PRESS SECRETARY TO THE
PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
BALOZI WA
Na Maura Mwingira
15/12/2006
Aliyeteuliwa
na kupitishwa kwa kauli mmoja,
ni Balozi Liberata Mulamula kutoka
“
Mara
baada ya tangazo hilo, ukumbi mzima uliojaa wajumbe
waliokuwa wakihudhuria mkutano wa siku
mbili wa Kimataifa wa Ukanda wa
Maziwa Makuu ulilipuka kwa shangwe
na vigeregere hali iliyodhihirisha kukubaliwa kwa uteuzi wa Rais
Jakaya Kikwete.
“Shangwe hii inadhihirisha
kukubaliwa kwa mteule wetu” akasema
Kikwete hali iliyoamusha shangwe tena kutoka kwa wajumbe wakiwamo kutoka
Uteuzi huo ulidhibitishwa na kupokelewa kwa
kauli moja na viongozi wakuu wa nchi na
serikali ambao ni wanachama wa
Ukanda wa Maziwa Makuu.
Mara
baada ya kutangazwa kwake ya
wajumbe waliokuwa wakifanya kazi kwa karibu na Balozi Mulamula tangu kuanzishwa kwa Mchakato wa Ukanda
wa Maziwa makuu, baada ya
mkutano wa kwanza uliofanyika Dar es salaam mwaka 2004, walijipanga moja baada ya
mwingine kumpongeza kwa furaha kubwa.
Baadaye
Balozi Liberata Mulamula akiwa amejawa na
machozi ya furaha, alipita mbele ya viongozi
wakuu wa nchi na serikali
na kushikana nao mikono.
Akizungumza
katika hotuba yake fupi ya
kushukuru na kukubali uteuzi huo, Balozi Mulamula
alisema kuwa amejawa na furaha
kubwa na isiyokuwa na kufani
na amefarijika sana kwa uungwaji
mkono kutoka kwa viongozi na
wajumbe wa mkutano huo.
Alisema anaahidi kufanya kazi kwa
juhudi na maarifa na kwamba
atashirikiana kwa karibu na viongozi
wakuu wa nchi na
serikali wa Ukanda wa Maziwa
Makuu katika kuhakikisha kwamba amani, utulivu na maendeleo yanatawala
katika eneo hili.
Aliwashukuru
viongozi hao kwa imani kubwa
walionyesha kwake, na hususani Rais
wake Jakaya Mrisho Kikwete kwa kumteua
na kwamba hiyo ni heshima
kubwa sana kwake na kwa
Tanzania nzima na kwamba hatawaangusha katika utekelezaji wa majukumu yake
hayo makubwa.
Kabla ya Uteuzi huu,
Balozi Liberata Mulamula alikuwa mkuu wa kitengo cha Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Katika
Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa.
Aliteuliwa na kuwa balozi mwezi
mwaka 2003 na Rais Benjamin Mkapa.
Katika Mkutano huo, Rais
Jakaya Kikwete alisema kuwa
Ofisi za Sekretariati ya Ukanda wa Maziwa Makuu itakuwa
Katika siku ya mwisho
ya mkutano wa pili wa kimataifa
wa Ukanda wa Maziwa Makuu,
viongozi wakuu wa n hi na serikali
waliohudhuria mkutano huo, walitia saini Mkataba
wa Usalama, Amani na Maendeleo
katika Ukanda wa Maziwa Makuu.
Mkataba huo unaeleza kwamba
wakuu wa nchi na serikali
wanachama wa mkutano wa kimataifa
wa Ukanda wa Maziwa Makuu,
wanatambua haja ya kuheshimu demokrasia
na utawala bora, misingi muhimu iliyoainishwa ndani ya mkataba wa
Umoja wa Mataifa na Mkataba
wa kuanzishwa Umoja wa Afrika,
ambayo ni kuheshimu mipaka ya nchi, uhuru
wa nchi kujiamulia
mambo yake bila ya kuingiliwa na
nchi nyingine na kuondokana na vitendo vya uchokozi, kukataa
nchi mwanachama kuruhusu matumizi ya ardhi yake
kama ngome ya uvamizi au kuhujumu
nchi nyingine mwanachama.
Viongozi hao pia
wamesema wanatambua haja ya kuwa
na utashi thabiti na madhubuti wa
kisiasa katika kutafuta suluhu za migogoro kwa
njia ya amani
na hususan kwa kuheshimu
ahadi zetu katika hali ya kuaminiana.
Vile
vile viongozi hao wamesisitiza dhamira ya kujenga
uhusiano kati ya nchi zao
kwa kufuata misingi iliyoainishwa katika hati za
kisheria za kimataifa na kanuni
na misingi inayokubalika duniani, vipaumbele vya kisiasa na kufuata
misingi kama ilivyoelekezwa katika Azimio la Dar es Salaam, pamoja na kubadilisha Ukanda wa Maziwa
Makuu, kwa kusudio la pamoja, kuelekea kuwa na
eneo la amani na usalama wa
kudumu, eneo tulivu kisiasa na kijamii, pia
kuwa na eneo
lenye uchumi unaokua na maendeleo
ya pamoja kupitia ushirikiano katika sekta mbalimbali
kwa manufaa ya watu wao.
Aidha katika Mkataba huo, viongozi hao
wanasema kuwa wamedhamiria kuhakikihsa utekelezaji wa misingi ya sheria
za kimataifa za kibinadamu, hususani zile zinazohusiana
na kulinda na kusaidia wanawake,
watoto, wakimbizi na watu waliolazimika
kuyahama makazi yao ambapo ukiukwaji
wa wa sheria
hizo huwa na athari mbaya kwa jamii
husika.
Wamesema kuwa wanasisitiza uamuzi waliochukua Dar es salaam wa kuutangaza
Ukanda wa maziwa Makuu kuwa Eneo Maalum la Ustawi na Maendeleo na
kwa pamoja kukabiliana na changamoto za ustawi na maendeleo kwa kuhakikisha ushiriki wa wote, hususani kwa kushirikisha
jumuia za kiraia, vijana, wanawake, sekta binafsi, mashirika ya dini na
kwa kushirikiana kwa karibu na
jumuia muhimu za kikanda,
umoja wa Afrika, umoja wa
Mataifa, na Jumuia ya Kimataifa.
Ndani ya Mkataba huo
wenye ibara 35 viongozi hao wamedhamiria
kupitisha na kutekeleza kwa pamoja mipango ya utekelezaji wa Itifaki na
mifumo ya kutafsiri kwa vitendo
vipaumbele vya kisiasa na kanuni
elekezi za Azimio la Arusha.
Mwisho