TATHMINI YA ZIARA YA RAIS YA
KUTEMBELEA MASOKO YA NAFAKA YA DAR ES SALAAM
Tarehe 6/2/2206, Mhe. Rais alifanya ziara ya ghafla ya kutembelea
masoko yanayouza nafaka katika jiji la Dar es Salaam. Lengo la ziara hiyo lilikuwa ni kujionea hali
halisi ya chakula ilivyo pamoja na bei zake.
Masoko ambayo Mhe. Rais aliyatembelea ni Tandale, Tandika na Kariakoo.
Baada ya Ziara hiyo, Katibu wa Rais aliitisha mkutano wa wasaidiza wa
Rais kwa lengo la kufanya tathimini ya ziara hiyo.
Wajumbe waliohudhuria mkutano huo
1. D. Jairo -
Mwenyekiti
2. F. Kuzilwa -
Mjumbe
3. R. Luhwavi -
Mjumbe
4. S. Kamhanda -
Mjumbe
5. Col. Simule -
Mjumbe
6. Col. Kimarao -
Mjumbe
7. M.Mwingira -
Mjumbe
8. Col. N. Kaisi
- Mjumbe
Akifungua mkutano huo, Katibu wa Rais aliwataka wajumbe kuchangia kwa
maana ya kuitathimini Ziara ya Mhe, Rais katika masoko yale, na kutoa
mapendekezo ya kumshauri Mhe.
·
Kwa
ujumla wajumbe waliridhika kwamba ziara hiyo ilikuwa ya mafanikio, kwani
ilikidhi matarajio ya Mhe. Rais ambayo yalikuwa ni kujionea hali halisi ya
chakula ilivyo katika masoko hayo.
·
Wajumbe
walikubaliana kwamba hali ya chakula katika masoko hayo hususani nafaka haikuwa
mbaya wala nzuri. Kwamba kulikuwa na nafaka ingawa si kwa kiwango cha
kuridhisha.
·
Baadhi ya
maeneo ambayo hutumika kuhifadhi nafaka wakati wa neema yalikuwa matupu, ni
sehemu chache tu ndizo zilikuwa na magunia machache ya nafaka.
·
Aidha bei
za nafaka hizo pia ilikuwa inatofautiana kutoka kwa muuzaji moja hadi mwingine.
·
Baadhi ya
nafaka kama vile unga wa sembe uliuzwa kilo shilingi 480, mchele uliuzwa
shilingi 650 hadi 800 kwa kilo. Bei hii pia ilikuwa ni tofauti kwa masoko ya
Kariakoo ambako kilo ya mchele ilikwenda
hadi shilingi 1000.
·
Kupanda
kwa bei za nafaka kulielezwa na wachuuzi hao kwamba kulitokana na uhaba wa nafaka zenyewe, gharama za
usafirishaji na ubora wa nafaka kulingana na maeneo inakotoka.
·
Katika
masoko yote matatu, kilio cha wananchi kilikuwa ni bei kubwa ya nafaka hizo, na
walimwomba Mhe. Rais kuingilia kati.
·
Wajumbe
waliridhika pia kwamba gharama za nafaka zinasimamiwa zaidi na soko huru kwa
vile serikali ilikuwa imejitoa katika udhibiti wa bei, hivyo kila mchuuzi
alijipangia bei kulingana na mazingira ya wakati ule.
·
Wajumbe
walielezwa pia kwamba hata nafaka ambazo zilikuwa zimeingizwa nchini na wafanyabiashara
ambao wameondolewa ushuru na serikali, nazo zilikuwa zikiuzwa kwa bei ya juu,
kinyume na matarajio ya serikali kwamba nafaka hizo zingeuzwa kwa bei nafuu.
·
Katika
kukabiliana na hili wajumbe walipendekeza kwamba, utafiti zaidi ufanyike,
kwanza wa kupata taarifa kutoka ofisi ya Waziri Mkuu- Idara ya Maafa kuhusu
utaratibu mzima ikiwa ni pamoja na
makubaliano yaliyopo kati ya serikali na wafanyabiashara hao. Jukumu hili
alipewa Mshauri Mkuu wa Rais, Col. Kaisi.
·
Aidha wajumbe walipendekeza pia kuwa ipatikane
kutoka kwa watu wa masoko bei halisi za
nafaka katika masoko hayo hususani katika kipindi hiki ambako kuna uhaba mkubwa
wa nafaka.
·
Aidha ilikubalika pia kwamba pawepo na
usimamizi kamili wa kusimamia tangu pale meli inayoleta chakula inapoingia
bandarini, upakuaji wake, usafirishaji
wa chakula hicho hadi usambazaji wake.
·
Wajumbe
walipendekeza hili lifanyike, ili kuwabana
baadhi ya wafanyabiashara wasio
waaminifu ambao wanaweza kuhujumu juhudi za serikali katika kukabiliana na
balaa hili la njaa.
·
Wajumbe
pia waligundua kuwa licha ya
wafanyabiashara wa masoko hayo kulipa ushuru, hali ya masoko hayo hususani
Tandale na Tandika ilikuwa mbaya, uchafu uliotapakaa kila mahali, na barabara
za kuingia na kutoka kwenye masoko hayo zilikuwa mbovu.
Mwisho