PRESS SECRETARY TO
THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State
House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Balozi Andrew Young azungumza na Rais Kikwete …. 1
Mwenyektii wa Mfuko wa kuendeleza biashara katika nchi za Kusini mwa Afrika (SAEDF), Balozi Andrew Young amemhakikishia Rais Jakaya Kikwete kwamba mfuko huo uko tayari kumsaidia katika uwezeshaji wa wafanyabiashara wadogo na wa kati hapa nchini.
Balozi Andrew Young ameyasema hayo leo Ikulu jijini wakati yeye na ujumbe wa mfuko huo walipomtembelea Rais Kikwete na kuzungumza naye.
“Tueleze wapi unataka tukusaidie, na sisi tuko tayari
kukusaidia, tutafungua miradi zaidi hapa
Mfuko wa kuendeleza biashara katika nchi za Kusini mwa Afrika, ulianzishwa na Rais mstaafu wa Marekani Bill Clinton mara baada ya kuzaliwa Afrika Kusini huru mwaka 1994.
Madhumuni hasa ya mfuko huo ni katika kuwawezesha Waafrika hasa weusi ( black empowerment) ili nao waweze kushiriki katika umiliki wa uchumi kwa kuendesha viwanda vidogo na vya kati.
Balozi Andrew Young amemueleza Rais ya kuwa mfuko huo unataka kujielekeza sasa katika kuwawezesha Watanzania kimitaji, kimenejimenti na katika mbinu za upembuzi yakinifu zitakazowawezesha kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo vidogo na vya kati.
Mwenyekiti huyo akasisitiza
umuhimu wa Waafrika hususan wazalendo kuwa na uwezo wa
kumiliki taasisi za kifedha tofauti
na ilivyo hivi sasa ambapo
alisema ni Waafrika wachache
Aidha Balozi Young alipongeza
msimamo wa
Balozi Andrew Young azungumza na Rais Kikwete ….2
Akazitaja nchi hizo kuwa ni
Katika mazungumzo hayo Rais Kikwete alimweleza Mwenyekiti huyo wa SAEDF kwamba mfuko huo umekuja katika wakati muafaka ambapo serikali inajipanga vema katika mbinu na mikakati ya kuwawezesha Watanzania walio wengi kumilikia uchumi na kuupiga vita umaskini.
Akasema juhudi hizo za serikali zinakwamishwa na uwezo mdogo wa kifedha na vile vile katika uandaaji wa sera na mikakati ya uwezeshaji na ndio maana mifuko kama hiyo inakaribishwa ili iweze kusaidiana na serikali.
Miongoni mwa wajumbe wa Bodi ya mfuko huu ni pamoja na Balozi mstaafu Ami Mpungwe.
SAEDF inaendesha shughuli zake katika nchi 10 ambazo ziko katika Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
Mwisho
Ikulu
13 Februari, 2006