Mawasiliano ni
sekta iliyo na dhima kubwa katika maendeleo ya jamii na uchumi
Tanzania. Utendaji wa sekta umeendelea kukua kutokana na juhudi za
uwekezaji wa Serikali na sekta binafsi kwenye kukarabati barabara,
kupanua huduma za simu, kuweka vifaa vya kisasa katika viwanja vya
ndege , na kuboresha huduma za usafiri majini, reli na angani.
Huduma za simu
Mawasiliano
ya simu yanapatikana sehemu nyingi nchini na yameuganishwa na nchi
nyingine duniani kupitia Dar es salaam. Huduma za simu zimeendelea
kuboreka kutokana na juhudi za Kampuni ya Simu Tanzania, na
ushiriki wa makampuni binafsi, zikiwemo MOBITEL, TRITEL, ZANTEL na
VODACOM. Namna nyingine za mawasiliano zimewekwa na kuendelezwa,
hasa FAX ambazo zinahitajiwa zaidi kuliko huduma za Telex.
|