Mambo ya Nje:

 

.

Mahusiano ya Kimataifa

.

Uanachama katika jumuiya za uchumi za mikoa na kimataifa.

 

§                     SADC

§                     EAC

§                     UNDP

 

MIKATABA YA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA NCHI NYINGINE.

 

 

USHIRIKIANO NA WABIA WAKUBWA KATIKA MAENDELEO  

Ubelijiji, Canada, China, Denmark, Finland, Ujerumani, Ireland, Japani, Uholanzi, Norway, Sweden, Uingereza, Umoja wa Nchi za Ulaya. 

Balozi za Tanzania Nje 

Balozi Ndogo za Tanzania Nje 

Balozi zilizopo Tanzania 

Mashirika ya Kimataifa 

Tanzania ni mwanchama wa jumuiya za kimataifa na kimaeneo, ndiyo kusema Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi Kusini mwa Afrika(SADC).  Jumuiya ya Afrika Mashariki ina nchi wabia tatu:  Uganda, Kenya, na Tanzania. 

Jumuiya ya Afrika Mashariki ilianzishwa chini ya mkataba uliotiwa saini na nchi wabia Novemba 30, 1999.  kwa kuanzia, Jumuiya itaunda umoja wa forodha na soko la pamoja ambazo mikataba yake inatarajiwa kukamilishwa kutiwa saini katika kipindi cha miaka minne kuanzia Novemba 1999.  Hatua nyingine za ufungamanisho ni kuundwa kwa umoja wa mambo ya fedha na hatimaye uundaji wa shirikisho.  Jumuiya ya Afrika Mashariki inanuia kuimarisha utengamano wa uchumi wa nchi hizi kwa kutoa vipaumbele, na kwa misingi ya vitendo, ikiwemo kufanikisha biashara kwa kulinganisha ushuru, malipo, usafiri, matembezi ya watu mipakani, na kusawazisha nyanja nyingtine zenye maslahi ya pamoja, kama vile siasa, jamii na utamaduni. Uanachama wa Tanzania SADC ulianzia pale ilipoanzishwa jumuiya hiyo mapema miaka ya 80.  Jumuiya ya SADC ni ya nchi 13 ambazo ni Angola, Botswana, Lesotho, Malawi, Muaritius, Msumbiji, Namibia, Afrikaya Kusini, Swaziland, Tanzania, Zambia, Zimbabwe na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.

Wanachama wa SADC walitia saini hati za awali za mkataba wa biashara Januari 25, 2000,  wenye lengo la kuanzisha eneo huru kwa  kuondoa vikwazo vya biashara na huduma, kuweka sheria  zifaazo za biashara (kukataza kuuza kwa bei nafuu katika nchi nyingine bidhaa zisizotakiwa soko la nyumbani, ruzuku, kufidia ushuru na ulindaji wa biashara).  Eneo huru la biashara la SADC linatarajiwa kuwa litaanzishwa katika kipindi cha miaka nane kuanzia Septemba, 2000. 

Tanzania pia imejifunga katika mipango mingine ya kimataifa, kama ile ya Shirika la Biashara Duniani(WTO), Afrika, Caribean-Pasifiki (ACP) na Umoja wa Ulaya (EU)

UANACHAMA NA NCHI JIRANI NA ZA KIMATAIFA KATIKA MAKUNDI YA KIUCHUMI

 

JUMUIYA YA MAENDELEO YA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA (SADC)

 

Madhumuni:

 

Kukuza maendeleo ya uchumi unaojitegemea na muungano katika nchi za SADC pamoja na kuendeleza amani na usalama katika nchi hizo.

Mipango mikuu inayoendelea

 

Utekelezaji wa SADC programme of Action unajumuisha yafuatayo:-

 

¨      Mpango wa SADC wa Takwimu.

 

¨      Mpango wa SADC wa kudhibiti madawa.

 

¨      Mpango wa SADC wa jinsia

 

¨      Mpango wa SADC wa kufikia kilele cha uchumi (SADC Economic Summit Programme).

 

¨      Itifaki kuhusu Ruksa na Upendeleo (Immunities and privileges).

 

¨      Itifaki kuhusu mifumo ya mgao wa mwenendo wa maji (shared water course systems).

 

¨      Itifaki kuhusu Nishati

 

¨      Itifaki kuhusu usafirishaji mawasiliano na  Hali ya Hewa.

 

¨      Itifaki kuhusu Biashara

 

¨      Itifaki kuhusu kupambana na Biashara ya Madawa ya kulevya (Combating Illicit and Drug Trafficking).

 

¨      Itifaki kuhusu madini.

 

¨      Itifaki kuhusu Elimu na Mafunzo.

 

¨      Itifaki kuhusu utalii.

 

 

 

 

 

 

Anwani:

Katibu wa SADC

Private Bag 0095

Government Enclave

Gabarone

BOTWASANA

Website:  www.sadc.com

 

JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI (EAC)

 

Madhumuni:

 

Kuimarisha ushirikiano wa uchumi, jamii, utamaduni, siasa, teknolojia na ushirikiano mwingine kwa kuleta maendeleo sawa na ya kudumu ya nchi husika (Tanzania, Kenya, Uganda).

 

Mipango mikuu inayoendelea:

 

Kutathimini Mpango wa Maendeleo ya EAC kwa kipindi cha 1999-2000 na kuridhia mpango wa maendeleo wa EAC kwa 2001-2005.  Mipango inayoanzishwa na iliyopo inahusu yafuatayo:

 

¨      Kuanzisha pasi/pasipoti za kusafiria zilizo sawa kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na utoaji wa vitambulisho vya kitaifa.

 

¨      Kuanzisha nyumba ya biashara (Stock Exchange) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na soko la fedha (Capital Market).

 

¨      Kupunguza urasimu katika kutayarisha hati za wateja (simplification of customers documentation).

 

¨      Kupunguza viwango vya kodi kufuatana na mapendekezo ya “Cross Border Initiative - CBI)”.

 

¨      Itifaki juu ya kupambana na Biashara ya Madawa ya kulevya katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 

¨      Itifaki juu ya kuwa na viwango vilivyosawa, bidhaa zilizo mathubuti, Hali ya Hewa na Uchunguzi (Standardisation, Quality Assurance Meteorology and Testing).

 

¨      Uchunguzi wa Sheria za taratibu kwa ajili ya mikutano ya Wakuu wa nchi (Observance of the rules of procidure for the summit of heads of state).

¨      Uchunguzi wa sheria za taratibu kuruhusu nchi za nje katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 

¨      Uchunguzi wa sheria za taratibu za kuruhusu

 

¨      waangalizi/wachunguzi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

 

¨      Itifaki juu ya kuanzisha muungano wa ushuru wa forodha kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki iko katika hatua za mwisho.

 

Anuani:

Katibu wa Tume ya EAC

S.L.P. 1096

Arusha

TANZANIA

Website: http/hometwiga@.com/eac

 

 

SHIRIKA LA MAENDELEO LA UMOJA WA MATAIFA (UNDP)

 

Madhumuni:

 

Kuimarisha na kuendeleza maendeleo ya uchumi na ukuaji.

 

Mipango mikuu inayoendelea:

 

Utekelezaji wa mpango wa 6 wa UNDP wa Nchi (6th UNDP Country Programme) kwa ajili ya Tanzania ambao unajumuisha yafuatayo: -

 

¨      Mpango wa kupunguza umaskini.

¨      Mpango wa kurekebisha utumishi serikalini.

¨      Kujenga uwezo kwa ajili ya kusaidia maendeleo katika ngazi za Serikali Kuu na serikali za mitaa.

¨      Mpango wa kurekebisha sheria.

¨      Mpango wa Utawala bora.

¨      Mpango wa UKIMWI.

¨      Mpango wa kurekebisha Serikali za Mitaa.

¨      Mpango wa TCDC.

 

 

 

 

MAKUBALIANO YA NCHI MBILI YA UWEKEZAJI KATI YA TANZANIA NA NCHI NYINGINE:

 

Tanzania imeshaweka saini mkataba wa uwekezaji na Uingereza na kuweka saini mikataba inayofanana na huo ambayo iko katika hatua ya kuthibitishwa na Serikali za nchi ya Sweden, Denmark, Uholanzi na Jamhuri ya Korea.

 

Hatua za mwisho zimefikiwa za Uwekezaji kati ya Serikali za Finland na Italy.

 

Maeneo yanayohusika na mikataba hiyo ni pamoja na: -

 

¨      Kukuza na kulinda uwekezaji

¨      Transfer of Principal, returns, proceeds, payments, compensation and earnings.

¨      Expropriation and Compensation

¨      Kusuluhisha mogogoro.

 

USHIRIKIANO WA WASHIRIKI WAKUU KATIKA MAENDELEO:

 

Tanzania kama nchi nyingine zinazoendelea inamakubaliano ya ushirikiano na washiriki kadhaa, kwa madhumuni ya kusaidia maendeleo ya Tanzania  ya kijamii na kiuchumi. Mpango huu unafanikishwa kwa msaada wa fedha, ufundi na misaada ya vifaa (ruzuku na mikopo kwa Tanzania). Washiriki wakuu wa kusaidia kuleta maendeleo ni wafuatao: -

 

BELGIUM:

 

Ushirikiano wa Maendeleo ya Belgium Tanzania unaendeshwa kupitia serikali na kupitia mfumo usiokuwa wa serikali. Makubaliano rasmi wa ushirikiano wa Maendeleo baina ya nchi hizo mbili uliwekwa saini mwaka 1984. Maeneo yanayoshughulikiwa sasa ni yafuatayo: -

 

i.                     Usafirishaji na Mawasiliano.

 

¨      Contral Railways Corridor Programme involving weigh bridges, mobile container crane and 12 petrol tanks.

¨      Mafunzo kwa  ajili madereva wa magari moshi.

¨      Karakana ya matengenezo.

¨      Provision turnout’s/switches and truck fittings.

¨      Kutoa vifaa na mafunzo kwa ajili ya matengenezo na vyombo vya kuzolea uchafu chini ya maji bandarini (provision of equipment and training for maintenance and dredging in the harbour).

 

¨      Kuazimisha wataalam wa Kibelgji wa kompyuta.

¨      To assist in the computerisation of the principal and voyage account.

 

ii.                   Maendeleo ya Sekta ya Vijijini.

-         Kuendeleza Mkoa wa Kagera

-         Kuendeleza zao la ndizi na uzalishaji wa mazao ya biashara.

-         Uchimbaji wa malambo.

-         Afya.

-         Vituo vya upimaji.

 

iii.                  Kupunguza  umaskini

Mpango huu unatekelezwa na UNDP kupitia juhudi za “National Income Generation Programme”.

 

iv.                 Kuendeleza Sekta Binafsi.

 

-         Uchunguzi wa kutambua maeneo ya kuendeleza sekta binafsi umekamilika na inaelekea kwamba shirika la “Tanzania Venture Capital Funds’ huenda likapendekezwa kushughulikia.

 

v.                   Mfuko wa kuishi – Ngara (survival fund)

 

-         Kusaidia upatikanaji wa kuni na ustawishaji wa misitu chini cha usimamizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia wakimbizi na kutekelezwa na CARE.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

CANADA:

 

Utangulizi:

 

Ushirikiano wa Tanzania Canada Maendeleo ulianza 1965.  Msaada wa Canada kwa Tanzania unatolewa kupitia wakala ya Msaada wa Maendeleo (Development Aid Agency) inayojulikana kama Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Canada (Canadian International Development Agency – CIDA).  Msaada unalenga katika mahitaji ya binadamu maendeleo ya wanawake, sekta binafsi, utawala na haki za binadamu.

 

Miradi inayoendelea

 

Sekta                                                               Mradi

 

Miundo mbinu na usafirishaji            -            Vifaa vya kutengenezea magari

                                                                        Moshi ya  Shirika la Reli la Tanzania                                                                         (TRC)

                                                                        Msaada na mafunzo kwa ajili ya                                                                               TRC

                                                                        Kituo cha mawasiliano cha Kagera

                                                                        Kupiga picha za anga Hanang

 

Elimu                                                    -            Mfuko wa mafunzo kwa ajili ya                                                                               wanawake.

                                                                        Community based for girls?

                                                                        Basic Education Specialist/

 

Maendeleo vijijini                            -            Mfuko wa Hanang wa maendeleo ya                                                                           ushirikishwaji

 

                                                                        Mradi wa vifaa na Afya ya mtoto

 

                                                                        Mfuko kwa ajili ya maendeleo ya                                                                           viwanda vya mazingira.

 

Utawala                                                -            Mradi wa Maendeleo ya Demokrasia                                                                                     Tanzania.

 

Maendeleo ya biashara

ndogondogo                             -            Mennonite Economic Development                                                                            Associates (MEDIA).

 

                                                                        Mfuko wa Canada kwa ajili ya                                                                               kusaidia juhudi za binafsi kwenye                                                                         makazi.

 

                                                                        Mfuko wa Tanzania wa kurekebisha                                                                                     majengo.

 

Miradi mingineyo                                 -            Kamusi za kiingereza – Kiswahili

 

Mifuko ya Ushirikiano wa Tanzania Canada.

 

                                                                        Tanzania program support unit

 

                                                                        Uchunguzi wa gesi ya songosongo.

 

                                                                        Food monitization

 

Kuendeleza mipango na usimamizi wa sekta ya afya

 

Miradi ya Mikoa                          -            Decentralized Democratic                                                                                           Development

 

                                                                        Mpango wa mafunzo ya UKIMWI                                                                            kusini mwa Afrika (Southern African                                                                         AIDS Training program (SALTZ).

 

CHINA

 

Utangulizi:

 

Ushirikiano baina ya Tanzania na China ulianza tangu 1964 kwa mapatano ya kutoa mikopo yenye masharti laini ya biashara.  Ushirikiano uliopo sasa unalenga kwenye kilimo, viwanda, usafirishaji na mawasiliano, ujenzi, madini, biashara, afya na elimu.

 

Miradi inayoendelea

 

  • Mradi wa makaa ya mawe wa Kiwira: 

Mradi unaendeshwa kwa pamoja ambapo China inamiliki hisa asilimia 62 na Tanzania asilimia 38.

 

  • Urafiki

Mradi wa nguo unaoendeshwa kwa pamoja

 

 

Miradi inayobuniwa

 

  • Shamba la mpunga la Mbarali:  Kampuni ya Kichina ya Jiangsu Agricultural and Forest Department imeonyesha nia ya kuingia ubia na serikali ya Tanzania.

 

  • Shamba la mpunga la Ruvu:  Jitihada zinafanyika kuipata kampuni ya kuingia naye ubia

 

  • Kiwanda cha zana za kilimo cha Ubungo (UFI):  Kampuni ya Kichina iitwayo Tianjin Machinery Import Export Cooperation imeonyesha nia ya kuingia ubia.

 

  • Kiwanda cha kutengeneza mashine cha Mang’ula: Mipango inafanywa ya kumpata mmbia wa kuwekeza.

 

DENMARK

 

Ushirikiano wa maendeleo wa Tanzania – Denmark ulianza katika miaka ya mwanzo ya 1960 kupitia shirika la Nordic Aid Project. Kuanzia wakati huo Tanzania imekuwa moja wa washiriki wakuu wa ushirikiano wa maendeleo na  Denmark.  Kutokana na mkataba wa makubaliano uliowekwa saini tarehe 7 Agosti, 1995 mpango wa baadaye wa ushirikiano utaelekezwa katika kusaidia mipango ya sekta na “sector concentration”.  Licha ya “sector concentration” Denmark inaendelea kujihusisha na masuala ya kuendeleza haki za binadamu – zikiwemo haki za wanawake,.  Utawala bora na maendeleo ya demokrasia.

 

Mpango wa kusaidia sekta ya afya – awamu ya kwanza

 

  • Mipango ya afya ya kushughulikia masuala ya UKIMWI na magonjwa ya zinaa kwa gharama nafuu kwenye hospitali za Wilaya, vituo vya afya, dispensari na katika jumuiya.

 

  • Mfumo wa afya wa usafirishaji wa kitaifa/kiwilaya.

 

  • Kuimarisha sehemu muhimu katika  Wizara ya Afya.

 

  • Kuendeleza watumishi,mipango na uwezo wa usimamizi katika Wizara ya Afya.

 

 

 

 

 

 

Mpango wa kusaidia sekta ya kilimo

 

  • Mpango huu unalenga katika kuimarisha uwezo wa kuanzisha uzalishaji wa mbegu shambani, miradi ya wakulima wadogo wadogo ya  umwagiliaji maji, utafiti wa mawe ya phosphate na hifadhi ya mazingira.

 

Mpango wa kusaidia Sekta ya Barabara

 

  • Sehemu ya Barabara Kuu

 

(i)                 Matengenezo ya barabara ya Dar es Salaam –Mlandizi, Daraja la Mto Wami na Barabara ya Chalinze – Segera.

(ii)                Usimamizi wa matengenezo ya barabara kuu awamu ya pili.

 

  • Sehemu ya Barabara za Mikoani

Ukarabati wa kilomita 150-200 wa barabara za mkoa wa Pwani.

 

  • Sehemu ya Barabara za Wilaya

Ukarabati wa barabara za Wilaya ya Rufiji katika Mkoa wa Pwani.

 

  • Kusaidia Asasi/Taasisi (institutional support)

-         Elimu ya ufundi na mafunzo

-         Kuimarisha Benki ya ushirika na Maendeleo ya Vijini (CRDB).

-         Kuendeleza hazina Ndogo

-         FEDHA Funds (risk capital for long term investment).

-         Msaada kwa vyama vya wafanyakazi na vyama vya biashara.

 

Mpango wa kusaidia sekta ya Maliasili na Utalii, misitu na Nyuki.

 

  • Mradi wa kusaidia uongozi wa msitu wa Udzungwa katika Mkoa wa Iringa.
  • Msaada kwa jumuiya ya Natural woodland Management Project (Iringa).
  • Msaada kwa eneo la Hifadhi la Ngorongoro.

 

Mpango wa kusaidia mazingira

 

(i)                  Kuendeleza Arusha

 

(ii)                Kusaidia vijiji kusimamia misitu na nyika katika Mkoa wa Lindi.

 

(iii)               Kuendeleza Mwanza.

 

 

FINLAND

 

Utangulizi

 

Ushirikiano wa Maendeleo wa Tanzania – Finland ulianza katika miaka ya mwanzo ya 1960 wakati shirika la Nordic Aid Project lilipoanzishwa.  Aina ya msaada mkuu ulikuwa kusaidia miradi kwa njia ya fedha  mikopo au ufundi.

 

Miradi inayoendelea

 

Mazingira na misitu ambayo inajumuisha yafuatayo:-

 

-         The Tanzania Forest Action Plan (TFAP)

 

-         The East Usambara Catchment Forest Programme

 

-         Establishment of Amani Nature Reserve, Catchment Forest, Farm Forest,kuimarisha na kutafiti pamoja na kusimamia utekelezaji.

 

-         Utafiti wa Misitu nchini Tanzania Awamu ya Kwanza: madhumuni ya keni kuimarisha utafiti na kuendeleza uwezo katika Taasisi ya utafiti wa Misitu Tanzania (Tanzania Forestry Research Institute – TAFORI).

 

-         Mradi wa kuendeleza misitu Zanzibar: madhumuni ni kushughulikia masuala ya umaskini vijijini na upungufu katika kusimamia maliasili.

 

-         Mradi wa Zanzibar Intergrated Lands and Environmental management (ZILEM).  Mradi  unalenga kuendeleza  uwezo katika maeneo yanayoshughulika na mpango wa matumizi ya ardhi, usimamizi wa ardhi na usimamizi wa mazingira.

 

  • Mradi wa Maji na Maji Taka

 

-         Mpango wa maendeleo ya maji katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

-         Mradi wa maji mjini Zanzibar.

 

  • Mradi wa Maendeleo Vijijini

 

-         Rural Integrated Programmes Support (RIPS)katika mikoa ya Mtwara na Lindi awamu ya III.

 

 

 

  • Elimu na Utamaduni

 

-         Mfuko wa Elimu.

-         Mfuko wa kusaidia Elimu ya ufundi.

-         Elimu ya shule ya msingi Wilayani.

-         Mfuko wa shughuli za utamaduni.

 

  • Msaada kwa Wakimbizi

 

  • Msamaha wa madeni

 

  • Utawala Bora

 

-         Urekebishwaji wa Serikali za Mitaa na “redeployment”

-         Msaada kwa kuendeleza demokrasia.

-         Mfuko wa Demokrasia.

-         Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) – Integrated Tax Administration Programme.

-         Msaada kwa kutayarisha mchanganuo wa Sera ya Hazina.

-         Demokrasia, haki za binadamu na usawa.

 

UJERUMANI

 

Utangulizi

 

Mkataba wa kwanza wa ushirikiano wa maendeleo baina ya Tanzania na Ujerumani ulitiwa saini 1962, ambao uliisaidia Tanzania kupata msaada wa kusaidia maendeleo ya uchumi kwa njia ya mikopo na ruzuku.

 

Licha ya ushirikiano wa kiserikali ushirikiano mwingine wa Tanzania na Ujerumani unajumuisha yafuatayo:

 

  • Huduma za kujitolea kupitia German Development Services (DED).

 

  • DEG Investment activities (German Private Investment cooperation).

 

  • Shughuli za Biashara na Viwanda

 

  • Non project tied scholarships.

 

  • Integrated experts through center of international migration (CIM).

 

Miradi inayoendelea

 

(i)                  Ushirikiano na makanisa katika kuhudumia miradi ya jamii.

 

(ii)                Miradi ya ushirikiano na shirika la Reli la Tanzania

 

 

(iii)               Mradi wa umeme wa Kihansi chini wa kusambaza umeme unaotokana na maji.

 

(iv)              Kukarabati transfoma na mitambo ya kuwashia na kuzimia umeme wenye nguvu kubwa.

 

(v)                Mpango wa kuongeza uwezo wa nishati

 

(vi)              Marekebisho katika kugharamia barabara.

 

(vii)             Marekebisho katika kusimamia  mtandao wa barabara.

 

(viii)           Mradi wa maji  vijijini.

 

(ix)              Mradi wa maji Hai vijijini awamu I na II.

 

(x)                Mradi wa maji Ngara – Karagwe.

 

(xi)              Usimamizi wa maliasili.

 

IRELAND

 

Utangulizi:

 

Ushirikiano wa kwanza wa Tanzania – Ireland ulianza miaka ya 1970 kati ya Irish Ropes na kiwanda cha Kilosa cha Mazulia (Kilosa Sisal Carpet Factory). Kuanzia 1981, ushirikiano wa Ireland ulilenga Wilaya ya Kilosa na Kuanzia 1980 Wilaya ya Ulanga na Kanda ya Pwani ya Tanga ziliongezwa.  Ushirikiano unaelekezwa kwenye kupunguza umaskini, upatikanaji wa huduma za msingi, usawa wa jinsia, maliasili na utawala bora.

 

Miradi inayoendelea

 

  • Kuendeleza mipango ya maendeleo katika wilaya za Kilosa, Ulanga,Kilombero na Muheza.

 

  • Kuimarisha mpango wa sekta ya elimu wa maendeleo.

 

  • Kuendeleza Idara ya Elimu ya ramani ya bahari na mito (hydrology) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam .

 

  • Ukarabati wa shule za msingi katika mkoa wa Kigoma (Katika maeneo yaliyoathiriwa na wakimbizi).

 

 

  • Mpango wa kurekebisha sekta ya afya (kuimarisha rasilimali ya watumishi).

 

  • Mfuko wa sekta ya afya wa “Basket”
  • Kuimarisha usalama wa chakula.
  • Mradi wa kupanua Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Morogoro.
  • Mpango wa mafunzo ya utalii.
  • Hifadhi ya asilia (Tanga Coastal Zone Conservation program).
  • Mradi wa utafiti na upanuzi wa kanda ya mashariki.
  • Msaada kwa mpango wa urekebishaji wa serikali za mitaa.
  • Mchango wa kusaidia bajeti ya kupunguza umaskini.

 

JAPAN

 

Utangulizi

 

Ushirikiano  na Japan umeanzia miaka ya 1970.  ushirikiano wa sasa unaendeshwa chini ya utaratibu wa JICA katika maeneo muhimu yafuatayo:-

 

§         Miundombinu

 

-         Mitambo kwa ajili ya matengenezo ya barabara kuu

-         Usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Kilimanjaro

-         Usambazji wa mtandao wa simu

-         Ujenzi wa barabara za jiji la Dar es Salaam

-         Kuimarisha madaraja katika Mikoa ya Lindi na Mtwara.

 

§         Afya

 

-         Kuangamiza ugonjwa wa kupooza (poliomyetis) kwa watoto walio chini ya miaka mitano.

 

§         Elimu

 

-         Msaada kwa elimu ya msingi pamoja na elimu ya sekondari.

 

§         Maji

 

-         Kuimarisha huduma za maji na afya katika maeneo yaliyoathiriwa na wakimbizi.

 

§         Mahitaji ya msingi

 

-         Miradi ya kupunguza umaskini katika Wizara zinazohusika na Kilimo, Maji na Afya.

 

§         Msaada wa ruzuku kupunguza madeni

 

-         ulipaji wa madeni ya Tanzania unagharamiwa na Serikali ya Japan kwa utaratibu wa Tanzania Debt Relief Cover kwa ajili ya kuingiza bidhaa kupitia njia za kawaida za biashara.

 

Mpango wa msaada wa chakula (KR I and KR II)

 

Kuhamisha mali ili kuweka sawa hali ya ulaji kwa misingi ya upatikanaji wa chakula  katika soko (KR I) na kutoa pembejeo na zana za kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula (KR II).  Msaada wa chakula kama vile mchele, unauzwa ili kupata fedha ambazo zinatumika kusaidia nguvu za serikali katika kugharamia maendeleo ya miradi katika sekta zinazohudumia kilimo na jamii.

 

UHOLANZI

 

Utangulizi

 

Ushirikiano baina ya Tanzania na Uholanzi ulianza miaka ya 1970

Miradi inayoendela

Elimu

 

Mradi unajumuisha mfuko wa elimu kusaidia utayarishaji wa mpango wa kuendeleza Sekta ya Elimu, msaada kwa mradi wa vitabu vya watoto,mpango wa muda wa vitabu vya kufundishia, kusaidia elimu ya juu,kitengo cha utafiti wa kiuchumi cha chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Uhandisi, Idara ya Utafiti kuhusu kupunguza umaskini (REPOA), msaada kwa elimu ya msingi kupitia wilayani, msaada kwa  elimu kupitia mpango wa wilaya wa kuendeleza vijiji hasa kwa kupitia SNV, na mpango wa masomo (wanafunzi wapatao 80 – 100 huenda kusomea kozi nchini Uholanzi kila mwaka

 

 

 

Afya

 

Shughuli zinazoendelea chini ya mpango wa afya ni pamoja na mpango wa Taifa wa kifua kikuu na ukoma, mpango wa afya ya uzazi kwa nia ya kuzuia UKIMWI na utafiti juu ya UKIMWI na mahusiano ya jamii na uuzaji wa kondomu.

 

Maji

 

Miradi ya maji katika mikoa miwili ya Singida na Morogoro ya uchimbaji wa visima vifupi, jinsi ya kuvitumia na kuvihudumia.

 

Serikali za Mitaa

 

Kurekebisha, kuendesha, kushauri na kuanzisha mfumo wa usimamizi wa fedha (platinum) katika mikoa kumi na moja

 

Maendeleo vijijini

 

Mikoa kumi na moja inashiriki katika mpango huu, nayo ni Biharamulo, Bukoba, Kahama, Karagwe, Kondoa, Maswa,Mbulu, Meatu, Monduli, Songea na Ngara.  Mpango huu uko katika awamu ya tatu na una nia ya kuongeza umilikaji katika mahali na uwajibikaji katika kutumia mifuko ya maendeleo ya Wilaya na kuongezeka kwa jukumu la kuisaidia serikali kuu kutoa msaada kwa wilaya.  Mipango mingine inahusu Multilateral Debt Fund, mazingira, miundombinu na wanawake katika maendeleo.

 

Miradi/mipango inayogharamiwa na Uholanzi chini ya ORET

 

(i)                  Barabara ya Kongowe – Mjimwema Kivukoni.

 

(ii)                Kuimarisha hudumna za viwanja vya ndege (zima moto na dharura).

 

(iii)             Kukarabati huduma za uchunguzi na yakini ya mgonjwa – Wizara ya Afya.

 

NORWAY

 

Utangulizi

 

Ushirikiano wa maendeleo kati ya Norway na Tanzania ulianza miaka ya mapema ya 1960 katika nyanja ya ushirikiano  wa kiufundi yanayohusu maeneo ya utawala, afya na elimu. Kutoka 1995, ushirikiano umekuwa unaongozwa na mkataba wa makubaliano wa maendeleo wenye madhumuni ya kuendeleza uchumi imara wenye kulenga katika  sekta zifuatazo:

 

§         Kuimarisha uchumi.

§         Miundombinu.

§         Utafiti na elimu.

§         Marekebisho ya siasa.

§         Mazingira na usimamizi wa rasilimali

§         Uhusiano wa biashara na utamaduni.

§         Mipango ya ushirikiano na nchi za jirani kwa mfano Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)

§         Co-financing with multilateral organizations.

§         Msaada kwa vyama visivyo vya kiserikali (NGO’s) na huduma za kujitolea.

 

Miradi inayoendelea

 

  • Kukuza jitihada za vijiji na maendeleo ya biashara (promotion of Rural Initiatives and Development Enterprises (PRIDE) katika mikoa ya Arusha, Tanga na Dar es Salaam.

 

  • Ujenzi wa kituo cha umeme chini ya ardhi na bwawa la kuzalisha umeme katika kituo cha Kihansi.

 

  • Ujenzi wa kituo kidogo cha umeme katika maeneo ya Kunduchi na Magomeni jijini Dar es Salaam.

 

  • Kuvuta nyaya za kusambaza umeme kutoka Mbala (nchini Zambia) hadi Sumbawanga (Mkoani Rukwa).

 

  • Kusaidia Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo cha Maendeleo ya Uongozi (Mzumbe) na Taasisi ya Dar es Salam ya mafunzo ya Bahari.

 

  • Mradi wa mbao wa Sao Hill.

 

  • Mradi wa kuhifadhi ardhi na misitu katika mkoa wa Shinyanga.

 

  • Msaada  kwa sekta ya Maliasili.

 

  • Mpango wa UKIMWI Mkoani Arusha na Kilimanjaro.

 

  • Ukarabati wa barabara kuu (barabara ya Himo – Holili).

 

  • Matengenezo ya barabara za vijiji katika mikoa ya Mbeya na Tanga.

 

  • Ujenzi wa daraja la Mgoda (mradi wa ubia)

 

  • Upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam (Kurasini Oil Jetty).

 

  • Msaada kwa bajeti ya kusaidia kupunguza umaskini.

 

  • Mipango ya maendeleo ya vijiji.

 

SWEDEN

 

Utangulizi

 

Ushirikiano wa Tanzania Sweden ulianza 1963, ukilenga kwenye miradi maalum iliyopo Mikoani, kusaidia ulipaji wa mikopo, misaada ya dharura, miradi ya mazingira, vyama visivyokuwa vya kiserikali pamoja na shughuli za demokrasia na haki za binadamu.

 

Miradi inayoendelea

Elimu

 

¨      Kusaidia vifaa vya shule, mafunzo ya walimu, mradi wa mpango wa vitabu vya shule na mfuko wa utamaduni wa Tanzania.

 

Fedha na Utawala

 

¨      Mpango wa Serikali wa Maendeleo ya Taarifa za Hesabu (Government Accounting Development Programme – GADP), mpango wa Idara ya Utumishi wa Jinsia, Mamlaka ya Kodi Tanzania na Capital Markets Development.

 

Usafirishaji na Mawasiliano

 

Kuimarisha na kuendeleza kampuni ya simu Tanzania (TTCL)

 

Nishati

 

Kusaidia mradi wa kuzalisha umeme wa Kihansi na Kampuni ya Umeme Tanzania (kuweka magurudumu ya kuzalisha umeme wakati wa dharura yanayoendeshwa kwa njia ya gesi).

 

¨      Mazingira

 

Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

 

 

¨      Maliasili

 

EBD – SAPU

 

¨      Serikali za Mitaa

 

Mpango wa kusaidia Wilaya, mpango wa kusimamia ardhi – Babati, Kiteto na Simanjiro, kusaidia mipango ya Wilaya ya Singida na utawanyaji wa vifaa vya elimu.

 

¨      Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto

 

Mradi wa afya na maji (HESAWA)

 

Mipango mingine

 

Inajumuisha kushirikiana katika utafiti, masuala ya urari wa malipo, na kusaidia mipango inayoendeshwa kwa kushirikiana na FAO, WFP, UNICEF, NGOs za Sweden na SCAPA.

 

UINGEREZA

 

Utangulizi

 

Ushirikiano wa maendeleo wa Tanzania – Uingereza ulioanza mwaka 1961, unahusu msaada ya fedha na ushirikiano wa kiufundi.  Ushirikiano wa Uingereza pia unatolewa kupitia Umoja wa Ulaya (EU), mfuko wa Maendeleo wa Ulaya, msaada wa Dharura, NGOs na msaada wa chakula.

 

Miradi inayoendelea

 

¨      Maliasili

 

Kusimamia mradi wa wanyamapori wa Ruaha kwa madhumuni ya kuendeleza utalii nchini, kuhifadhi, kuhudumia wanyama pori na kulinda wanyama ambao idadi yao inapungua (tembo).

 

¨      Kilimo

 

Mpango wa  utafiti wa korosho unaolenga katika utafiti wa kilimo juu ya uzalishaji wa zao la korosho mkoani Mtwara kwa nia ya kufufua viwanda vya kahawa.

 

Mradi wa kilimo cha mazao ya kibiashara, Zanzibar, wenye madhumuni ya kuongeza pato la fedha za kigeni na kuongeza kipato cha jumuiya ya wakulima kwa kuendeleza sekta ya mazao ya biashara.

 

¨      Afya

 

Mradi wa Afya ya familia wenye lengo la kuimarisha afya ya uzazi na kuzua kuenezwa kwa magonjwa ya zinaa.  Mradi huu uko katika wilaya nne za Mkoa wa Mbeya.

 

Mradi wa kusaidia Afya na Lishe (Mbeya na Tukuyu).  Madhumuni ya mradi ni kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya, kuimarisha mfumo wa maji na maji taka, huduma za uzazi wa mpango wa majira, kuongeza uwezo wa kliniki na vituo vya afya pamoja na kutoa huduma muhimu za afya na huduma za jamii.

 

Kuchangia huduma za afya.  Nia ya mradi ni kuelezea na kuanzisha utaratibu wa kuchangia huduma za afya kwa kuchunguza masharti yaliyopo kwa watumishi wa Serikali kuingia mkataba wa lazima wa bima ya afya na kuanzisha mpango wa kuchangia matibabu katika hospitali zote.

 

¨      Usafirishaji na Miundombinu

 

Kuimarisha mpango wa matengenezo ya barabara katika mikoa ya Iringa na Ruvuma, ukarabati wa mifumo ya kupashana habari ya Shirika la Reli la Tanzania na ukarabati wa magari moshi na mataruma.

 

¨      Mradi wa kukarabati Bandari ya Tanga

 

Kuimarisha shughuli za bandari ya Tanga na kusaidia mradi wa Benki ya Dunia ya kuimarisha bandari ya Dar es Salaam.

 

¨      Urari wa malipo

 

Kusaidia urekebishaji wa uchumi wa nchi

 

¨      The Multilateral Debt Relief Fund (MDF)

 

Mfuko wa MDF ulianzishwa mwezi Julai, 1998 kwa  nia ya kushughulikia malipo ya madeni na kuchangia fedha kusaidia sekta ya jamii yenye kujiwekea akiba.  Nchi  sita zikiwemo Uingereza, Sweden, Ireland, Norway, Finland na Denmark ziliweka saini kuuchangia mfuko huu.

 

 

¨      Kuendeleza Sekta Binafsi

 

Mradi unalenga kuzisaidia biashara ndogondogo za ngazi za kati, pamoja na kuzitafutia masoko ya nje.  Mipango mingine inayobuniwa ni pamoja na kusaidia mpango wa biashara na kuongeza mapato kwa ajili ya wanawake.

 

Maeneo mengine yanahusu kusaidia Venture Capital  Fund na Tanganyika Development Finance Company Ltd (TDFL).

 

¨      Mipango ya kibanadamu

 

Kusaidia shida ya maji katika jiji la Dar es Salaam, wakimbizi wa Rwanda na dharura.

 

¨      Mabadiliko ya Kituo cha Tanzania cha Uwekezaji

 

Kutayarisha marekebisho ya mpango wa biashara wa kituo cha uwekezaji.

 

¨      Idara ya Taifa ya Takwimu

 

Kusaidia matayarisho ya zoezi la kuhesabu watu litakalofanyika mwaka 2002.

 

MAREKANI (USA)

 

Utangulizi

 

Ushirikiano wa maendeleo baina ya Tanzania na Marekani unalenga katika maeneo makuu matano ya afya, mazingira na maliasili, utawala, maendeleo ya sekta binafsi na miundombinu.

 

¨      Miradi inayoendelea

 

Kuongeza juhudi za kutumia mpango wa uzazi wa majira na kuzuia ugonjwa wa ukimwi.

 

Kupanga na kutathmini usimamizi wa wanyama pori.

 

Mradi wa ushirikishwaji wa kusimamia mazingira na rasilimali.

 

Kusaidia juhudi za kujenga demokrasia nchini Tanzania.

 

Kusaidia kuanzisha na kuimarisha kituo cha biashara.

 

Kutayarisha ramani za barabara za kumsaidia mwekezaji.

 

Kuanzisha “Venture Capital Fund” na  Social Action Trust Fund”

 

Kusaidia mabaraza ya biashara

 

Kusaidia mipango ya maendeleo ya mambo ya fedha na biashara.

 

BENKI YA AFRIKA YA MAENDELEO (ADB)

 

Benki ilianza shughuli za kukopesha nchini Tanzania mwaka 1971.  Hadi kufikia tarehe 31/12/2000 Benki iliidhinisha shughuli 69 ikiwemo miradi 33, mikopo 3 yenye mwelekeo wa viwanda, shughuli 20 za utafiti na 4 zinazohusu sera, na kusaidia mikopo 2 inayohusu ushauri wa fedha.

 

¨      Shughuli za Sekta Binafsi.

 

Tangu kuanza kushughulika na sekta binafsi hapo 1991, Benki imeidhinisha mikopo miwili nchini Tanzania, ambayo ni Graphan Limited (kuhusu madini) na Aquva Limited (kuhusu masuala ya kilimo).

 

Katika kipindi cha muda mfupi serikali itaingia mkataba na watoaji huduma watakaotoa mafunzo na kujenga uwezo wa wakulima na wanachama wa vyama vya ushirika (MAMCOS) ili kuwawezesha kupata huduma zinazohitajika kutoka wakala wa Taifa wa Umwagiliaji (National Irrigation Agency – NIA) na mashirika mengineyo.  Watoaji hao wa huduma pia watawasaidia wakulima kupata masoko ya bidhaa zao.

 

¨      Mpango wa Benki wa kukopesha wa muda mfupi na wa kipindi cha 1999 – 2001

 

Msukumo wa kukopesha kwa Tanzania katika kipindi hiki unalenga kusaidia maeneo ya kilimo, huduma ya jamii na huduma zinazotumika na watu wote kama ifuatavyo:-

 

-         Mradi wa kukarabati mfumo wa maji safi na maji taka jijini Dar es Salaam.

 

-         Ukarabati wa barabaa vijijini.

 

-         Structural Adjustment Loan II kwa ajili ya

¨      Utawala

¨      Maendeleo ya binadamu

¨      Maendeleo ya kilimo na ya vijijini

¨      Kusimamia na kutathmini mpango wa umaskini (PRSP).

 

-         Kusaidia uwezo kwa Wizara ya Afya.

-         Kusaidia utafiti wa matengenezo ya barabara ya Dodoma – Singida.

 

-         Mradi wa kusaidia masuala ya  rutuba ya udongo na ukuzaji wa shughuli za kilimo.

 

¨      Miradi inayobuniwa.

 

-         Mradi wa Elimu ya kazi na ufundi II.

-         Mradi wa kukarabati viwanja vya ndege.

-         Mradi wa maendeleo ya uvuvi Zanzibar.

-         Mradi wa utafiti na upanuzi wa kilimo II

 

UMOJA WA ULAYA (EU)

 

Utangulizi:

 

Tanzania ni mwanachama wa mkataba wa LOME I (1975) na kwa sasa ni mwanachama wa ACP kwenye mkataba wa LOME IV (kipindi cha 1991 – 2000 na kusainiwa 1989).

 

¨      Mipango na kazi zinazoendelea

 

¨      Mfuko wa 8 wa Maendeleo ya Ulaya (European Development Fund – EDF)

 

Makubaliano ya ushirikiano kwa ajili ya “National Indicative Programme (NIP) ya 8 ya mfuko huo uliwekwa saini Machi, 1997 na unashughulika na sekta/miradi ifuatayo:

 

¨      Usafiri

 

-         Matengenezo ya barabara za Mwanza.

 

-         Matengenezo ya barabara ya Mwanza – Nzega/Isaka.

 

-         Kuimarisha sekta ya barabara

 

-         Matengenezo ya msimu

 

¨      Upatikanaji wa maji na kushughulikia maji taka

 

-         Utoaji maji mjini Iringa.

-         Kushughulikia mfumo wa maji machafu Mwanza.

-         Utoaji maji mjini Mwanza

 

¨      Elimu

 

-         Mpango wa Maendeleo wa sekta  ya elimu.

 

¨      Kilimo

 

Msaada kwa sekta ya kilimo unatolewa kupitia mpango wa STABEX na bajeti iliyotayarishwa na siyo kupitia miradi ya “National Indicative Progrmme” (NIP).

 

Tanzania chini ya makubaliano ya LOME IV, imefaidika na msaada kwa ajili ya mazao ya kahawa, pamba, chai, katani na karafuu.  Kutokana na umaarufu wa kahawa kuwa moja ya zao kuu linaloiingizia Tanzania fedha za kigeni, mfuko wa 8 wa maendeleo ya Ulaya litasaidia katika kuleta mabadiliko na mipango katika kuiimarisha uzalishaji wa kahawa.

 

¨      Utalii na Maliasili

 

-         Kusaidia mradi wa hifadhai ya Serengeti.

 

-         Kuimarisha sekta ya utalii (TANAPA)

 

¨      Maeneo mengine ya ushirikiano.

 

-         Kupunguza shida inayosababishwa na wakimbizi kwa kuimarisha  miundombinu, huduma mbalimbali na  hifadhi ya mazingira katika eneo la kaskazini-mashariki ya Tanzania.

 

-         Mkopo wa Benki ya uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank – EIB) kwa viwanja vya ndege vya Dar es Salaam na Kilimanjaro kwa ajili ya mitambo ya kuongoza/mawasiliano ya ndege, umeme na vifaa vya taa katika viwanja vya ndege.  Mradi huu unaghramiwa kwa pamoja na Benki Kuu/IDA na ORET.

 

-         Mpango wa kutoa mikopo ya rasilimali kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki, Stanbic Tanzania na CRDB Bank ili kuzikopesha sekta binafsi zikiwemo kilimo, ulimaji wa maua, madini, utalii na kazi zingine zinazofanana.

 

 

 

Title

.

Title

.

Title

.