
THE UNITED
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WAFANYA BIASHARA WAWEZA KUKUZA KILIMO CHA AFRIKA NA
MISAADA NI MUHIMU KWA MAENDELEO.
PREMI KIBANGA,
JAN 26, (DAVOS, USWIS)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema wafanyabiashara wana uwezo mkubwa wa kuleta mapinduzi ya kilimo na kukifanya kiwe chenye tija zaidi kiasi cha kuleta maendeleo na kubadili maisha ya watu wa Bara la Afrika.
Wafanyabiashara waweza kufanya hivyo wenyewe, kwa kushirikiana na serikali au hata kwa kushirikiana na wakulima wenyewe popote walipo barani Afrika
Rais amesema hayo jana (25.Jan.07) mwanzo wa moja ya vikao vya Baraza la Uchumi Dunian (World Economic Forum) linaloendelea Davos Uswis. Rais Kikwete alikuwa mwenza wa kikao hicho akishirikiana na Bw. Antony Burgamans, Mwenyekiti wa Uniliver huko Uholanzi.
Kilimo
Afrika bado ni duni wakati asilimia sabini ya watu
wake wanakitegemea, hakitumii
teknolojia ya kisasa na pia
kinategemea
Amesema wafanyabishara wanaweza wakaja Afrika kuanzisha mashamba makubwa ya umwagiliaji, wanaweza kujenga viwanda vyenye muelekeo wa kilimo kwa ajili ya mbolea, mbegu na hata pembejeo na pia kuweka mfumo mzuri wa masoko.
Ametoa mfano wa
Nina hakika
Naye Rais wa Liberia Ma Ellen Johnson Sirleaf amewaambia washiriki kuwa Mapinduzi ya Kilimo ya nchi za Asia (maarufu kama Green Revolution) pia yanaweza kurudiwa barani Afrika ikiwa kilimo hicho kitafanyiwa utafiti wa kisayansi kwani kwa sasa bado kilimo cha Afrika ni cha matumizi kutosheleza tu na hakuna ziada na pia miundo mbinu iimarishwe na haya yote Afrika haiwezi kufanya peke yake inahitaji msaada.
Afrika
inawasubiri, vikwazo vyote vilivyokuwepo
Washiriki
wa kikao
hiki wametoka nchi za
Rais Kikwete pia amekuwa miongoni mwa wana jopo saba katika mdahalo wa wazi kuzungumzia hali ya misaada inayotolewa kwa Afrika na nini matokeo yake.
Misaada ni muhimu kwa Afrika, imetusaidia katika elimu, afya, maji na nishati na miundo mbinu, tunaihitaji kwa maendeleo zaidi katika kilimo na afya, amesema ila ameshauri kuwa wanaopewa misaada washirikishwe zaidi kwani wao ndiyo wanaojua mahitaji yao zaidi.
Washiriki mbalimbali walibainisha mapungufu na matatizo ya misaada kwa Afrika huku wengine wakisema inahitaji kuwepo na mfumo wa kuwajibika zaidi kwa misaada inayotolewa.
Baraza la Uchumi la Dunia hapa Davos, mwaka huu linazungumzia mambo ambayo ni muhimu sana kwa Afrika ikiwa ni pamoja na Afya, Elimu, Kilimo na misaada, ambapo Rais Kikwete anatumia nafasi hii kuendeleza na kuzungumzia zaidi diplomasia ya kiuchumi zaidi kwa lengo la kuvutia uwekezaji na wenza katika biashara na uchumi ili Afrika, hususan Tanzania ijikwamue kutoka kwenye umaskini.
Mwisho.