|
HOTUBA
YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,
KWENYE SIKUKUU YA WAFANYAKAZI, DAR ES SALAAM, MEI MOSI, 2001
Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi,
Ndugu
Margaret Sitta;
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi,
Ndugu
Nestory Ngula;
Waziri wa Kazi, Maendeleo ya Vijana na Michezo,
Mhe. Prof. Juma A. Kapuya, Mb.;
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,
Mhe. Yusufu Makamba;
Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani, ILO;
Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania;
Viongozi wa Vyama vya Siasa na Serikali;
Ndugu Wafanyakazi na Wananchi;
Mabibi na Mabwana.
Ninayo
furaha kubwa kuungana nanyi wafanyakazi wote katika kusherehekea Sikukuu ya
Wafanyakazi. Nawashukuruni
sana viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kwa kunialika kwa mara nyingine kuwa
mgeni rasmi katika maadhimisho ya Mei Mosi.
Mwaliko huu ni kielelezo cha dhamira yenu kushirikiana na Serikali katika
kutafuta ufumbuzi wa matatizo mbalimbali ya wafanyakazi, na ya nchi yetu.
Ahsanteni sana.
Ndugu
Wafanyakazi,
Baadhi
yenu mlisimamia Uchaguzi Mkuu mwaka jana. Kwa
sehemu kubwa sana uchaguzi ulikwenda vizuri; na ninawapongeza na kuwashukuru
wafanyakazi wote waliohusika. Najua
kura za wafanyakazi nazo zilichangia ushindi wangu mkubwa. Walionipigia kura
nawashukuru sana; na waliowapigia wagombea wengine nao nawashukuru kwa kuleta
uhai katika demokrasia yetu ya vyama vingi ambayo bado tuna kazi kubwa ya
kuirutubisha, kuilea na kuikomaza.
Naushukuru
uongozi wa vyama vya wafanyakazi uliopita chini ya Muungano wa Vyama vya
Wafanyakazi (TFTU), na wafanyakazi wote, kwa mahusiano mazuri tuliyokuwa nayo.
Hata pale tulipohitilafiana, tulizungumza, kwa uwazi na ukweli, kisha
tukaendelea kujenga nchi, si kuibomoa. Mahusiano
mazuri kati ya wafanyakazi na Serikali, na utendaji wa wafanyakazi mbalimbali,
ni moja ya mambo muhimu yaliyochangia mafanikio makubwa tuliyopata katika
kurekebisha mfumo wa uchumi wetu hadi tukasifiwa duniani kote. Leo napenda
katika hadhara hii, na kupitia vyombo vya habari, niwashukuru sana wafanyakazi
wa Tanzania. Naomba tuendelee
kushirikiana hivyo, kwa manufaa ya taifa na wananchi wote.
Aidha,
uvumilivu na utulivu wenu ulitupa fursa ya kushughulikia matatizo makubwa ya
uchumi yanayoikabili nchi yetu. Siku
zote nimekuwa muwazi na mkweli kwenu na kwa wananchi wote.
Nashukuru mmenielewa kuwa nia yangu ni njema, na kwamba kuzungumza
matatizo ya taifa letu kwa uwazi na ukweli ndiyo mwanzo wa kukubaliana juu ya
ufumbuzi endelevu.
Namshukuru Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), kwa salamu zake
na kwa misaada na ushirikiano wao kwa Vyama vya Wafanyakazi na vya
Waajiri, na katika kukuza na
kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali, waajiri na wafanyakazi.
Nazishukuru pia Serikali za Denmark na Marekani wanaotusaidia kuboresha
utendaji katika sekta hii ya kazi.
Natoa shukrani vile vile kwa Mwakilishi wa Chama cha Waajiri Tanzania
(ATE), kwa hotuba yake nzuri na kwa kuendeleza ushirikiano mzuri
na Serikali, na Vyama vya Wafanyakazi.
Hivi punde nimetoa zawadi kwa wafanyakazi bora.
Naungana nanyi katika kuwapongeza sana, na kuwaomba waendelee na kazi yao
nzuri ili wengine wajifunze kutoka kwao.
Pongezi
na shukrani zangu za mwisho ni kwa viongozi na wananchi wa Dar es Salaam kwa
kuubeba vizuri sana mzigo wa kuwa wenyeji wa sherehe za Mei Mosi mwaka huu.
Nakipongeza pia Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi,
Teknolojia, Ufundi Stadi, Habari na Utafiti (RAAWU) kilichosimamia na kuratibu
maandalizi ya Mei Mosi hii. Wamefanya kazi nzuri, na ninawashukuru sana.
Vyama Huru vya Wafanyakazi
Ndugu Mwenyekiti,
Mei Mosi ya mwaka huu ni ya kihistoria, iliyoandaliwa na kusimamiwa na
uongozi mpya, wa vyama vipya vya wafanyakazi, vilivyo huru kabisa.
Vyama huru vya wafanyakazi ni sehemu muhimu sana ya demokrasia, na
vikifanikiwa vitachangia sana kuimarisha uelewa, uwajibikaji, na utekelezaji wa
haki za wafanyakazi.
Nawapongezeni nyote kwa kuunda vyama vyenu vya wafanyakazi, na Shirikisho
la Vyama Huru vya Wafanyakazi Tanzania, (Trade Unions Congress of Tanzania)
na kuchagua viongozi wake. Natoa
pongezi za dhati kabisa kwako Mama Margaret Sitta kwa kuchaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa kwanza wa Shirikisho, na kwa imani kubwa wenzako waliyoionyesha
kwako. Hongera sana, na ninakuhakikishia ushirikiano wa dhati unapoanza
kutekeleza majukumu yako.
Nakupongeza
pia Katibu Mkuu mpya, Ndugu Nestory Ngula, pamoja na nyote mlioaminiwa na
wenzenu na kupewa uongozi. Hongereni
sana, na ninawahakikishieni ushirikiano wa kutosha kutoka Serikalini.
Hata hivyo napenda kuwatanabahisha kuwa mwisho wa kuundwa kwa vyama, na
kuchagua viongozi, ndio mwanzo wa kazi yenyewe, katika mazingira magumu na
matatizo mengi ambayo hamuwezi kuyamaliza yote kwa mara moja.
Nimepokea malalamiko yenu kuwa Sheria iliyoanzisha vyama huru vya
wafanyakazi ina mapungufu. Iwapo
hoja ya marekebisho itathibiti, tutakuwa tayari kukaa nanyi, pamoja na washika
dau wengine, ili kuirekebisha sheria hiyo kwa namna itakayozingatia maslahi ya
kila upande. Maana, Serikali lazima pia ijali maslahi ya washikadau wengine,
wakiwemo waajiri, wawekezaji, na wananchi kwa ujumla.
Ndugu Viongozi Wapya,
Katika mazingira haya mapya, na kwa kuzingatia ushindani mkali unaoletwa
na utandawazi, ninayo mambo matatu ya kushauri vyama vipya na huru vya
wafanyakazi.
Kwanza, hakikisheni mikataba iliyopo sehemu za kazi, na sheria za nchi,
inafuatwa na waajiri wenu. Maana
hakuna faida kutafuta haki mpya na maslahi mapya, kama hata yale ya awali
hayajatekelezwa kwa ukamilifu. Nitatoa
mfano. Serikali imeweka kima cha
chini cha mshahara kisheria, lakini nasikia bado wapo wafanyakazi wanaolipwa
chini ya kiwango hicho. Ninyi mkiwa viongozi wao mnalo jukumu la kuwatetea.
Ninaambiwa
pia wapo wafanyakazi ambao hawana barua na mikataba rasmi ya ajira.
Hilo nalo inabidi vyama vya wafanyakazi vilichunguze na kuchukua hatua.
Nasikia waajiri wengine wamegeuza ajira karibu yote iwe ya vibarua tu.
Hoja ya vibarua inaeleweka, lakini ina kikomo chake.
Haiwezekani wafanyakazi karibu wote wawe vibarua.
Fanyeni utafiti wa kutosha na kisha kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo kwa
kushirikiana na Serikali na waajiri.
Pili, jijengeeni uwezo na utaalam wa kujua hali halisi ya uzalishaji
katika kila sehemu ya kazi, undani wa uzalishaji na biashara mnayoifanya, au
huduma mnayoitoa, na kuelewa mwenendo wake katika ulimwengu wa ushindani. Ujuzi
huo utawawezesha kujiamini mnapokaa na waajiri kuzungumzia mbinu za kuongeza
uzalishaji na tija, na kuongeza uwezo wenu wa ushindani katika soko huru, na
baada ya kuongezeka kwa uzalishaji na tija, kupata nguvu, haki na msingi wa
kudai maslahi bora zaidi. Maana
kama uzalishaji na tija haviongezeki, na kama faida haiongezeki, madai ya
maslahi bora zaidi yatahimiliwa na nini?
Tatu, zingatieni wajibu wa kujadiliana na waajiri juu ya hali bora za
kazi. Mnapaswa kujiimarisha
kitaaluma kabla ya kukabiliana na waajiri ili muweze kujenga nguvu za
hoja, si kutumia tu hoja ya nguvu itokanayo na wingi wenu. Sheria ya
Mahakama ya Kazi imeweka utaratibu wa majadiliano ya pamoja kati ya waajiri na
waajiriwa kupitia vyama vyao, ili kufunga mikataba ya hiari ya hali bora za kazi.
Sheria hii itaangaliwa upya wakati wa kurekebisha sheria zote za kazi.
Lakini ni muhimu mikataba mtakayoifunga isaidie kuchochea uzalishaji,
tija na faida ili uwezo wa kuitekeleza mikataba hiyo upatikane.
Kamwe msisahau kuwa Serikali, na sekta ya umma kwa ujumla, sasa si
mwajiri mkubwa kama ilivyokuwa zamani. Wanachama
wenu wengi sasa watakuwa kwenye sekta binafsi.
Na kwa kadri sekta binafsi inavyotwaa majukumu mengi zaidi ya kiuchumi na
utoaji wa nafasi za ajira, ndivyo wajibu na kazi za vyama vya wafanyakazi
zinavyoongezeka. Jiandaeni vizuri
kuubeba mzigo huo, na Serikali itawasaidieni kwa dhati.
Amani na Utulivu
Ndugu Mwenyekiti,
Tukumbushane umuhimu wa amani na utulivu kwetu sisi wafanyakazi. Maana ni rahisi kudhani kuwa anayehusika na amani na utulivu
ni Serikali na wanasiasa tu. Lakini
ukweli ni kuwa maslahi yenu kama wafanyakazi yanategemea sana hali ya amani na
utulivu. Kwa sababu hiyo, kila
mfanyakazi ni mshika-dau katika kuhifadhi na kutetea sifa yetu kama kisiwa cha
amani na utulivu.
Tunaishi katika dunia ya ushindani kwenye kila jambo, ikiwemo ushindani
katika kuvutia mitaji na vitegauchumi, ushindani wa ajira, na ushindani wa
biashara. Sifa moja inayotuongezea uwezo wa ushindani katika Bara la Afrika ni
hali yetu ya amani na utulivu. Mwekezaji
binafsi, ambaye sasa ndiye tunayemtegemea atoe nafasi za ajira, hawezi kuja
kuwekeza Tanzania tukipoteza sifa hiyo. Watalii tunaowategemea sana kwa ajira na
mapato nao wataikwepa nchi yetu.
Hivyo wafanyakazi wawe wakereketwa wa amani na utulivu. Kwanza, wao wenyewe wasishiriki au kufumbia macho vitendo
vinavyoashiria uvunjifu wa amani na utulivu.
Na pili, washirikiane na Serikali katika kukemea tabia inayoanza kuota
mizizi ya kutoheshimu sheria au maelekezo mengine halali ya Serikali yenye lengo
la kudumisha amani na utulivu.
Inawezekana
wapo wanasiasa wanaofikiri kuwa ghasia, fujo na vurugu kwao ni mtaji wa kisiasa;
lakini kwako mfanyakazi wa Tanzania ujiulize utapata faida gani nchi hii ikianza
kukwepwa na wawekezaji na watalii.
Umaskini na Maendeleo
Ndugu Mwenyekiti,
Tanzania ni miongoni mwa nchi maskini sana duniani, na sasa tumeazimia
kuondokana na aibu hiyo. Tumebuni
Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 inayokusudia kutufanya tuwe taifa ambalo watu
wake walio wengi watakuwa na maisha bora; taifa lenye amani, utulivu, na umoja;
taifa linaloongozwa kwa misingi ya utawala bora, utawala wa sheria; taifa lenye
watu walioelimika na wanaoendelea kujielimisha; na taifa lenye uchumi unaohimili
ushindani, uchumi unaokua na kutoa ajira na mapato, uchumi endelevu usioharibu
mazingira yetu, na uchumi utakaonufaisha washika-dau wote, na kuhimili matumaini
yetu ya maisha ya kisasa.
Hayo ni malengo, lakini utekelezaji wake unategemea sana jasho na maarifa
ya kila Mtanzania, kila mfanyakazi, kila mkulima, kila mfugaji, kila mvuvi, na
kila mfanyabiashara, wa kike na wa kiume. Nchi
yetu itaendelea kwa kazi, si kwa maneno matupu au tamaa ya maisha bora.
Hatuwezi kuendelea kwa kutegemea fadhila za mataifa mengine.
Wao si ndugu zetu, na wakati mwingine wanaweza kuwa na agenda zao ambazo
si lazima zishabihiane na malengo yetu. Na
hata kama wangekuwa ndugu zetu, wahenga walishatuambia, “Mtegemea cha ndugu
hufa maskini”.
Haki za binadamu zinazungumzwa sana, lakini jambo ambalo halizungumzwi
sana ni ukweli kuwa adui mkubwa wa haki za binadamu ni umaskini.
Kwa mtu ambaye hana uhakika wa chakula, haki yake ya msingi ni chakula.
Kwa mtu ambaye hana nguo, haki yake ya msingi ni nguo.
Na kwa yule ambaye hana mahali pa kuishi haki yake ya kwanza ni
kujiwezesha kupata makazi.
Umaskini, na unyonge unaotokana na umaskini na utegemezi, ndiye adui
mkubwa sana wa nchi yetu. Tusipokuwa
waangalifu, tunaweza kuondolewa kwenye mkazo unaostahili kwenye umaskini,
tukang’ang’ania mambo yapitayo ambayo hayampi shibe mwenye njaa, hayamvishi
aliye uchi, na hayampi makazi asiye na mahali pa kuishi, sisemi kumpeleka mwanae
shule au kumtibu akiugua.
Hivyo ni muhimu sana kwa wanasiasa wote – katika Chama Tawala na katika
Upinzani – kuwajali zaidi wananchi kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwenye vita
dhidi ya umaskini. Mwanasiasa
katika nchi maskini kama yetu, iwapo anao uadilifu wowote wa kisiasa ndani yake,
ataona uchungu juu ya umaskini wa watu wetu, na ataunga mkono jitihada zote za
Serikali kupiga vita umaskini.
Lakini
kama wapo wanaofikiri kuwa bidii ya kuandaa maandamano na mikutano ya kudai mimi
na Rais Karume tuwapishe Ikulu ndiyo njia sahihi ya kupiga vita umaskini,
wanaota ndoto za mchana. Mimi, na
nina hakika Rais Karume, tutaendelea kuweka
mkazo sahihi na unaostahili katika kukuza uchumi kwa manufaa ya wananchi
wote, ikiwemo kukuza ajira, kuboresha maslahi ya wafanyakazi, kuboresha huduma
za jamii, na hatimaye kufikia malengo yetu ya kuondosha umaskini kwa faida ya
wananchi wote.
Matokeo na Athari za Utandawazi
Ndugu Wafanyakazi,
Dunia
yetu ya leo ina sifa mbili kubwa. Moja
ni kasi kubwa ya mabadiliko ya teknolojia, na ya pili ni mageuzi makubwa katika
mifumo ya kijamii na kiuchumi. Mabadiliko
na mageuzi hayo yanachochewa na utandawazi, ambao ni wimbi kubwa. Tunakabiliwa
na chaguo ama kuacha kubadilika tusombwe na wimbi hilo, na kuendelea kuserereka
pembezoni mwa maendeleo ya dunia ya karne ya 21; au tubadilike haraka kisera,
kiutendaji, na kimtazamo, na kutafuta mbinu za kuhakikisha nasi tunafaidika
katika mfumo huu mpya wa mahusiano duniani, na hivyo kuwahami wafanyakazi wetu.
Utandawazi huu unafuta mipaka baina ya nchi na nchi, bara na bara.
Mipaka ya kijiografia haiwezi tena kuzuia maingiliano ya fikra,
teknolojia, ujuzi, biashara na mitaji. Katika
hali hiyo ushindani unakuwa mkali sana, kwenye kila kitu; ushindani ambao sisi
tunauingia tukiwa dhaifu kuliko wenzetu.
Katika mazingira haya, uwekezaji mitaji ndio njia pekee ya kukuza uchumi,
kupatikana kwa nafasi za ajira, na kuboresha maisha ya wananchi. Ndiyo maana nchi zote, kubwa na ndogo, tajiri na maskini,
zinashindana kuvutia wawekezaji mitaji, kwa kushindana kuweka mazingira mazuri
ya uwekezaji kisera, kiutendaji, kisheria - ikiwemo sheria za kazi - na kwa
kuboresha miundo mbinu.
Iwapo sisi hatutabadilika, tutajipunguzia mvuto wetu kwa wawekezaji,
wakati ambapo sisi wenyewe ndani ya nchi hatuna uwezo wa mitaji na ujuzi
kuzalisha bidhaa na kutoa huduma za kushindana kwenye soko la kimataifa. Ni kweli baadhi ya hatua tunazolazimika kuzichukua zinaweza
kuathiri baadhi ya wafanyakazi, hasa kwa siku za mwanzo.
Lakini, ingawa dawa siku zote ni chungu, hatima yake ni kupona.
Kinyume chake ni kukaribisha maradhi, na hata kifo.
Hata
hivyo, napenda niwahakikishieni kuwa tunachukua, na tutaendelea kuchukua, kila
tahadhari ili kulinda na kutetea maslahi ya taifa letu, maslahi ya wafanyakazi
na maslahi ya wananchi. Hatufanyi
mageuzi, na hatuchukui hatua za kuvutia wawekezaji, kwa mtindo wa “bendera
fuata upepo”. Tunakuwa makini, na
kuona hoja ipi inakubalika, na ipi haikubaliki.
Kwa upande wa ushindani wa kibiashara tunayo kazi kubwa mbele yetu
inayohitaji ushirikiano mkubwa kati ya Serikali, waajiri na wafanyakazi.
Kwanza, lazima tuongeze uzalishaji na tija.
Lazima tubadili mtazamo wetu kuhusu kazi, na tupende kufanya kazi
kwa kujituma zaidi kuliko kungoja kutumwa, tufanye kazi kwa bidii, kwa ubunifu
na kwa maarifa. Pili, lazima tuongeze ubora wa bidhaa tunazotengeneza na
kuzifunga vizuri kama washindani wetu katika soko la dunia wafanyavyo. Tatu, lazima
tupunguze gharama za uzalishaji na uendeshaji ili bei ya bidhaa zetu iweze
kushindana katika masoko ya dunia. Nne, lazima tupunguze gharama za kufanyia
biashara. Na tano lazima
tuwe hodari zaidi katika kujitangaza na kutafuta masoko mapya, ikiwemo
masoko yaliyo jirani nasi.
Na
hapa napenda nirudie tena mwito wa kuwa na ushirikiano wa karibu sana kati ya
Serikali, waajiri, na wafanyakazi. Tusipokuwa kitu kimoja, na badala
yake kuendekeza malumbano na mivutano, hatutafanikiwa.
Tuazimie kuanzia leo kuvuta pamoja, si kuvutana.
Upo
pia ushindani wa ujuzi na maarifa. Tanzania
tuna maliasili nyingi, lakini dunia ya leo, na hasa dunia ijayo, itatawaliwa na
wenye maarifa, kwa maana ya sayansi, teknolojia, elimu na ujuzi.
Kuwa na maliasili peke yake haitoshi.
Hatuna budi tujinoe kwa elimu na ujuzi, na hasa elimu inayomfanya mtu
aajirike au ajiajiri.
Yapo malalamiko kuwa wawekezaji kutoka nje wanaajiri sana wageni.
Tatizo hili linakuzwa mno kuliko hali halisi ilivyo.
Ukiacha sekta kama vile madini ambapo hatuna wataalamu wa Kitanzania wa
kutosha, kwenye sekta nyingine nyingi wawekezaji hao hawaruhusiwi kuajiri zaidi
ya wageni 5. Utafiti tulioufanya kwenye baadhi ya miradi unaonyesha kuwa kwenye
sekta ya viwanda, wageni walioajiriwa ni chini ya asilimia moja ya wafanyakazi
wote; kwenye utalii ni zaidi kidogo ya asilimia moja; kwenye madini ni karibu
asilimia 15, na kwenye huduma ni asilimia moja.
Hivyo hali si mbaya sana, na itazidi kuwa nzuri siku zijazo.
Changamoto kwetu Watanzania ni kuhakikisha tunao wataalamu wa kiwango
kinachoweza kushindana na wataalamu wengine duniani, tukianzia na soko la ajira
la Afrika Mashariki.
Ndugu Mwenyekiti,
Tutaendelea kulinda viwanda vya ndani dhidi ya ushindani usiokuwa wa haki
kutoka bidhaa zinazoagizwa kutoka nje, ikiwa ni pamoja na kudhibiti uingizaji wa
bidhaa kwa njia ya magendo. Lakini
katika dunia ya utandawazi, hoja ya kulinda viwanda vya ndani ni hoja ya mpito
tu wakati nchi changa zinajenga uwezo wa kuhimili ushindani.
Hivyo utaratibu wa kulinda viwanda lazima uende sambamba na juhudi za
makusudi kuongeza uwezo wa ushindani. Na
hilo halitawezekana iwapo tutavilinda mno viwanda vyetu.
Kazi na Ajira
Ndugu Wafanyakazi,
Leo napenda pia nizungumzie dhana ya kazi kwa upande mmoja, na
dhana ya ajira kwa upande mwingine.
Lazima tujifunze kubadili uelewa wetu wa kazi, na uelewa wetu wa ajira.
Maana si lazima kila penye kazi pawe na ajira, na si lazima kila penye
ajira kuwe na kazi.
Mfano mzuri wa kazi bila ajira ni kina mama.
Wanafanya kazi kubwa na muhimu katika familia. Lakini hawana ajira, wala
hawalipwi mshahara. Kwa upande
mwingine, na hasa kwenye sekta ya umma, wapo watu wana ajira, lakini hawana kazi,
au wanagawana kazi ambayo ingeweza kufanywa na mtu mmoja tu. Wapo wanaolipwa
mshahara kamili kwa nusu kazi, au robo kazi, na wapo hata wanaolipwa kwa vile tu
wameajiriwa, hata kama hawakufanya kazi yoyote.
Tatizo la baadhi ya watu kupenda kulipwa bila kufanya kazi inayolingana
na malipo si letu peke yetu. Ipo
hadithi ya bwana mmoja kutoka nchi tajiri mojawapo ambaye alikuwa na tabia hiyo.
Yeye alikuwa amepunguzwa kazi na akawa analipwa fedha za kujikimu kwa vile
alikuwa hana kazi. Ikafika wakati
utaratibu huo wa kulipwa bila kazi ukafutwa, akalazimika kutafuta kazi.
Akamwendea mwenye nyumba mmoja na kumwomba kazi ya kufyeka majani kwenye
bustani yake.
Mwenye
nyumba akamwambia, “Kwa kawaida anakuja kijana wa jirani yangu kufanya kazi
hiyo, na ninamlipa sh.20,000/=. Lakini
kwa vile nakuona una shida ya kazi, wewe nitakulipa sh.25,000/=.”
Yule
bwana akamjibu, “Tafadhali mwache kijana aendelee na kazi yake; wewe nipe tu hizo sh.5,000/=.”
Ndugu Wafanyakazi,
Mengine haya yanachekesha, lakini kujenga uchumi wa kisasa, unaohimili
ajira kubwa, na maslahi bora zaidi, si jambo la lelemama, au jambo la kuchekesha.
Tupende tusipende, tunakabiliwa na ushindani mkubwa sana, na tukiendelea
na tabia hii hatutaweza kuuhimili ushindani huo; viwanda vitafungwa; na ajira
ama itahamia nchi za nje, ikiwemo nchi jirani, au wao watakuja nchini kuchukua
kazi zetu.
Katika uchumi unaohimiliwa na sekta binafsi ajira na maslahi ya
wafanyakazi havipatikani kwa amri ya Serikali, bali kwa uwezo wa kuzalisha,
kushindana, na kupata faida. Kama
tunataka uchumi ukue, uweze kushindana na kuvutia wawekezaji wengi zaidi, lazima
tujenge ushirikiano na kuaminiana zaidi kati ya Serikali, wawekezaji, wananchi
na wafanyakazi. Tuunde ubia wa
kuhakikisha taifa linafanikiwa, wawekezaji wanafanikiwa, na wafanyakazi nao
wanafanikiwa.
Mwaka hadi mwaka tunalalamika kuwa wapo vijana 600,000 – 700,000
wanaoingia katika soko la ajira, wakati sekta rasmi inaweza kuajiri kiasi cha
25,000 tu kwa mwaka. Lakini pia
tujiulize hao vijana 600,000 wanaweza kufanya kazi gani ya kuajiriwa? Wana ujuzi gani wenye soko katika hali halisi ya uzalishaji
na utoaji huduma nchini? Ukweli ni
kuwa wengi wao hawaajiriki kwa urahisi.
Lazima tukubali pia kuwa tunaposema uti wa mgongo wa uchumi wetu ni
kilimo, ufugaji na uvuvi, maana yake ni kuwa uti wa mgongo wa uhakika wa ajira
ni kilimo, ufugaji na uvuvi, pamoja na viwanda vya kusindika mazao ya sekta hizo.
Tunasema hakuna ajira, lakini tunayo ardhi tele inayofaa kwa kilimo na
ufugaji, na tunayo bahari, mito na maziwa yenye samaki.
Kwa vyovyote vile haitawezekana kwa sekta rasmi kuajiri wote watafutao
kazi. Kwa Watanzania wengi, ajira maana yake ni kujiajiri katika kilimo, ufugaji
na uvuvi. Huo ni ukweli ambao hatuna budi sote kuukubali.
Ndugu Wafanyakazi,
Ni kweli Serikali ina wajibu wa kufuatilia wawekezaji ili kuhakikisha
wanatekeleza masharti ya mikataba na maelewano yetu, na kufuata sheria za nchi.
Tutaendelea kutekeleza jukumu hilo, na kuongeza uwezo wa ukaguzi.
Vyama vya wafanyakazi navyo viwe macho. Kwa upande wake, Serikali imeamua
kukifanya Kitengo cha Afya na Usalama wa Wafanyakazi kuwa Wakala wa Serikali ili
kiweze kujiendesha kwa ufanisi na kutoa huduma bora zaidi kwa wafanyakazi na
waajiri.
Ipo pia mipango mingi ya kuimarisha uwezo wa Wizara ya Kazi, Maendeleo ya
Vijana na Michezo, kwa msaada wa wahisani mbalimbali.
Tunao mradi wa kuimarisha Idara ya Kazi unaofadhiliwa na Serikali ya
Denmark. Lengo ni kuweka mazingira
bora zaidi ya kisera na kisheria katika mahusiano ya kikazi, kuwa na sheria za
kazi zinazoenda na wakati na kuvutia uwekezaji zaidi, kuboresha mazingira ya
kufanyia kazi, kuongeza uzalishaji na tija za wafanyakazi, na kujenga maelewano
mazuri sehemu za kazi.
Mradi mwingine, ambao huu unafadhiliwa na Serikali ya Marekani, ni wa
kuanzisha Soko la Ajira. Kazi
iliyoanza Aprili mwaka jana ya kukusanya takwimu za msingi kuhusu ajira
inatazamiwa kukamilika mwezi Juni mwaka huu.
Kituo cha kwanza cha Soko la Ajira (Employment Exchange Centre) kitaanzishwa
hapa Dar es Salaam, na baadaye mikoani. Miongoni
mwa majukumu ya vituo hivyo itakuwa kutoa ushauri nasaha kwa wanaotafuta kazi,
kusaidia kuwaunganisha watafuta kazi na waajiri, na kukusanya na kutoa takwimu
za hali ya soko la ajira kwa ujumla. Huduma hii itawarahisishia waajiri kutafuta
wafanyakazi, na wanaotafuta ajira kujua kazi ambazo wana ujuzi nazo zinapatikana
wapi.
Ndugu Wafanyakazi,
Tunalo pia bado tatizo la unyanyasaji na ubaguzi wa wanawake katika jamii
zetu, katika shule na vyuo, na katika ajira.
Kutokana na jitihada zinazochukuliwa na Serikali tatizo linapungua,
lakini halijakwisha. Natoa tena
wito kwetu sote kufuta aibu hii ya kunyanyasa au kubagua wanawake.
Serikali pamoja na wabia-jamii, kwa msaada wa Shirika la Kazi Duniani (ILO),
tumetekeleza mradi wa kuangalia upya hali ya ajira kwa wanawake katika mazingira
ya mageuzi ya uchumi. Tayari ripoti
imekamilika na imetupa mahali pa kuanzia katika kutetea na kulinda maslahi ya
wanawake. Ikibidi tutabadili sheria
na taratibu. Lakini, kazi kubwa
zaidi ni kubadili fikra, mazoea, mila na desturi zinazokwamisha ukombozi wa
kweli wa wanawake. Kazi hiyo si ya
Serikali peke yake; ni ya jamii nzima. Na
hapa tena navipongeza vyama huru vya wafanyakazi kwa kuonyesha njia, na
kumchagua Mama Sitta awe Mwenyekiti wa kwanza wa Shirikisho lao.
Hiyo ni ishara kuwa tutashirikiana vizuri kutetea haki na maslahi ya
wanawake sehemu za kazi.
Sheria na Mikataba
Ndugu Mwenyekiti,
Serikali inatambua umuhimu wa kuridhia Mikataba ya ILO kuhusu malipo sawa
kwa kazi sawa, kuondosha ubaguzi katika ajira, na kupiga marufuku ajira mbaya
sana ya watoto. Mikataba hiyo pia
inahusu haki za msingi za binadamu ambazo zimo ndani ya Katiba yetu.
Hivyo tatizo si nia ya kuridhia, bali utaratibu tu wa kufanya hivyo.
Na hivi sasa hatua za kuridhia mikataba hiyo karibu zitakamilika.
Kuhusu ajira ya watoto, tangu mwaka 1994 Tanzania imetekeleza Mpango wa
Kimataifa wa Kuondosha Ajira ya Watoto kwa kushirikiana na waajiri na
wafanyakazi. Juhudi hizo
ziliipelekea Tanzania kuwa kati ya nchi tatu duniani zitakazotekeleza mpango wa
muda maalum kumaliza ajira mbaya sana ya watoto.
Tunatambua pia kuwa umaskini ndicho chanzo na kishawishi kikubwa cha
ajira ya watoto. Hivyo juhudi zote
za Serikali za kuondosha umaskini zinalenga pia kuondosha tatizo la ajira ya
watoto.
Nia ya Serikali ni kuwa na sera na mfumo wa sheria za kazi zinazolinda
maslahi ya wafanyakazi, na maslahi ya waajiri, ili mahusiano mema kazini yawe
yale ambayo msingi wake ni kuheshimu haki na maslahi ya wafanyakazi na waajiri,
yenye tija katika uzalishaji, yanayowezesha ushindani, na kwa hiyo kuleta
maendeleo na maisha bora.
Mikopo ya Nyumba kwa Wafanyakazi
Ndugu Mwenyekiti,
Mojawapo ya matatizo ya wafanyakazi wengi ni kukosa uhakika wa nyumba za
kuishi wakiwa kazini, lakini hasa baada ya kustaafu.
Kumiliki nyumba kunatosheleza hitaji muhimu la mwanadamu; na kumpa
heshima na utulivu wa fikra na maisha.
Katika miaka 10 ya kwanza baada ya uhuru, kulikuwa na mfuko wa mikopo ya
nyumba kwa watumishi wa umma. Mfuko
huo uliwasaidia watumishi wa umma wakati huo kujijengea nyumba.
Leo hakuna mfuko kama huo wenye uwezo wa kutosheleza kujenga nyumba za
watumishi kwa mkopo. Matokeo yake, na kwa vile mfumo wa ukopeshaji fedha kwa ajili
ya kujenga nyumba kwenye benki zetu bado haujaimarika, inabidi wananchi walio
wengi wajenge nyumba kwa fedha kutoka mifukoni mwao.
Ujenzi
wa namna hiyo ni ishara ya kuwa nyuma sana kimaendeleo, na kwa watumishi wa umma
ni chanzo, kichocheo na kishawishi
kikubwa sana cha rushwa. Dunia ya
leo watu hawajengi hivyo; na ni matumizi mabaya ya fedha hata kwa wale ambao
wanazo. Kwa vile nyumba ni mali
isiyohamishika, hakuna sababu ya kujenga kwa fedha kutoka mfukoni; na wala
hakuna sababu kwa benki zetu kutaka mkopaji arejeshe mkopo katika muda mfupi.
Kwenye nchi zilizoendelea mikopo ya nyumba inalipwa kwa hata zaidi ya
miaka 25.
Kwa sababu hiyo nimeamua, kwa kuzingatia sera ya Chama changu, kuwa
tuanzishe mfumo ulio wazi wa mikopo ya nyumba na uwekaji nyumba rehani kwa jumla;
na pia kuwa na utaratibu mwingine maalum kwa watumishi wa umma.
Hivi sasa Serikali inashauriana na washika-dau mbalimbali, pamoja na
benki zetu, kuona namna bora ya kutekeleza jambo hili kwa haraka, lakini kwa
makini sana, maana hatutaki yale yaliyoisibu Benki ya Nyumba yarudiwe tena.
Lazima nitoe tahadhari. Mkopo
ni mkopo, na lazima urejeshwe kulingana na makubaliano kati ya mkopaji na
mkopeshaji. Ujanja wa kukwepa
wajibu wa kulipa hauwezi kupewa mwanya tena kwenye sheria zetu.
Maandalizi ya kisera na kisheria yanaendelea.
Karibu tunakamilisha Kanuni za Sheria ya Ardhi ya mwaka jana kwa
kushirikiana na washika dau wengine ili kuvutia benki kukopesha kwa ajili ya
ujenzi wa nyumba. Serikali pia
itaendeleza sera za jumla za uchumi zitakazosaidia kuweka mazingira bora kwa
ukopeshaji wa muda mrefu, kama vile kuendelea kushusha mfumuko wa bei, na riba
za benki.
Nawaombeni viongozi wa vyama vya wafanyakazi nanyi mhamasishe wafanyakazi
kuanzisha vyama vya kuweka na kukopa, na kwa ajili ya ujenzi wa nyumba,
muanzishe ushirika wa nyumba. Tatizo
la nyumba ni kubwa, na ufumbuzi wake lazima utuhusishe na kutushirikisha wote.
Rushwa na Ubadhirifu
Ndugu Wafanyakazi,
Nizungumzie kidogo kuhusu rushwa na ubadhirifu. Wote wawili hawa ni
maadui wakubwa wa maendeleo na ustawi wetu.
Ipo rushwa inayopotosha haki, na kuifanya iwe bidhaa ya kuuzwa na
kununuliwa. Na ipo rushwa
inayopotosha maamuzi ya kiutendaji na kuliingizia taifa au taasisi yoyote ile
hasara kubwa. Mfano ni pale ambapo
barabara ambayo ingeweza kujengwa kwa sh.5 bilioni, inaishia kujengwa kwa sh.10
bilioni, na mzigo huo unabebwa na uchumi wa taifa, na hatimaye wananchi.
Dhahiri rushwa ni kitu kibaya sana katika jamii na lazima tupigane nayo
bila kuchoka au kukata tamaa.
Na rushwa si janga la Tanzania peke yake.
Hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kuthubutu kusema kuwa wao ni
watakatifu kabisa katika suala hili. Tofauti
zilizopo ni aina ya rushwa baina ya nchi na nchi, kiwango cha rushwa, na uwazi
uliopo katika kujadili uwepo wa rushwa katika jamii na taifa.
Tanzania tumekuwa wazi sana kuhusu rushwa.
Sijui ni nchi ngapi zimeunda Tume kama niliyounda mimi chini ya Jaji
Warioba kutafiti rushwa kwa undani katika nchi yetu, kubainisha chanzo chake, na
kuweka mpango maalum na mkakati wa kuipiga vita rushwa.
Na utekelezaji unaendelea kwa kuziba mianya ya rushwa upande mmoja, na
kwa upande mwingine kuongeza uwezo wetu wa kupokea, kuchunguza na kuchukua hatua
za kisheria kuhusu tuhuma zote za rushwa. Upo mkakati wa kitaifa, na upo mkakati kwa kila sekta na kila
Wizara.
Kazi ya kupiga vita rushwa ni ngumu sana, hasa ikijipenyeza pia kwenye
vyombo vinavyosimamia sheria na haki. Nyote
ni mashahidi kuwa kesi za rushwa zinachukua muda mrefu mno.
Wakati mwingine ni vigumu kupata ushahidi utakaothibiti mahakamani, hasa
pale wale wenye taarifa za ndani na ushahidi hawako tayari kushirikiana na
Serikali.
Siwezi kuwalaumu wananchi wanapoishiwa na subira.
Wakati mwingine hata mimi natamani ningekuwa na uwezo wa kutia watu ndani
pale tuhuma nzito dhidi yao zinaponifikia. Lakini zama hizo zimepita.
Leo dhana inayoshamiri ni ya utawala wa sheria, ambapo mtuhumiwa
anahesabika hana hatia hadi mahakama itakapoamua kesi inayomkabili.
Hali hiyo inaiweka Serikali katika hali ngumu sana.
Vyombo vya habari vinaandika tuhuma za rushwa, na kuifanya jamii iamini
kuwa yanayotajwa ni kweli, na hivyo wanataka wasikie kesho yake mtuhumiwa
kafungwa au kafilisiwa. Hata
marafiki zetu kutoka nchi za nje nao wanakosa subira.
Lakini hao hao, na waandishi wa habari hao hao, ndio wa kwanza kutupa
darasa juu ya haki za binadamu, utawala bora, na utawala wa sheria!!
Napenda niwahakikishieni, Ndugu Wafanyakazi, kuwa dhamira na utashi wa
kisiasa wa kupiga vita rushwa sio tu upo pale pale, bali unaongezeka.
Ambacho nina uhakika hakiongezeki ni ushirikiano wa wafanyakazi katika
kupiga vita rushwa na ubadhirifu. Mimi
ninaelewa wananchi wa kawaida wakinyoshea kidole Serikali na taasisi zake.
Lakini napata taabu nikiambiwa wafanyakazi wanalalamikia rushwa.
Maana, hakuna mtu anayeitwa Serikali anayepokea rushwa. Mpokea rushwa
si Serikali; ni mfanyakazi mwenzetu, tunamjua, lakini tunaoneana haya.
Huo ndio ukweli, na unafanya kazi yetu iwe ngumu sana.
Huko
mikoani niliwahi kuwataka wananchi wafanye mikutano ya hadhara na kupiga kura ya
maoni kuhusu wanaowatuhumu kula rushwa. Najua
huu si utaratibu mzuri sana, lakini ulitupa pa kuanzia kwa kuwajua wanaotuhumiwa,
na kuanza kuwachunguza.
Sasa niambieni. Ni mara
ngapi mmesikia kuwa katika Wizara au Taasisi fulani wameitisha mkutano wa
wafanyakazi wote kwa lengo la kupiga kura ya maoni, ya siri, ya kuwafichua
wenzao wanaowajua kuwa ni wala rushwa? Maana
haiwezekani awepo muuguzi katika hospitali anayedai rushwa kutoka kwa wagonjwa,
halafu wenziwe wasimjue. Vivyo
hivyo kwenye Jeshi la Polisi, Mahakama, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Ardhi,
Wizara ya Elimu, na kadhalika.
Nakubali wito wenu kuwa vita dhidi ya rushwa izidi kuongezwa nguvu na
kasi. Lakini nasema nafasi bado ipo
kubwa kwa wafanyakazi kusaidia vita hivyo pale walipo, kwa wenyewe kuacha rushwa
na ubadhirifu, na kwa kutoa taarifa za wenzao wanaochafua jina la mahali pao pa
kazi kwa kupanukisha rushwa. Zama za ukimya wa kulindana sasa ziishe.
Na wakati mwingine kunyosheana vidole baina ya sekta na sekta, wizara na
wizara, idara na idara, haisaidii sana kama watu wasipoanza kusafisha rushwa
pale walipo. Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam yupo hapa. Yeye hupenda kusema, “Mkia wa mbuzi ni mfupi; unasafisha
pale alipolala.”
Na
sisi sawia. Mfanyakazi wa Wizara ya
Elimu anakuwa mwepesi kulaumu rushwa aliyopambana nayo alipoenda mahakamani,
lakini ile rushwa mtumishi wa mahakama aliyopambana nayo katika kumwandikisha
mtoto wake shule haioni.
Natoa wito kwa vyama vipya vya wafanyakazi vione kuwa mojawapo ya kazi
zao ni kusafisha jina la sehemu yao ya kazi, na jina la taaluma zao.
Vyama vya wafanyakazi vione haya, na kuchukua hatua, pale jamii
inapowanyooshea vidole kuwa ni wala rushwa au wabadhirifu. Vibuni mikakati ya
kujisafisha, na ikibidi viombe msaada wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa katika kupanga
na kutekeleza mikakati hiyo. Lazima
pia, wote kwa pamoja, kujenga utamaduni wa kuona rushwa na ubadhirifu kuwa ni
jambo la aibu, na kuwa mali isiyotokana na jasho, mali inayonuka rushwa,
ubadhirifu na wizi, ni aibu na fedheha kubwa!
UKIMWI
Ndugu Wafanyakazi,
Nimefarijika kusikia risala yenu ikieleza kutambua kwenu kuwa janga la
UKIMWI linahitaji elimu kwa jamii yote pamoja na waajiri ili kufanikisha
mapambano dhidi yake. Mmetoa mwito pia kuwa wafanyakazi walioathirika wasitengwe
au kunyanyaswa mahali pa kazi. Nakubali
na ninaungana nanyi kabisa katika hoja yenu hiyo.
Ningependa sote tujiulize tena maswali magumu bila aibu na tuchukue hatua
bila ajizi. Je, tangu mwaka huu uanze tumeshiriki kiasi gani kuzuia kuenea kwa
UKIMWI? Je, wewe umekwisharekebisha
mwenendo wako na kuacha tabia zinazochangia kuenea kwa UKIMWI?
Je, hapo kazini pamekuwa na mwamko mpya wa kupambana na UKIMWI?
Wewe mfanyakazi unashiriki vipi?
Ndugu Wafanyakazi,
Kila mmoja atafakari kwa dhati moyoni mwake
na achukue hatua. Nawaomba pia
waajiri wawe mstari wa mbele katika
vita hivi na wawasaidie wafanyakazi wao kwa kila hali kuweza kujikinga, na kwa
walioathirika tayari kuwatendea haki bila ubaguzi. Kila sehemu ya kazi sasa iwe na utaratibu wa kukumbushana
mara kwa mara juu ya UKIMWI, na mkakati mahususi wa kuzuia kuenea kwa virusi vya
UKIMWI.
Hitimisho:
Ndugu Wafanyakazi,
Napenda kumalizia hotuba yangu kwa kuwakumbusha kuwa njia ya maendeleo
imejaa jasho na vumbi. Tuzingatie
utamaduni wa kupenda kufanya kazi kwa bidii, maarifa, ubunifu na kujituma.
Lawama ni tamu ikitoka mdomoni, lakini peke yake haitapeleka mkono
kinywani. Na katika kujituma kila
mfanyakazi akumbuke kuwa la muhimu si muda anaotumia kufanya kazi, bali kiasi
cha kazi anayoweza kuifanya katika muda aliopewa.
Wenzetu majirani na duniani kote wanajishughulisha, usiku na mchana,
kuongeza uzalishaji na kunoa uwezo wao wa tija na ushindani. Na sisi tuamke.
Nina matumaini makubwa nanyi viongozi wapya wa vyama huru vya wafanyakazi
kwamba mtashirikiana vizuri na Serikali na waajiri ili nchi yetu ijikomboe
kiuchumi na kuleta ustawi kwa wananchi wake.
Hakuna njia ya mkato, isiyo na machungu. Tuwaongoze wafanyakazi kujua na
kuzingatia jambo hilo. Na
tuwashirikishe kama tunataka kushinda vita hivi.
Bwana mmoja aliwahi kusema, “Mtu akikwambia ametajirika kutokana na kazi
nzito, muulize, kazi hiyo nzito ameifanya nani?”
Na sisi sote tunatamani maisha bora, ya kisasa. Tunajua pia kuwa utajiri na maisha bora chanzo chake ni kazi
nzito. Swali. Kazi hiyo nzito aifanye nani?
Nawatakieni Sikukuu njema.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.
HOTUBA
YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,
KWA WANANCHI, TAREHE 27 APRILI 2001
Ndugu Wananchi,
Kama nilivyosema nilipozungumza nanyi mwezi uliopita, ni wajibu wangu
kuwa karibu nanyi. Njia mojawapo ya
kufanya hivyo ni kuzungumza nanyi moja kwa moja kuhusu mambo mbalimbali ya
kitaifa. Nitaendelea kujitahidi
kufanya hivyo angalao mara moja kwa mwezi.
Leo ninapenda kuzungumza nanyi juu ya dhana ya utawala wa
sheria na haki ya kuishi, ambayo ni haki ya msingi ya kila
raia.
Nianze na utawala wa sheria.
Utawala wa sheria ni sehemu muhimu ya utawala bora katika jamii za
wanadamu. Utawala wa sheria ni
mojawapo ya sifa zinazotofautisha jamii ya wanadamu, na jamii za wanyama.
Penye utawala wa sheria mahusiano kati ya watu, na kati ya Serikali na
watu, yanatawaliwa na kuongozwa kwa mujibu wa sheria.
Jamii inayokataa kuongozwa kwa mujibu wa sheria, inafananishwa na himaya
ya wanyama, ambapo kwao haki anakuwa nayo mwenye mabavu kuliko wengine.
Na sheria ni msumeno, inakata kote kote, maana ni mkusanyiko wa kanuni na
taratibu halali kwa lengo la kusimamia mahusiano kati ya mtu na mtu, mtu na
jamii, mtu na Serikali, jamii na Serikali, na kadhalika.
Kila watu, kila jamii, na hata Serikali yenyewe, hufanya kazi zake na
kudai haki zake, kwa mujibu wa sheria, bila upendeleo.
Na uhalali wa sheria unatokana na ukweli kuwa katika nchi ya demokrasia
kama ilivyo yetu, wanaotunga sheria ni wenzetu tuliowachagua kwa hiari yetu
watuwakilishe katika vyombo vinavyotunga Katiba, Sheria na Sheria Ndogo, yaani
Bunge, Baraza la Wawakilishi, na Halmashauri za Jiji, Manispaa, Miji na Wilaya.
Kwa
hiyo sehemu ya kwanza ya utawala wa sheria ni kutungwa kwa Katiba na Sheria,
kazi inayofanywa na wawakilishi halali wa wananchi, waliopatikana kwa misingi ya
demokrasia, yaani kupitia uchaguzi huru na wa haki.
Na Katiba ikishatungwa, kwa mujibu wa sheria, pamoja na sheria nyingine
zinazotungwa kwa mamlaka yatokanayo na Katiba hiyo, wajibu wa raia, wajibu wa
jamii au kundi la watu, na wajibu wa Serikali, ni kukubali kutawaliwa na
kuongozwa na sheria katika maisha yetu, katika mahusiano yetu na katika utendaji
wetu wa kazi.
Na wajibu huo unamtaka kila raia kutii vifungu vyote vya Katiba na Sheria.
Maana, Katiba ina yote mawili – inatoa haki za raia, na inadai wajibu
kutoka kwa raia. Si ruksa hata
kidogo kutambua na kuheshimu vifungu vile tu vinavyokupa wewe haki, ukapuuza au
kutotii vile vinavyodai wajibu kutoka kwako.
Hivyo, sehemu ya pili ya utawala wa sheria ni kwa kila mtu, kila jamii,
kila taasisi na hata Serikali yenyewe, kutii sheria.
Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema
ifuatavyo:
“26
(1)
Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii Katiba
hii
na Sheria za Jamhuri ya Muungano.
(2)
Kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria, kuchukua
hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba na sheria za nchi.”
Kifungu
30(1) cha Katiba hiyo nacho kinasema ifuatavyo:
“30 (1)
Haki na uhuru wa binadamu ambavyo
misingi
yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana
ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu
wengine au maslahi ya umma.”
Ndugu
Wananchi,
Ni
wazi haiwezekani kila kifungu cha Katiba, au cha sheria, au cha sheria ndogo na
kanuni, kikamfurahisha kila raia. Hata
mwizi angetamani isiwepo sheria ya kuharamisha wizi na kutoa adhabu kwa kosa
hilo. Lakini, hakuna nchi yoyote duniani inayotoa ruksa kwa raia
kuheshimu na kutii vile vifungu tu vya Katiba, sheria, au sheria ndogo
anavyovitaka. Wajibu ni wa kutii
vifungu vyote. Kila mmoja akichagua
na kutii vile vifungu tu anavyovitaka, hatutakuwa tena na utawala wa sheria.
Na
kwa kujua kuwa si kila mtu ataridhika kuwa ametendewa haki, Katiba yetu
inaelekeza utaratibu wa kudai marekebisho ya utekelezaji wa sheria ili haki
itendeke. Kifungu 30 (3) cha Katiba
kimeweka jambo hili wazi kama ifuatavyo:
“30
(3)
Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika
Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au
wajibu kwake, limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote
popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu.”
Huo,
Ndugu Wananchi, ndio utaratibu halali, ndani ya mfumo wa utawala bora, utawala
wa sheria, ambao mtu au kundi lolote la watu ni ruksa kuutumia pale wanapoamini
kuwa sheria au Serikali haiwatendei haki. Narudia.
Huo ndio utaratibu pekee unaokubalika chini ya mfumo wa utawala wa sheria,
na hii ndiyo sehemu ya tatu ya utawala wa sheria.
Ndugu
Wananchi,
Sote
tuna wajibu wa kufuata sheria, na utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria
katika kudai haki, au katika kuhakikisha wengine nao hawavunji sheria. Atendaye kosa la jinai, avunjaye sheria, anastahili adhabu.
Lakini si kila raia, akiwemo raia mwema, ana haki ya kuamua kama
mtuhumiwa kweli amevunja sheria, na wala si kila raia ana haki ya kutoa adhabu.
Katika
mfumo wa utawala wa sheria raia anayo haki kumpeleka mtuhumiwa mbele ya vyombo
vya sheria, lakini hana haki ya kumhukumu na kumuadhibu.
Chini ya utawala wa sheria kila raia ana haki ya kukamata wahalifu na ana
wajibu akifanya hivyo kuwakabidhi Polisi. Jeshi
la Polisi ndio wanaochunguza uhalifu. Wakiridhika kuwa uhalifu umetendeka na
ushahidi upo watawafikisha wanaowatuhumu kufanya uhalifu huo mbele ya mahakama
zetu, zilizoundwa kwa mujibu wa Katiba na sheria.
Mahakama nayo baada ya kusikiliza pande zote mbili – upande wa mashtaka
na upande wa utetezi – ndiyo ina madaraka ya kisheria kuamua kama mtuhumiwa
ana hatia au la, na kama ana hatia kumpa adhabu ambayo nayo imewekwa kwa mujibu
wa sheria.
Ndugu
Wananchi,
Ili
kuhakikisha haki inatendeka, na utawala wa sheria unahimili mfumo wa utoaji haki,
hakuna taasisi yoyote moja iliyokabidhiwa madaraka yote ya kukamata, kuchunguza,
kushitaki, kutia hatiani, kuhukumu, na kutekeleza adhabu.
Kazi zote hizi zingefanywa na mtu mmoja, au taasisi moja tu ya dola,
ungekuwapo uwezekano mkubwa wa uonevu, na pengine uvunjwaji wa haki za msingi za
raia. Na sidhani yuko yeyote
miongoni mwetu ambaye angependa kupambana na mtu au taasisi yenye madaraka yote
hayo.
Lakini
wapo wenzetu ambao wao wanataka kuwa watu au taasisi za namna hiyo, zenye
madaraka makubwa kuliko Polisi, Mahakama na Magereza kwa pamoja.
Na hii ni pale wanapochukua sheria mikononi mwao.
Hii ni ile hali ambapo raia waliokerwa na uvunjwaji wa sheria, ikiwemo
wizi, unyang’anyi au uvunjaji nyumba, badala ya kutumia haki yao ya kisheria
ya kuwakamata na kuwafikisha mikononi mwa Polisi watuhumiwa, wao huamua kuwa
Polisi, Mahakama na Magereza kwa pamoja. Wanawakamata,
wanawahukumu na kuwaadhibu watuhumiwa, ikiwemo kwa kuwapiga, kuwachoma moto, na
pengine kuwaua. Vipo pia vitendo
vya kuua watu wanaodhaniwa ni wachawi, au yale mauaji yaliyotokea Kilosa ambapo
wananchi waliamua kupeana adhabu wenyewe kwa wenyewe bila kufikishana kwenye
mkondo halali wa sheria.
Ndugu
Wananchi,
Vitendo
hivyo vimenisikitisha na kunifadhaisha sana, na
vinazidi kunisikitisha na kunifadhaisha.
Tena vimeitia nchi yetu katika orodha ya nchi zinazovunja haki za
binadamu kwa njia hiyo. Maana,
tunahukumu watu kifo, tena kifo cha kikatili, bila kuwapa fursa yao ya kisheria
kupata utetezi wa kisheria. Na hata
kama wangekuwa na hatia, raia hawana madaraka ya kutoa hukumu, licha ya
kuitekeleza. Na zaidi ya hayo, mengi ya makosa ambayo yanawafanya
watuhumiwa wauwawe na raia waliochukua sheria mikononi mwao, adhabu yake, kwa
mujibu wa sheria zetu, si kifo. Napenda
niwaulizeni, Ndugu Zangu. Hivi
kweli ni sawa kutoa roho ya mtu kwa wizi wa mkufu wa dhahabu wenye thamani ya
sh.50,000/=? Tunakubali kushusha
bei ya uhai wa binadamu wenzetu kiasi hicho?
Tusisahau
pia kuwa mojawapo ya haki za msingi za kila raia, ni haki ya kuishi.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kifungu cha 14, inasema:
“14.
Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata kutoka kwa
jamii
hifadhi ya maisha yake, kwa mujibu wa sheria.”
Sasa
ni sheria gani inayompa raia, au kundi la raia, haki ya kutoa uhai wa mtu
mwingine, hata kama ameonekana akiiba? Mwizi
anastahili adhabu, jambazi anastahili adhabu, mnyang’anyi anastahili adhabu,
hata mchawi naye, akithibitika, anastahili adhabu, maana sheria ya kuadhibu
wachawi ipo pia. Lakini ni adhabu
zitokanazo na sheria, na zinazotolewa kwa mujibu wa sheria peke yake, si
vinginevyo.
Ndugu
Wananchi,
Leo
nimeona nizungumzie jambo hili maana vitendo vya watu kuuawa kwa tuhuma
mbalimbali na watu wanaochukua sheria mikononi mwao vinaongezeka kwa kasi sana,
na lazima sasa vikemewe kwa nguvu zote. Nimewauliza
Jeshi la Polisi juzi waniambie wanajua vitendo vingapi vya watuhumiwa kuuawa kwa
njia hii. Takwimu zinatisha.
Kwa
nchi nzima, kuanzia Januari hadi Desemba mwaka jana, vilitokea vitendo kama
hivyo 219, na kati ya hivyo, 66 (au 30%), vilitokea Dar es Salaam.
Na kuanzia Januari mwaka huu hadi sasa, ninaambiwa nchi nzima kuna
matukio 78 yaliyotolewa taarifa, kati yake 26 (33%) yakiwa yametokea Dar es
Salaam. Na hawa ni wale tu
waliouawa kwa tuhuma za wizi, ujambazi, uvunjaji na unyang’anyi.
Watuhumiwa wengine wa vitu kama uchawi hawamo kwenye orodha hii.
Kwa
vile wanaouawa ni wale wanaotuhumiwa kuwa ni wezi, wanyang’anyi au wachawi, si
wananchi wengi wanaowaonea huruma, hivyo ni wachache wanaozungumza kwa niaba yao
na familia zao. Lakini mimi ni Rais wa kila raia, akiwemo raia mhalifu.
Lazima nikemee tabia hiyo, lazima nimtake kila raia akubali kuongozwa na
wajibu wake wa msingi wa kutii sheria, na kuheshimu uhai wa raia wengine, japo
wawe wahalifu.
Najua
yapo malalamiko kuwa kuna rushwa kwenye vyombo vya haki na sheria, ikiwemo
Polisi na Mahakama, na ndio maana baadhi ya watuhumiwa wanaokamatwa wanaachiwa.
Pengine pia baadhi ya sheria zetu zinatoa mianya ya wahalifu kupenya.
Lakini kasoro za namna hiyo si jambo la ajabu katika ulimwengu wa
wanadamu, na ni vigumu kila wakati kuwa na sheria zinazokidhi kila hali na kila
dharura. Ndiyo maana tuna kazi
kubwa ya kushirikiana kusafisha rushwa kutoka kwenye vyombo vya sheria na utoaji
haki, na kubadili sheria mara kwa mara ili kukidhi mahitaji mapya.
Kasoro hizo kamwe haziwezi kuwa leseni ya wananchi kuchukua sheria
mikononi mwao na kuua wenzao.
Tusikubali
kurudi kwenye sheria za mwituni, tubaki kwenye mstari wa utawala wa sheria.
Tusitafute njia ya mkato ya kuadhibu wahalifu, tufuate njia ya uhakika wa
haki na utawala wa sheria, njia itakayoheshimu haki ya msingi ya kila raia, hata
awe mhalifu, ya kuwa hai. Haki
itafutwe ndani ya sheria, si nje ya sheria.
Maana kila mtu akitafuta haki nje ya sheria, hatutakuwa tena na utawala
wa sheria, na hivyo hatutapishana sana na wanyama.
Ndugu
Wananchi,
Nachukua
nafasi hii kuhimiza tena vyombo vya usimamizi na utoaji wa haki na sheria,
ikiwemo Polisi, Mahakama na Wanasheria, kuboresha utendaji wao ili wananchi
waone, na kuridhika, kuwa haki inapatikana kupitia vyombo hivyo, na si lazima
waitafute haki nje ya vyombo hivyo. Na
pili jitihada za kusafisha rushwa, uzembe, na ucheleweshaji wa utoaji haki,
zifanywe kwa ari na bidii mpya. Na
katika yote hayo, ushirikiano wenu wananchi ni muhimu sana. Mkikata tamaa, na
kuchukua sheria mikononi mwenu, hatutaimarisha utawala bora, utawala wa sheria,
na tutazidi kuonekana kama taifa la watu wasiostaarabika, wanaoishi kwa kufuata
sheria ya mwituni, badala ya utawala wa sheria.
Tuazimie
sasa, kwa pamoja, raia na vyombo vyote vya utoaji na usimamizi wa haki na sheria,
kukomesha vitendo vya raia kuchukua sheria mikononi mwao. Najua
sana uchungu wa kuibiwa, au kunyang’anywa mali; tena ni uchungu mkubwa sana.
Raia pia ana haki ya kujilinda na kulinda mali yake. Lakini pamoja na
yote hayo, tuupe uhai wa mtu mwingine thamani inayostahili, kama vile sisi nasi
tunavyothamini uhai wetu na wa familia zetu.
Ahsanteni
kwa kunisikiliza.
Mungu
Ibariki Afrika.
Mungu
Ibariki Tanzania.
HOTUBA
YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,
AKIFUNGUA MKUTANO WA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA MAGEREZA, CAPRICORN HOTEL,
MARANGU-MOSHI, 19 APRILI 2001
Waziri wa Mambo ya Ndani,
Mhe. Muhammed Seif Khatib, Mb;
Mkuu wa Magereza,
Kamishna Mkuu, O. E. Malisa;
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,
Mhe. Hilda Ngoye, Mb;
Makamanda wa Vikosi Mbalimbali vya Ulinzi
na Usalama;
Makamanda na Wajumbe wa Mkutano;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.
Kwanza
kabisa nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, pamoja na Kamishna
Mkuu wa Magereza, kwa mwaliko wenu wa kufungua mkutano huu muhimu.
Nawashukuruni pia makamanda na wajumbe wote kwa mapokezi mazuri mliyonipa
asubuhi hii. Shukrani za pekee ni
kwa wasanii waliotutumbuiza, na wakati huo huo kutupa ujumbe muafaka kwa siku ya
leo. Ni wazi kabisa kuwa Jeshi la
Magereza ni moja ya taasisi za dola zenye wasanii mahiri sana. Hongereni, na ahsanteni sana.
Mheshimiwa Waziri,
Furaha
yangu kuwa nanyi leo inatokana pia na ukweli kuwa hii ni mara yangu ya kwanza
kufungua mkutano kama huu wa Jeshi la Magereza.
Na kwa kweli sijawahi kukutana na uongozi wote wa juu wa Jeshi la
Magereza nchini kwa pamoja kama ilivyo leo.
Tumekawia, lakini sasa tumefika. Sababu za kuchelewa zinaeleweka; lakini
kwa wenye mashaka napenda kuwahakikishia kuwa mimi ni Amiri Jeshi Mkuu wa
Majeshi yote ya Ulinzi na Usalama. Sibagui
hata kidogo baina ya Jeshi moja na jingine.
Ndiyo
maana siku zote nimefuatilia kwa makini utendaji wenu, mafanikio yenu, na
matatizo yenu. Najua matatizo yenu
ni mengi, kama ilivyo kwa wenzenu katika majeshi mengine, na Serikalini kwa
ujumla. Leo pia nimekumbushwa
baadhi ya matatizo hayo.
Matatizo
ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Hata
mataifa tajiri duniani hayajaweza bado kumaliza matatizo yao yote, yakiwemo
matatizo ya vyombo vyao vya ulinzi na usalama.
Sembuse sisi ambao ni miongoni mwa nchi maskini kuliko zote duniani!
Lazima tujenge kwanza uwezo wa kuhimili gharama za mahitaji yetu muhimu
kwa njia endelevu.
Hivyo
nawapongezeni sana kwa uzalendo wenu na uvumilivu wenu, na kuendelea kufanya
kazi kwa bidii na maarifa katika mazingira magumu.
Kwa mtu anayejituma, mtu mwadilifu na mchapa kazi, matatizo ni changamoto
ya fikra mpya na ubunifu. Ninyi pia
mmejitahidi, si tu kuorodhesha matatizo yenu, bali pia kupendekeza mbinu na
mikakati ya kupunguza baadhi ya matatizo hayo. Sasa mjiandae kuyatekeleza kwa
ukamilifu yote mnayoazimia.
Mkifanya
hivyo mnaweza kupunguza matatizo yenu. Maana,
hainifurahishi hata kidogo kusikia mlolongo wa matatizo ambayo askari wetu na
maafisa wao wanapata. Ipo hadithi
ya Afisa Ustawi wa Jamii aliyetembelea gereza moja kuona hali ya wafungwa. Moyo wake ukaguswa sana na hali ya huzuni aliyokuwa nayo mtu
mmoja aliyemuona pale gerezani. Akamwendea.
“Pole
sana bwana”, akamwambia, “Kifungo chako ni cha muda
gani?”
“Inategemea
wakubwa wangu, Mama,” akajibu mtu yule. “Mimi
ni
askari
jela tu hapa”.
Ubunifu
na Kujituma
Mheshimiwa
Waziri,
Tusikubali
kufika mahali ambapo askari wetu wanakuwa wanyonge, kama vile na wao wapo jela.
Lakini, narudia. Matatizo ni
sehemu ya maisha, na unapokuwa maskini lazima ukubali kuwa matatizo yako
yatakuwa makubwa zaidi, yanayohitaji ubunifu zaidi na uvumulivu zaidi wakati
tunajenga uwezo wa kuyapunguza. Maana,
tulichopungukiwa si nia; tulichopungukiwa ni uwezo.
Tatizo
la nyumba za kuishi askari, kwa mfano, mimi linanigusa sana, hasa nikiangalia
wake na watoto wao. Mmesema zaidi ya askari na maafisa 6900 hawana nyumba za
kuishi kambini. Ni vigumu
kumaliza upungufu wa kiasi hicho kwa mara moja.
Lakini nina hakika mkiiga utaratibu uliotumiwa na Jeshi la Polisi
kupunguza tatizo kama hilo, na kwa kutumia ufundi na nguvukazi iliyo ndani ya
Jeshi la Magereza, tutaanza kupunguza tatizo hili.
Ubunifu
katika kushughulikia matatizo yetu ni jambo la lazima, maana uwezo wa Serikali
hautoshi. Hivi sasa mapato yetu ya
ndani, yanayotokana na nguvu ya uchumi wetu na kodi zitokanazo na uchumi huo, ni
wastani wa Sh.700 bn tu kwa mwaka. Na
hii ni baada ya juhudi kubwa ya kuongeza makusanyo na kuziba mianya ya kukwepa
kodi. Miongoni mwa kazi ngumu sana
Serikalini, na hasa wakati huu tunapoanza kuandaa bajeti ya mwaka wa fedha ujao,
ni kutafuta utaratibu bora wa kugawana kiasi hiki.
Ni kazi ya kugawana umaskini, na wakati mwingine tunaishia kulipa watu
mishahara bila kuwapa vitendea kazi. Hivyo
wanalipwa kwa vile tu wameajiriwa, si kwa vile kuna kazi ya kujenga taifa
wanayoifanya.
Najua
ninyi wa Jeshi la Magereza mmekuwa mkipata wastani wa 50% ya mahitaji halisi
mnayopeleka Serikalini kama makisio yenu. Kwa
mgao unavyokwenda, kiwango cha 50% si kibaya hata kidogo.
Wapo wengine wanaopata chini ya hapo.
Ni
vizuri mfahamu pia kuwa hivi sasa tunawania kusamehewa baadhi ya madeni yetu ya
nje ya nchi. Lakini ili uamuzi huo
ufikiwe lazima tuonyeshe kuwa tuko makini katika mpango wetu wa kupunguza
umaskini. Mojawapo ya vigezo vya
umakini vinavyokubalika ni kiasi cha bajeti ya Serikali kinachoelekezwa kwenye
maeneo muhimu katika mkakati wa kupiga vita umaskini, kama vile elimu, afya, na
huduma nyingine za jamii. Vyombo
vya ulinzi na usalama, ikiwemo Jeshi la Magereza, si mojawapo.
Huo ndio ukweli, na hapo ndipo pa kuanzia kama tunataka kupata ufumbuzi
wa kudumu wa baadhi ya matatizo yetu.
Nikianzia
hapo mimi mwenyewe, naona kuna njia tatu za kukabiliana na matatizo yetu.
- Ya
kwanza, ni kuboresha usimamizi wa bajeti;
- Ya
pili, ni kupunguza idadi ya wafungwa; na
- Ya
tatu, ni kuongeza uwezo wa Jeshi la Magereza kujitegemea.
Usimamizi
wa Bajeti
Ndugu Wajumbe,
Kwa
miaka mingi kumekuwapo Serikalini mtindo wa kuandaa bajeti ambazo hazilingani na
hali halisi – hali halisi ya mapato na hali halisi ya vipaumbele vya matumizi.
Kwa vile inajulikana kuwa Wizarani, na hatimaye Wizara ya Fedha,
wanapunguza makisio ya Idara na taasisi nyingine, makisio ya awali yanakuzwa mno
kwa dhana kuwa kiasi kitakachobaki baada ya kupunguzwa na HAZINA ndicho
kitatosha. Lakini kwa vile HAZINA
wanajua mchezo huo, nao hukata tu pengine bila kuzingatia mahitaji halisi
yasiyokwepeka, kama vile chakula na nguo kwenye majeshi yetu.
Kuanzia
sasa tunataka kila sehemu wawe makini zaidi kwenye kuandaa makisio yao ya
matumizi. Lazima kuwe na uwiano
mzuri zaidi baina ya mishahara na marupurupu mengine, na vitendea kazi.
Aidha, lazima kuwe na bajeti zinazolingana na hali halisi kwa yale mambo
ambayo hayaepukiki. Nimeona, kwa mfano, kuwa baada ya jitihada zote za kupunguza
madeni ya ndani, bado kati ya Julai 1998 hadi Desemba 2000 Jeshi la Magereza
peke yake tayari mmepeleka HAZINA kwa uhakiki na kulipwa madeni mapya ya
wazabuni na ya watumishi ya Sh.10.5 bn!! Maelezo
yake yanaweza kuwa ya aina mbili tu. Ama
makisio ama maidhinisho yetu ya yale matumizi ambayo hayakwepeki yalikuwa sio
sahihi, au fedha iliyopo ilitumika kwa mambo mengine, na kwa yale ambayo kila
mtu anajua ni matumizi yasiyokwepeka, tunakopa.
Nasema sasa lazima tuboreshe maandalizi ya bajeti zetu ili matumizi
yasiyokwepeka yapewe fedha za kutosha, zinazotumika kwa mambo hayo tu.
Lakini
pia lazima kuimarisha usimamizi wa matumizi ya fedha kidogo inayopatikana.
Baba wa Taifa alituasa miaka mingi iliyopita kuwa “Kupanga ni Kuchagua”.
Lazima sasa tuizingatie kwa makini kabisa dhana hiyo.
Kwa umaskini wetu, yapo mambo mengi mazuri, ya muhimu, ambayo tutashindwa
kuyafanya. Hivyo lazima kukubali
wajibu wa kuchagua, tena kwa misingi ya vipaumbele vinavyozingatia maslahi ya
taifa, haki za binadamu, na uwezo uliopo.
Lakini
hivi sasa bado tunalo tatizo kubwa la kulipa madeni makubwa ya wazabuni, stahili
za askari na madeni ya kantini, maduka ya Magereza na Shirika la Magereza.
Pamoja na jitihada za kuweka utaratibu mzuri ili malimbikizo ya aina hii
yasitokee tena, lazima tuendelee na jitihada ya kuhakiki madai yaliyopo na
kutafuta uwezo wa kuyalipa. Madai
ya haki, yaliyohakikiwa, hayana budi kulipwa.
Sisi ni maskini, lakini Serikali yetu si ya kihuni.
Kila uwezo ukipatikana tutalipa madeni yetu ya ndani.
Tayari
yapo madeni ambayo yamekwisha kulipwa. Kwa
mfano, kwa madeni hadi 30 Juni 1998, Jeshi la Magereza lilipeleka HAZINA madai
ya Sh.6.6 bn, na baada ya uhakiki kiasi cha Sh.5.6 bn kilionekana kinastahili
kulipwa. Hadi sasa tumefanikiwa kulipa Sh.4.5 bn, na ni Sh.1.1 bn tu
bado hazijalipwa. Jitihada
zinaendelea kutafuta fedha za kumalizia deni hili la kipindi cha hadi Juni 1998.
Kwa
madeni ya Sh.10.5 bn kwa kipindi cha Julai 1998 hadi Desemba 2000 hivi sasa kazi
ya uhakiki inaendelea. Kazi hiyo ilianza mwishoni mwa mwezi uliopita, na hadi wiki
jana madai 6,662 kati ya 48,145 yameshughulikiwa.
Aidha,
baada ya kugundua kuwa madeni mengi ya wazabuni ni ya chakula, tuliamua kuwa
Jeshi la Magereza lipate chakula moja kwa moja kutoka Akiba ya Nafaka ya Taifa (SGR).
Hatua hii ninaamini itapunguza sana ongezeko la madeni ya wazabuni kama
ilivyokuwa huko nyuma. Tutaangalia
uwezekano wa kuendeleza utaratibu huu siku zijazo.
Kwa
upande wa madeni yatokanayo na Kantini ya Magereza, Maduka ya Magereza na
Shirika la Magereza (Corporation Sole),
pamoja na stahili za askari, nadhani kiasi kikubwa kimekwisha kulipwa.
Kazi inayoendelea hivi sasa ni kuhakiki madeni yaliyobaki, na kisha
kutafuta uwezo wa kuyalipa pia.
Lakini
narudia. Utaratibu huu wa
kulimbikiza madeni si mzuri, na si sahihi hata kidogo. Lazima baada ya kumaliza
kulipa madeni hayo tuwe tumeridhika kuwa tunao sasa utaratibu wa kuhakikisha
hatuingii tena kwenye madeni makubwa kiasi hiki.
Idadi ya
Wafungwa
Mheshimiwa Waziri,
Ni
jambo la kusikitisha sana kwamba magereza yetu yamefurika, na kusababisha
mlundikano mkubwa wa wafungwa kuliko uwezo wake.
Uwezo uliopo ni wafungwa 21,000 tu, lakini waliopo ni 45,000, yaani zaidi
ya mara mbili ya uwezo.
Jibu
rahisi kwa nini mlundikano huo upo ni kwamba tangu Uhuru hatujajenga magereza
mpya.
Ni kweli tunahitaji magereza mapya, hasa kwa wilaya mpya ambazo hivi sasa
zinalazimika kuchangia magereza na wilaya jirani. Lakini pia yapo maswali ya msingi ya kujiuliza:
- Kwa nini idadi ya wafungwa inaongezeka?
- Hivi ni lazima wahalifu wote wafungwe? Hakuna adhabu nyingine?
Mheshimiwa Waziri,
Wafungwa 45,000 walio gerezani ni asilimia 0.14 tu ya Watanzania, hivyo
ni rahisi kusema kuwa wafungwa hao si wengi sana.
Lakini ni ukweli pia kuwa
uhalifu unaongezeka, sambamba na mageuzi ya kiuchumi na kijamii.
Lazima kama jamii tulichunguze suala hili, kuona chanzo chake, na namna
bora ya Serikali na wananchi wanavyoweza kushirikiana kulishughulikia.
Maana ni wazi mageuzi haya yanaongeza tofauti ya mapato katika nchi yetu,
na maisha ya wenye mali yanaongeza tamaa miongoni mwa hata wale ambao hawana
uwezo wa maisha hayo. Aidha,
maendeleo ya teknolojia yanatuonyesha sisi sote, hata wale fukara kabisa, maisha
ya kisasa na kifahari waishiyo wengine duniani.
Tamaa ya mali ni chanzo kikubwa cha uhalifu nchini – iwe udokozi, wizi
wa kutumia silaha, wizi wa kalamu, biashara ya madawa ya kulevya au rushwa.
Uhalifu mwingi chanzo chake ni kutafuta njia ya mkato ya maisha bora
zaidi. Peke yetu Serikalini hatuna
jibu jepesi; lakini kama jamii ya Watanzania hatuwezi kukwepa wajibu wa
kutathmini hali hii na kutafuta njia za kuwezesha wananchi kuboresha maisha kwa
jasho lao, na kwa njia halali. Kazi hiyo lazima ianzie kwenye kaya, kwenye kijiji, shuleni,
na ndani ya jamii kwa ujumla, ikiwemo kwa kutumia ushawishi wa viongozi wa jamii,
na hasa viongozi wa dini.
Viongozi wa kisiasa, hususan viongozi wa vyama vya upinzani, nao hawana
budi kujishughulisha na tatizo hili. Haki
za binadamu ni pamoja na haki za binadamu walio kifungoni.
Lakini kama magereza yetu yataendelea kubebeshwa mzigo wa kuhudumia
wafungwa wengi mara mbili ya uwezo wake ni vigumu kuwapa wafungwa hao huduma na
haki wanazostahili kama wanadamu wengine. Hivyo
pamoja na kuwaita vijana, na watu wengine wasio na njia za uhakika za mapato,
kwenye mikutano ya hadhara na maandamano ya kudai Katiba mpya, na madai mengine
ya kisiasa, ingekuwa bora vilevile kubuni mipango na miradi ya kuwasadia kupata
mapato ya uhakika, na hivyo kuepuka kuishia kwenye magereza yanayofurika.
Haitoshi kuwajaza pumzi za kisiasa, kuwatumia kwa malengo ya kisiasa, na
kuwashibisha chuki dhidi ya Serikali. Hatimaye
wanahitaji utulivu utakaochangia uchumi ukue na fursa za kujiondoa kwenye
umaskini kupatikana, na kuwashibisha chakula.
Pamoja na hayo lazima kama jamii tutafakari upya dhana ya kufunga mtu
jela. Na hapa tena yapo maswali
kadhaa ya msingi ya kujiuliza.
- Je, tunafunga mhalifu ili kumuadhibu, au ili kumtenga na jamii?
Kwa wale wahalifu ambao hawaleti hatari yoyote kwa jamii, je ni
lazima adhabu yao pia iwe kifungo, tena kifungo cha jela?
- Je, ni lazima tuwe na idadi kubwa hivi ya mahabusu?
Ni kiasi gani kuharakisha kupeleleza na kusikiliza kesi kutapunguza
mlundiko wa wafungwa?
- Je, ni lazima kila mfungwa atumikie kifungo chake chote hata pale
anapoonekana dhahiri kuwa hatahatarisha jamii, amejirudi na ana tabia njema?
- Je, tunapofunga mhalifu lengo letu ni kumuadhibu tu, kumtenga na
jamii tu, au vilevile ni kumrekebisha aache uhalifu na kuwa raia mwema?
Ndugu Mwenyekiti,
Nauliza maswali hayo kwa makusudi kabisa ili kama taifa tuanze kujiuliza
maswali ya msingi kuhusu mfumo na utaratibu wetu wa kuadhibu wahalifu.
Binafsi, ninaamini tunafunga watu wengi mno bila sababu, na kujibebesha
mzigo mkubwa unaotushinda sasa, kwa vile tumezoea utaratibu tuliorithi kwa
wakoloni wa kulundika wahalifu wote jela bila kupima kila mhalifu, na kuupima
kila uhalifu.
UTARATIBU HUO UMEJENGWA JUU YA DHANA POTUFU KUWA KILA MHALIFU ANASTAHILI
KUFUNGWA, CHINI YA ULINZI WA ASKARI JELA. UPO
MSEMO KUWA ASKARI MAGEREZA HUPOKEA WAGENI AMBAO HAKUNA MWINGINE ANAYEWATAKA.
LAKINI, HASA KWA WALE WAGENI AMBAO SI HATARI KWA JAMII, WAKATI UMEFIKA WA
KUWAPA ADHABU BILA NA SISI WENYEWE KUJIADHIBU KWA KUJITWISHA UGENI UNAOTUSHINDA.
Kijana anaiba kuku mmoja mwenye thamani ya Sh.2,000/= kisha anakaa
rumande, na hatimaye anafugwa. Nimeambiwa
gharama ya kumlisha mfungwa mmoja kwa siku ni Sh.730/=. Hivyo akifungwa miezi sita, kwa kosa la kuiba kuku wa
Sh.2,000/=, Serikali inaingia gharama ya Sh.131,400/=.
Hivi hasa aliyeadhibiwa hapa ni nani, ni mwizi au ni Serikali?
Dhahiri tunahitaji mfumo wa adhabu ambao ni nafuu zaidi. Isitoshe, kijana
huyo anafungwa na majambazi sugu wanaoweza kumkomaza zaidi kwenye uhalifu.
Nafurahi kuwa hapa nchini, kama ilivyo duniani kote, maswali yanaulizwa
iwapo adhabu ni jela tu. Na takwimu
zinaonyesha kuwa si wahalifu wote wanaogopa jela.
Maana, kati ya asilimia 12 – 15 ya wafungwa wote wanarudia uhalifu, na
kujikuta wanarejea jela kila mwaka. Takwimu
pia zinaonyesha kuwa wengi wao ni wale wenye vifungo vifupi, chini ya miaka 5.
Hawa ni wale wenye makosa madogo madogo ambao wangeweza kutafutiwa adhabu
nyingine badala ya kulundikwa gerezani ambako inaelekea wanapazoea, na pengine
kujifunza uhalifu zaidi badala ya kujirekebisha.
Hao ni kama yule mfungwa aliyecheleweshwa kuachiwa kwa wiki nzima baada
ya kumaliza kutumikia kifungo chake. Afisa
wa Magereza anayehusika alipogundua kosa hilo alimtaka radhi ifuatavyo:
“Tuwie radhi, Bwana. Tumechelewa
kukuachia kwa wiki nzima”, alisema.
“Usijali, Afisa. Hiyo wiki
nakukopesha. Utaikata nitakaporudi”.
Lazima
sasa kubuni utaratibu wa kuadhibu wahalifu kwa njia itakayosaidia zaidi
kuwarekebisha, si kuzidi kuwatumbukiza kwenye uhalifu, na bila kuibebesha
serikali gharama kubwa mno. Ningependa
Wizara ya Mambo ya Ndani, kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza, na kwa
kuzingatia uzoefu wa nchi nyingine, walete haraka Serikalini mapendekezo ya
mabadiliko ya sheria yatakayowezesha wahalifu ambao hawana hatari yoyote kwa
jamii watumikie vifungo vyao nje, na watumikie jamii kama sehemu ya adhabu yao.
Tutathmini pia mara kwa mara utaratibu wa kupunguziwa vifungo vya ndani (Parole),
kwa lengo la kuuboresha zaidi.
Napenda
nitumie fursa hii kutoa wito kwa wananchi kwa ujumla kuyakubali mabadiliko
tunayokusudia kuyafanya kwani tunayafanya kwa nia njema kabisa ya kuboresha
mfumo wetu wa sheria na haki. Serikali
itahakikisha kuwa tahadhari zote zinachukuliwa ili kuzingatia kwa ukamilifu
lengo kuu la kulinda na kuimarisha usalama wa jamii.
Natoa wito huo kwa sababu ni wajibu wangu; lakini natambua pia kuwa
mafanikio ya sera au sheria zinazohusu masuala ya kijamii kama haya hutegemea
sana kueleweka na kukubalika kwake na jamii yenyewe.
Kwa hiyo nawatakeni ninyi Makamanda wa Jeshi la Magereza muwe mstari wa
mbele nchi nzima kuielimisha jamii ipasavyo kuhusiana na mambo haya kama
mojawapo ya kazi zenu na mikakati yenu ya utekelezaji wa mipango
mtakayokubaliana hapa.
Ningependa
vyombo vya habari navyo vitusaidie kujenga hoja ya kupunguza mlundikano wa
wafungwa. Tatizo hili si letu peke
yetu. Duniani kote tatizo hili lipo
na kila nchi imejaribu kutafuta mfumo wa adhabu utakaolipunguzia taifa lao
gharama, na wakati huo huo kuongeza uwezekano wa wafungwa kujirekebisha.
Hivyo ni vizuri tukajifunza pia kutokana na uzoefu wa wengine. Miongoni mwa mifano mliyonipa ni uzoefu wa nchi jirani ya
Kenya, na pia nchi za Afrika Kusini na Namibia.
Nchini Kenya, kwa mfano, walianza kutumia rasmi utaratibu wa Adhabu ya
Kutumikia Jamii (Community Service)
mwezi Desemba, 1999, na hadi kufikia mwanzoni mwa mwaka huu tayari watu 20,000
walishahukumiwa kufanya kazi za huduma za jamii kwenye shule, hospitali,
halmashauri za miji, na mashambani. Utaratibu
huo uliokoa fedha nyingi ambazo Serikali ingelipa kwa ajili ya huduma hizo.
Aidha, watu hao 20,000 waliepuka kwenda gerezani ambako si tu Serikali
ingetumia fedha za walipa kodi kuwatunza bali pia wangekumbana na adha ya maisha
magumu gerezani, na wengi wao
kuharibiwa tabia na wafungwa sugu tunaowatenga na jamii kwa kuwaweka gerezani.
Lakini suala la msingi zaidi pia ni kwamba watu
hao wameweza kutumikia adhabu zao huku wakiendelea kuishi na familia zao ambazo
zingekuwa katika matatizo makubwa kama wangelifungwa gerezani.
Kwa upande wa Afrika ya Kusini, wafungwa waliokuwa gerezani mwaka jana
walikuwa wastani wa 162,000 kwa siku, wakati waliokuwa wakitumikia adhabu zao
kwenye jamii chini mipango ya Community
Service, Parole na Probation
walikuwa ni wastani wa 61,000 kwa siku. Hii
ni sawa na asilimia 38 ya walio jela. Kama
mipango hii isingelikuwepo, ina maana kwamba watu hao wote wangelikuwa gerezani.
Hali kadhalika huko Namibia, ambao ninyi ndio mmewasaidia kuanzisha Jeshi
la Magereza la Namibia huru, waliokuwa gerezani mwaka jana walikuwa wastani wa
5,700 kwa siku, wakati wale waliokuwa nje kwenye adhabu za Parole
walikuwa ni wastani wa 730 kwa siku, sawa na asilimia 13 ya walio jela.
Kwa mifano hii hai, nadhani wananchi wataelewa umuhimu wa kuwepo kwa
mabadiliko kwenye mfumo wetu wa adhabu hapa nchini.
Kuongeza Kujitegemea
Mheshimiwa
Waziri,
Sana nizungumzie ile njia ya tatu ya kupunguza matatizo ya Jeshi la
Magereza, nayo ni kuongeza uwezo wa kujitegemea.
Tunaweza kabisa kutumia wafungwa vizuri zaidi, wakazalisha mali zaidi, na
mzigo wa Serikali katika kuhudumia wafungwa ukapungua zaidi.
Hakuna sababu kwa nini nguvukazi ya wafungwa isitumike kikamilifu, na
badala yake kodi za raia wema zitumike kuwatunza wao.
Kwa kuanzia, ningependa yawepo mawasiliano na mashauriano Wizara
zinazosimamia sekta ambazo Jeshi la Magereza lina uzoefu nazo, na uwezo wa
uzalishaji mali au utoaji huduma. Wizara
hizo ni kama vile Wizara ya Kilimo na Chakula, Wizara ya Maji na Mifugo, Wizara
ya Viwanda na Biashara, na kadhalika. Lengo
la mashauriano hayo liwe kutafuta njia muafaka za kutumia nguvukazi ya wafungwa.
Mojawapo ya mambo ambayo lazima mjiulize ni kwa nini kusiwe na uzalishaji
endelevu kwenye kilimo, ufugaji, au viwanda vidogo vidogo vya Jeshi la Magereza.
Tutafute sasa mbinu za kuyafanya mashamba yanayotegemea nguvukazi ya
wafungwa yazalishe ziada itakayotumika kununulia zana za kilimo, madawa, na
pembejeo nyingine. Miradi ya kilimo,
ufugaji, na viwanda inaweza kujitegemea badala ya kungojea bajeti ya Serikali.
Tubuni njia za kuifanya miradi hiyo ipate faida na ziada ya kutosha
kununua zana, kama vile trekta, na kugharamia ukarabati wake.
Bila hivyo nina wasiwasi miradi ya Jeshi la Magereza inaweza kugeuka kuwa
kama mashirika ya umma, pamoja na matatizo yote yaliyoua mengi ya mashirika hayo. Ndio maana naunga mkono wazo la kuanzisha ubia na sekta
binafsi katika kuendesha miradi hiyo ili kuimarisha nidhamu na usimamizi kwa
misingi sahihi ya biashara.
Ninachotaka ni kuwa miradi hiyo iwe chanzo cha mapato, bila kutegemea
kwanza ruzuku za Serikali. Hoja
inaweza kujengwa kuwa miradi hiyo ipewe kipaumbele katika kupewa kazi au zabuni
za Serikali. Kwa nini, kwa mfano, mashamba ya Magereza yasipate zabuni za
kulisha shule, au majeshi mengine, kwa mkataba? Vivyo hivyo kwa samani za Serikali na Idara zake.
Maana kila mwaka kwenye Maonyesho - ama ya Kilimo au ya Kimataifa -
ninaonyeshwa mfano wa kilimo bora, na vifaa vizuri vinavyotegenezwa na Magereza.
Mafanikio hayo yanaweza yakajitafsiri katika uzalishaji wa kibiashara na
faida.
Hapa lazima pia niungane nanyi katika kudai kuwa wale wanaonunua bidhaa
zenu, au huduma mbalimbali, wawalipe, tena kwa wakati.
Magereza wanastahili kulipwa sawa na wazabuni au wadai wengine.
UKIMWI
Mheshimiwa
Waziri,
Kama ilivyo ada yangu siku hizi, kwa masikitiko makubwa, inanibidi
nizungumzie maradhi mabaya ya UKIMWI yanayohatarisha maendeleo, ustawi na
hatimaye uhai wa jamii zetu na taifa kwa jumla.
Mojawapo ya matatizo yenu ni upungufu wa askari, ambapo nasikia mna
upungufu wa askari zaidi ya 6,500. Nina
uhakika vifo vinavyotokana na UKIMWI vimechangia kwa kiasi kikubwa upungufu huo.
Tatizo la UKIMWI ni mzigo mkubwa kwa taifa, maana tunapoteza vijana
tuliowasomesha kwa gharama kubwa, na ambao mchango wao katika ujenzi wa taifa na
malezi ya familia zao unahitajika sana. Ni
wazi kabisa kuwa majeshi yetu yote ya ulinzi na usalama ni mojawapo ya taasisi
zilizoathirika sana.
Kwa waliofariki, hatuna budi kujenga hoja, ninayoiunga mkono, ya
kuajiriwa wengine badala yao. Lakini
ufumbuzi wa kudumu ni kufanya bidii kubwa zaidi kuzuia maambukizi ya UKIMWI
katika jamii, na hususan katika majeshi yetu.
Kwa vile kwa kiasi fulani tabia ya mtu huchangia ama kuambukizwa, au
kupona, tunayo kazi kubwa ya kufanya ya kuelimishana na kukumbushana bila
kuchoka, kwa lengo la kubadili tabia, na kwa lengo pia la kujikinga kwa
ukamilifu kwa wasioweza kujizuia vitendo vinavyoeneza virusi vya UKIMWI.
Na kwenu wa Jeshi la Magereza mnao wajibu mkubwa pia kuzuia kuenea kwa
virusi vya UKIMWI kwa wananchi mliokabidhiwa kuwahifadhi, yaani wafungwa.
Kweli wameadhibiwa kwa uhalifu wao; lakini UKIMWI si sehemu ya adhabu yao.
Wao bado ni Watanzania wenzetu, ni ndugu zetu na ni jamaa zetu.
Uhalifu wao haufuti ukweli huo. Wao pia ni sehemu ya jamii – wametoka
kwenye jamii na wakimaliza vifungo vyao watarejea kwenye jamii.
Hivyo, katika vita vyetu dhidi ya UKIMWI hatuwezi kuwasahau wao pia.
Ningependa mshirikiane na Tume ya Taifa ya UKIMWI kubuni namna bora ya
kufikisha ujumbe wa UKIMWI kwa wafungwa wote, na namna ya kuzuia kuenea kwa
maradhi hayo kwenye jela zetu. Mimi
napinga sana mfumuko wa semina na warsha nchini; lakini kwa jambo hili natoa
ruksa ifanyike warsha maalum ya namna ya kukabiliana na tatizo la UKIMWI, na
magonjwa kama vile TB, matumizi ya madawa ya kulevya, na kadhalika, katika
magereza yetu. Warsha hiyo hatimaye
iandae mkakati maalum unaohusisha washika dau wote wa kupambana na UKIMWI kwenye
Jeshi la Magereza, na miongoni mwa wafungwa.
Hitimisho
Mheshimiwa
Waziri,
Napenda nimalizie kwa kuwasomea muhtasari wa kumbukumbu za mkutano mmoja
wa Wakaguzi wa Magereza, katika nchi ambayo sitaitaja.
Baada ya kupokea malalamiko mengi ya viongozi wa Magereza, na kujionea
hali halisi ya gereza mojawapo, wakaguzi hao, katika mkutano wao, wakaazimia
ifuatavyo:
- Imeamuliwa, kwamba gereza lililopo
halitoshi, na kwamba jingine lazima lijengwe.
- Imeamuliwa, kwamba vifaa vya ujenzi
vya gereza lililopo ndivyo hivyo hivyo vitumike kujengea gereza jipya.
- Imeamuliwa, kwamba gereza la zamani
lisibomolewe kwanza mpaka jipya likamilike.
Ndugu Wajumbe,
Ninachotazamia kutoka kwenu katika mkutano huu si utambuzi tu wa mambo
mengi mazuri, ya muhimu, yanayopaswa kufanywa, kwa uwezo wa fedha na nyenzo
ambao haupo. Tofauti na wenzenu hao, nadhani mnaweza kuelewana vizuri
zaidi namna ya kuongeza ubunifu, kujituma zaidi, na kuandaa mapendekezo
yatakayosaidia kupunguza ukali wa matatizo, na kuiwezesha Serikali kuchangia
mafanikio yenu vizuri zaidi. Nitangojea
kwa hamu kuona mapendekezo hayo, ambayo naahidi tutayazingatia na kuyatafakari
kwa uzito unaostahili.
Na sasa napenda kutangaza kuwa Mkutano huu wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi
la Magereza umefunguliwa rasmi.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.
HOTUBA
YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,
KWA WANANCHI,
31 MACHI 2001
Ndugu
Wananchi,
Ni wajibu wangu kuzungumza nanyi mara kwa mara juu ya mambo au maamuzi ya
msingi Serikali inayoyafanya kwa niaba yenu.
Tunataka kujenga katika nchi yetu misingi ya demokrasia ya kweli, ambapo
kila kiongozi mmoja mmoja, na kwa ujumla wao kama Serikali, katika kila ngazi ya
utawala, watazingatia na kutekeleza wajibu wao wa kuwajibika kwenu wananchi.
Demokrasia ya kweli si uhuru wa kupiga siasa za domo kaya maradufu.
Kielelezo cha demokrasia ya kweli ni utawala unaotokana na ridhaa ya wananchi,
na unaowajibika kwa dhati kwa wananchi; utawala unaozaa matunda, kwa faida ya
wananchi walio wengi.
Mmesikia kuwa hivi karibuni nimefanya mikutano na semina mbalimbali na
viongozi wakuu wote wa Serikali kule Dodoma.
Tarehe 15 na 16 Februari nilikaa na Mawaziri, Naibu Mawaziri, na Makatibu
Wakuu wote. Tarehe 19 mpaka 22
Machi niliwaongeza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, na
Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa na Jiji. Na, tarehe 23 na
24 Machi, tuliwahusisha wawakilishi wa washika-dau wa sekta ya kilimo, taasisi
za fedha na wahisani kwenye sekta hiyo.
Ndugu Wananchi,
Mnayo haki ya kuuliza kwa nini niliamua
kufanya hivyo. Maana, gharama ya
mikutano hiyo ni kubwa na imelipwa na mapato yatokanayo na kodi zenu.
Zipo sababu kadhaa, na madhumuni maalum.
·
Kwanza, baada ya Uchaguzi Mkuu nimefanya uteuzi wa viongozi wapya.
Wao, na wale wa zamani, ilibidi tukae pamoja ili kuelewana,
na kuwa na mwelekeo mmoja, kuhusu
kazi wananchi mliyotutuma tuifanye, nayo ni kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM,
kwa maendeleo na manufaa ya wananchi wote;
·
Pili, ilikuwa muhimu kuelewana namna bora ya kujipanga kimuundo na kiutendaji ili kufikia malengo ya jumla
tuliyojiwekea katika kupiga vita umaskini na kuharakisha maendeleo;
·
Tatu, ilitupa fursa kujadili suala la uwezeshaji ili kufikia
malengo hayo muhimu, hasa yale yatakayoimarisha na kudhibiti uhuru wetu na
maendeleo yetu, tukianzia na kujijengea uhakika wa chakula;
·
Nne, nilitaka kusisitiza tena umuhimu wa viongozi katika ngazi zote,
kila mmoja, na kwa umoja wao, kutambua kuwa wana wajibu wa uwezeshaji, na wajibu
wa kuwa chachu ya maendeleo na vita dhidi ya umaskini hapo walipo na kuwajibika
ipasavyo kwa wananchi; na
·
Tano, nilitaka tuelewane juu ya dhana na umuhimu wa utawala bora na
demokrasia ya kweli katika kila ngazi, hadi ngazi ya kijiji, ili kazi tuifanyayo
hivi sasa ya kupeleka madaraka karibu zaidi na wananchi ilete matunda
yaliyokusudiwa.
Ndugu Wananchi,
Mikutano yote hiyo ilifanikiwa sana.
Viongozi wenu wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri wanaporejea kwenye maeneo
yao ya kazi ninaamini wanakuja na ari mpya, mwelekeo mpya, ushirikiano mpya, na
msisitizo sahihi wa masuala yote ya msingi tuliyoyazungumza. Nawaombeni sana,
Ndugu Wananchi, mshirikiane nao ili mrahisishe kazi yao, ikiwemo kazi ya
kusimamia utawala bora, usimamizi wa sheria, kuongoza vita dhidi ya umaskini na
kuwajibika kwenu. Nitazungumzia
baadaye kidogo baadhi ya yale ambayo ningependa wananchi nanyi myafanye.
Lakini kwanza niwajulishe machache tu ya hayo masuala ya msingi
tuliyoyajadili, kuelewana, na kuyawekea mikakati ya utekelezaji.
·
Tumejadili malengo mahsusi katika
vita dhidi ya umaskini, tukayawekea vipindi maalum vya utekelezaji, na
kubainisha vigezo na viashirio vya utekelezaji. Malengo ya kitaifa yatagawanywa sasa katika malengo ya kila
mkoa, wilaya na hata kijiji; na nimeagiza niwe napata taarifa ya utekelezaji
kila mwaka. Bila tathmini za kila
mwaka, katika kila ngazi, hatutajua kwa hakika iwapo tunapiga hatua mwaka hadi
mwaka, katika vigezo muhimu vya vita dhidi ya umaskini na kuchochea maendeleo.
Viongozi wenu watakuja kushirikiana nanyi kutathmini kero zenu, kuona raslimali
mlizo nazo, kubuni mipango ya kuondoa kero kwa kutumia raslimali hizo, kugawana
majukumu ya utekelezaji, na kuona wapi ni lazima mchango wa Serikali au wahisani
utafutwe. Maendeleo ya kweli na
endelevu ni yale yatakayotokana na utaratibu wa mipango shirikishi ya kijamii,
ambapo kazi ya Serikali na wahisani ni kuongeza uwezo wenu wa kuyatekeleza yale
mliyoamua wenyewe. Tunataka mipango ya maendeleo sasa ianzie kwenu wananchi,
badala ya kuanzia Serikalini, lakini kwa kuzingatia kikamilifu malengo yetu ya
kitaifa na kimataifa katika kupiga vita umaskini;
·
Pili, tumezungumzia sera mpya ya maendeleo
vijijini inayozingatia dhana hiyo mpya ya mipango shirikishi kwa lengo la
kufikisha kwa wananchi uwezo mkubwa zaidi wa wao wenyewe kuongoza vita dhidi ya
umaskini na jitihada za maendeleo katika kila ngazi. Wananchi mlio wengi, karibu asilimia 80, mpo vijijini.
Tunataka maisha yenu yawe bora zaidi, muweze kuzalisha bidhaa za kilimo,
mifugo na uvuvi kwa wingi na ubora zaidi; na kisha muweze, kwa kupitia barabara
za uhakika, kuzifikisha kwenye masoko, na kulipwa bei ya haki na uhakika;
·
Tatu, tumezungumzia na kukubaliana juu ya mbinu na ratiba ya kufufua ushirika
kama mkakati mahsusi wa utekelezaji wa sera hiyo ya maendeleo vijijini -
ushirika wa kweli, ulio huru, unaoendeshwa kwa misingi ya demokrasia na
kumilikiwa kwa dhati na wanaushirika wenyewe, badala ya kugeuzwa mali ya
viongozi wachache;
·
Nne, tumejadili hifadhi ya
mazingira.
Rais Mstaafu, Mzee wetu Ali Hassan Mwinyi, alituasa kuwa uharibifu wa
mazingira na umaskini ni watoto mapacha, na mama yao ni ujinga.
Hatuwezi kupiga vita umaskini iwapo tutaangamiza mazingira yetu
yanayohimili uhai wetu na shughuli zote za kiuchumi na kijamii.
Ardhi inayochujuka kwa vile tunakata miti hovyo haiwezi kutupa chakula
cha kutosha. Maji yatazidi kukauka
tukiharibu vyanzo vyake. Mifugo
yetu itakosa maji na malisho. Hivyo,
tumepeana majukumu ya kutoa upya elimu ya mazingira, na kubuni mipango ya kuokoa
maeneo yaliyoharibika, na kuzuia mengine yasiharibiwe katika kila ngazi na eneo,
tangu kaya hadi kijiji, wilaya hadi mkoa, na hatimaye taifa;
·
Tano, tumezungumza kwa kina kuhusu hali ya kilimo na ufugaji nchini, na namna tunavyoweza kuboresha matumaini
yake kwa siku zijazo. Tumeelewana
juu ya vipaumbele katika sekta hii. Kwanza kabisa ni kuhakikisha kuwa katika
miaka michache ijayo tunaachana kabisa na aibu ya kuomba chakula; tena wakati
mwingine tukisaidiwa na nchi ambazo hazina ardhi nzuri, maji mengi na hali ya
hewa inayofaa kwa kilimo kama tuliyo nayo sisi!! Hatutaridhika na kujitosheleza kwa chakula tu.
Sisi ni watu ambao tukiamua tuna uwezo mkubwa wa kulisha nchi nyingi
zinazotuzunguka. Tumezungumza na
kuelewana ni nini kifanyike ili kufikia lengo hilo, na viongozi wenu watafikisha
ujumbe huo kwenu. Nawaombeni, wananchi, muupokee vizuri ujumbe huo;
·
Sita, tulizungumza sana pia juu ya namna bora ya kuwasaidia na kuwawezesha wananchi, wakiwemo wahitimu wa vyuo vyetu
vya kilimo, wawe wakulima wa kisasa na wa kibiashara. Hii ni dhana mpya na muhimu ya ajira, yenye maana na tafsiri
ya kujiajiri!!;
·
Saba, tulikubaliana na kuazimia kuweka mkazo mpya kwenye kusindika
mazao yetu ya kilimo kwa kiwango kitakachoyawezesha kuuzika katika masoko ya
kimataifa, kama tulivyofanikiwa kufanya kwa minofu ya samaki kutoka Ziwa
Victoria. Tanzania tunaruhusiwa kuuza bidhaa nyingi huko Ulaya na Marekani bila
ushuru. Hiyo ni fursa adimu sana
kwa dunia ya leo, ambayo bado hatuitumii kikamilifu.
Tuko tayari sasa Serikalini kuweka vivutio maalum kwa wawekezaji katika
kilimo na ufugaji wa kibiashara, na katika kusindika mazao ya kilimo na ufugaji,
viwanda vya kwanza vikiwa vya kusindika
kile tunachozalisha. Kwa kuongeza
thamani ya mauzo yetu nje ya nchi, tutapata fedha nyingi zaidi za kigeni, na
wananchi watapata ajira. Tunao
mfano hapa Dar es Salaam wa kiwanda kidogo tu cha kubangua korosho kiitwacho Premier Cashew Industries ambacho kinaajiri wanawake 1,200; na
·
Nane, tulizungumzia huduma za jamii, ikiwemo elimu na afya.
Katika sekta hizo tunayo mipango mahsusi ya uboreshaji wake, na kubadili
mfumo wa utoaji wake. Kwa upande wa elimu
tunakusudia kurejesha elimu ya msingi kwa watoto wote waliofikia umri wa kuanza
shule, yaani miaka 7. Na hilo litawezekana tu kwa kufuta ada za shule kwenye
shule za msingi za Serikali, kwa kuongeza idadi na ubora wa walimu – ikiwemo
kuwahamisha baadhi yao ili kuleta uwiano mzuri zaidi - na kwa kuongeza idadi ya
madarasa, nyumba za walimu, ofisi, vyoo, na kuimarisha huduma za ukaguzi.
Tutahitaji sana ushirikiano wa wananchi, si tu katika kuandikisha watoto wao
wote, wa kike na wa kiume, na kuhakikisha kweli wanahudhuria masomo bila kukosa,
bali pia kwa kuchangia nguvu na mali zao katika kujenga shule mpya, kuongeza
vyumba vya madarasa, vyoo, madawati, ofisi na nyumba za walimu.
Katika mikutano yetu tulielewana juu ya namna bora ya kuwashirikisheni
wananchi katika kazi hii; tulielewana pia juu ya mchango wa Serikali – kama
vile mabati, saruji, mbao, na misumari pale itakapowezekana – ili kwa haraka
kuongeza na kuboresha miundombinu ya kutolea elimu. Viongozi wenu wanajua
malengo tuliyojiwekea, na ninawaombeni sana, Ndugu Wananchi, mshirikiane nao
kuweka mipango na mikakati ya utekelezaji wake katika kila kijiji, wilaya na
mkoa;
·
Tisa kwa upande wa afya,
tunataka kueneza sana elimu ya kinga na chanjo kwa watoto ili kupunguza
maambukizo ya maradhi, na wakati huo huo kuwezesha kila kaya kuhimili gharama za
tiba pale inapobidi. Mkakati
tutakaoutilia mkazo sasa ni kuanzishwa kwa Mifuko
ya Afya ya Jamii. Zipo wilaya ambazo tayari zimeanzisha mifuko hiyo na
kupata mafanikio makubwa, kama vile Wilaya ya Igunga. Zipo wilaya nyingine
ambazo nazo zimepiga hatua. Kwa kila kaya kuchangia sh.5,000/= au 10,000/= tu
kwa mwaka, au kiwango tofauti ambacho wananchi wenyewe mtakubaliana, pamoja na
mchango wa Serikali, kila kaya itaweza kupata matibabu bila malipo mengine kwa
mwaka mzima. Pale viongozi wenu
watakapokuja kuwahimizeni kuanzisha au kujiunga na Mifuko hiyo naomba sana
mshirikiane nao na nyote mjiunge. Mafanikio
yake mtayaona;
·
Kumi, tumezungumzia pia UKIMWI.
Viongozi wenu watakuja na ari mpya ya kuhimiza na kueneza elimu ya kujua
namna ugonjwa unavyoenea na njia zilizopo za kujikinga.
Hali ya maambukizo ni mbaya sana, tena sana!
Sehemu nyingi UKIMWI sasa ndicho chanzo kikuu cha vifo, ujane na uyatima. Nawaombeni sana, Ndugu Wananchi, mzinduke na kuzingatia kwa
ukamilifu yale yote mnayoshauriwa na wataalamu na viongozi wenu juu ya ugonjwa
huu; na
·
Mwisho, ni suala la rushwa na
utawala bora. Tulijadiliana kwa
kirefu sana. Nia ya Serikali kupiga
vita rushwa iko wazi, lakini ili tufanikiwe msaada wenu wananchi unahitajika
sana. Ninafurahi kuwa idadi ya taarifa za rushwa zinazotolewa na wananchi
imeongezeka kutoka 432 mwaka 1998 hadi 1461 mwaka jana. Ningependa idadi hiyo
iongezeke zaidi; maana hiyo ndiyo njia kuu ya kuhamasisha vita dhidi ya rushwa.
Mtu haandikwi usoni kuwa ni mla rushwa; lakini wananchi mnawajua wala
rushwa. Tusaidieni kuwafichua ili
tusafishe uovu huu katika jamii yetu. Tumewajadili
pia Watendaji wa Vijiji na Kata kama watu muhimu sana katika kusukuma maendeleo
na kusimamia shughuli mbalimbali za Serikali.
Baadhi yao wanafanya kazi nzuri. Lakini
wapo pia wengine ambao wamekuwa kero kubwa kwa wananchi, ambao tutawadhibiti
kikamilifu iwapo wananchi mtawatolea taarifa.
Tutajitahidi pia kutoa mafunzo kwa watendaji hao ili waelewe madaraka yao
na mipaka yao. Aidha, tutajitahidi
kuwapeni wananchi elimu ya uraia ili nanyi muelewe ni nini Mtendaji wa Kata au
Kijiji anaruhusiwa kukifanya, kwa madaraka gani, na kipi haruhusiwi kukifanya;
na akikifanya mwananchi ana haki kutoa taarifa wapi. Tukishirikiana, tutahakikisha unakuwepo utawala bora zaidi
katika ngazi hii muhimu ya uongozi wa nchi yetu.
Ndugu Wananchi,
Hata kabla viongozi wenu hawajawafikieni, napenda, kwa lengo la kujipatia
uhakika wa chakula, nitangulize ushauri wangu ufuatao.
Msimu huu mvua za vuli zimekuwa nzuri kwa sehemu kubwa ya nchi yetu.
Wale mnaovuna sasa, naomba mvune kwa uangalifu ili msipoteze chakula
chochote. Na kisha mhifadhi vizuri
sana chakula hicho kisiharibiwe na mvua, wadudu au wanyama.
Epukeni kuuza kwa haraka mavuno yenu, na mnapouza iwe ni baada ya
kujiwekea akiba ya kutosha kulisha familia zenu hadi mavuno mengine.
Msisahau pia kuwa wakati wa mavuno bei zinashuka sana, hivyo kama huna
dharura usikimbilie kuuza. Vile
vile tupunguze sherehe, na matumizi yasiyo ya lazima ya nafaka kama vile pombe
kupita kiasi.
Kwa wale wanaopata hivi sasa mvua za masika, wazingatie ushauri wa
maafisa kilimo, na kutunza vizuri mashamba yao.
Narudia. Inawezekana kabisa
kujitosheleza kwa chakula kama tulivyowahi kufanya siku za nyuma wakati wa
kilimo cha kufa na kupona.
Nimezitaka pia Bodi za Mazao kujiandaa vizuri kwa ongezeko la uzalishaji
wa mazao ya biashara na chakula. Huduma
za ugani ziimarishwe. Kanuni za
kilimo, uvunaji, uwekaji madaraja ya mazao na uhifadhi zizingatiwe kwa ukamilifu. Soko la mazao liheshimu kanuni na taratibu tulizojiwekea.
Wawekezaji na wafanyabiashara wetu, nawaomba pia wajiandae kufanya
biashara ya mazao, na kuwekeza zaidi kwenye usindikaji wa mazao ya kilimo. Lengo letu kuu liwe
kuwa hatimaye tusindike mazao yetu yote ya kilimo na mifugo ndani ya mipaka ya
nchi yetu. Hili pia
linawezekana iwapo Vyama vya Wafanyabiashara vitajituma zaidi na kuwania hivyo
kwa dhati. Kama nilivyosema,
Serikali iko tayari kuweka vivutio maalum kwa wawekezaji katika kusindika mazao
ya kilimo na mifugo, hasa pale ambapo tunaridhika kuwa bidhaa bora zitazalishwa
kwa kiwango cha kuuzika kwenye masoko ya kimataifa.
Mwisho, Ndugu Wananchi, narudia tena rai ya kubadili fikra zetu juu ya
dhana ya maendeleo, na mgawanyo wa majukumu katika kuyatafuta.
Maendeleo kwa heshima, na maendeleo endelevu, chanzo chake ni azma
– azma katika ngazi ya mtu binafsi, azma katika kaya, na azma katika jamii. Tusipoazimia kwa dhati katika ngazi hizo, na kukubali kutoka
jasho na kutumia maarifa, hatutaweza kufanikiwa.
Mipango shirikishi katika kila ngazi ya jamii ni muhimu sana.
Wananchi azimieni kuondokana na kero mbalimbali, na kupiga hatua katika
kujiletea maisha bora zaidi. Tutawapeni
fursa kuamua ni mambo gani yapewe kipaumbele, na mgawane vipi wenyewe majukumu
ya utekelezaji na tathmini. Kwa
upande wake Serikali inaandaa mazingira yatakayowawezesha wananchi wote
walioamua na kujipanga vizuri wafanikiwe, na Serikali ichangie kiuwiano
mafanikio hayo. Kila kijiji kiwe na
malengo yake, mpango wake wa kazi wa kuyafikia malengo hayo, ratiba yake ya
utekelezaji, na viashirio vyao vya mafanikio. Chagueni machache muyafanye vizuri;
msitawanye mno nguvu zenu na mali zenu. La
muhimu ni kuwa siku hadi siku, mwaka hadi mwaka, ionekane wazi tunapiga hatua
kwenye mambo na maeneo fulani.
Ndugu Wananchi,
Hatma yetu kama watu binafsi, kama jamii, na kama taifa, imo mikononi
mwetu. Tupunguze basi utegemezi kwa
wahisani.
Maisha ni yetu na nchi ni yetu; juhudi ni zetu na jukumu ni letu;
mafanikio nayo yatakuwa yetu, ila tukifanya ajizi tutageuka kweli kuwa nyumba ya
njaa. Lakini kila mmoja akiazimia, kwa pamoja tunao uwezo wa
kuifanya Tanzania iwe nchi ya kuheshimika zaidi, na maisha yetu kuwa bora zaidi.
Naomba sana tufanye hivyo.
Mungu Ibariki Afrika.
Mungu Ibariki Tanzania.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.

SPEECH
BY THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, HIS EXCELLENCY BENJAMIN
WILLIAM MKAPA, AT THE INAUGURATION OF THE TANZANIA NATIONAL BUSINESS COUNCIL,
DAR ES SALAAM SHERATON HOTEL, 9 APRIL 2001
Chairman of the Tanzania Private Sector Foundation,
Mr.
E. Musiba;
Honourable
Ministers;
Representatives
of the Donor Community;
Chief
Executives and Representatives of the Private Sector;
Distinguished
Guests;
Ladies
and Gentlemen.
I am truly glad the day has finally come for me to officially launch the
Tanzania National Business Council. Soon
after assuming office, in November 1995, I realised the need to change the way
the national economy is managed.
This need was made more acute by the fact that our country was moving
from a public sector led economy to a private sector driven market economy.
In other words, the private sector was assuming an increasingly larger
and crucial role in national development and poverty reduction.
It became necessary, therefore, for the government to maintain a
continuous dialogue with the private sector and other stakeholders on critical
issues affecting private sector development, and the economy as a whole. That is
why I committed myself to creating a forum and a mechanism for institutionalised
dialogue between the Government and the Private Sector.
But, little did I know then that the negotiations and the preparatory
phase for the establishment of the National Business Council would outlive
the entire first term of my administration!
But, that the process has been so long may not necessarily be a bad
thing. For it means we have had time to consult widely within the
country, and learn from the experiences of other countries about public-private
consultative mechanisms.
We
did not want to force anyone’s hand, and we did not want to proceed
precipitously. For, it is only by
winning the confidence and total commitment of all actors that we can succeed
and guarantee sustainability. And
to build confidence, trust and commitment requires patience, preparation and
consultations that are both wide and deep in scope and content.
A
story is told of an overworked tailor who agreed to make a suit for a customer,
but warned it would take 30 days. The
customer was outraged.
“Why,
God took only six days to make the entire world,” he exclaimed.
“True,”
said the tailor, “but have you taken a good look at it lately?”
So,
without divine inspiration, we took our time; and I think it was time well
spent, and a job well done.
The
Business Council we are launching today is the first fruit of the consultative
culture, and the spirit of give and take, we seek to nurture in Tanzania.
Consultations have taken place between the different actors in the private
sector, leading to the formation of the Tanzania Private Sector Foundation.
Consultations have, likewise, taken place between the government and the private
sector within the context of the Steering Committee and the Task Force. The
experience both sides have thus gained is the initial valuable capital we
jointly bring into the national consultative process we are launching today.
Let me, therefore, thank all those in Government and in the private
sector, who worked so hard and tirelessly to bring these preparations to this
happy conclusion.
I also wish to thank USAID, UNDP and UNIDO who have supported us so
generously during this preparatory phase, as well as DANIDA and SIDA.
We shall continue to count on their support. They helped to mid-wife the Tanzania National Business
Council, and we now call upon them to back us up as we nurse and nurture the
newborn baby. We do not seek to
develop or entrench dependence on donors. Indeed
our goal is to have a self-supporting Council, but it has to be weaned gradually
to that state.
The Case for Smart Partnership
Mr.
Chairman,
Tanzania espouses the Smart Partnership Concept in developing countries,
demonstrated by our participation in the Southern Africa International Dialogue.
It is pertinent on an occasion like this to revisit the theoretical basis
for the concept and its main elements, and see how it can be utilised as the
driving force for the work ahead of the Tanzania National Business Council.
The first premise in a smart partnership is that the economy, indeed the
entire society, at each level, is an integrated and interdependent whole. There
may be many components, many players and many stakeholders, with as many
different, and often conflicting interests.
But each stakeholder, through actions or omissions, affects the others.
The
Government depends on taxes to maintain law and order, and to build and maintain
the requisite economic and social infrastructure on which the business sector
depends. But the Government cannot
get taxes if its citizens – both individual and corporate – do not make
money. And if the individual and
corporate citizens do not pay taxes, the government cannot build and maintain
the economic and social infrastructure, or invest in necessary human resources
development.
If
workers demand wages that existing levels of production and productivity cannot
sustain, the enterprise will at some point grind to a halt and jobs will be
lost. And if politicians pursue
social and economic policies that are harmful to business, the economy will
collapse along with the house of cards such politicians may have built.
Clearly, we are very dependent on one another, and it does not make sense
to undermine each other, or to work parallel to each other.
The sensible thing to do is to create a holistic framework and a
mechanism for working together, for supporting each other, for bringing out the
best in each other, in a manner that will guarantee each stakeholder wins in the
end. We must unite people,
enterprises and institutions in pursuit of common and shared values, visions and
prosperity. But to do that all
stakeholders must agree to the principal of give and take.
That is the only way to produce a win-win situation for everyone that is
central to the smart partnership concept and spirit.
But, the last five years have shown us that it is one thing to embrace
the theoretical basis for smart partnership, and quite another to get it
operational.
Attitudes
Must Change
So, the second imperative to this Smart Partnership is to come to terms
with our past, and then irrevocably change our attitudes and mind-sets. For over 30 years now we have propagated the policy of
self-reliance. But the fact is that
as a nation, and as individuals, we have embraced dependency.
The public sector driven economy contributed a lot to this.
Until this day, people look to Government directly for jobs, even as
economic reforms have reduced the capacity of Government to employ. People still
look to Government to solve their problems.
A celebrated case is where children in one village could not get
life-saving vaccinations because the refrigerator for vaccines at the local
dispensary had no kerosene!! That
is not partnership, it is untenable dependency!
At a different level, until recently the public sector economy did not
always create a conducive environment for the emergence of a strong and thriving
private sector. The views of the
private sector were not routinely sought, and taken into account during policy
formulation or implementation. The relationship between the public service and
the private sector was even adversarial at times.
The
business community on its part attributed many of their problems to government
indifference, even when the real problem did not lie with the Government.
Its contact with the government took the form of complaints or
representations from business associations, rather than holistic constructive
suggestions. Efforts by some in the
private sector to have influence in government gave rise to suspicions of
corruption. This does not bode well for building partnerships that are so
necessary between the Government and the private sector.
I am glad to note, therefore, that much reform has taken place over the
last six years. But much work remains to be done at all levels of government
and the private sector before we can bury the unhelpful mind-set on all sides
for good.
I must at this point commend the private sector for beginning to shed the
image of disorganisation that used to cast a shadow on its ability to play the
role expected of it in the new partnership and dispensation. In the two years
that the Tanzania Private Sector Foundation has been in existence, it has
managed to bring some order into the cacophony of advocacy groups, each trying
to put across its narrow sectoral views and influence policy in favour of the
interest it represents, often to the detriment of national goals, objectives and
aspirations. I believe we now have
a credible focal institution that can collect the views and demands of the
private sector, sift them, analyse them and articulate them as inputs into the
policy review and formulation process.
Mr. Chairman,
We, in government, have clearly begun to unlearn the prejudices and
inhibitions of the past, to unlearn the experiences of central planning and
control, and learn the new culture of a business friendly public sector.
But the journey remains long, and we must keep on at it.
That is the message I also gave to Regional and District Commissioners
when I met them a few weeks ago. Encouraging
entrepreneurship and facilitating the private sector is now part and parcel of
their work.
Mr. Chairman,
A well functioning private sector, at all levels, helps society allocate
its resources more efficiently, productively and without excessive transaction
costs. This implies doing more with
a given set of resources; it also implies increasing productivity and reducing
cost. So, much as I am committing my Government to supporting and aiding the
private sector, I must add a caveat that it must on its part shed the
“parastatal mentality”, and learn to operate profitably within existing
constraints. For, we all live in
the real world, a world of constraints and limited resources.
There is a limit to the number of appeals the Government can meet.
There is a story of a certain clergyman in charge of a poor church who
habitually suffered financial difficulties and was constantly appealing to his
Bishop for help. The Bishop, losing
patience, finally chided the man for making so many appeals.
Not long after, the Bishop received a cable from the clergyman, which
said, “This is not an appeal. It
is a report. I have no pants!”
I want to assure you that my Government will not be inclined to so resent
your appeals as to leave you in the end without your economic pants!
Vision
and Mission
Mr. Chairman,
We can also be partners if we share a common vision for the future, if we
share values, and if we are committed to working together, shouldering our
responsibilities even as we demand our rights.
I am pleased, therefore, that the preparatory work over the last five
years has enabled us to agree on the vision and mission of the Tanzania National
Business Council that is in line with the overarching National Development
Vision 2025. This is a vision of a
nation that is politically stable, united
and at peace with itself. A
nation where governance wears a human face and is people-centred
and striving towards the provision of high
quality livelihood for a well
educated and learning society; a nation where the private sector is the
bedrock of a competitive economy
capable of producing sustainable growth and shared benefits for all.
Our mission is to promote a healthy and robust economy where the guiding
hand of government, through enlightened legislation and transparent governance,
enhances the development of private initiatives, encourages local and foreign
investments, and generally provides an enabling environment for economic growth.
Competitiveness
in the Global and Regional Market
Mr. Chairman,
Trends in today’s world have created opportunities and challenges for
governments and firms in both developed and developing countries.
The globalisation of economic activities and the fierce competition this
entails has made it necessary for African governments to search for new models
of economic management.
Tanzania cannot live in isolation, and we have to adjust to these
realities of today and tomorrow. We
need to organise ourselves internally, in partnership, and work towards
attaining the three main attributes of competitiveness, namely good quality,
right price and timely delivery. We
have no choice if we are to remain in the game.
We must also remember that time is running out and deadlines are fast
approaching for throwing doors open to foreign trade within the context of the
East African Community, the SADC and the World Trade Organisation.
We will, therefore, endeavour to improve our laws and regulations so as
to enable the public to save and invest in productive activities, so as to
increase job opportunities and contribute to poverty reduction.
Market driven incentives will be provided to make Tanzania an attractive
place to invest for both domestic and foreign investors.
But I repeat and stress the importance of rules and regulations.
For, a market economy is only robust and good if it is properly and
fairly regulated; otherwise it augurs chaos.
Objectives
of the National Business Council
Mr. Chairman,
What are we now agreed should be the objectives of the Tanzania National
Business Council? These are:
·
First, to provide a forum for public-private sector dialogue with a view
to reaching consensus or mutual understanding on strategic issues relating to
the efficient management of development resources;
·
Secondly, to promote the goals of economic growth with social equity and
even development;
·
Thirdly, to review from time to time developments in the external and
domestic business environment, the challenges they pose to Tanzania, and propose
appropriate courses of action;
·
Fourthly, to exchange views on the prevailing operating and regulatory
environment, and propose ways to facilitate the public service, to improve on
service delivery and make the civil service business friendly;
·
Fifthly, to review and propose changes in the policy environment, to
enhance the attractiveness of Tanzania for both domestic and Foreign Direct
Investments (FDI), and improve the competitiveness of Tanzanian products in the
world market;
·
Sixthly, to encourage and promote the formulation of co-ordinated
policies on social and economic matters, including consideration of existing and
proposed economic legislation, and make appropriate recommendations; and
·
Finally, to consider any other matter deemed relevant to the achievement
of the above objectives.
Priorities
for the Future
Mr. Chairman,
In pursuit of these objectives, it will be necessary for the Council to
prioritise its agenda. There is such an over-abundance of pressing needs and
competing expectations that if we are not careful we may bite more than we can
chew, and may end up without any concrete results towards the attainment of our
objectives.
In my view, therefore, the Council’s immediate agenda should focus on
the following areas:
·
First, it must direct itself to proposing ways of improving the tax
regime quickly in order to support firmly our development objectives while
generating adequate budget revenue;
·
Secondly, it has to review the regulatory system, including the legal
and judicial systems, with a view to recommending ways of making it more
investor-friendly and consistent with the popular yearning for good governance;
·
Thirdly, the Council has to take a close look at our domestic industry,
including the export and import-competing sectors, particularly the processing
of agricultural and livestock products. We
must expand our manufacturing capacity and become increasingly competitive,
regionally and internationally. The
deep-seated supply side constraints in sectors such as energy, transport, and
communications, also need attention. The labour market and related regulatory framework needs
urgent reform. And, not least, we
have to redouble our efforts in finding markets for our products, including
making special efforts to make maximum utilisation of opportunities for duty
free access to European and American markets;
·
Fourth, the Council must suggest ways to ensure the opportunities and
fruits of economic growth are broadly shared, through mutually beneficial
co-operation among large, medium and small enterprises, including relatively
large traders and the petty traders at the street corners;
·
Fifth, openings must emerge for financing productive activities in all
sectors, including agriculture and medium, small or even informal activities.
The Council has to suggest ways to facilitate and expand such financing
substantially; and
·
Sixth, in order to entrench the decision of Economic Reform we must find
ways to ensure that the principles of good governance are accepted and practiced
tenaciously by the public sector as well as the private sector and the NGOs.
Requirements
for Success
Mr. Chairman,
The Tanzania National Business Council is not a panacea, and is in itself
not enough to bring about the practical results we so much need.
Those to whom we entrust this task must, therefore, put all their hearts
and minds to it. But even that is
not enough.
All
parties, both in government and the private sector, must exhibit a high level of
commitment to dialogue, which in turn requires the support of all political
leaders - not just those in Government but those in Opposition as well.
They must see dialogue and consultation as a positive approach to solving
all problems.
There
must also be an adequate commitment of time
and money to the economic
consultative process by all parties concerned.
As much as possible it must not be donor-driven, and that is why the
financing of the Council must as much as possible be underwritten by the
Government and the Private Sector in shared partnership and shared
responsibility.
Mr. Chairman,
An
effective national consultative mechanism will also be influenced by the
existence and support of strong and powerful sectoral associations with the
technical capacity to diagnose and analyse sectoral and other contemporary
issues.
The National Business Council cannot be a single channel or contact
mechanism between the Government and the private sector.
Contacts between line ministries and agencies and their client sectoral
or sub-sectoral associations have to continue, because implementation
bottlenecks will still have to be solved at those levels.
For that reason, each ministry must identify its customers, maintain a
continuous dialogue with them, and understand their operational problems, and
their aspirations. This will enable
the government to intervene as and when necessary without undue delay.
We should also bear in mind that the Tanzania National Business Council
is neither an alternative government, nor is it an extended cabinet.
It is only a forum where partners jointly review critical socio-economic
issues, as well as constraints arising from the regulatory or operating
environment for business, and make recommendations. But it is a forum that the government intends to hold in
great esteem, if only because of our joint membership in it, and the fact that I
will be its Chairman.
Conclusion
Mr. Chairman,
Today
everyone realises that the task of managing economic growth in Tanzania must
involve public and private sectors, employers and labour, government and
non-government organisations. The
public service wants to become business friendly; and the private sector needs
to learn how to balance the demands of the market with other national interests.
Both sides need to agree on how to optimise the use of development
resources.
The
purpose, therefore, of having a National Business Council is to create a forum
for both consultation and dialogue, leading to a consensus or at least a high
level of understanding of the issues of National Economic Management.
From now on, we must consider ourselves business partners, indeed
development partners, who must consult more, dialogue more, and strategize on
how we can work together to meet the national challenges of the future.
Those
sitting in the Council will have a special duty and a unique opportunity to
steer this country on the road to sustainable development in dignity, as an
independent and self-reliant nation.
Our
country is a land of many opportunities and great potential.
It is a united and peaceful country, with a fairly good climate and
fertile arable land; a country richly endowed with mineral and other natural
resources, and waters teeming with fish and other marine life; a country well
positioned geographically. It is
our duty to find the key that will unlock all these opportunities and potential
for the betterment of the lives of our people, and the development of our
nation. The hopes are many; we must
strive to meet as many of them as possible.
We
are here today for one, and only one purpose:
To work together to make Tanzania a better place.
We should, therefore, make the most and best contribution we can, singly
and collectively. And if Tanzania,
as a result of having put us in charge at this time, becomes a better place than
it was before we came in, then we shall have fulfilled our promise.
Let
us always remember that strength and weakness have nothing to do with courage or
muscle; only recognition. Strong
people recognise their weaknesses. They
also recognise their ability to overcome those weakness.
Weak people, on the other hand, deny their weaknesses, and fail to
recognise how strong they truly are.
I
call you to duty, to action, conscious of the challenges ahead, and the
weaknesses derived from underdevelopment.
But by recognising those weaknesses, and by taking those challenges by
the horns, we can, and we must, succeed.
A
Chinese proverb says, “Strong souls have willpower; weak ones only desires.”
Let us then summon the willpower to give Tanzanians the strength to
realise their desires.
I now have the pleasure to declare the Tanzania National
Business Council officially launched.
I
thank you for your kind attention.
|
|
SPEECH BY THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, HIS EXCELLENCY BENJAMIN WILLIAM MKAPA, AT THE OPENING OF THE NINTH CONFERENCE ON THE STATE OF POLITICS IN TANZANIA, NKRUMAH HALL, UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM,
10TH MAY, 2001
Mr. Chairman and Vice-Chancellor of the
University of Dar es Salaam;
Honourable Ministers and Members of Parliament,
House of Representatives, and Councillors;
Your Excellencies, High Commissioners
and Ambassadors;
Leaders of Political Parties;
Members of the Academic Staff;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen.
I am the Chairman of the Ruling Party, Chama Cha Mapinduzi. But I want to make it clear from the outset that I shall be addressing you today not in that capacity, but only as President of the United Republic of Tanzania; a President fully committed to fulfil with maximum diligence the solemn oath of that High Office. It is a commitment:
· To be faithful to the United Republic of Tanzania, to serve it with all my heart, and to preserve, protect and defend the Constitution of the United Republic of Tanzania;
· To do justice to all people according to the law, customs and traditions of the United Republic of Tanzania, without fear, favour, affection or ill-will; and
· To defend and sustain the unity of the United Republic of Tanzania in accordance with the Constitution of the Republic.
I shall also be addressing you as one on whose shoulders rests the ultimate responsibility and accountability for democratic governance, and for the pillars of a rule-based competitive political dispensation, a dispensation underwritten by the rule of law.
You can, therefore, believe me when I say how very pleased I am to once again accept an invitation from the leadership of the University of Dar es Salaam to officiate at the opening of yet another conference on the State of Politics in Tanzania, organised by the Department of Political Science and Public Administration of the University of Dar es Salaam, through its Research and Education for Democracy in Tanzania Programme, (REDET).
I say “once again” because I had the honour and privilege to perform a similar function at the 1994 Second Annual Conference of this ongoing conference series, whose proven sustainability deserves much praise. At that time, I was Guest of Honour in my capacity as Minister for Science, Technology and Higher Education.
I believed then, as I do now, that such a forum was, and continues to be, an important source of inspiration, where our young multi-party democracy is apt to find wise counsel and nurture. My wish at the time was to see the conference subsequently become an uninterrupted annual event. The fact that today I am officiating at the 9th Conference, seven conferences after the one I opened in 1994, shows that my wish has been fulfilled. I thank you deeply, as I renew my wish for continued sustainability and resourcefulness of this conference series in the future.
Mr. Chairman,
I have on different occasions encouraged our Universities to be increasingly engaged in the topical issues and challenges confronting our nation, and to strive to be relevant to the society at large. The University of Dar es Salaam, in particular, has a glorious past in that respect, a past it is now called upon to live up to. This campus used to be the “Mecca”, and the fountain of intellectual inspiration, for those across the world that believed in freedom, in equality, in social justice, and in people-centred development. Time has passed, and circumstances have changed internally, regionally and globally, but I believe this University can, and must, continue to uphold a name and a special place for itself in the new Tanzania, the new Africa, and the globalising world.
These series of REDET Conferences are one way to go about it, and I urge you to keep the tradition alive and well. As President, I have a particular interest in your deliberations, hoping that out of them will emerge new ideas on how we can consolidate democracy and democratic governance in Tanzania. I always enjoy a good debate; and I cannot claim to have all the answers to the challenges that the evolution of multi-party democracy poses for us as a nation. Give me good counsel, and I will give it the sincere consideration it deserves.
The Case for Democratic Consolidation
Mr. Chairman,
The theme of this Conference, “Issues in Consolidation of Democracy and Democratic Governance in Tanzania” implies two things. First, that there is democracy and democratic governance in Tanzania, and, secondly, that such democracy and democratic governance as we have needs to be consolidated, or even improved. I should like, even at this stage, to say that this is, indeed, a valid proposition.
This day, the 10th of May, happens to be the day Sir Winston Churchill became Prime Minister of Great Britain in 1940. In 1947, two years after the end of his first term as Prime Minister, he made a speech in the House of Commons, from which is often quoted the following dictum.
Many forms of government have been tried, and will be tried in this world of sin and woe. No one pretends that democracy is perfect or all-wise. Indeed, it has been said that democracy is the worst form of Government except all those other forms that have been tried from time to time.
Mr. Chairman,
The historical experiences of practically all nations have proven Sir Winston right. Democracy is best, but there is no perfect democracy; not even in the oldest democracies in the world. Democracy is not a destination; it is a journey towards an ideal. And the democratic ideal is akin to the rainbow, beautiful to behold from afar, yet impossible to hold in your hand. For, the parts that constitute the ideal keep on mutating and realigning over time, as they relate to societies in which, by their nature and technological advancement, the only constant is change.
The quest, indeed the imperative, to improve democracy and democratic governance, and to amend Constitutions and laws, is not therefore unwelcome to those committed to the ideal of democracy, as we are in Tanzania, and neither are they specific or unique to Tanzania. The issue, therefore, is not whether or not we should seek to improve governance, or our Constitution; the issue is how best we can do it, and what we can afford to do, under which time-frame and what sequence, while at the same time safeguarding and consolidating democratic governance.
Democratic Change
Many are agreed that there is democracy in Tanzania; the question, therefore, is how best we can improve it, including by amending our Constitution and laws. Do we improve democracy by democratic means; or do we regress into anti-democratic means. I say so because there is a political concept that is gaining currency called “people power,” to which the self-appointed viceroys of democratic governance have curiously shut their eyes, ears and lips. As I know it, “people power” is only legitimate through an election; and an election that is disputed is resolved through legal or political means, not through mob violence. Anything else is not “people power,” but “people thuggery.”
And unless this distinction is appreciated, Africa will not make much headway in the consolidation of democratic governance. As the American politician, Alfred Smith, said in 1933, “All the ills of democracy can be cured by more democracy.” This Conference would be well advised to figure out how this pithy advice can be internalised into our political system. For even in our own world of sin and woe, the best way to cure the ills of our democracy is none other than through democratic means.
Mr. Chairman,
We can only build by building, not by demolishing. Consolidation of democracy and democratic governance means strengthening what has already been achieved in these fields, and in my opinion what has been achieved so far is impressive. Much progress, for instance, has been attained by the enactment of the Thirteenth Constitutional Amendment; by the amendment of election laws both at central and local government levels; by the restructuring of central, regional and local administrations to make them more efficient and effective, while remaining responsive and accountable to the citizenry through their elected representatives; and by the enactment of several other laws which broaden and protect citizens’ rights and liberties. The list is long and deserves recognition, especially considering the short time and economic difficulties in which these far reaching legal and structural reforms have been undertaken.
Mr. Chairman,
The terms “democracy” and “democratic governance” encompass a wide spectrum of political attributes that empower the citizenry to participate in shaping the common good of society in freedom, dignity and responsibility. Such political attributes are too many to be covered adequately, either by me in such a short opening speech, or even by you, conference participants, in the two-day session that has been allocated for that purpose. I will thus avoid the futility of trying to expound on all the theoretical or even practical notions relating to the consolidation of democracy and democratic governance.
But as I was browsing through your programme, I pleasantly noticed that the conference organisers managed to capture salient issues for discussion, which are very pertinent to our national experience in democracy and democratic governance. These include: Prerequisites for democratic consolidation; the state of institutions of governance; the state of political parties and civil society; lessons from the 1999 neighbourhood/village/local government elections and the General Elections of October 2000; and, finally, the political problems in Zanzibar.
These are indeed important issues, which deserve an in-depth and objective analysis. But analysis alone would fall short of usefulness if the conference does not come up with strong and action-oriented recommendations that would help to consolidate our democracy and democratic governance in practical terms.
A Rule-Based Political System
Mr. Chairman,
Based on some of those issues, which are going to be discussed at this conference, let me give you a few stimulating thoughts. We know, for instance, that the kind of representative democracy we are trying to build is based on party political competition through elections. Such competition is governed by rules. One prerequisite for consolidation of democracy is for political players to agree on the rules of the game and obey them.
In the case of our country, such rules are embodied in the constitution and other legitimate pieces of legislation enacted by legitimate bodies. In order for party political competition to produce a respectable representative democracy dividend, the political parties contesting an election must play by the existing rules of competition. When a party enters an election contest, this is a sign that it agrees with, or is at least acquiescent to, the existing rules and that it will, therefore, accept the outcome of the contest. Anything else is a prescription for, and a harbinger of, veritable anarchy.
The outcome of an election contest can be either victory or defeat. Our political parties must understand and accept this reality without equivocation. Rules of competition in a democracy include celebrating victory with humility when a party wins, and accepting defeat with grace when it loses. When the loser is not satisfied with the results, the right thing to do is to seek redress through the channels stipulated by the existing rules. For instance, our laws grant Parliamentary and House of Representatives candidates the right to petition in the High Court when they do not agree with election results. Exercising such a right, rather than resorting to any other means of reacting to defeat, is what democracy is all about. I would like this conference to suggest ways in which we can consolidate this democratic culture of rule-based political competition, and bring all political parties on board.
When the existing rules are inadequate, and this may be true because even in the most advanced democracies shortcomings in the rules of the game continue to be discovered, the proper place to amend the rules to suit the needs and interests of all political players is the houses of representatives. We have two such houses in Tanzania: the Union Parliament and the Zanzibar House of Representatives. I challenge this conference to impress upon political parties and their elected candidates that the only legitimate and democratic way to change rules is through active participation in the legislative bodies. Democrats fight for change in those bodies; they do not boycott them.
Boycotting does not only fly in the face of our attempts to improve and consolidate democracy and democratic governance, it is also a great injustice to the people, and one may even add that the people are being exploited in pursuit of the political agenda of their leaders. An election costs a lot of money, public money. This justifiable expense is intended to produce people’s representatives in the organs that according to the constitution make laws, regulations, and decisions about public revenue and expenditure. To deny the people this constitutional right to representation, on whatever pretext, is a grave injustice to them, and a terrible assault on our efforts to consolidate democracy. By boycotting you do not punish the ruling party, you do not punish the government, you punish innocent people, who voted in good faith.
The pursuit of, and conformity to, the individual position of a political party cannot supersede the constitutional right to representation by all people. For, a constituency is not composed of followers of only one party. Its members are a cross section of all political parties, as well as many other people who do not belong or pledge loyalty to any party, and who therefore are not bound to defer to the position of any party.
You see, Mr. Chairman, we are not a very litigious society; otherwise, someone in those constituencies where legally elected Members of Parliament or House of Representatives have abdicated their duty to represent people, could have taken them to court for denying them their constitutional right to representation. And, I am not instigating anyone to do it. My primary concern, rather, is to consolidate democracy and democratic governance.
Those who refuse to represent their constituencies in Parliament and the House of Representatives would be wise to accept the counsel of the American politician, William Fulbright, who in a speech to the United States Senate in 1966 said:
“In a democracy dissent is an act of faith. Like medicine, the test of its value is not in its taste, but its effects.”
And the effect of the boycott by CUF Members of Parliament and the House of Representatives has been essentially to undermine the evolution of democratic governance, and entrenching further the dominance of Chama Cha Mapinduzi in the Councils of State. For, in a democratic state such a boycott can serve no greater or deeper purpose; at the very least it only tempts the victorious side to paraphrase Shakespeare in King Richard II and say,
“Not all the water in the rough rude sea
Can wash the balm from a duly elected President.”
Political Tolerance
Mr. Chairman,
Consolidation of democracy also requires political tolerance, which in turn implies and recognises the existence of divergent views. But it also means that such divergences must be managed on the basis of accommodation, restraint and mutual respect. Lately, there have been signs that political tolerance has degenerated in our country despite our repeated reminders that unity, peace and solidarity constitute the most cherished cultural heritage of our nation, and the foundation upon which all else must be built.
I, therefore, challenge you to find the root cause of this spectre of political intolerance that has been gaining ground in our midst. I also call upon participants to prescribe some medicine that will help to exorcise that evil spirit, but without hurting the witch. You may wish to bear this challenge in mind when you discuss the political problems in Zanzibar, which as I noted earlier, have thoughtfully been included in your agenda. I strongly believe that political intolerance has contributed significantly to the political malaise we have experienced in Zanzibar.
The Government, on its part, has tried hard to be tolerant as its contribution to the consolidation of democracy in our country. The assumption in being tolerant is that some of these problems, however unpleasant and unjustified, are transitory – the birth pangs of a responsible political opposition, an opposition that one day can be a credible alternative to the Government in power. But sometimes, it is as if there are people who are determined to probe the limits of Government tolerance. That is injudicious, dangerous, and inimical to the consolidation of genuine democracy. The Italian writer and politician, Ignazio Silone, in his book The School of Dictators, written as the Second World War was about to begin in 1939, warned thus:
“For democrats in troubled countries, the height of the art of governing seems to consist in accepting slaps so as to avoid kicks… The enemies of democracy take advantage of this and grow daily more insolent.”
Mr. Chairman,
My Government is determined to be as tolerant as it can so as to consolidate democracy and democratic governance. But, for any government, in any country, there is a limit to the number of slaps it can take. Drawing the line at an appropriate point is also part of good governance. Let this conference press the case for the civil society to politically dialogue with a civil tongue!
Law Enforcement
Mr. Chairman,
I have also noted with interest the time slot given to the discussion of the state of the instruments of governance, such as the relationship between the three branches of government, and the performance of various government services, including the state defence and security establishments. All these institutions are bodies that are there to enhance, and not to hamper, the consolidation of rule-based democracy and democratic governance. In performing their duties, they too must obey and enforce existing laws and rules. They wield power and authority, but they must do so in a way that demonstrates responsive and responsible leadership, which strictly observes civic respect, policy openness and the rule of law.
Where these instruments of governance are performing their duties according to existing laws, the citizens on their part must show compliance and trust, and must never provoke them beyond tolerance. Where, on the other hand, these instruments of governance act outside the law, they need also to be held accountable. One way we have tried to accomplish this is through the training given, and the necessary skills imparted on them, as well as the sensitivity demanded of them to their duty to discharge their responsibilities according to the law. But they are human beings, and there is always scope for error. That is why we have now legislated for the establishment of the Commission for Human Rights and Good Governance to which all complaints can be directed for investigation, determination, and ultimately remedial action.
There may be areas where the laws governing the instruments of governance are defective. There may even be instances of abuse of power by some officials. To put such matters right, we need to empower our citizens in exerting influence and oversight in governance. Politically competent citizens will have defective laws corrected in the respective legislatures through their representatives. Such citizens will also be able to have occasional abuses of power redressed through lawful and politically acceptable methods, as in the case of the Commission for Human Rights and Good Governance I have already made reference to.
Civic Education
But citizen influence and oversight must be cultivated through civic education. At present, the state of civic education in Tanzania is far from being satisfactory. This applies to both ordinary folks in our society and a great number of politicians, in all political parties. The task of providing and disseminating civic education is one in which government could work in partnership with other stakeholders, such as political parties, non-governmental organisations, religious organisations and others, provided that a standardised form of content and methods for such education can be agreed upon, and observed by all. For, civic education must not degenerate into politicking in disguise.
There is also a huge difference between civic education, or even the development of informed political opinion, and the stoking of the fires of political sentimentalism and sensationalism. The former helps to consolidate democracy, but the latter undermines democracy. Regrettably, I would attribute the demonstrations and public rallies taking place in our country now as falling in the second category. Political parties are not creating informed political opinion; they are creating political sentimentalism, whipping up waves of resentment knowing very well they may find expression in anti-democratic and unruly actions and behaviour.
I, therefore, challenge the non-governmental stakeholders to think about appropriate ways to develop citizens’ influence and oversight on governance through responsible civic education. There are important values that you can impact, such as: political equality, inter-group tolerance, inclusiveness in associational membership, and the importance of political participation. But above all, the pursuit of politics must never be allowed to threaten national unity and concord, or peace, stability and public security.
Mr. Chairman,
While I am still on this subject of civic education, I would like to congratulate REDET for its recent publication of a civic education manual for primary schools entitled “KATIBA NA HAKI ZA RAIA TANZANIA” which was launched by my Minister for Education and Culture, Hon. Joseph Mungai, MP. This is another achievement that lends credibility to the University’s contribution to consolidation of democracy through education. I thank and commend you.
Economic Growth and Development
Mr. Chairman,
I know there is only so much you can discuss in these two days you will be here. But one thing I want you to keep in mind is the capacity to manage and sustain the democratic political dispensation we have adopted. And today I am not talking about technical capacity, I am talking about the capacity of the economy to underwrite all the things we want to see done in order to consolidate democracy and democratic governance. And that is why you will always hear me talking about the economy, in terms of the imperative of reform and of engendering economic growth and broad-based development.
We have so far held two General Elections under a multi-party democratic political system. And both times we could not afford wholly to finance the elections ourselves. We reduced this dependency on donors last year, but the need for external support remains. It is, therefore, important for all political players to give sufficient attention to that part of our polity that gives us the wherewithal to sustain a democratic political system. The cost of one by-election, in one constituency, is way above what a whole district is allocated from the national budget for development expenditure for a whole year. You can imagine what the situation would be like if we were to be forced, by law, to hold 15 by-elections within a month!
But the importance and relevance of economic growth to the consolidation of democracy is not only in terms of financing our elections. It is also in terms of fully funding and building capacity in the institutions of governance through the three branches of Government: The Executive, in terms of a public service that is ethical, people-centred, and service-oriented; the Parliament and House of Representatives in terms of technical and financial capacity to represent people; and the Judiciary in terms of prompt adjudication of disputes and the interpretation, application and enforcement of laws. If I can’t guarantee the supply of paper needed by judges and magistrates to record cases, how can the people’s confidence in the Judiciary be strengthened?
Free Trade Unions
Mr. Chairman,
The economic reforms we have embarked upon are increasingly shifting economic activities, and hence job-creation, from the public to the private sector, including multinational corporations. In terms of democratic governance, therefore, the role of effective and efficient free trade unions is critical and unmistakable.
But our trade unions lack the requisite capacity and experience to negotiate good working conditions and remunerations with the private sector. For the duration of most of our independent statehood, trade unions were, at least in terms of structure, not antagonistic to the Government, which was the largest employer. Trade Unions were even, for several years, an organ of the ruling party.
It is only two weeks ago that the long journey towards the establishment of free trade unions in Tanzania ended. The new trade unions need the help of everyone, in terms of education, advice and developing the technical competence for analysis and negotiations, as they find their feet in the huge challenges they now have to face. An enlightened organised workforce is a factor of good governance.
Mass Media
Mr. Chairman,
The print and electronic media are also an important component in the consolidation of democracy and democratic governance. A free and objective mass media can act as another institution offering checks and balances against the Government and other players in a democratic political system.
But more needs to be done to improve the quality of journalism in our country. The tendency is too much on the business aspect, on the desire to make profits, including through sensational reporting, rather than truly informing and educating the public. The mass media has a great responsibility which if executed well can help consolidate democracy, and spread the inspirational momentum for development. As it is, there is too much reportage of what politicians say, rather than the analysis of policies, decisions and trends.
What a distinguished person, including the President, says may be news, especially if it is inconsequential. But a series of inconsequential pronouncements, even by the President, are not only NOT NEWS, but also downright boring! It is said that great minds do not discuss people; they discuss events and ideas. We need greater minds in the forest of newspapers, radio and television stations, sprouting and flourishing on a fertile and hungry audience that Tanzania has become, and the freedom of expression our Constitution guarantees.
Mr. Chairman, Ladies and Gentlemen,
In conclusion, I wish to reiterate my keen interest in the proceedings of this conference as one of the inputs, which may contribute to our thoughts and actions in the government’s efforts to play its part in consolidating democracy and democratic governance. The rich plurality of the backgrounds of participants in this conference should guarantee very fruitful deliberations.
Pericles, the Athenian statesman and orator of ancient Greece, four centuries before the birth of Christ, said:
“Our government is called a democracy because power is in the hands not of the few but of the many.”
Today, 2,400 years later, his definition still holds. And to you who have met here to review the state of politics in Tanzania, with a view to consolidating democracy and democratic governance, I have one basic request. Help us to determine the best way to make sure power is, and remains, firmly in the hands not of the aspiring few, but of the many that every five years tread to polling stations, standing patiently in long queues, to express their opinion, and pass judgement on aspiring politicians, through the ballot box.
We need a pervasive re-commitment to a rule-based democratic political dispensation, a strong and growing economy that can sustain it, and working democratic institutions with the capacity to arbitrate between competing demands and interests, and install the necessary checks and balances into our system. I will follow the deliberations of this Conference with keen interest, for ultimately, as President Harry Truman would say, the buck stops with me.
I now declare this 9th Conference on the State of Politics in Tanzania officially open.
I thank you for your patience and attention.
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 MEI 2001
Ndugu Wananchi,
Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu tafsiri ya umaskini wetu, na malengo tuliyojiwekea kama Serikali, kwa kushirikiana nanyi wananchi, na kwa mchango wa marafiki na wahisani kuupunguza umaskini huo. Katika miaka 5 iliyopita, Serikali yenu imejitahidi sana kukamilisha kazi ya kurekebisha sera, sheria, milki, mfumo na utendaji katika uchumi wetu. Mabadiliko hayo yalikuwa ya lazima ili kujenga msingi wa uchumi utakaokua kwa uendelevu.
Kwa kiasi kikubwa kazi hiyo imekamilika, na kuweka mazingira muafaka, na msingi wa kuanza kujenga upya uchumi wetu. Tunayo sasa matumaini makubwa kuwa mafanikio tuliyoyapata katika kuimarisha uchumi mkuu yatatoa fursa kwa wananchi kujiendeleza na kufaidika katika ngazi ya uchumi mdogo, na kupunguza umaskini kwenye ngazi ya kaya na vijiji jambo ambalo ndilo lengo letu kuu katika miaka 5 ijayo.
Mkutano wa Brussels
Ndugu Wananchi,
Kwa niaba yenu, nilialikwa kuhudhuria na kuhutubia katika Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Nchi Maskini Kuliko Zote uliofanyika mjini Brussels, Ubeljiji, wiki mbili zilizopita. Tulialikwa Wakuu wa Nchi wachache, na tukazungumza kwa niaba ya nchi nyingine maskini.
Mikutano mingine miwili kama huu ilifanyika mjini Paris, Ufaransa, mwaka 1981 na mwaka 1990. Lengo kuu la mikutano hiyo, kama ilivyokuwa kwa mkutano wa juzi, lilikuwa kuona jinsi ambavyo nchi tajiri zinaweza kusaidia jitihada za nchi maskini kuondosha umaskini.
Kilichojitokeza wazi pale Brussels ni kuwa maazimio ya mikutano ya awali hayakufanikiwa kututoa katika umaskini wetu. Mwaka 1981 kulikuwa na nchi 25 tu kwenye kundi hili la nchi maskini sana. Hadi sasa ni nchi moja tu, Botswana, iliyofanikiwa kuondoka kwenye kundi hili na kuingia katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Badala yake, idadi ya nchi maskini sana imeongezeka kutoka 25 hadi 49, kati yake 34 zikiwa barani Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Umaskini wa Mapato
Ndugu Wananchi,
Umaskini una sura nyingi, mojawapo ikiwa umaskini wa mapato. Inakadiriwa kuwa mwaka 1997, wastani wa mapato ya kila mwananchi katika nchi maskini kuliko zote ulikuwa sh.211,500 tu (USD 235) kwa mwaka, ikilinganishwa na sh.22 milioni (USD 24,522) katika nchi tajiri. Sisi, Tanzania, baada ya juhudi zote, inakadiriwa sasa tumefikia wastani wa mapato ya kila mwananchi wa sh.243,000 (USD 270) kwa mwaka. Hivyo, Mtanzania akiwa na sh.1, binadamu mwenzake katika nchi tajiri ana sh.91. Hiyo ndiyo sura mojawapo ya umaskini wetu.
Hivyo katika vita vyetu dhidi ya umaskini silaha yetu lazima iwe bidii za kuongeza mapato halali ya wananchi wetu, kwa kukuza uchumi kwa asilimia 8 – 10 kwa mwaka. Ongezeko hilo ndilo litatuwezesha ifikapo mwaka 2010 kuongeza kipato cha wastani kwa kila Mtanzania kwa karibu mara mbili.
Umaskini wa Mahitaji Muhimu
Ndugu Wananchi,
Sura nyingine ya umaskini ni upungufu, au kutokuwa na uhakika, wa mahitaji muhimu ya mwanadamu; kama vile chakula, mavazi na makazi. Sura hii ya umaskini inaonekana zaidi vijijini ambapo karibu kila Watanzania 8 kati ya 10 wanaishi, maisha yao yakihimiliwa kwa kiasi kikubwa na kilimo, ufugaji na uvuvi. Hivyo hakuna njia nyingine ya kuondoa umaskini wa mapato, na umaskini wa kukosa mahitaji muhimu, isipokuwa kwa kuongeza uzalishaji na tija kwenye kilimo, ufugaji na uvuvi.
Lengo letu kitaifa ni kuongeza ukuaji wa sekta ya kilimo kutoka asilimia 3.6 hadi asilimia 5 kwa miaka 3 ijayo, na kwa kiwango kikubwa zaidi miaka inayofuata. Kasi hiyo itatuwezesha kupunguza idadi ya wasio na uhakika wa chakula, na wasio na uhakika wa mahitaji mengine muhimu. Aidha tunalenga kupunguza utapiamlo mkali kutoka 6% hadi 2% ifikapo 2010.
Mimi nina uhakika kuwa inawezekana malengo haya kuyafikia na kuyavuka. Lakini kwanza lazima kila mwananchi aazimie, na kutekeleza wajibu wake, wa kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Bila hivyo, juhudi za Serikali peke yake za kuweka mazingira bora zaidi ya shughuli za uzalishaji, biashara na huduma hazitazaa matunda tunayoyakusudia.
Umaskini wa Huduma Duni za Kijamii
Ndugu Wananchi,
Sura nyingine ya umaskini wetu ni viwango vya chini vya huduma za jamii, hususan elimu, afya, na maji. Huduma hizi, pamoja na lishe, ndizo humpa mtu afya, nguvu, na maarifa ya kufanya kazi na kujiondoa katika umaskini. Ndio maana upatikanaji na ubora wa huduma hizi ni kigezo muhimu cha mafanikio kwenye vita dhidi ya umaskini.
Hebu tuone Tanzania tunalinganishwa vipi na nchi tajiri. Wakati ambapo kwenye nchi tajiri watoto karibu wote wanaandikishwa, na wanamaliza elimu ya msingi, sisi kwa kila watoto 100 wenye umri wa kuanza shule, tunaandikisha 77 tu, na wanaomaliza ni 57 tu. Hapa petu ni watoto 6 tu kati ya 100 wenye umri wa kusoma elimu ya sekondari ndio wanasoma, wakati ambapo katika nchi tajiri wamefikia 96 kwa 100.
Na kwa mpango wetu tulioupeleka Brussels tunatarajia kuongeza watoto wanaoandikishwa darasa la kwanza hadi 85 kwa kila 100 ifikapo mwaka 2003, na kupunguza wanaokatisha masomo kutoka 6.6% hadi 3% tu. Tunakusudia pia kuongeza idadi ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa darasa la 7 kutoka 20% hadi 50%; na wanaoingia sekondari waongezeke kutoka 15% ya wanaomaliza shule ya msingi hadi 21%. Aidha, tunataka kuongeza elimu ya watu wazima.
Kwa ulinganisho na nchi tajiri tunayo kazi kubwa sana, lakini lazima ifanyike ili angalao tupunguze tofauti hizi kubwa sana katika elimu. Bila elimu na ujuzi hatuwezi kuendelea katika dunia ya leo, wala hatutaweza kushindana na mataifa mengine. Ndiyo maana umuhimu wa elimu kwa nchi maskini tuliuzungumzia sana kule Brussels, na kukubaliana kuwa nchi tajiri ziongeze misaada yao ili ikichanganywa na juhudi za wananchi na serikali zao, kasi ya utoaji na uboreshaji wa elimu iongezeke.
Kwa upande wetu tunayo kazi kubwa, inayotegemea sana ushirikiano wa Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Wananchi na Mashirika yasiyokuwa ya Serikali, ikiwemo Mashirika ya Dini, na wahisani. Serikalini tumeamua kufuta ada kwa watoto wa shule za msingi. Kwa kushirikiana, tutaongeza shule, madarasa, madawati, nyumba za walimu, vifaa vya kufundishia, huduma za ukaguzi wa shule, ajira ya walimu, na kadhalika. Hatuna hiari katika jambo hili. Ukweli ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani iliyopiga hatua endelevu ya maendeleo bila kuwekeza vya kutosha katika elimu na ujuzi.
Kwa upande wa maji na afya hali kadhalika. Tofauti kati yetu na nchi tajiri ni kubwa mno. Wakati katika nchi tajiri karibu kila mtu anapata maji safi, sisi ni asilimia 54 tu. Wakati katika nchi tajiri ni watoto 6 tu kati ya 1,000 wanaozaliwa hai wanakufa wakiwa wachanga, sisi tunapoteza watoto 90. Wengi wa watoto hao wanakufa kwa magonjwa yanayozuilika kirahisi kwa chanjo au tiba. Hicho ndicho kiwango cha umaskini wetu.
Hivyo miongoni mwa malengo yetu katika miaka 3 ijayo ni kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 90 hadi 85 kwa kila watoto 1,000 wanaozaliwa hai; kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka 5 kutokana na malaria kutoka 12.8% hadi 10%; kuongeza chanjo kwa watoto chini ya miaka 2 kutoka 71% hadi 85% ya watoto wote; kufikisha kampeni maalum dhidi ya UKIMWI kwa 75% ya wilaya zote, na kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama mijini na vijijini.
Malengo yote haya yanaweza kufikiwa, na kuvukwa. Lakini lazima tushirikiane wote, Serikali Kuu, Serikali za Mitaa Wananchi, na Wahisani.
Na lazima tuweke mkazo maalum kwa watoto – kwa elimu yao, afya yao, uhai wao, na mazingira yao. Ripoti ya Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa, UNICEF, kuhusu hali ya watoto duniani mwaka huu inabainisha kuwa watoto wadogo wanazidi kufa bila sababu. Kiasi cha watoto milioni 11 hufa kila mwaka duniani, wengi wao katika nchi maskini, kabla ya kufikisha umri wa miaka 5 kwa sababu zinazozuilika. Maana, kwa kila watoto 100 wanaokufa kabla ya umri huo, 20 wanakufa kwa matatizo wanapozaliwa, 18 kwa magonjwa ya njia ya hewa, 17 kwa magonjwa ya kuhara, 15 kwa magonjwa yanayoepukika kwa kupewa chanjo, 7 kwa malaria, na 23 ndio hufa kwa sababu nyingine. Kwa maneno mengine, tuna uhakika kuwa inawezekana kuzuia vifo vya watoto 77 kwa kila 100 wanaokufa hivi sasa. Inawezekana. Na nikinukuu kutoka katika ripoti hiyo:
“Kuacha kuwapatia watoto wadogo matunzo na malezi haya ya awali ni kosa lenye gharama kubwa kuliko makosa yote.”
Tuazimie basi kuwapa watoto wote chanjo; kuwapeleka hospitali wakiumwa, si kupiga ramli; na kuwapeleka shule wote, wa kike na wa kiume.
Umaskini wa Kukosa Kauli
Ndugu Wananchi,
Sura nyingine ya umaskini ni unyonge unaosababisha hali ya kutojiamini, na hivyo kupuuzwa katika kufanya maamuzi. Katika ngazi ya kitaifa, Tanzania tumesifiwa sana kwa hatua tuliyopiga katika kukataa umaskini wa aina hiyo. Katika miaka ya hivi karibuni Serikali Kuu imejichukulia madaraka makubwa zaidi ya maamuzi katika kubuni sera, mipango, mikakati na vipaumbele vya maendeleo yetu. Hali hiyo sasa tunakusudia kuifikisha kwa wananchi, kwa kupeleka madaraka karibu zaidi nao kupitia Serikali za Mitaa, na kuwashirikisha katika miradi ya maendeleo katika ngazi ya kijiji. Uwajibikaji wa wanasiasa, na watendaji wa Serikali, kwa wananchi katika ngazi zote ni jambo la muhimu sana. Hivyo, tutaendelea kuuimarisha uwajibikaji huo kwa njia mbalimbali, ikiwemo kukuza demokrasia ya vyama vingi, kuendeleza uhuru wa vyombo vya habari, kuboresha utendaji na kuongeza uwezo wa Serikali za Mitaa, na kuendeleza uwazi katika maamuzi na utendaji wa kiserikali.
Lakini ni jambo moja kwa Serikali kutoa upeo mkubwa zaidi wa wananchi kujiamulia mambo yao, na ni jambo tofauti kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika kubuni mipango shirikishi na kuitekeleza. Naomba wananchi wote wakubali wajibu huo na wautekeleze kwa ukamilifu.
Utawala bora ni zaidi sana ya vita dhidi ya rushwa, au kufanya Uchaguzi Mkuu. Utawala bora pia ni kupanua uhuru wa wananchi - uhuru wa maoni, uhuru wa kuchangia mawazo kuhusu hatma ya jamii, uhuru wa kudai uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi, uhuru unaoimarishwa kwa elimu, ikiwemo elimu ya watu wazima na elimu ya uraia.
Mwananchi lazima aelewe kuwa ni haki yake, na ni wajibu wake, kumtaka diwani wake awaeleze wananchi wa kata yake kuhusu mapato, matumizi na mipango ya maendeleo ya kata na halmashauri inayohusika. Mwananchi aelewe madaraka, na mipaka ya madaraka hayo, aliyo nayo Mtendaji wa Kijiji au Mtendaji wa Kata. Kisha aelewe nini cha kufanya Mtendaji anapovuka au kukiuka maadili ya kazi zake, au mipaka ya madaraka yake. Uhuru wa kiwango hicho nao ni silaha katika vita dhidi ya umaskini utokanao na unyonge wa kukosa kauli, na ni chachu muhimu ya utawala bora.
Mazingira ya Nje ya Nchi
Ndugu Wananchi,
Nchi yetu si kisiwa, na katika dunia yetu ya utandawazi, ambapo maingiliano kati ya nchi na nchi nyingine ni makubwa, yanayotokea nje ya nchi yetu yanatugusa, ama kwa faida au kwa hasara.
Hivyo mojawapo ya mambo tuliyoyapigia kelele sana kule Brussels ni:
-
Kuzitaka nchi tajiri zitimize ahadi yao ya kuchangia angalao 0.7% ya pato la taifa kama msaada kwa nchi zote maskini; na 0.2% kati ya hizo ikielekezwa kwa makusudi kwa nchi maskini kuliko zote;
-
Kuzitaka nchi tajiri kusaidia, kwa sera na ushawishi mwingine, uwekezaji mitaji katika nchi maskini;
-
Kuzitaka nchi tajiri zote, sio zile za Ulaya tu, kufungua milango yao kwa bidhaa zote, isipokuwa silaha, kutoka nchi maskini; na
-
Kufuta au kupunguza sana madeni ya nchi maskini.
Kimsingi wametukubalia; na kwa kweli sisi kama Tanzania tumefaidika sana na misaada, uwekezaji, ahadi ya kupunguziwa madeni, na fursa za biashara. Tunawashukuru wanaotusaidia. Lakini, kwa ujumla wao nchi tajiri hazijatimiza ahadi zao kwa nchi maskini. Nitatoa mfano.
Kule Paris, mwaka 1990, tuligawana na tulikubaliana juu ya majukumu katika vita dhidi ya umaskini. Sisi nchi maskini tumetekeleza mengi kati ya majukumu yetu. Nchi maskini, pamoja na nyingi barani Afrika, zimezingatia kuliko wakati wowote ule wajibu wa utawala bora, demokrasia ya vyama vingi, uhuru wa vyombo vya habari, sera za uchumi wa soko, kufungua milango ya biashara na nchi za nje, na kadhalika. Na sisi Tanzania ni mfano halisi wa waliotimiza wajibu wao.
Lakini kwa upande wao, nchi tajiri zilizo nyingi hazikutimiza yale tuliyokubaliana. Kwa mfano tu, badala ya kuongezeka, misaada kwa nchi maskini kuliko zote imepungua kwa asilimia 45. Pale tulipokuwa tunapata 100 sasa tunapata 45! Misaada kupitia mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa yanayotusaidia sana nayo imepungua sana kwa sababu wachangiaji wamepungukiwa nia.
Uwekezaji mitaji nao unaathirika kutokana na mazingira magumu, ikiwemo miundo mbinu isiyokuwa mizuri na ya kuaminika, kama vile umeme, barabara, reli, simu na kadhalika. Wakati mwingine, kwa umaskini wetu, mazingira hayo yanaweza kuboreshwa tu kwa kutumia fedha za misaada na mikopo. Na sisi ni mfano. Barabara zetu za lami karibu zote zimejengwa kwa kiasi kikubwa kwa mikopo na misaada. Vivyo hivyo kwa miradi ya umeme, maji na kadhalika.
Inakadiriwa pia kuwa iwapo nchi za Ulaya zingeruhusu kwa dhati kuwa mazao ya nchi maskini sana yaingie barani humo bila ushuru au kikwazo chochote, nchi hizi 49 maskini kuliko zote zingepata nyongeza ya sh.166.5 bilioni (USD 185 m.) kwa mwaka. Lakini mazao yetu mengi ni ya kilimo ambayo yana vikwazo vingine vingi vilivyojificha. Kwa mfano, ni vigumu kwa wakulima wa Tanzania, ambao hawapati ruzuku yoyote, kushindana na wakulima wa baadhi ya nchi tajiri wanaopewa na Serikali zao ruzuku ya wastani wa sh.900 bilioni (USD 1 bi) kwa siku.
Kwa upande wa madeni, nchi nyingi bado hazijafikia hatua ya uamuzi wa mwisho wa kupewa msamaha kufanywa, na bado maswali yanaulizwa iwapo msamaha utakaopatikana utatosha kweli kuchochea vita dhidi ya umaskini au bado fedha zinazohitajika kwa elimu na afya itabidi ziendelee kutumika kulipa madeni.
Ufumbuzi ni Nini
Ndugu Wananchi,
Tulichopata Brussels ni mambo mawili ya msingi. Kwanza, nchi tajiri zilirejea tena kauli yao kuwa vita dhidi ya umaskini ni jukumu la dunia nzima; ingawa wajibu wa kwanza ni wa kila mtu, kila jamii na kila taifa maskini. Pili, walitupa ahadi nyingine kuwa wataongeza misaada, watapunguza madeni, watafungua milango ya biashara na kuhimiza uwekezaji mitaji. Na sisi tumeahidi uwajibikaji, utawala bora, na kukusanya nguvu zetu za misuli na akili.
Lakini fundisho kubwa kwetu ni kuwa lazima tukubali kuwa umaskini ni wetu, na ni sisi wenye wajibu wa msingi kuupiga vita. Wengine watatusaidia, wakipenda. Sisi hatuna hiari hiyo. Tusaidiwe au tusisaidiwe lazima tujitahidi kufanya kila tunaloweza kupambana na umaskini. Viongozi watapita kwenye maeneo yenu pamoja na wataalam wa ushirikishwaji jamii. Tafadhali wasikilizeni, na mkubali kushiriki vita dhidi ya umaskini katika kila ngazi – tangu ngazi ya kaya na familia, hadi kijiji, kata, tarafa na wilaya.
Bainisheni kero zenu, na viashirio vya umaskini pale mlipo, kisha jadilianeni namna ya kuzikabili kwa nguvu zenu zote, mali zenu zote, na maarifa yenu yote. Kwa yale yaliyo nje ya uwezo wenu, Serikali Kuu na Serikali za Mitaa zitakusanya nguvu zake, kwa njia ya kodi, misaada ya wahisani na mikopo ya masharti nafuu, kuongezea kwenye nguvu zenu. Kwa kushirikiana hivyo, bila shaka katika miaka 10 ijayo, kulingana na Mpango wetu tulioupeleka Brussels, tutaifikisha nchi yetu mahali pazuri zaidi.
Huo, Ndugu Wananchi, ndio wito wangu leo. Tukubali kuwa sisi ni maskini, lakini tunayo maliasili, akili na nguvu za kutosha kupiga vita umaskini huo kwa mafanikio, na kwa muda mfupi tufanye kazi basi kwa bidii, maarifa na kushirikiana.
Mungu Ibariki Afrika.
Mungu Ibariki Tanzania.
Ahsanteni kwa kunisikiliza.
|