THE   UNITED   REPUBLIC   OF   TANZANIA

 

PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT

 

Fax. No. 255-22 2113425                                              The State House,                                 

Tel: 255-22-2116539/2116913                                     P.O. Box 9120,

 E-mail:  press@ikulu.go.tz                                                    DAR ES SALAAM.

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Waziri Mkuu wa China …. 1

 

China imeipatia Tanzania Yuan milioni 80 ukiwa ni mkopo kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ukiwamo mradi wa ujenzi wa uwanja mpya wa michezo unaoendelea kujengwa.

 

Pamoja na kutoa mkopo huo, China pia imeipatia serikali ya Tanzania na Zambia mkopo usiokuwa na riba wa Yuan milioni 50 kwa ajili ya maendeleo ya Reli ya Uhuru (TAZARA) inauyoziunganisha Tanzania na Zambia.

 

Pamoja na kutoa fedha hizo China itaendelea kutoa msaada wa kiufundi katika shirika hilo.

 

Uamuzi wa China kuipatia mikopo nafuu Tanzania ulitangazwa rasmi hapa jana na Waziri Mkuu wa China, Mhe. Wen Jiabao wakati wa mazungumzo rasmi yaliyofanyika jana kati yake na Rais Jakaya Kikwete Ikulu jijini.

 

Waziri Mkuu huyo alikuwa nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili kwa mwaliko wa Rais Kikwete; anaondoka leo.

 

Katika mazungumzo hayo, Waziri Mkuu huyo Wen Jiabao alisema kuwa China pia inakusudia kujenga nchini Tanzania kituo cha kisasa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya kilimo ambapo pia itatoa wataalam wa kuwafundisha wataalam wa Kitanzania na wakulima.

 

Pamoja na kujenga kituo hicho, China pia itajenga kituo cha kisasa kwa ajili ya kuzuia na kutibu malaria.

 

Aidha kwa mujibu wa Waziri Mkuu huyu, China pia itajenga shule ya msingi ya kisasa katika kijiji kitakachochaguliwa.

 


Waziri Mkuu wa China ….2

 

Makubaliano  ya mikopo hiyo  yalitiwa saini na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.  Asha-Rose Migiro kwa upande wa Tanzania na Waziri wa Biashara Mhe. Bo Xilai kwa upande wa China.

 

Akizungumza kuhusu ujenzi wa uwanja wa Taifa,  Waziri Mkuu huyo alibainisha kuwa mradi wa ujenzi wa uwanja huo ambao kwa asilimia kubwa umegharamiwa na China, kwamba ni mradi mkubwa wa pilina wa aina yake baada ya TAZARA kwa nchi yake kufadhili.

 

Alisema kukamilika kwa uwanja huo kutazidi  kuimarisha na kuweka kumbukumbu imara ya uhusiano wa kihistoria kati ya nchi hizo mbili.

 

Aidha Waziri Mkuu huyo wa China pia alisema serikali yake itatoa dawa za kutibu malaria  zenye thamani ya Yuan milioni 3.

 

Akizungumza kuhusu ombi lilitolewa na Rais Jakaya Kikwete kuhusu nchi hizo mbili kuangalia uwezekano wa kushirikiana na kuona namna wanaweza kujenga hospitali  kwa ajili ya kutibu magonjwa ya moyo alishauri kuwa majadiliano yafanyike kati ya pande hizo mbili.

 

Wakati wa mazungumzo hayo, Rais alisema Watanzania wengi wamekuwa wakipoteza maisha yao kwa vile tu wamekosa tiba ya magonjwa hayo.

 

Rais Kikwete alisema, serikali pia imekuwa ikitumia fedha nyingi kuwapeleka watu wenye matatizo ya moyo nchini za nje kwa matibabu, kwa ukosefu wa vifaa inawa wataalam wapo..

 

 

Aidha Waziri Mkuu huyo alisema Tanzania na China zinatakiwa kuimarisha  na kuendeleza uhusiano kati yao ikiwa ni pamoja na kutafuta maeneo mapya ya ushirikiano.     

 

Alisema pia serikali yake inaendelea kuwashawishi watalii wengi kuja kutembelea Tanzania kama njia ya kuiongezea mapato Serikali.

 

Aliongeza kuwa atawahimiza wawekezaji zaidi kuja kuwekeza nchini na akatoa changamoto kwa Watanzania kutengeneza bidhaa zenye ubora ili ziweze kuingia katika soko la China.

 

China imefuta kodi kwa bidhaa za Tanzania zinazoingia katika nchi hiyo.

 

 

Waziri Mkuu wa China ….3

 

Kwa upande wake Rais Kikwete alimshukuru Waziri Mkuu huyo kwa kuitembelea Tanzania pamoja na misaada ya kimaendeleo na uchumi ambayo nchi hiyo imekuwa ikiipapatia Tanzania.

 

Rais alisema kuwa Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, ushirikiano ambao ni wa kihistoria.

 

Katika mazungumzo hayo, Rais alieleza changamoto mbalimbali ambazo  serikali yake imekuwa ikikabiliana nayo.

 

 

Wakati huo huo, Serikali  hiyo ya China imeipatia Zanzibar mkopo nafuu wa Yuan million 20 kwa ajili  ya kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo visiwani humo.

 

Aidha Zanzibar na China  pia zilitiliana saini na kubadilishana hati mbili za makubaliano ambapo China itafanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya  kukarabati uwanja wa Taifa.

 

Hati ya pili inahusu Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupatiwa mtambo wa kati ya kurushia matangazo kilowatts 50, channel ya kupokelea matangazo  ya CCTV-9 na kituo cha Radio.

 

Utiaji saini huo ulifanywa na Waziri wa Fedha na Uchumi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Mwinyihaji Makame na Waziri wa Biashara wa China Mhe. Bo. Xilai.

 

Mwisho

 

Ikulu

Dar es Salaam

 

23/06/2006