PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT

 

Fax. No. 255-22 2113425                                               The State House,                            

Tel: 255-22-2116539/2116913                                        P.O. Box 9120,

                                                                                        DAR ES SALAAM.

E-mail:  press@ikulu.go.tz

 

 

 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

Premi Kibanga,

London,

15.1. 07

 

Serikali ya Uingereza itachangia paundi za uingereza 105 milioni kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2007/8 kutoka  paundi 90 milioni za mwaka huu wa fedha unaomalizika mwezi wa June. Mchango huu katika bajeti ni kwa ajili ya kusaidia juhudi za serikali katika kupunguza umaskini kwa wananchi wa Tanzania

 

Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa Hilary Benn amesema leo baada ya mkutano wake na Rais Kikwete na pia kutangaza azma hiyo wakati wa mhadhara kuhusu Maendeleo ya Afrika juu ya Marekebisho ya Sekta ya Utumishi wa Umma.

 

 

Afrika inamudu kujifanyia marekebisho ikidhamiria, demokrasia inatendeka, uchumi unakuwa, Tanzania ni ishara nzuri ya mategemeo barani Afrika na hasa katika nchi zilizo kusini mwa Sahara, imeonyesha mfano, na imedhihirisha kuwa mageuzi makubwa yanaweza kufanyika barani Afrika, napenda kuchukua nafasi hii kukupongeza kwa hilo”. Bwana Benn amemwambia Rais Jakaya Kikwete mara baada ya Rais kutoa mhadhara katika jumba la mikutano la Chattam, jijini London.

 

 

Bwana Benn ameyataja mafanikio ya Tanzania kuwa ni kuongezeka kwa idadi ya watoto waliojiandikisha katika shule za msingi kuongezeka     maradufu kutoka milioni 4 mwaka 2000 hadi milioni 8 hivi sasa, ikiwa ni ongezeko la asilimia 96.(tisini na sita), kukua kwa pato la Taifa na uchumi kwa ujumla kutoka asilimia 5 (tano) tangu mwaka 2000 hadi asilimia 7 (saba) kwa sasa na kupungua kwa vifo vya watoto wachanga katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

 

Mapema katika Mhadhara kususu marekebisho ya Utumishi serikalini, Rais Kikwete amesema Tanzania inafanya marekebisho kwa nia ya kuleta mawazo mapya, malipo mazuri na hatimaye kumpatia mtumishi wa umma maslahi mazuri yenye kutia ari na nguvu katika kufanya kazi.

 

Rais Kikwete amesema tayari tume ya kuangalia upya maslahi ya watumishi wa umma imeshakamilisha kazi yake na serikali itaanza kuyatafakari mapendekezo yake, na kuwa ana uhakika kwamba mapendekezo hayo yatatumika katika maamuzi..

 

Marekebisho haya ya utumishi wa umma yanahusishwa sana na juhudi za serikali kuondoa umaskini na pia yanahusishwa katika sekta zingine mbalimbali za serikaliniRais amesema.

 

Mhadhara huo ulihudhuriwa na wanasiasa, wafanyabiashara, wasomi, watafiti na mabalozi kutoka sehemu mbalimbali barani Afrika na Ulaya ambao walipata nafasi ya kuuliza maswali na kujibiwa na Rais.

 

Rais aliwasihi Waafrika walioko ulaya kushiriki ipasavyo katika kuleta maendeleo na kuondosha umaskini barani Afrika kwa kuunganisha nguvu na mitaji yenye lengo la kuweka vitega uchumi barani.

 

Wito wangu kwa Waafrika wote nje ya bara letu, mkusanye raslimali kwa nia ya kuendeleza Afrika kwani hata wao pia tunawahitaji na ni wenza katika maendeleo na kuondosha umaskini.

 

Mapema kabla ya kutoa mhadhara katika jumba la Chatam, Rais Kikwete alizungumza na wafanyabiashara wa Uingereza, hususan kwenye sekta ya Fedha na kuwahimiza kuleta vitega uchumi na kuwekeza Tanzania.

 

Katika kikao hicho Rais ameelezea umuhimi na faida watakazopata kwa kuwekeza Tanzania kuwa ni pamoja na kuwa na uhakika wa kufanya biashara katika mazingira ya amani na utulivu, kuweza kupata wigo mkubwa katika kufanya biashara na masoko kwani Tanzania ni moja ya nchi za Afrika Mashariki na pia ndiyo lango kuu la kuingilia na kutokea nchi za Maziwa Makuu.

 

Rais Kikwete leo asubuhi ( 16 Jan. 07) anakutana na Waziri Mkuu Tony  Blair, Waziri wa Fedha Gordon Brown na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Don McKinnon, Wabunge, viongozi wa vyama vya siasa na dini kabla ya kufanya mkutano na waandishi wa habari kuzunngumzia ziara yake.

 

Mwisho