TUMSAIDIE RAIS KIKWETE KWA KUFANYA KAZI- ASKOFU ELIOPHOO
SIMA
Na Maura Mwingira
Singida
16.1.2006
Askofu Eliophoo Sima wa Kanisa la Kiinijili
la Kilutheri Dayosisi ya Kati Singida amewahimiza Watanzania kufanya kazi kwa
bidii ili kumwongezea nguvu za kiutendaji Rais Jakaya Kikwete.
Alitoa
kauli hiyo jana baada ya kuwekwa Wakfu na kusimikwa kazini, katika ibada
iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu la Imanuel Mkoani Singida, ambapo
Rais Jakaya Kikwete alikuwa mgeni rasmi.
“Ikiwa
kila mmoja wetu atafanya wajibu wake vyema, kwa nguvu zake zote na kwa akili
zake zote bila shaka wewe uliye kiongozi wetu utakuwa na nguvu nyingi
Na
kuongeza, “Huwezi kuwa Rais mwenye nguvu kama sisi raia wako tutashindwa
kutumia vipaji vyetu ipasavyo, na tukafikiria kuwa matunda yote yanatoka Ikulu, tutazitafuna
Askofu
Eliophoo Yohana Sima ambaye aliwekwa Wakfu na kuingia kazini kuwa Askofu wa
Dayosisi ya Kati Singida alichaguliwa kushika nafasi hiyo katika mkutano mkuu
wa Sinodi uliofanyika Juni 20 mwaka jana.
Alisisitiza
kwamba, kila mwanadamu mahali alipo anaouwezo wa kutosha na kumfanya aishi bila ya matatizo.
Hata hivyo akasema kuwa upo uzembe unaofanya
na baadhi ya wanadamu, uzembe wa kutotaka
kutumia vipaji vyake, uwezo wake na
hazina ya maarifa ya kuyamudu maisha
yake na hatimaye kujikuta akiwa amezungukuwa na taabu nyingi.
“Iko
tabia mbaya ya watu wengi, na hii ni tabia mbaya
Askofu
huyo akaongeza kuwa
Akamwomba
Rais Kikwete na Watanzania wote kuifanya
Akasema
maswali yote hujibiwa kwa kazi nzuri, wenye kazi wana maneno machache. Na
kwamba kazi nzuri, kazi halali ni ufunguo wa mafanikio.
Hata hivyo Askofu Sima amesema kuwa ili
kila mtu afanye kazi, mfumo wa elimu unastahili kuboreshwa zaidi.
Akasema kuwa mfumo uliopo sasa umepungukiwa
“Elimu inayotolewa sasa inawafanya watoto
wetu wasiwe wabunifu, mtoto anayemaliza kidato cha nne, vijana wanaomaliza
kidato cha sita na chuo kikuu, bila ya kuajiriwa na serikali au na mashirika
mengine wanashindwa kabisa kupiga mbizi katika bahari hii yenye mawimbi”.
Akapendekeza kuwa itakuwa vyema
Akasisitiza kuwa mafaniko yaliyopo hivi
sasa yanatokana na raia waaminifu, ambao siku zote wamekuwa wakiamini kuwa bila
kuhenya huwezi kupata mafanikio.
Akatahadharisha kwa kusema “nguvu zao, muda
wao na kwa fadhila zao, wamejitolea kwa
uaminifu kwa nchi hii, mafanikio hayo yasitumiwe ovyo na watu wasio na huruma.
Kwani kwa kufanya hivyo kunawakatisha tamaa watu wengine kutumikia kwa uaminifu,
wakati wengine wakisubiri kuyatafuna bila huruma matokeo mema ya kazi hiyo au
kuyaharibu”.
MWISHO.