HOTUBA YA MGENI RASMI, WAZIRI
WA MAMBO YA NDANI MHE. OMAR RAMADHAN MAPURI KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA SIKU
YA SILAHA UMOJA WA MATAIFA ‘UN ARMS DAY’ ITAKAYOFANYIKA VIWANJA VYA JANGWANI
TAREHE
· Waheshimiwa
Mabalozi wanaowakilisha nchi zao katika maadhimisho haya.
· Mheshimiwa
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na
Mwakilishi wa UNDP nchini Mhe. John Hendra.
· Kamishna
wa Polisi, Laurean Tibasana.
· Wajumbe
wa Kamati ya Taifa ya kuratibu na kudhibiti silaha na
Wajumbe wa Kamati ya kuratibu na kudhibiti silaha Mkoa wa
· Mwenyekiti
wa Shirika lisilo la kiserikali la CEPEDE, Bw. Emanuel
Mallya na Viongozi wa NGO zinazoshiriki.
· Wawakilishi
wa vyombo vya habari waliopo.
· Washiriki
wengine wote.
· Mabibi
na Mabwana.
Awali
ya yote napenda kuchukua fursa hii kwa niaba ya
wananchi wote kuwashukuru waandaaji wa sherehe hii muhimu ya kimataifa ya
kuadhimisha Siku ya Silaha ya Umoja wa Mataifa (UN Arms Day) kwa uamuzi wao wa kuadhimisha siku hiyo hapa Mkoani
Uamuzi
uliofanywa na Jeshi la Polisi, asasi zisizo za kiserikali, wananchi na Serikali
kwa ujumla wa kuamua kuadhimisha Siku ya Silaha ya Umoja wa Mataifa ni wa
busara, hasa ukizingatiwa kuwa tatizo la uzagaaji wa silaha ndogo unaleta maafa
na kuathiri shughuli za maendeleo kwa wananchi wetu kwa kiasi kikubwa. Ni kweli kabisa kwamba hali ya uhalifu
unaotokana na uzagaaji wa silaha ndogo ilivyo humu
nchini mwetu haiwezi kulinganishwa na hali ilivyo kwenye baadhi ya nchi
zinazotuzunguka zenye migogoro na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe na hata
kusababisha wakimbizi wengi kuingia nchini mwetu na silaha. Lakini ukweli huo hauwezi kutupa faraja
kutokana na fadhaa inayowapata Watanzania kila
yanapotokea matukio ya uhalifu wa kutumia silaha. Matukio mengi ya uhalifu
Silaha
hizi haramu ambazo zimo mikononi mwa majambazi zinaleta madhara makubwa kwa wananchi wetu na hivyo hazina budi kudhibitiwa. Kumbukumbu zinaonyesha kwamba
silaha nyingi haramu bado zimo mikononi mwa wahalifu. Kwa mfano, takwimu zinaonyesha kuwa katika kipindi
cha kuanzia Januari hadi Desemba mwaka 2003, jumla ya silaha haramu 850
zilikamatwa nchini na watuhumiwa 838 walikamatwa,
ambapo katika mkoa wa
Ndugu washiriki wa
sherehe hizi,
Matukio
ya unyang’anyi wa kutumia silaha nayo bado ni
mengi. Matukio haya mbali ya kuleta
maafa kwa wananchi wasio na hatia, pia yanasababisha
uporaji wa
Matukio
haya ya unyang’anyi wa kutumia silaha mbali na kwamba
yanatokea katika mikoa mingine nchini, lakini ninasema kuwa mkoa wa
Ndugu washiriki wa
sherehe hizi,
Hayo ni baadhi tu ya madhara yaletwayo na uzagaaji holela wa
silaha ndogo nchini. Kuna
kila sababu ya kuhakikisha kuwa tatizo hili linapatiwa ufumbuzi. Umefika wakati sasa kwa
jamii na wananchi kwa jumla watambue kuwa jukumu la kukabiliana na hatimaye
kutokomeza tatizo la uzagaaji na matumizi mabaya ya silaha si jukumu la Jeshi
la Polisi pekee, bali jamii nayo inawajibika.
Waathirika
wakubwa wa matukio mengi ya uhalifu utokanao na
matumizi mabaya ya silaha ni raia wa kawaida tu. Kwa hali hiyo wananchi wanapashwa kutoa
ushirikiano na sio kuliachia Jeshi la Polisi. Tunafahamu uwezo wa Jeshi hili ni mdogo kwa
idadi ya watumishi wake, pamoja na vitendea kazi vyake duni ukilinganisha na
idadi ya wananchi na ukubwa wa nchi yetu, hivyo hatuna budi kwa ujumla wetu
kulisaidia Jeshi hili kukabili uhalifu nchini na hili naomba nilisisitize
sana. Pamoja na
wito huo lakini, sina budi niwashukuru wananchi kwa ushirikiano wao ambao sasa
wanaonekana kuutoa kwa Jeshi la Polisi hivi siku za karibuni. Lakini wapo wanaojitoa muhanga kukabiliana na wahalifu wakiwemo majambazi. Matokeo ya ushirikiano huo wa
wananchi ni kwamba sasa uhakika ni mkubwa wa kukamatwa kwa wahalifu kila
linapotokea tukio la uhalifu. Hata
silaha zinazokamatwa, zinapatikana kutokana na taarifa
za wananchi.
Napenda
kutoa wito maalumu kwa waganga wa kienyeji waache
kusaidia kisaikolojia wahalifu eti kuzindika silaha zao au kuwapa imani kwamba
eti hawatoweza kuonekana watapokuwa wakifanya uhalifu. Huo si aina ya uganga wa
kienyeji tunaoutaka kwani unachochea uhalifu.
Nawaomba waganga hao kwamba wanapoendewa na
wahalifu, watafute njia ya kuwaripoti Polisi.
Ndugu washiriki,
Kuna
mipango ambayo inaandaliwa na Jeshi la Polisi
kuhusisha wananchi hasa kwenye ngazi za kata, vijiji na serikali za mitaa ili
kutoa mafunzo kwa askari mgambo, sungusungu na vikundi vingine vya ulinzi ili
kufanyike operesheni za pamoja kwa kushirikiana na asasi zisizo za
kiserikali. Vikundi hivi vya ulinzi
pamoja na asasi zisizo za kiserikali baada ya kupewa
mafunzo hayo ya awali watakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kushirikiana na
vyombo vyetu vya dola katika kuwafichua wale wote wanaomiliki silaha kinyume
cha sheria na hatimaye kuwafikisha katika vyombo vya sheria. Mkakati huo unaoandaliwa na
Jeshi la Polisi ninauunga mkono na nina hakika kwa kufanya hivyo tutaweza
kuboresha hali ya usalama wa nchi yetu.
-
Kwa kuzishirikisha asasi zisizo za kiserikali
ambazo zina nafasi kubwa ya kuwafikia wananchi wa
kawaida walio wengi katika maeneo
-
Asasi hizi zisizo za kiserikali vile vile
zinaweza kusaidia kutoa elimu kwa jamii ili jamii na
wananchi kwa ujumla watambue kuwa jukumu la kukabiliana na uzagaaji na matumizi
mabaya ya silaha si la Jeshi la Polisi pekee, bali nao wana nafasi kubwa ya
kusaidia.
-
Asasi zisizo za kiserikali vile vile zinaweza
kusaidia kuanzisha au kuendeleza shughuli mbadala za kiuchumi ili kuweza kuwasaidia wale wachache wenye fikra potofu za
kutegemea kufanya uhalifu waweze kuungana katika vikundi na kufanya shughuli za
maendeleo.
-
Tunategemea asasi zisizo za kiserikali kufanya
harambee ya kuchangisha fedha zitakazosaidia kutekeleza Mpango wa Taifa wa Kuratibu na Kudhibiti Silaha, hususani wakati wa
kufanya operesheni za pamoja za kukamata silaha na wahalifu.
Ndugu
washiriki nisingependa kuwachosha kwa kusema mengi,
ila napenda kumalizia kwa kuwakumbusha kuwa maadhimisho haya yanalenga katika
kutukumbusha sote madhara ya uzagaaji na matumizi mabaya ya silaha ndogo, na
hivyo tuungane kwa pamoja ili tudhibiti na hatimaye kutokomeza kabisa tatizo
hili.
Ninamalizia
kwa kutoa wito kwa wananchi wote kwa ujumla kuendelea
kushirikiana na vyombo vyetu vya dola ili nchi yetu na Ulimwengu kwa ujumla
tuwe kwenye amani na utulivu.
Ahsanteni
kwa kunisikiliza