Maji

.

Upatikanaji wa maji salama ni muhimu katika kupigana na umaskini na matatizo ya afya.  Watu maskini ambao wengi wao huishi vijijini wana nafasi finyu ya kupata maji safi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kwa ajili ya mazao na matumizi ya afya. Faida za uchumi zinaweza kupatikana siyo kwa njia ya moja kwa moja tu bali kwa kuwa na afya bora na kuokoa muda unaotumika kuhangaika na kazi za kuchosha za kubeba maji kwa umbali mrefu.  Takwimu zinaonyesha kuwa magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya maji hupatikana zaidi katika sehemu ambapo watu wanatumia maji yaliyoambukizwa au hawana maji ya kutosha kwa matumizi yao ya kila siku.

 

Idadi ya magonjwa hayo ni zaidi ya nusu ya magonjwa yanayowaathiri watu na kwamba asilimia themanini ya magonjwa yanayowashambulia watanzania wanaoishi vijijini.  Serikali inalenga katika upatikanaji wa maji vijijini.  Usimamizi wa maji pia unawashirikisha washika dau wote kwa ajili ya kufanikisha upatikanaji wa maji wa kutegemewa, unaofaa na maji hayo yanatumika ipasavyo, yanalindwa na kuhifadhiwa.

 

Sehemu moja ya tatu ya Tanzania inapokea chini ya milimeta 800 ya mvua na hivyo kusababisha sehemu hiyo kuwa kavu au nusu jangwa.

 

Ni sehemu moja tu ya nchi ambayo hupata zaidi ya milimeta 1000 za mvua.  Aidha, msimu wa kiangazi, ambao hudumu kuanzia mwezi Juni hadi Oktoba hupunguza mtiririko wa maji katika mito na maji hukauka kwenye mabwawa.  Lakini asilimia 7 ya Tanzania hufunikwa na maziwa ya maji kwenye mipaka yake licha ya maziwa mengine ya maji ambayo  yako ndani ya nchi. 

 

Maziwa hayo  ya maji ni pamoja na Ziwa Victoria (Ziwa la maji baridi la pili kwa ukubwa duniani), Ziwa Tanganyika (la pili kwa kina kirefu duniani), na Ziwa Nyasa.  Maziwa ya maji ambayo yako ndani ya nchi ni pamoja na maziwa Rukwa, Eyasi na Manyara.  Ipo pia mito mingi mikubwa ambayo humimina maji kwenye maziwa.  Maji yaliyo chini ya ardhi pia ni chanzo kingine cha maji kwa ajili ya maeneo ya makazi ya mijini na vijijini.

 

Matumizi makubwa kuliko yote ya maji ni ya nyumbani.  Kutokana na shughuli za kiuchumi na za kuhudumia jamii ambazo, kwa njia moja au nyingine, zote zinatumia maji, upatikananji na usambazaji wa maji umekuwa ni mzigo mkubwa kwa serikali ambayo haiwezi kuubeba peke yake bila ya ushirikiano wa sekta bianfsi.  Nia  ya sera ya serikali kuwashirikisha wafadhili katika mirdi yote ya maji mijini na vijijini.  Kwa muda mrefu mchango wa sekta ya maji kwa pato la taifa (GDP) limebaki kuwa asilimia 0.2 ambacho ni kiwango kidogo sana ikitilia maanani umuhimu wa sekta hii katika uchumi kwa kulinganisha na sekta, kwa mfano ya kilimo ambayo kwa mwaka 1999 ilichangia asilmia 48.9 ya pato la taifa.  Lakini maji kwa vyovyote vile, ni muhimu zaidi katika kukuza maendeleo ya uchumi wa Tanzania kwa sababu sekta khiyo inaunganisha sekta nyingine zote kwa mfano, hata kilimo ambayo ni sekta kubwa kuliko zote, haiweze kufua dafu bila maji kwa bahati nzuri, maji nchini Tanzania ni sekta ambayo ina uwezo wa kukua ikilinganishwa na sekta nyinginezo mwaka 1999 maji yalichangia kwenye pato la taifa ongezeko la asilimia 3.0.  hivyo, Serikali inahamasisha uwekezaji binafsi katika sekta hiyo ya maji.

 

Vyanzo vya maji vilivyopo:

 

Tanzania ina vyanzo vya kutosha vya maji kukidhi mahitaji yake, na vyanzo hivyo ni pamoja na maji yaliyo juu na chini ya ardhi.  Asilimia 7 ya ardhi imefunikwa na maziwa ya maji matamu ambayo yako mpakani licha ya maziwa mengine ambayo yako ndani ya nchi.

 

Hata hivyo kuna tofauti kubwa ya kuwepo kwa maji katika sehemu mbalimbali za nchi.  Tofauti hiyo inatokana na tabia ya mahali, mvua na hali ya hewa.

 

Maji yaliyo juu ya ardhi

 

Vyanzo vya maji yaliyo juu ya ardhi yanatokana na maziwa ya maji, mito, chemichemi, mabwawa na maziwa ya maji yaliyotengenezwa na binadamu.  Asilimia 50 ya maji yaliyo juu ya ardhi yanapatikana kwenye mito ambayo humwaga maji yake moja kwa moja katika Bahari ya Hindi.  Mito hiyo ni ya Pangani, Wami, Mkondoa, Ruvu, Rufiji, Ruaha, Mbwemkulu, Lukuledi na Ruvuma.  Asilimia 50 ya maji ya juu iliyobaki imegawanywa katika maji ambayo hutiririka na kuishia katika mabonde bila kufika baharini.  Maji hayo yanaishia Ziwa Rukwa, Bonde la Bubu, Ziwa Eyasi na Ziwa Manyara.  Maji ya mito mengine hutiririka katika Ziwa Victoria (mito Meri, Maru na Kagera), mto Malagarasi humwaga maji yake katika Ziwa Tanganyika na mto Songwe na Ruhuhu inatiririka kuelekea kusini na kumwaga maji katika mfumo wa Ziwa Nyasa – Zambezi.

 

Mabwawa

 

Tanzania ina hekta 5,439,000 za maziwa na mabwawa ambayo ni asilimia 5.8 ya ardhi yote ya nchi, lakini asilimia hiyo haijumuishi mabwawa ambayo hutokana na mafuriko ya msimu wa mvua.

 

 

 

Mfumo wa kuchukua maji

 

Tanzania imegawanywa katika mifumo mitano ya kuchukua maji yanayotiririka kutoka mito yake.  Mifumo hiyo ni:

 

1.            Mfumo wa kuchukua maji yanayoingia katika Bahari ya Hindi.

 

2.            Mfumo wa maji yaingiayo katika Ziwa Eyasi, Natron na Bonde la Bubu.

 

3.            Mfumo wa Ziwa Rukwa.

 

4.            Mfumo  wa Bahari ya Atlantic na

 

5.            Mfumo wa Bahari ya Mediterranean.

 

Vyanzo vya maji yaliyo chini ya Ardhi

 

Maji yaliyoko chini ya ardhi ni chanzo kikubwa cha maji katika maeneo mengi ya Tanzania na ni njia nyingine ya nyongeza ya kuaminika ya kupata maji katika maeneo ya kati na kaskazini ya nchi ambayo  yanakabiliwa na ukame katika mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga, Tabora, Mwanza, Mara, Arusha, Pwani na kusini mwa Kilimanjaro.

 

Sera ya Sekta ya Maji

 

Maendeleo ya sekta ya maji nchini Tanzania inaongozwa na sera ya sekta ya maji.  Sera inayotumika ni ile iliyotolewa mwaka 1991.  Hivi karibuni serikali imeanzisha marekebisho ya mpango ambao utahusisha sekta zote za jamii, uchumi na siasa ikiwemo na ya maji.  Hivyo sekta ya maji imeongezewa nguvu kwa mpango unaoendelea kwa kurekebisha sekta hiyo ambayo  itastawisha sera ya maji katika kuimarisha masuala ya usimamizi na utendaji kwa kuzingatia yafuatayo:

 

¨      Maji  hustahili kufikiriwa kuwa ni hitaji la msingi.

 

¨      Sera  ya Serikali ina nia ya  kufanikisha mpango wa upatikanaji wa maji safi na salama na ya uhakika katika maeneo ya vijijini na mijini.

 

¨      Lengo la sera ni kuhakikisha kuwa maji safi na salama yanapatikana katika umbali usiozidi mita 400 kutoka sehemu wanazoishi watu.

 

¨      Shughuli za kuendeleza na usambazaji wa maji ziongozwe na soko huru ambapo wote wanaohusika, kama vile jamii, sekta binafsi vyama visivyo vya kiserikali viwe vya hapa nchini au nje ya nchi viweze kuwekeza katika sekta hii ili kusaidia juhudi za serikali katika kuendeleza na upatikanaji wa huduma za maji.

 

¨      Serikali itaamsha jitihada za kuishirikisha sekta binafsi na wahisani katika huduma ya upatikanaji wa maji kwa madhumuni ya kuongeza ufanisi na uwezo na hivyo kujenga huduma za maji zinazotegemewa.

 

Jukumu na kazi za Serikali

 

Wakati sekta ya maji ni eneo huria kwa vyombo vya aina yote vyenye moyo wa kuipenda sekta hiyo, Serikali kwa kupitia wizara yenye dhamana ya maji ina wajibu na kazi kuu zifuatazo:

 

¨      Kuendelza, kukagua na kukuza sera ya maji safi na maji taka.

¨      Kuhimiza, kushirikisha, kusimamia na kuratibu huduma za maji safi na maji taka kwa ajili ya watu wote kwa kutilia maanani  masuala ya jinsia.

¨      Kuwaendeleza wataalam wenye uwezo mkubwa kushughulikia sekta hiyo.

 

Sheria

 

Usimamizi na taratibu za kuongoza masuala ya maji uko katika Control and Regulation Act Na 42 ya mwaka 1974 na Sheria ya  marekebisho Na. 10 ya 1981 pamoja na Miscellaneous Act No. 17 ya 1989.   Sheria kama ilivyorekebishwa, imetamka kuwa maji yote ya nchi yako chini ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeweka taratibu za matumizi ya maji na kumpa madaraka Afisa Mkuu wa Maji kutayarisha sera na  kugawa haki ya kutumia maji kwa ngazi ya kitaifa.  Maji ambayo yako kwenye mabonde yatakuwa chini ya ofisi za maji ya Bondeni anayewajibika na maji hayo ni Afisa maji wa Bonde.

 

Utendaji kazi wa sekta

 

Hadi sasa maji mengi yanayotumika ni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.  Ingawa asilimia 80 ya watu wanaishi vijijini na asilimia 20 tu wanaishi mijini, maji mengi zaidi hutumika vijijini.  Hata hivyo, licha ya umuhimu mkubwa wa maji ambao haujionyeshi, vyanzo vingi kvya maji bado viko duni na kwamba idadi kubwa ya watu wanatumia maji kutoka vyanzo duni havikutengenezwa.  Vyanzo hivyo duni ni maziwa ya  maji, mito, mabwawa, visima vifupi na vya wazi.  Hadi kufikia mwaka 1999, asilimia 45 wa watu waishio vijijini na asilimia 68 ya watu wanaoishi mijini wana uwezo wa kupata maji safi na salama.  Wakati tarakimu hizo zinaonyesha wastani tu wa kitaifa lakini hali halisi inatofautiana sana kati ya sehemu na sehemu kadiri ilipo kijeografia.

 

Kuhusu huduma ya maji machafu, maeneo mengi ya mijini huendelea kuathirika na huduma duni inayotolewa.  Ni asilimia 7 tu ya wakazi wa mijini ambao huduma zao za maji machafu zimeunganishwa kwenye huduma iliyoko ya mifereji ya maji taka ambayo hupatikana kwenye miji michache tu na kwamba mifereji hiyo ilijengwa miaka mingi iliyopita.

 

Washika Dau wakubwa wa Sekta  ya Maji.

 

Ni kutokana na sera ya maendeleo ya nchi ambayo kwa muda mrefu imeweka mkazo mkubwa wa kuendeleza sekta za jamii, ikiwemo ya maji, aidha, na ni kutokana na sera ya maji ambayo imewahamasisha washika dau wengine (mbali ya serikali) kushughulika na maendeleo ya sekta ya maji, ndiyo maana hii leo Tanzania inayo orodha ndefu ya mashirika ya serikali na ya watu binafsi wanao shughulika katika kuendeleza na kusambaza huduma za maji safi na maji taka..

 

Nafasi za kuwekeza

 

Ziko dalili zinazoashiria kuwa zipo nafasi na faida za kuwekeza katika sekta ya maji kwa wakati huu na miaka mingi ijayo kama ifuatavyo:-

 

¨      Kiko chanzo kikubwa sana cha maji ambacho bado hakijatumiwa kwa kupata faida.

 

¨      Yako mahitaji makubwa ya  huduma kwa ajili ya sekta ya maji ambayo bado hayajashughulikiwa na kwamba mahitaji bado yanaongezeka kadiri idadi ya  watu inavyokuwa na wa maendeleo ya uchumi yanavyongezeka.

 

¨      Sera ya sasa ya Serikali ni kuziendeleza kuzishirikisha sekta nyingine katika kufanikisha sekta za jamii ikiwemo sekta ya maji.

 

¨      Iko tayari idadi kubwa ya mashirika yaliyowekeza katika sekta khii ambayo tayari yana uzoefu wa kujivunia na ambayo yako tayari kutoa nafasi ya kuingia ubia na mwekezaji mwingine yeyote.

 

¨      Sekta ya maji inayo maeneo mengi ya kuweza kuwekeza kama vile katika kuhifadhi maji au katika ujenzi wa miundo mbinu (kwenye vyanzo vya maji, chemchem), au kuwekeza katika utengenezaji au upatikanaji wa mashine, vifaa pamoja na kuendesha mafunzo ya watalaamu.

Title

.

Title

.

Title

.