THE
UNITED REPUBLIC
OF TANZANIA

PRESS
SECRETARY TO THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State
House,
E-mail: press@ikulu.go.tz DAR ES SALAAM.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
Ujumbe wa Al Bashir … 1
Rais Jakaya Kikwete leo asubuhi amepokea
ujumbe maalum kutoka kwa Rais
Omary Al- Bashir wa Sudan,
ulioletwa kwake na Waziri wa
Ushirikiano wa Kimataifa wa Sudan Dr. Tijan
Salehel Fidel.
Katika ujumbe huo, Rais
Bashir amemwomba Rais Kikwete, kushiriki
katika juhudi za kuleta amani
na hasa katika
utekelezaji wa makubaliano ya kuleta amani huko
magharibi mwa Sudan, hususan katika jimbo la Darfur na pia
kusaidia katika kushawishi vikundi vingine ambavyo havijasaini makubaliano hayo ya kusitisha
mapigano ya Abuja , Darfur Peace Agreement (DPA) yaliyotiwa saini mwezi Mei mwaka
huu.
Mgogoro wa Darfur huko
magharibi mwa Sudan ulianza miaka mitatu
iliopita kati ya serikali ya
rais Bashir na kikundi kikuuu
cha Sudan Liberation Movement (SLM) Ingawa makubaliano ya amani yameshatiwa saini na baadhi
ya makundi bado
kuna vikundi vingine ambavyo havijasaini makubaliano hayo.
Kikundi kingine cha Uasi kijulikanacho kama Sudan Liberation Army (SLA), kimegawanyika katika makundi mawili moja likiongozwa na Minni Minnawi
na lile la Abdul Walid Mohammed Al –Nur ambaye anashinikiza maelewano zaidi kutoka kwa serikali
ya Omar Al Bashir.
“Serikali ya Sudan inaiomba Tanzania kama mjumbe wa Baraza
la Usalama la Umoja wa Mataifa kuvishawishi
vikundi ambavyo havijatia saini na kufikia makubaliano
vifanye hivyo ili utekelezaji uweze kwenda haraka
zaidi”. Waziri Fidel amemueleza Rais Kikwete wakati akimpa ujumbe toka
kwa Rais
Bashir.
Ujumbe wa Al Bashir …2
Waziri huyo wa
ushirikiano wa kimataifa wa Sudan amemueleza Rais Kikwete kuwa
migongano ilioko Sudan ni
ya kisiasa na kiuchumi hivo
jitihada zaidi zinahitajika kuelezea umma kuwa si
lazima kutumia silaha kufikia maelewano.
Mjumbe huyo wa Rias Bashir pia
amemuomba Rais Kikwete arudishe uhusiano wa kibalozi
kati ya nchi
mbili hizi
Tanzania
ilifunga ubalozi wake huko Sudan
kwa muda tangu Machi 1989
kutokana
na matatizo ya kiuchumi, lakini
majengo ya ubalozi yana kodishwa
na Uganda.
Waziri huyo wa
ushirikiano wa kimataifa wa Sudan
alifuatana na balozi wake hapa Tanzania,
Balozi El -Mughira Ali Omar.
Mwisho
Ikulu,
Dar es Salaam
23 Juni,
2006