PRESS SECRETARY TO
THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22
2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@Ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUNA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA KATIKA
HALMASHAURI-KIKWETE
Na Mwandishi Maalum
Rais Jakaya Kikwete amesema haridhiki na hali ya utendaji kazi wa halmashauri nyingi za wilaya hapa nchini, na hususani katika matumizi ya fedha.
Ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na wakuu wa mikoa mara tu baada ya kuwaapisha katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu, Chamwino.
“Serikali inatoa fedha nyingi kwenye halmashauri, lakini matumizi ya fedha hizo yaharidhishi kabisa, kuna ubadhirifu mkubwa katika halmashauri, na nyinyi ndio wawakilishi wa Rais na ndio wasimamizi wa serikali, basi zisimamieni kwa karibu halmashauri “ akasisitiza Rais.
Akaongeza kuwa hataka
Akionyesha dhahiri kuchukizwa na matumizi
mabaya ya fedha katika halmashauri hizo, Rais alisema wakuu hao wana wajibu wa kuyatumia madaraka
usimamizi wa matumizi hayo ya fedha zinazopelekewa katika halmshauri ikiwa ni pamoja na kujua nini kinafanyika ndani ya halmashauri hizo.
“Halmashauri nyingi zinaendeshwa hovyo
hovyo tu, lazima mjue wanafanya nini,
sisemi muwaingilie
Kwa mujibu wa Rais, halmashauri za wilaya
zimekuwa zikipokea mamilioni ya fedha, kutoka Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya
Msingi, Mfuko wa Barabara, TASAF, Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari,
fedha ambazo amesema
Katika mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na Makamu Rais, Dk Ali Mohamed Sheni, Waziri Mkuu, Edward Lowasa na Waziri wa Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa, Mizengo Pinda, Rais alisema kuwa amewateua wakuu hao wa mikoa kushika nyadhifa hizo kwa kuwa anawaamini.
Akawaambia “Nimewateua kwa sababu ninawaamini, na imani huzaa imani. Ningekuwa na wasiwasi nanyi nisingewateua, ni matumaini yangu mtaniwakilisha vizuri na hamtaniangusha”.
Rais Kikwete aliwataka pia wakuu hao wa mikoa, kuzingatia maadili ya uongozi na maadili ya kazi, na kuongeza kuwa uhusiano na urafiki kati yake na wakuu hao utasimama katika utendaji wa kazi na matokeo ya kazi hizo.
“Jamani tukafanye kazi, sisi sote ni watu wazima, si vizuri kukumbushana juu wa wajibu wa majukumu yetu, sitegemei kufanya hivyo, lakini pale nitakapoona mambo yanakwenda ndivyo sivyo, basi nitakuwa sina njia nyingine bali kukubushana wajibu huo, lakini sitarajii tufikishane huko”, akasisitiza.
Akasema , Mkuu wa Mkoa ni kiongozi mkubwa sana, na kwa sababu hiyo matendo yake lazima yaendane na nafasi hiyo na lazima awe mfano mbele ya jamii kwa kuwa na maadili mema.
Aidha Rais kama ilivyokuwa kwa mawaziri, aliwaeleza wakuu hao wa mikoa kwamba wanakwenda kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, na kwa hiyo utendaji kazi wao lazima ulenge katika Ilani.
Amewataka watakapowasili katika vituo vyao vya kazi kupanga mikakati ya utekelezaji wa Ilani hiyo, ikiwa ni pamoja na kukusanya ahadi zote zilizotolewa wakati wa kampeni ili ziwekewa mikakati ya utekelezaji.
Kuhusu suala la ukame, njaa, na magao wa umeme, Rais aliwakumbusha wakuu hao wa mikoa kusimamia vema ugawaji wa chakula kwa kuzingatia uwezo wa wananchi katika kukipata chakula hicho.
Na kusisitiza kuwa asingependa kusikia taarifa za watu waliokufa kwa kukosa chakula.
Aliwataka pia kusimamia mgao wa umeme na kuwakumbusha TANESCO kuheshimu ratiba zao za mgao.
Kuhusu suala la ulinzi na usalama, Rais
alisema kwa kuwa wakuu wa mikoa ndio wenyeviti wa kamati za ulinzi na usalama,
basi wanawajibu mkubwa wa kusimamia amani katika maeneo
Aidha Rais aliwataka pia wakuu hao wa mikoa
kulisimamia kwa karibu tatizo la
utumiaji wa madawa ya kulevya kwa vijana. Amesema kuwa tatizo
Kwa upande wa utunzaji wa mazingira, Rais aliwaagiza wakuu hao, kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa karibu, upandaji wa miti, kusimamia ukataji wa miti pamoja na utunzaji wa vyanzo vya maji na uoto wa asili.
Akasema kuwa utunzaji wa mazingira ni ajenda kudumu na hivyo akawaasa kutoimba wimbo wa utunzaji wa mazingira bila ya kuweka mikakati madhubuti na ufuatiliaji wake.
Akawataka kuwasimamia kwa karibu, mabwana
misitu ambao aliwaelezea kuwa wao ndio vinara katika suala zima la uharibifu wa
mazingira kwani baadhi
Akizungumza kwa niaba ya wakuu wenzi wa mikoa, mkuu wa mkoa
wa
Akasema kwa upande wao watajitahidi
kumsaidia Rais kwa kutekeleza majukumu
Mwisho.