
THE UNITED
REPUBLIC OF TANZANIA
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY TO THE PRESIDENT
Fax. No. 255-22 2113425 The State House, Tel: 255-22-2116539/2116913 P.O.
Box 9120,
DAR ES SALAAM.
E-mail: press@ikulu.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TANZANIA NA TRINIDAD NA TOBAGO KUSHIRIKIANA KATIKA GESI.
Viongozi wa Tanzania, Trinidad na Tobago
wamekubaliana kushirikiana katika kutafiti
na kuendeleza gesi hapa nchini.
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Trinidad na Tobago
wamekubaliana hayo wakati wa mazungumzo yao leo katika Ikulu ya Dar-es-Salaam.
Tanzania
ina hifadhi ya gesi katika maeneo matatu hadi sasa, maeneo hayo ni Songosongo,
Mnazi Bay na Mkuranga eneo ambalo limegundulika hivi karibuni.
“Kuna
maeneo mengine kadhaa ambayo yanasemekana yana hifadhi ya gesi, bado utafiti
unaendelea katika gesi na petroli pia,” Rais Kikwete amemueleza Waziri Mkuu wa
Trinidad na Tobago Mheshimiwa Patrick Manning.
“Gesi
ni kitu cha thamani sana, Trinidad na Tobago tumefanikiwa kupunguza matatizo ya umeme kwa ajili ya
gesi na pia ni chanzo kizuri sana cha
kukuza sekta ya viwanda, sisi imetusaidia sana na tuna uzoefu sana nayo kwa
hiyo tuko tayari kuwasaidia katika stadi mbalimbali kuhusu gesi,” Bwana Manning
amemwambia Rais Kikwete. Na kueleza kuwa Tanzania itapiga hatua kubwa kiuchumi
ikiitumia gesi yake vizuri.
Nchi
ya Trinidad na Tobago imefanikiwa kiuchumi kutokana na sekta ya nishati hususan
gesi na petroli ambapo mwaka 2006 uchumi wake ulikuwa hadi asilimia 12 kutoka
asilimia 8 mwaka 2005 na pato la taifa kutokana na sekta ya nishati ni asilimia
41.2.
Trinidad
na Tobago ina watu wapatao milioni 1.3
wakiwemo wenye asili ya Afrika, India, Ulaya, China, Mashariki ya Kati na watu wenye
asili mchanganyiko.
Waziri Mkuu wa Trinidad na
Tobago yuko nchini kwa ziara ya siku tatu kufuatia mwaliko wa Rais Kikwete.
Kesho
(02.Feb. 07) Bwana Manning atatembelea Zanzibar kabla ya kuelekea Manyara.
Jumamosi (03 Feb. 07) ataelekea Bagamoyo kutembelea maeneo ya kihistoria na
baadaye kuondoka nchini.
Baada ya Mazungumzo yao, Rais
na mgeni wake walishirika dhifa ya kitaifa, iliyoandaliwa kwa heshima ya Bwana
Manning.
Mwisho.
Imetolewa na Premi Kibanga,
Ikulu-Dar-es-Salaam
1 Feb, 07