TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
UFAFANUZI
KUHUSU AMRI YA KUPIGA MARUFUKU VYAMA VYA SIASA KUENDESHA MAFUNZO YA JUDO NA KARATE
1.
Tarehe 25/3/2004
katika mkutano na waandishi wa habari huko Zanzibar, Mheshimiwa Capt. (Mst.) John Chiligati (Mb), Naibu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi alitangaza amri ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi ya kupiga marufuku vyama vya siasa kuendesha mafunzo ya judo na karate. Toka wakati huo
Chama cha CUF kimekuwa kikitoa kauli kupitia taarifa kwa vyombo vya habari na
hotuba za baadhi ya viongozi wake kwenye mikutano ya hadhara zikikejeli na
kubeza tangazo hilo na kujaribu kuonyesha kana kwamba tangazo hilo lilikuwa la
Mheshimiwa Chiligati mwenyewe tu na kwamba eti lilipingana na amri ya Waziri
mwenyewe wa Mambo ya Ndani ya Nchi, yaani mimi.
2.
Napenda
kuthibitisha kwamba amri iliyotangazwa na Mheshimiwa Chiligati ni amri yangu
ambayo niliitoa kimaandishi kwa Jeshi la Polisi toka tarehe
Ruhusa
Ya Mafunzo na Masharti yake
3.
Napenda nieleze
kwa ufupi ruhusa niliyokuwa nimewapa CUF na mazingira niliyoitolea.
4.
Muda mrefu huko
nyuma tulikuwa tukipokea taarifa za kiintelejensia kwamba CUF ilikuwa ikifanya
kwa siri mafunzo ya kijeshi na
kigaidi. Wakati mwengine ilidaiwa kwamba
mafunzo ya karate na judo yalitolewa hata katika baadhi ya
misikiti, dai ambalo liliunganisha na tuhuma za udini zinazoelekezwa kwa CUF,
haidhuru huwa inazikanusha.
5.
Kwa bahati mbaya
kila tulipozifuatilia taarifa
6.
Tarehe
7.
Tarehe
(a) Kabla ya kuanza mafunzo waliarifu Jeshi la Polisi ili
lijiridhishe kwamba mafunzo hayo hayana mwelekeo wa kijeshi.
(b) Watakapofanya mafunzo baada ya kuruhusiwa na Polisi
waliarifu Jeshi
8.
Kwa upande wa
pili, nililielekeza Jeshi la Polisi liwape CUF ushirikiano
Kwa
Nini Niliwaruhusu?
9.
Niliwaruhusu kwa
sababu zifuatazo:
(a)
(b) Pili, suala la chama cha siasa kutoa mafunzo kwa
wanachama wake ni jambo la kawaida.
Tunazo taarifa za vyama vingi vinavyotoa mafunzo mbali mbali kwa
wanachama wao katika mazingira ya uwazi na hatuna matatizo navyo.
(c) Tatu, kwa dhamira ya Muafaka, nilitaka niwape CUF
fursa ya kujisafisha na tuhuma dhidi
(d) Nne, nilitaka watoke mafichoni ili tuyafuatilie
mafunzo hayo na kuyadhibiti yasichukue sura ya kijeshi
Walivyofanya
CUF
10.
Wameyapuuza
kabisa masharti niliyowapa ya kutoa taarifa za mafunzo
11.
Mbaya zaidi ni
kwamba walimofumwa wamekutikana wakifanya mafunzo ya karate na judo yenye
mwelekeo wa kijeshi na hayahusiani kabisa na siasa au itikadi isipokuwa labda
Kufutwa
kwa Ruhusa
12.
Kutokana na hali
hiyo iliyojitokeza ambapo CUF imevunja muamana, tarehe
13.
Jambo la
kufurahisha ni kwamba katika kauli zao za kubeza tangazo la Mheshimiwa
Chiligati, CUF wamekiri hadharani kwamba wanaendesha mafunzo ya karate na judo. Hii ni tofauti na huko
nyuma ambapo walikuwa wakijaribu kuvungavunga na kubabaisha. Kukiri kwao huko sasa kumetuongezea uhalali
wa kuvisaka vikundi vyao vinavyofanya mafunzo hayo kwani sasa tuna uhakika wa
kuwa tunasaka kitu ambacho kipo kweli.
Ukweli tuliokuwa tunautafuta CUF sasa tumeupata na hapawezi tena kuwa na
madai ya kusingiziwa.
14.
Hata hivyo,
inasikitisha kwamba viongozi wa CUF inaelekea wanawaficha wafuasi wao kwamba
hiyo ruhusa ya mafunzo nimekwishaifuta.
Badala yake wanawaambia wapuuze tangazo la Mheshimiwa Naibu Waziri. Sielewi nia
15.
Nasisitiza tena
kwamba mafunzo ya judo na karate yamepigwa marufuku; na marufuku
haya ni kwa vyama vyote ikiwemo na CCM.
Jambo la faraja ni kwamba amri hii haitokuwa na taathira yoyote kwa
vyama vingine ukiondoa CUF, kwani katika programu zao za mafunzo vyama hivyo
havina kipengele cha mafunzo ya judo
na karate.
Wito
16.
Napenda kutoa
wito kwa wafuasi wa CUF wanaohimizwa kujiunga na mafunzo ya karate na judo wasikubali kuuzwa na kuingizwa matatani.
17.
Aidha, napenda
kutoa wito kwa raia wote wema kutoa taarifa Polisi kila watapoona dalili za
mafunzo ya karate na judo ili hatua za kisheria
zichukuliwe. Mafunzo hayo hayana nia
njema kwa jamii na yana lengo la kuvuruga amani na utulivu wa nchi yetu.
Indhari
18.
Kwa nia njema
kabisa, napenda kuwaasa CUF wajihadhari