowekwa katika ngazi ya wizara kuu ili kusaidia kuoanisha utaratibu katika ngazi zote. Katika ngazi ya serikali kuu, kuna programu mbalimbali ambazo serikali inatekeleza. Baadhi ya programu hizo zina utaratibu bayana uliowekwa wa kupima mafanikio dhidi ya shabaha. Yafuatayo ni mapitio ya mifumo ya ufuatiliaji, na tathmini kuhusu Mkakati wa Kupunguza Umaskini; Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; na Bajeti. Mkakati
wa Kupunguza Umaskini na Mfumo Wake wa Ufuatiliaji 174. Mfumo huu umeendelea kutekelezwa kama iilivyobainishwa katika Mpango Kamambe wa Ufuatiliaji mwenendo wa hali ya umaskini chini ya vikundi vya kitaalam vilivyoainishwa ndani ya mfumo huo. Njia zinazotumika ili kuhakikisha mchakato unafanyakazi vizuri ni utayarishaji na usambazaji wa taarifa mbalimbali, kama vile taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa Mkakati wa Kupunguza Umaskini; Taarifa ya Hali ya Umaskini na Maendeleo ya Watu; na usambazaji wa taarifa za tafiti na chunguzi mbali mbali. Taarifa hizi zinatoa na kuonyesha wazi mwenendo wa viashirio vinavyopimika na hufichua picha halisi juu ya kutekelezeka au kutotekelezeka kwa shabaha za Mkakati zilizowekwa, na kuona kama hatua za kurekebisha hali iliyojitokeza zitahitajika. Mambo muhimu katika mfumo wa ufuatiliaji wa mwenendo wa hali ya umaskini ni pamoja na ufafanuzi wa taarifa zinazotakiwa; taratibu za kiasasi; njia za ukusanyaji wa takwimu na taarifa za kitakwimu ; vipaumbele vya utafiti, usambazaji wa taarifa; na kuongeza uwezo wa utendaji. 175. Tatizo kubwa katika mfumo huu ni pamoja na kutopatiwa fedha kwa wakati kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli za mfumo, na uhaba wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ipasavyo. Changamoto inayojitokeza ni jinsi ya kuhuisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za mfumo zinazoshabihiana. Aidha, kumejitokeza haja ya kuzingatia shughuli ambazo zinatekelezwa na sekta binafsi pamoja na kuimarisha uratibu wa mfumo na kuhakikisha ufuatiliaji wa mara kwa mara ili kuuwezesha mfumo kufanya kazi zake vizuri zaidi. Dira
ya Maendeleo ya Taifa 2025 177. Katika mchakato wa kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa, Mpango wa Muda wa Kati wa kipindi cha miaka mitatu umebainishwa kama nyenzo muhimu ya utekelezaji. Ingawa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji katika Mpango wa Muda wa Kati haujaanza kutumika lakini ni muhimu kuwa na njia thabiti na sahihi za kufanya ufuatiliaji wa mabadiliko yanayotokea katika vipindi husika. 178. Ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mpango wa Muda wa Kati umeweka viashirio vyenye kupimika ambavyo vitatumika katika mchakato wote. Kuna viashirio vya vipindi vya muda mrefu, muda wa kati na muda mfupi. Njia zitakazotumika katika mchakato ni pamoja na ukaguzi wa programu na miradi inayoendelea; ukaguzi kwa vipindi vya mara kwa mara wa programu, miradi na shughuli; kuchunguza kwa makini taarifa za utekelezaji halisi wa miradi na matumizi ya fedha na taarifa za mapitio ya mwaka, nusu mwaka, robo mwaka na mwezi. Kwa mfano, Kitabu cha Hali ya Uchumi kinachotayarishwa na serikali ni moja kati ya taarifa za mwaka ambazo zinaonyesha mapitio ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa mwaka uliopita. Vile vile, kutakuwepo na mpangilio wa kiasasi ambao unajaribu kuunganisha watendaji wote katika mchakato. Asasi zitakazoratibu mchakato huu zitakuwa zile zilizopewa dhamana ya kusimamia uchumi na mipango ya maendeleo; na fedha. Asasi mbili hizi zitafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na wizara za kisekta pamoja na sekta binafsi. Umuhimu
wa Bajeti Katika Ufuatiliaji wa Mipango/Programu Mapitio
ya Matumizi ya Serikali
181. Kimsingi, Mapitio ya Matumizi ya Serikali yana malengo muhimu mawili ambayo ni kusaidia mchakato wa kuandaa bajeti na usimamizi wa bajeti, na kutoa mrejeshonyuma kwa serikali na wadau wengine kuhusu matumizi ya serikali na masuala ya usimamizi kupitia kwa wafanya tathmini wa nje ya serikali. Mfumo
wa Matumizi wa Muda wa Kati 183. Uanzishwaji wa mchakato wa bajeti huanza kwa kuandaa rasimu ya mwongozo wa bajeti. Mwongozo wa bajeti kimsingi ndio chombo kikuu kinachotumiwa na serikali kushinikiza mkakati wa udhibiti wa mgawanyo wa rasilimali kwa kipindi cha Mfumo wa Matumizi wa Muda wa Kati. Mwongozo unatoa kwa kifupi sera na malengo ya mikakati kwa mwaka unaofuata. Kwa kuzingatia madhumuni ya sera na uhaba wa rasilimali kwa ujumla, kikomo cha juu cha bajeti huwa kinawekwa. Kikomo hicho kinakuwa kama kiashirio cha ufuatiliaji. 184. Ugumu wa kufuatilia bajeti ya maendeleo unatokana na uwezo mdogo wa kukagua utekelezaji halisi wa miradi na kupima mafanikio katika kufikia malengo kabla na baada ya utekelezaji wa mradi. Pia, hakuna utaratibu wa kufanya mapitio ya kina, baada ya mradi kukamilika, ya miradi yote iliyokamilika, na inayoendelea ili kuweza kupata uelewa utakaoongeza ubora wa mradi. Tathmini inayofanyika baada ya mradi kukamilika inakuwa na manufaa zaidi iwapo itatanguliwa na tathmini, kabla ya kuanza miradi, inayobainisha malengo na gharama tarajiwa. Hii inawezesha pia kuweka msingi sahihi wa kuorodhesha kwa umuhimu wake miradi itakayoingizwa katika bajeti ya maendeleo 185. Tatizo la miaka mingi katika kupanga bajeti na taratibu za kuidhinisha matumizi ni jinsi ya kudhibiti upotevu wa fedha unaotokana na kujirudia kwa matumizi kutokana na kuingiliana kwa shughuli zinazofanana lakini zinafanywa na watekekelezaji tofauti. Kwa sasa takwimu za fedha za serikali ndizo zinazotumika kama utaratibu wa ufuatiliaji katika suala hili. Hii inawezesha kupunguza kujirudia matumizi katika vitu vinavyofanana ambavyo vinajitokeza katika programu tofauti au katika bajeti zote - ya maendeleo na ya kawaida. Mapendekezo
ya Mwelekeo wa Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini Hitimisho. 188. Mipango mingi ya serikali kuu ina mifumo ya ufuatiliaji na tathmini lakini haijionyeshi dhahiri. Ukiachilia mbali Mkakati wa Kupunguza Umaskini ambao una mfumo madhubuti wa ufuatiliaji, mipango mingine ya serikali kuu haijabainisha waziwazi taratibu na viashirio vya ufuatiliaji. Taarifa na takwimu za ufuatiliaji huwa zinatolewa kwa baadhi ya programu na kila moja ikilenga kutimiza lengo la programu husika. Hata hivyo, kuna haja ya kuwa na mfumo rasmi wa kuunganisha mifumo ya utoaji takwimu na taarifa za ufuatiliaji na tathmini kwa programu zote za serikali kuu, katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na Mkakati wa Kupunguza Umaskini. | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||