WIZARA YA FEDHA

 

 

WARAKA WA HAZINA NA. 14 WA MWAKA 2003 MGAO WA FEDHA ZA MATUMIZI MENGINEYO (O.C) KWA ROBO YA TATU YA MWAKA KWA MWEZI JANUARI, 2002/2003

 

         Kuanzia mwezi wa Desemba, 2000; Serikali ilianza kutangaza kupitia vyombo vya habari fedha zinazotolewa kwa ajili ya matumizi mengineyo (other charges OC) kwenye ngazi ya Taifa, Mkoa na Halmashauri.  Hii ni taarifa ya tatu kwa mwaka wa fedha wa 2002/2003.  Taarifa hii inatakiwa iwekwe kwenye mbao za matangazo ya kila Afisa Mhasibu.  Kwa muhtasari fedha zilizotolewa Januari mwaka 2002/2003 ni kama ifuatavyo:-

 

       (i)     Deni la Taifa               sh 20,440.0mln

       (ii)    Utawala                        26,170.3mln

       (iii)   Ulinzi na Usalama             10,702.2mln

       (iv)   Huduma za Jamii             39,357.2mln

       (v)    Huduma za Uchumi                    9,253.8mln

       (vi)   Uzalishaji                        4,907.7mln   

                             JUMLA       Sh 110,831.2mln

 

       Mchanganuo wa fedha zilizotolewa kwa Wizara, Mikoa na Halmashauri, umeonyeshwa kwenye majedwali 1, 2, 3. Fedha za sekta zinazopewa kipaumbele za elimu, afya, maji, barabara, kilimo, sheria na mahakama zimetolewa kwa  kipindi cha miezi miwili.

 

 

 

KATIBU MKUU

WIZARA YA FEDHA

DAR ES SALAAM

 

 

Makala zilizopita