PRESS
SECRETARY TO THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22
2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
JK-WANABUNDA
UCHUKIENI UMASKINI
·
Asema wakiisubiri serikali
watachelewa
Na Mwandishi Maalum
Rais Jakaya Kikwete ametoa changamoto kwa wananchi wa
Wilaya ya Bunda kuichukia hali ya wilaya
“Nchi yetu iko nyuma
Alitoa changamoto hiyo jana usiku, wakati wa hafla ya chakula cha hisani ya kuchangia mfuko wa Elimu wa Wilaya ya Bunda. Hafla hiyo ilifanyika katika hoteli ya Golden Tulip ambapo Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi. Alichangia 1.5 milioni.
Alisema “
Rais Kikwete aliwaambia wageni waliohudhuria hafla hiyo wakiwamo wafanyabiashara, wawekezaji na wananchi kutoka wilaya ya Bunda na wilaya jirani, na Mkuu wa Mkoa wa Mara Isidori Shirima, kwamba, elimu ndio jambo litakaloitoa wilaya hiyo ya Bunda hapo ilipo.
Alibainisha kuwa yeye (Rais) amekuwa mpiga debe mkubwa wa elimu na anafanya hivyo kwa kuamini kwamba elimu ndiyo itakayowaletea Watanzania, tofauti za kuelekea kwenye maendeleo.
Rais alisema hali ya umaskini inayoikabili wilaya hiyo si kwa sababu haina raslimali, bali kinachokosekana ni maendeleo ya raslimali watu watakaowezesha raslimali zilizopo ziweze kutumika na kuleta tofauti ya maendeleo inayohitajika.
Alisema
amefurahishwa
“Uamuzi huu mliofanya ndio uamuzi wenyewe, mkingojea serikali mtachelewa, haya tunayofanya sisi leo hii, wenzetu wengine waliyagundua mapema, wakajenga shule ndio maana utasikia, profesa fulani, daktari bingwa fulani, mwishoni mnasema hawa wana ukabila, hapana, si ukabila, wamesoma” akasema na kuwafanya washiriki kuangua kicheko.
Alisema kuwa jambo la msingi ni kwa wale ambao nao wamezinduka na kutambua umuhimu wa elimu kongeza jitihada za kuchangia katika maendeleo ya elimu badala ya kuisubiri serikali.
Rais Kikwete aliongeza kuwa, serikali inatoa mgao wa fedha kwa nchi nzima, hali aliyosema kwa wale wenye mahitaji maalum inakuwa si rahisi kwao kupata zaidi.
Hivyo akatoa ushauri wa wale wenye mahitaji maalum kwenda kwa watu wenye fedha ambao wana moyo wa kutoa na kuchangia katika shughuli za maendeleo ili mradi waridhike kwamba wewe unayekwenda kuomba unayo dhamira ya dhati ya kufanya kile unachoombea.
Awali akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya elimu katika wilaya hiyo ya Bunda, Mkuu wa Wilaya Bibi Chuku Gallawa, alisema kuwa jumla ya shilingi milioni 535 zinahitajika ili kukamilisha uboreshaji wa shule 24 zilizopo katika kata 20 za wilaya hiyo.
Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 201.8 tayari zimekwisha kupatikana kutoka kwa wananchi wa wilaya hiyo ya Bunda na wahisani mbalimbali.
Katika hafla hiyo ya jana, jumla ya milioni 286,485 zikiwa ni fedha taslimu zilipatikana, na ahadi zikiwa ni shilingi milioni 156.9 na hivyo kufanya jumla ya michango yote kuwa shilingi milioni 443.385
Mkuu huyo wilaya alisema kuwa fedha hizo zitatumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa na kwamba taarifa za matumizi zitawekwa wazi
Alisema kukamilika kwa shule hizo kutatoa fursa kwa wanafunzi wote 5,579 waliofaulu katika mtihani wao wa darasa la saba mwaka jana kuendelea na elimu ya sekondari.
Watu wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na baadhi ya Mawaziri na Waziri Mkuu Mstaafu, Joseph Sinde Warioba.
Mwisho