PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT OF THE
UNITED
The State House,
Tel:
255-22-2116539/2116913
P.O. Box 9120 ,
Fax. No. 255-22 2113425
DAR
ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TANZANIA .
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Kikwete amesema maendeleo ya sayansi na teknolojia
ndiyo mambo yanayozitofautisha
nchi zilizoendelea na zinazoendelea. Na kwa sababu
hiyo amesema anaunga mkono shule
ambazo zinazitilia mkazo
ufundishaji wa masomo ya sayansi.
Ameyasema hayo
leo mara baada ya kufungua shule ya sekondari ya wasichana ya Kandoto inayofundisha masomo ya sayansi na kauli mbiu yake
ni sayansi kwa maendeleo endelevu. Shule hiyo yenye kidato
cha kwanza hadi cha sita inamilikiwa
na Kanisa Katoliki Jimbo la Same.
“ Baba Askofu Koda umenifurahisha
sana, umenifurahisha kwa mambo mawili,
moja ni hili la upendeleo
wa elimu kwa mtoto wa kike,
na pili ni hili la kutilia mkazo masomo ya sayansi, yote haya mawili mimi nayaunga mkono” akasema Kikwete.
Akisisitiza
kuhusu umuhimu ya sayansi na teknolojia
katika maendeleo ya nchi, Rais amewaeleza
wananchi waliohudhuria ufunguzi wa shule
hiyo, kwamba hakuna maendeleo bila sayansi na
teknolojia na kwamba kama Tanzania inataka kuendelea lazima itilie mkazo
eneo hilo .
“Ramli haziwezi
kutuletea maendeleo, sayansi ndiyo itatuletea
maendeleo na tofauti zilizopo kati ya nchi zilizoendelea
na zinazoendelea ni maendeleo ya sayansi. Sayansi ni elimu ya utambuzi wa kanuni zinazotawala maumbile na mazingira
na hivyo kutengeneza zana na vifaa ambazo ndiyo teknolojia ya kuleta maendeleo” akafafanua.
Akizungumza upendeleo wa elimu
kwa mtoto wa kike, Rais amesema
mtoto wa kike lazima apate
fursa ya kupata elimu, kwa kuwa kwa miaka mingi jamii
imekuwa haitoi kipaumbele kwa mtoto wa kike.
Aidha ameainisha kwamba katika utoaji wa
fursa ya elimu kwa mtoto wa kike,
ni vema pia akapata fursa ya kujifunza masomo ya sayansi, kama ambavyo
Kanisa Katoliki Jimbo la Same lilivyofanya.
Amelipongeza Kanisa Katoliki nchini kwa kuwa na heshima ya kutoa
mchango mkubwa
sana wa elimu hapa nchini, na
kuwanufaisha Watanzania wengi.
Amesema serikali itendelea kuyaunga mkono mashirika ya dini na taasisi nyingine
ambazo zinachangia juhudi za serikali katika
kuendeleza sekta ya elimu hapa nchini.
Akitoa maelezo mafupi ya Shule hiyo y ya Sekondari ya Kandoto, Askofu wa Jimbo
la Same, Mhashamu Koda amemweleza Rais kwamba kanisa
hilo limeamua kutoa kipaumbele cha elimu kwa mtoto wa kike,
lakini na kutilia mkazo masomo
ya sayansi kwa kuwa kanisa linatambua hakuna maendeleo bila elimu.
Askofu huyo
amesema Kanisa Katoliki halitaacha kutekeleza wajibu wake wa kujenga
na kuendesha shule za sekondari,
msingi, ufundi na shule za
awali zitakazotoa elimu yenye ubora
wa hali ya juu kabisa.
Akasema
“Mhe. Rais, Kanisa Katoliki litaendelea na kazi yake ya kutilia mkazo elimu,
kanisa litaendelea kutilia mkazo ubora
wa elimu na ubora wa
mazingira ya kusomea. Hata kama wenzetu
wote watatilia mkazo ujenzi wa
miradi yenye faida kubwa, sisi
Kanisa Katoliki tutaendelea kukazania elimu.
Shule hiyo ya Sekondari ya Kandoto yenye kidato
cha kwanza hadi cha sita ilianza
kujengwa miaka miwili iliyopita na jiwe lake
la msingi liliwekwa na Rais Kikwete
wakati huo akiwa Waziri wa
Mambo ya Nje na mgombea urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Shule hiyo ambayo imekamilisha
ujenzi wa vyumba vya kisasa
vya madarasa 18, ofisi za walimu
12, na majengo mengine imegharimu shilingi milioni 420 na bado inaendelea
kujengwa.
Pamoja na kufungua shule
hiyo ya Kandoto Rais pia alifungua shule nyingine ya kisasa ya awali na msingi
anayomilikiwa na masista wa Kanisa
Katoliki kutoka Italia na imegharimu shilingi
milioni 374.
Katika siku yake ya ziara
yake ya siku saba mkoani Kilimanjaro,
Rais Kikwete pia alifungua shule
nyingine ya sekondari ya Alikachenje iliyoko katika kijiji cha Makanya inayomilikiwa na kuendeshwa na
Profesa Mlacha.
Shule hiyo ya Alikachanje itakuwa na uwezo
wa kuchukua wanafunzi 1000 na tayari imeanza na wanafunzi 20 wa kidato cha kwanza na 20 wa sekondari.
Rais amempongeza Profesa Mlacha kwa
kujenga shule inayoendana na karne ya 21 ikiwa
na mazingira mazuri ya kusomea,
majengo ya kutosha na mazuri,
maktaba zenye vitabu va kutosha
na maabara.
Rais pia amekagua mradi
wa kilimo cha umwagiliaji wa Ndugu. Rais pia
amewaeleza wananchi waliojitokeza kwa wingi kusalimiana naye katika vijiji mbalimbali
kwamba serikali imeanza kazi ya utekelezaji wa ahadi alizoahidi wakati wa kampeni
katika wilaya hiyo ya Same.
Baadhi ya ahadi hizo ni ujenzi wa barabara ya lami katika maeneo
mbalimbali na tatizo sugu la maji kwa wilaya hiyo na vitongoji
vyake. Ametumia fursa hii kuwashukuru
wananchi wa wilaya ya Same kwa kumpigia kura na
kuichagua CCM.
Mwisho.
M.
Mwingira
Same, Kilimanjaro.
3
Agosti, 2007