Hifadhi ya Chakula

.

Uendelezaji kilimo ni lengo kuu la Taifa. Mkazo umewekwa kwenye uzalishaji wa chakula na kupunguza umaskini.

 

Kwa miaka mingi uzalishaji wa chakula nchini umeshindwa kutimiza mahitaji ya chakula, na hivyo kusababisha uagizaji kutoka nje na misaada ili kufidia pengo.  Kwa maana hiyo, Serikali imeruhusu masoko huria masoko na bei.

 

Sekta binafsi inasaidiwa ili izalishe chakula, upatikanaji wa pembejeo na shughuli za masoko. Serikali inatumia mikakati ifuatayo: -

 

¨     Uboreshaji wa vivutio katika kurahisisha chakula kwa kukuza uuzaji nje wa mazao yasiyo asilia na yale ya chakula kwa kuufanya huria mfumo wote.

 

¨     Kusaidia utafiti na ugani na kuboresha ufanisi, kukuza ushiriki wa sekta binafsi katika uzalishaji, usindikaji, uhifadhi, pembejeo na masoko.

 

¨     Kuboresha miundombinu vijijini.

 

¨     Kukuza biashara ya mipakani kwa nchi majirani na uuzaji nje.

 

¨     Kuzuia upotevu wa chakula baada ya uvunaji.

 

¨     Kufuatilia mara kwa mara na kutathmini hali ya chakula vijijini kwa kupitia utaratibu na mfumo mzima wa utoaji tahadhari mapema na ufuatiliaji mazao.

 

¨     Kupitia sheria zinazoathiri ushirikishwaji wa sekta binafsi kwenye kilimo na masoko katika sekta ya kilimo.

 

¨     Kuondoa vikwazo vya biashara katika ngazi ya taifa, mikoa na wilaya; na kurekebisha sheria zinazotawala usafirishaji wa chakula kuvuka mipaka ya wilaya, mikoa na nchi.

 

¨     Kuunda upya Hifadhi ya Taifa ya Akiba ya Nafaka ili ifanye kazi kwa ufanisi na tija.

 

Sekta binafsi inashiriki katika kununua chakula kutoka kwa wakulima, na pia kuagiza chakula kutoka nje ya nchi. Kampuni binafsi ni pamoja na: -

 

¨     Mohamed Enterprises

¨     EECO Traders

¨     Mbutano Investment

¨     Andre & CIESA

¨     Sky Coach

 

 

Masoko ya Kilimo:

Tanzania bado inategemea uuzaji wa mazao asilia nje, ila inakabiliwa na tatizo la mabadiliko ya bei katika soko la dunia na kuzorota kwa biashara katika sekta ya kilimo. Mkakati wa kuuza nje umelenga katika kuuza mazao tofauti na wakati huo kuhakikisha ubora wa hali ya juu, na kuyapa thamani zaidi kwa kuyasindika. Soko la mazao ya kilimo, mifugo na pembejeo limefanywa huria. Makampuni binafsi na vyama vya ushirika hushiriki kwa viwango tofauti.

 

Mwitiko wa sekta binafsi kwa fursa zilizojitokeza kutokana na kuachia uchumi uwe huria na ubinafsishaji umekuwa mkubwa. Hisa za sekta binafsi katika masoko ya mazao mbalimbali zimekuwa kubwa. Biashara yote ya mazao ya chakula inaendeshwa binafsi isipokuwa shughuli za Hifadhi ya Taifa ya Nafaka.

 

Tasasi za Sekta Binafsi:

 

Asasi kadhaa binafsi zimeanzishwa, zikishughulika na ununuzi wa mazao ya chakula na biashara, pamoja na pembejeo kwa wakulima. Ni pamoja na: -

 

¨      Chama cha Walimaji wa Kahawa Tanzania, 

¨      Chama cha Pamba Tanzania,

¨      Chama cha Korosho Tanzania,

¨      Chama cha Chai  Tanzania,

¨      Chama cha Mkonge, Tanzania,

¨      Chama cha Walimaji Maua Tanzania,

 

 

Kuna tasasi binafsi za jumla zinazowakilisha biashara binafsi na kuwa na mkabala wa pamoja katika kuwasiliana na kuzungumza na serikali kuhusu maendeleo ya sekta binafsi. Hizi ni: -

 

¨      Chama cha Biashara, Viwanda na Kilimo, (TCCIA)

¨      Shirikisho la Viwanda Tanzania, (CTI)

¨      Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF)

Baraza la Taifa la Biashara

Title

.

Title

.

Title

.