MAENDELEO YA UCHUMI JUMLA | UENDELEZAJI WA SEKTA BINAFSI | MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
| MAENDELEO KATIKA SEKTA MBALIMBALI | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Kilimo |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Utangulizi 257. Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa miaka ya karibuni imekuwa chombo muhimu katika uchumi na maendeleo ya nchi. Mchango wa sekta hii katika mwenendo wa uchumi unaendelea kukua. Mwaka 2003, serikali iliandaa Sera ya Habari na Teknolojia ili kuhakikisha kuwa teknolojia hiyo inatumika ipasavyo katika kusaidia kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Matumizi ya Teknolojia ya Mawasiliano na Habari yameboresha utendaji kazi katika wizara, mikoa, idara na wakala mbalimbali wa serikali pamoja na sekta binafsi. Usajili wa Kampuni za Mtandao 258. Hadi Desemba 2004, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ilikuwa imesajili kampuni 23 za mtandao. Kati ya hizo, 15 zilikuwa zinatoa huduma za mtandao na kampuni 8 zilipata usajili lakini zilikuwa bado hazitoi huduma hizo. Baadhi ya kampuni hizo ni pamoja na Simba Net, TTCL, University Computing Centre, Raha.com. Kampuni hizo zinatoa huduma za tovuti katika mikoa, wizara, idara na wakala mbalimbali wa serikali. Mwaka 2004, jumla ya tovuti 113 zilisajiliwa ikilinganishwa na tovuti 98 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 16.3. Hii ilitokana na kuongezeka kwa watumiaji nchini. Jedwali Na. 16.1: Idadi ya Vituo vya Tovuti na Huduma za Mitandao Zilizosajiliwa 2000-2004
Chanzo: Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Radio na Televisheni 259. Hadi mwanzoni mwa miaka ya tisini, Tanzania Bara ilikuwa na radio moja tu ambayo ni Radio Tanzania Dar-es-Salaam. Mwaka 1993, Bunge la Tanzania lilipitisha sheria ya kuruhusu vyombo binafsi kuingia katika shughuli za habari. Kupitishwa kwa sheria hiyo kulitoa fursa kwa sekta binafsi kuanzisha vituo vya radio na televisheni. Mwaka 1994, kituo cha kwanza binafsi cha radio na televisheni kilianzishwa na kuanza kurusha matangazo yake hewani. Fursa hii ya kuruhusu sekta binafsi kutoa huduma ya habari na utangazaji ilileta changamoto ya kuanzishwa kwa vituo vingi zaidi vyenye ushindani wa kimaendeleo. Hadi kufikia mwaka 2004, jumla ya vituo 33 vya radio vilisajiliwa. Kati ya hivyo, 2 vinamilikiwa na serikali na 31 sekta binafsi. Vituo vya televisheni vilifikia 15 ambapo kimoja kinamilikiwa na serikali na 14 vinamilikiwa na sekta binafsi. Radio 260. Mwaka 2004, idadi ya vituo vya redio iliongezeka hadi 33 kutoka 29 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 14.0. Vituo vya mitambo ya kurushia matangazo viliongezeka kutoka vituo 59 mwaka 2003 hadi 63 mwaka 2004, sawa na ongezeko la asilimia 6.7. Kasi ya ukuaji huu ilitokana na kuongezeka kwa mahitaji na idadi ya watumiaji wa vyombo hivi kupata habari za matukio na masuala mbalimbali ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na burudani. Vile vile, kukua kwa teknolojia ya habari na mawasiliano kumechangia kuongezeka huko. Jedwali Na. 16.2 linaonyesha idadi ya vituo vya radio na television vilivyosajiliwa mwaka 1994 – 2004. Jedwali Na. 16.2: Vituo vya Radio na Televisheni vilivyosajiliwa kuanzia mwaka 1994 – 2004
Televisheni 261. Hadi mwaka 2002, idadi ya vituo vya televisheni vilivyokuwa vimesajiliwa nchini vilifikia 15, idadi ambayo haikubadilika hadi mwaka 2004. Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya kupata taarifa mbalimbali kupitia televisheni, baadhi ya Miji na Halmashauri za wilaya zilianzisha vituo vya televisheni ambavyo hurusha bure matangazo ya vituo vingine, hivyo kuwawezesha watumiaji kupata huduma hiyo kwa urahisi zaidi. Hadi mwaka 2004, vituo hivi vilifikia 16, kama inavyoonyeshwa katika Jedwali Na. 16.3. Aidha, vituo mbalimbali vilitoa huduma kwa malipo yanayowawezesha wananchi kupata matangazo ya vituo vya televisheni kwa kuwaunganisha watumiaji na matangazo ya vituo mbalimbali. Hadi mwaka 2004, vituo hivyo vilifikia 16, kama ilivyoonyeshwa katika Jedwali Na. 16.4. Hadi kufikia mwaka 2004, kulikuwa na vituo 5 vinavyorusha matangazo kwa njia ya satellite, ikilinganishwa na 3 mwaka 2003. Vituo hivyo ni TVT, ITV, Star TV, Channel Ten na Channel 5. Jedwali na 16.3: Vituo vya Televisheni vinavyorusha matangazo ya Televisheni nyingine.
Chanzo: Taasisi ya utangazaji Tanzania . Jedwali na 16.4: Vituo vya televisheni vinavyorusha matangazo kwa kuwaunganisha wateja kwa kutumia waya maalumu.
Chanzo: Taasisi ya Utangazaji Tanzania. Taasisi ya Utangazaji Tanzania (TUT) 262. Mwaka 2004, Taasisi ya Utangazaji Tanzania ilianzishwa baada ya kuunganishwa kwa Radio Tanzania Dar-es-Salaam (RTD) na Televisheni ya Taifa (TVT). Taasisi hii hutoa huduma za kijamii na kibiashara. Mwaka 2004, Taasisi ilipata jumla ya sh. 1,516.6 milioni kutokana na mapato ya biashara ikilinganishwa na sh. 1,289.2 milioni mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 16.6. Kiwango hiki cha mapato kilifikiwa kutokana na mikakati mizuri ya masoko na kuboreshwa kwa vipindi mbalimbali. Jedwali Na 16.5. linaonyesha mwenendo wa mapato. Jedwali na. 16.5: Mwenendo wa mapato mwaka 2001 - 2004 sh. milioni
263. Hadi mwishoni mwa mwaka 2004, Taasisi iliweza kufikia asilimia 80 ya usikivu kwa upande wa radio kupitia mitambo yake 9 ya kurushia matangazo. Uwezo huu ulitokana na kukarabatiwa kwa mtambo wa Kunduchi. Aidha, urushwaji wa matangazo kwa njia ya televisheni ulifikia asilimia 40 baada ya kufungwa mitambo katika mikoa ya Dodoma, Arusha na Mwanza. Jedwali Na. 16.6 : Vituo vya mitambo ya kurushia matangazo ya Radio na Televisheni.
Chanzo: Taasisi ya Utangazaji Tanzani a * Usikivu hauko eneo zima. Magazeti na Majarida 264. Magazeti na majarida yanayochapishwa hapa nchini huandaliwa kwa lugha ya Kiswahili na Kingereza. Hadi Desemba mwaka 2004, jumla ya magazeti na majarida 693 yalikuwa yamesajiliwa ikilinganishwa na 654 mwaka 2003, sawa na ongezeko la asilimia 6.0. Asilimia 90.0 ya magazeti na majarida yote yaliyosajiliwa, husambazwa mijini na zaidi ya asilimia 50.0 husambazwa katika mkoa wa Dar-es-Salaam. Aidha, kati ya magazeti na majarida yaliyokuwa yamesajiliwa, 171 pekee ndiyo yalikuwa yakitolewa kwa kipindi kilichopangwa. Jedwali Na. 16.7: Magazeti na Majarida yaliyosajiliwa Mwaka 1990 - 2004 .
Chanzo: Idara ya Maelezo na Habari Tanzania . Jedwali na 16.8: Vituo vya Radio vilivyosajiliwa kuanzia Mwaka 1994 hadi Mwaka 2004.
Chanzo: Taasisi ya utangazaji Tanzania. Jedwali na 16.9: Vituo vya televisheni vilivyosajiliwa kuanzia mwaka 1994 hadi waka 2004.
Chanzo: Taasisi ya Utangazaji Tanzania. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||