HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
WANANCHI, TAREHE 31 MEI, 2006
UTANGULIZI
Ndugu
Wananchi;
Katika hotuba zangu za kila mwisho wa mwezi, kwa Taifa,
nimekuwa nazungumzia masuala muhimu ya Kitaifa na wakati mwingine ya Kimataifa
yenye maslahi kwa nchi yetu. Kuna baadhi
ya mambo nimekuwa nikiyazungumzia mara kwa mara
Nimekuwa nafanya hivyo kwa sababu ya unyeti wa masuala hayo
na kwamba jitihada za kuyatafutia ufumbuzi zilikuwa zinaendelea. Kila wakati nimekuwa nikiwafahamisha hatua
mbalimbali ambazo Serikali imekuwa inachukua au inajiandaa kuchukua katika
kukabiliana na matatizo yote hayo.
Ndugu Wananchi;
Kwa vile matatizo hayo bado yapo, hata leo pia nimeonelea
nitumie fursa hii kuyazungumzia ili nanyi muweze kuelewa hali halisi ilivyo
hivi sasa. Aidha, nitawafahamisha hatua tunazoendelea kuchukua katika
kukabiliana na matatizo hayo yote.
Shukrani
Ndugu
Wananchi;
Sina budi kuwashukuru
Hali ya Chakula Nchini
Ndugu Wananchi;
Naomba nianze na suala la chakula.
Kwa jumla, hali ya
upatikanaji wa chakula nchini bado ni tatizo kwani bado Wananchi wenzetu wengi
wanaishi kwa kutegemea chakula cha msaada kutoka Serikalini na kwa wafadhili
wengineo.
Hivi sasa Serikali inaendelea kuwahudumia wananchi wenzetu
wenye shida. Kwa ajili hiyo tunaendelea
kusambaza tani 42,000 za chakula cha msaada kwenye maeneo yenye upungufu. Kwa mujibu wa hali ya mvua ilivyokuwa msimu
huu kuna dalili kwamba huenda mavuno yakawa mazuri kwa sehemu kubwa ya nchi
yetu. Yatakuwepo maeneo machache
yatakayokuwa na upungufu ambao hautakuwa kero kubwa. Matumaini yetu ni kwamba mgawo wa sasa wa
chakula cha msaada utakuwa ndio wa mwisho ulio mkubwa kutoka Serikalini kabla
ya mavuno.
Ndugu
zangu;
Wananchi
Wenzangu;
Tatizo la uhaba wa chakula lililoikumba nchi yetu msimu huu
limetufundisha mengi, na hasa yapo mafunzo makubwa mawili. Kwanza; kwamba kuwa
na Hifadhi ya Taifa ya Chakula yenye akiba ya kutosha ni jambo la msingi na
muhimu
Nimekuwa najiuliza
Hivyo basi, katika msimu ujao wa mavuno tutahakikisha kuwa
tunanunua chakula cha kutosha na kukihifadhi kwenye maghala ya Hifadhi ya
Chakula ya Taifa (SGR) yaliyoko sehemu mbalimbali hapa nchini. Utaratibu huu umetufaa
Nafurahi kusema kuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
ameshaanza kuchukua hatua kuhakikisha kuwa Hifadhi ya Taifa ya Chakula inayo
akiba ya kutosha. Nia yetu ni kuwa na
akiba ya chakula ya kutosha wakati wote bila kujali
Ndugu
Wananchi;
Jambo la pili kubwa tulilojifunza linahusu hali ya kilimo
chetu. Ni jambo lililo wazi kuwa kilimo
chetu bado ni duni na hakina tija ya kutosha.
Hali hii inasababisha matatizo kila tunapokosa mvua hata kama kwa msimu
mmoja
Tumedhamiria kuchukua hatua za dhati kuboresha kilimo
chetu. Kwa ajili hiyo tuko mbioni
kukamilisha mkakati kabambe wa kuendeleza kilimo nchini. Naamini tukifanikiwa katika utekelezaji wa
programu zake tutakuwa tumejenga ngome kubwa ya kupambana na upungufu wa
chakula.
Hali ya Umeme
Ndugu Wananchi;
Tatizo la umeme bado halijaisha ingawa kumekuwepo na unafuu
katika siku za hivi karibuni ikilinganishwa na miezi ya nyuma. Bado hali ya maji katika bwawa la Mtera ni
mbaya ingawaje kina kimepanda kwa mita tatu tu hadi kufikia mita 690 tangu
msimu wa mvua uanze. Kina hicho ni
pungufu kwa mita nane (8) na msimu wa mvua ndiyo umefika ukiongoni. Kutokana na hali hii ni dhahiri basi kwamba
tutalazimika kuendelea na mgao wa umeme mpaka hapo hatua za dharura za kuongeza
uzalishaji wa umeme utokanao na gesi zitakapokamilika.
Watanzania
Wenzangu;
Naomba tuendelee kuwa na subira wakati ambapo mipango ya kupata
ufumbuzi wa muda mfupi, wa kati na muda mrefu inaendelea kushughulikiwa. Tena kwa taarifa nilizopewa mipango hiyo
inakwenda vizuri. Tayari utaratibu wa
kuipatia TANESCO mitambo mipya ya megawati 100 itakayofungwa pale Ubungo
umekamilika. Uagizaji wa mitambo hiyo
utafanyika wiki chache zijazo baada ya
kukamilisha taratibu za manunuzi.
Pia, inatarajiwa wiki hii TANESCO na Serikali zitakamilisha
mazungumzo kuhusu uagizaji toka nje wa mitambo ya kukodisha ya megawati
100. Wakati huo huo maandalizi ya awali
ya mradi wa umeme wa Kinyerezi na ule wa makaa ya mawe kule Kiwira yanaendelea
vizuri.
Wananchi Wenzangu;
Napenda kurudia kauli yangu ya huko nyuma kwamba: Naamini
kuwa mara baada ya kukamilisha miradi yote hii nchi yetu itapata ufumbuzi wa kudumu
wa tatizo la umeme ambalo limekuwa ni kero kubwa kwa miaka kadhaa sasa.
Ndugu
Wananchi;
Katika hotuba zangu za nyuma nimekuwa nikielezea tatizo la
bei kubwa ya mafuta duniani.
Nilipolizungumzia mara ya kwanza mwezi Januari mwaka huu kwenye mkutano
wangu na Wazee wa Mkoa wa
Nilielezea ukweli
kwamba ni tatizo ambalo hatuna uwezo nalo kulizuia kwani hatuna mafuta hapa
nchini na uchumi wetu hauwezi kuhimili kutoa ruzuku ya bei ya mafuta. Nimekuwa nawasihi wananchi wenzangu kuutambua
ukweli huo na kwamba tujitahidi kuwa waangalifu na wabanifu katika matumizi ya
mafuta. Na leo napenda kusisitiza tena
ombi
Ndugu
Wananchi;
Tatizo la kupanda
Aidha
napenda kuitumia nafasi hii kuwaonya watu wenye tamaa ya utajiri iliyokithiri
wasitumie fursa hiyo kudhulumu. Si
sawa, si haki na ni kukosa utu kufanya
hivyo. Kwa kweli si jambo jema hata
kidogo kwa mtu au kampuni kutumia shida za wananchi kupata utajiri wa haraka
haraka. Naziomba mamlaka zinazohusika na
nishati (EWURA) na usafiri (
Ujambazi
Ndugu Wananchi;
Mapambano dhidi ya ujambazi na majambazi yanaendelea kwa
nguvu, ari na kasi ile ile. Hatutalegeza
uzi hata kidogo. Tayari tumewanyima
majambazi fursa ya kutamba
Napenda kuwahakikishia Wananchi wenzangu, kuwa tutaendelea
kupambana nao hadi ushindi kamili.
Mwelekeo wa ushindi ni mzuri na sasa tunakaribia kuuvunja uti wa mgongo
wa ujambazi. Navipongeza
Tuendeleze
ushirikiano huo mzuri ili tupate ushindi mapema. Kwa upande wake Serikali itaendelea
kuviimarisha vyombo vya usalama kwa nyenzo na utaalamu ili viweze kutekeleza
majukumu yake kwa ukamilifu na kwa ufanisi mkubwa zaidi.
MAMBO
MAPYA
Ziara Nchi za Nje:
Ndugu
Wananchi;
Katika miezi ya hivi karibuni nimekuwa nikifanya ziara za
kujitambulisha kwa nchi rafiki na majirani. Majuzi nimemaliza ziara ya nchi za Falme za Kiarabu, Ufaransa,
Marekani na Uingereza. Pamoja na
kujitambulisha
1.
2.
Pili, ni kudumisha na kuendeleza maslahi ya
kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kiusalama ya nchi yetu miongoni mwa mataifa
na mashirika ya kimataifa; na
3.
Tatu, kuipatia nchi yetu marafiki wapya na
kudumisha waliopo katika jumuia ya kimataifa.
Hii ndiyo kazi niliyokuwa
naifanya katika ziara zangu za nchi za nje.
Ziara hizo zimekuwa za mafanikio makubwa na tumefikia malengo yetu. Nitaendelea nazo siku za usoni kwa mataifa
mengine rafiki ambayo sijayatembelea.
Wakati huo huo pia tutawaalika viongozi toka mataifa rafiki duniani waje
kututembelea na kutimiza malengo yetu hayo hapa hapa nyumbani.
Mwelekeo wa Bajeti ya Serikali 2006/2007
Ndugu
Wananchi;
Jambo la mwisho ninalotaka kulizungumzia ni Bajeti
ijayo. Tarehe 15 mwezi ujao Serikali
itawasilisha Bungeni bajeti yake kwa mwaka 2006/2007. Bajeti hiyo itakuwa ndiyo ya kwanza kwa
Serikali ya Awamu ya Nne. Ni mwanzo wa
safari ya miaka mitano ya kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi
na masuala mengine muhimu kitaifa.
Tutaanza kuchukua hatua za kuongeza kasi ya kukuza uchumi na kupambana
na umaskini wa kipato wa Watanzania.
Kadhalika tutaanza kuchukua hatua za kukuza ajira na
kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii.
Pia tutaanza safari ndefu ya kuboresha maslahi ya watumishi wa
umma. Bahati mbaya bajeti hiyo
imeandaliwa wakati uchumi wa nchi yetu umetikishwa na matatizo ya ukame,
upungufu wa chakula, umeme na bei kubwa za mafuta.
Ni dhahiri kwamba hali hii inaweza kuwa na athari kwa
mwenendo mzima wa bajeti ya mwaka ujao, ukuaji wa pato la taifa, na hasa kwa
uzalishaji katika sekta ya kilimo na viwandani.
Pia inaweza kuathiri akiba ya pesa za kigeni, mapato ya Serikali na hivyo
kupunguza kwa kiasi fulani uwezo wetu wa kutekeleza mipango na mikakati ya
maendeleo tuliyoibuni. Hata hivyo, ni
dhamira yetu kuhakikisha kuwa tunajitahidi kuchukua hatua mbalimbali ili
kupunguza makali ya athari hizo.
WAJIBU
WETU
Ndugu
Wananchi;
Sisi sote tunao wajibu wa kuhakikisha kwamba uchumi wetu
unaendelea kukua licha ya matatizo niliyoyaeleza hapo juu. Kila mmoja wetu anao wajibu wa kufanya kazi
kwa bidii na maarifa pale alipo. Aidha,
sote tunawajibika kuchangia katika kukuza mapato ya serikali. Kadhalika, tuongeze juhudi za kuvutia mitaji
toka ndani na nje na kuongeza misaada toka nje ili kujijengea uwezo mkubwa
zaidi wa kuleta maendeleo yetu na ya nchi yetu.
Ndugu Wananchi;
Mwisho, napenda kuwashukuru tena nyote kwa uelewa wenu
mkubwa wa hali inayoikabili nchi yetu kwa sasa.
Nawashukuru pia kwa uvumulivu wenu, ushirikiano na mshikamano wenu.
Nawaombeni tuendelee kushirikiana, kushikamana na
kusaidiana.
Daima tukumbuke msemo wa wahenga kuwa, Umoja ni nguvu, Utengano ni
udhaifu. Na, Silaha ya Mnyonge ni Umoja. Hima tushirikiane, tuwe kitu kimoja.
Kwa
pamoja tutashinda!
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki
Ahsanteni kwa Kunisikiliza.