PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT

 

Fax. No. 255-22 2113425                                        The State House,                             

Tel: 255-22-2116539/2116913                                  P.O. Box 9120,

                                                                                  DAR ES SALAAM.

E-mail:  press@ikulu.go.tz

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

 

JK AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA AKUKWETI

 

  • Mwinyi, Mkapa wahudhuria

 

Rais Jakaya Kikwete leo amewaongoza waombolezaji katika utoaji wa heshima za mwisho kwa  mwili wa Marehemu Juma Akukweti, uliofanyika nyumbani kwa marehemu Masaki, Jijini  Dar es Salaam.

 

 Shughuli za utoaji wa heshima kwa mwili wa marehemu Akukweti zilifanyika  kuanzia saa moja asubuhi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo marais wastaafu, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa,  Makamuwa Rais, Dk Mohammed Shein, na Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

 

Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar aliwakilishwa na Waziri Ramadhani Shabani, ambaye alisema kwamba,, Rais Karume amepokea kwa mshituko mkubwa  taarifa za kifo cha Mhe. Juma Akukweti na kwamba anaungana na familia ya marehemu katika kipindi hiki cha majonzi.

 

Viongozi wengine waliotoa heshima  za mwisho, ni Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, Jaji Mkuu Barnabas Samatta, Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo, wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mawaziri, Naibu Mawaziri, Wabunge, Makatibu Wakuu, viongozi wa vyama vya siasa, wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki.

 

Baada  ya shughuli za  kutoa heshima za mwisho kukamilika, ilifuatia sala kwa marehemu na dua zilizoongozwa na  Naibu  Mufti Sheikh Mkuu Abubakari Zuberi.

 

Baada ya sala na dua mwili wa marehemu Akukweti ulingizwa katika gari la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) namba 1776 JW04 na kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere tayari kwa safari ya kwenda Tunduru, mkoani Ruvuma kwa mazishi hayo kesho.

 

Mazishi hayo yataongozwa na Rais Jakaya Kikwete ambaye anaondoka leo mchana kuelekea Masasi na kesho Tunduru.

 

Mwisho.

 

Ikulu

06 Januari, 2007