PRESS SECRETARY TO THE
PRESIDENT
Fax. No. 255-22
2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Na Maura Mwingira
CapeTown
Afrika ya Kusini
1.6.2006
Imeelezwa kuwa
Mkurugenzi Mtendaji
na Mjumbe wa Bodi ya Taasisi isiyo ya kiserikali
ya World Economic Forum, Bw
Peter Torreale, aliyasema hayo wakati wa
hafla ya chakula maalum kilichoandaliwa kwa ushirikiano wa taasisi hiyo na
serikali ya Tanzania, kwa lengo la kuinadi
Tanzania kama nchi yenye vivutivo vizuri vya uwekezaji
katika bara la Afrika na duniani.
Bw. Torreale aliwaeleza wageni waliohudhuria chakula hicho, wageni ambao
ni waalikwa wanaohudhuria mkutano wa maendeleo ya
uchumi katika Afrika kuwa
Alibainisha kuwa katika utafiti uliofanyika mwaka jana na wataalam
wa masuala ya uchumi, ulionyesha
kuwa
"Mkiendelea na utaratibu huu,
sina shaka kwamba ifikapo mwaka 2011
Katika chakula hicho na ambacho
Rais Jakaya Kikwete ndiyo aliyekuwa
akiinadi nchi yake, na kujibu
maswali mbalimbali kutoka kwa wageni
hao, Bw. Torreale alisema kuwa hivi sasa Tanzania inashika nafasi ya tatu
duniani baada ya Brazil na Turkey kwa kuwa na
mazingira mazuri ya uwekezaji na
kuvutia mitaji. Na kuongeza kuwa ina kila nafasi ya kuzipita
nchi hizo.
Akiinadi
Alisema kuwa serikali yake itaendelea
na uboreshaji
wa mazingira ya uwekezaji, ikiwa
ni pamoja na kupitia sheria
mbalimbali, kupunguza gharama za kufanya
biashara.
Aidha Alisema kuwa Tanzania ni kituo kikubwa
cha biashara katika nchi za Afrika
Mashariki na Kati na kusisitiza kuwa
mazingira ya kufanyia biashara ni mazuri na
masoko yapo na hivyo kuwahimiza
waje kuwekeza Tanzania.
Aliongeza kuwa
"Njooni muwekeze
Pamoja na
Rais Kikwete kutoa maelezo yaliyowagusa
na kuwavutia wageni waliohudhuria chakula hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji,
Bw Ole Naiko, alitoa maelezo kwa njia ya
powerpoint na namna gani
Katika maelezo yake, Bw.Ole Naiko
alisema kuwa wawekezaji hawana sababu ya kutokuja
na kuwekeza nchini kwa kuwa taratibu zote za kuwawezesha
kufanya hivyo zimekwisha kuainishwa na serikali.
Alibainisha kuwa katika utafiti uliofanywa na Gazeti
la Financial Times toleo la 2005/2006, kuhusu nchi za
Afrika zenye mwelekeo mzuri, alisema kuwa gazeti
hilo liliitangaza Tanzania kama nchi inayoongoza
katika Afrika Mashariki na Kati, katika kuvutia mitaji (FDI), na ikawa ya pili
katika vigezo ya culture and heritage na
ikawa ya pili nyuma ya Afrika
ya Kusini katika vigezo vya
eneo muhimu la kiuchumi ( economic pontential
category).
Baadhi ya Maeneo
ambayo wageni hao walioonyesha kuvutiwa nayo ni
katika uendelezaji wa sekta ya
kilimo na elimu ambapo walitaka
kujua serikali imeweka mikakati gani ya kuboresha
maeneo hayo lakini vilevivile inatoa vivutio gani kwa watu
wanaotaka kuwekeza katika maeneo hayo.
Rais Kikwete leo anaendelea
na mkutano ambapo atashiriki katika mijadala mbalimbali.
Mwisho.