_files/image001.gif)
THE UNITED
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State House,
Tel:
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
AU YAMPONGEZA BAN-KI MOON KWA UTEUZI WA MIGIRO
Na Maura Mwingira
29/01.2007
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, Bw. Alpha Konare, amempongeza na kumshukuru Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Ban Ki- Moon kwa uamuzi wake wa kumteua mwana wa Afrika, Dk. Asha-Rozi Migiro kuwa Naibu wake.
Bw. Konare amesema uamunzi wa Moon kumteua Dk. Migiro kuwa Naibu wake, ni kilelezo cha namna gani anavyolijali Bara la Afrika na nia yake ya kutaka kuleta mabadiliko ya dhati katika Umoja wa Mataifa.
Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa nane wa siku mbili wa viongozi Wakuu wa nchi na Serikali wa nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika ambao umeanza leo hapa Addis Ababa , Ethiopia.
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa viongozi wakuu wa nchi wanaohudhuria mkutano huu akiongoza ujumbe wa Tanzania, unaowajumuisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe, Bernard Membe, Waziri wa Utawala Bora kutoka serikali ya mapinduzi Zanzibar, Ramadhani Shabani, Mbunge kutoka CUF, Khalifa S. Khalifa na Mbunge wa CCM Dk, James Wanyancha.
Bw. Konare alisema uamuzi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhudhuria mkutano huu wa AU ikiwa ni takribani mwezi mmoja tu tangu achukue uongozi wa Taasisi hiyo ni udhihirisho wa namna anavyotoka umuhimu wa kipekee kwa bara la Afrika.
Aliueleza mkutano huo ambayo ajenda yake kuu ni Sayansi, Teknolojia na Utafiti kwa Maendeleo ya Afrika, pamoja na Mabadiliko ya Hali ya Hewa kwa Afrika, kwamba, Umoja wa Afrika, unaamini kwamba Katibu Mkuu huyo ataendelea kutoa kipaumbele cha pekee katika mazuala yote yanayolihusu bara la Afrika.
Akaongeza kwamba licha ya hali tete ya usalama katika maeneo mengi ya bara la Afrika, AU itaendelea kushirikiana na Umoja wa Mataifa katika changamoto za kukamilisha malengo ya maendeleo ya millennia na kupamba na umaskini.
Konare alibainisha kwamba, mabadiliko ambayo Ban Ki Moon ameanza kuyafanya katika UN kama vile kumchagua Naibu wake kutoka Afrika, yanapashwa kufanyika pia katika Taasisi nyingine za UN kama kile UNESCO na WHO.
Alisema afrika inahitaji mabadiliko ya kweli ili na nayo iweze kutambulika, na kujulikana na kusisitiza kwamba mabadiliko yoyote yatakayofanyika katika UN ni lazima yafanyike kwa haki na uwazi.
Aidha Mwenyekiti huyo wa Tume ya Umoja wa Afrika, alisisitiza kuwa muhimu kwamba mabadiliko katika Umoja wa Mataifa yakajadili kwa kina uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Nchi za Afrika na Taasisi za Fedha za Kimataifa ambazo zimekuwa zikitoa misaada yake kwa Afrika.
Hata hivyo alisema licha ya Taasisi hizo kutoka misaada yake wa Afrika, masharti yanayoendana na misaada hiyo yanaendelea kuziumiza na kuzikandamiza nchi za Afrika. Hali aliyosema, Katibu Mkuu huyo anapaswa kuiangalia hali hiyo kwa kina.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki Moon alisema. “Anashukuru
Aliongeza, kuwa bila shaka wajumbe wa mkutano huo wa
nane wa Umoja wa Afrika watakuwa wanamfahamu vizuri, Naibu wake, Dk. Asha-Rose
Migiro ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa
Bw. Ban Ki Moon alisema kuwa amesimama mbele viongonzi wakuu wa nchi na serikali za nchi wanachama wa Umoja wa Afrika, kutoa shukrani zake kwa imani kubwa walioonyesha kwake na kufanikisha yeye kuchukua uongozi wa Umoja wa Mataifa.
Alisema kuwa imani kubwa ambayo ilionyeshwa na viongozi wa Afrika, pamoja na kumpigia kura wakati wa mchakato wa kumpata katibu mkuu wa umoja huo, ni udhihirisho kwamba walimwamini kuwa anaweza kuliongoza jahazi hilo.
Alibainisha kwamba, katika kupindi chake kifupi cha uongozi katika UN, tayari amekwisha kujenga urafiki na uhusiano wa karibu na viongozi wa Afrika, na kwamba ni matumaini yake kwamba watampatia ushirikiano mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yake.
Alitumia nafasi hiyo kutoa
shukrani zake kwa mtangulizi wake, Bw. Koff Annan aliyemwelezea
Aliongeza kuwa Bw. Annan aliweza kukuza na kuboresha mahusiano kati ya bara la Afrika na Umoja wa Mataifa hali ambayo umoja huo hivi sasa unalitambua bara la Afrika kuwa ndilo chimbuko la mwanadamu.
“Annan alifanya kazi kubwa
Aliahidi kufanya kazi bega kwa
bega na Umoja wa Afrika katika kukabiliana na changamoto mbalimbali
zinazolikabili Bara
Mwisho.