HOTUBA YA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI,

MHE. OMAR RAMADHAN MAPURI (MB) KUMKARIBISHA

RAIS WA ZANZIBAR, MHE. AMANI ABEID KARUME KUFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA MAAFISA WAKUU

WA JESHI LA POLISI NCHINI KWENYE UKUMBI WA MIKUTANO WA KIMATAIFA ARUSHA TAREHE

15 DESEMBA, 2003

 

·        Mheshimiwa Amani Abeid Karume, Rais wa Zanzibar

·        Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Mohammed Babu

·        Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Omari Mahita

·        Makamishna wa Jeshi la Polisi

·        Naibu Makamishna wa Jeshi la Polisi

·        Makamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa na Vikosi

·        Viongozi mbali wa Serikali Mkoani Arusha

·        Mstahiki Meya wa Manispaa ya Arusha

·        Wakuu wa Madhehebu mbalimbali ya dini Mkoani Arusha

·        Wageni Waalikwa

·        Mabibi na Mabwana

 

Mheshimiwa Rais

Kazi yangu asubuhi hii ni kukukaribisha rasmi kutufungulia mkutano wa mwaka wa Maafisa Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini, unaofanyika hapa mjini Arusha.  Lakini kabla sijafanya hivyo napenda kuchukua fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kutoa shukrani zetu nyingi za dhati kwako kwa kukubali kuja Mkoani Arusha kutufungulia mkutano huu.

 

Mheshimiwa Rais

Jana tarehe 14/12/2003 tulikuwa nawe Wilayani Same Mkoa wa Kilimanjaro ambapo ulitufungulia Kituo cha Polisi Same kilichojengwa kwa nguvu za wananchi na leo tupo nawe hapa Arusha ukitufungulia mkutano wa mwaka wa Maafisa Wakuu wa Jeshi la Polisi.  Mheshimiwa Rais hatuna lugha ya kueleza shkrani zetu nyingi za dhati kwako, kwani katika hali ya kawaida, siyo rahisi kuwa na kiongozi mkubwa wa hadhi yako, kwa siku mbili mfululizo, katika mikoa miwili tofauti kwa shughuli za idara hiyo hiyo moja.  Kwa kweli tunakushukuru sana.  Jambo hili siyo tu linatupa faraja kubwa kwa jinsi viongozi wetu mnavyoonyesha upenda na moyo wa kutujali, bali pia linatupa changamoto na ari ya kuongeza ufanisi katika utendaji kazi zetu.

 

Mheshimiwa Rais

Mambo mengi kuhusu Jeshi la Polisi, yakiwemo mafanikio na matatizo umeshaelezwa kwa kirefu na ufasaha na Inspekta Jenerali wa Polisi.  Sitapenda kukuchosha kwa kurudia kusisitiza hayo.  Hata hivyo, napenda kuchukua fursa hii kuishukuru Serikali ya Awamu ya tatu ya CCM kwa kutekeleza kikamilifu ilani yake iliyouza kwa wananchi mwaka 2000 kuhusu vyombo vya ulinzi na usalama likiwemo Jeshi la Polisi.

 

Mheshimiwa Rais

Kama alivyosema IGP Serikali imekuwa ikifanya juhudi kubwa kutatua matatizo mbalimbali ya Jeshi la Polisi, ikiwa ni pamoja na kuongeza bajeti